Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com MAPENZI & PESA - PART 4 - SEHEMU YA 44. - Naomi Simulizi

MAPENZI & PESA - PART 4 - SEHEMU YA 44.

Ilikuwa jumamosi iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu, na wengi kutaka kushuhudia harusi hiyo ya mapacha hao wa nje, inayofanyika siku moja, sehemu moja. Lilikuwa tukio la kushangaza kwa wengi waliohakikisha wanapata mualiko kwa kutoa pesa ya kutosha. Iliandaliwa kwa kiwango cha juu sana.

Kwanza wanao oa wenyewe walikuwa na wadhifa wa juu huko kazini, pili walikuwa vijana wa mchungaji wa kanisa la watu wenye pesa zao wanao mpenda na kumuheshimu sana huyo mchungaji. Wakaweka juhudi kumfanikishia harusi ya vijana wake.

Japokuwa mchungaji alitangaza itakuwa ni harusi isiyozidi dakika 45, yaani ibada nzima, kuanzia mwanzo maharusi hao wawili Jelini na Emelda wakiingia, mpaka mwisho wakitoka kama mume na mke, lakini, kanisa lenyewe lilipambwa kwa unadhifu na garama kubwa sana, utafikiri ni harusi itakayofungwa kwa juma zima!

Ukumbi wenyewe walikodi kutokana na wageni wao, kwa hiyo nao ulichukua pesa ya kutosha kwani kulipangiliwa kwa muundo wa harusi mbili. Jukwaa au sehemu yao wanne hao, ilibeba thamani kubwa sana. Kila mwenye macho na kujua tukio hilo, walitaka kuhudhuria.

Junior na Ezra walivaa suti nzuri sana, zinazofanana kila kitu pamoja na pete zao. Emelda na Jelini nao walivaa kila kitu kinachofanana mpaka pete zao zote. Za uchumba na hizo walizotegemea kuvalishwa siku hiyo pia zilifanana.

~~~~~~~~~~~~~~~

Mchungaji alishakuwa amesimama mbele na vijana wake, pamoja na wasimamizi wa kiume pamoja na wakike wanne kila upande wakisubiria bibi harusi hao waanze kuingia, wakitaka kujua wanaingia kwa staili gani.

Kinanda kilipoanza kupigwa, watu wote wakasimama wakitaka kushuhudia. Wakaanza kuingia watoto wakike wawili. Wazuri wakuvutia. Wametengenezwa kwa nadhifu mno. Wote walishika vimto vyeupe, vilivyozungushiwa na rembo za rangi ya dhahabu iliyozidi kupendezesha hivyo vimto vilivyokuwa na muundo wa moyo. Vilibeba pete. Waliingia vizuri, kwa ustadi, wakavutia macho.

Kisha wakafuata vijana wawili, wakiume, safi, wakawa wanavuta kapeti jekundu, kuanzia mlangoni mpaka juu kabisa madhabahuni alipokuwa amesimama mchungaji. Likatanda na kuenea kwenye hiyo njia katikati ya viti. Kisha wakaingia watoto wawili, wakike na wa kiume, wakimwaga maua juu ya hilo kapeti mpaka juu madhabahuni.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Ndipo Mungu anayetengeneza njia pasipo njia. Mungu anayejibu kwa moto. Yule anayefanya mambo ya ajabu ambayo hakuna mwanadamu anaweza hata kuyafikiria. Ampaye amtakaye, na hakuna wa kumuuliza kwa nini! Akamtoa mwanamke aliyekuwa akichekwa na kuzomewa kijijini, akichechemea kwa maumivu ya kipigo cha kudharaulika, manyanyaso na mumewe. Mwanamke aliyekuwa akilala topeni. Njaa ni sehemu ya maisha yake. Hata lugha ya kiswahili hakuwa akiizungumza sawasawa.

Siku hiyo akaingia kwenye majibu ya muujiza uliokuwa ukiombwa kwa kufungwa na maombi si ya siku moja! Ni tokea vijana hao wapo shule ya sekondari walikuwa wakimsihi Mungu kwa ajili ya siku hiyo.

Watu wakiwa wanashuhudia maajabu hayo. Pesa iliyomwagwa kwa ajili ya harusi hiyo, kumbe ni majibu ya maombi yaliyoombwa, na kuishi maisha ya kujikana kwenye tamaa za ujanani. Siku hiyo Ezra na Junior, Mungu wao akiwaheshimisha hadharani, basi na mama Emelda naye akawa mmoja wao. Mungu alimkumbuka mama huyo aliyekuwa akilea hao watoto kwa kilimo, huku ni mgonjwa.

Mwanae naye akaenda kuweka hazina ya kumdai Mungu kwenye nyumba ya mchungaji kwa kutumika bila kuchoka wala kiburi. Baraka alizokuwa amebeba huyo binti hapo, kutoka kwenye kinywa cha mchungaji na mkewe, ziliwaka usoni mwake kama taji aliyokuwa amevaa, na shela ya thamani. Nyeupee kama theluji iliyokuwa imetupiwa vimawe vya kung’aa kama alumasi. Wakati akiingia na mama yake amemshika mkono, ungejua ni Mungu mwenyewe, wala si kazi ya mwanadamu aliye waheshimisha.

Ungedhania mama Emelda, ni mama wa mjini. Mama mchungaji alimuosha na yeye akaosheka. Alivaa kwa thamani, akavutia na binti yake ambaye naye, alijitunza, akikana shida zake na tamaa za mwili za ujanani mpaka siku hiyo Mungu akimuheshimisha kwa kumpa Junior.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Junior akaanza kusugua mikono kwa shauku kadiri Emelda alivyokuwa akiwasogelea, mpaka mchungaji na Ezra wakacheka. Alivutia Emelda kama tausi! Watu walikuwa wakishangaa wasijue aina hiyo ya shela aliitolea wapi huyo Emelda, msichana wa kazi za ndani, asiye na elimu kubwa kichwani, aliyekuwa akitumika upande wa watoto muda wote hapo kanisani wala haonani na washirika wengi useme aliona staili fulani fulani.

Ilikuwa ya kipekee na tofauti sana. Alivuta taratibu gauni lake lenye mkia mrefu, uliotengenezwa kwa unadhifu wa hali ya juu, akiwa amefunikwa na shela ambayo nayo ilining’inia mpaka kuanguka nyuma kwa chini kabisa. Kwa hakika aliwaka.

Mchungaji aliwapokea walipofika pale mbele. Junior naye akawa pembeni ya baba yake. Mchungaji akauliza, “nani anamtoa binti huyu, Emelda, kuwa mke wa Junior?” Mama Emelda akajibu, “Ni mimi.” Kukazuka shangwe hapo. Vigelele. Vijana wakaanza kuimba na kucheza wakati mchungaji akimalizia maneno yake katikati ya Junior, mama Emelda na Emelda.

Junior akamshika kama alivyokuwa ameshikwa na mama yake, akasogea na Emelda wake pembeni, Ezra akisaidia kutengeneza shela na mkia wa gauni. Waliposimama pembeni, Ezra akapanga shela vizuri na hilo gauni.

Junior akamgeukia. “Nina hamu na wewe Emelda!” Akamsikia akimnong’oneza kwa kulalamika. Zilishapita siku 5, hawajaonana. Akamgeukia akiwa bado amefunikwa shela. “Na mimi nimekumiss Junior. Leo tutakuwa wote.” “Nilikuwa nakusubiria kwa hamu!” Emelda akacheka na kuongeza. “Umependeza sana!” “Nafanya kwa ajili yako mpenzi. Wewe umependeza zaidi.” “Asante. Na asante kwa kila kitu.” Wakaendelea kuzungumza wawili hao wengine wakishangilia.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Ukasikika tena mlio uleule alioingia nao Emelda. Kanisa zima wakanyamaza na kugeukia mlangoni kwa haraka wakijua ni Jelini tu. Swali ni je, kama Emelda amependeza hivyo, huyo Jelini mtoto wa mjini, na anayejipenda hivyo, je?!

Wakaona watoto wengine wawili tena, wanaingia wakimwaga maua juu ya hilo kapeti vilevile kama wa mwanzo. Ikawa kama wanaoongezea maua juu yake. Hawakupunja. Yalimwagwa vizuri na kuenea kwenye hilo kapeti jembamba lakutoshea watu wawili kupita kwa wakati mmoja. Zito na zuri ambalo haliwezi kujikunja kwa urahisi.

Ndipo na mama Jema naye, kwa mara ya pili, akapata heshima ya kumsindikiza mwanae kwenye safari ya ndoa. Jelini hakuwa na tofauti na Emelda. Kila kitu kilifanana. Kuanzia juu mpaka chini. Kwa hakika na yeye alipendeza.

Chachu ndogo, huchachua donge zima.

Ikawa mabadiliko ya mtoto mmoja tu ndani ya nyumba hiyo ya kipagani. Waliokuwa hawamuabudu Mungu wala hawana ugomvi na shetani. Maisha yao yanakwenda kwa kadiri mama yao anavyoongoza. Jema alipompa Yesu maisha, haikuwa kazi rahisi. Kukataliwa na kupingwa kwa hali ya juu. Lakini Jema alikutana na Mungu wa kweli. Alionja uhuru na furaha ya wokovu wa kweli.

Akasimamia imani kwa shida. Kutoka kwenye familia iliyokuwa haimjui Mungu wala kuamini kwa mwanamke kuolewa! Yaani kuwa chini ya mwanamke! Yeye Jema akamlilia Mungu wake nyuma ya pazia. Huku akisimama na huyo Jelini, tokea anashinda baa. Akimtunza bila kuchoka huku akimuombea, mpaka hapo mama yake anavuna matunda.

Chachu ndogo ya Jema, ikachachua donge zima kwenye familia yake. Je, wewe, unaleta mabadiliko gani kwenye familia yako?

~~~~~~~~~~~~~~~

Jelini akawa si majibu tu ya Jema, naye akaingia kwenye majibu ya Mungu ajibuye kwa moto. Muujiza wa Ezra. Mungu ampaye amtakaye. Jelini aliyekuwa akibakwa mchana na usiku huku akiteswa na mwalimu wake. Aliyepita kwingi kwenye mahusiano ya wanaume! Kina Kasa! Jelini mshinda baa! Mlevi mchana na usiku! Mwenye mtoto tayari! Eti Mungu huyohuo anayeyajua yote hayo, asimpe Ezra mwanamke bikra, akamkabidhi Jelini.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Jelini aliyejua anachokitaka tokea zamani, japo jamii ilijua anaomba au kutamani kisichowezekana, wake wa peke yake! Nani ajuaye Mungu ana watu wengi? Kwa sababu umezungukwa na waovu, HAIMAANISHI Mungu hajajisazia watu waamini kama kina Ezra.

Vijana waliofanikiwa kwenye maisha katika kila eneo. Wakajitunza. Na kubakiwa na hofu ya Mungu. Mungu hajaishiwa. Bado kina Joshua, Junior na kina Ezra wapo katika ulimwengu huu huu wa wanaume waliokosa uaminifu.

Kama Jelini angekata tamaa. Na kusikiliza wengi, pengine asingeishia na Ezra siku hiyo akiwa anasubiriwa na ndoa yenye msingi imara, Yesu kristo. Haimaanishi hawatapitia majaribu kama wanandoa wengine! Hapana. Lakini msingi wao utabaki imara.

Na ili kumpata Ezra, na kile alichokiamini, Jelini ALIBADILI maisha yake kabisa. Alirudi kanisani. Akawa kama wao. Kufunga na kuomba, na kuhakikisha yupo nao kanisani kila inapolazimu. Si kazi rahisi kukana nafsi na kufuata njia nyembamba inayosonga, njia ya uzima, haswa ukiwa umeshaishi maisha ya kujirusha kama Jelini. Kutoka kukesha klabu mpaka kukesha kanisani!

Akikana hisia nzito za penzi la mwanzo kabisa, penzi la Colins aliyerudi na kumkuta alishatoa ‘ndiyo’ yake kwa Ezra. Yote hayo alifanya akiwa ameshajua anachohitaji, akapata na watu waliosimama naye kumkumbusha ni nini bora na nini alitaka, kina Jema, mpaka siku hiyo Mungu alipo mzawadia na yeye.

~~~~~~~~~~~~~~~

Furaha ilizidi kuongezeka kwa kadiri alipokuwa akimsogelea Ezra. Kulijaa shangwe na vigelegele, lakini wawili hao walibaki wakiangaliana wao tu. Alijawa checko ndani ya shela yake ungeweza liona. Macho kwa Ezra.

Akashindwa kuvumilia, akampungia mkono taratibu akitumia mkono wa kulia ambao hakuwa ameshikwa na mama yake. Ezra naye akajikuta akimpungia mkono. “Nakupenda Jelini.” Akajikuta akisema. Jelini akazidi kucheka ila aliweza kumuelewa, alisoma midomo yake. “Na mimi nakupenda Ezra.” Akarudisha wakiendelea kusogea mpaka walipowafikia pale juu madhabahuni.

~~~~~~~~~~~~~~~

Hapo napo mchungaji akamuuliza mama Jema kama alivyo muuliza mama Emelda. Alipojibu na Ezra kupokea ule mkono, tayari Junior alishafika hapo nyuma ya Jelini kumsaidia mkia wa gauni. Kukawekwa mazira ya kuwa na nafasi ya kutosha hapo katikati. Jelini akiwa ameshikwa na Ezra, Junior akisaidia kubeba gauni la Jelini asijikwae au kuanguka huku wakisogea mpaka pale alipokuwa amesimama Emelda.

Wake zao katikati, wao pembeni yao. Akamchungulia Emelda, na kumfinya kidogo. Uchokozi mpaka kanisani! “Jelini!” Emelda akamgeukia akicheka. “Tulia bwana!” “Upo serious sana bwana.” Wakaanza kuongea wakati walishinda wote saluni wakipambwa. Wameachana kwenye limousine hapo nje ya kanisa. Cheko limemjaa.

“Umemuona Junior lakini?” “Kapendeza sana mpenzi wangu.” “Kama Ezra.” Jelini akadakia kwa haraka. Wakacheka, Junior na Ezra wakawachungulia pale katikati. “Tupo kanisani Jelini!” “Ni mkeo huyo ndio ameanza, sio mimi.” “Jelini!” Akashangaa Emelda, wote wakacheka wakijua ni Jelini tu asiyeweza kutulia wala kunyamaza.

Watu wakiendelea kushangilia, wanne hao mbele ya mchungaji walikuwa na yao mpaka aliposikika mchungaji akisema, “Amen, Amen.”

~~~~~~~~~~~~~~~

“Hii ibada ni ya kuwaombea baraka hawa wanne. Kama yupo mwenye kizuizi, aseme sasa lasivyo asisema daima. Maana atakacho kiunganisha Mungu hii leo, mwanadamu yeyote, hata hawa wanne wenyewe, asikitenganishe.” Shangwe na vigelegele wakijua ndio ibada imeshaanza hivyo. Akaomba ukimya wa dakika tatu, kuwapa nafasi watu wenye kipingamizi.

Kimya mpaka muda ulipoisha. “Kwa ukimya huu, inamaana nina kibali cha Mungu na serikali kufungisha ndoa hizi.” Vigelegele. Kelele na shangwe.

Kama waliokuwa wamejipanga, bila kuambiwa. Kila mmoja akamgeukia mwenza wake na kushikana mikono baada ya mabwana harusi hao kusaidia maharusi hao kutengeneza shela zao. Wao ndio wakawa waoaji na haohao nao wakawa wasimamizi wa wake zao.

Watu wakazidi kuvutiwa na jinsi wanavyofanya kwa ustadi. Mchungaji akashuka kutoka mimbarini na kuwasogelea.

“Ezra!” Wakamsikia mchungaji akimuita Ezra. Akajua ni nafasi yake. Akashuka kiapo chake mbele ya kanisa, akiwa anamwapia Jelini. Alitengeneza kiapo kizuri sana. Kwa hakika kilivutia. Watu walishangilia sana.

“Junior!” Mchungaji akasikika akimuita Junior, wakashangaa sio Jelini. Junior akaanza kwa kusema, “Emelda!” Akarudia kiapo kama cha Ezra. Neno kwa neno mpaka wanawake zao wakashangazwa. Kama waliokuwa wamekiandika pamoja na kukikariri. Watu walishangilia sana. Ndipo akaja Jelini, kisha Emelda. Wawili hao hawakuwa wamejipanga kwa pamoja.

Kila mmoja alitoa chake. Emelda yeye alisema kwa kifupi tu. “Nakupenda Junior. Nakupenda kwa moyo wangu wote, mpaka kifo changu.” Junior akamnyanyua mkono wa kushoto uliokuwa wakulia kwake, na kumbusu kiganjani akimwangalia, mwenzie akaendelea. “Nakuahidi kusimama na wewe katika kila hali. Nitakuombea bila kuchoka. Nakuhidi kuwa mwaminifu kwako kama kwa Mungu wangu. Na Mungu anisaidie.” Watu walishangilia sana wakati sauti nzuri na tulivu ya Emelda ikimalizia.

Ndipo akamalizia Jelini. Kanisa zima kimya. “Ezra wewe ni majibu ya maombi yangu ambayo kila mtu aliniambia naomba kitu kisichowezekana. Umekua mwaminifu kwangu. Unanijali na kunipenda kwa dhati. Umeyabadili maisha yangu kwa kusimama na mimi bila kunikatia tamaa, kuhakikisha nakuwa mwanamke niliyeweza kukaa kanisani na kuweza kumuomba Mungu peke yangu.” “Usilie sasa.” Ezra akasikika akimtuliza kwa upendo.

“Basi hapo ataharibu vipodozi vyote!” Akasikika Junior na kufanya watu wacheke kidogo. “Mimi sasahivi sijali.” Jelini akajibu na kuendelea akisikika akitokwa na machozi. “Umenitoa mbali Ezra, tena bila kunichoka wala kunikatia tamaa. Umenivumilia ukionyesha uthamani wangu hata wakati mwingine kwa wengine ilipokuwa haileti maana.” “Nakupenda Jelini.” Ezra akamjibu na kumfuta kabisa machozi.

“Na mimi nakupenda Ezra. Nakupenda sana mpenzi wangu. Nakuahidi kuwa mke mwema kwako. Nitakuwa mwaminifu kwako. Kamwe sitakusaliti. Nitakuwa rafiki mzuri zaidi ya Junior!” “Jelini!” Akasikika Junior akihamaki, wote wakacheka mpaka Jelini mwenyewe.

Kisha akaendelea. “Katika magonjwa, shida, huzuni, jua Jelini wako atakuwa na wewe. Hata ukifukuzwa kazi, ujue mimi…” Junior akawa wa kwanza kucheka. “Jelini!” Junior akasikika. Watu wote wakazidi kucheka. “Kweli! Hata kama Ezra wangu akiishiwa kila kitu, ajue amejiwekea hazina yake kwangu.” Watu wakazidi kushangilia.

“Nitakutunza Ezra wangu. Nitakupenda. Nitakuheshimu. Nitasimama na wewe katika kila hali na kila kitu. Nitawaunga mkono wewe na Junior katika maamuzi yenu, sababu nyinyi wawili ni wa kuaminika.” Watu wakashangilia sana, mpaka Junior na Ezra wakapiga makofi.

“Watoto wa Emelda na Junior watakuwa wetu pia. Katika shida na raha, nitaombea ndoa yetu na ya kina Emelda pia, pamoja na watoto wetu Mungu atakao tujalia, akiwepo na Jeremy, na Mungu anisaidie.” Jelini akahitimisha watu wakishangilia mpaka kushindwa kukaa. Kulikuwa na miluzi humo kanisani. Shangwe za aina yake. Mtoa kiapo mwenyewe ni mrembo Jelini! Mungu ampe nini Ezra! Kichwa kikazidi kuwa kikubwa akimshukuru Mungu wake.

Mwishoe akasikika mchungaji. “Mungu wa mbinguni awaabariki nyinyi na watoto wenu. Mkono wake usiondoke juu yenu na watoto wenu.” Wanne hao waliposikia tu hivyo, wote kama walioambizana, wakapiga magoti kwa haraka mikono juu. Mzee alitamka baraka hapo, wakajua ndio ibada inahitimishwa. Kimya kikatanda kanisa zima, kila mtu akanyoosha mkono kwa maharusi hao waliokuwa wote wanne wamepiga magoti.

Mchungaji alitoa baraka utafikiri hatakuja bariki tena! Aliombea safari yao nzima, ndipo akamaliza na “Ameni”. Watu wote wakaitika. Ndipo maharusi wakasimama.

“Sasa mmekua mke na mume, ruksa.” Wakageukiana na kiss zikaanza hapo mbele ya watu wakishangilia sana. Ikawa ya stara, watoto wa mchungaji hawakufanya mengi. Maandalizi yalikuwa nyuma ya pazia.

~~~~~~~~~~~~~~~

Wakati Jelini anatoa viapo siku hiyo, ndio ilikuwa maandalizi ya kumrudisha Kamila alikolelewa. Kina Komba kujitambulisha huko kwa masista, na kusema lengo la kutaka kumuoa huyo Kamila. Mzee Komba aliona afanye hivyo kuliko kuolewa kimyakimya. Kwamba baada ya hapo na taratibu za huko kwa masista kukamilika ndio vikao vya harusi vianze na Colins naye apate mke.

~~~~~~~~~~~~~~~

“Junior na Ezra, kabla hamjatuacha kwa mwezi mzima naombeni wimbo mmoja kwa ajili ya kumshukuru Mungu kukamilisha hii safari.” Akasikika mchungaji na kufanya wanao wajua hao kwa uwimbaji, kushangilia sana.

“Jamani, kuona wamesimama hapa mbele yenu hivi, hawa wawili na hiki walichokifanya hapa, na hawa wake zao hawa, hakika haikuwa kazi rahisi hata kidogo. Huu ni ushuhuda naona mama yao ndio atakuja kushuhudia siku nyingine, maana hawa wawili wanaweza wasieleze ukweli wote.” Junior na Ezra wakacheka kwa masikitiko.

“Kwani ni uongo? Mtafunga hata tatu kavu. Mnajinyima nao. Mnamlilia Mungu. Akijibiwa mmoja ujue hayo maombi bado hayajajibiwa wala hawatafurahia. Unabakia na kazi ya kubembeleza na kuwaambia, tushukuru kwa kila jambo! Napo wala havisaidii. Unalaumiwa weweee, utafikiri wewe ni Mungu! Bora mje hapa mnisaidie kumshukuru Mungu wangu. Maana katika hili, hana deni. Au mnasemaje? Si wake wazuri hawa?” Wakawaachia wake zao watu wakishangilia haswa.

Junior akashika kipaza sauti na kwenda kukaa kwenye kinanda. Mchungaji mwenyewe akachukua gitaa la bezi. Ezra akachukua gitaa la kawaida, kiziwanda wa mchungaji, Noah, kwenye ngoma. Zilikuwa shangwe, kelele, hawakutegemea.

“Acha tuwafaidi kwa mara ya mwisho kabla kawajaondoka hapa kanisani. Nishajua nitakuwa na ibada nne, bila wao. Acha watuage. Na nimewashitukiza makusudi wajue japokuwa wameoa, bado ni watumishi. Jumapili ya tano kuanzia sasa, watahitajika hapa kanisani na wake zao, asubuhi na mapema kabla wengine hawajafika hapa.” Akasikika mchungaji na kufanya watu washangilie zaidi. Tayari wakajua wanne hao wana fungate la mwezi mzima.

“Wao na wake zao, bila kukosa. Si ndicho wake zao walicho tuahidi hapa?” “Ndiyoooo!” Wakazidi kushangilia. Jelini na Emelda wakazidi kucheka.

“Sasa tuone vitendo. Utumishi wa waume zenu, ni wenu.” Akaongeza mchungaji na kuanza kupiga gitaa watu wakishangilia. Kwa hakika ilipendeza mno. Junior aliimba vizuri, akisindikizwa na vyombo vya mziki kana kwamba walikuwa wamejipanga kutoa hiyo sadaka ya sifa kwa Mungu, kumbe walishitukizwa tu, akili ilishakuwa fungate.

Watu walicheza mpaka kuvua viatu. Ibada ikageuka kuwa ya sifa, hata wafanyakazi wenzao wengine wasio kwenda kanisani, siku hiyo walijikuta kanisani wakimsifu Mungu na wao. Ikapendeza sana.

Fungate.

Waliposikia alichokifanya Kumu siku ya kwanza ya ndoa yao, wakakusudia kuiga. Baada ya watu kula na kunywa ukumbini, wanne hao wakaagwa rasmi kama mke na mume. Wakakimbilia kwenye limousine, kila mmoja na wake, kissing za nguvu zisizoisha mpaka wakashushwa majumbani kwao.

Zikaendelea kissing mara tu walipoingia ndani. Nyumba yenyewe iliandaliwa vilivyo. Maua yalimwagwa kuanzia mlangoni mpaka chumbani.

Sasa huku kwa kina Jelini, wao mambo yao yakaendelea. Jelini kashazoea mchezo na alishakusudia kumfurahisha Ezra vilivyo. Mzoefu. Siku ya mwisho Ezra alipokwenda nyumbani kwao kutengeneza, waliachana kwenye gari kwa ahadi ya kuweka kumbukumbu kwenye usiku wao wa kwanza. Na walipokuwa ukumbini Ezra alimnong’oneza akimdai. Jelini akamjibu yupo tayari kumlipa. Hapo hapakuwa na maneno, vitendo tu.

Shela ilishatolewa tokea hawajapandisha ngazi. Hapo Jelini alikuwa na chupi tu na sidiria. Walipofika tu juu, akamshusha suruali akiwa amesimama katikati ya chumba, kwa mara ya kwanza Ezra akapata midomo ya mwanamke. Ni vile alijikaza kiume, asitie aibu, lakini Jelini mwenyewe alijua anampa raha kwa ute uliokuwa akimtoka.

Alimnyonya huku akimchezea kokwa vilivyo. Sasa na yeye Ezra alikuwa na uchu wa kumtizama Jelini. Yale aliyokuwa akiyaona kwa nje, basi ayashuhudie kwa macho. Mchungaji alishatoa ruhusa. Jelini alipokuwa anapumzika mdomo akimchua kwa mikono akiwa amepiga magoti mbele yake, akamnyanyua na kuanza kiss huku akimmalizia kumvua chupi na sidiria na kumuweka kitandani.

 Akawa akimwangalia huku akimalizia kujivua nguo kwa haraka maana jamaa alichomolewa tu na kuanza kunyonywa. Jelini hakujiachia hovyo hapo kitandani, akajipanga vizuri. Biashara matangazo. Akaupanga mwili wake, kuvutia zaidi. “Jelini wewe ni mzuri!” Akafurahi huyo Jelini, “Na wewe nimekukubali.” Maana mzee wa haja alikuwa hewani. Akajirusha kitandani, safari yao ya mapenzi ikaanzia hapo.

~~~~~~~~~~~~~~~

Sasa huku kwa mabikra wawili romance iliendelea Junior akijua Emelda hajawahi kufanya mapenzi kama yeye tu. Kwa hiyo lazima amtayarishe. Akafanya utundu wote waliojipanga na Ezra mpaka Emelda, na kuongezewa kwenye bag party. Akafanikiwa bao la kwanza, kabla hajampa la pili, Junior mwenyewe akalemewa, ashasubiri tokea anabalehe, na hapo kwa mkewe napo asubiri! Uzalendo ukamshinda. Akaingia akijua mwenzie yupo tayari.

Anamalizia kupiga bao, Emelda anatokwa damu kama mbuzi aliyechinjwa. Junior akapaniki. Akambeba mkewe kumkimbiza hospitalini na kuwapigia simu kina Ezra. Fungate ya nyumbani ikaishia hapo kwa hao wawili. Jelini na Ezra wao wakaendelea kupeana dozi kama kawaida wakimuuguza Emelda.

Naye Junior kwa hukumu akijilaumu pengine alipiga pupa mpaka kumuumiza mkewe, akamgeuza mgonjwa wa kulea kitandani. Kila kitu anampelekea hapohapo, hataki hata atembee asije akajitonesha, damu zikaanza tena. Bafuni, chooni anambeba. Uzuri Emelda hakuwa na mwili mkubwa kama Jelini, anabebeka kiurahisi. Emelda deko, pumu imepata mkohozi. Wala hajivungi kudekezwa.

Hapakuwa na kupika. Walikuwa wakiletewa vyakula. Wakiamka, wanakuta vyakula vimeletwa. Kazi ya mama mchungaji. Kuanzia cha asubuhi mpaka usiku. Kazi ikabakia kula, starehe, hakuna hata kuosha vyombo.

Baada ya siku tano Emelda alipopona kabisa, ndipo wakasafiri sasa hao wanne kwenda kuanza fungate rasmi.

Vai&Bale.

Vai na Bale walibarikiwa ndoa nzuri iliyojaa mafanikio tele ya mali, lakini hapakuwa na mtoto. Walihangaika kupita kiasi kumfanya Vai kushika mimba lakini haikuwezekana.

Alikuwa akifunga na kuomba bila kuchoka akimsihi Mungu akumbuke tumbo lake na yeye aje ashike tena mimba. Alitoa sadaka kila alikoshauriwa, ilimradi tu kugusa moyo wa Mungu bila mafanikio. Hiyo hali ikaendelea kiasi cha kuanza kupunguza furaha kwenye ndoa yao. Majuto na kujilaumu kusiko isha. “Pengine Mungu hajanisamehe.” Hilo ndilo likabakia moyoni kwa Vai.

Wakiwa kwenye hiyo hali, ndipo Bale akakumbushwa moyoni wazo lake la mwanzoni kabisa, na kujirudi hata kumsaidia Vai mkewe aliyekuwa amechanganyikiwa na swala la mtoto huku na yeye akimsindikiza kila mahali bila mafanikio.

“Najua shida ni mtoto. Lakini nataka kujua unataka kunyonyesha au mtoto?” Vai alikuwa kwenye kilio cha uchungu. “Nataka mtoto Bale.” Akamdai mumewe kama Raheli kwa Yakobo. {Mwanzo30:1}

“Basi turudie mpango wetu wa mwanzoni. Tunaanza na mtoto gani?” “Mimi sishiki mimba.” “Zungumza na mimi, kana kwamba ndio umebahatika kuzungumza na Mungu uso kwa uso. Halafu anakuuliza jinsia ya mtoto wako wa kwanza, ungemuomba yupi?” “Wakiume kwanza. Lakini simpangii Mungu.” Akajibu Vai. “Basi tulia.” Akamtuliza mkewe usiku huo, angalau wakalala.

~~~~~~~~~~~~~~~

Bale akaanza kufanya utafiti kwenye vituo vya watoto yatima, akaulizia utaratibu wote na kujiridhisha hatamuumiza mkewe, hata akimwambia kusije tokea kushindikana katikati ya process ya adoption. Alipojiridhisha kwamba wanaweza pata mtoto kwenye vituo vya watoto yatima, ndipo akamwambia Vai.

Hakuamini utayari wa Bale. Alikuwa tayari kwa moyo mmoja. Akampeleka na kuonyeshwa watoto wa pale. Vai akajikuta akipenda kitoto cha mwaka mmoja cha kiume, ndipo safari yao ya uzazi ikaanzia hapo.

Wakwanza alipokaribia miaka miwili, wakaenda kuchukua mtoto wa pili. Napo wakapenda wakiume tena. Safari hii Vai akapatwa hamu ya kunyonyesha kabisa. Wakamchukua kachanga kabisa. Vai akaanza kunyonyesha kama aliyezaa. Wakalea watoto hao wakiume wawili kwa upendo kana kwamba ni wao wa kuwazaa kabisa. Na ndugu wa karibu nao waliwapenda hao watoto, na kuacha historia nzuri kwa walichokifanya.

Nyumba yao ikajawa furaha na fujo zote kama za familia zenye watoto wadogo. Wakasahau kabisa swala la kuzaa au kutafuta kushika mimba kwa Vai. Sex nje nje wakati wote wakipata kimwanya. Hakuna uzazi wa mpango wala kinga, si Vai hashiki mimba! Wakawa wanajiachia.

Akiwa bado ananyonyesha mtoto hajafikisha miezi sita, Vai akaanza dalili za mimba. Akajua ni homoni tu, zinabadilika sababu ya kunyonyesha. Akapuuza. Lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda, vikazidi. Vai hawezi kula chochote na ananyonyesha. Hakuna kinapita kooni hata mate yake mwenyewe, hayaendi.

Akaendelea kupambana na yote. Kazi, watoto wawili, tena wakiume, huku anakazana kunyonyesha. Siku na hiyo Bale akiwa kazini akapata simu kutoka kwa msichana wa kazi kuwa, mkewe ameanguka na kuzimia akiwa anatoka kwenda kazini, mchana. Uzuri Naya alikuwepo tu nyumbani, na ni karibu, akamuomba akamwangalie.

Naya akampeleka hospitalini kwani alikuwa amekaukiwa haswa. Baada ya vipimo, akawekewa maji na kupumzishwa Bale naye akawasili. Kufika na majibu nayo yanatoka, Vai ni mjamzito. “Mwanangu bado mdogo!” Akalalamika Vai akijisau kama alikuwa akitafuta hiyo mimba kwa muda mrefu wa kuchanganyikiwa. Wakati wa Mungu ukawa si wakati wake.

~~~~~~~~~~~~~~~

Jelini na Emelda wakaweka na wao uzazi wao wa mpango. Kuomba Mungu na kushika mimba kwa pamoja na kuzaa kwa pamoja. Kukawa na mapacha wengine wa nje, kwenye familia hizo, mbali na baba zao.

Wote wakaendelea na ndoa zao, na changamoto za mahusiano kama wengine.

~~~~~~~~~~~~~~~

 MWISHO.

Usipitwe Na  Simulizi Mpya,

Love At First Sight.

Huko Utajua Kwa Undani

Ø Kilichompata Mike, Wa Kamila.

Ø Sababu Ya Wawili Hawa Kushindwa Kupata Mtoto.

Ø Penzi La Mill Kwa Pam. Mwanzo Wao na jinsi ilivyo rahisi KUBOMOA lakini huchukua muda KUJENGA. Na mengine mengi ya kuburudisha na kujenga.

§  KARIBU.


CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment