Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com MAPENZI & PESA - PART 4 - SEHEMU YA 32. - Naomi Simulizi

MAPENZI & PESA - PART 4 - SEHEMU YA 32.

Ilikuwa bado mapema sana siku hiyo ya jumamosi wakati hatimaye ndoto za Bale, zikiwa zinatimia. Na yeye siku hiyo, kwa mara ya kwanza, akitizamia starehe ya mwanamke. Ilikuwa tafrija ya watu wachache, tena wakaribu na Bale, wale waliongezeka na kumsamehe baada ya uovu mkubwa aliotenda.

Joshua na Geb waliandaa harusi hiyo kwa kiwango cha juu sana. Kitu kidogo, cha thamani. Suti yenyewe aliyokuwa amevaa Bale, ungejua maandalizi yake yameandaliwa na watu walio nazo.

Vai alishafanyiwa shuguli ya fujo, huko kwao Moshi, mama yake alifanya sherehe ya fungulia mbwa, akitangaza neema kwenye uzao wake. Alishatangulia James. Amemuozesha, akabakiwa na mabinti wawili, hatimae kiziwanda naye akawa anaolewa! Basi mama James alijawa majigambo, hata ubahili aliweka pembeni kumsaidia James kuandaa hiyo shuguli ya kumuaga binti yake huko mjini Moshi.

Walikodi ukumbi, vyakula vikawa vingi vyakusaza. Nako huko Vai alipendeza sana, kwani Jema naye alihakikisha wanaandaa vizuri akijua kina Naya nao wamejiandaa.

Nanaa akagawana na mumewe. Yeye akasaidiana na Jema kuandaa mambo ya nyumbani na James. Geb na Joshua ndio walikuwa wakiandaa harusi. Pesa ipo, ikawa ni kuwaza tu, wafanye jambo zuri. Na kweli wakafanikiwa kwenye sendoff, ikaenda vizuri na kuwawakilisha huo upande wa bibi harusi ipasavyo.

Hapo James amesimama, mwepesii, tena kiufahari kwa ukoo wao,  mtoto wa kwanza wa kiume, akisubiri dada yake aingie, ndoa ifunge, ameshamaliza jukumu la kumuaga dada yake, tena alilimaliza kwa heshima akiwa mstari wa mbele akisaidiana na baba yao mzazi. Na alishahudhuria bachelor party ya Bale. Nayo walimfanyia kama shemeji yake, James, ambaye alioa akiwa hajawahi kufanya mapenzi na mwanamke yeyote, Jema ndio mwanamke wake wa kwanza.

Na yeye Bale akapitishwa kwenye shule ya undani tena kwa kina bila kufishwa. Jinsi ya kumchezea mkewe bila kinyaa wala aibu. Akasisitiziwa kuacha mazoea na uvivu akifupisha romance kabla ya tendo la ndoa.

Hapo amesimama akimsubiria Vai ampe kiapo chake, lakini ashajua chakufanya usiku huo. Hawakutaka kufanya harusi ya usiku. Ilikuwa ikifungwa saa nne asubuhi, kisha sherehe fupi hapohapo nyumbani kwa Kumu, kisha chakula cha pamoja cha mchana, mawili hao waende kujifungia mahali kwa siku mbili, kisha safari ya fungate ndio ianze, Kumu akiwa ndio mlipa garama.

Wasimamizi wote walishakuwa wamesimama sehemu ya juu ya kufungia harusi, wakimsubiria Vai na baba yake.

Mpiga kinanda alipoanza tu, wote wakasimama wakijua ndio bibi harusi anaingia. Mapigo ya Bale yakaanza kwenda kasi. Huyo Vai hakuwa amemuona takribani siku 7 tokea alipokwenda kwao Moshi. Alishakuwa na hamu naye, hana maelezo.

Moyo ukajawa furaha kadiri alipokuwa akitembea akiwa ameshikwa mkono na baba yake wakimsogelea. Akajikuta amejawa tabasamu la wazi kabisa. Hatimaye Bale akakabidhiwa mke waliyekuwa wakijuana mapungufu yao, hakuna siri ila mapenzi matupu.

~~~~~~~~~~~~~~~

Sherehe ikawa nzuri na yakufana. Vai aliyekuwa amezoea kuchezea ligi kuu za Uingereza, hakuwa na tumaini kubwa sana na mchezo wa usiku huo, akijua Bale ni mgeni. Ila tu ikabaki furaha kwamba na yeye anaolewa, tena anaolewa na Bale aliyemkubali alivyo, akijua hana uwezo wa kuzaa. Hana chakujificha kwake.

Lakini tumaini lilianza kidogo jinsi alivyoweza kumkiss baada ya kufungishwa ndoa. Wakiwa wameshotoa viapo vyao. Bale alilitendea haki hilo kiss mpaka akamshangaza  Vai. Kwa kituo bila papara.

Mvumilivu Anakula Mbivu Na Baraka Za Mungu Juu Yao.

Sasa mlango wa chumbani ulipofungwa, kwamba ndio wamebakia wao wawili, akashangaa uchangamfu wa bila maneno ukaanza kutoka kwa Bale aliyejua yupo viwanja vya ugenini asijue mwenzie alishaupangilia huo usiku kwa muda mrefu, na hapo ana shule ya kutosha.

Vai alianza kwa kucheka kadiri alipokuwa akimnyonya shingoni, midomoni, huku akimtoa nguo. Vicheko vilianza kupungua, pale alipotua kwenye chuchu, mkono ndani ya chupi akipekenya tamu yake kama pipi. Na yeye akawa kama amemfanyia kusudi, kumbakisha na chupi tu.

Taratibu mpaka kitandani huku aking’ang’ania kunyonya ulimi wake, mkono unaendelea na kazi yake ndani ya chupi. Kabla hajamuweka kitandani, Vai akaona anamchelewesha, akatoa chupi yeye mwenyewe huku akigugumia. Akamuweka kitandani haraka sana akapanua miguu kwa haraka, mwenzie ana nguo!

Akaanza kumng’ang’ania zipu ya suruli kama achomoe, Bale akaongeza nguvu akimsugua kwenye kijimrija cha sehemu ya kukojolea bila kupotea japo alikuwa akiteleza sababu alikuwa akitokwa ute kupitiliza. Akamfanyia hivyo kwa muda akamuona anakakamaa, mikono ametoa kwenye suruali, amemshika kwa nguvu mpaka akapata bao ambalo hakutegemea. Alipotulia ndipo akatoa mdomo kwenye chuchu na mkono huko chini, Vai anahema haswa.

Akaanza kujitoa nguo zake na kurudi kitandani. Ikawa kama na yeye amezidiwa, akakimbilia matiti alikoona huwa akipitisha mdomo huko anaishiwa nguvu kwa haraka, akaingia yeye mwenyewe akitetemeka.

Vai anawaka kwelikweli hapo kitandani anakomulikwa na taa. Chuchu za rangi ya pinki, mwenyewe Bale alikuwa kama ana njaa wakati ametoka kula! Akashindwa kutoa mdomo, mzee anasugua chini. Bale hajawahi onja joto la mtoto wa kike, akasalimu amri kwa haraka sana mpaka akajisikia vibaya mbele ya Vai.

Vai alipomuona anakosa raha, na ujasiri kupungua, akaanza yeye utundu mpaka mzee akaamka tena, akamuweka chali na kumkalia. Alijizungusha mtoto wa kike akijipimia, akashangaa Bale anapiga magoti, akamuweka mbele yake. Akawa amemkalia ila amempa mgongo.

Alikuwa akimpapasa kwa hisia, huku Vai akiendelea kujizungushia mzee kalengeshwa golini, akiikatikia huku akinyanyuka kidogo na kukaa. Mikono ya Bale ikawa huru kufanya anachotaka kwenye huo mwili huku akimnyonya maeneo ya nyuma ya shingo mpaka mgongoni alipomgeukia. Mkono mmoja matitini, mwingine mbele kwenye tamu ya Vai.

Iliyokuwa ikisikika hapo ni miguno ya utamu. Vai mlalamikaji kwenye raha, hajiwezi akichezewa kinembe. Mlowaji wa haraka kwa sababu ya hisia nzito alizokuwa amezibeba kwa Bale, akisubiria hilo penzi. Naye Mungu hakumpunja kwa uume wa mumewe. Ukamtoshea kwa raha kama zote! Ile hali ya utelezi na uchezaji wa Vai, na huku akimchezea kama mwanzo, akaanza Vai mwenyewe kupiga bao. Ile kelele nzuri, ikamfanya na Bale naye apate la pili, wakajitupa pembeni wanahema.

“Nimekumisi Bale! Siku 7 bila wewe!” “Mimi ndio zaidi. Nakupenda Vai! Nakupenda sana! Halafu kumbe ndio mzuri hivyo mpaka ndani!” Vai akacheka sana kwa aibu akijificha pembeni yake. “Hakika nakupenda Vai. Na asante umenikubali.” “Na wewe asante kunipokea nilivyo.” Wakaanza kukiss. Safari hii ikawa kiss ya muda mrefu haswa wakiwa wamekumbatina hapo kitandani, kiubaridi cha A/C kikiwasaidia wasitokwe jasho la kukera.

Huku Kwa Colins

Ilipofika majira ya saa moja, akiwa bado ofisini akapokea simu kutoka kwa Peter yule mwenye hoteli. “Najua hunifahamu, Colins ndugu yangu, lakini sina jinsi ya kukushukuru. Yaani wewe ukifika pale hotelini kwangu, kula na kunywa yako yote ni juu yangu.” Akacheka alivyomsikia mpaka sauti imebadilika.

“Naona na sauti imetoka kabisa!” “Aisee sisi tulipotoka hapo kwako, tulijiongeza. Nilitafuta ndugu zangu polisi, nikawaonyesha ile video, nikawapa na motisha kidogo, wakaenda kukamata wale wanawake wawili. Mmoja alikuwa ndio ametoka hospitalini, lakini wakahakikisha wanawakamata. Wameshikiliwa tena na polisi. Wanasema wale ni wauuaji, hawawezi kukaa nje bila ulinzi. Wanaweza dhuru mtu mwingine.” Colins alifurahia, asiamini!

“Haiwezekani!” “Jamaa wote pale kituo cha polisi walinishauri nichangamke lasivyo wale wanawake wanaweza nirudisha migombani.” Lafudhi ya kichaga iliweza kusikika bayana. Colins akacheka sana kwa ushindi. “Kama walivyoniwahi mara ya kwanza, na mimi nimewawahi.” “Sasa na yule wakili wako asichelewe.” “Mbona ameshafanya kama ulivyomshauri! Amemtafuta hakimu na kumwambia amepata ushahidi mpya tena wa hakika. Hapa tunapozungumza, ushindi upo upande wangu kabisa.”

Wakati Wakuvuna Kila Mmoja alichopanda.

Alifurahi Colins, ikawa kama ametuliwa mzigo mzito. Love na Kemi wametoka mtaani! Alitamani kuruka ruka akifurahia uvunaji wao. Hatimaye amefanikiwa kuwafikisha kwenye mavuno yao. Na Jelini amefanikiwa kumpatia haki yake. Safari hii atakapoitwa mahakamani, hatafika mnyonge tena, ila mshindi. Akajikuta akivuta pumzi kwa nguvu sana na kuzishusha taratibu.

Akabaki akifikiria. Akajikuta ni kama kilichokuwa kikimzuia asiwe na furaha, KIMEISHA. Ukweli ukabaki palepale, Jelini hatakaa akamrudia tena. Ezra ameshikilia kweli kweli! Kinachomzuia na yeye kuendelea na maisha yake ni nini! Akaona mama yake yupo sahihi.

 “Kama Kamila aliyependwa hivyo, yupo tayari kuendelea!” Colins akawaza huku akijisuta akirudia maneno ya mama yake. “Sembuse mimi niliyepitishwa kwenye machungu tokea mwanzo, nazuiliwa na nini! Ni kweli sijui hata raha ya mapenzi! Kwamba nikaishi na mwanamke akanipenda na kunitunza, akinisubiri kwa kunivumilia kama hivyo Kamila!” Akazidi kujitia morari mwenyewe.

~~~~~~~~~~~~~~~

Akatoka kurudi nyumbani akiwa amekusudia mwanzo wa zaidi ya muvi za kifilipino. “Huyu Kamila si anadhani alipendwa na Mike!” Colins akazidi kujipampisha. Akiandaa usiku huo wa mapinduzi. Akafanya yake huko mtaani akitaka kumfurahisha Kamila, kwa manunuzi ya kipekee. Si kitajiri kama alivyozoeshwa na Mike, lakini very romantic.

Akaangalia muda, akaona itoshe, awahi kurudi nyumbani kwa haraka akitarajia kumkuta Kamila lakini mpaka anafika nyumbani, bado hakuwa amerudi. “Salimia watoto ya muda wote huo!” Akajinung’unisha. “Huyu Mill asije jinufaisha na upweke wa Kamila.” Gafla haamini mtu na Kamila aliyekuwa naye siku zote! Akaendelea kuwaza akiangalia muda na kuzunguka humo ndani. Mwishoe akahisi watamshitukia. Akatoka na laptop yake na kukaa kwenye meza ya kulia chakula, akimsubiria Kamila huku akijifanya busy na ya msingi. Kumbe akili ipo alipo Kamila na Mill.

~~~~~~~~~~~~~~~

 Mama yake huwahi kutoka. Saa nane mchana, kazi huwa amemaliza. Mzee yeye ndio anafanya kazi kwenye hospitali tatu. Akimaliza kwenye hospitali kuu ya Muhimbili, basi hufanya kliniki ya mambo ya moyo kwenye hospitali nyingine mbili mbali na hiyo yao. Kwa hiyo kwenye mida ya saa mbili usiku ndio anakua anaingia nyumbani.

~~~~~~~~~~~~~~~

Akamkuta Colins mezani na laptop yake. “Vipi?” “Safi tu, shikamoo.” “Marahaba. Unahama lini?” Akitegemea ni swali rahisi ambalo lingemchangamsha, ila akamuona amenyamaza. Akashindwa kuelewa.

“Pesa hizi huwa hazitoshei Colins! Hata kama unataka kufanyia biashara ile nyumba, inaweza kusubiri.” “Tatizo sio pesa.” Akajibu hivyo bila yakumuangalia baba yake na kuendelea na yake kwenye laptop. Mzee akataka kuuliza zaidi juu ya hilo, akaona anyamaze.

“Mama yako yuko wapi?” “Amepita hapa sasahivi, yupo chumbani kwenu.” Mzee akamfuata mkewe.

~~~~~~~~~~~~~~~

“Huyu vipi mbona tena hana haraka ya kuhama!?” Akanong’ona akimuuliza mkewe. “Nafikiri ni sababu ya Kamila tu, vile alivyokataa kuhama naye. Ndio amekwama. Na najua ni sababu ya kugomba kwake huko, amemtisha mtoto wa watu, na Jelini haimtoki mdomoni. Ndio unamuona amekwama hapa!” Mzee akazidi kuumia akijutia.

Akakaa kabisa. “Nimemuharibia  maisha yake!” Akawaza kwa sauti. “Lakini mimi nilijua namsaidia!” Akaendelea kusononeka. “Njoo hapa baba Coly.” Akatoka kabisa, ikabidi amfuate. Mpaka alipokuwa amekaa Colins.

Hakuna Jinsi Ya Kutengeneza Nyuma.

“Kaa hapo, mimi nataka kuzungumza na nyinyi wote wawili.” Mzee  akabaki na mshangao usoni. “Kaa Henry!” “Ukishaniita jina langu nakua kama nipo matatizoni! Sasa safari hii nimefanyaje tena!?” Colins akabaki akiwatizama.

“Nitakwambia kama nilivyomwambia Colins. Hapo mlipo wewe na Colins, lazima mtoke. Wote wawili mmekwama, na wala haiwasaidii. Tupende tusipende ukweli ni kwamba tumeshaharibu, hatuwezi kutengeneza, na Jelini anaolewa. Umenisikia Colins? Na kabla hujajibu.” Akamgeukia mumewe.

“Japokuwa Love amekosea sana, ameingiza familia yake kwenye matatizo na aibu yote hiyo, Simba na mkewe wamesamehe makosa wanaendelea kupambana kumsaidia binti yao. Wamefanikiwa kumtoa jela, wapo naye siku nzima hospitalini, wakimuuguza. Nyinyi mmebaki mnapambana, na vita yenu haiishi.” Kimya akisikiliza akijua bado hawajui kilichompata Love.

“Sio mimi, ni Colins ndio hataki kunisamehe!” Mzee akajikuta akisemelezea kama mtoto. “Wewe…” “Subirini kwanza. Maana nyinyi wawili nawajua. Hamtakaa mkamaliza na mnamfanya Connie anashindwa kurudi nyumbani.”

“Mimi sijamzuia kurudi nyumbani!” “Kweli Coly!?” Akamuuliza kwa kumsuta. Akajirudi. “Ameniumiza mama!” “Sasa utakaa na jambo hilo mpaka lini? Mwenzio anahamu na wewe, anakazi ya kunisumbua! Haishi kuja kazini kwangu anakulilia. Na wewe mwenyewe ndiye uliyemzoesha vibaya, umemlemaza mwenzio, hawezi kuishi bila wewe.” “Mbona aliishi karibia mwaka  mzima bila kujua nilipo?”

“Coly, ni vile umekasirika, umekataa kuelewa ukweli. Hapakuwa na mazingira ya kukufikia mwanangu! Na usifikiri ilikuwa rahisi kwetu kuishi bila kujua ulipo. Lakini kina Simba walikuficha kwelikweli, na uongo wakupitiliza. Muulize baba yako kama sikumpigia simu nikiwa Kigamboni nakutafuta, nalia, usiku, sikuoni, na bado wananidanganya. Nikamwambia baba yako, nina hisia mbaya, zinanisumbua juu yako, kuna kitu hakipo sawa.”

“Hapo nilikuwa nazunguka kama mwehu, na pale hospitalini ulipo sasa ni kama wote walionywa waseme walichoambiwa. Unafikiri wananiita mvivu pale kazini kwa kusingiziwa?” Kimya.

“Nilikuwa natoka mida ya kazi, tofauti tofauti ili kuona kama nitakukuta popote! Nilikuwa nikikufuata mida tofauti tofauti kila mahali ili tu kuhakikisha sidanganywi, ni kweli upo busy, na ni mzima. Nilifanya hivyo kwa muda mpaka nikaridhia kuna jambo halipo sawa.”

“Muulize huyu kama sikumtoa kwenye kliniki zake nikamwambia lazima atoke, anitafutie mwanangu mpaka nimpate, kuna jambo halipo sawa! Napo pia alidanganywa, ndio na yeye akafanya kama mimi. Kuvizia pale mlipokuwa mkiishi na Love, mpaka akakupata. Ulitaka nifanye nini Coly?” Mpaka mama yake akaanza kulia tena.

“Basi mama yameisha. Nimeelewa. Na samahani kwa kukuku…” Akanyamaza. “Sasa hapo lazima uombe msamaha wakueleweka Colins.” “Baba!” “Sasa unaombaje msamaha wa hivyo?! Umemkosea sana mama yako.” Wakaanza kulumbana tena hao wawili hawamalizi.

“Bora nife, naona ndio mtaridhika na ndio kutakuwa na amani humu ndani.” Wote wakanyamaza. “Basi mama. Mimi nimekosa.” Mzee akakohoa kama anayemuuliza umekosa nini. Colins akamwangalia na kutingisha kichwa kwa masikitiko kama amjibu, ila akaendelea.

“Nimekosa mama. Nimekuvunjia heshima.” Mzee akakohoa tena. Colins akaelewa. “Nilikukaripia. Niliacha mtu mwingine aniuguze. Nimekulaumu. Haya, kingine ni nini baba?” “Naona hayo ndio makosa yako makubwa.” “Kweli baba!?” Colins akashangaa, asiamini.

“Kwahiyo unataka tuendelee tena, ili uje uombe tena msamaha hapa?” “Sawa. Mimi naomba yaishe.” “Unamaanisha kwetu sote!? Yaani familia nzima au?” Mzee akachomekea. Akanyamaza akiuma meno.

“Wewe muweke wazi mama yako jinsi unavyotaka yaishe.” “Baba wewe una…” Akaona anyamaze. “Sema tu. Na leo ijulikane anayetaka kuendelea kumuumiza mama yako ni nani, ili isije tokea kuja kulaumiana baadaye, mambo yanapokuja kuharibika.” “Wala hakuna litakaloharibika. Nitakufa kwa pressure isiyoweza kushuka, wote tupumzike. Na kama hamjajua, nyinyi wawili ndio mnaoharibu amani ya humu ndani, mpaka na wageni nao wanashindwa kuishi humu.”

“Mbona mimi nimeshaomba msamaha mama! Na nimeomba yaishe.” “Yanaishaje nusunusu?” “Naona tuanze mimi na wewe mama.” Mzee akacheka sana na kuongeza. “Kwamba mimi na Connie ndio tunabakia kuwa wabaya wako?” Colins hakujibu ila akaendelea na mama yake.

“Umeridhika mama?” “Mimi hivyo vya msamaha wa nusunusu siviwezi Colins. Wewe unauwezo wa kurudisha amani humu ndani au kuendelea kupoteza na kuumiza watu, wakati wenzetu wote maisha yao yanaendelea vizuri.” “Hujui kilio walicho nacho kina Simba usiku huu.” Wakashituka sana.

“Kwa nini tena!?” “Jioni hii Love amerudi tena rumande. Na wala hatakaa akatoka TENA, kuja kumdhuru mtu mwingine. Nitahakikisha maisha yake yanaishia jela daima.” Wote wakabaki wakimwangalia kwa mshangao mkubwa kama walioona chatu ndani ya nyumba.

“Na katika ‘hili’ naomba usiingilie mama. Ni bora kumsamehe Connie kuliko Love.” “Mbona mimi ambaye nataka amani ndio hunitaji!?” “Wewe ni chanzo cha yote baba.” “Kwa kukupenda na kukujali nikikuwazia mema ya baadaye ndio kosa langu?” “Kwa kutonisikiliza mimi na kumsikiliza Love.” Wakaanza tena kubishana, hawamalizi. Wakamuona Mama Colins ananyanyuka.

Colins akasimama kwa haraka na kumuwahi. “Mama! Mama!” “Acha nikuache Coly. Naona umeamua kuangamiza hii familia. Acha nikuache. Lakini hivi sivyo tulivyokutegemea. Tulijua tumepata mtoto wa kiume wa kwanza, utaendesha hii familia vizuri. Lakini naona umeamua kuingamiza. Yaani wewe dada mmoja tu anakushinda kweli!? Je ungekua mrithi wa ndugu 11 kama Joseph aliyeuzwa na ndugu zake utumwani?”

 “Akateseka mpaka kufungwa jela kwa makosa ya kusingiziwa tu. Tena kote huko anapata shida, wala si siku moja au mwaka! Ni miaka anateseka akiwa amesababishiwa na ndugu zake! Mbona yeye alisamehe ndugu zake wote na kufanyika msaada mkubwa sana kwa familia yake hiyohiyo iliyo mfanyia ubaya kuliko huu wetu!? Wewe tunakwambia tulifanya kwa upendo, unashindwa kusamehe!?”

“Basi mama. Yameisha. Baba naomba usiongeze neno. Wewe nyamaza kabisa. Ila mama jua nimesamehe. Hutanisikia nikigomba tena.” “Na Connie?” Akanyamaza. “Colins?” “Nitamtafuta.” “Labda ungempa mama yako siku unayopanga kumtafuta Connie.” “Baba?” “Ni wazo tu! Mbona ukali tena!?” Akamtizama, hakumjibu, akamgeukia mama yake.

 “Wewe usiwe na wasiwasi mama. Nitamtafuta.” “Lini?” Mama yake akauliza. “Kwa sasa nina mambo meng..” Mzee akakohoa tena. Mpaka akamfanya Colins akacheka kwa masikitiko.

Akamgeukia mama yake na kumshika kwa upendo. “Unataka tukazungumze tukiwa peke yetu? Mimi na wewe tu. Kwa utulivu.” Akamuuliza kwa kumbembeleza. “Unataka kwenda kumdanganya mama yako huko! Ukamrubuni kwa maneno ya kumbembeleza mpaka umpoteze malengo. Wewe zungumza hapa tumalize, ndio muondoke. Na nakuhakikishia itakusaidia wewe mwenyewe.” Hata hakumgeukia baba yake, wala kumjibu.

Akaendelea na mama yake. “Eti mama? Twende?” “Inamaana wewe upo busy kiasi chakushindwa kumtafuta dada yako na kumjulia hali tu?!” Mama yake hakusogea, akamuuliza swali akijua mumewe yupo sahihi. Akiondoka naye tu hapo, ndio basi.

“Eti Coly?” “Basi namtumia ujumbe sasahivi kumtakia usiku mwema.” Mama yake akabaki amesimama. “Kwamba unasubiria!?” “Si umesema sasahivi, au unanidanganya? Mwenzio yupo kipindi cha mwisho huko chuoni. Akili haijatulia. Kweli wewe unashindwa kumtuliza akamaliza shule yake vizuri, na mimi nikajivunia mwanangu!? Watatucheka familia yetu mpaka lini?!”

“Basi mama.” Akavuta simu ilikuwa mezani pembeni ya laptop. Akaanza kuandika. “Ungempigia kabisa, ndio ingekuwa vizuri zaidi.” “Naomba baba wewe usiingilie kabisa. Tafadhali sana. Nyamaza.” “Kwamba wewe unaona shida kusikia sauti ya dada yako?” Mama mtu akauliza. Colins akamwangalia baba yake akamkuta anacheka kama wasimuone. Alipoona anamwangalia akaacha kucheka na kumuuliza. “Mimi nimetoa wazo. Kosa langu ni nini?” Akajishauri akionekana anapata uzito, ila akapiga.

“Coly!” Connie akampokea kwa haraka na kwa upendo kama aliyekuwa na simu mkononi. “Vipi? Unaendeleaje?” “Nimekuumiza, lakini unajua nakupenda Coly. Naomba nisamehe. Connie akaanza kwa kubembeleza sauti kama mama yake. Wakamuona anaondoka hapo kuelekea chumbani. Wakajua amelainika, anakwenda kuweka mambo sawa.

~~~~~~~~~~~~~~~

“Asante.” Mzee akanong’ona. “Tafadhali usirudie tena baba Colins. Umeingiza familia kwenye…” “Kwa hiyo na wewe umeamua kumpokea mwanao?” Mama Colins akamwangalia na kuanza kuondoka.

“Mbona mimi hujanirekebishia, unaondoka?!” “Nimekurekebishia kwa Connie, mwanao. Ridhika.” “Hii familia inapenda kunitenga! Misamaha yenu ya upendeleo upendeleo!” “Wewe endelea kufanya kwa vitendo. Maneno huyo yamemchosha.” Akaingia chumbani kwake, mzee akafuata.

~~~~~~~~~~~~~~~

Inaendelea…


 

 

 

CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment