Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com Love At First Sight - Sehemu ya 38. - Naomi Simulizi

Love At First Sight - Sehemu ya 38.

Baada ya kikao cha familia ambacho ni kama hawakujua kama kilifanikiwa au la, walirudi hotelini kimya kimya. Walichukua chumba chenye vitanda viwili. Mina akaingia kuoga, akarudi kulala. “Mbona mapema? Hatuendi kula pamoja?” “Naomba mkale, mimi mniletee. Nasikia kuchoka Andy! Acha nipate usingizi hata wa lisaa tu.” “Labda sababu ya safari. Unahamu yakula nini?” Mina akafikiria, akamtajia. Lakini mwishoe Andy akaamua aagize wale tu hapo hapo chumbani. Mina akaanza kusinzia na kupitiwa na usingizi kabisa.

Kama baada ya lisaa na madakika, akamka. Andy akamuona, akaenda kumfuata pale kitandani akajilaza pembeni yake. “Unajisikiaje?” “Naona sasa hivi hata ukinipa jembe, naweza kulima.” Wakacheka kidogo.

“Nataka kukuuliza kitu Mina.” “Nini?” “Hukunijibu juu ya swala la zile karatasi.” “Kwamba tunaweza kuzichana na kuendelea?” Mina akauliza. “Ndiyo.” Andy akajibu.  “Kivipi Andy wakati ulinirudisha nyumbani na kumwambia mama na Ron kuwa umeniacha! Sasa tunarudiana vipi kimya kimya tena!?” Mina akamuuliza akiwa ametulia tu ila kwa mshangao.

“Mwanzoni ulianza ukisema unafanya kwa heshima. Hata kuwa kwenye mahusiano na mimi ulikwenda ukazungumza na Ron kwanza ndipo ukaenda kwa mama. Leo unataka iwe kimya kimya!? Au umeshanidharau kwa kuwa nina mimba, unaona thamani yangu haipo tena?” Mtoto huyo wa kike mwenye shule robo ya watoto wa Ruhinda akaanza kuwazungusha vichwa vijana wa Ruhinda.

Hapana Mina! Sitaruka kitu hata kimoja. Nilitaka kujua kama umeridhia kuwa na mimi tena. Ndipo nirudi nyumbani. Sitafanya chochote mpaka niende kwa mama na Ron.” “Hapo sawa. Sasa ukienda utasema nini?” Andy akatulia. Ghafla thamani ya Mina ikarudi. Mina akawa wakubembelezwa na kung’ang’aniwa.

“Maana unaweza ukajikuta aidha unaenda kumuombea msamaha Pius, au kumfunga. Hapo lazima ufikirie.” “Na mimi SIWEZI kwenda kumuombea msamaha kama hajaniomba mimi msamaha. Hakika lazima aniombe msamaha.” Andy akajitutumua na yeye.

“Basi itabidi kusubiri mpaka Pius aamue kujirudi, akuombe msamaha ndipo na wewe ukazungumze na mama pamoja na Ron, ndipo tufikirie kurudiana.” Mina akamuwekea na yeye ngumu. Andy akapoa. Inamaana hamtaki mpaka arudi nyumbani kwao.

Pakatulia, na chakula kikaletwa kabisa. Wakala, Mina akamuona amepoa kama anayefikiria kitu. Na yeye akawa kimya na mwanae, akimtaka ale vizuri ashibe.

Baada ya kula akampeleka bafuni kuoga. Akamvalisha nguo za kulalia. Akamlaza kitandani kwake yeye. Pale alipokuwa amelala, na chupa kubwa ya maziwa, akamfunika. Ayan akamnusa na kumkanyaga mama yake, mpaka akalala. Mina akamtoa hiyo chupa mdomoni, akamfunika vizuri. Akabaki amejilaza pembeni ya mtoto wake, wameacha kitanda kingine kisafi kwa ajili ya Andy.

Andy alipoona mtoto amelala na Mina ametulia, akamuita. “Mina!” Mina akamwangalia. “Mimi naona sitamsubiria Pius. Nitakwenda kuzungumza na mama kivyangu.” “Utamwambia nini?” “Sitaongea mambo mengi, nitamwambia nataka kumrudia mke wangu, basi.” Mina akamwangalia na kunyamaza.

“Unafikirije?” “Mimi sijui Andy! Wewe fanya kile unachoona ni sawa.” “Sasa unafikiri mama atanielewa?” “Sijui Andy! Mambo mengine yatajijibu huko huko. Ila mimi huko kwa mama, sitarudi leo wala kesho. Mama alinifukuza nikiwa namuhitaji sana. SIRUDI. Wewe nenda kwa wakati wako.” Mina akajifuta machozi. Akamuona Andy anatoa simu mfukoni. Akapiga. Ikaita bila kupokelewa. Akafanya hivyo mara tatu, akaona simu iliyopigwa haijapokelewa. Akamuona amekunja uso.

Kwa Ron!

Baada ya kama nusu saa akamuona anapokea simu. “Mzima Ron?” “Mzima kabisa Kiongozi. Kwema huko kanda ya kati?” “Kwema. Lakini nipo mjini. Upo nyumbani na mama? Nilitaka kuja kuwaona.” Pakazuka ukimya. “Ron?” “Kuna nini tena? Maana kama ni Mina, si ulishaachana naye? Au kafanya nini tena?” “Hapana. Ni jambo la amani?” Pakazuka ukimya mwengine.

“Ron?” “Labda uzungumze na mimi Andy.” “Kwa nini nisije kuwaona kabisa?” Akauliza Andy kwa kubembeleza kidogo. “Nisikilize Andy. Kumbuka mimi ndiye niliyekukaribisha na kukufanya uwe karibu na mama. Ukavunja mahusiano kwa namna yako. Labda hujaelewa. Na nikukumbushe nilivyokwambia mwanzoni kabisa. Chochote kitakachotokea kati yako na Mina, nilikwambia nitakuwa upande wa Mina.” Ron akaendelea.

Tulikukabidhi Mina akiwa mzima kabisa. Lakini ulimrudisha Mina aliye mjamzito, tena mgonjwa. Ukamtelekeza hapa bila hata pesa ya matumizi. Ikawa ni kama msichana uliyemuokota tu. Uliondoka bila hata kugeuka nyuma, wala kuuliza juu ya mama uliyemrudishia mtoto mjamzito, kujua anaendeleaje! Ukamuachia fedheha, hata mjukuu hukumrudisha kusalimia.  Hivi unajua kama Mina alifukuzwa hapa nyumbani?” “Nafahamu Ron, ndio maana nataka kuja kutengeneza. Najua niliharibu.” Mina akabaki kimya akisikiliza.

“Unakuja kutengeneza wapi Andy? Kwa nani? Mama aliyekuwa akilia kanisani akimtafuta mtoto wake arudi nyumbani, aliweza kumfukuza huyo mtoto. Hajazungumza naye kwa kipindi chote hicho cha miezi karibu 7 sasa! Unaweza kufikiria hali ya mama ilivyo?” Andy kimya.

“Haya, Mina ulimuacha kama malaya tu. Mimi sijui kilichotokea kati yenu. Lakini ulimjua Mina tokea mwanzo. Ukasema unamchukua hivyo hivyo. Kwa hiyo ulimuoa ukimjua Mina vizuri sana. Uliwezaje kumuacha anahangaika mjini peke yake wewe unafanya kazi mikoani? Ulishindwa vipi kuwa na familia yako popote unapokwenda? Ukamuacha Mina anahangaika peke yake mjini, watu baki ndio wanamtunza! Anakuja kupata mimba, unamuacha vibaya vile!”

“Halafu kwa jeuri uliyokuwa nayo, ukashindwa kuzungumzia kabisa swala la mtoto ambaye Mina alikuwa akihangaika naye zaidi ya miaka mitatu mfululizo, peke yake! Shule na kulea kwa taabu. Akihangaika kila mahali na mtoto! Ulimrudisha Mina nyumbani na masanduku tu! Unaposema unakuja kutengeneza, ni kwa nani?” Ron akawa mkali kweli.

“Inawezekana umetuangalia na kutudharau Andy. Kwa vyovyote ilivyo na ulivyotukuta, tulikuwa na amani SANA. Ulimkuta Mina ametulia nyumbani, ukamtoa hapa, ukaenda kumchanganya. Akabaki akihangaika mjini hajulikani kama ana mume au la. Akawa kama kijakazi wako ukimtuma huku na kule na mtoto mgongoni. Leo unataka kuanzisha nini tena?” “Mina ni mke wangu na namtaka mke wangu.” Andy na yeye akaongea kwa ukali.

“Wewe si ulimuacha? Sasa mke wako kivipi!?” “Uliona wapi ndoa ya kanisani inavunjika?” Andy akauliza kwa ukali na kumshangaza hata Ron. “Nilifanya kosa, nilishatubu kwa Mina tokea nipo Uswiz. Mina akanisamehe na tukakubaliana nikirudi tunaanza upya nikiwa nimebadilika. Nilipo ndipo na yeye atakapokuwepo. Akaniambia madhaifu yangu yote. Nikataka hata kuacha mafunzo nirudi nyumbani niwe naye baada yakugundua ni kwa kiasi gani nimemuumiza mke wangu. Mina mwenyewe alinitia moyo nibaki tu nimalize, atanisubiri. Narudi nyumbani namkuta mjamzito. Mimi kama binadamu nilipaniki. Nikafanya makosa bila kufikiria. Pengine ni sababu ya uchovu!” Andy akaendelea.

“Wewe uliponiona siku namrudisha Mina nyumbani nilikuwa na furaha?” Andy akauliza kwa kugomba. “Au ulitaka unione nalia mbele yako ndio ujue na mimi nimeumizwa? Na mimi nilikuwa kwenye maumivu Ron! Nikafanya makosa nikiwa kwenye hasira. Siku namuacha Mina pale kwenu, tayari nilishakuwa na hamu na mke wangu hata kabla sijaondoka kwenu.” Mina akashangaa sana.

Hakuna usiku uliopita tokea niachane na Mina, nikalala kwa furaha nikijua Mina hayupo kwenye maisha yangu! Nampenda mke wangu. Nakwambia namtaka mke wangu. Sitajali alivyo, namchukua Mina vile alivyo sasahivi na nitampenda kama mwanzo au zaidi nikiwa nimejionya kutorudia kosa, na wewe unaniwekea ugumu! Unataka Mina azae peke yake? Au wewe umesahau kama Mina ni mama wa mtoto wangu pia? Unataka kuniwekea ugumu ili mwanangu akue bila mama yake? Na juhudi zote za Mina, shida zote alizopitia Mina nikimuacha nyumbani, mimi nikihangaika kufika hapa nilipo, iwe bure? Yaani matunda haya aje ale mtu mwingine?” Kimya.

“Wewe vipi Ron?!” Andy akashangaa kwa hasira kama hajakosa! “Sasa nimeshakwambia nataka kuja kumuona mama na wewe. Niwaombe msamaha na niwatarifu kuwa namrudia mke wangu. Unikaribishe usinikaribishe NAKUJA.” Andy naye akaweka ubabe.

 “Wewe unajua Mina alipo?”  Akauliza Ron kwa kutulia. “Ndiyo, najua. Wewe niambie nije saa ngapi.” “Ratiba ya jumapili kwetu ni ileile. Labda jioni.” “Mimi nakuja sasa hivi. Kesho asubuhi narudi Dodoma. Jumatatu natakiwa kazini.” “Sasa hivi Andy!?” “Sitakaa muda mrefu Ron! Mbona kama unaniwekea ugumu wa MAKUSUDI tu? Au unataka nini kitokee!?” “Daah! Andy ukiamua jambo wewe! Unakuwa mbishi na mgumu kubadilika!” “Nakuja Ron. Tafadhali niwekee mazingira mazuri.” Andy akakata simu. Mina mwenyewe akashangaa jinsi Andy alivyo ng’ang’ania.

~~~~~~~~~~~~~~

Ila alishamjua, akimnyima penzi, anakuwa kama mwehu. Atafanya lolote lile atakalomwambia ilimradi tu amuweke kitandani. Alimnyima mapenzi kabla ya ndoa, Andy akahamisha milima mpaka akafanikiwa kumuoa nchini Nairobi. Na usiku huo alimuwekea ngumu kusudi, akapambana mpaka kurudi kwa wazazi ili kwenda kuomba msamaha.

Taka Cha Uvunguni.

Ilikuwa saa tatu na nusu usiku Andy alipokuwa mlangoni nyumbani kwa kina Mina. Ron akamfungulia. “Karibu.” “Asante.” Andy akapita na kumkuta mama Ron amekaa tu hapo sebuleni. Amepoa kuliko kawaida yake. “Shikamoo mama.” “Marahaba Andy mwanangu. Karibu.” Andy akakaa.

“Majibishano yako na Ron ndio yameniamsha. Kwa sehemu nimekusikiliza. Zaidi hapa mwisho na kama nimeelewa vizuri, umesema unajua Mina alipo na unataka kumrudia. Hivyo hivyo alivyo!?” Akauliza mama Ron kinyonge sana tena kwa mshangao bila kupoteza muda.

“Ndiyo. Hata kisheria nilikuwa sijaachana na Mina. Yale makaratasi niliyowaonyesha siku ile, yalianza kuwa mzigo siku ileile nilipomuacha Mina hapa. Nilijuta sana, hata sikuyarudisha kwa mwanasheria ili iwe talaka halali japo nilikuwa na hasira na sikujua hata kama tusipoachana tutaendelea vipi kuanzia pale akiwa na mimba ya mtu mwingine.”  “Sasa, sasa hivi ushajua utaishije naye? Maana ni kweli ni ngumu. Inamaana huyo mtoto atakuwepo kwenye maisha yenu yote ya ndoa akikukumbusha yeye sio mwanao na aliingilia katikati.” Akauliza mama Ron kwa upole kama aliyefedheheka.

“Hivi tunavyozungumza naishi na Mina. Kama miezi miwili iliyopita aliomba nimpelekee mtoto, yeye ndio aishi naye. Nikakumbuka jinsi Mina alivyohangaika na Ayan. Nikajua sitamtendea haki nikimuwekea ugumu. Alikuwa akiishi Iringa.” Wote wakashangaa. “Iringa kwa nani?!” Akauliza Ron.

“Alipanga kajinyumba kadogo tu kenye chumba cha kulala kimoja. Alikuwa akiishi peke yake. Ndipo nikampelekea Ayan. Niliwaacha kama majuma mawili au moja na siku. Lakini mama, nilishindwa. Mina alihangaika na mimi kujenga ile nyumba ya Kigamboni. Yeye ndio kwa sehemu kubwa alihangaika na ule ujenzi mimi nikiwa nipo safarini kikazi. Achilia mbali shida alizopata na mtoto wangu wakati mimi sipo! Nilishindwa kumuacha Mina kwenye kile chumba kimoja na mtoto, wakati nilikuwa nikihangaika kwa ajili yao wao wawili. Nikawachukua na kurudi nao Dodoma ambako nilinunua nyumba huko.” Andy akaendelea, wakimsikiliza kwa makini tu.

“Tukaanza maisha kama wazazi tu wa Ayan. Lakini nataka mke wangu. Naona naweza kuishi na Mina vile alivyo na akawa mke wangu. Nampenda Mina, namtaka mke wangu. Nimerudi hapa kuomba radhi jinsi nilivyoondoka vibaya. Naomba mnisamehe. Nilikuwa nimekasirika na nilifanya vibaya.”

“Juu ya makosa ya nyuma, nishazungumza na Mina tokea nilipokuwa Uswiz,  tukasameheana kama nilivyokuwa nimezungumza na Ron.” “Nilisikia Andy, mwanangu.” “Basi ni hilo mama yangu. Nimekosa, naomba unisamehe kama vile ambavyo ungeweza kumsamehe Ron.” Ron akacheka na kutingisha kichwa.

“Wewe mzee nimekuvulia kofia! King’ang’anizi mpaka ukweni!” Angalau wakacheka. “Naona unataka kuninyima mke wangu! Siwezi kukubali! Mina anafahamika mpaka ofisini kama yeye bado ni mke wangu. Nilishindwa kumtoa kabisa.” Wakatulia kidogo.

“Kwa hiyo, hilo moja, na nishukuru kunisamehe. La pili, najua mama jinsi ulivyohangaika na Mina. Nilitaka kukutaarifu kuwa nipo naye. Tunaishi Dodoma. Ni mjamzito wa miezi 7 na siku chache. Anaye daktari mzuri tu anamfuatilia afya yake. Anaendelea vizuri kabisa, naomba mama usiwe na wasiwasi.” “Nashukuru Andy mwanangu. Mungu akubariki baba. Nawaombea kila la kheri.” Andy akapumua kwa nguvu na kucheka.

“Sasa hivi nakwenda kuchana zile karatasi. Naendelea na mke wangu.” Wakacheka lakini kama wanawaza. “Ron anayo namba yangu mpya. Najua hampo kwenye mawasiliano na Mina, ila mkiwa na maswali yeyote, muda na wakati wowote mnipigie. Mama, ukitaka kuzungumza na Ayan, tafadhali usisite kupiga. Halafu Dodoma si mbali. Kule tunayo nyumba kubwa sio kama pale tulipokuwa tukiishi mwanzo. Karibuni muda na wakati wowote. Hata ukitaka nauli, tafadhali usisite. Nijulishe. Mimi na Ron tutafanya mipango, uje kuona wajukuu.” Mama Ron akafuta machozi. “Asante Andy. Tunashukuru.” Ikabidi Ron ndio ashukuru kwani mama yake bado alikuwa akilia akikumbuka jinsi walivyoachana na Mina. Andy akaaga na kuondoka.

Mina & Andy Tena.

Alirudi hotelini akamkuta Mina anakula chakula walichokuwa wamebakiza. Andy akaingia na cheko. Mina akacheka na kutingisha kichwa. “Hivi ujue Ron ni kama baba yako mkwe, wewe Andy!” “Hata kama angekuwa mzee Ruhinda! Ndio atake kuninyima mke!” Mina akamwangalia na kuendelea kula. “Sasa mbona huniulizi mambo yaliendaje?” Andy akauliza. “Kwani mimi sikujui wewe, unapotaka kufanya jambo lako? Nilijua hutarudi hapa mpaka uwaweke sawa.” Andy akacheka sana.

“Ujue sasa hivi wewe ni mke wangu kihalali?” “Mbona sasa mimi hujaniomba turudiane?” Mina akauliza. “Ngoja kwanza nikaoge vizuri, niwe msafi ndio nije kuomba msamaha wangu.” Mina akatoa tabasamu huku akiendelea kula kama aliyeelewa. Hata Mina naye alikuwa na hamu na Andy. Alijua mchezo wa Andy sio wakitoto. Akajua usiku huo atalala vizuri.

~~~~~~~~~~~~~~

Andy akamsogelea pale baada yakupata tabasamu, akajua amekubaliwa. “Nilivyo na hamu na hiyo midomo!” Mina akacheka taratibu kama kwa aibu. Akamsogeza karibu, akasimama naye kwa kumvuta juu. “Pole kwa kukutelekeza mpaka ukaingia matatizoni. Na samahani kukuacha vibaya. Nisamehe.” “Yameisha Andy. Mimi mwenyewe nimefurahi tunarudiana. Napenda ndoa yangu.” Andy akainama kupata busu. Mina akatoa ushirikiano.

Hali ikabadilika, wakachukia kwa Ayan kuwepo hapo. “Heri tungemchukulia chumba chake huyu! Atanipunja sana usiku wa leo.” Mina akaanza kucheka taratibu. Andy akamvutia bafuni. Akaanza kumtoa nguo.

“Tukirudi Dodoma tunachoma yale makaratasi moto.” “Asante Andy.” “Na mimi nakushukuru Mina. Leo umenirudishia heshima nyumbani.” “Na wewe leo umenirudishia heshima nyumbani.” Wakakumbatiana na kissing za uchu zikaendelea Andy akiwa na hamu na Mina, ya karibia mwaka, yaani miezi 11. Ilibidi hapo bafuni pafae tu. Andy hakuweza kusubiri.

Wakarudi chumbani, wakazima taa kabisa, wakahamia kwenye kitanda alichokuwa ameachiwa Andy. Mina na tumbo hilo la miezi 7 akatoa ushirikiano wa nguvu. Walifanya mapenzi kama ndio wapo fungate kasoro kupunjwa uhuru sababu ya mtoto. Lakini walilala wakiwa wameridhika. Mina akiwa amekumbatiwa. Akashukuru angalau atarudishiwa pete zake za ndoa, atazunguka na tumbo akiwa ndani ya ndoa. Na angalau hataendelea kuwa kicheko kwa ndugu.

Mwanzo Wenye Sura Mpya

Siku inayofuata walirudi Dodoma, Andy akiwa na furaha yakumpata Mina, japo kilichowapeleka ni kama hakijaweza kuchukua picha inayo eleweka. Pius hakuomba msamaha, ila Andy akawa ametulia kabisa. Mina alionyesha kumuheshimu na kumthamini mbele ya familia ya Ruhinda ambako alikuwa na uhakika kabisa alipoteza heshima kwao. Wawili hao ungejua ni wazazi wa Ayan, waliingia nyumbani kwao hata Judy akajua lipo badiliko.

~~~~~~~~~~~~~~

Mina akapata muda na Judy. Akamshuhudia yote yaliyotokea huko na kumshukuru sana Judy. “Wala sio mimi mama Ayan. Ni Mungu wako huyo. Tena amekujibu kwa haraka sana na amekurejeshea heshima. Mshukuru Mungu.” “Nilikuwa namshukuru njia nzima. Hakika amenitendea makubwa. Amenisamehe na kunirudisha kwenye ndoa ambayo wengi walibashiri sitaweza kuishi na mume! Hakika nashukuru Judy. Nimepata utulivu wa hali ya juu.” Wakacheka hapo jikoni, Andy akiwa na mwanae sebuleni.

~~~~~~~~~~~~~~ 

Wakiwa ndio wamerudisha amani na furaha katikati yao, nyumba imetulia, siku ya ijumaa mzee Ruhinda akampigia simu Andy na kumuomba kwa heshima ya Mina, ampokee tu Pius. “Hata kama utashindwa kusamehe tokea moyoni, tafadhali fanya hili jambo liishe Andy. Najua ni ngumu, lakini nimezungumza sana na Pius. Nimeona amefika kwenye majuto ya kweli. Tafadhali naomba urahisishe haya mambo. Wewe upo na hiyo dhamana.”

“Mpokee, ili mjue mtafanya nini kuanzia hapo. Mungu akipenda huyo mtoto atazaliwa. Na Pius anaonekana anataka mahusiano na huyo mtoto. Lazima wewe uwe katikati yao na uendeshe huo uhusiano bila kuzembea. Sijui kama umenielewa?” “Nimeelewa baba.” Andy akakubali bila shida. Na hivi ashahakikishiwa penzi na Mina! Hakuona tatizo tena.

~~~~~~~~~~~~~~

Siku ya jumamosi mchana, Andy alituma dereva akamfuate kaka yake uwanja wa ndege ili amlete nyumbani. Alifika Pius peke yake, hakusindikizwa na yeyote. Alikuwa mstaarabu mpaka akamshangaza Mina! Hakupoteza muda, akaenda moja kwa moja kwenye lililompeleka.

“Naomba unisamehe Andy kwa kulala na mke wako. Nilikosa na hakuna jinsi ya kujitetea katika hili. Naomba unisamehe.” Andy akamwangalia. Mina akashangaa kimya. Na yeye akanyamaza. “Unaposema unataka mahusiano na mtoto, unamaanisha nini? Maana sitaki uje unizunguke tena Pius.” “Sitarudia tena. Naahidi hata kwa Mina.” Akakiri Pius.

“Sasa nataka ujue kabisa, mimi na Mina tumerudiana. Mina ni MKE wangu kihalali kabisa. SITAKI uwasiliane na mke wangu bila mimi kujua. Na uache kumtumia mke wangu pesa. Tabia yako ya kwenda kumuwekea mke wangu pesa benki, iishe Pius.” “Nataka kumtunza mtoto wangu! Sitaki mtoto wangu..” “Sasa unamuona mtoto wako hapa?” Andy akauliza kwa ukali. Mina kimya.

Usiniudhi zaidi Pius!” “Nisikilize Andy. Nataka huyo mtoto azaliwe kwenye mazingira mazuri na..” “Wewe unaona hapa tulipo tupo kwenye mazingira mabaya? Au uliona Ayan alizaliwa kwenye mazingira mabaya?” “Sitaki sasahivi mumpeleke kwenye kliniki za ajabu ajabu. Maana kliniki aliyokuwa akienda Mina, kule Iringa ilikuwa nzuri na ni mimi ndiye niliyemtafuta huyo daktari kwa kuwa niliambiwa ni mzuri. Nataka Mina ahudumiwe na daktari mzuri ili mtoto wangu awe kwenye mikono mizuri na salama.” “Sasa, sasahivi Mina hayupo Iringa, yupo Dodoma. Tafuta daktari yeyote unayemtaka hapa, niambie, nitakuwa nikimpeleka.” “Sawa.” Hapo wakakubaliana.

“Kuna jambo jingine.” Mina na Andy wakamwangalia. “Japokuwa Mina hakutaka kujua jinsia ya mtoto, lakini mimi nilizungumza juzi na yule daktari aliyekuwa akimshugulikia Mina kule Iringa, nikamuulizia jinsia.” Mina akabaki akimtizama. Andy kimya.

“Nimekuja na jina. Hilo jina ndio nataka tuanze kumuita huyu mtoto kuanzia sasa hivi ili ajue tunamfahamu na tunamsubiria.” “Ujue wewe Pius unataka kuniharibia ndoa yangu wewe!” Mina akashangaa sana. “Hapana Mina. Nia yangu ni nzuri tu.”  Pius akajitetea. “Nia yako nzuri ipi? Niambie jina lenyewe.” “Pius Junior Ruhinda.” “Haya naomba uondoke Pius.” “Subiri kwanza Mina!” Mina akasimama kama anayetaka kuondoka.

“Naomba wewe maliza kuomba msamaha, uondoke. Lasivyo utataka kuniudhi uje urudi tena kuja kuomba msamaha mwingine.” “Mbona naongea kwa amani tu! Tatizo liko wapi?!” “Cha kwanza, umekwenda kuangalia jinsia ya mtoto nikiwa nimekwambia wazi sitaki kujua, nataka kukutana naye siku anazaliwa. Hilo moja, halafu unajua wazi hii ni familia ya Andy. Unakuja kupenyeza jina lako hapa katikati ya familia ya mwenzio kama hutaki mimi niondolewe na huyo mtoto mwenye jina lako ni nini?” Andy kimya.

Pius naye akasimama. “Naomba mnielewe jamani! Huyo ndio mtoto wangu wa pekee wa KIUME.” “Ujue Pius umechanganyikiwa wewe!” Mina akamshangaa sana. “Tafadhali Mina. Nataka mtoto wangu akue akijitambua kama nampenda na ni mtoto wangu MIMI.” “Nani amekwambia upitishie mtoto wako kwenye hii familia yetu kama sio fujo ni nini? Nenda kazae mtoto wako na Raza, ndio ukampe hayo majina yako halafu marefu. Ondoka Pius.” “Raza hana uwezo wa kuzaa tena.” “Ujue Pius umechanganyikiwa wewe, nenda hapo kwenye hospitali ya vichaa ukapimwe wewe!” Mina alikuwa akimshangaa sana asielewe.

“Mpaka nahisi nia yako ilikuwa mtoto wa kiume kwa mke wangu Pius! Uliona Mina amenizalia mimi mtoto wa kiume, ukaona akuzalie na wewe mtoto, ukiamini atakuwa ni wa kiume tu.” Andy akaongea kwa kuumia sana. “Jamani mbona hili jina la Pius Junior halina tatizo? Maana kama mnataka afanane na watoto wenu, kumbukeni wote ni kina Ruhinda.” Hakutaka hata kujibu shutuma, akaendelea na hoja ya jina kwa mwanae.

“Unaondoka au nimpigie simu mzee Ruhinda nimwambie hujaja kwa amani unataka kuvuruga ndoa yangu?” “Mimi naondoka Mina. Ila naomba mnifikirie na mimi.” “Nakuhakikishia Pius, kwa namna yeyote ile utakayosababisha hapa ndani pakosanike amani sababu ya huyu mtoto ambaye unataka aanze kuonekana ni tatizo wakati mtoto wangu sio tatizo, ujue atakuwa huyu mtoto bila kuwa na mahusiano na wewe kabisa.” Mina akamtisha.

“Basi Mina, nimeomba tu. Naomba na wewe ufikirie.” Pius alikuwa ameshafika mlangoni. “Huyu mtoto atakuwa kama Ayan, na kama mtoto wa hii nyumba. Acha kuanza kutuwekea hekaheka zisizo na sababu.” “Basi kama alivyoniruhusu Andy, nikimpata daktari mzuri wa wakina mama, nitawataarifu ili uanze kwenda huko. Nitazungumza naye pia anishauri ni wapi utajifungulia. Sitaki kutokee kosa lolote. Nataka siku hiyo akili na mawazo ya kila atakayehusika kwenye kujifungua kwako viwe kwako tu na mtoto. Na mimi nitakuwepo siku hiyo ili kuhakikisha hakuna uzembe. Naamini katika hilo ni sawa jamani! Mtoto wangu azaliwe na mimi nikiwepo.” Mina akabaki kama ameduaa kwa muda.

“Njoo kwanza ndani.” Mina akamvuta mkono mpaka ndani. “Kaa hapa.” Pius akakaa. Mina akachukua simu ya Andy, akampigia simu mzee Ruhinda. “Ni mimi baba.” Mina akajitambulisha mara mzee Ruhinda alipopokea na kumuita Andy. “Hujambo Mina mwanangu?” “Mimi ninashida kubwa sana baba yangu. Hapa nilipo, nahisi kuchanganyikiwa.” “Nini tena mama?” Mzee Ruhinda akamuuliza kwa upole.

“Pius anataka kunivunjia tena ndoa yangu, baba.” Mina akaanza kulia. “Tulia kwanza unieleze. Tulia kwanza mama.” “Ulisema anakuja kuomba msamaha, lakini hajaja kuomba msamaha. Amekuja kuanzisha familia yake ndani ya FAMILIA ya mwenzie.” “Hapana Mina! Mbona mimi nimeomba tu!” Pius akaongea kwa unyenyekevu.

Akaenda kumpokonya simu Mina. “Baba, mimi sijafanya fujo. Nimeleta maombi yangu tu!” Pius akajitetea. “Hayo maombi anayoomba baba, ni yakumchanganya tu Andy. Ananiharibia mahusiano ya huyu mwanangu na Andy. Anataka mtoto wangu azaliwe aonekane tatizo humu ndani na si baraka.” “Mpe simu Mina.” “Naomba upokee na simu yangu baba.” Pius akarudisha simu kwa Mina na yeye akampigia simu baba yake. Wakaweka kwenye conference call. Andy kimya. Akiwaangalia.

“Naomba utulie tuzungumze mama.” “Siwezi kutulia baba! Pius ananiharibia kwangu wakati akitoka hapa, anarudi nyumbani kwake, kwa mke wake na watoto wake!” “Naomba unisikilize na mimi baba. Mina ana mtoto wangu wa pekee wa kiume. Nimeomba ajifungulie sehemu nitakayotaka mimi. Hilo hata Andy amekubali. Nikaomba wampe jina la Pius Junior Ruhinda na siku akijifungua niwepo.” “Sasa hebu fikiria baba, inakuaje hiyo yakumpa mtoto jina la Pius Junior katikati ya familia ya Andy kama sio kutaka mtoto wangu aonekane ni tatizo humu ndani na kuchanganya watoto wa humu ndani?” Mina akamuuliza mzee Ruhinda huku akilia.

“Mbona hilo ni jina tu baba!? Lina shida gani?” “Lakini wewe ulitoka hapa kwa makubaliano unakwenda kuomba msamaha Pius! Hujaweka mambo sawa, unaanza kupeleka mahitaji yako! Hivi unatambua kwamba umekosa na unahitaji kuwapa muda wenzio wajenge imani tena na wewe?” “Basi baba. Inawezekana nimewahi sana.” “Hata baadaye, huyu mtoto hataitwa jina lako humu ndani.” Mina akaweka msisitizo.

“Tafadhali fanya lililokupeleka Pius. Sitaki uharibu huko kwa mwenzio.” Mzee Ruhinda akamtahadharisha Pius. “Ndilo analolifanya hapa baba. Hata msahama wenyewe bado kwa Andy hata hajapewa, ameenza kuleta mahitaji yake! Halafu nilimwambia asizungumze na mimi mpaka aende akazungumze na mama pamoja na Ron. Lakini anazungumza na mimi wakati ameniharibia mahusiano yangu na mama yangu, hilo hajali!  Naomba umwambie aondoke tu. Tafadhali baba. Mimi mwenyewe nitazungumza na Andy.” Mina akawa analia.

“Naomba kuzungumza na Andy, Mina. Nikiwa nao wote hao. Nataka amani.” Mina akamsogelea Andy huku akifuta machozi. “Baba anataka kuzungumza na wewe.” Andy akapokea. “Baba!” “Vipi Andy?” Mzee Ruhinda akauliza kwa kujali. “Sijui baba! Hakika sielewi!” Andy akajibu kwa kuchoka. “Nataka kwanza amani.” “Unategemea kutakuwa na amani gani baba, wakati Pius yupo katikati ya ndoa yangu!?” “Nisikilize Andy. Hiki kitu kimekuja wote hatukukitegemea. Kinashitua na kuumiza sana. Tafadhali naomba tujipe muda wa jinsi gani ya kukikabili.”

“Pius, naomba waache kwanza. Kwa leo naomba omba msamaha tu, ondoka. Waache kabisa.” “Sawa baba. Lakini nilishaomba msamaha.” Pius akajieleza kwa upole. “Andy umesemaje?” Mzee Ruhinda akakuliza. “Nimemsikia baba.” Andy akajibu kwa kuumia pakatulia kidogo. “Andy?” Baba yake akataka aendelee. “Sijui baba, Pius haonekaniki kama alikosea wala kujutia alichofanya! Pius ALIKUSUDIA kuzaa na Mina, baba! Sasa hivi ndipo nakumbuka vile Pius alivyokuwa akitaka mtoto mwingine akisema anauhakika kama Raza asingekuwa na matatizo, pengine angemzalia mtoto wa kiume. Nahisi ukaribu wa Pius kwa Mina, aliufanya makusudi ili amzalishe mke wangu.” Andy akalalamika.

“Pius hajakosea baba! Naumia kuona amemchagua mke wangu kumzalia mtoto.” “Naomba hayo mengine muachie Mungu, Andy. Fanya kwa nafasi yako.” “Sawa baba.” Akakubali Andy akisikika na maumivu bado. “Haya Pius naomba uondoke bila hata kuongeza neno, au hata kuaga. Nashauri acha kwanza patulie.” “Sawa.” Pius naye akakubali kuondoka bila kukanusha tena shutuma za mdogo wake. Ikawa ni kama aliyekubali zile shutuma. “Namaanisha hiyo ‘sawa’ niisikie ukiwa nje kabisa ya hiyo nyumba.” Bila kuongeza Pius akatoka kimya kimya. Andy akakata simu. Wakabaki pale ndani wamezubaa.

Mina kwa Andy.

Mina akamshika Andy mkono mpaka chumbani kwao. “Naomba nisikilize Andy. Naomba usichoke kabla huyu mtoto hajazaliwa. Najua kitendo ni kibaya. Lakini huyu mtoto hakuchagua azaliwe hivi Andy! Ni kama vile Ayan hakuchagua azaliwe na mimi pamoja na wewe. Nakuomba uwe na mimi katika hili.” “Sijui ndio itakuaje Mina!” “Hata mimi sijui mpenzi wangu. Lakini najua sisi tunapendana. Si ndiyo?” Mina akamuuliza kwa upendo.

“Au umeshaona hamna jinsi tukaendelea tena?” “Hapana. Ila naona kama itakuwa na mchanganyiko fulani hivi!” “Labda kama mimi na wewe hatutakuwa upande mmoja. Nitahakikisha huyu mtoto anakuwa akijitambua hapa ni kwao na sisi ni wazazi wake wa kwanza. Sitafanya kitu chochote bila kushauriana na wewe. Nataka mimi na wewe tusigombane kwa ajili ya huyu mtoto Andy. Huyu mtoto hana hatia. Tafadhali Andy.” “Sawa. Lakini sitaruhusu mawasiliano kati yako na Pius au..” Mina akaanza kumtoa suruali, na kumshusha boxer haraka, akapiga magoti mbele yake na tumbo lake, akaanza utundu. Kichwa mdomoni, mkono ukimchezea taratibu. Akamsikia akicheka taratibu kwa hisia.

“Sasa nitaongeaje Mina!” “Mimi nakusikiliza. Wewe endelea kuniambia yote ambayo huyataki na kuyataka. Atayafuata tu. Nakupenda Andy wangu. Nataka tubakie wote, hili lisitutenganishe tena.” “Kwa mwendo huu, sidhani!” Mina akacheka na kuendelea kumnyonya huku akimchua mpaka akalemewa, maneno hayatoki tena. Andy kwa penzi la Mina huwa hajiwezi. Akachangamkia penzi. Mchana kweupe, Mina akajituma hapo chumbani mpaka akamuona Andy ametulia. “Kabla yakujifungua si tutakwenda mapumzikoni?” “Lazima Andy. Fungate ya pili.” “Nahitaji Mina! Bado sitosheki, naona kama tunabanwa! Muda na mazingira. Lakini tukienda sehemu, tunatulia huko kwa muda mpaka akili iamini wewe ni wangu na hakuna wakukutoa kwangu.” Mina akamdaka midomo, kissing zikaendelea.

Pius kwa wazazi.

Pius alimuomba baba yake kwa magoti amsindikize kwa mama yake Mina. Ikabidi Mzee Ruhinda ndio ampigie simu mama Ron, amuombe kikao. Mama Ron akiwa anajua ni kuhusu Andy kurudiana na Mina, akakubali kwa heshima. Akawatayarishia juisi na nyama tu za kukaanga za kuku ambazo alizikaanga vizuri sana. Ilikuwa ni siku ya jumamosi jioni kama kwenye saa kumi hivi.

Pius alisindikizwa na wazazi wake wote wawili. Walimkuta Ron na mama yake wakiwasubiria. “Karibuni kwanza chakula.” “Naomba nikuombe kitu mama Ron. Tafadhali tusikilize kwanza ndipo utukaribishe chakula chako.” Mama Ron akacheka. “Mimi naona kama kuna kupigana kwenye hayo mazungumzo, tupigane tukiwa angalau kuna kitu tumboni, mama Ruhinda.” Akalazimishia wageni wao, wale kwanza. “Hata hivyo ni chakula tu kidogo. Mjitafune msiondoke bila hata kula.” Wakahamia mezani.

Mina alishapabadilisha kwao. Mama huyo akawa ameshaingiwa na ustaarabu wa visu na uma. Glasi nzuri alishanunua akiwa na Mina Ruhinda. Makochi na meza safi yakulia, tena za kioo nzuri ya thamani. Mwanae alimnunulia kipindi yupo na Andy mwanzoni kabisa. Pesa ya Pius nayo ikaongeza nguvu. Nyumba hiyo ikawa imesakafiwa vigae safi na madirisha yakawekwa aluminium tupu, nje akaweka madirisha ya urembo wa vyuma. Safi.

Watoto hao wakashirikiana, wakaweka ukuta, chini kukajengewa matofali mazuri mpaka getini. Kwa kifupi Mina aliwekeza kwao. Ndani na nje pakavutia haswa. Ndio maana Mina hakuamini siku anafukuzwa pale na mama yake. Ni kama alipajenga upya akisaidiwa na Ron, tena kidogo tu. Ila wazo la nini kifanyike hapo alikuwa ni Mina.

~~~~~~~~~~~~~~

Basi kina Ruhinda wakaandaliwa kwa hadhi yao. Meza safi mpaka na napkins. Wakala lakini wakawaona sio kama wanavyojitahidi kuwachangamkia wao! Wakawa wamepoa mno! Hata wao wenyewe wakawa hawaongeleshani. Ron na mama yake wakaona watulie. Wakajua kuna kubwa lililowaleta.

Wakamaliza, Ron akasafisha, wakahamia sehemu ya sebuleni. “Kwema?” Akauliza mama Ron. “Naomba kwa heshima yangu tu, mama Mina, umpe nafasi Pius, ajieleze.” Akaanza mzee Ruhinda, mama yake kichwa chini. “Karibu baba.” Mama Ron akamkaribisha kwa moyo mweupe akijua wema na upendo wa Pius. Alimjali sana Mina hata yeye alikuwa akilijua hilo. Na alishafika hapo mara kadhaa kuwaleta Mina na mwanae au kuwachukua akiwa na zawadi tofauti tofauti kwa mama huyo.

Vyakula mbali mbali au hata matunda. Hakuwahi kufika hapo mikono pitupu. Kwa hiyo walifahamiana kwa karibu tu kama Andy, ila Pius alikuwa na ucheshi zaidi, Andy mkimya. Walikuwa wakizungumza na stori hata za kazini kwa mama Ron, huko kwenye shule anakofundisha na kutaniana kwa hili na lile.

~~~~~~~~~~~~~~

“Siku ile matokeo ya Mina yalipotoka.” “Matokeo yapi tena!?” Akauliza mama huyo mwalimu. “Yale ya chuo.” Akajibu Pius. “Ooooh! Na nilisahau kuwashukuru. Najua na wewe ulimsaidia sana kumaliza shule yake. Na wazazi pia. Nashukuru jamani! Najua bila wote kuingilia kati, pengine asingemaliza. Asanteni sana.” Akashukuru mama Ron kwa kumaanisha, lakini kimya. Akashangaa mbona hawaitiki, wanyonge!

“Sasa siku ile nikasema kwa juhudi alizofanya Mina, tununue champagne. Nikanunua yenye kileo, tukanywa. Wote tukalewa ndipo nikajisahau nikalala naye.” Pakazuka ukimya, yule mama akabaki ameduaa nakushindwa hata kupepesa macho.

“Wewe ndiye uliyempa Mina mimba!?” Akauliza Ron kwa mshituko mkubwa. “Kabla sijajibu hilo naomba niseme hivi, hata Mina hakujua kama hilo lilitokea. Alilewa sana. Namaanisha hata hakujua kama tulifanya mapenzi usiku ule, hakuwa akijua. Yaani swala la kuwa ni mjamzito alilijua hospitalini alipopelekwa na Paulina. Na hakuwa akijua hata aliipataje hiyo mimba, mpaka siku chache zilizopita.” Akajieleza Pius akimtetea Mina, akiwa amejawa na wasiwasi sana mpaka jasho lilikuwa likimtoka.

“Ila wewe ulijua kama mimba ni yako?” “Nilijua kwa asilimia 99, kwa kuwa muda mwingi nilikuwa na Mina, Mina hakuwa na mahusiano yeyote yale ya kimapenzi nje ya ndoa yake. Na miezi miwili kabla ya kugundulika kuwa ni mjamzito au mwezi mmoja kabla ya tukio,” “Sema kabla hujambaka.” Akaongea Ron kwa hasira.

“Mina alikuwa kwenye siku zake na aliugua sana na tumbo, mimi ndiye niliyempelekea dawa za maumivu. Maana alikuwa akilalamika siku nzima akashindwa hata kutoka hapo nyumbani. Kwa hiyo najua Mina sio kwamba alishika hiyo mimba kwa umalaya. Ni pombe ilinizidia. Naomba radhi.” Pius akapiga na magoti.

“Nimetoka nyumbani kwa Andy na Mina, nimeomba msamaha kwao. Na nyinyi nimekuja kuwaomba msamaha.” Mama Ron akaanza kulia. “Kweli mwenye nacho anaongezewa na asiyenacho ananyang’anywa kabisa!” Akaongea mama Ron kwa uchungu, akilia. “Yaani katika wanawake woote hawa mjini, ukaamua kwenda kuniharibia mimi ambaye mali yangu ni hawa watoto wawili tu, jamani! Kweli Pius?” “Ni pombe mama yangu. Lakini nimemwambia hata Andy, nitawajibika kwa asilimia 100, na nimeomba kumtunza mwanangu.” “Itasaidia nini kama sio kuongeza tu matatizo!? Yaani kweli Pius wewe umeenda kupenyeza mtoto wako katikati ya ndoa ya mwanangu!”  Mama Ron alikuwa akilia sana. Akajifunika kabisa akizidi kulia kama amepewa taarifa za kifo.

“Natamani ungemchagua mtu mwingine wakumfanyia ukatili huo lakini sio yule mtoto. Mina ndio anatulia kwenye maisha, na wewe ndio ukaamua kwenda kumkatili! Nimehangaika na hawa watoto, imekuwa kama mkosi jamani! Utafikiri mwanangu ndio ameandikiwa matatizo daima!” Mama huyo alilalamika huku akilia.

“Nimekosa mama yangu, na sikukusudia kumtesa Mina milele. Ningeweza kunyamaza kabisa. Lakini sikuwahi hata kumuacha hata dakika moja. Tokea anaondoka hapa nyumbani, nilimtafuta na kuhakikisha anatibiwa. Nikamsaidia pesa ya sehemu ya kuishi mpaka nikahakikisha anapata daktari mzuri hata huko Iringa. Japokuwa sikuwa nimemwambia kama ni mimi, lakini nilikubali kuwajibika. Nikahakikisha simuachi akihangaika na mimba peke yake, mpaka akachukuliwa na Andy, bado nilikuwa nikimtunza.” Pius akajitetea huku amepiga magoti.

“Na nimewaambia nitasaidia kwa kadiri watakavyoniruhusu.” “Wewe unafikiri hivyo ndio unasaidia au unaendelea kumtesa Mina? Inamaana wewe na huyo mtoto mtakuwa katikati ya maisha ya Mina na Andy daima! Huo msaada wako unaosema hapa, niambie utasaidia vipi katikati ya ndoa yao, kama sio utakuwa mwiba daima!?” Mama Ron akaendelea kuuliza kwa kuumia sana akilia kwa uchungu.

~~~~~~~~~~~~~~

Wanasema disco imeingia mmasai, ila wasafari hii, ni mmasai wa uchi.

Mina amerejeshewa ndoa, ila na mtoto wa Pius juu.

Ni hali ya taharuki, hakuna ajuaye chakufanya kwenye hali hiyo.

Akiwa amejaza WEMA kwa wote. Ametenda zaidi ya wote na kila mtu anamjua Pius mtu wa kujali. Sasa je, na huko kwa mama Ron atapokea msamaha, au ndio kutaongezeka kesi kwa shitaka la kumbaka Mina kama Ron alivyotangulia kusema?

Na je ndoa ya Mina mwenyewe, penzi pekee kati yake na Andy, litatosha kuponya na kujenga kwa upya ndoa yao, akiwepo huyo mtoto wa Pius katikati yao?

Usikose kufuatilia sintofahamu hii.

 


CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment