Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com Mapenzi & Pesa! - PART 2 - SEHEMU YA 25. - Naomi Simulizi

Mapenzi & Pesa! - PART 2 - SEHEMU YA 25.

 Kitumbua Chaingia Mchanga. Asubuhi siku ya nne ambayo Jelini anapunguziwa madawa, mama Jema akaingia kama aliyeongozana na Colins. Akasalimia na kutaka kusogelea kitanda, mzee akamuwahi. “Subiri kwanza Colins. Ni nini kinaendelea!?” Mama Jema akashituka, akatafuta sehemu akajiegemeza vizuri. “Kuhusu nini?” “Wewe si ndugu wa Jelini, kwa nini upo hapa asubuhi, mchana na jioni?” “Nataka kujua maendeleo ya Jelini!” Jelini akafungua macho akabaki kusikiliza. “Kama nani? Maana nilikupigia simu kwa heshima kabisa kutaka kujua kama unamfahamu Jelini. Kwa kinywa chako ukaonekana huna hata ukaribu naye! Gafla umejaa hapa na kumshikashika! Unataka nini!?” Colins akababaika kidogo asijue alikuwa akitazamwa wakati wote.

“Mimi ni muwazi na sitataka unipotezee muda kwa kuninyima raha.” Zenda akawa mkali wala asione aibu mbele ya mama Jema. “Jinsi unavyomshika na kumfunika Jelini sipendi na SITAKI. Hata kukuona hapa mara kwa mara sifurahii, naona unazidisha! Sijui kama unanielewa?” Kimya. “Jelini ni jukumu langu mimi, naomba ibakie hivyo na wewe uliheshimu hilo, maana nilishakupigia simu kukuulizia juu yake, ukajiweka pembeni. Ibakie hivyo. Unanielewa Colins?” “Kwa hiyo siruhusiwi kuja kumjulia hali mtu ambaye anaumwa!? Jelini yupo na maumivu, yaani ulitaka mimi nisijue maendeleo yake! Siwezi.” Mpaka Jelini akashangaa. Maana alitegemea Colins angekata tamaa, akaondoka! Lakini bado yumo tu!

“Kwa nini?! Na wewe kama nani kwake?” “Nafahamiana naye, na nasikia uchungu akiwa kwenye maumivu.” Mpaka mama Jema akashangaa ila moyo wa Jelini ukashituka na kujawa furaha ya ajabu. Hakutegemea kumuona Colins bado anapambana kujieleza kwa wazi vile mbele ya mzee Kasa, wala hakubabaika wala kuondoka kirahisi ila kueleza hisia zake! Akajawa na furaha japo mwenzie yupo matatizoni.

“Lakini sivyo ulivyoniambia siku nakupigia simu kukuulizia juu ya Jelini! Unakumbuka?” “Ndiyo. Lakini..” “Usinipotezee muda wangu. Kuwa na msimamo. Acha kutuyumbisha. Sitakuruhusu, na sitaki kukuona tena kuja hapa. Haya ondoka.” Colins akamuangalia Jelini, akakuta akimtizama.

“Na ninakuonya, usimguse wala kusogelea kitanda chake. Hapo uliposimama, iwe ndio mwisho. Hatua ingine utakayopiga, iwe ni ya kutoka kwenye hichi chumba.” “Ugua pole Jelini.” Colins akatoka. Pakazuka ukimya hapo, Zenda akasimama pale alipokuwa amekaa na kuingia bafuni.

Raha Ya Penzi, Kupendwa.

Jelini akabaki pale kitandani akitafakari. Baada ya muda Zenda akatoka. Jelini akamuita na kumshika mkono vizuri. “Usikasirike, utakuwa na siku mbaya leo. Naomba tulia.” Akamzungumzisha taratibu, kwa upenzo na kumshangaza zaidi mama Jema jinsi Jelini alivyotulia. “Leo wanakupunguzia dawa kali.” “Nashukuru kuwa na mimi hapa. Asante. Najua unachoka, hulali vizuri. Naomba nitoke hapa Zenda, nikajiuguze nyumbani na wewe upate masaa ya kulala na kufanya kazi vizuri. Tusikwame wote kwenye swala moja la ugonjwa.” “Acha nitazungumza na madaktari tuone.” Jelini akambusu ule mkono.  

“Tutakuwa sawa Zenda. Usiwe na wasiwasi.” “Una uhakika?” Mama Jema akashangaa hilo swali! “Kwa asilimia zote. Naomba utulize mawazo hapa nilipo mimi.” Akabaki akimwangalia, ila akajua anatulia. Mama Jema akatoka kama kuwapa nafasi. Zenda akashukuru. “Nahisi nimekumisi Jelini. Hatuzungumzi! Hata nikiwa hapa huniangalii! Nikileta zawadi pia huna habari nazo!” “Mimi nakutaka wewe Zenda, kuliko chochote kile utakachonipa. Na ndio maana ukiwa hapa mimi nalala usingizi mzuri nikijua Zenda wangu yupo.” Hayo maneno yakawa faraja kwa Zenda aliyekwisha tishwa na Colins.

“Nitatoka na tutakuwa wote. Pole.” “Ukitoka hatutakuwa wote Jelini!” “Kwa muda tu mpaka niwe sawa. Nahitaji msaada wa mama, wewe ukiwa kazini. Sijui nitakuaje bila hizi dawa na wakinitoa hii mirija ya haja ndogo. Sijui kama nitakuwa na kizunguzungu au la! Lazima niwepo na mama kwa muda mpaka niwe sawa. Nikijisikia vizuri tunaendelea na maisha yetu, kama kawaida. Usiwe na wasiwasi.” Akatulia kama anayefikiria.

“Nenda kazini, na ukatulize akili. Kila kitu kitakuwa sawa.” “Nataka ubadili namba ya simu ili Doro asiwe na mawasiliano yako. Anakutafuta sana na jumbe zake kwako ni za kukushawishi vibaya.” Jelini akashangaa amejuaje! Zenda akajua. “Ninayo simu yako. Na Gumbo sijui nani, hao wanaume wa huko baa wanakutafuta mchana mpaka usiku wa manane! Hapana Jelini. Mimi hivyo SITAKI.” “Basi kweli tubadili namba. Na nini tena?” Akamuona anafikiria na kusita.

“Ni juu ya Colins?” “Kwani ni nini kinaendelea kati yenu?!” “Wala hapana stori ndefu. Usiwe na wasiwasi.” “Mimi nina wasiwasi Jelini. Anakuganda kupita kiasi bwana!” “Colins anaye mchumba wake. Na hata mimi aliniambia kabisa. Wapo serious. Ni mwaminifu kwake, hawezi kumsaliti.” “Usiseme hivyo Jelini! Hujamuona jinsi alivyokuwa hapa na wewe.” “Nafikiri Colins ni wale watu, watoto wa mama. Wanahuruma zile za kupitiliza. Sidhani kama ni nia mbaya.” “Sitaki huruma zake kwako.” “Ulishamfukuza, sasa unawasiwasi gani?” “Naomba na wewe uwe na msimamo naye. Tafadhali Jelini. Ajue wewe huna nafasi yake.” “Sitakusaliti Zenda. Tafadhali naomba uniamini.” “Nitakuona baadaye. Na wakikuruhusu nitakuja kukuaga.” “Sawa. Ila ujue nimefurahia umeniuguza. Sitasahau Zenda. Asante.” Zenda akainama na kumbusu mdomoni, juu tu. Akaondoka.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Mama yake akarudi. Wakaanza kucheka taratibu. “Kazi ipo.” “Namuhurumia Zenda wangu. Sitaki awe na wasiwasi.” “Lazima. Ungemuona huyo Colins!” “Kwani alikuwa akifanyaje!?” “Mmmh! Tutakuja kukusimulia mimi na Jema. Alikuwa akija hapa asubuhi, mchana na jioni.” “Colins!?” “Unafikiri kafukuzwa bure? Alijaa hapa na akiingia hapa utafikiri hakuna mtu mwingine ila wewe tu. Na anavyokugusa!” “Mimi siamini! Maana yeye alikuwa chaguo langu la kwanza, wala sikudanganyi mama yangu. Colins nilimpenda kutoka moyoni wala sitaona haya kusema.”

“Nikawa nikimuona au tu ile kumfikiria, napatwa na hisia za ajabu sana. Nasikia raha ile tu kujua yupo mtu kama yeye hapa duniani. Nikawa namuwaza mchana na usiku, siwezi kujisaidia. Nikajisikia kumpenda kupita kiasi na haikuwahi kunitokea kabla! Mpaka nikawa najishangaa!” “Jelini!” “Wala sitakuficha mama. Na hivi unanihangaikia hapa, bora tu nikwambie ukweli. Kwa mara ya kwanza, japo nazungukwa na wanaume na natongozwa na wengi, moyo wangu ukampenda sana Colins. Sasa nikajidanganya kutokana na kutongozwa kwingi na wanaume, nikisifiwa uzuri wangu mchana na usiku, nikajua itakuwa hivyohivyo kwa Colins, atavutiwa na mimi. Lakini ikawa kinyume kabisa! Aliniambia hata nisimsogelee anaye mchumba wake! Niliumia mama! Niliumia sana.” Akashangaa na machozi yanamtoka. “Moyo uliniuma kama niliyekuwa nikikatwa moyoni. Pombe ikanisaidia kuweza kulala. Maana kila nilipokuwa nikimfikiria yeye yupo hapa duniani, na si wangu, halafu hanitaki! Nilikuwa nikiumia sana.” “Pole mama yangu.” Jelini akacheka na kufuta machozi.

“Lakini mama, pia alizidi sana kunivutia na kuweka shauku mpya ya mimi kupata mtu wangu. Nikajiambia inamaana unaweza kupata mwanaume mzuri vile. Msomi na mwenye maendeleo kama Colins, na bado akawa muaminifu! Ikanigusa sana. Mbali na Jema na yeye akaongezeka kwenye kichwa changu. Kwamba si watu wote ni malaya.” “Na kweli. Maana si angeendelea tu na wewe huku akiwa na mwanamke wake?” “Sawasawa. Ila kitendo cha kunikataa mimi sababu ya mahusiano aliyokwisha kuwa nayo, na mimi najijua si mbaya, kiliniuma sana. Ila nikajiambia si wanaume wote au watu wote ni malaya na Colins ni kama Jema.” “Mbona humtaji na James?”

“Mimi nawajua wanadamu kwa kuishi nao mtaani mama. Wakiwa hawana macho ya watu wanao wafahamu kwa karibu, ila washikaji tu ambao wapo huru kufanya chochote mbele yao. Wanafanya mambo ya ajabu, lakini ukiwakuta kwa wenza wao au nafamilia zao, hutaamini kama ni wale wanaume wanao vuliwa suruali na malaya popote. James simjui kiundani ila kumsikia tu. Jema nimeishi naye, nimeyaona matendo yake akiwa hana pesa na anayo. Na Jema ni mzuri mama. Anavutia, mtoto wa mjini. Kitendo cha kuepuka vishawishi na kujituliza vile, amenigusa sana. Na namsemea Colins kwa kuwa alikataa hata nisimsogelee japo wenzie walibabaishwa sana na mimi, mpaka mtoto wa Zenda, lakini Colins alibaki kuwa mwaminifu kwa mpenzi wake. Aliniumiza sana, lakini pia alinigusa sana.”

 “Na kweli Zenda pia alishampigia simu kumuuliza kama ananifahamu. Akanikana! Sasa iweje aje, ajae hapa amchanganye Zenda wangu?!” “Mimi sijui kinachoendelea kwenye kichwa chake Colins, lakini mmmh! Lipo jambo!” Jelini akabaki akifikiria, ila moyoni kufurahia kumuona Colins kuwa amejali kuugua kwake na amekuwa akienda kumuona. Akafurahia, ila akajionya kwa haraka, kujiongeza zaidi ya pale juu ya Colins. Asije kuharibu kwa Zenda.

“Kama kuna watu wanaweza kuwa waaminifu, na mimi nataka kuwa miongoni wa hao waaminifu mama. Si kwa ajili ya Zenda tu, hata kwa ajili yangu mimi mwenyewe. Nitakana nafsi yangu kama Jema na yeye mwenyewe Colins, ili na mimi niongezeke kwa hao wachache waamini.” “Kweli Jelini!?” “Kabisa mama. Mimi sijawahi kuwa kwenye mahusiano kama hivi mimi na Zenda. Na kama Colins angenikubali yeye kwanza, kwa hakika nisingekuwa na Zenda hata iweje. Lakini alinikataa, sasa hivi nipo na Zenda, nitabaki kwake Zenda. Japokuwa nampenda san.…” Akasita. “Sitamsaliti Zenda kwa yeyote yule. Mimi nitabaki kuwa mwaminifu tu.” Jelini akajithibitishia, mama yake akimsikiliza huku akashangazwa naye. Hakuwa akimjua Jelini kwa namna hiyo. Alishajua ni mtoto aliyeshindikana vibaya sana na hatengenezeki tena! Akabaki kimya akitafakari.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Jelini akaruhusiwa, Zenda ndiye alilipia garama zote, mama Jema akashukuru, wakarudishwa nyumbani, Zenda hana raha. Kila akimkumbuka Colins na aliyokuwa akimfanyia Jelini, huko nyumbani asipomuona si ndio atahamia! Kuanzia Jelini anaondoka hapo hospitalini, mzee roho juu, Jelini hana habari. Anafikaje nyumbani kwao na kuhakikisha hakuna anayemsogelea! Hawezi. Alishindwa hata kumpa simu yake. Akabaki nayo. Wala Jelini hakumkumbusha simu yake. Akamuacha tu ili kujaribu kumtuliza.

Alipofika nyumbani kwao yeye akapitiliza chumbani, kitandani, usingizi. Ilipofika jioni ya saa kumi na mbili, dereva akaja kuleta simu. “Nimetumwa kumuangalia na kama mnahitaji kitu chochote.” “Tokea afike hapa, hajatoka kitandani zaidi ya kwenda chooni. Na naona hapa tupo vizuri, hakuna uhitaji. Tunashukuru.” Mama Jema akajibu kwa shukurani. Devi akaondoka kurudisha majibu.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Jioni yake kina mama G na Nanaa wakaleta vyakula hapo ilimradi tu kuonekana wapo na hiyo familia. “Ibakie kazi ya kuuguza tu lakini isiwe tena unafikiria kupika. Mpaka vitafunywa tumekuletea. Vitakusogeza.” Mama Jema akashukuru sana. “Kwani huna msichana wa kazi?” Nanaa akamuuliza kwa kujali. “Siwezi. Nilishindwa. Nilijaribu kuweka mmoja wakati huyu Jelini mdogo, nikashindwa.” Wakaanza kucheka jinsi alivyojibu.

“Hakika nilishindwa. Niliona amejaa humu ndani, nina kazi ya kumfundisha tu, halafu haelewi wakati mimi nina watoto wawili wakufundisha pia. Nikaona kazi moja ambayo ningefanya mimi mwenyewe kwa dakika 5, inachukua masaa! Unaelekeza. Halafu inakosewa. Inabidi kurudia! Nikamtoa haraka sana, nikabakia na wanangu. Kuanzia wakati huo, sijatafuta tena mtu. Labda nje tu. Ila ndani, ni mimi na wanangu tu. Sitaki kero. Nimebaki kusikiliza visa visivyoisha vya dada yangu na wasichana wake wa kazi. Kwake kunapita kila kabila na vijambo! Mimi hivyo siwezi.” Kwanza mama Jema mwenyewe alionekena mtu wa kazi. Mwepesi haswa kwa kumtizama tu haitaji msaada wa mtu kumpikia chai. Wakaendelea kuzungumza wakicheka, mwishoe wakaondoka na kumuacha mama Jema na faraja. Ukweli mahusiano hujengwa. Wakaanzisha kitu kingine kati ya mama G na mama Jema.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Akampigia simu Jema kumwambia. “Basi nikitoka kazini nakuja na mimi kula.” “Jema!” “Sasa vyakula vyote hivyo si vitaharibika mama na wewe!” “Wameviweka vizuri na kupanga kwenye friji. Nenda kapike kwako, mumeo ale.” “Wala usiwe na wasiwasi. Nitamwambia mkweo usiku tukutane hapohapo kumuona Jelini kumbe nataka niponee kwako. Wewe tuandalie. Tukija tunakula, anaenda kwenye mambo yake, mimi narudi kwangu kulala tu. Kesho naenda kazini mwepesi.” Akawa kama amekumbuka tena kitu kingine.

“Tena nifungashie na sambusa pamoja na vitumbua vya kunywea chai kazini, sitaki maandazi.” “Jema wewe mtoto! Na utataka na vya mumeo!” “Mama naye? Sasa unataka mkwe akanywee chai nini?” Mama Jema akakata simu, Jema akabaki akicheka.

Mapenzi.

Juma hilo likaanza kuwa zito kwa Zenda, mikono, akili, macho na moyo vinamtaka Jelini. Jelini hana habari analala asubuhi mpaka asubuhi. Ukali ukazidi huko kazini, hakuna kinachoenda sawa. Anagomba kuanzia anaingia mpaka anatoka jioni. Akawa kama mwehu. Kwenye mazungumzo ya Devi na dereva wake yeye mwenyewe Zenda ndipo Devi akagundua hiyo hali. “Mimi nahisi ni mwanamke wake. Ananituma kwao kila wakati!” “Sasa kabla wote hatujakosa kazi, akafunga kampuni, tafadhali nenda kazungumze na Jelini.

Kabla hawajaenda mbali kwenye mazungumzo yao, simu ya Zenda ikaingia. “Huyu hapa.” “Aisee pokea kwa haraka.” Devi akasimama kama anayemuona. Bila ya salamu, akamwambia aende akashinde hukohuko kwa kina Jelini na awe anamwambia kila anayefika hapo.

Devi akahamia nyumbani kwa mama Jema asiseme alichotumwa. Sasa mama Jema akawa anashangaa Devi haondoki! Amekaa tu. Mama Jema akamuhurumia. “Hapa hakuna kazi Devi. Nenda tu kapumzike.” “Yule mzee atanipiga bastola, aniue.” Mama Jema akawa hajaelewa.

“Nimeambiwa nikae hapa mpaka mnakwenda kulala.” “Ukifanya nini!?” “Mama yangu acha tu. Hapo kwake kuna vunjwa vitu vya thamani mchana na usiku. Nikikwambia vitu vya thamani ni thamani zile za mapesa mengi. Meza za vioo na marembo ya glasi yale mazuri haswa. Anapasua kwa hasira kwa jambo dogo ambalo hakuwahi kuwa na tatizo nalo kabla. Kashafukuza wafanyakazi wake wa ndani na wa nje wote. Hakuna sababu. Nasikia huko kazini hali ni mbaya. Amekua mkali kuliko pilipili, japo mwenyewe pia ni mkali, lakini nasikia vimezidi. Sasa watu wanahisi ni sababu ya Jelini.” “Makubwa! Sasa si aje amuone!” Devi akacheka.

“Mama wewe hujaelewa. Mimi nipo hapa kulinda pia. Mzee wivu. Hataki mtu amsogelee Jelini. Sasa na hivi hata simu zake hapokei! Akiniuliza namwambia dada Jelini anakuwa analala tu, ndio akiamka wakati anakula ndio anaweza kupiga simu, anazidi kuchanganyikiwa.” “Basi kazi ipo!” Jelini akiwa usingizini akasikia hayo mazungumzo, akaamka na kusikia kila kitu, akatoka chumbani. “Acha niende nikamtulize mama. Namjua Zenda, atarukwa akili.” “Sasa utafanyaje na wewe mgonjwa?” “Acha akaniuguze yeye mwenyewe ndio akili yake itamtulia.” “Unarudi?” “Nitakaa kama siku mbili hivi. Nilale bila wasiwasi wa kupigiwa simu zake na kuzikosa. Kesho ijumaa. Nilale na jumamosi, jumapili nitarudi.” Jelini akajikusanya, akatoka na dereva.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Akajiegemeza kwenye kiti, akalala mpaka nyumbani kwa Zenda. Alimwambia yule dereva asimwambie kama anakwenda naye. Kwa hiyo alipomuamsha kuwa wamefika, ikabidi atembee mpaka mlangoni. Akabonyeza kengele. Baada ya muda Zenda akafungua. Hakuamini alipomuona Jelini. Bila salamu akaanza mabusu. Alimkumbatia nakuzidi kumbusu hapohapo mlangoni. Devi alipoona hivyo akaenda kuegesha gari, siku ya kazi akajua ndio imeisha.

Uchu wa Mapenzi.

Jelini alimsikia jinsi anavyotetemeka huku akiendelea kunyonya midomo yake. Akamuacha tu kisha akamvutia ndani na kufunga mlango kwa mguu. Akaendelea kwa muda akinyonya midomo yake, kisha akamkumbatia tu bila hata kuvuka mipaka. Akatulia. “Nilikumisi Zenda wangu.” Akazidi kumloga. “Unajisikiaje?” “Sio mbaya. Bado natumia dawa kila baada ya masaa 8 ili nisisikie maumivu sana.” “Pole sana. Nimefurahi umekuja kuniona. Nilikuwa nahamu na wewe, sikujua chakufanya. Sikupati kwa simu kwa wakati, wala hakuna zile jumbe zako nzuri zinazo niliwaza! Nipo mpweke kuliko nitakavyokwambia.” “Ndio maana nimekuja.” Akambusu tena na tena ila juu ya mdomo.

“Naomba leo tulale Jelini. Najua itakua ngumu kufanya mapenzi kwa kuwa unaumwa lakini angalau nikushike tu.” Jelini akaanza kumchangamkia. Akaanza kumchezea mashine yake, Zenda anagugumia asiamini kuwa hatimaye mikono ya Jelini ndio inamchezea. Akalainika kama mtoto wa kike. Akamsogeza mpaka kochini, akamtoa suruali laini aliyokuwa amevaa kushindia hapo ndani. Ndio aina ya nguo zake anazovaa akiwa tu nyumbani. Akamwinamia na kuanza kunyonya huku akisikia maumivu ya kichwa, kisha akamkalia. Zenda akamtoa kigauni cha juu na sidiria, akaendeleza kumpapasa matiti na mwili kwa uchu huku penzi likiendelea. Kisha akamuinamisha kwenye kochi, ameshikilia tako huku penzi likiendelea mpaka akamaliza. Akarudi kukaa akamvutia Jelini kifuani, wakaendelea kuhema mpaka wakatulia.

“Asante kunifikiria Jelini wangu. Nilikuwa na hali mbaya kimawazo! Naona imeshakuwa ngumu kuishi bila wewe.” “Twende tukaoge, nilale.” Wakaoga bila mambo mengi, Zenda akijua Jelini si mzima. Ila alifurahi sana kuwa naye usiku huo.

Lakini Motoni, Tui Hufura.

Zenda akamwangalia akiwa amemlalia kifuani, ametulia Jelini tuli kama tui la nazi. Akambusu na kumtoa Jelini mawazoni, akamrudisha pale, akacheka taratibu kama kumuonyesha yupo naye pale. “Najua unajua kama Colins alikuja nyumbani. Lakini nilishindwa kumuona.” “Acha kunichanganya Jelini! Ulishindwa kumuona!?” “Ni lugha tu. Lakini nataka kukwambia hatukuonana.” “Najua.” Jelini akatulia.

“Na ilinibidi kumfuata na kuzungumza naye.” Jelini alishituka mpaka akakaa bila kutarajia na ndipo akaelewa ni kwa nini Colins hakurudi tena. Tui lishatiwa motoni, mkaa umechochewa. Kumekuguswa pabaya, sirini. Jelini akasikia kumuhurumia Colins. “Unashituka nini? Kwamba ulitaka awe anaendelea kukufuatilia?!” “Mimi nahisi umekuza Zenda. Yule kijana…” “Unasema nini Jelini?!” Akauliza kwa ukali mpaka Jelini akatulia. “Naomba tulia Zenda. Tulia.” “HAPANA. Sitaki michezo ya kijinga na SITAKI kuingiliwa.” Akazidi kukaripa.

Jelini hakujibu tena, akajirudisha kujilaza kwenye mto si kifuani tena. “Kwamba umekasirika mimi kumfuata Colins!?” Ukweli moyo wa Jelini uliumia sana asijielewe kinachomuuma ni nini wakati yupo na Zenda wala Colins si mpenzi wake! Lakini akakumbuka ahadi yake mwenyewe. Kuwa muaminifu. “Nawajibika kwenye furaha ya Zenda.” Akajionya na kujirudi kwa haraka akizizidi hisia zake.

 “Eti Jelini?” “Hapana Zenda. Ila naona macho yako, yako kwingi na si kwangu na ninacho kwambia.” “Yapo kwako na ndio maana naona wanaotaka kuniharibia.” “Kwa nini huwaachi tu, sisi tukatulia na yetu?” “Jelini!” “Mimi natulia na wewe Zenda na ndio maana nipo hapa. Hakuna mtu atanitoa kwako isipokuwa wewe mwenyewe ukianza kuwa na wanawake nje. Hapo tu ndio nitashindwa. Maana katika hilo tulikubaliana hapatakuwa na mjadala.” Jelini akamjibu taratibu akijaribu kumtuliza maana alishajua hasira zimempanda mpaka mwisho.

 “Ndio maana na mimi sitaki mtu atuingilie.” “Basi ndio maana mwenzio natulia, najiangalia mimi na ahadi zangu kwako ili nisije kukukosa. Kwa hiyo tafadhali tujiangalie sisi kuliko wengine. Ni hilo tu Zenda. Sitakusaliti hata iweje. Na ninamaanisha.”  Jelini akajirudisha kulala akiwa amempa mgongo.

          Sitaomba msamaha kwa kumfuata Colins. Mimi nakupenda na nitakulinda.” “Na ninashukuru kwa hilo. Nimefurahi kuwa hapa na wewe Zenda.” Akamwambia kwa upole ili kumtuliza. “Nilikumisi mpenzi wangu.” Jelini akaongeza kwa upendo, ujeuri wote wa Zenda ukaisha. Akamsikia akimsogelea, kisha akamkumbatia kwa kumuwekea mkono. Akajivuta juu kabisa kwenye mto akaanza kumbusu masikioni na shingoni mpaka Jelini akamgeukia.   

Wakaendeleza kiss za haja, akamuona anaingia ndani ya shuka, akaanza kucheka akijua kinachofuata. Zenda alizama huko akimnyonya vizuri mpaka Jelini akafanikisha bao. Maana mara ya kwanza ni Zenda ndio aliibuka mshindi. Akamtoa kinguo cha kulalia, akamnyanyua miguu juu nakuilaza mabegani kwake, akawekwa mtu kati. Akawa anaangalia vile anavyoingia na kutoka taratibu huku akigugumia yeye mwenyewe kama anayesikia raha ya ajabu. Amekamata hips za Jelini kwa nguvu zote, kama asiyeamini usiku huo yupo naye. Naye Jelini alimsindikiza kwa sauti ya huba, akilalama kwa utamu na kuzidi kumpagawisha Zenda.

Alianza taratibu kwa hisia zote mikono ikiendelea kubarizi kwenye paja zake, akimbusu mara kadhaa pale kwenye miguu ilipotulia mabegani kwake huku akiendelea na Jelini akizidi kulalama kwa raha aliyokuwa akiipata. Si mara zote Jelini alikuwa akipiga bao kwa staili hiyo, lakini alikuwa akimgusa maeneo yaliyokuwa yakimpa sana raha. Taratibu kwa utulivu mpaka akamaliza na kujilaza pembeni yake kama mfu. Jelini alimfuta na kumfunika, hana habari. Usiku ukaisha bila kutajwa tena Colins, na Jelini akajionya kabisa asipeleke mawazo huko kwa Colins. Akamtizama Zenda vile alivyolala, akambusu na kumkumbatia vizuri na yeye akapotelea usingizini.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Unaweza kutawala Hisia.

Itaendelea…

Mazito Na Mazuri Yapo Mbeleni. Usipitwe.

CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment