Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com Mapenzi & Pesa! - PART 2 - SEHEMU YA 29. - Naomi Simulizi

Mapenzi & Pesa! - PART 2 - SEHEMU YA 29.

 Ukimya ukaendelea kila mmoja akikumbuka uharibifu wake. Vai akamtizama Bale, akamuona yupo mbali sana na pale. “Bale!” Akawa kama amegutuka kutoka usingizini. “Ilikuaje?” Vai akauliza taratibu tu, Bale akacheka kwa kuguna. Kisha akajibu na kuendelea. “Haraka za maisha. Ndio maana siku ile ulipozungumza jinsi ya kusubiri, nilitulia nikijua ni ujumbe wangu.” “Mimi nilikuja kujilaumu baadaye. Nikasema sikutakiwa kukwambia vile.” “Hapana. Mungu alikutumia tu, kunikumbusha. Ulikuwa ujumbe wangu.”

“Ni nini kilitokea, Bale?” “Mama alifariki na kansa ya mapafu. Ila baba na mdogo wangu, walikuwa na bibi pamoja na mtoto mwingine alikuwa akilelewa na bibi, walikufa siku moja. Mimi nikiwa nimeshiriki kuweka mipango ya kuchoma moto mali za baba, nikidhani niliyekuwa nikiweka naye mipango hiyo tupo pamoja. Kama kumfundisha baba yangu adabu kwa kumkumbusha alikotoka. Kumbe mwenzangu alikuwa na nia nyingine kabisa. Alikusudia kumtoa baba yetu hapa duniani, ili yeye ammiliki Naya atakavyo!” Akazidi kumchanganya Vai, ila akawa mvumilivu kusikiliza.

“Kwa hiyo vijana waliotumwa kuchoma gala ya baba tukidhani au nikidhani ni utajiri aliopata kutoka kwa huyu mume wa Naya, Joshua, kama njia ya kumrubuni baba atoe baraka zake amkabidhi Naya kwake kama mke, mpaka kumuozesha kwake na si Malon mwanaume wa kwanza wa Naya, ambaye ndiye tuliyekuwa naye kwenye hiyo mipango ya kumuangamiza baba. Mimi nikidhani hao wachomaji wamepewa maelekezo ya kuchoma tu hilo gala, kumbe walikuwa na maagizo ya tofauti kutoka kwa Malon.” “Kwa hiyo ukaja kugundua baba yako hakuwa amehongwa hizo mali ikiwepo hilo gala ili kumuozesha Naya?” “Hapana aisee Vai! Kumbe mzee alikopa. Na nilibidi kuja kulilipa hilo deni kubwa sana. Na si kwamba alipewa na Joshua, ila Joshua alimuunganisha kwa mtu mwenye biashara kama hiyo. Ndio wakawa wakimpa baba mazao, anauza, asilimia fulani ya mauzo, analipa deni huku akijiendeleza. Niliumia Vai! Sina jinsi nikaeleza mtu akaelewa. Lakini ikawa ni mjukuu wa majuto. Nimechelewa, nishafanya uharibifu.”

    “Nilimpokonya baba tonge mdomoni. Kitu alichokuwa akifunga na kuomba kwa muda mrefu sana, akimsubiria Mungu kwa unyenyekevu bila kutaka kuharibu mahusiano yake na Mungu, kama mimi nilivyofanya mabaya mengi ili kupata pesa kwa haraka mpaka kuuza bangi niliyojua inadhuru watu, lakini pesa yake ya haraka. Nilikuwa na pesa Vai! Asikwambie mtu. Pesa haswa. Lakini sikuwa nikilala kwa amani na usingizi mzuri, kama nilivyokuwa nikilala nyumbani kwa baba yangu nilipokuwa nikipadharau, na kupaona fukara. Ule usingizi haujawahi kurudi tena Vai. Na nilipata yote niliyokuwa nikihangaikia, tena kwa haraka sana, ila nikapoteza ndugu, furaha na amani.”

    “Kweli nilimpita mbali sana baba kimaendeleo. Yaani hilo deni alilokuwa akidaiwa, la biashara tuliyoangamiza, nililipa kama mchezo tu, mpaka wenyewe hawakuamini. Maana baba yangu alitaka kulilipa taratibu kwa kadiri ya uwezo wake, hakutaka kona kwenye maisha, akaomba wampe muda. Wakakubaliana hivyo na yeye akawa akiwalipa kutokana na anavyopata pesa.”

    “Vai, baba yangu alimpenda Mungu mpaka kero kwa mtu unayemfahamu kwa undani. Alitulia akimsubiria Mungu kwa kila jambo, wakati unajua kabisa, angefanya hiki au kile kwa kukata kona fulani fulani, angefanikiwa kwa haraka na kutoka kwenye shida aliyokuwa nayo. Mimi nilishindwa aisee. Nilimdharau kupita nitakavyokwambia. Nilimuona mjinga, mzubaifu hajui mambo halafu hashauriki! Nikaamua kuachana naye. Kuondoka nyumbani kuhangaika kivyangu, kumbe nikawa napishana na majibu ya Mungu, utafikiri mimi ndiye niliyekuwa nikiyazuia wakati wote!”

    Yaani mimi natoka tu, ndio mafanikio ya mali, si vinginevyo. Maana kwetu tulikuwa na kila kitu ila utajiri ndio ilikuwa hangaika yangu mimi na mama nakupitwa na ile furaha, amani na utulivu vilivyokuwepo pale nyumbani. Nikakosa wakati mzuri nyumbani, wakati wote sisi ni vilio tukitaka ziada kwenye maisha. Mungu akiwa ndio amemjibu, ameunganishwa na watu sahihi kumsaidia kufikia ndoto zake za muda mrefu. Akiwa ndio amefanikiwa tu na mimi nikaingilia kati, tena akiwa anahangaika kunitafuta, kunirudisha kwenye familia, ndio mimi nikarudi kumuangamiza kabisa. Akiwepo huyo mdogo wetu, ambaye ni kinyume kabisa na mimi pamoja na Naya. Mpole. Mtoto asiye hatia. Nikawaangamiza kwa ujinga tu. Haraka zikinisaidia.” Bale kwa mara ya kwanza akapata mtu wa kumsimulia upande wake wa maisha. Ila safari hii akikubali kuwajibika, majutoni. Si kumtupia lawama zote Malon.

    Alikiri kila kitu bila ya kuficha na kumshangaza sana Vai. “Bale! Sasa Naya naye aliishia wapi?” “Kwanza hivi unavyoniona mimi, ndivyo Naya alivyo. Tulifanana na mama yetu mpaka ukucha. Huu urefu ni wake mama. Lakini kujibu swali lako, Joshua alimpenda sana Naya. Japokuwa alirudi akiwa amejeruhiwa vibaya sana na Malon na hamkumbuki tena Joshua!” Bale akainama na kuanza kulia.

    “Pole sana Bale.” “Aisee hapa duniani Mungu ana watu wake Vai! Kile kingekuwa kipindi cha Joshua kumtelekeza au kututelekeza. Lakini yule mwanaume anampenda Mungu aisee. Ndiye mtu wa pili mbali na baba yangu, nimemuona hapa duniani, mwenye hofu ya Mungu. Japokuwa alijua kwa hakika tupo yatima. Hakuna anayemuangalia. Hata mkewe hamkumbuki, Joshua alimchukua Naya, akamtibu na kumuweka kwake mpaka aliporudi kumkumbuka. Na usifikiri ni siku chache!”

    “Aliishi naye, Naya akiwa hakumbuki chochote mpaka tena huyuhuyu Joshua alipokuja kuniokoa na mimi nikiwa nakaribia kufa. Sina mtu! Nimeibiwa kila kitu. Huu mguu umeoza! Sina hata mtu wakunipa maji ya kunywa, achilia mbali chakula! Nalala kwenye maboksi, nasubiria kifo, ndio Joshua akaja kunitoa pale.” “Pole sana, Bale.” Bale alisimulia akilia kwa uchungu sana. Akamsimulia Vai mpaka hapo alipo, Vai akabaki akimwangalia na yeye akikumbuka ubaya waliomfanyia Nanaa wakati wakiishi naye. Akapoa haswa akishindwa kumuhukumu, maana hawakuwa na tofauti kubwa na Bale.

     “Imekua ngumu kurudi kuwa ndugu tena.” Mwanaume akajifuta machozi na kamasi mbele ya huyo mrembo. Alishindwa kujizuia. “Undugu haufi ila mahusiano.” Vai akaishia kusema hivyo, na kubaki akifikiria. “Natamani majuto yasingekuwa mjukuu. Natamani kurudisha siku nyuma, niyaishi yale maisha ya nyumbani tena. Hatukuwa na vingi, lakini tulikuwa pamoja. Hatukuwahi kulala njaa. Hatukuwa tukila kama matajiri, lakini Vai, nahisi kile chakula kilikuwa na mkono wa Mungu aisee! Tangia nimetoka nyumbani, sijawahi kula nikaridhika kama pale kwa baba, mpaka nikawa nashangaa!”

    “Nilikuja kushika pesa kama nilivyotamani. Lakini sikuwahi kulala usingizi kama wa nyumbani kwetu, sikuwahi kutosheka. Unafikiri unahamu ya kula hiki, ukila, unashiba, lakini hutosheki! Inakuwa ni kama unayekimbiza tu upepo! Unalala umechoka, unaamka umechoka. Unaingiza mamilioni ya pesa, lakini bado unahangaika kutafuta mamilioni ya pesa.” Akamsimulia maisha aliyoishi akiwa na Malon mpaka kufika hapo, wakiwa wamekaa hapohapo mezani bila kujali muda.

Ya Upande Wa Vai.

    “Daaah! Unahistoria ngumu Bale!” “Husikii kukimbia?” Bale akamuuliza. “Nitakuwa nikikimbia kivuli changu mwenyewe. Wala hatuna tofauti sana aisee, mpaka nimeshangaa na kuamini, tabia huvuta watu wa tabia moja! Unakumbuka nilikwambia Mungu aliwapa wanadamu akili ya kutengeneza viungo vingine mbadala ya alivyoumba mwenyewe na vingine ameficha wanadamu ufahamu. Kiasi ya kwamba unapewa na Mungu mara moja tu. Ukiharibu ndio umeharibu. Unakumbuka?” Vai akauliza.

    “Ulinipa wakati mgumu wa kutafakari!” “Uliweza kuelewa?” “Ndiyo.” Bale akajibu akimtizama. Vai akatulia kwa muda kisha akacheka kwa hujihurumia. “Yaani hivyo unavyotamani wewe siku zirudi nyuma, upate tena nafasi na familia, basi mimi nilifika mahali nikiwa naishi na mwanaume, ambaye nilitamani sana anioe, kumbe alishanigundua hata siku zangu sikuwahi kupata tokea niwe naye. Na yeye kwao ni mtoto wa kwanza wa kiume na anategemewa sana. Hawezi kuoa mwanamke ambaye hazai! Aliniacha Bale.” “Pole.”

    “Acha aisee! Mtoto wa mwisho kumtoa, yule alikuwa mkubwa kabisa Bale. Mkubwa wa kucheza kabisa namsikia. Lakini mwanaume aliyekuwa amenipa ile mimba au mtoto wa mwisho niliyeua, alinidanganya hajaoa, na angenioa. Akawa akinitunza vizuri na mapenzi yanayofanana na kweli kabisa. Nikajiachia mpaka kushika mimba. Tukaja kugundua ni ujauzito wa karibu miezi miwili. Nikamwambia, hakuonekana kushituka. Kumbe ni baba wa familia yake, mimi nilikuwa mtu tu wa nje, hana mpango wa kumuacha mkewe, na hana mpango wa mtoto mwingine.” “Sasa mlikuwa mkikutana wapi!?”

    “Acha Bale. Kuna watu ni washenzi waliopitiliza aisee. Na mtu husikia anachotaka kusikia, hata kama anaambiwa au kuona tofauti. Ndio mimi. Niliona na kusikia kile akili ilitaka kusikia na kuelewa kwa yule mwanaume, japo haikuwa kweli. Kumbe tulipokuwa tukikutana wakati wote nikidhani ni kwake kumbe palikuwa kwa rafiki yake! Mimi naenda pale mpaka nalala siku nzima! Kupika mimi siwezi. Na wakati ule nilikuwa sitaki kazi yoyote ya mkono. Basi tunatumikiwa hapo, chakula tunakula nje au kutuma kuletewa hapo ndani, kumbe sio kwake! Sasa alipojua nimeshika mimba, si akaanza kunidanganya, eti amehamishwa kikazi hapa Dar, ameambiwa lazima akaripoti Dodoma. Kwa hiyo anakwenda kuandaa mazingira yangu mimi na mtoto wetu.”

    “Kama mjinga vile, nikaamini. Akawa anatuma pesa, mimi najua yupo Dodoma, kumbe tapeli yule yupo hapahapa mjini. Mawasiliano yakaanza kupungua. Ukimuuliza anakwambia anakuwa vikaoni. Mchezo huo ukaendelea huku mimba nayo inazidi kukua mpaka akapotea kabisa. Simpati kwa simu wala ujumbe. Ndio nikarudi tena pale tulipokuwa tukikutana. Nikamkuta huyo rafiki yake, ikabidi anieleze ukweli. Na akasema jamaa ana ndoa yake na familia yakueleweka. Yupo mjini lakini mimi nishakuwa tatizo ambalo hatakubali liingie kwenye familia yake. Akanimbia ofisi anazofanyia kazi.”

    “Ulikwenda?” “Nilikwenda Bale. Nilitaka tu kujiridhisha. Nikamkuta ametulia tuli ofisini kwake. Sikutaka kesi nikajua tu nishatapeliwa. Kwa hasira na haraka nikaenda kununua dawa zakua yule mtoto, nikiamini mimba itatoka. Acha Bale. Mtoto aliniuma yule! Nusura kufa. Nilioza mpaka nikawa natoa harufu, maana kuna vipande vyake vilibakia ndani. Vikaoza mpaka kuharibu kizazi. Mama akanipeleka hospitalini. Ndio kusafishwa.” “Walitoa kizazi?” “Sijui na wala sitaki kuhakikisha.”

    “Ila kama nilivyokwambia, baada ya hilo tukio ndio nilikuja kuishi na yule kijana. Ikawa tena tofauti. Mwanaume huyu anataka mtoto, mimi sishiki tena mimba. Na tulikaa naye muda tu. Akanifukuza. Tena alinifukuza vibaya sana, kwa kunirudisha nyumbani akinionya nisiwahi kuja kurudi tena kwake, kwa kuwa sina uwezo wa kuja kumzalia watoto. Niliumia Bale! Niliumia sana nikitamani hiki kingine kama ulichotamani wewe.” “Kwamba kama majuto yasingekuwa mjukuu?” “Kabisa. Maana nilikaa kama mgonjwa kwa muda mrefu sana. Ila nikifikiria pia nasema bora hakunioa, maana na yeye aliishia kufungwa jela.” “Nini tena!?” “Aaah! Walisoma na kaka. Wakawa kundi kubwa la marafiki. Wakageukana kama tu hivyo stori yako wewe ilivyo. Wakafikia hatua yakutaka kuuana. Ndio mwenye pesa zake na akili, akawawahi kuwashitaki kisheria. Sijui tena habari zake.”

    “Ila ninachojua, nalipa garama yake Bale. Na huyo ni mmoja, nikajitia kichwa ngumu. Nikajiingiza kwenye mahusiano na mwanaume mwingine. Na yeye hakutaka hata twende mbali. Mapema, akaniambia anataka kuanzisha familia. Tupime, tuanze kuzaa.” “Bila ndoa!?” Bale akashangaa sana. “Acha Bale. Nimepita kwingi mimi! Kwa hiyo na kwa huyo japokuwa nilikuwa nikipata siku zangu, na yeye akishuhudia, lakini mimba iligoma kabisa. Akasubiri mwezi wa kwanza na wapili, akaniaga, wala yeye hakutaka kupotezeana muda au kuzungushana. Akasitisha mahusiano kwa wazi kabisa.”

    “Ikaniingizia hofu kupita kiasi. Nikashindwa kabisa kurudi kuwa na mahusiano ya kimapenzi. Nikaona nitulie tu. Kwanza nishafanya mengi, sina nililobakiza. Nikakaa nikijifikiria. Mimi shule sina, kuzaa sitazaa tena, halafu sina maisha ya kueleweka! Nikapiga mahesabu. Nikajua kimoja nishaharibu, sina uwezo wa kubadili. Ila hivyo vingine, naweza nikajikaza nikafanikiwa. Basi ndio wifi yangu akanikalisha chini na kuniuliza kama nilishawahi kuwa na ndoto zamani. Nilipomwambia nilitamani kuwa daktari, akaangalia vyeti vyangu, akazungumza na kaka, wakanirudisha shule. Kwahiyo ndio nimejificha hapo. Shule iwe mkombozi. Nisikose vyote. Maana najua ndoa na maswala ya watoto imeshindikana. Ila shule, hiyo nitapambana nayo mpaka kieleweke.”

    Bale akabaki kimya akitafakari. “Nimekukumbusha watoto ulioacha na wewe mtaani nini?” Vai akamchokoza kwa swali kama kumrudisha pale. “Mimi katika upande huo, sikujaribiwa kwakweli. Nilifanya mabaya mengi, lakini si wanawake. Na sijui kwa nini, aisee! Ni jambo ambalo halikuwahi kuwa tatizo kabisa. Ila chuoni nilipata msichana. Tukataka kama kuanza hivi, nafikiri akagundua mbali na muonekano wangu wa nje, sina kitu. Akaweka mazingira ya wazi kabisa, kuwa hataki mahusiano ya kimapenzi kati yetu. Na nafikiri hata yeye alichangia kwa asilimia fulani kutaka maendeleo ya haraka.” “Kwa nini?”

“Kuna jinsi fulani hivi alinibadilikia, halafu akaanza kuzungumza kwa mafumbo kwamba maisha ni zaidi ya muonekano. Kwamba watu wanapenda kukimbilia kwenye ndoa, wakizinguliwa na muonekano wa mwanaume mwanzoni na kusahau uhalisia. Wakishaingia kwenye ndoa, wakikutana na uhalisia, wanaanza majuto. Sasa kwa kuwa na mimi nilitoka kwenye mazingira ya familia kama aliyo zungumzia, nikamuelewa kwa haraka sana. Kukosekana amani nyumbani kwetu sababu ya mama kulalamikia maendeleo au ufukara, nikamuelewa kwa urahisi sana yule binti.”

    “Japokuwa alikuwa mzuri sana. Mzuri tu, na kwa hakika alivutiwa kwa haraka sana na mimi mpaka alipokuja kujua ufukara wangu. Nikamuacha kabisa wala sikutaka tena ukaribu naye, akili nikahamishia kwenye harakati ya kutafuta pesa, nikitaka nisiwe kama baba yangu. Kumbe bora vile alivyokuwa baba, kuliko nilivyokuwa mimi. Kufanikiwa bila baraka za Mungu. Kwa hiyo kujibu swali lako, sijawahi kuwa na mwanamke maishani. Nilijiona ni bora niwe peke yangu, au niseme niliona matatizo niliyo nayo yanatosha, sikutaka kukaribisha hata kwa bahati mbaya, fujo za mapenzi.” Wakatulia hapo kila mmoja akiwaza lake.

    Kuja kugutuka tayari nje kuna giza. Vai akasimama. “Nikusaidie nini kabla sijaondoka?” “Hamna. Acha nikusindikize tu. Ila unakaribishwa siku nyingine. Ukichoka kelele na chakula cha mtaani. Wewe niulizie nilipo, kama nina nafasi, nitakupikia uje kula.” “Hiyo ofa sitaifikiria mara mbili. Na wewe ukipika tu kingi kama hivi, ukajisikia huwezi kula. Wewe niite nije kukusindikiza.” Bale akacheka sana.

    “Mimi nakwambia ukweli.” “Basi acha nikufungashie chakula kesho.” “Bora nipate sababu yakurudi nikijidai narudisha chombo.” Angalau wakacheka wakizungumza hiki na kile mpaka Bale akamsindikiza kituoni. Wakafika tena kituoni, wakakaa wakizungumza nakushindwa kuagana kwa haraka. Daladala zinakuja na kuondoka, wao wamekaa tu.  

Ikawapata hisia ya uhuru kati yao. Hakuna wakujificha kwa mwenzie. Wote walikosa sana, hakuna wa kumuhukumu mwenzie. Hapakuwa na kujidai tena kati yao. Wakakaa hapo mpaka wakagutuka kuona kituoni hakuna tena daladala zinazopita. Wakaanza kucheka ndipo wakaanza sasa kusaka taksii.

    “Si kwangu umepaona palivyo patulivu?” Vai akamwangalia kutaka kujua anataka kuzungumzia nini! “Kipindi hiki cha sikukuu, karibu uje usomee kwangu na mimi nitakusaidia kusoma. Ukimaliza mtihani wa tarehe 28, tunapumzika angalau siku hiyo kwa kwenda hata kuangalia movie. Halafu tukitoka nakusaidia tena kusoma kwa mtihani wa tarehe mbili.” “Kwako!?” Vai akauliza kwa wasiwasi.

    “Ndiyo, kwangu. Unakua na uhakika wa utulivu, na chakula kizuri. Usiku nakurudisha chuo. Unaonaje?” Vai akatulia kidogo. “Itanisaidia na mimi Vai. Nakua mpweke, sina mtu wa kuwa naye. Nakua peke yangu!” “Basi nitakuja, Bale. Na asante kunikaribisha.” “Ulikuwa mwema kwangu wakati nikiwa mkali kwako. Uliniokota na kunisafisha. Wewe ni rafiki mzuri Vai.” “Nimeshakuwa rafiki!?” “Kabisa. Au hutaki?” Vai akacheka akijifikiria kisha akajibu. “Ujue mimi ni rafiki mzuri sana?” Bale hakutegemea, akaanza kucheka.

    “Umeona ujisifie mwenyewe?” “Acha nijiuze. Mbele ya kupikiwa na kusadiwa kusoma!” “Usijiuze sana. Ushanunulika hivyo ulivyo. Kitendo cha kujua maovu yangu bado ukabaki na kunitizama kama mwanzo, kimenifariji sana Vai. Nashukuru kunisikiliza. Nilihitaji mtu kama wewe, wakunisikiliza tu.” “Karibu. Muda na wakati wowote. Hata usiku ukishindwa kulala, wewe piga simu kwangu. Na nikwambie ukweli Bale, fungua moyo. Naamini utakuwa sawa tu. Usijikatie tamaa. Na wewe hujaharibikiwa kama mimi. Unanafasi kubwa sana yakutengeneza na ukawa na maisha mazuri tu ambayo uliyatamani. Kwa kuwa umegundua kosa na kwa kukusikiliza, nimegundua hutaki kurudia kosa. Utakuwa sawa kabisa. Usiogope.” “Nashukuru. Na hayo uliyoniambia, usiache kunikumbusha Vai. Huwa naingiwa hofu, nashindwa hata kula au kulala.” Wakaendelea kuzungumza wakitembe kutafuta usafiri. Bale akalipia, ndipo Vai akaondoka na kumuacha Bale kwa mara ya kwanza baada ya muda mrefu wa machungu, na furaha. Angalau ushauri wa Joshua ukaanza kuleta matunda. Amejitengenezea rafiki wa kwanza.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~

    ‘Nashukuru kwa ushauri na maombi Joshua. Nimefanyia kazi. Mwanzo si mbaya. Nilifanikiwa hata kwenda gym.’ Hapohapo Joshua akampigia. “Ulifikaje gym maana gari ilikuwa hapa siku nzima!” “Niliamua kumuacha Lembo apumzike leo. Nikapanda daladala. Lakini Joshua, nimekua na wakati mzuri sana leo.” Joshua akacheka. “Afadhali. Hata kusikika, unasikika lipo tumaini. Ila nina wazo lakutaka uthubutu wako.” “Nini?” Bale akauliza.

    “Haya magari siku hizi tunaendesha na mguu mmoja. Kwa nini usijiendeshe mwenyewe, Bale?” “Unakumbuka sina mguu wa kulia?” Bale akauliza kwa masikitiko kidogo. “Lakini unao mzima, wa kushoto. Ni akili tu. Unaweza kutumia wa kushoto na ukafanikiwa vizuri kama unatumia wa kulia. Umeshaona jinsi watu wasio na mikono yote miwili na bado wanaweza kumudu mazingira yanayo washinda hata wenye mikono miwili?” Bale akaanza kuhamasika. “Sitaki kukulazimisha, lakini nafikiri itakurahisishia sana wewe kwenye mizunguko yako hapo mjini. Usafiri binafsi si jambo baya.” “Sasa hata nikiweza kuendesha na mguu wa kushoto, napata wapi gari, Joshua?”

    “Kuna magari hapa nyumbani hata tukitoka mimi na mke wangu wote kila mmoja akatumia lake, na bado magari yanabakia. Kweli utakosa gari hapa! Wewe ukiwa tayari mwambie Lembo tuwasiliane ili nizungumze na Naya, amkabidhi akuletee gari. Sidhani kama hilo si tatizo.” Bale akapatwa ganzi akabaki kimya. “Usiwe na haraka. Fikiria.”

“Naomba nianze kutendea kazi kesho. Lakini nianze nikiwa na Lembo.” “Nitazungumza na mke wangu. Tukiwekana sawa, kesho nitamwambia aje nalo kabisa. Hapo kwako pako salama. Na mwenye nyuma ana ulinzi mzuri. Zungumza naye ulaze kwake ndani anapolaza magari yao.” “Nakushukuru sana Joshua. Asante.” “Karibu na usiku mwema.” Wakaagana, Bale asiamini.

 

Siku Ya Kufa Nyani, Miti Yote Huteleza.

Jelini akatua Dar majira ya saa tatu asubuhi, taksii mpaka nyumbani kwa Zenda. Getini wanamfahamu, toto ya mzee, anapita bila yakusubiri. Jelini akawa amehamasika kwelikweli. Alifika hapo na pochi tu. Anashida gani anazo nguo kwa Zenda kama kwake tu.

Kumbe yeye akiwa anahangaika usafiri ya jinsi ya kufika hapo kwa Zenda  asubuhi kumfurahisha, Koku aliamka akataka cha asubuhi. Zenda yupo usingizini, anasikilizia raha ya kunyonywa. Akadhani ndoto. Akaendelea kufurahia ndotoni. Lakini kadiri Koku alivyoendelea kumnyonya, Zenda akahisi fujo isiyo ya kawaida, unyonywaji wa Jelini una utamu wake na ladha ya tofauti, si hivyo. Akafungua macho na kugundua kweli ananyonywa. Harufu ya pafyumu ikamuingia kichwani akagundua ni Koku. Akashituka sana na kuruka pembeni.

“Unafanya nini wewe!?” “Jana hukuniridhisha vizuri.” Koku akajilalamisha kwa deko lakini akazidi kumchanganya Zenda. “Unazungumza nini wewe!?” “Unakumbuka jana uliponiomba tuje wote hapa, ukiomba nikusaidie penzi?” “Haiwezekani!” Mzee akahamaki kwa mshituko mkubwa. Koku akacheka kumtuliza. “Nimalizie basi na mimi niende. Nina hamu na wewe Kasa! Jana umenifanyia nusunusu si kawaida yako. Nisaidie.” “Siwezi Koku. Sasa hivi nipo kwenye mahusiano. Siwezi kumsaliti…” “Na jana nilivyokusaidia wewe hukuwa kwenye mahusiano, leo mimi nakuomba ndio unaniletea jeuri! Kwani mimi nimekuomba ndoa?” Koku akamjia juu akimlaumu kuwa yeye ni mbinafsi. Akiwa anataka yeye, huwa yeye Koku anaahirisha mambo yake na kumfuata amridhishe. Lakini yeye anamuwekea ngumu!

“Sasa mimi nishafika hapa, nimekutuliza jana, leo siondoki mpaka unikamilishie. Usinifanye mimi mtoto mdogo hapa.” Koku akamjia juu. “Ila naomba leo iwe mwisho Koku. Tafadhali. Nimekusudia kutulia na Jelini tu.” “Unaongea sana Kasa. Utatumia muda mrefu kuniamsha tena. Acha kufikiria kesho. Kwani jana ulipanga kuwa na mimi? Lakini mbona uliniomba na nikakubali kukukamilishia? Saa iweje unalalamikia jambo ulilotaka mwenyewe? Tulia tufurahie, hii si adhabu.” Basi Koku akaanza kumuamsha mzee.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Huku Jelini akafika. Jumba la Zenda kubwa kama hekalu. Mbaya kwake Zenda, Koku hakuweka alamu. Jelini alipofungua mlango mkubwa bila kelele, akajua Zenda ameamka. Akanyata mpaka sebuleni. Akavua nguo zote akicheka akijua ataweka furaha asubuhi hiyo kwa mpenzi wake, maana Zenda alikuwa na likizo ambayo anarudi kazini tarehe 5 mwezi wa kwanza. Ilikuwa Jelini akirudi mjini, wakajifungie mahali siku tatu ndio Zenda arudishe akili kazini. Na walisubiria hizo siku tatu kwa hamu sana.

Basi Jelini akiwa uchi kama alivyoletwa na mama yake hapa duniani, ila ameshikilia matiti, na tabasamu kubwa usoni, akaendelea kunyata mpaka kwenye korido ya karibu ya chumbani kwake Zenda. Akasimama maana hapo nje ya chumba palikuwa na sebule ndogo tu. Pazuri sana kulikosheheni thamani za hali ya juu mno lakini na kabati kubwa lenye vitabu.

Kabla hajaingia chumbani Jelini akaanza kusikia sauti za mapenzi. Kwa haraka sana akahisi Zenda anaangalia movie. Lakini kadiri alivyoendelea kusikiliza akisogelea kitasa cha mlango kwa kunyata na tabasamu akagundua sio sauti ya kutoka kwenye tv, ni kama watu waliopo ndani wakifanya yao. Tabasamu ikaanza kupotea kadiri alivyoendelea kusogea na kusikia sauti ya mdada akilalama kimahaba. Jelini alishituka, akahisi anaota.  

Kwa haraka sana, akili ikamtuma akimbie hapo kabisa ili wasimuone na yeye asije shuhudia Zenda akimsaliti. Akataka kuondoka ili baadaye Zenda hata aje amdanganye hakuwa yeye, lakini miguu ikashindwa kunyanyuka kabisa kama iliyokufa ganzi, lakini sasa imekakamaa au umegongelewa misumari. Kuondoka anashindwa, kufungua mlango hawezi anasikia Zenda anavyofurahia mchezo, na mdada anavyolalama.

Jelini alisimama pale kama aliyeadhibiwa na kuambiwa, ukisogea tu, nakuchapa, SHUHUDIA. Basi akasimama pale nje akisikia kila kitu, machozi yakimtoka. Akahangaika mpaka akafanikiwa kukaa chini kabisa, akakunja miguu na kuinamia magoti akijaribu kufunga masikio, asisikie. Ikawa tena kama kuna nguvu ya ajabu imemkamata, anatetemeka na kulia kwa uchungu sana. Jelini alilia kwa kwikwi huku ameficha uso wake katikati ya mapaja na kuziba masikio.

Zenda anamalizia kupiga bao na kujitupa pembeni akihema kwa mechi nzito, maana Koku mashine kubwa haswa. Alijaliwa maeneo mengi tu. Mla chips yai lazima uchemke kwa mrembo Koku. Sasa Zenda mfanya mazoezi kila siku, chakula bora kila mlo, alishamjulia zilipendwa wake. Alijua wapi ashike, mchezo upi acheze ili kumuingiza kwenye ulimwengu wao. Hapo Zenda alikuwa hoi, ametoka kujituma kweli kweli,  Jelini akisikilizia fujo zao, amejitupa kitandani akihema haswa.

Wakiwa wanatulia hapo kitandani, kila mmoja pumzi zikianza kurudi kuwa za kawaida, wakasikia kama mtu analia. Wote wawili wakatulia. Wakaangaliana. Kile kilio kikaanza kusikika sasa bayana, maana si mchezo umeisha! Magoli yashafungwa, washangiliaji wameondoka na kombe, kiwanja shwari. Sasa, sauti iliyobaki hapo ni ya shabiki ambaye timu yake imefungwa. Hasibu wake ndio kaondoka na ushindi. Ile sauti ikasikika mpaka kwenye moyo wa Zenda.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Ni nini Kitaendelea?

Nani kawa surprised?

Usikose Muendelezo……..


CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment