Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com Love At First Sight - Sehemu ya 46. - Naomi Simulizi

Love At First Sight - Sehemu ya 46.

Baada ya kifuangua kinywa cha nguvu, Shema akamchukua baba yake mpaka mtaani kucheza mpira. Walikaa huko, baada ya muda wakasikia kelele
majirani wakielekea huko wanakocheza mpira. Ikabidi Pam akimbilie huko kujua kulikoni. Akakuta watu wa hapo kijijini, majirani wanaangalia huo mpira wa Mill, mwanae na watu wengine. Akashangaa kulikoni!

Mama Eric naye akiwa na wazazi wake nao wakaona wakajionee. Mpira ukaendelea. Ila sasa Mill yeye timu yake alikuwa na mtoto mdogo tu, jumla wawili. Halafu Shema na watoto wengine kama umri wake watatu. Basi huo mpira ukachezwa kwa ushabiki mpaka wakawashangaza.

Mwishoe timu ya Mill ikafungwa. Shema akawa anafurahia sana na wenzie. Dogo ambaye ni timu ya Mill akaanza kulia. Akawa anamkimbilia mama yake akiwa analia, Mill akamuwahi. Akaanza kumtuliza watu wakimwangalia. Akampa maneno mazuri mpaka akatulia, kisha akampa na zawadi ya mpira mmoja akimwambia aendelee kufanyia mazoezi. Dogo akafurahia na kuondoka kwa furaha. Ndio wakarudi nyumbani sasa.

Mill Na Ushindani wa Mpira Huko Lushoto.

“Kwani kulikuwa na nini?” Pam ikabidi kuuliza. “Shema huyo! Eti tumefika uwanjani, yeye ndio kocha. Anapanga timu. Akaanza kwa mkwara. Kwamba yeye ndio mpangaji wa timu, hakuna kuchagua. Nikashangaa mimi napewa yule mtoto, halafu wao wamejipanga wanne kama vile mlivyowaona! Namuuliza mbona sisi timu yetu ipo vile, akaniambia mimi na wale wengine pale, eti, mtu mchaguzi huyo si mchezaji.” Wakaanza kucheka.

“Mbona bado!” “Ehe!” Pam, mama yake, bibi na babu wanataka kujua zaidi. “Basi, mpira ukaanza. Bwana yule mwenzangu yeye kumbe uchezaji wake si wamiguu tu, anasaidiwa na mikono pia.” Walicheka mpaka machozi. “Sasa mkumbuke kocha wetu, ndio na ni refa hapohapo. Basi mwenzangu akigusa tu ule mpira, filimbi imepigwa, tunapokonywa mpira, tumecheza faulo. Wenzetu wanatupiana mpira mpaka golini. Mwenzangu yeye kilio, amepokonywa mpira, hanisaidii tena kupambana.” Walicheka. Mbavu hawana.

“Na timu pinzani hawasubiri. Refa akipiga filimbi, tunapewa ule mpira wakati mwenzangu akimalizia kilio, hajapiga teke hata moja, ananyang’anywa mpira. Badala tupambane tuuchukue, yeye anazidi kulia. Basi tukaendelea kufungwa, sisi kazi yetu ni kupokonywa mpira tunafanya faulo kila wakati.”

“Dogo alipoona si kwamba hatufungi tu ila hata kucheza kwenyewe hatuchezi, kila saa kipenga, akaenda kuuchukua ule  mpira akakimbilia nao kwao.” Walicheka. Walicheka mpaka machozi. “Sasa mimi nikabaki nimeduaa! Mwenzangu kaondoka na mpira, analia. Hapo mkumbuke kocha wetu ndiye mmiliki wa mpira pia. Basi, kocha anataka mpira wake. Haya, ikabidi kwenda kumtafuta mpaka kwao.”

“Naenda, huku ile timu pinzani inanifuata nyuma, wanasema tumeshashindwa, sisi hatujui mpira. Ndio sasa ile kelele, wengine nao wakaanza kutufuata nyuma mpaka nyumbani kwa yule mchezaji mwenzangu.”

“Nikamkuta amepakatwa na mama yake, na yeye kapakata mpira wa watu.” Hawana mbavu. “Ikabidi sasa nijitambulishe. Nikasema, mimi naitwa Mill, mume wake Pam, binti wa Shelukindo, baba yake Shema, ambaye ndiye Kocha wetu kule mpirani. Huyo uliyempakata tupo naye timu moja. Tulikuwa tukicheza naye, naona amekimbia na mpira wa Kocha wetu. Pale nao wakaanza kucheka.”

“Ile timu pinzani sasa, wakaanza kutusemelezea. Sisi hatujui mpira. Tukifungwa ndio kulalamika, na dogo ndio kakimbia na mpira. Dogo hataki tena kurudi uwanjani, anasema wale timu pinzani wazulumishi. Kila saa wanafunga wao tu, sisi wanatupokonya mpira. Ukaanza ubishani, dogo hataki kutoa mpira wa Shema. Tukazidi kukusanya watu. Basi watu wote pale wakajua sisi wafungwaji, hatujui mpira.”

“Ndio ikabidi nizungumze na mwenzangu, kwamba, twende tukafungwe kiume, mchezo uishe. Mama yake akatuhurumia, akambemba na kumrudisha uwanjani na mpira pia kashikilia. Ndio ile mechi pale niliyomsihi hata afanyaje, ASITHUBUTU KUSHIKA mpira, atumie miguu tu. Ndio kama mlivyotuona pale. Mwanzo mwisho tulikuwa na kazi ya kukimbia tu, hatujashika mpira zaidi ya sekune 5.” Walicheka hapo. Walicheka sana.

“Shema! Kakufanyia kusudi.” “Najua. Maana nilimwambia mimi najua sana kucheza mpira. Sekondari walikuwa wakinitegemea. Sasa nahisi akanifikiria, akaona anikomoe, abakie yeye mshindi hapa kijijini, mbabe awe yeye peke yake. Ndio kunipa yule mtoto!” “Sasa na wewe ulishindwa vipi kuwafunga?” “Nilijua ningemuharibia siku yake nzima! Kule nimemuacha anasifika, kama sijui mcheza ligi kuu ya Uingereza! Nimeona nimuache tu. Acha nioge, nikatembee kidogo na Pam.” Akaenda kuoga na kuwaacha wakicheka.

Mill Aeleza Ukweli Kwa Pam.

Walitoka wakitembea taratibu mpaka sehemu moja ilionekana imebeba uzuri mzuri sana wa asili. Kulikuwa na maji kweli yanayo tiririka kutoka milimani. Maji masafi sana. Pakajitengeneza bwawa zuri sana hapo chini ya mlima panapo tiririka maji, ungetamani kuogolea ila ilikuwa baridi.

“Aisee ni pazuri sana hapa!” “Basi ndio sehemu za kujificha baada ya kutoroka shule au tulikuwa tukitumwa kuni, tunakuja huku. Tunaogelea ndio tunakwenda kutafuta kuni, au kuni kwanza halafu ndio tunakuja kuogelea.” “Wenzio wako wapi?” “Wamesambaa ila hukuhuku vijijini. Walishaolewa na wana watoto wakubwa tu. Wengine wakubwa kuliko Shema na wengine ndio hao wanacheza na Shema. Wapo.” Mill akatulia, Pam naye akampa muda.

Walikuwa wamekaa juu ya jiwe. “Uliyoyasema siku ile, yalikuwa kweli. Japokuwa ulizungumza kwa hasira, lakini ilikuwa kweli.” Pam akawa hajaelewa ila akaumia. “Ulisoma barua niliyokuwa nimekuandikia?” “Nilisoma.” “Nilikuomba msamaha Mill! Na narudia kukuomba msamaha. Sikufanya vizuri, naomba unisamehe.” “Nilishasamehe Pam. Hiki ni kitu kingine.” Pam akatulia.

“Juu ya wale watoto. Ulizungumza jambo nilipokufuata kazini kwako. Kwamba nilikutana na tapeli mwenzangu, akanibambikizia watoto wa tapeli mwenzetu. Unakumbuka?” Pam akabaki ameinama. “Sasa yale maneno yakaendelea kunikera. Na wale watoto walishanilemea Pam. Walikuwa wakorofi na hawanisikilizi kabisa. Sasa kila nilipokuwa nikimwangalia Shema, jinsi alivyonipokea bila maswali kwamba niliwatelekeza, halafu wale wakawa na kinyongo cha kuwatelekeza, mama yao aliponifunga…” Pam akazidi kushangaa.

Ndipo ikabidi sasa Mill amsimulie kwa undani, mwanzo wake na Kisha, jinsi zile mimba zilivyotungwa, alipomfunga jela na kumuhamishia Trey nyumbani kwake. Akaishia kumtoa jela kwa makubaliano ampe hao watoto, halafu mali zote amuachie Kisha.” “Haiwezekani Mill!”

“Acha mama. Na Kisha wala hakupinga. Alisema waziwazi mbele yangu na wanasheria wetu kwamba watoto watakuwa ni wa Trey kwa sababu hawakuwahi kuachana, hata tulipokuwa naye.” “Mill!” Pam akazidi kushangaa. “Kabisa. Kulalamika siwezi, maana kweli ile ilikuwa ndoa ya mkataba. Nilimlipa akanifanikishia kupata uraia. Nilibaki naye kila mmoja akiendelea na maisha yake, japo nakiri wazi kabisa, kwakweli alikuwa na heshima.”

“Hata siku moja sijawahi mkuta na huyo Trey. Wala usingemkuta kwenye simu na wanaume, labda aliyafanya hayo nilipokuwa sipo nyumbani. Ila nilipokuwa nyumbani, ni ukorofi wake tu, ila sikuwahi hata muhisi anawanaume.” Pam akaumia sana akijua anamlenga yeye.

“Mimi sio muhumi Mill! Na wala kwangu pale si dangulo! Tafadhali naomba uniamini!” “Hata nisipokuamini, au nikaamini, haina maana Pam. Tuyaache hayo. Turudi kwangu na kile ninachotaka kukuomba.” Pam akatulia.

“Basi, hakuwa na shida akasema yeye atachukua watoto wao kitu kilichokuwa kikinitia wasiwasi kwa sababu kisheria wale watoto ni wangu na niliwapigania kwelikweli. Hata yule mwanasheria alikuwa akisema, wangekuwa watoto wa kawaida, hakika ningewalea.” “Kweli Mill?” “Kabisa. Uwezo ninao, kungekuwa na shida gani? Ningewalea ila ningewaambia ukweli, ili kama wangekuwa wanataka kurudi kwa wazazi wao, kila likizo ningewarudisha. Lakini nilifika mwisho Pam.”

“Bwana watoto walilia wale! HAWAKUTEGEMEA.” “Kwani walikuwa hawajui?” “Sikuwaambia kwa sababu wakati naenda nao, sikujua hatima yetu. Kisha ni mkorofi sana. Hakubali kitu kwa urahisi. Ila kwa jinsi alivyokubali safari hii, mpaka akanishangaza ndio nikajua ALIJUA.”

“Wale watoto ilibidi kuwaambia ukweli. Aisee, walilia. Safari hii mpaka wakaomba  msamaha, wanataka warudi na mimi kwa ahadi ya kubadilika. Ila nikaona sitaweza kuwa nao wao, pamoja na Shema. Kwanza ni waongo sana. Wangeweza nikubalia pale mbele za watu. Nikapewa tena kisheria, wakaja nigeuka.”

“Nikarudi nao huku nyumbani, wakarudia tena tabia zao, kama mama yao, wakati wameshaniharibia mahusiano na Shema, mtoto mzuri asiye na hatia. Halafu damu yangu! Nikajiambia hapana. Mwanangu hawezi endelea lipa garama ya makosa yangu. Ndio nimewaacha huko, na mama yao, ila nasikia baba yao amekimbia baada ya kumtapeli mama yao.” “Tena!? Si walikuwa wapenzi wa muda mrefu?” Pam akashangaa.

“Kwa mujibu wa Kisha mwenyewe. Kwamba wameuza mali zote, ndio akakimbia. Kwa hakika nawahurumia wale watoto. Maisha niliyoishi nao, na kinachowakabili mbeleni! Mungu awasaidie tu. Lakini hayanihusu tena. Nimerudi. Sasahivi nipo mimi kama unavyoniona, na Shema tu.” Kimya.

“Ndipo linakuja OMBI langu sasa. Kwa kuwa wewe mwenzangu umepata mtu ambaye unataka kuendeleza naye maisha, na ninaamini Mungu atawajalia watoto, naomba mimi ambaye bado, nimchukue Shema.” Alishituka Pam, kama anatolewa roho.

“Nyie Mill!” “Kwa hiyo wewe unataka Shema Mgini, alelewe na Mgaya wakati mimi mwenyewe nipo?” “Acha nikwambie ukweli juu ya Mgaya. Ni kweli ananipenda sana. Ila unaona mpaka sasahivi sijamleta huku au hakuna muendelezo ni kwa ajili ya huyohuyo Shema. Ni kama hajampokea. Mazungumzo yake ya baadaye ni mimi na yeye na watoto tutakao zaa, lakini hutamsikia mipango juu ya Shema.”

“Au hutamsikia hata mara moja akitoa zawadi kwa Shema hata ukimpa habari zake njema. Umsifie, pengine amekuwa wakwanza darasani! Au amepewa zawadi shuleni, au chochote kile kizuri kumuhusu Shema, hutamsikia akiongeza neno. Hiyo ikanifanya nisite kwake. Na Shema mwenyewe ni kama unavyomuona au kama umemuangalia vizuri, akili yake imekua ya darasani tu, na kwenye mpira, lakini kwengine hajiwezi bila mimi.”

“Sasa nikawa nikiwaza, leo ndio najiingiza kichwakichwa kwa yule mwanaume, itakuaje kwa Shema! Nikabaki mguu mmoja, ndani mwingine nje. Ukweli kwao wananipenda sana. Sana. Hata wazazi wake wamenipokea vizuri tu. Yeye hajatoka kwenye familia kama hivi sisi. Kwao ni ile familia inayoamini ndoa TAKATIFU, ya mke mmoja. Wazazi wake wapo pamoja mpaka hivi tunavyozungumza, na ni wale wakristo wenye upendo.”

“Kaka zake Mgaya na dada zake, ni wasomi, nao ni wale wenye ndoa takatifu na ni wakarimu mno. Lakini hapo tu kwa Shema ndipo nimeshindwana na Mgaya ndio maana mpaka leo umenikuta sina ndoa bado. Ila nafikiri kama angempokea Shema, pengine angeshanioa.”

“Kumbe ndio mpo serious kiasi hicho!” “Ndiyo na hapana. Wala nisikudanganye. Ndiyo, kwamba ananipenda na anatamani kunioa hata kesho. Ila ni mimi tu.” “Kwa hiyo?!” “Hata sijui Mill! Na yeye pia nimemwambia hivyohivyo juzi tulipokuwa tukizungumza. Nafikiri wewe ulipokuja, umemtisha ndio ameongeza pressure ya kutaka tuoane.” Akawa kama amemaliza.

Mill akamgeukia vizuri. “Sasa umemjibu nini?” “Hata sijui Mill!” “Hapana Pam. Lazima kujua. Umebeba hatima yangu na mwanangu. Na wewe ndio tunakuangalia. Huwezi kubakia njia panda.” “Naomba muda Mill. Tafadhali.” “Kwamba hujui au!?” “Najua lazima niolewe. Sitaki kubakia hivi peke yangu. Kilichokuwa kikinifanya nisite ni kumuona Shema kama mtoto wa kambo nikiwa nimeolewa na Mgaya. Sasa, sasahivi wewe upo, na unampenda hivi Shema, inanifanya nitulie na kufanya maamuzi nikijifikiria na mimi pia. Sijui kama unanielewa?”

“Maana mwanzoni nilikuwa nikimfikiria Shema tu. Ila jinsi ulivyorudi, inanifanya nijifikirie na mimi pia. Halafu kingine, Mgaya si mtoaji kama hivyo wewe. Si mtu atakukumbuka kwa chochote na mimi kuomba ni mzito sana. Lazima nitafute kazi yakueleweka kabla sijafikiria mambo mengine. Mama na kina bibi wananitegemea. Zaidi mama. Nisipomkumbuka mimi, basi jua ni mzigo wa wakina bibi ambao wanatunzwa na mjomba au niseme shangazi, mke wa mjomba.”

“Sijatulia Mill. Nina mambo mengi naona nahitaji kuyakamilisha kabla sijafikiria maswala ya ndoa na kabla sijamtoa Shema moja kwa moja. Ila nina wazo. Kwa jinsi unavyompenda Shema na kumjali, tuanze kumzoeza taratibu kuja kwako hata kulala. Akiweza…” “Kwamba ndio hawezi kulala bila wewe!” “Hakika hawezi. Bibi yake anakuwa na hamu naye. Anamwambia walale naye. Anaweza kukubali kwa lisaa, anamwambia hapati usingizi bila mimi kuwepo kitandani.”

“Pam! Ujue Shema ni kijana mkubwa sana!” “Naelewa. Ila mazingira tuliyokuwa nayo ni ya chumba kimoja, kitanda kimoja. Nimelala naye tokea analetwa hapa duniani mpaka leo. Hajui maisha mengine bila hivyo.” Mill akakwama.

Tusikate tamaa. Taratibu. Unaweza hata mchukua siku za ijumaa akitoka shule, ukamjaribisha kumwambia akalale kwako. Akiona kuna chumba kinamsubiria, anaweza akajaribu.” Akatulia.

~~~~~~~~~~~~~~

“Kazi unataka kutafuta wapi?” “Popote pale. Mwenzio sijasoma Mill. Sina sifa za kuchagua kazi. Yeyote na popote.” “Mimi nina kliniki yangu ndani ya hospitali ya familia ile uliyowaona wamekuja siku ya Shema anapewa zawadi. Unawakumbuka?” “Siku ile nilikuwa na maumivu, niliyemuona pale kwa hakika ni Shema na wewe. Hata wale wanao siwakumbuki vizuri.”

“Basi walikuwepo. Ni kliniki yenye mashine ya vipimo mbalimbali. Nimeajiri watu baadhi. Na wewe unaweza pata nafasi. Nitakulipa vizuri na inakuja na gari na nyumba.” Pam alicheka sana.

“Yaani mbali ya mshahara utanipa nyumba na gari!” “Kabisa. Ila si wote nawafanyia hivyo. Ni wewe nakupa kwa kunizalia Shema. Na usiogope. Gari linakuwa lako kabisa kama lile la mwanzo. Na nyumba tunaandikishana kabisa. Ni padogo kama pale tulipokuwa tukiishi pamoja.” “Kwa Mike!?” “Ewaah!” Pam akakunja uso.

“Inamaana nitakuwa nikiishi nyumba ndogo ndani ya uwa wako?” “Na sitakubughudhi. Unaingia na kutoka utakavyo. Utakua huru.” Pam akatulia. “Najua umesema umejitengenezea watu wako, lakini Pam, pale mnapoishi, sipo. Pako duni sana. Najua ulifanya uwezavyo kukabiliana na maisha, lakini sasahivi nipo. Na si lazima ukaachana urafiki na kina mama Batuli.” Pam akacheka.

“Ushawajua majina?” “Nitafanyaje na ndio hao nimeambiwa ni bora, wanaaminika kuliko mimi! Halafu wananitunzia na mwanangu! Tafadhali fikiria.” “Sina haja hata yakufikiria Mill. Nilivyo na shida! Hakika nimekubali na nakushukuru sana. Hata kwa magoti nakushukuru.” “Sasa acha kupiga magoti bwana!” “Ujue nakushukuru sana. Nilikuwa natamani mabadiliko, lakini hapakuwa na dalili. Asante sana.” “Karibu.” Wakatulia.

~~~~~~~~~~~~~~

“Ungependa tukitoka hapa tukatembelee mbuga za wanyama kabla hatujarudi Dar?” Pam akamwangalia. “Unamaanisha sisi?” “Wewe na Shema.” “Kwani ulitaka tuondoke wote?” “Si mnahama? Ndio nafikiria kupata muda kabla shule hazijafungua, aanze kuzoea mazingira.” Pam akatulia.

“Unaonaje?” “Ningependa Mill! Ningependa sana. Asante. Nashukuru.” “Pam kwa shukurani!” Akacheka. “Nayajua maisha kwa kuyaishi Mill! Na nimekuwa na Mgaya, nimemuona jinsi inavyomuwia vigumu kutoa. Si jambo rahisi.” “Kwamba ndio mgumu hivyo!” “Nahisi nikilema chake. Yaani mnaweza kukutana hata kwa kinywaji. Mkala tu chips yai, lakini utamuona jinsi anavyohangaika ikifika kwenye swala la kulipa. Mpaka inabidi kulipia.” “Haiwezekani Pam!”

“Hakika. Usifikiri ni bure kuniona nipo naye njia panda! Kwa binadamu kama binadamu, ni mwanaume mzuri tu. Hana makuu. Si muhuni hata. Pale mtaani anasifika. Mpole na mnyenyekevu.” “Hilo nimeliona. Japokuwa nilimpandishia sana, aliweza kutulia mpaka akanishangaza!” “Basi ndivyo alivyo. Lakini! Mmmmh!” Wakatulia.

~~~~~~~~~~~~~~

“Mill.” Akamwangalia. “Najua ulinihangaikia nije kuwa na wewe Marekani. Lakini natamani ungeniambia juu ya maswala ya kuoa.” Mill akavuta pumzi kwa nguvu na kuzishusha akashindwa cha kujibu. “Ila nashukuru kuja huku. Mama amefurahi sana, SANA. Alikuwa anasononeka, anajua nitaishia kama yeye ndio maana nilijiambia lazima niolewe ili tu kumfuta machozi. Asante kwa kuja huku milimani.” “Nakupenda Pam. Nakupenda sana. Hakuna umbali nitashindwa kwenda kwa ajili yako.” Pam akainama akifikiria.

Mwishoe akamuuliza. “Ulitaka tuondoke lini?” “Ukiwa tayari, hata kesho tuondoke. Huku kuna shida ya mtandao. Mambo yangu ya mtandaoni yanakwama. Ni hilo tu. Ila nimejichukulia kilikizo ili niwe na nyinyi.” “Basi acha tujiandae, tuondoke hata kesho mchana.” Wakakaa hapo wakijipanga, mwishoe wakaondoka kurudi nyumbani.

Hatimaye Mill, Pam & Shema Mapumzikoni.

Kesho yake majira ya saa sita, watatu hao wakawa wakiondoka Lushoto ila akawa ni kweli ameosha. Kila mtu pale kijijini alishajua Pam ni kama mama yake tu. Kuzalishwa na kuachwa. Wenzie Pam walishakuwa na familia za kueleweka hapo kijijini na walitulia na waume zao. Kitendo cha Mill kurudi na kujitambulisha ni mumewe hata kwa majirani! Ikawa amemfuta machozi hata mama Eric.

Hata Mill aliweza muona jinsi alivyokuwa na furaha hapo ndani ya gari. Alikuwa ametulia kiti cha mbele, Shema cha nyuma, ila akiangalia nje ya dirisha. Mara kadhaa aliweza ziona dimpozi zake kama ambaye amekumbuka kitu kikamfurahisha. Hakuacha kumuonyesha Mill hiki na kile huko barabarani ilimradi tu alijisikia vizuri.

Njiani walisimama na kupata mlo mzuri kwenye migahawa ya maana. Ukweli watatu hao walipendeza, ungependa kuwaangalia. Pam alivaa kila kitu alichokuwa ameletewa na Mill. Akanukia vizuri kama mtoto wao. Mill alikuwa amejawa na furaha ya kupitiliza.

Walifika Arusha ilishakuwa usiku. Mill akalipia vyumba viwili kwenye hoteli nzuri sana ya kitalii. “Nimechukua vyumba viwili.” “Mimi nalala na mama.” Akawahi Shema kwa haraka na akili zake za miaka karibu 10, lakini mrefu kuliko huyo mama yake. Pam akacheka kimyakimya.

Hapana Shema. Umeshakuwa mkubwa. Nakuomba jaribu kulala peke yako.” Bwana mtoto alishangaa huyo, kama baba yake anamuomba roho. “Kwa nini!? Mimi huwa nalala na mama yangu!” Ikabidi Mill ashike kazi ya kumuelezea, Pam ametulia kimya akiwasikiliza huku Shema akiuliza maswali ya kushangaa sana wakielekea huko vyumbani. Mpaka wakala na kumaliza, bado Mill anamuelezea mwanae ila hawafiki popote. Shema haelewi kabisa. Pam kimya akisikiliza, akijua lengo la Mill ni kumzoeza ili akihamia kwake aweze kuwa akilala peke yake asijue anajingine.

Akajieleza mpaka akaishiwa, ikabidi aombe msaada wa Pam. “Wewe ushamuuliza Dula kama huwa analala na mama yake?” Akatulia akifikiria mpaka akapata jibu. “Ila Dula yeye mtoto mbaya, sio kama mimi mama!” Akampa mifano ya rafiki zake wote pale mtaani tena wadogo kuliko yeye. Ndipo akaanza kutulia.

“Ni kwa sababu sikuwa na uwezo Shema. Lakini si sawa.” Akapoa. “Jaribu mtoto mzuri. Tuanze taratibu. Mimi nitakuwa hapo kitanda cha pembeni. Silali mpaka wewe ulale.” “Na mimi nitakaa hapohapo na mama. Mkilala tu, ndio naondoka.” Akakubali.

Kila mmoja akaingia chumbani kwake kuoga na kuvaa nguo za kulalia. Vyumba alivyokuwa amekodi milango ya ndani inaingiliana. Kwa hiyo huhitaji kutoka nje koridoni kuingia chumba kingine. Mill alimaliza yeye kuoga akahamia chumbani kwao. Akajilaza kitanda alichojua atalala Pam.

Shema yeye alishaoga akabaki kitandani kwake na baba yake kitanda kingine. Pam alioga huko bafuni na kubadili nguo kabisa akatoka na nguo za kulalia ila za heshima. Akaanza kubabaika pakukaa. Mill alitulia kimya kama hamuoni huku akizungumza na Shema, wote wamelala kila mmoja kitandani kwake, akawa amemuachia Pam nafasi.

Akaanza kukaa kwenye kochi. Akatulia hapo kwa muda kisha akamuona anahamia kwenye pembe ya kitanda. Akaanza kumuona anahangaika baridi, akamuhurumia. “Njoo nikufunike hapa. Nitakukumbatia, hutasikia baridi.” Akacheka kwa wasiwasi kama amwambie huoni mtoto! “Njoo.” Akajisogeza na kulala kwa mbele.

Mill akamfunika na kumchungulia kwa mbele. “Naweza kupunguza baridi kama imezidi au niwapigie simu mapokezi wakuongezee comfoter?” “Naona vyote. Punguza baridi na naomba comfoter jingine.” Akanyoosha mkono na kuwapigia simu mapokezi kuomba comfoter mbili, kisha akapunguza baridi kidogo tu.

“Mkijifunika na mkalala kwenye kiubaridi, ndio mtalala vizuri.” Alishamjua Mill kwa kupenda baridi kali. Baada ya muda mfupi tu wakaletewa. Moja akamfunika mwanae, jingine akamfunika Pam. “Huwa mnaangalia movie?” “Kwetu hatuna tv.” Akajibu Shema. “Lakini kama ni kuangalia movie, mngependa movie gani?” “Ya kupigana.” Akawahi Shema. Wote wakacheka.

Akatafuta movie, akaweka. Pam akashangaa na yeye anaingia ndani ya yale macomfoter kitandani kwake. Akatulia ila rohoni akifurahia. Akamsogelea vizuri kisha akamkumbatia kwa kumvuta kabisa kwake kama katoto kapaka. Pam akacheka akijisogeza. Mill akamkumbatia vizuri.

“Unavyojua kukumbatia Mill! Kama kifaranga cha kuku!” Mill akacheka. “Nilivyokumiss kukuweka mkononi!” Pam akacheka taratibu na kutulia, movie ikiendelea. Akazipata sawia pumzi zake. Pam mwenyewe akaanza kulemewa.

Aliujua mchezo wa Mill. Alijua kuuchezea huo mwili kupita atakavyoeleza Pam mtu akamuelewa. Mill akawa ametulia tu. Mara wakaanza kusikia Shema anakoroma. “Huyo mpenda movie za ngumi, ashalala.” “Ndio anakoroma hivyo!” “Hapo bado. Anakoroma huyo! Sababu ya kuchoka kucheza mpira siku nzima.” “Sasa unalalaje?!” “Inanibidi. Sina jinsi Mill! Ni mwanangu na sina pakumuhamisha. Hivi leo ndio kwa mara ya kwanza amelala peke yake, tokea mama alivyoondoka naye akiwa mdogo sana, tena kwa muda mfupi, maana nilishindwa kulala kabisa alivyoondoka naye. Hawezi kulala bila mimi. Mpaka nahisi uchovu ndio umemlaza na kujua nipo hapa.” Wakawa wanamwangalia.

“Ila kama ni mtoto mzuri, hakika Mungu amenipa. Nakushukuru kwa kunizalia na kunitunzia. Nitakuenzi daima.” Pam akacheka na kujirudisha pale alipokuwa amekumbatiwa.

“Nenda na wewe kapumzike Mill. Umeendesha muda mrefu! Najua umechoka.”  Nigeukie nikuulize kitu.” Akageuka. Akambusu usoni. Pam akacheka. “Huna hamu na mimi kabisa, Pam? Maana nimeona nilikushika ukaruka kama nimekuchafua! Ndio umepetwa kinyaa na mimi kwa kiasi hicho?” “Ni tofauti kabisa na hivyo unavyofikiria.” Mill akakunja uso kama hajamuelewa.

“Pale nilikuwa nakimbia kwa sababu ulinishika, ukaamsha hisia zilizokuwa zimekufa Mill. Halafu tulikuwa nyumbani, kina mama walikuwa nje wanasikia kila kitu. Nikaogopa nisije nika…” Akakwama. Mill akaanza kucheka kwa furaha.

“Kumbe ndio hujiwezi hivyo mbele yangu!” “Unanifanyia makusudi Mill wewe! Bila kujali madhara yake!” Mill alicheka hana mbavu. “Mimi nilikuwa nikiangalia jeraha. Kosa lipo wapi?” “Huna lolote! Unaangalia jeraha kama ulivyokuwa ukinifanyia zamani, ukitaka kufanya mambo yako?” “Mambo yetu bwana!” Halafu akawa kama amekumbuka kitu alichosema.

“Unaposema madhara, unamaanisha madhara gani?” “Bado nipo kwenye mahusiano na Mgaya! Na wewe unataka kuanzisha jambo wakati sijafikia muafaka na yeye.” Hapo akapoa mpaka uso ukabadilika.

Uliondoka Mill. Ukaoa na kuanzisha familia huko. Kweli ulitegemea mimi nibakie vilevile? Mpaka lini?” “Hapana. Upo sahihi. Upo sahihi kabisa.” Akamuachia kabisa, akimfunika.

“Nisikilize Mill. Najua kwa hakika Mgaya akinioa itamvuruga Shema, haswa akija kuelewa maana ya ndoa hapo baadaye, na wewe ukiwepo.” “Unafikiri sasahivi haelewi?” “Mrefu kwa kimo tu. Ila akili yake huyu ni ya mtoto kabisa. Ukikaa kuzungumza naye ndio utajua ni mtoto na mawazo yasiyo na hatia. Mgaya ameshindwa kabisa kumpokea.”

Unajirudia Pam. Hayo yote ulishayasema. Na najua wewe unaakili, unajua kitu chakufanya, ila unaogopa kwa sababu nilishakutenda, na Mgaya ni kama unauhakika wa kuwepo kwake sio kama mimi. Unashikilia huko, na huku kwangu unajua kutoka moyoni kuwa nakupenda, ila unaogopa kurudia kosa japokuwa nimekuahidi haitakaa ikatokea tena.”

Hujaniambia hivyo Mill! Na wala sina uhakika ni kwa nini isitokee tena. Wewe ni raia wa Marekani, Mill! Inamaana upo hapa nchini kama mgeni. Ukiamua kuondoka tena?” “Kwa sababu IPI initenge na mwanangu au wewe? Nilifanya yote kwa ajili ya sisi tuwe pamoja. Nimekamilisha kwa makosa, na kulipa garama kubwa sana kwa ajili yetu. Narudi kwako na wewe unaniadhibu!”

“Sasa nakuadhibu kwa lipi?!” “Najua, unajua mimi si malaya, Pam. Unajua kabisa sikuwa na mwanamke tokea wewe zaidi ya Kisha.” “Ningejuaje?” “Nimekwambia! Na najua kwa vile ulivyo na akili, ulishajua kwa tabia yangu sijafanya uzinzi huko nje.” “Mimi sijui!”

“Basi jua hivi. Tokea mimba ya Mia, sijalala na mwanamke kwa hofu ya kumpa mwanamke mwingine mimba au kusingiziwa jambo kwa vile nilivyokuwa nimefanikiwa kule Marekani. Niliogopa kuanzisha lolote au hata kuwa karibu na wanawake sababu ya kuja kusingiziwa jambo, maana wanawake wa kule hawakawii kukusingizia kuwashika kwa namna wasiyotaka wao, wakakusingizia ukaishia jela. Ndio nikawa namuachia Kisha awe anadili na wafanyakazi wote, mimi nikajiweka pembeni.”

“Sasa kwa namna hiyo unafikiri naishije mimi na sina tatizo lolote kama mwanaume, kama si na wewe kunitesa kusiko na sababu?” “Mimi sikujua!” “Najua unajua, ila unaogopa. Na sina jinsi ingine ya kukuaminisha kuwa nipo kwa ajili yako isipokuwa hivi ninavyokwambia Pam.  Sasa ni juu yako. Ila na mimi ujue sitaendelea hivi daima. Sina sababu yakuendelea kujitesa. Kama unaendelea na Mgaya, niambie na mimi nijue moja. Nianze kufikiria jinsi ya kutafuta MKE, maisha yaendelee.”

“Moyoni na akilini bado nakutambua kama wewe ni mke wangu na ndio maana kila mahali najitambulisha hivyo.” “Na mimi nakushukuru kwa hilo. Umenirejeshea heshima pale kijijini.” “Lakini siwezi kuendelea kuwa mume jina, Pam! Siwezi kuendelea kujitesa bila sababu! Kama umenikataa moja kwa moja, niambie nijue moja.”

“Naomba muda Mill!” “Mpaka lini?” “Niweke sawa jambo la Mgaya. Huyu mtu amenitambulisha mpaka kwao! Ndugu zake wote wananifahamu na wanajua siku moja atanioa. Siwezi nikahitimisha kiholelaolela au bila kufikiria.” “Sasa wakati ukihitimisha huko, mimi unanisaidiaje?” “Mill!?” “Kwa hiyo unataka usikie nimefungwa kwa kubaka ndio uelewe nilizidiwa?” “Hakuna kubaka wala kulala na mwanamke mwingine.”

Hunitaki, wivu wa nini?” “Naomba utulie Mill.” “Kwani hilo ni tatizo. Wewe niambie natuliaje na hali hii.” Akajitoa kwenye shuka kabisa, mzee amesimama wima.

Pam akaanza kucheka. “Unanifanyia kusudi Pam!” “Wewe usipeleke mawazo huko. Tulia tuweke mambo sawa halafu…” “Ndilo nililokuwa nikilifanya miaka yote. Na ndio maana nikaweza. Sasa, sasahivi wewe upo, siwezi tena. Labda kwa kipindi hiki uwe unanisaidia. Halafu hakuna kulala na Mgaya tena.” Pam akakaa.

          “Kwamba unamaanisha tuwe tunafanya mapenzi!?” “Kila ninapojisikia, unanisaidia.” Pam alicheka mpaka machozi. “Hivi unajua nakujua sana Mill wewe! Sitakaa nikamaliza kukusaidia. Na naijua dozi yako. Ni asubuhi, mchana na jioni. Na ndio maana vya asubuhi vilikuwa vikikutana na vya mchana, kisha usiku. Tunajikuta hatutoki kitandani, ni mapenzi mfululizo.” “Nitakuwa na kiasi.” Pam akacheka akimtizama.

          “Hakika tena. Nitakuwa na kiasi. Ila na wewe ukitaka nikusaidie usisite kuniambia. Mimi si mchoyo. Muda na wakati wowote.” Pam alicheka mpaka machozi tena. “Mill! Kwamba wewe ndio mwema wa kiasi hicho?” “Kabisa. Haswa kwako.” “Sawa, tutakuona.” Ikawa amehamasika kupata penzi.

Akaruka kitandani na kuanza kupata kiss iliyomsisimua sana Pam. Akaanza kulegea. Ni Mill wake. Mwanaume wake wa kwanza. Alishakuwa na hamu naye tokea anamuona aliporudi. Ile mikono mwilini mwake, akajiachia kabisa. “Tuhame hapa, Mill. Sio sawa mbele ya Shema.” Akatoa wazo lakini Mill akaendelea kunyonya shingo aliyokuwa akiipenda, lakini gafla akagutuka.

Tamu Yageuka Shubiri.

          “Subiri kwanza Pam. Ulipokuwa ukijamiiana na Mgaya, mlikuwa mkitumia kinga?!” Pam alishituka, hakuamini. Kicheko chote kikamuisha. “Nina maana yangu Pam. Sasahivi tuna mtoto. Uzembe wowote ule unaweza muathiri yeye zaidi. Nayajua madhara ya kufanya ngono bila kinga. Imenigarimu muda na asilimia 80 ya mali yote niliyotafuta kwa shida sana huko ugaibuni.”

“Kama ningekuwa nikitumia kinga na Kisha, ningeweza kujua kwa haraka kama wale watoto si wangu, na pengine hata asingeweza nisingizia. Lakini nilifanya uzembe. Madhara yake ndio hayo Mungu amenitoa kwa garama kubwa sana. Lakini nimetoka.”

          “Kosa la maradhi ya kudumu kama UKIMWI, tusipo kuwa waangalifu tutamuacha Shema yatima. Nataka kujua kama mlikuwa mkitumia kinga? Na mara ya mwisho kujamiiana ni lini ili hata tukienda kupima, tujiridhishe.” “Mill!” Pam hakuamini.

 “Hakika katika hili sinaga masihara. Asiee nipo makini mno. Baba yangu alikufa na kisukari. Mungu alimuokoa na UKIMWI, lakini kwa kumsikia yeye mwenyewe akisema tena akiwa amelewa, akizungumza na wale vijana wake kuwa ilikuwa hata alewe vipi, hasahau kinga na hajawahi muamini mwanamke wa barabarami mpaka akae nao awachunguze ndio alikuwa akijiachia, tena kwa lengo la kuzaa nao. Ndio mama zetu, na alikuwa akisema alitakaga watoto wengi. Alikuwa hazai hovyo na kila mwanamke. Na alisema wazi, katika watoto wake wote, hajawahi zaa na wanawake aliokuwa akikutana nao ulevini. Kwamba hajawahi bambikiziwa watoto, wote alijua ni wake bila swali, kwa aina ya wanawake waliokuwa wakirudi na watoto wake.”

“Kwa hakika kiliniingia sana hicho kitu. Na kwa kuwa nilitaka kuwa tofauti na yeye tokea zamani, mimi nikaongeza uwaminifu na kuacha tamaa za hovyo kwa wanawake, na bado nikaangukia kwenye mitego ya Kisha. Na nimeapa sitarudia hilo kosa. Ndio maana na wewe na kuuliza. Mara ya mwisho kujamiiana na Mgaya ilikuwa lini? Je, mlikuwa mkitumia kinga?” “Kwamba huniamini?!” Akauliza kwa jazba.

Wewe, nakuamini, ila Mgaya simuamini hata kidogo kwa sababu simfahamu kwa undani. Sijui siku alizokuwa akikuhitaji na wewe upo busy na mtoto, haja zake alikuwa akitimiza wapi! Hilo jibu hata kama unamuamini vipi, huna uhakika nalo. Ndio maana nakuuliza Pam. Kwa heshima kabisa. Kama unaona haupo tayari kunijibu, tafadhali nijulishe utakapokuwa tayari.” Pam hakuamini.

“Japokuwa NAKUHITAJI sana, lakini sitahatarisha maisha yangu ambayo ni hatima ya Shema.” Akakaa kabisa akimtizama. Kimya. Pam akishindwa kujibu. “Basi, kwa kuwa wewe haupo tayari na mimi, nakuacha mpaka utakapokuwa tayari, utanijulisha kwa kuyajibu haya maswali. Vinginevyo sitakubugudhi, tutalea huyu mtoto kwa upendo wote.” Akaendelea.

“Nafasi ya kazi na ahadi ya nyumba pamoja na gari vipo palepale. Havitabadilika. Tutatumia ua mmoja, nyumba yako itakuwa ikijitegemea. Kama utaendelea na Mgaya, sitakuzuia. Ila kuwa makini, halafu nijulishe siku anakuja kukutembelea, ili Shema ahamie nyumba kubwa.”

“Mtakapokuwa tayari kabisa kwa ndoa, nashauri tuzungumze na Shema. Ajifunze kutoka kwako na mimi nitafanya hivyohivyo. Kitakapofika kipindi naoa, sitafanya siri. Nitatembea naye kwa hatua, ajue njia sahihi ya kupata mwanamke kihalali.” Pam hakuwa akiamini. “Kwamba huyu amefikia hatua yakuniambia ataoa mwanamke mwingine!” Akawaza moyoni akijua anamaanisha kabisa, japo hakuwa tayari kumjibu.

“Hofu ya Mgaya kuwa hamtaki Shema, sasahivi ondoa. Sasahivi mimi baba yake, NIPO. Kama unampenda na kumuamini, usiendelee kuishi hivyo. Halalisheni, muishi kihalali. Usiku mwema.” Kama utani, Mill akatoka kitandani na kuondoka. Nyege zote zilikata kwa Pam, akapoa kama amemwagiwa maji, haamini.

~~~~~~~~~~~~~~~~~

Inaendelea…


CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment