Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com Love At First Sight - Sehemu ya 63. - Naomi Simulizi

Love At First Sight - Sehemu ya 63.

Raza alirudi chumbani kwake, akaomba Mungu akimsihi amsaidie kwa mumewe ile hasira ya mwanzo isirudi tena. Kwa kuchoka akapatwa na usingizi mzito, mumewe anateseka sebuleni, yeye hana habari. Pius anajumlisha na kutoa, jibu analopata  ni akizira, wenzie wala! Wivu. Raza anamtaka, hasira akiona amedhalilishwa. Akitaka kumchukia, dhamira inamkumbusha na yeye amezaa na mke wa mdogo wake, ndio mbaya zaidi. Akabaki anawaza, mwenzie keshatubu, kaamini amesamehewa, ile ahadi ya Mungu ya awapendao huwapa usingizi kama watoto wachanga ndio ikampata Raza, hana moja na ya ulimwenguni.

Akiwa kwenye usingizi mzito, akasikia mlango unafunguliwa kwa nguvu. “Hata kama ni kunidharau na kuniona sifai, si kwa kiasi hichi!” Raza akakaa kwa mshituko. “Nilikuomba msamaha, ndio unanirudishia vitu nilivyokupa! Ulitaka nifanyaje? Kwamba unaona mimi sifai hata vitu nilivyohangaika kuvisaka kwa pesa nyingi nikijinyima muda wangu, unaona havina maana!?” Akaendelea kulalamika akigomba.

“Kwa kweli sijui natakiwa kufanya nini hapa duniani! Naona ni kama nimejishusha vya kutosha!” Akatoka na kumuacha Raza amekaa kitandani ameshikilia moyo kwa mshituko.

Ndipo akili ikamjia. Hasira zile si za zawadi aliyomrudishia. Wazi Pius alitaka mambo yaishe. Ila hali ya uwanaume, anajirudije wakati alimuacha chumbani kwao akiwa na hasira za wivu juu ya Chezo! Aseme na mimi nimejifikiria naona wote tunamakosa! Pius! Akajua malalamishi juu ya kurudishwa kwa zawadi ndio njia ya kurudi na kumtangazia msamaha, akitaka yaishe.

Hata hivyo alimjua mumewe si muhuni kabisa. Hajui kulala na wanawake mbali na yeye, ndio maana Mina alimtisha sana Raza. Aliwezaje!?

Akajua hasira hizo pia nikuzidiwa tu. Na hivi amerudishiwa nguvu zake, anazo za masaa 24, akajua hizo hasira wala si nyingine. Amezidiwa, na kuomba moja kwa moja bado ni kama anajishauri kwa Raza. Hasira juu ya Chezo, ila mke anamtaka.

Na Raza alijulia kumtuliza mumewe. Kwa swala la kitandani tu, alijaliwa mchezo wa ukweli. Hakuwa mzembe na si mvivu kitandani. Pius alikuwa akirudiwa nguvu ki ukweli, alikuwa akiweweseka. Ila ni muda mrefu sana wawili hao kufanya mapenzi ya mwendo mrefu. Ilikuwa kama Pius akifanikiwa, basi hata dakika 5 hamalizi anakuwa ameshamaliza na hawezi tena kuendelea. Tena mara nyingine Raza alikuwa akimchezea tu na kumfikisha bila hata kufanya naye mapenzi.

~~~~~~~~~~~~~~

Akatoka hapo chumbani na kurudi chumbani kwao. Akamkuta amezima taa kubwa amewasha ya pembeni ya kitanda kama anayemalizia kusoma kitu. “Nilikuwa nikitumia kinga muda wote. Na pia nilipima kujihakikishia nipo salama.” Akamwambia akikaa pembezoni mwa kitanda, Pius akimwangalia.

“Nimekumiss Pius!” Akajilalamisha kusudi kumuonyesha yeye ndio mwenye shida. “Imekuwa muda mrefu hujanishika mume wangu.” “Wewe si unanikimbia, mpaka umehama chumba!” Mtoto wa kike hakuongeza neno, akavua nguo hapohapo akimtizama na kupanda kitandani. Akaanza kumtoa suruali akimvuta miguu ili alale chale. Naye Pius akajiachia ili ashugulikiwe.

Ukweli Raza hakuwa na uhakika ana uwezo wa kiasi gani. Alitaka kumnyonya angalau kumsaidia alale. Yeye hakuwa hata na hamu! Alikuwa amechoshwa na mengi, ya siku nzima. Tokea adamke asubuhi, kazini, kurudi hapo na kupika! Ya Polla nayo, kisha kuja kulia hapo kwa mumewe, maombi aliyokuwa akiomba hajui ni lini atajibiwa, hata mzuka wa mapenzi hakuwa nao.

Ila akajifanyisha tu ili kumtuliza. Akaanza kumnyonya akimchezea kengele zake kwa ustadi wote. Ingekuwa zamani kidogo, kwa hakika angeshahitimisha, Raza alale, lakini usiku huo hola! Mtoto wa kike akafanya yote mpaka midomo ikaanza kuuma, kitu kimekakamaa, kipo hewani.

Ndipo akaamua kumkamkalia, amnyongee nyonga mambo yaishe. Kabla hajajiingizia akiwa amechuchumaia, Pius akamgeuza na kumuweka chali, akaanza romance.

Alifurahi Raza, hapakuwa na jinsi. Na Pius naye alikuwa taratibu kama ambaye anataka kumthibitishia Raza, hajazeeka na ni bora kuliko mwizi wake huko nje. Raza aliimba nyimbo zote usiku huo. Alimnyonya kwa uchu wote. Ile raha ya kushikwa na mumewe akimromance bila kinyaa ila shauku, Raza alikuwa akipiga mabao kulia na kushoto.

Alipomgeuza ili aingie, Raza akaanza kwa kasi akikatika ili tu amfurahishe. “Nashukuru, ila naomba taratibu. Nimekumiss Raza, nataka kukufurahia. Hatuna haraka. Au umechoka?” “Nilitaka ufurahi.” “Basi taratibu. Nataka kukusikia mwilini mwangu, nikufurahie.” Hakuamini! Hayo yakawa mageni kabisa masikioni mwa Raza mwenye ndoa naye ya zaidi ya miaka 19 umri wa binti yake.

Akamuweka kifo cha mende, akapitisha mkono chini yashingo yake kama mto, akaanza kumkiss taratibu kama kumtuliza kabisa huku mkono mwingine ukimchezea titi. Akamlegeza kabisa huku akimnyonya ndipo akaingia na kumvuta mkono akipishanisha vidole.

Usiku huo Raza hakuwa akiamini kama ni Pius aliyemuoa kwa miaka yote hiyo! Bwana alitulia. Halafu akaongeza ufundi kitandani kama ni kwa msichana mpya kwake kumbe ni yeye mkewe! Yalikuwa mapenzi ya muda mrefu ila ya hisia nzito za namna yake.

~~~~~~~~~~~~~~

Ukweli wawili hao hawakuwa na penzi lile la undani tokea mwanzo. Ilikuwa ni kama Raza ndiye anayebembelezea mahusiano yao. Pius alikuwa wa kubembelezwa wakati wote. Lakini mpaka wanalala usiku huo, ni kama kitu kipya kikawa kimejengeka katikati yao.

Na wakati wote ilikuwa ni Raza kujituma hapo kitandani akimtumikia Pius ili kumfikisha golini bila kujijali yeye binafsi. Kisha kujipikilisha na kuhakikisha huyo Pius asiyejua kukaa na njaa anapata milo yote ya uhakika hata kama msichana wa kazi yupo, basi lazima chakula cha Pius atakisimamia yeye. Na kumtumikia hapo ndani kama kijakazi wake wala si kimapenzi.

Ila usiku huo ikawa kama anayelipa deni kwa mkewe. Pius akamuonyesha kitu cha tofauti kabisa hapo kitandani, mpaka akashangaa kwa furaha.

Jinsi alivyomshika na kufanya naye mapenzi, ikawa kwa thamani si kufanya ili yaishe. Alimtayarisha kwa utulivu akimnyonya sehemu alizokuwa akiamsha hisia kwa utulivu wala si papara. Walilala kimyakimya lakini ungejua hapo kitandani wamelala wanandoa na si wapangaji wawili waliokubaliana kanisani au msikitini au kisheria.

~~~~~~~~~~~~~~

Asubuhi aliamshwa na mikono ya mumewe akimpapasa sehemu za matakoni alipokuwa amempa mgongo. Akahisi anaota. Lakini akagundua ule mkono umeshafika mbele. Akijitahidi kupenya katikati. Usiku uliopita alimfuta mumewe vizuri, yeye akarudi kuoga na kuvaa gauni jepesi la kulalia bila chupi wala sidiria.

Akapenya mpaka akafanikiwa kufika kunako. Raza akakumbuka mumewe mpenda cha asubuhi. Akacheka na kugeuka chali. Midomo ikahamia kwenye matiti huku akimchezea vizuri. Alimnyonya matiti huku akipekecha kidude mpaka Raza akili zikajua anataka ampigishe bao.

~~~~~~~~~~~~~~

Yeye hakuwa wa mapenzi ya asubuhi asubuhi. Mwanzoni kabisa wanaoana, ndio ilikuwa kazi hiyo. Pius hatoki kitandani mpaka apate cha asubuhi. Basi alishamjulia. Atamtengea. Zaidi kuinama. Akimbana kwa makusudi na kumkatikia kidogo tu Pius anamaliza. Ndipo anapotoka kitandani na kuanza siku.

Sasa safari za kikazi zilipoanza kuwa nyingi. Ndipo Raza akaona akammalize nguvu asije tafuta wa kuwa akisafiri naye, au wakumwamsha huko anakokuwa nje ya nyumbani, bila ya kujua Pius hakuwa muhuni, yeye mwenyewe Raza alimlemaza. Alikuwa akimfanyia mambo ambayo kwake yalikuwa mageni kabisa. Pius mwadilifu, hakupitia wanawake wengi kabla ya huyo Raza mtaalamu wa kitanda.

Na ambao alishalala nao, wasomi wenzie huko vyuoni zaidi waliyekutana naye nchini Uingereza alipokuwa akisoma shahada ya pili. Ndiye msichana angalau ungesema alikuwa na mahusiano naye ya muda mrefu, na alikuwa mdada wa kizungu, kutokea nchini Poland. Walikutana wote hapo chuoni kwa shahada ya pili. Basi wakaanza mapenzi na chuo. Walipomaliza ndio kila mtu akarudi nchini kwao na Raza kumdaka Pius. Pius akiwa na wazo la kuja kumtafuta msichana wake, maana waliishi vizuri sana lakini Pius alikataa kuishi Uingereza na yeye hivyohivyo.

Irena na yeye alisema asingeweza ishi nchini Uingereza, lazima arudi nchini kwao. Wawili hao wakaachana wakiwa wameachiana kumbukumbu nzito za mapenzi, maana waliishi vizuri sana.

Irena kama maana ya jina lake lilivyo, kiini cha amani, alijua kumtuliza kweli Pius kwa muda wote alipokuwa nchini Uingereza. Waliishi pamoja kwa utulivu wa namna yake, shida tu walitokea nchi tofauti na wote ilikuwa ni lazima warudi makwao.

Pius asingethubutu kwenda kuishi nchini Poland eti sababu ya mwanamke akiwa kichwa cha familia, mzee Ruhinda anamsomesha akitegemea arudi nchini aje ashike majukumu mazito ambayo yeye mzee alishindwa kufikia ndoto zake. Na Irena naye alipelekwa na serikali yake hapo nchini kwa masomo maalumu. Alitumwa na serikali yao, walimtegemea arudi nchini kwao kwa makubaliano ya kulipiwa ada lakini ni lazima kwenda kutumikia serikali yao baada ya kuhitimu angalau kwa miaka 5 ndipo awe huru kufanya kazi popote.

Japokuwa wote walikuwa wakisomea shahada tofauti tofauti, lakini waliongozana kusoma kila mahali na bado waliweza kuishi nyumba moja yaani apartment moja na kufanya maisha ya shule kuwa rahisi na matulivu.

Raza anaingia kwenye maisha ya Pius akakuta tayari Irena ameacha kumbukumbu nzito ya mapenzi tena mwenye machungu. Kwani Pius alifika nchini akiwa bado hajakata tamaa akiamini watakuja kurudiana na Irena. Alibaki akitafuta njia ya kuja kuwaweka yeye Irena pamoja wala hakuwa na mpango na mwanamke yeyoye yule. Alikuwepo nchini akisubiria hiyo miaka mitano iishe, wajipange upya na Irena huku wakiwasiliana kwa karibu sana.

Baada ya miaka miwili tokea watengane nchini Uingereza, Irena alipata mwanaume mwingine akaolewa kitu kilicho muumiza sana Pius. Akasusa kabisa maswala ya wanawake. Raza alikuja kukutana na Pius aliyejeruhiwa moyo. Akijilaumu kwa hili na lile juu ya kutengana kwake na Irena. Mpweke. Hajashika mwanamke zaidi ya miaka miwili.

Irena alikuwa mzuri sana wa sura. Macho ya rangi ya kijani fulani hivi, midomo mizuri mwekundu. Pius akakutana na Raza naye amekamilika, ila sasa ikawa zaidi kitandani. Pius asiyejua mengi akaonjeshwa penzi la mtoto wa Kitanzania. Akaanza kutafuta muda hata mchana, anamuita Raza akamtulize.

Aliponogewa akawa akimkaribisha mpaka kwake. Anahudumiwa usiku, asubuhi anaagwa na penzi. Akamlemaza Pius akawa anamtaka tu kitandani naye Pius anampa pesa kama mchezo tu.

Pius ametoka kwenye familia yenye pesa. Mshahara wake haulizwi na mtu na hapo alikuwa akifanya kazi na mshara wa juu haswa. Raza alipoona huo mjengo anao jenga, halafu hatangazi ndoa ila kufaidi tu penzi huku bado na hasira za Irena, akaona ayafanye marefu yawe mafupi.

Shoga yake akamsindikiza kwa mganga, akafanya yake. Raza mtoto aliyekuzwa na mama mtanzania, uswahili, maadili kwa mtoto wa kike ni kwa asilimia 100. Shule imekaa kichwani! Kuja kupelewa kwa kina Ruhinda, na hivi Pius alikuwa amegoma kuoa. Raza adabu kama mtoto wa Kinyakyusa, salamu mpaka goti, halafu amesoma! Anajielewa, mama Ruhinda akampigia kifua kwa kijana wake.

Pius akajiambia maadamu Irena ameolewa, basi yeyote. Akatangaza ndoa na Raza, moyo kwa Irena. Kwa hiyo wakaingia kwenye ndoa ambayo Pius ni kama ametimiza wajibu, akipewa penzi tamu, kisha kutoa pesa. Na Raza naye ameingia mjengoni. Ndoa ya kikristo, tena katoliki, hamna talaka, Pius wake mpaka kifo! Pesa anayotaka yeyote anapewa. Akabaki akijituma hapo bila kujali hisia zake binafsi yeye kama mwanamke.

Akajitoa kafara kwa malipo ya pesa. Anajituma kuanzia asubuhi mpaka asubuhi siku zikienda bila kufikiana mioyo yao. Raza ni mwanadamu, upweke ukamzidia. Anayo pesa, hana mpenzi ila ndoa. Ndipo akaja kujitengenezea kundi lake la kumtoa upweke baa. Akijikuta nyumbani peke yake, pesa ipo, majukumu ya nyumbani ameweka sawa, Pius ana yake, basi anaenda kwa mashoga zake kunywa na kula baa, akirudi nyumbani ni kulala. Akimkuta mume anamuhitaji, anamkatia mauno, wanalala.

Maisha yakasonga. Wabaa hawamfikii hisia zake yeye kama kwanza mwanadamu, pili mwanamke. Alipokutana na Chezo, na yeye mkewe kisirani. Akianza kugomba mpaka majirani watajua kwao kuna jambo. Kuzira tendo la ndoa ndio fimbo yake kwa mumewe. Akimkera tu, hampi tamu.

Ndipo maisha yakamkutanisha na Raza mpweke ila pesa anayo, hataki kuhongwa ila mtu wa kumsikiliza tu. Sasa naye Chezo alijaliwa utulivu, halafu mapenzi ya kitandani kwake ni sanaa kwelikweli. Akimuanzia Raza kichwani ujue atamnyonya mpaka kidole gumba! Halafu anaweza msikiliza na kumliwaza! Raza anarudi kwake mwepesi. Maisha ya wawili hao yakaendelea kama wanandoa, ila hakuna aliyepata moyo wa mwenzie.

Mpaka hapo majanga yalipowapata na Mungu kuingilia kati ndio Pius sasa kukumbuka romance za kizungu na penzi la utulivu. Kwa mara ya kwanza akajisikia kitu cha tofauti kwa Raza. Ndio aina hiyo ya mapenzi hata yeye akajishangaa.

~~~~~~~~~~~~~~

Alimnyonya ziwa akimchezea kisimi mpaka Raza akapiga bao. Akiwa anahema na bado mbichi akamgeuza kumuinamisha akiwa amempandisha tu gauni kwa nyuma.  Akamkamata kiuno kwa nguvu mpaka Raza alikuwa akipata shida kukatika! Bwana Pius alijipakulia mpaka akawa anamuamsha tena Raza. Taratibu, kwa hisia zote, akafanikiwa kumfikia Raza kwenye G spot ambayo haikutoa bao, lakini raha aliyokuwa akiipata, ilimuacha si mkavu. Hakwenda muda mrefu sana, mumewe akamaliza na kujitupa pembeni.

“Haya ndio mambo nilikuwa nakumiss nayo Raza. Ulinizoesha vibaya! Ukanilemaza na penzi kabla ya kazi. Hivi nini kilitokea?” Yeye Raza alikuwa akikumbuka vizuri sana. Huko kunogewa ndiko kulikomtisha Raza na kumfunga ili asije kamatwa na wanawake wengine huko nje awapo safarini.

Akacheka tu akiwa anajirudisha kulala akihema baada ya kutingishwa vilivyo. Akamvuta na kumuweka kifuani akihema. “Pumzika hapa kidogo.” Raza alifurahi huyo, penzi na kuwekwa kifuani! Akajituliza hapo akawa akimpapasa taratibu wakiwa wanajaribu kutulia.

Akatupia macho kwenye saa ya ukutani, akajua akiendelea hapo kupendana, atachelewa majukumu ya hapo nyumbani. “Si unaingia kuoga kabisa au unataka nikusafishe?” “Natulia kidogo tu ndio nioge. Asante.” “Basi acha mimi nianze siku.” “Hutaki tuoge wote!” Kwa sekunde kadhaa, Raza akabaki amepigwa mshangao. Hawajawahi oga wote hata fungate!

“Nisubiri tukaoge wote.” “Ningependa Pius, lakini nikiendelea kulala hapa jua Polla anaweza kwenda shule bila kula, tena akachelewa maana haamki amkiamshwa na mwingine kama sio mimi. Wewe mwenyewe utaondoka hapa na njaa.” “Ujue umemuendekeza sana Polla, wewe Raza! Umri huo Poliny alikuwa akimka mwenyewe, anajiandaa, dereva akija hapa anamkuta tayari.” Raza akawa anacheka akielekea bafuni. “Nilikwambia watoto hawafanani, Pius.” Akabaki hapo kitandani Raza anaanza majukumu.

~~~~~~~~~~~~~~

Ikawa kama amejimwagia tu maji na kutoka kwa haraka, yeye akapitiwa tena na usingizi maana muda wake wa kuamka ulikuwa bado. Akapata usingizi wa asubuhi hiyo tena kama dakika 45. Kausingizi kazito baada ya sex murua. Alamu yake ilipomuamsha ndipo akatoka kitandani.

 Yaani yeye anatoka kitandani kuoga, Raza anashugulika kwenye ajira yake ya kwanza. Kuhakikisha Polla ameamka, amejiandaa, ameshamaliza kumtayarishia kifungua kinywa chake. Akaanza kula huku mama yake anahangaika hapo jikoni kumuandalia baba yake kifungua kinywa.

Mwajiriwa huyo kuja kuangalia muda, ameshachelewa. Hana hata muda wa kula. Akarudi chumbani akikimbia ili kujiandaa. “Vipi?” “Nakaribia kuchelewa.” “Ushakula sasa?” “Nikisema nikae tu nile, nitachelewa. Nitakula mchana. Ila chakula chako kipo mezani. Wahi ule kabla hujatoka.” Hayo anaongea akikimbilia tena bafuni kuoga ili kutoa harufu ya vyakula.

~~~~~~~~~~~~~~

Kidogo Pius akaanza kumfikiria mkewe. Huruma ikamuingia. Hangaika yote hiyo ni kwa ajili ya kumuandalia yeye, hata yeye hajala! Akamaliza kuvaa na kumfuata bafuni. Akamkuta akijipaka mafuta kwa haraka. Alishatoka kuoga. “Nashukuru kwa kifungua kinywa.” “Mbona kama umekula mbiombio!” “Bado sijala, ndio nakwenda. Ila nasema asante kwa kudamka, na kututengenezea chakula mimi na Polla.” Raza hakutegemea.

Huwa anashukuru akishakula, kama watu wengine. Ila ya siku hiyo aliifanya maalumu na kumaanisha. “Nakushukuru kujali Raza. Najua ungeweza kuwa na sababu nzuri tu yakutofanya yote haya kwa sababu hatuna msichana wa kutusaidia hapa kazi. Lakini kwa kuwa unanijulia. Unajinyima muda wako nakuhakikisha nakula kitu kizuri. Nguo zangu hazikosi kupelekwa drycleaner. Nazikuta zimepangwa vizuri, nikajua ni msichana wa kazi kumbe ni wewe! Asante. Nakushukuru.” Raza akacheka. “Karibu. Nenda ukale usichelewe.” Pius akatoka. Ila alimgusa vilivyo mkewe.

"Baada ya Dhoruba, Mapenzi Yamechomoza Tena"

Kwenye mida ya saa nne, sekretari akapokea fruit basket. Bwana ilionekana vizuri kila mtu pale ofisini akataka kujua inapelekwa wapi na imetoka kwa nani! Wakamfuata mpaka ofisini kwa Raza. Raza alikuwa busy, hata hakutegemea.

“Mumeo katuma mtu akuletee.” Kwa sekunde kadhaa, Raza alibaki ameduaa, asiamini. Akavuta ile basket karibu. Akakuta kijikadi cha wazi tu kikining’inia chenye jina kutoka kwa Pius Ruhinda. Raza alitamani kulia, ila akajikaza. Pius alimfuta machozi na kumtoa aibu kwa hali ya juu hapo ofisini kwao. Maana alishasemwa sana na wafanyakazi wenzie kuwa mume amemuacha sababu ya kuzaa watoto wa kike.

Kabla hajafungua, akapiga picha na kumtumia na ujumbe. ‘Asante SANA kwa kunifikiria.’ ‘Punguza njaa. Nikimaliza kikao nakuja tukale. Kinaweza vuta, lakini unisubirie nitakuja kukuchukua tukale wote.’ ‘Nitakusubiri Pius.’ Hakumjibu. Watu wakaondoka mmoja baada ya mwingine wakamuacha Raza kama haamini!

Kwa Andy.

Wakati mwingine neno samahani, ni zaidi ya kulitamka kwa mtu uliyemuumiza sana. Pius alifikiria jinsi ya kujirudi kwa Andy vizuri na kwa heshima, akaona ajishushe, amuombe msaada, kusudi tu. Akampigia. “Naomba msaada wako.” Kwa sekunde kadhaa Andy alitulia. Ni Pius. Kifedha amemzidi, na ameshakuwa mjini kwa muda mrefu anajua watu na njia za kumuharakishia mambo.

“Nimependa jinsi ulivyojenga nyumba yako. Japokuwa ulikuwa busy au haupo mjini uliweza kutumia watu waliokujengea vizuri na kwa haraka. Tafadhali naomba niige.” Hapo akampata. “Ooh yeah! Jamaa alikuwa mwaminifu sana. Nilitumia kampuni yake. Naweza kukurushia namba yake.” “Na unisaidie kunitambulisha tafadhali. Itanirahisishia kuanzia karibu.” “Haina shida kabisa. Nitazungumza naye, kisha nitakutumia na namba yake.” Hapo wakaanza kwenda sawa.

“Aisee nitashukuru. Utakuwa umetusaidia sana.” “Ukisema ‘uta’, unamaanisha na mzee?” “Hapana. Ni nyumba ya Raza. Nataka kumuunga mkono.” “Mpe hongera sana. Ujenzi siku hizi ni garama sana. Kujenga ni kujimaliza kabisa.” Akasikika ni Andy aliyetulia si mwenye uchungu.

“Atasikia. Vipi Ayan na mdogo wake?” Kitu ambacho hakutarajia akamsikia Andy akicheka. “Vipi?” “Ayvin! Ayvin mtundu sana. Huwa ananikumbusha Mina wa kwanza niliyekutana naye. Mchokozi na mtundu wakupitiliza. Si unajua anatambaa sasahivi!” “Aisee! Tayari!?” Pius hakuamini, ila Andy akazidi kucheka.

“Sasa Ayan anampenda sana, ila ni mkimya na anapenda akifanya kitu chake, atulie kabisa, na mawazo apeleke kwenye anachofanya. Azingatie kabisa. Sasa Ayvin hawezi kaa sehemu moja. Akimuona kaka yake ametulia anazingatia jambo, anakuwa kama anamnyatia, anamfinya. Sasa jificha yake eti kaka yake asimuone alivyomfinya ndio utacheka.” Andy mwenyewe akawa anacheka.

“Na akianza kucheka. Hata kama humuoni, utajikuta huko ulipo unacheka tu. Na hata kama upo kwenye simu, utajikuta unacheka mpaka uliyenaye kwenye simu anaweza asielewe. Anacheka yake hiyo, halafu kwa sauti. Atacheka mpaka eti anajilaza chini kabisa. Yaani hata kama una stress, ukiwa naye yule, zinaisha. Nimemrikodi, kicheko chake ndio nimefanya ring tone yangu.” “Haiwezekani Andy!”

“Nitakutumia video zake. Huwa nawachua yeye na Ayan, wakiwa hawajui. Tunaishia kucheka na Mina tukiwa wenyewe chumbani, tunakuwa kama wajinga vile! Hata nikiwa kazini naangalia, nakucheka peke yangu. Mtundu sana. Halafu mchekaji. Acha nikutumie.” “Nashukuru sana.” Kwa hakika Pius hakutegemea.

“Halafu ana akili sana. Amemsoma mama yake, ameshajua huwa anachanganyikiwa akilia. Basi anatumia kilio chake kama silaha kwa mama yake. Na nimemwambia Mina. Ayvin anaakili sana. Ashakusoma. Ashajua udhaifu wako. Akimuona mama yake, hali kabisa. Chakuwa cha usiku huwa namlisha mimi au dada yao, Mina asiwepo. Na atakula vizuri tu. Akimuona mama yake, ndio mwisho wa chakula, anataka nyonyo tu.” Pius akawa akicheka.

“Hii nakutumia sasahivi nikiwa nawaogesha kwenye sinki, Mina alituchukua. Utacheka sana. Huwa nawajazia povu kwenye sinki la kuogea bafuni kwetu, nawatupiaga hizo toi humo ni za plastiki, kama hizo za bata, zinakuwa zikielea, kisha nawaweka wote wawili kabla ya kulala. Inanirahisishia muda. Sasa muone jinsi alivyojitwisha povu kichwani na usoni, halafu anavyofanya kusudi kumwaga sakafuni ila eti kwa siri maana nilishamkataza. Sasa wakati nikimsugua mwenzie, yeye ndio anafanya hivyo na kuficha toi. Nikimgeukia, ndio kicheko hicho.” Ungejua Andy amepata faraja.

Alikuwa akisimulia huku akicheka kwa furaha. “Siku za ijumaa, huwa nawachelewesha kulala makusudi. Maana anapenda sana michezo. Na nyumba ikichangamka, hata ufanyaje, hutamuweka kitandani kwake akalala.” “Analala bila kubebwa?” “Ila kusiwe na shuguli nje. Huwezi mfungia chumbani eti awaache nyinyi mnafurahia nje! Hapo humlazi. Atataka kutoka tu. Ukitaka alale, aone nyumba imepoa. Taa zimezimwa. Kumetulia. Hapo ukimuweka kitandani, ukamsomea kitabu, atalala bila shida.”

“Sasa siku za ijumaa au wakati mwingine jumamosi, nawafanyia kusudi kuwachelewesha kulala ili tuwe nao muda mrefu usiku. Wakati mwingine Mina yeye analala, ananiacha nao. Sasa akiwa amechelewa kulala, ajue asubuhi atachelewa kuamka. Hapo nyumba haikaliki bila yeye.”

“Mimi na Ayan kila wakati tunaenda kumchungulia kila wakati, tunataka aamke, aanze fujo zake, pachangamke. Tunajikuta mimi na Ayan tunapeana zamu ya kwenda chumbani kwake mpaka Mina anagomba. Maana jumamosi siku ya usafi. Ukimtoa Ayvin kitandani kwake, ujue atazagaa hapo, anataka michezo hakuna kitakachofanyika.”

“Tukifanikiwa kumuamsha, Mina amekasirika. Ujue hapo nitafungashiwa, na kutolewa naye hapo ndani, tunaambiwa tuhamie barazani. Naye hana neno. Akianza kucheka barazani, wenyewe wanatufuata nje. Wanamtaka.” Pius akawa akicheka.

“Bado anakubali kila mtu?” “Hapana. Amebadikika sana aisee! Kama hakujui, akikuona, anataka nimshike mimi au mama yake kama yupo karibu. Basi hapo atajificha begeni mpaka mgeni aondoke. Hataki kushikwa na mgeni. Sura alizozoea ndio hizohizo. Ila babu yake na bibi yake hawasahau. Baba huwa anacheka hapa, mpaka anaondoka akicheka. Mama huwa anasema hajawahi ona mzee Ruhinda akicheka hivyo.”

“Kumbe huwa wanakuja kuwaona?” “Sana tu. Tena siku hizi baba wala hafikii hotelini. Hapahapa alipo cha uchokozi. Tena mara nyingine anaweza akaja katikati ya juma, utafikiri ameshastaafu jinsi anavyokuwa ametulia hapa. Namuuliza,  ‘huna kazi mzee Ruhinda?’ Atacheka tu na kuendelea na wajukuu zake. Yeye zaidi kuliko mama.” “Mama kazi!” “Anavyosema. Ila anasema akijisikia stress zinamzidia ndio anakuja. Zaidi weekend. Anaweza akaja ijumaa usiku, anaondoka jumamosi usiku kuwahi misa na wakati mwingine huwa wanaondoka jumapili jioni, misa wanafanyia hukuhuku na wajukuu zao.” Akamsikia Pius akicheka.

“Umeamini sasa?” “Ujue anaakili zaidi ya umri wake!” Pius akaongeza akicheka. “Nakwambia ni Mina mtupu. Lakini eti anakataa. Anasema yeye alikuwa mtoto mzuri. Roni ndio huwa ananisaidia kumkumbusha.” “Na Roni huwa anakuja!?” “Sio sana. Ile kazi niliyomuachia kule inambana! Ila mama yao alikuwa hapa zaidi ya mwezi. Mina aliugua sana.” “Nini tena?!” Kidogo Pius akashituka.

“Ni mjamzito. Alikuwa akitapika, hakuna kinachokaa tumboni. Sasa mimi mwenyewe kazini, Ayan wakumtuma angalau maji ya kunywa anakuwa shuleni na Ayvin ni wa kumuangalia masaa yote mpaka alale. Msichana wa kazi naye anakuwa na mambo yake. Mina alilemewa. Ndio mama yake akatusaidia.”

“Hongereni sana.” “Asante.” “Anaendeleaje sasahivi?” “Mzima na ananyonyesha kama kawaida.” “Ananyonyesha tena!?” “Huna lugha ukamwambia Ayvin akaelewa anapokuwa na mama yake, asinyonye.” “Si angempa maziwa mengine?” “Yote anakunywa. Na si unamuona mwili huo?” “Amekuwa kibonge!” “Bibi yake alimwanzishia ugali wa dona. Mama yake asipokuwepo, anakula kila kitu. Lakini akiwa na mama yake, ni nyonyo tu. Na huna utakalomwambia Mina kwa wanae. Ana jinsi yake kwa watoto wake, ukimrekebisha anakosa raha kabisa!”

“Huyo Ayan baba mzima, mpaka leo, hata akitoka shule. Akiogeshwa, akilishwa, anapewa chupa ya maziwa, Mina anakaa naye mahali, basi anamuacha anyonye hayo maziwa huku akimnusa mpaka alale.” “Mpaka leo!?” “Mpaka hivi mchana atakaporudi kutoka shule.” Pius akacheka sana.

“Baba ameniambia nimuache tu. Namuuliza hawatakuwa wazubavu? Akasema wanaakili sana. Washamsoma mama yao, wamejua hiyo ndio njia ya kumfanya awe karibu nao.” “Akijifungua sasa?” “Hata sijui Pius! Namuona habari iliopo akilini mwake ni kulea tu hao watoto, na wala si ajira ya nje ya hapo. Anawamudu vizuri tu na yeye mwenyewe anaafya nzuri tu. Hajachoka.”

“Mmeshajua mnatarajia mtoto gani?” Akamsikia akicheka tena. “Amejua jana, naona kama hajafurahia!” “Dume jingine tena nini?” Andy akacheka sana. “Alikuwa ameshaandaa jina la mtoto wa kike. Akawa akimshika na kumuita Ayana. Kutwa anawafundisha wanae kuwa ni Ayana, dada yao. Sasa jana kwenye Ultrasound tumejua ni wa kiume, aisee amepoa sana. Japo hajasema, ila amebadilika. Nimeona nimpe muda aingize taarifa kichwani, azipokee ndio nianze kumkumbusha maswala ya jina la huyu mtoto maana yeye ndio hodari wa kutengeneza majina yao.” “Aisee hongereni sana. Bora ni mzima.” “Nakutumia hii nyingine na babu yao. Utamuona mzee Ruhinda anavyocheka.” Akamtumia.

Yaani jinsi alivyozungumza juu ya Ayvin mpaka Pius akafurahia na kutamani kwenda. “Mnampango wa kurudi huku Dar?” “Aisee namshukuru Mungu, nimepata nafasi ya juu zaidi huko. Natakiwa kuanza mwanzoni mwa mwezi ujao. Mina amefurahi sana.” “Naona sisi tutakuja week ijayo. Acha niweke mambo ya nyumbani sawa, tutakuja kuwaaona kwa zile siku mlizonipa.”

“Nyinyi karibuni muda na wakati wowote ule.” “Una uhakika Andy? Maana ni kweli siku za kazi ni ngumu.” “Nyinyi karibuni tu.” Hilo alilifurahia sana Pius. “Uwe unanitumia video zake huyu cha utundu na kaka yake. Ni kweli zinabadilisha siku.” “Umeonaa! Hiko kicheko kikikukuta katikati ya siku ngumu ya kazi, unajikuta mambo yanaenda.” Pius akacheka na kuagana naye.

Kwa Mkewe.

Akatoka kumfuata mkewe kwa ajili ya chakula cha mchana. Akiwa njiani akapokea simu ya mtu aliyejitambulisha ametumwa na Ruhinda, ana kampuni ya ujenzi. Akajua ni Andy tu. Wakazungumza na kujipanga ndipo akawa amefika ofisini kwa mkewe. Akaamua kwenda kabisa mpaka juu ilipo ofisi ya mkewe.

Kama kawaida yake akaanza utani kwa sekretari wa ofisi. Pius alikuwa mcheshi na wakati mwingine ilimlazimu kuanzisha mazungumzo ya kawaida ilimradi tu kufanya apokelewe bila tension kwenye sehemu anazoingia na wanazo mfahamu yeye na wadhifa wake.

Vikajaa vicheko Raza akisikiliza ofisini kwake, kidogo akasikia kama ukimya wakizungumza kwa kuteta. Akatulia kabla hajanyanyuka kujua kulikoni, isijekuwa ni surprise akaharibu. “Naomba nimfuate ofisini kwake. Usimuite. Si yupo?” “Yupo.” Pius akaamua kwenda kusudi tu kuweka furaha kwa mkewe.

Raza alifurahi kumuona ameingia mpaka ofisini kwake na kusimama mbele ya meza yake! Kama hakutegemea! “Ungenipigia nikakufuata chini. Usingehangaika kuja mpaka huku juu tena.” “Umenisubiria vyote hivyo, na bado unifuate!” “Nisingejali. Kwanza nilikuwa busy na mimi.” Akasimama na kuchukua mkoba wake iliwatoke.

Akamvuta karibu. Akamshika kiuno, akamdaka midomo. Raza hakuamini maana alidhani ni ya juu tu ya mdomo maana hapo kulikuwa na watu wengine! Ila akashangaa vinakuwa vya muda haswa kama aliyekuwa na hamu naye wakati na asubuhi waliyamaliza kitandani!

 Bwana alimnyonya kwa utulivu, ya kizungu matupu! Raza hakuamini, maana haijawahi tokea. Ikawa kama ndio wanaanzana! Eti Pius kama anayetongoza tena! Alifurahi Raza, alifurahi sana. Pius alitoa ujumbe hapo na kwa haraka sana akarudisha heshima ya mkewe. Alifanya kwa utulivu ndio akamuachia. “Pole na kazi.” Wakamsikia akimwambia mkewe taratibu wakati akimuachia. “Asante. Na wewe.” Wakawa wanatoka.

~~~~~~~~~~~~~~

Njiani Raza alikuwa akichekacheka nakushindwa kujizuia mpaka wakafika kwenye mgahawa wa hadhi ya Pius. “Nimezungumza na contractor ambaye ndiye atakaye malizia nyumba yako.” Raza akakaa sawa kwa mshituko na kumtizama. Maana walipofika hapo na muhudumu kuwaletea juisi walizoagiza kwa haraka tu ndipo Pius akampa hizo taarifa.

“Mambo ya contractor tena! Itakuwa garama Pius! Mshahara niliotoka kulipwa ni kama wote nimetumbukiza huko. Ndio maana nilitaka kukutana na Chezo ili…” Bwana Pius nusura aanguke pressure. “Unasemaje Raza!?” “Unapandisha sauti, kila mtu ametugeukia sisi. Tulia tuzungumze.” “Wewe unataka kunichanganya bila sababu. Na nikichanganyikiwa mimi, jua na mimi nitamfuata mbele ya bosi wake.” “Hiyo sauti bado ni ya juu sana kwa mazungumzo ya amani, yanayo tafuta suluhu.”

“Basi SITAKI suluhu na yeye. Mwizi mkubwa asiye na nidhamu. Anaye…” “Pius! Tafadhali tulia na punguza sauti. Niambie kile unachotaka tufanye.” “Nishakwambia, lakini unaona msaada wangu mimi si kitu ila wake. Unaona mimi sifai. Yeye ndio anafaa. Unanidharau Raza. Unataka nifanyaje?!” “Tulia. Na HAPANA Pius! Sikudhara mpenzi wangu. Ungejua ulivyoweka furaha moyoni mwangu! Sema nafikiria swala la pesa. Nilitaka kujua kama bado hajawapa mafundi na kufanya manunuzi mengine aache na anirudishie pesa yangu. Maana yeye ana usafiri wa ofisini kwao na ana muda. Ananunua na kupeleka kule bila shida. Na sijamtafuta kwa heshima yako. Nilitaka kuzungumza na wewe kwanza.” “Basi mimi SITAKI.” “Sawa.” Raza akakubali bila kelele.

“Kama ungekuwa hujakasirika ningekuuliza juu ya pesa yangu niliyompa. Lakini naona nikuache kwanza. Maana pesa yangu inaniuma Pius!  Ni mshahara wangu karibu wote! Utakuwa kama unapotea hivihivi!” “Acha upotee. Ndio kujifunza kutokana na makosa.” “Sawa. Kunywa basi hiyo juisi. Inaonekana nzuri kweli!” Akabadili mazungumzo.

“Nimefurahi sana.” Akajaribu kumtuliza. “Nini?” “Kuniunga mkono kwenye ujenzi.” “Nimejivunia sana. Unaakili. Sikutegemea. Hata Andy nimemwambia.” “Andy!?” “Ndiye aliyenipa huyo contractor. Ndiye aliyemjengea nyumba yake ile ya Kigamboni.” Raza akashangaa sana.

“Pius wewe unataka mambo makubwa sana! Picha uliyonayo ya nyumba ninayojenga si hata nusu ya ile ya Andy.” “Usiwe na wasiwasi. Ndio tutakwenda kuiangalia halafu atatushauri. Kama walikuwa wakikuibia cement wanajenga kwa mchanga tu, ndio itabidi uanze upya. Na usiogope garama. Mwenzio nitakuwa natumia hiyo juhudi yako kuwafundisha binti zangu. Kuwa unaakili ya maendeleo. Umetumia pesa yako vizuri kufanya kitu kikubwa.”

“Pius! Unavyokuza! Acha uone nyumba yenyewe kwanza!” “Hakika si jambo dogo. Na tutaijenga iwe nzuri sana. Wakija kuioa, wajue unaakili sana ya maendeleo. Waige. Nimefurahi sana. Hongera.” Raza akajisikia vizuri. Akamuona Pius anacheka.

~~~~~~~~~~~~~~

“Nini?” “Nimemuomba Poliny aje atukalie na Polla, kuanzia leo usiku, ili sisi tukapumzike sehemu, anasema hataweza. Namuuliza kwa nini! Anasema kwanza Polla mwenyewe hatakubali kumsikiliza. Akimwambia asome vitabu atakataa ndipo watakapoanza kugombana, kisha kupigana. Ataanza kulia anamtaka mama yake, huo usiku utakuwa mrefu, hapata pambazuka. Na itabidi walinzi wote wahamie kulinda ndani na si nje.” Raza alicheka ila kwa mshangao asiamini.

“Ulitaka tutoke kabisa?!” “Tumekuwa na wakati mgumu sana. Najihisi ni kama tulishapotezana japo tulikuwa tukiishi nyumba moja. Nataka muda na wewe Raza. Tukumbushane nia ya kuona. Tuanze msingi upya. Unaweza usiwe kama mwanzo, lakini utakuwa mwanzo wetu mpya na naamini utakuwa mzuri zaidi.”

“Nataka twende sehemu utakayopumzika tu. Hakuna kupika kwa muda wote huo. Na wewe unaagiza na kutumikiwa kama sisi unavyotufanyia. Nimemwambia sekretari wangu anitafutie sehemu watakayokupatia full spa. Wakuminye huo mwili na kukutoa stress zote. Wakutengeneza mpaka ukirudi hapa, unajisikia una mwili mpya.” Raza alifurahi, alifurahi sana. Kwa hakika hakutegemea.

~~~~~~~~~~~~~~

Baada ya miaka ya majaribu na machozi, hatimaye wajikuta wamesimama tena bega kwa bega, mioyo yao ikiwa imeunganishwa na nguvu mpya ya upendo wa kweli. Walitambua kwamba kila maumivu waliyopitia yalikuwa darasa lililowaandaa kwa mwanzo huu mpya — mwanzo uliojaa matumaini, msamaha, na ahadi ya kushikamana zaidi kuliko hapo AWALI.

Jua lilipochomoza juu ya maisha yao mapya,

WOTE (Love at first Sight), walitabasamu, wakijua kuwa safari yao haikuwa ya kumalizika, bali ya KUANZA UPYA kwa

upendo uliopevuka na usiovunjika.

USIKOSE Fungate Ya Pili Na Mwanzo Mpya Wa Raza Na Mumewe.

Mungu ajibuye kwa wakati wake, amemjibu Raza kwa MOTO.

Usipitwe na yale aliyoandaliwa na mumewe.


CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment