Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com Mapenzi & Pesa! - PART 2 - SEHEMU YA 24. - Naomi Simulizi

Mapenzi & Pesa! - PART 2 - SEHEMU YA 24.

Mama Jema akajua Colins ataharibu hapo. “Vipi Jelini mama yangu?” Mama Jema akaingilia kwa haraka. “Mama!” Jelini hakuwa amemuona mama yake. Alijua wapo tu wawili na Colins. “Nipo. Ndio nimeingia muda si mrefu.” “Zenda yuko wapi?” “Alikuwa akijiandaa aondoke. Nafikiri anaosha mikono hapo chooni.” Zenda akatoka maana alikuwa akisikilizia chooni.

“Vipi Jelini?” “Nimelala sana. Ila nilikusikia usiku ukinisomea kitabu ila nilikuwa nikishindwa kufungua macho.” Zenda akacheka taratibu asijue Jelini anajaribu kumpooza maana alimjua Zenda kwa wivu. “Vipi maumivu?” Ikabidi Colins asogee maana alijaa hapo kwenye kitanda! “Sisikii kabisa ila usingizi tu.” “Pole. Wape hizo siku tatu, wakulaze tu ili usiteseke maumivu.” “Unaondoka?” “Nitajitahidi kuwahi kurudi.” “Hapana. Fanya kazi. Mimi utanikuta hapahapa. Sitoroki.” Wakacheka. Zenda akatamani kumbusu, lakini mama Jema alikuwepo na Colins amejaa hana hata mpango wa kuondoka. Akamshika mkono na kumbusu. Jelini akacheka taratibu. “Jitahidi ule. Ukiwa macho unipigie simu, nikusikie.” “Nitajitahidi.” Zenda akatamani kumfukuza Colins aondoke pale, akashindwa aanzeje. Au abaki na yeye! Lakini alishaaga.

“Kukiwa na uhitaji wowote tafadhali msisite kunipigia, na wauguzi pia wanayo namba yangu. Nimewaambia kukitokea mabadiliko yeyote yale, nijulishwe kwa haraka. “Wala usiwe na wasiwasi. Huyu atakuwa sawa tu. Nitamuosha na kumlisha, ndio arudi kulala. Atakuwa sawa tu, wewe katulie kazini.” “Nashukuru.” Akamgeukia Colins. “Tunaweza kuongozana tu ili kumpisha mama, amsaidie Jelini kujisafi.” Akamwambia Colins kiungwana lakini ndio alikuwa akimfukuza pale. Mama Jema hakutegemea. Akapigwa na bumbuwazi. Na Zenda alivyo, akamsubiri Colins atoke mlangoni ndipo akafuata na yeye akatoka na kufunga mlango.

Mama Jema akabaki ametoa macho mdomo wazi. “Jelini!” “Ana wivu wa kupindukia na hajifichi. Sasa mimi kumsaidia, simu zake zote nampigia kwa video au kupokea video.” Mama Jema akaanza kucheka. “Sasa na huyu kijana naye mwenye sura ya kike naye ni nini?” “Yupo hivyo na sura yake hivyohivyo. Anafanya kazi na shem.” “Mbona hilo nalijua. Stori yake naye ni ipi!?” “Wala si ndefu. Wewe nisafishe mama yangu.” “Ila Colins mzuri bwana huyu kijana! Midomo ya pinki kama kapaka rangi ya midomo! Macho! Yupo kama mtoto wa kike! Ila sauti sasa! Ikajaa chumba kizima, tena yakubembeleza!” “Acha kunichombeza mama Jema, kunitoa maneno! Mwenzio mgonjwa.” Wakaanza kucheka.

Ipo Garama Ya Kulipa Kupata Amani/Upendo.

Kwenye mida ya saa nne asubuhi mama Jema akiwa amejikalia peke yake akaingia mama G na Nanaa. “Jema aliniambia mtakuja, niwasubirie nisitoke kabisa.” “Ulikuwa ukienda wapi? Maana kama ni kitu chakununua mimi naweza kukimbia nikakununulia.” Nanaa akawahi. “Ni chakula tu. Niliondoka nyumbani mbiombio kumuwahi huyu, sikufanikiwa kula.” “Basi hicho tumekuletea chakutosha.” Mama G alijiandaa kwelikweli kwa mapishi, wakati Nanaa akijituma kitandani, alfajiri hiyo kwa mumewe.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Tena kwa raha zote baada ya kulala kwa furaha ya angalau amezungumza na Jema, akajituma kwelikweli mpaka Geb akajua mkewe amerudia hali yake. Halafu likawa penzi la kushitukizwa, wala hakuomba. Geb mpenda usingizi kama mwanae Liv, alitolewa usingizini na midomo ya Nanaa. Alimtoa nguo ya chini ya kulalia, akaanza kula tamu yake taratibu. Akidhani ni ndotoni, akanyoosha mkono kumgusa mkewe akijua amelala pembeni yake, bila kufungua macho, alipomkosa pembeni yake ndipo akili ikamjia si ndoto. Nanaa wake amerudi. Akaanza kucheka usingizini.

Akajiweka sawa, chali ili asijipunje. “Unapenda raha wewe!” Akamsikia Nanaa akiongea ndani ya shuka chini. “Kutoka kwako, sijivungi mama. Wewe endelea na yako, mimi nakutengea tu.” Akamsikia Nanaa anacheka na kurudisha mdomoni. Alipohakikisha mashine imewaka vilivyo, akataka kumkalia akiwa uchi kabisa. Na Geb aliipenda hiyo staili pia. Akiwa amelala, basi autazame mwili wa mkewe ukiwa mtupu kwa juu, akiwa amemkalia. Basi atamtizama penzi likiendelea kwa muda akimshika na matiti. Na Nanaa alimjua. Hachukui muda mrefu hapo, atakaa ili ampakate, aweke ziwa mdomoni, aendeleze mchezo mpaka apate kimoja, ndipo anabadili mchezo. Kama hatarudia, basi atamuinamisha mkewe ashike matako akiangalia kiuno au atarudia yakumpakata ili apate vyote kwa wakati mmoja.

Lakini asubuhi hiyo Nanaa akawa amechochea penzi. Mla ugali huyo kila siku, akaamka na nguvu. Hakutaka vya haraka, wakati akijiandaa kumkalia, akamdaka na kumlaza chali, na yeye akaingia chuvuni huku mkono ukivuta rimoti kuwasha tv kupunguza kelele za Nanaa, maana alijua baada ya muda mfupi tu, atamchanganya. Ikawa kweli. Geb alimchezea mpaka akampatia, Nanaa aliyekuwa hana hata wazo la bao asubuhi hiyo ila tu kutaka kumuweka sawa mumewe, akatulizwa mpaka akarudisha akili kwenye penzi. Akamchochochea kwa midomo, mpaka akamwaga mambo hadharani, Geb akamuinamisha bila kusubiri atulie. Nanaa akajua asubuhi hiyo sio bao moja. Mumewe hafungi penzi bila ya ziwa mdomoni. Hapo ndio anakuwa amekata kiu ya wakati huo.

Alikwenda mwendo mzuri, mpaka Nanaa akasikia raha tena. Akiwa ametoka tu kupiga bao, lakini akaamshwa tena hisia. Geb akaendeleza mchezo kwa muda mrefu mpaka akamshangaza Nanaa. Akamuweka chali na kumnyanyua miguu, akaibeba. Hapo ndipo akamchanganya zaidi Nanaa aliyelianzisha mwenyewe. Akajisahau ni mama wa watoto watatu na mama mkwe anaishi hapo, akajiachia haswa, mumewe akaongeza sauti ya tv na kuendeleza mchezo kama alivyomfundisha James, akimwambia hiyo staili akiitumia kwa makini huwa haiongopi kwa mwanamke yeyote maana lazima ashike G-spot. Sasa na yeye akaipatia, akaikamata na kuendelea kuisugua taratibu alipoona mkewe analalamika sana, kelele zinazidi, akamalizia kwa mdomo. Nanaa alipiga kelele ya huba maana Geb alikiminya akikinyonya kwa nguvu mpaka Nanaa akapaliwa na mate wakati akipiga bao la pili. Geb akaanza kucheka.

“Acha kunikomeshea bwana Geb!” Geb anacheka hana mbavu. Akakaa na kumpakata mkewe, Nanaa akajua hapo ndipo anajifidia. Huanza akijificha katikati ya matiti ya mkewe huku akimkumbatia na kumpapasa kwa uchu kila mahali, mpaka Nanaa mwenyewe anajua mwili wake unapendwa. Atamsaidia kumnyanyua huku wakiendelea taratibu, kisha ziwa litawekwa mdomoni, hapo hataki fujo. Nanaa atamuona jinsi anavyopandwa na hisia akimpapasa kwa nguvu mpaka anamaliza, ziwa hatatoa mdomoni kwake mpaka tone la mwisho kabisa, ndipo anaachia ziwa na kujilaza pembeni. Basi Nanaa naye atamkamua kabisa mpaka aridhike ndipo ananyanyuka. Asubuhi hiyo ilikuwa bao moja kwa mbili, lakini mchezo wa haja.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Nanaa anashuka chini baada ya kuoga kwa haraka, anakuta mama G alishapika kila kitu yupo chumbani akijiandaa, Jery anaondoka na watoto. Akaaga wanae, siku ikaanza mwepesi! Akaanzia ofisini na mumewe. Mama G akampitia hapo akiwa na vyakula ndipo wakaelekea hospitalini. Wakaaa na mama Jema kama lisaa tu, wakaondoka kwa ahadi ya kurudi tena kesho yake mida kama hiyo. Hilo walilofanya likamfariji mama Jema aliyezoea kulea peke yake akisaidiwa na dada zake, wanawake watafutaji wa mjini. Wapo busy kila wakati.

Kina mama G wanatoka, na wao wakaingia. Mode na dada yao mkubwa. Wakakaa na mama Jema kwa muda tu wakiongea yao na kucheka, na wao wakaondoka na kumuacha mama Jema peke yake. Lakini ameshiba, hana afanyalo maana kila kitu mgonjwa alikuwa akifanyiwa. Labda usafi tu wa ziada na kumpaka lotion asipauke, basi.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Wakati Nanaa na mama G wanatoka wapo sehemu ya kuegesha magari, wakamuona Bale anapita na magongo yake. “Hujambo Bale?” Mama G akawa kama amemuita. Naye aliposikia salamu ya kutambuliwa, akageuka. “Shikamoo. Sikuwa nimewaona.” “Unaendeleaje?” Akawasogelea. “Siyo mbaya, namshukuru Mungu. Huwa nakuja kwa mazoezi hapa.” “Joshua anajitoa nyie! Hakika naamini Mungu atakufungua macho na moyo, uone jinsi huyu mtu anavyojitoa kwako Bale, na umuheshimu kwa hilo. Hapa anakulipia garama kubwa sana. Nina uhakika ni mamilioni ya pesa anayokulipia hapa. Angeweza kukuacha tu au kukupeleka kwenye mahospitali ya hali ya chini, lakini ona garama za juu anazokulipia!” “Nanaa, najua. Hakika najua.” Bale akajiweka sawa akiegemea magongo.

“Najua sistahili kabisa kwa nilichomfanyia, najua. Lakini hata kwako na mama hapa, naomba nikiri nilikosa. Nimekosa mno. Najua ni ngumu kueleweka, na mimi sijui jinsi ya kujitete au kumfanya mtu akanielewa. Lakini ninachoweza kusema na kuwaomba, ni msamaha. Naombeni mnisamehe. Yaani kabla mtu mwingine hajaweka hukumu yake kwangu, mjue mimi mwenyewe naishi na hukumu kila siku. Nimeua..” “Sasa hapo Bale lazima utoke.” Akawahi mama G.

“Unanisikia Bale?” “Sina ji…” “Hapana Bale. Kama Mungu mwenyewe anasema amekusameha na hatazikumbuka tena dhambi zako, sasa wewe usimsikilize tena shetani. Hutatoka hapo. Atakuwa na kazi ya kukukumbusha kila wakati, na wewe mkumbushe shetani umesamehewa. Usimpe nafasi. Na najua hata kama ungepata nafasi na baba yako sasahivi, ukamuomba msamaha, kwa jinsi nilivyomjua baba Naya, na upendo aliokuwa nao kwenu nyinyi watoto, angekusamehe kabisa.” “Unafikiri hivyo?” Bale akauliza machozi yakimtoka.

“Sina shaka juu ya hilo kabisa. Baba Naya aliwapenda sana nyinyi watoto. Na alimjua Mungu kwa kumuishi. Ndio maana hakuwahi kuhadaika nje ya mapenzi ya Mungu mpaka kifo chake. Wewe jinyenyekeze chini ya mkono wa Mungu. Fuatisha alichokwambia baba yako enzi za uhai wake. Punguza haraka kwenye maisha, utafanikiwa kiroho, nafsi yako na mwili wako pia. Joshua ni Mungu kazini. Mwache afanye kile Mungu anamuagiza kwako.”

“Na mwigize jinsi anavyofanya mambo yake. Binafsi amenisaidia sana nilipokuwa kwenye wakati kama wako. Amenishauri, ameniombea, nikatembea kwenye ushauri wake. Sio rahisi, lakini namuamini Mungu atanitoa kwenye kosa langu maana nimeshaanza kuona mwanga. Sasa na wewe fuata anachokwambia. Na ujue ni nafasi ya upendeleo wa juu sana huyu Mungu amekupa kuwa na mtu kama Joshua. Yule kaka ana mambo mengi sana, lakini ona anavyojitoa kwako. Na ujue Joshua hafanyi jambo bila kibali kutoka kwa Mungu wake au bila kutumwa na Mungu. Ndio ujue Mungu hajakukataa Bale. Bado anakupenda na anakuhitaji.” Bale akalia sana hapo mbele yao.

“Naya anaendeleaje?” Akauliza akifuta machozi. “Anaendelea vizuri.” Mama G akamjibu kwa kifup tu. Akawashukuru na kugeuza akiwa anachechemea na magongo yake na wao wakimsindikiza kwa macho, mpaka akapotelea, na wao wakaondoka.

Pumu Na Mkohozi.

Mchana Colins akarudi tena. Ila Jelini alikuwa bado amelala. Akakaa hapo, mama Jema akimwangalia tu jinsi anavyomfunika Jelini na kuhangaika hapo akimtizama na kumshika viganja. Akakaa hapo kama lisaa. “Atapona tu.” Akajiambia, mama Jema kimya. “Ila afadhali hivi anavyolala ili asisikie maumivu.” Akaendela Colins, macho kwa Jelini. “Hivi ameamka hata kula chakula cha mchana kweli?” Hapo akamgeukia mama Jema. “Hajaamka. Na jana ilikuwa hivyohivyo. Alilala siku nzima.” “Si atadhoofu!” “Hayo maji hapo ni ya kumpa nguvu.” Akarudisha macho kwenye mkono uliokuwa na dripu. Akamuweka huo mkono vizuri. Akakaa hapo muda wakutosha tu akimtizama Jelini kama asiyetosheka. Mwishoe mama Jema akamuona anaangalia saa yake, akaaga na kutoka.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Kwenye mida ya saa kumi Jema akaingia. “Unacheka nini mama Jema?” “Pana hekaheka hapa, hujawahi ona. Zaa mwanangu ujionee.” “Haya?” Jema akataka stori. “Wewe unamjua Colins?” “Yule anayefanya kazi na James, anasura kama mtoto wa kike lakini sauti nzito na midomo kama kapaka rangi ya pinki?” “Umemaliza. Sasa sijui kamfahamia wapi Jelini, kutwa yupo hapa. Nasikia alikuja usiku na James wakamkuta Jelini kalala. Alfajiri kaamkia hapa, si kamkuta Zenda. Sasa wanaongeleshana pale, mimi na Zenda tunawasikiliza. Wanaongea kama wanao bembelezana. Yule baba kapatwa wivu, akatumia kama kaji uungwana lakini chalazima, kumfukuza.” “Mama!” Jema akashangaa.

“Bila aibu akamwambia atoke ili nimsafishe Jelini. Sasa naye alivyo, mchana akarudi. Kasimama pale pembeni ya kitanda cha Jelini zaidi ya lisaa. Anamfunika hivi, anaweka mkono vile, anaushika huo mkono na kujiongelesha mwenyewe.” “Wewe unasemaje?” “Kimya najiangalizia, maana ni kama asubuhi Jelini alimwambia, ‘uliniambia nikae mbali na wewe, nikaliheshimu hilo. Kwa nini upo hapa?’ Akasema..” “Mama! Jelini huyo?” “Jelini. Sasa huyo Colins anaonekana kama anajutia sana alichomwambia huyu. Naye Jelini hataki kabisa kumuongelea Colins kwangu ili nijue kinachoendelea. Sasa sijui walifahamiana wapi! Lakini ukiwaangalia na kuwasikiliza, utasema Zenda ana haki ya kuwa na wivu.” “Kazi ipo!” “Si kidogo. Na amesema atarudi.” “Mama wewe!” “Wewe usiwahi kuondoka, waje hapa, tujionee.” Wakaanza kucheka.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Baada ya muda akaingia James na Colins. James akambusu mkewe, na kumtakia hali kisha simu ikaingia, akatoka. Mama Jema akamkonyeza Jema maana Colins alipitiliza moja kwa moja kwenye kitanda. “Mama wewe!” “Sasa wewe angalia tu.” Colins akaanza kumtengeneza shuka kama limekaa vibaya! Wao wamekaa upande wa makochi, wakiwatizama Colins na Jelini.

James akarudi. “Vipi Jeremy?” “Anakazi yakuniongelesha kingereza hapo, namwambia mimi siwezi kuzungumza. Ananimbia ananifundisha nisione aibu kuongea. Kwa hiyo siku hizi ukija pale kwetu ujue lugha imebadilika. Si kichaga tena.” James akacheka sana.

“Naona mpaka mwaka uishe, nitakuwa nimekuwa mzungu na mimi.” “Na anavyopenda kujifunza!” Jema akamsifia. “Sana. Na kichwa chake kizuri sana. Hesabu huko ndio anaongoza. Na najua akiweza tu lugha, basi. Atawaburuza hao wazungu mpaka wamjue.” Ukimsikia mama Jema akimzungumzia Jeremy, utadhani mwanae wa kumzaa. Alimpenda kama kiziwanda wake.

Muda wote huo Colins alikuwa kama hayupo pale kwenye kile chumba. Kasimama pembeni ya kitanda cha Jelini akijipa kazi zisizomuhusu. Jema akamkonyeza mumewe. James akamtizama, amemshika Jelini mkono. James akakunja uso kama na yeye hajaelewa, akamsogelea. “Vipi?” James akamuuliza. “Haya mabandeji kichwani yanatisha!” Akaongea Colins akimtizama Jelini. “Namuhurumia!” “Atakuwa sawa tu.” James akamjibu na kujaribu kubadilisha mazungumzo ili kumtoa Colins pale, lakini Colins akawa anamjibu macho kwa Jelini. James akashangaa sana.

Disko Imeingia Mmasai Wa Uchi.

Mara Zenda akaingia na maua na mfuko mzuri sana, hawakujua ndani kuna nini. Ila akasalimia na kupitiliza alipokuwa mgonjwa, napo Colins akawa amejaa. “Sasa hapo ndio weka mgongo vizuri, jiegemeze, uone.” Mama Jema akamnong’oneza Jema. Jema akajiweka sawa. “Vipi  Jelini? Aliweza hata kuamka kidogo?” Zenda akauliza. “Amelala siku nzima. Kidogo tu alifungua macho tena nilikuwa nikimfuta, akarudi kulala.” Mama Jema akajibu. James akashangaa Colins hasogei!

 “Vipi na wewe kazi?” Akamuuliza James. “Tunaendelea tu. Tumepita mara moja kumuona Jelini, nihamie kazi ya upande wa pili kabla sijafunga siku.” “Pambana ukiwa bado una nguvu. Inakuja kulipa sana baadaye.” “Nashukuru kunitia moyo.” “Kabisa. Ukianza hiyo nidhamu mapema, na ukapata mke kama Jema anayekutia moyo, mkatulia hivyo, malipo yake ni mazuri. Sio baadaye tu, hata sasa.” “Nashukuru.” Akamtizama Jema na kucheka.

“Ila hilo namshukuru Mungu, aisee. Mke wangu muelewa mno. Ananifanya napata moyo wa kuendelea.” “Na hilo ndilo la msingi. Nyumba ikishagawanyika, hakuna baraka inakaa. Kwa hiyo mkigawana majukumu. Hata kama ni kwa muda, kwamba huyu apambane na kuweka ya nyumbani sawa, na wewe kuweka uchumi sawa, basi mkikusanya juhudi zeni, ujira ni mkubwa zaidi.” Mzee Kasa akashauri kiuungwana, James na Jema wakashukuru kwa nidhamu. Aliyefanikiwa akikushauri, lazima kusikiliza.

“Na wewe Colins umeoa?” Mama Jema akamkonyeza Jema baada ya Zenda kumuuliza swali Colins. “Bado.” Akajibu Colins na kurudisha macho kwa Jelini. Akamfunika tena vizuri huku akiweka sawa shuka la ndani. James akashituka, akaona amtoe pale. “Mimi naona sisi tuondoke. Jema, tutoe.” Colins akawa muungwana. Alivyosikia tu hivyo, akamuweka sawa mkono na kuaga na yeye. “Mungu atamsaidia atapona mama. Poleni sana.” “Asante Colins mwanangu.” Akatoka, James na Jema wakafuata nyuma.

Baada ya muda Jema akarudi. “Sasa mama Jema?” “Nisubiri unipe lifti.” “Dereva yupo nje anakusubiri.” Zenda akamwambia mama Jema. “Aah, nashukuru sana. Utakuwa umenisaidia. Ni sawa nikimuomba anipeleke nikamchukue na Jeremy?” “Mama Jema wewe! Mpaka mtu ajute?” Mpaka Zenda akacheka. “Nimeomba tu! Kama haiwezekani tutapanda hata bajaji.” “Hana kazi nyingine. Wewe mtumie mpaka umalize shuguli zako zote, ndio umruhusu. Usiwe na wasiwasi.” “Sasa si umeona bora nimeomba? Nashukuru sana. Na ndio nitapitia na sokoni kabisa.” “Mmmh!” Jema akaguna akikusanya vitu vyake. Wakacheka.

Wakajaribu kumuamsha Jelini. Akafungua macho. “Mama!” “Mimi ndio naondoka.” “Zenda yuko wapi?” “Yupo. Amekuletea na maua.” “Niwekee hapa kitandani niyashike. Ya jana sikuweza hata kuyashika.” Zenda akajisogeza. “Vipi?” “Pole na kazi?” “Asante. Unajisikiaje?” “Vizuri. Nimefurahi upo. Nishike mkono.” Jema akamtimza mama yake. Wambea hao! Zenda akamshika mkono usio na dripu na kuubusu. “Pole.” “Asante. Umekula?” “Nimewaambia waniletee chakula saa kumi na mbili. Utakuwa macho tule wote?” “Nitajitahidi. Nalala mwenzio, kama teja!” “Acha wamalize hizo siku walizopanga ili wakikutoa kwenye hizo dawa usisumbuke na maumivu.” Akavuta pumzi kwa nguvu na kutulia. Mama yake akamuwekea hayo maua hapo kitandani, wao wakaondoka.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Inaendelea...

CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment