Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com MAPENZI & PESA - PART 4 - SEHEMU YA 35. - Naomi Simulizi

MAPENZI & PESA - PART 4 - SEHEMU YA 35.

Mikono ya Colins mgongoni ndiyo iliyomtoa usingizini. Alikuwa akimpapasa taratibu nyuma ya mgongo mpaka pembeni mwa mbavuni. Akafungua macho akiwa amelalia tumbo. Akamkuta Colins amejiegemeza kwenye mto, akimwangalia. Akacheka taratibu.

“Kanisani?” “Nimechoka!” Akalalamika. “Naweza kuelewa. Umefanya kazi mfululizo bila kupumzika.” “Pamoja na mapenzi ya jana.” Colins akacheka sana jinsi alivyolalamika. “Kidogo hivyo!” “Mwenzio mimi sijazoea vya muda mrefu. Ilikuwa muda mfupi, unamaliziwa na…” Akasita na kubadili alichotaka kuzungumza.

“Wewe unachukua muda mrefu sana, bwana!” Colins akazidi kucheka. “Ila sema vinanoga.” Hapo akamfanya Colins acheke kwa sauti. Akajificha na mto. “Basi leo sikugusi kabisa. Nakuacha upumzike, na kesho sita…” Kamila akashituka sana na kujitoa chini ya mto.

“Mimi sijasema nataka mapumziko!” Colins alicheka mpaka machozi. “Si umesema umechoka wewe?” “Sasa ndio kutaka mapumziko jamani! Ni ile ya kuchoka vizuri! Mimi napenda kufanya mapenzi na wewe.” Zikaanza kissing hapo. Wameng’ang’aniana.

Akashangaa Kamila anamuachia kisha anaingia ndani ya shuka, akamkamata mzee, mdomoni. Akaanza utundu wa kuchezea na kokwa, huku anamnyonya! Hapo ndio Colins akaelewa kwa nini Mike alikuwa hawezi kulala bila huyo Kamila, na kwa nini alikuwa akimfuata nyuma kama mjinga.

Bwana alimfanyia kusudi! Kama kumkomoa! Mapya na mageni kwa Colins, anagugumia hajielewi. Kucha anapitisha taratibu kwenye vimistari vya kokwa, akazidi kumchanganya. Alipomuhisi anakaribia, maana na ute nao ukazidi kumtoka, akamkalia na kujiingizia.

Safari hii hakuchukua muda mrefu, mzee akasalimu amri. “Haiwezekani Kamila!” Kamila alikuwa akicheka, mbavu hana. “Upigaji gani kelele huo Colins wewe! Kama nyumba ya kupanga, tunafukuzwa.” “Umenikomoa Kamila!” Hana mbavu.

“Hatutoki hapa mpaka nikulipize.” “Mimi wala sikatai.” Colins alicheka, akacheka sana. Hakutegemea hilo jibu. “Kamila!” “Wewe nilipize kwa kadiri ya uwezo wako. Mwenzio napenda.” Colins hana mbavu.

“Sasa unaenda wapi?” “Chooni, kisha bafuni nijisafi kidogo ndio tuje tuendelee. Naona jamaa amekataa kushuka.” “Kamila kwa kujisafisha! Unajitia baridi. Acha..” Akakimbia maana alijua anataka amkataze.

Wakati yupo bafuni, na yeye akaingia. Zikaanza kissing za kwenye shower. Za muda tu huku Colins mkono upo kwa Kamila eti anamsafisha huku anamchezea! Alikuwa akitetemeka miguu maana pia midomo ilikuwa ikipita masikioni, na kumnyonya shingoni. Alikuwa akisisimkwa kupita maelezo.

Safari hii na yeye akapiga magoti akaanza kumnyonya mwenzie amesimama. Kama mtoto wa mbuzi! Miguu ikawa inakosa nguvu, inatetemeka kwa kuchanganywa kwa raha. Akashikilia ukuta, chini Colins ametawala. Hakumuachia mpaka akapiga bao ndio akasimama.

Naye Kamila akainama mbele yake, na mkono nyuma mpaka akampata mzee akaanza kujiingizia. Akaelewa mchezo unaendelea. Kwa hali ilivyokuwa, katikati ya shower, maji yanaendelea, utelezi mzuri, Colins akaendeleza mchezo amemshikilia kiuno anapata raha.

Kamila akadhania atamaliza, lakini akafunga maji na kumtoa hapo akimkisi na maji, mpaka kitandani wameloa chapachapa. Akamuweka chali. “Nataka nimalizie nikiwa nakuona, Kamila.” Akajilaza chali. Akamlalia kifo cha mende lakini akamkumbatia kwa mkono mmoja. “Naomba midomo yako.” Hapo anabembeleza, akamgeuzia kichwa.

Akachomeka, mkono mwingine akapata kiganja chake. Akapitisha vidole huku amemkumbatia. Mchezo uliojaa penzi zito, ukaendelea. Anamsugua ipasavyo. Kamila anasikia raha, Colins ile hali ya hisia pale ikazidi kumfurahisha. Ile kusuguliwa kiharage kwa muda, huku amekumbatiwa. Wameshikana mikono, wananyonyana midomo kwa aina yake, mchezo unazidi kuchezwa taratibu.

Kamila akasikia furaha na ulinzi wa kipekee akajiachia hisia zote. Wakati anafika kileleni na Colins naye akawa anapandisha. Alipomaliza tu, na Colins naye akawa anamalizia. Hakutoka kwa haraka maana Kamila alikuwa akiendelea kumbana huku akimalizia.

Akabaki amemlalia. Kamila amemkumbatia kwa mikono yote miwili anampapasa mgongoni huku anambana vilivyo akimalizia. Colins alikuwa akisikia raha ya ajabu mpaka akamaliza ndipo akajitupa pembeni na kumvutia juu yake na kumkumbatia vizuri kwa upendo. “Asante Kamila.” “Na mimi nimefurahia. Sikujua kama kifo cha mende inaweza kuwa tamu hivi! Asante.”  Wakabaki wamekumbatiana wakihema kwa nguvu.

~~~~~~~~~~~~~~~

“Nikuulize kitu Kamila?” Akatingisha kichwa akikubali akiwa amemlalia kifuani, anapitisha mikono mwilini mwake. “Kuna kitu umekirudia mara nyingi sana juu ya mapenzi. Ni katika kufahamiana vizuri na kujifunza pia. Utakuwa sawa nikikuuliza juu ya Mike?” Kamila akakaa sawa. Tena akajivuta kabisa kwenye mto wake akimwangalia ila kwa wasiwasi kidogo.

“Ulitaka kujua nini?” Colins naye akajiweka sawa, akamgeukia kabisa akiwa amelala kwenye mto wake na yeye. “Sio jambo baya. Nataka nijifunze kitu hapo.” Akaendelea. “Unaonekana wewe ulitulia na Mike tu. Hukuwahi toka nje ya mahusiano, japo ni kama hapakuwa na muda mwingi sana wa ufanywaji wa mapenzi. Kama nimekuelewa vizuri, au?”

“Acha nikwambie ukweli Colins. Kadiri siku zilivyokuwa zikienda na Mike, alikuwa akibadilika mpaka ikabidi kwenda kutafuta ushauri wa madaktari. Mapenzi yale ya kuiba ya shuleni, alikuwa yupo vizuri sana. Kama hivi wewe tu. Unafanya mapenzi mpaka unaridhika kabisa. Alikuwa akiweza kukuridhisha muda wote kwenye ufanyaji mapenzi tu.”

“Tulipoanza kuishi pamoja, akaanza kama utani tu. Mara wakati mwingine ashindwe kabisa, mara wakati mwingine anaweza ila kwa muda mfupi sana, kisha kunimalizia kwa romance. Hakuwahi kuniacha hivihivi. Sasa ile ikawa inamnyima raha yeye mwenyewe. Tukafikiri ni kazi nyingi, ndio tukaanza mtindo wa kuwa tukisafiri kwa mapumziko, lakini nako huko haikuwa ikisaidia.”

“Ndipo tukaenda kutafuta ushauri wa daktari, maana na mimi mimba zilikuwa hazishiki, anajilaumu yeye, na ziliposhika, zilikuwa zikitoka. Ndio tukaenda kwa daktari, wote hatukukutwa na tatizo.” “Alikuja kupona?” “Hapana. Hiyo hali iliendelea hivyohivyo mpaka mwisho wake.”

“Naomba uwe mkweli kwangu Kamila. Ni kwa nini uliendelea kuwa naye wakati hakuwa akikuridhisha kitandani? Nina sababu ya kukuuliza hili ndio maana nauliza.” “Kwangu Mike alikuwa zaidi ya kunimaliza haja zangu za kitandani! Alinipenda yule mwanaume, kuliko nafsi yake. Ilikuwa ni bora kubaki na Mike, kuliko kuwa na mwanaume atakayeniridhisha mimi kitandani, halafu akaridhishe na wanawake wengine huko nje, na pia asinipende. Akanidharau na mengine mengi kama unavyojua matatizo ya mahusiano.”

“Halafu nilimpenda sana Mike. Sana. Sikuwahi hata kufikiria kama naweza guswa na mwanamme mwingine nikaweza kuridhika. Hivi ulivyokuwa umenishikilia hapa baada ya mapenzi, ndivyo nilivyokuwa nikilala na Mike. Mchana na usiku utakua mikononi mwake. Na ukisikia anakuvuta katikati ya usingizi, ujue umegeuka au umetoka mikononi mwake akiwa amelala, ameshituka na kukuta haupo, ndio anakurudisha.”

“Alinijali kupita nitakavyokwambia. Ni kwa nini umeniuliza?” “Na mimi nilipita kama hapo alipopita Mike, lakini mimi ilikuwa kinyume kabisa. Sikujua kama unaweza pendwa hata kama ukiwa na tatizo kama hilo! Kwangu ilikuwa fimbo. Hakika Love alinitesa yule mwanamke!”

“Pole.” “Hakuna unachoweza mfanyia akaridhika. Na wakati wote atakukumbusha jinsi anavyoteseka sababu haridhiki kwenye mapenzi. Anaweza akatafuta mwanamme mwingine huko nje, pia kosa linakuwa langu.” “HAIWEZEKANI Colins!” Akahamaki. “Acha Kamila. Ndio maana mimi binafsi umenishangaza aisee! Na nafikiri pia umechangia sana kunifanya niwe hivi.” “Kwa nini!?”

“Hivyo jinsi ulivyo Kamila! Huna makuu! Mtulivu! Umejawa shukurani hata kwa kiss la shavu tu!” Akaanza kucheka kwa aibu. “Sikutanii Kamila! Hujui kulaumu! Unaridhishwa na vitu vidogovidogo! Hakika umenitia ujasiri na nafikiri sikuwa na tatizo ila ile hali ya kunyanyaswa. Kusemwa kila wakati na kuonyweshwa sijui au nina kosa,  ndio ilikuwa ikinimaliza nguvu. Lakini wewe umenifanya nimetulia mpaka mawazo, ikanifanya mwili kufanya kazi yake vizuri.”

“Kingine kikubwa umenishangaza, nilipojirudi hujanilaumu kukusukumia mbali nikikuletea Jelini kila wakati! Umenipokea kwa unyenyekevu, kiasi kilichonifanya nikatulia kabisa. Hakika wewe ni Mungu aliye nifuta machozi.” Akafurahi huyo na kuongeza.

“Na ujue sikuachi mpaka uniache wewe mwenyewe kama hivyo alivyoniacha Mike. Mwenzio mimi sio msaliti. Sijui kuhangaika hangaika.” “Na mimi nipo hivyohivyo Kamila.” “Usikimbilie kusema hivyo. Wewe bado Jelini yupo. Akirudi je?” Hapo hakujibu. Akanyamaza kabisa na kumuona amepotelea mawazoni. Hilo akalitunza moyoni ila akamuacha.

~~~~~~~~~~~~~~~

“Tumekubaliana na Mill alete watoto kanisani. Tuwe pamoja. Baada ya hapo awe na sisi wote, angalau watoto wajue watu wengine.” “Kwani sasahivi anafanyaje?” “Ndio amefanikiwa kuwapatia shule zinazoendana na kule walipoishia. Anataka waanze jumatatu. Ila akitoka anawaacha na mtu alimpata kwenye kampuni ya wafanyakazi.”

“Watoto wake hawampendi kabisa. Wanasema hawaelewani lugha. Ila Mill anasema ni tabia tu mbaya ya wanae, kwani alishawaambia wakitaka kitu wawe wanawasiliana na yeye, halafu yeye ndio atakuwa akiwasiliana na huyo dada, ambaye anasema anaelewa kingereza japo kuzungumza inaweza isiwe nzuri sana. Mill anasema kama ingekuwa ni watoto wa kawaida wasingesumbua.”

“Basi tutawataarifu wazazi watukute kanisani. Sisi tuwahi wasije jikuta peke yao tena.” “Hapa sijui kama unavyakula! Ningekupikia kitu chakula harakaharaka kabla ya kuondoka.” “Usijali. Tutakula tukitoka kanisani, halafu tutafanya manunuzi ya vitu unavyovitaka tuje navyo.”

“Kwani tutarudi tena hapa?” “Ninapokwambia siwezi tena ishi bila wewe Kamila, namaanisha. Kama utakataa kurudi hapa, ujue nitakufuata utakapokuwa.” Ikamgusa Kamila, akatulia maana ya kutojibu juu ya Jelini ilishamtia wivu.

“Nataka kuwa na wewe Kamila.” “Basi tujipange vizuri.” “Unamaanisha nini?” “Nina vitu bado kule kwa wazazi. Halafu sasahivi si kama vile nilivyokuwa na Mike. Sikuwa na watu wazima wakunisimamia kwenye maisha yangu. Nilikuwa nikiishi vile ninavyata mimi na Mike. Sasahivi siwezi tena. Nimeshajenga mahusiano na wazazi wako. Binafsi nawaheshimu sana. Wamenipokea kama binti yao. Siwezi nikajiondokea tu kama zamani. Sijui kama unanielewa?” “Nimekuelewa na nimekuheshimu kwa hilo.” Akafikiria kidogo kisha akaongeza. “Acha basi nitazungumza na wazazi.” Wakakubaliana kwenye hilo.

Watoto Walipa Garama Ya Maamuzi Ya Wazazi.

Walifika kanisani, wakamkuta Mill na wanae wanawasubiria kwenye gari. Safi. Walivyo tu na usafiri wao, walitangaza neema ya kiuchumi. Ila madogo yakakataa kusalimia. Mill alipolazimishia salamu, wa kike, yeye akasalimia. Wakiume aliwatizama. Akawaambia tu, ‘hi’ na kurudisha macho kwenye game yake alikuwa anacheza kwenye simu. Wakaamua kuwaacha.

Wakazungumza kidogo na Mill, kisha Colins akaenda dirisha la nyuma alikokaa mtoto wake wa kiume. Colins akamjaribu. “Una game gani upya?”. Kwa jinsi alivyomuuliza na lugha ya mchezo, fasaha kwake, kingereza kilichonyooka, yule mtoto akamtizama Colins. Ila akamuuliza kwa jeuri. “Wewe unajua ipi?” “Huwa nahakikisha nakuwa na kila toleo. Hata hii waliyotoa juzi ninayo.” Hapo akampata.

“Haiwezekani!!” Akamuuliza kwa kuhamasika haswa. “Ooh yeah! Siwezi kukosa. Inaniongezea uwezo wa kufikiri na kuweka mawazo yangu sehemu sahihi.” Hapo akawa kama amembana. Akatulia kidogo kisha akaongeza. “Game zangu zote zilipotea.” “Hazijapotea. Sema ukweli, usidanganye.” Mdogo wake akadakia kiushari. “Haimuhusu.” “Inamuhusu kama umeamua kumwambia.” Wakaanza kubishana hao ndugu wawili.

“Nimekwambia haimuhusu mtu. Acha kuingilia mambo yasiyokuhusu.” “Trey aliuza. Nishaingilia. Utanifanya nini?” “Eti nini!?” Mill akashituka sana. “Nakuonya Mia wewe!” Akamtisha mdogo wake kwamba asiseme. “Utanifanya nini? Utanifanya nini?” “Miles, nyamaza. Haya, Mia niambie.” Akamgeukia mtoto wake wa kike, huyo Mia.

“Trey alikusanya game zote ulizokuwa umemnunulia Miles akawa anauza ebay. Umeuza zote. Nikamsemelea kwa mama, mama akamuuliza, akakataa. Akanichapa akisema mimi namsingizia mwanaume wake. Ndio Miles alivyoona mama amenichapa sana, akatafuta ushahidi online mpaka akapata. Akamuonyesha mama. Wakagundua huwa anauza vitu vyetu vingi tu. Mama akaniomba msamaha, akasema tusimwambie mtu kama Trey anauza vitu vyetu.”

“Mimi nikamwambia sikubali. Yeye hakuniamini mimi, alimwamwamini Trey. Nikamwambia akija yule mwanaseheria wako, namtuma aje akwambie kule ulikokuwa. Akanipiga tena. Akasema nikisema tu, watakuja kutuchukua pale nyumbani, watatupeleka tukaishi nyumba za watu wengine. Tena watatutenganisha. Akaniambia nikisema sitakaa nikamuona tena Miles, ule ndio utakuwa mwisho wetu wakuja kuishi pamoja. Na huko yule mwanasheria wako atakapotupeleka ndio tutateswa sana. Bora tunyamaze yaishe.” Mill aliumia, aliumia sana, akashindwa chakujibu.

“Halafu Trey alikuwa akimpiga sana Miles.” “Mia! Mia wewe!” “Kwani uongo? Unaogopa nini sasa? Kwani atatufuata huku?” “Shauri yako! Kumbuka mama alivyokwambia.” Hapo wakashangaa ananywea kabisa, mpaka Mill akashangaa.

Akageuka tena. “Mama yenu aliwaambia nini!?” Kimya. “Mia?” Baba yake akazidi kumuuliza. Kimya. Akawa kama ameingiwa hofu kabisa, akanyamaza kabisa, safari hii hakujibu wala kuzungumza tena. Pakazuka ukimya.

“Ni sawa nikimkaribisha kwangu kwa ajili ya kucheza? Inaweza saidia.” Colins akamuuliza Mill kwa kiswahili akijua wale watoto hawaelewi hiyo lugha. Mill alikuwa ameshabadilika kabisa. Macho yamebadilika yakawa mekundu kama anayezuia machozi.

“Una uhakika? Maana watoto wenyewe ni kama hivyo unavyowaona.” “Usijali.” Kisha akarudi dirisha alilokuwa amesimama akimwangalia huyo mtoto. “Hey Miles.” Akamuita taratibu.

“Nina chumba maalumu cha games. Kina kila aina ya game. Ungependa kuja tucheze wote?” Akamwangalia na kunyamaza. “It’s okay.” Kimya. “Au unahofia nitakufunga sana?” Hapo akampata. Na alimfanyia  makusudi. “No way. Wewe huwezi kunifunga. Hata kama sijacheza muda mrefu, lakini wananijua mimi. Nilishafika kwenye level…” Akaanza kujigamba. Akijisifia kwa Colins vile alivyomahiri kwenye huo ulimwengu wao wa games.

Colins akacheka kwa kumtuliza. “Mimi naona tuache muda ujibu. Tutakuona.” Akawa amehamasika kwelikweli. Furaha. Na vile lugha yao wanaelewana, akaonekana kumfurahia Colins.

Kisha akamgeukia baba yake. “Naweza kwenda kucheza naye?” Na yeye akamgeukia Colins na kumuuliza. “Lini unakuwa na nafasi?” “Ijumaa wakitoka shule, mimi na anti Kamila tutakuja kuwachukua. Tunaenda kula, ndio tunakwenda kumtafuta mshindi.” Wakashangaa hilo wamelifurahia haswa. Angalau Mill akatulia.

~~~~~~~~~~~~~~~

Wazazi walikuja wakiwa na Connie. Wakaingia ibadani, watoto wametulia tu. Wakaenda kupata mlo wa pamoja, kwenye hoteli ileile aliyowekewa sumu Jelini lakini Colins akawa ameshatengeneza urafiki na yule mwenye hoteli. Alipapenda tokea mwanzo, akaona madhari yake yangemfaa Mill na wanae. Kwamba watoto wangepata kitu cha kuwafurahisha.

Ila akagundua Kamila amepoa! Akamtumia ujumbe katikati ya kundi hilo la watu. ‘Upo mbali na hapa!’ Akasoma na kumuona anatabasamu. Akamjibu, ‘Nipo sawa tu.’ Wakatulia, macho kwake muda wote. Kisha akamuomba Mill kama wanaweza kuzungumza pembeni. Wakatoka wao wawili wakitembea ufukweni, Kamila akiangalia watoto.

Colins & Mill.

“Samahani sana kwa tabia za watoto wangu.” “Mill, hawa watoto wana nafasi kubwa sana ya kukua. Tafadhali kwangu na kwa familia hii inayokuzunguka sasahivi, huhitaji kujificha wala kuomba msamaha. Sasahivi hawa watoto ni jukumu letu wote. Kama unadhania ni aibu, basi jua ni aibu yetu wote.”

“Inaniuma Colins, inaniuma sana. Sikujua kama walikuwa wakitesa wanangu! Na sijui walikuwa wakiwaambia nini kiasi cha kuwatisha mpaka wanaogopa kuzungumza!” “Muda utajibu Mill. Ninachoona kikubwa wanahitaji uhakika kuwa kule hawatarudi tena, na wewe hutakaa ukawaacha tena. Wakihakikishiwa hilo, utaona wanatulia. Kwa kuwatizama kwa haraka, ni kama wanahofia walipo. Hawana uhakika na usalama wao. Kama wewe upo na hutawaacha tena.”

“Kingine, kumbuka kule mlikokuwa mkiishi, ndugu wa upande wako waliyemuona ni Mike na Kamila. Nao wakapotea. Wakabakiwa na mama yao na watu wake. Hawana uhakika kama ukija ondoka tena, wanabakiwa na nani, isipokuwa kurudi kulekule. Na kingine, wewe unajua waliwaambia nini ulipoondoka? Mahali ulipo?” “Aisee nimerudi na mambo mengi! Yaani leo ndio hata nimejua kama walikuwa wakipiga wanangu na kuuza vitu vyao!”

“Sasa hilo ndilo la msingi. Pata nao muda wao kama wao. Kibinafsi kabisa. Ukiweza shuka kwenye ngazi yao. Unaweza kuwapata kirahisi.” “Unafikiri sijajaribu! Ni kama kumejengwa ukuta katikati yetu, na sijui jinsi ya kuuvunja. Tukiwa sisi watatu hatuzungumzi kabisa, bora Mia huwa anaweza hata sema njaa inamuuma, lakini si Miles! Amebadilika kabisa. Muda wote anajifungia chumbani kwake, na hataki mtu amuingilie.”

“Basi kumbe wazo la kuwatoa sio baya!” “Nimeshangaa wewe amekukubalia! Mkali kwa kila mfanyakazi ninayempelekea. Mkali kwa kila mtu, angalau kidogo kwa Mia ndio anajitahidi naye. Ila si vinginevyo.” “Wape muda, wanaweza badilika mpaka wakakushangaza na wewe.” “Aisee nasubiria kwa hamu sana.” Wakatulia wakiendelea kutembea.

~~~~~~~~~~~~~~~

“Nampenda Kamila.” Mills akamwangalia. Kama akataka kusema kitu, akakwama. “Nataka kumuoa.” Akaongeza. Mills alinyamaza kama aliyeshitukizwa, hakutegemea. “Nataka iwe mapema. Nikimaanisha sitasubiri.” “Utanisamehe kama nitavuka mipaka Colins. Lakini nina deni kwa Mike, lazima nimwangalie Kamila, bila ya kuzembea japo najua umemsaidia sana Kamila, ila ujue nawajibika kwake.” “Na mimi nitaliheshimu hilo.”

“Sasa mbona ni kama nilisikia yupo mwanamke kwenye maisha yako, huna nafasi ya yeyote yule. Iweje leo gafla unaniambia unataka kumuoa Kamila?!” Kabla hajajibu akaongeza. “Si kwa kukutisha, ila Kamila alipendwa na Mike. Mimi na utuuzima huu, sijawahi ona mwanadamu aliyempenda mwanadamu mwenzie kama Mike alivyompenda Kamila. Ni nini nataka kusema?” Colins kimya akimsikiliza.

“Mapenzi ya kuungaunga, jua wazi utamtesa yule binti. Na Kamila ni msichana mtaratibu sana. Namfahamu kwa kuishi naye. Na namfahamu kwa asilimia nyingi kwa kumuona mwenyewe na kuhakikishiwa na Mike. Kama nilivyokwambia, nina deni ambalo siwezi ondoka hapa duniani, sijalilipa. Wewe unaonekana ni mtu mzuri sana. Sitaki tuje tukosane.”

~~~~~~~~~~~~~~~

INAENDELEA.


CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment