Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com Mapenzi & Pesa! - PART 2 - SEHEMU YA 16. - Naomi Simulizi

Mapenzi & Pesa! - PART 2 - SEHEMU YA 16.

“Zenda anataka kuninunulia gari. Nilipomkatalia nikimwambia natakiwa kufikiria njia yakuniingizia pesa kwanza, kabla ya gari, ameniambia nifikirie na aina ya biashara ya kufanya, pia atanisaidia.” Mama wa kichanga akashangaa sana. “Jelini! Kumbe unaakili mwanangu! Lakini huyu Zenda ni mtu wa namna gani!?” “Siku ile ya harusi ya Jema kuna ambao walikuwa wakimfahamu, maana mtoto wake anafanya kazi na shem. Mimi nikamkataa mwanae, japokuwa alinihonga pesa nyingi, lakini mimi sikumpenda. Na ndiye niliyeamkia kwake siku ile baada ya harusi.” Mama Jema akazidi kushangaa.

“Sasa kwa nini hukumkubalia mwanae?” “Sijui kwa nini mama! Sikuwa na amani kabisa kila nilivyokuwa nikiwa naye. Chakushangaza, nilikutana na baba yake kwenye nyumba niliyoamkia. Nikiwa simjui kama ndiye Kasa mwenyewe niliyepewa habari zake kuwa ni tajiri sana na ndiye anayemfanya kijana yake kutamba mjini. Sikujua kama ni yeye maana Zenda ni mweupe, mama! Mweupe sana. Halafu kijana wake mweusi haswa. Kwa hiyo mimi sikumtambua. Halafu anamwili mzuri sana. Yupo kama kaka yake mwanae. Sasa kwa muda mfupi tukiwa naye…” Akamsimulia mama yake wakaanza kucheka jinsi walivyokutana na Zenda.

“Basi ndiye huyo. Mtu mzuri sana. Ila nimemuhisi ana wivu wakupindukia.” “Wewe ni mzuri sana Jelini. Lazima apatwe wivu. Na kama ni mtu mzima!” “Nitakavyotulia mama! Nampenda sana Zenda. Sana. Mbali na pesa, ni mtu ambaye nasikia raha kuwa naye.” “Mimi nina wazo la biashara.” Jelini akashangaa na kukaa sawa. “Nishauri mama yangu. Mimi sina moja.” “Mafuta ya taa na mkaa. Na si mafuta ya taa yakupima kwa mrija! Mafuta ya taa yakuweka kama kwenye kituo kabisa. Na mkaa. Utapata sana pesa. Mimi nilifikiria, ila nikawa sina mtaji. Na ni biashara ya uhakika, maana mkaa unatumika kila siku. Kingine gesi kwa wanao tumia gesi. Ukiuza hivyo! Aaahaa.” Jelini akafurahi sana.

“Asante mama yangu. Si tutafanya wote?” “Kama ukiniamini.” “Wewe nakuamini mama yangu, ndio maana nilikuwa nakuachia mwanangu.” Wakaanza kucheka. “Mwehu wewe!” “Kweli tena. Mwenzio nilikuwa nazurula sina wasiwasi nikijua mwanangu hatapata shida kwa kuwa wewe unaye. Ila nimebadilika. Na Zenda akinipigia jioni nitamwambia. Eneo?” Mama wa kichanga akachangamka. Wakatoka na Jelini kuanza kuangalia maeneo. “Mtu kama huyo hataki mambo ya kubabaisha.” Akafurahi Jelini. Akabaki akimshukuru mama yake.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Akaona Zenda anampigia. “Mwenzio nipo mtaani naangalia sehemu nzuri za kufanya biashara.” “Ndio upo shapu hivyo!?” “Nilikwambia pombe ndio zilikuwa zikinifanya nisifikirie Zenda. Umenifanya nitulie nijifikirie. Upo mzima lakini?” “Nipo mzima. Nilikuwa nikikuwaza wewe.” Jelini akacheka na kujisogeza pembeni ya mama yake. “Unaniwazia nini?” “Basi tu.” Ikawa kama amesita kusema. “Ndio umenipigia simu kunijulia hali?” “Nakuhakikisha upo salama.” “Mimi na mali zako zote, tupo salama.” Zenda alicheka sana. “Bora ningehakikisha mwenyewe.” “Fanya kazi Zenda wewe!” “Leo naomba tukutane mapema kidogo, nikuvue tena chupi.” Jelini alicheka sana.

“Kweli ajira umeipenda!” “Sana.” Alivyojibu, akamfanya Jelini acheke zaidi. “Acha nikushike tena na leo labda akili itatulia kazini. Kila nikifikiria, nakuona wewe tu. Mpaka nimeanza kuweka mazingira ya kuwahi kutoka!” “Basi usijali. Ukiwa tayari tu, tuma derava anilete popote ulipo.” “Hapo sawa. Na tukikutana uniambie hiyo biashara uliyofikiria na kuishukulia hatua kwa haraka hivyo!” “Sawa.” Wakaagana.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

“Huyo mwanaume kazi zitamshinda!” “Amesema anataka kuwahi kutoka kazini, tuwe wote.” Mama yake akacheka sana. “Na mimi nikiwa naye, namfanyia makusudi ili awe kama hivi.” “Basi atakua masikini.” “Hawezi. Anasema kazi zake zina mizizi. Hawezi kuharibikiwa. Acha nimbane mama, wasije kuniibia.” “Kwa hiyo na wewe una wivu naye?” “Sana. Nampenda.” “Sasa mwanae akija kujua?” Jelini akacheka sana.

“Mama wewe!” “Ndio ujipange. Maana yeye ulimkataa. Leo anaona unang’ang’ana na baba yeke!” Jelini akazidi kucheka akifikiria. “Nilikuwa sijaliwaza hilo. Ila wala simuogopi.” Mama yake akamtizama. “Naogopa mwaya.” Wakaanza kucheka. “Jasho litakutoka.” “Si kidogo.” Mama wa kichaga akampanga binti yake mpaka mipango ya biashara ikakamilika. Wakarudi nyumbani kumsubiria kaka.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Ikawa tofauti. Akarudi amepoa. “Ni nini tena?” “Kila mtu anazungumza kingereza, mimi sijui. Sina rafiki. Wananitenga.” Jelini akamuhurumia. “Nisikilize Jeremy. Wewe ni mtoto mzuri sana. Unaakili na mbali na hivyo pia ni rafiki mzuri. Lugha isikuogopeshe. Maana ukijitenga nao tu, ndio hutajua kuzungumza.” “Wao ndio wananitenga mama. Nikiongea kiswahili wananishangaa, halafu wanaondoka.” Jelini akakwama.

“Nisikilize Jeremy. Leo ndio siku ya kwanza. Jipe muda baba. Umenisikia?” Bibi yake akaingilia. “Au mimi nirudi tu kule shuleni kwa mwanzo?” “Basi utakuwa mtu wa kikimbia kila wakati. Hiyo ni nafasi nzuri sana, haitakaa ikajirudia tena. Hata hao watoto uliowakuta hapo hawajazaliwa wakizungumza kingereza. Walijifunza.” “Wengine wazungu.” “Si wapo na waswahili wenzako?” “Wapo, ila hawataki kukaa na mimi.” Jelini akaingia ndani nakuanza kulia.

“Nisikilize baba mzazi. Kama alivyosema mama yako, wewe unaakili sana Jeremy. Na leo ndio siku yako ya kwanza. Jipe muda. Utashangaa baada ya muda kwanza wewe mwenyewe utazoea. Halafu wataanza kukufuata wenyewe, kwa sababu wewe ni mtoto mzuri. Unavutia watu. Sasa hivi hawawezi kucheza na wewe kwa kuwa hawakujui. Na wenyewe ujue wanakusoma. Wakishakujua, ujue wataanza kukuomba urafiki.” Akanyamaza.

“Nionyeshe ulipoandika.” “Hesabu sio ngumu. Nimeweza zote. Ila kusoma ndio walinicheka. Wanasema nasoma kiswahili.” “Mwalimu akasemaje?” “Mwalimu aliwakataza wasinicheke. Akaniita nje, akanikabidhisha kwa mwalimu mwingine ndio nikawa nasoma naye. Yeye akasema mimi nina akili sana. Anahisi nitawafikia kwa haraka sana.” “Si umeona sasa? Jipe muda baba. Sawa?” “Kwa hiyo kesho nirudi tena kulekule?” Ikawa kama anaogopa! “Kulekule mpaka uweze na kuwapita. Sasahivi mimi na wewe kazi yetu kusoma. Nitamtuma mama yako akakununulie vitabu vingi, uwe unanisomea mimi.” “Wamenipa vitabu vya shule.” “Haya, badili nguo, uje ule, tuanze kusoma wote.” Akakubali, akaingia ndani.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Simu ya Jelini ikaanza kuita. Akaiangalia, alikuwa Doro. Akashituka ila hakutaka kupokea. Ikaita mpaka ikakata. Baada ya muda ikaanza kuita tena. Hata hakuiangalia simu yake. Ikaita mpaka ikakatika. Ikaita tena. Kisha ikaita tena na tena. Mwishoe akaivuta kuiangalia ili amtumie ujumbe kuwa atampigia baadaye. Kuangalia alikuwa Zenda. Amepiga mara 4. Akakaa kwa haraka na kumpigia kwa video. Akapokea.

“Acha kunitesa Jelini!” “Pole mpenzi wangu. Mwenzio nilikuwa nalia. Halafu nilijua ni dada Doro ndio maana nikaacha hata kugusa simu.” “Tuanze taratibu. Kwa nini unalia?” “Nitakwambia tukionana.” “Haya. Hapo ulipo ni wapi? Mimi nimepatwa wivu.” Jelini akaanza kumcheka. “Huibiwi Zenda.” “Mmmh! Mimi naota tu naibiwa. Hapo wapi?” Akasisitiza swali lake. Jelini akajua wivu kweli. “Haya, angalia vizuri.” Akaanza kuzungusha chumba kizima. “Hapa chumbani kwangu. Na hizi hapa kwenye droo ni chupi zangu.” Akamsikia akianza kucheka.

“Umeridhika?” “Nimeridhika. Na swali la mwisho, Doro anataka nini?” “Sijui Zenda. Wewe si umesema hutaki niwe kwenye mahusiano naye?” Hapo akamfurahisha. “Hakuongozi vizuri.” “Basi mimi sijawasiliana naye. Na ameniumiza kulala na Kasa. Mimi kwangu Kasa alikuwa mstaarabu. Sasa sijui wao wanafahamiana vipi, lakini sijapenda kulala kwake na Kasa, tena haswa akijua Kasa alikuwa na nia na mi...” Ila akasita. “Nisiseme sana. Maana nilishamkuta Kasa kwake. Sasa sijui! Labda walishakuwa na mahusiano. Lakini sasa kwa nini Kasa atake mahusiano na mimi tena? Au ndio Kasa ni muhuni wa kutembea na mtu na rafiki yake!?” “Sijui Jelini. Wao wawili ndio wanayo majibu ambayo sitaki ukaribu nao.” Jelini akanyamaza akijua kwamba hataki ukaribu hata na mwanae.

“Umenisikia?” Hapo mzee akasisitiza. “Labda kujua kulikoni kwa upande wa dada Doro kuliko kumuhukumu bila kumsikiliza.” “Utamfuata baa!?” Hapo akapoa. “Usitake kuniua kwa pressure Jelini, bwana!” “Usijali. Siendi tena kule baa. Siku hizi nikitoka…” Kimya. “Jelini? Malizia bwana usiniache roho juu.” “Nasoma ujumbe wa dada Doro umeingia.” “Unasemaje?” Akatulia akimalizia kusoma. Kisha akamtumia na Zenda kwa screen shot, ili tu kumtuliza.

Zenda alifurahia, roho ikamtulia. “Nimekutumia na wewe, umeona?” “Ndio nasoma. Kwa hiyo ndio unakwenda? Maana amesema itakua shangwe.” “Wewe mbona unasemea sehemu tu ya ujumbe huongelei juu ya Kasa?” “Kwa sababu najua amedanganya. Hakulala na Kevin kwa sababu Kevin alimtongoza yeye kwanza au walikuwa kwenye mahusiano. Kevin asingekuwa mjinga kukaa na wewe nyumbani kwake faragha, kwa uhuru, tena kwa baraka zake yeye mwenyewe, kama ulivyonisimulia.” “Lakini kweli! Maana mpaka alimwambia kuwa yeye ndio atanirudisha nyumbani. Tena Kasa alimwambia kama kwa amri kidogo!” Jelini akajaribu kukumbuka.

“Yeye alipatwa na tamaa kwa Kevin, sababu alikutaka wewe. Ndio na yeye akamtaka makusudi kama mashindano tu kukuonyesha na wewe kuwa anaweza kupata wanaume kama Kevin, au bado analo soko, au ni katika kulipiza kwake kisasi, au tamaa tu.” Jelini akabaki akitafakari. “Sasa unakwenda huko mziki na washikaji?” Akarudia swali lake la wivu. “Akuuu! Mimi sasahivi naenda kwa mpenzi wangu! Asitake kunichanganya. Wewe mwenyewe kukupata ni jioni tu, ndio nianze kwenda na miziki!” “Kwa hiyo ungenipata na mchana je?” “Labda kama wewe ungetaka, wala si wao. Mimi mwenzio napenda muda tunaokuwa na wewe, na sipendi nikuudhi Zenda. Najua upo na mambo mengi, mimi nataka ukiwa na mimi utulie. Sio tena na mimi nakuwa nakupa stress! Hapana. Kama ukitaka kwenda mziki, tutakwenda. Ukitaka tubaki nyumbani, tutabaki, ilimradi tukae na amani. Ndio maana nampenda mama yangu. Yupo kama wewe. Tukiwa naye huwa tunakuwa na amani sana.” Zenda akajisikia vizuri.

“Ila sitaki uone upo na mzee, anakubana.” “Wewe nibane tu.” Zenda alicheka sana. “Jelini!” “Kweli, nibane kwa kadiri ya uwezo wako na mimi nakuahidi nitakutii. Maana kunibana kwako wewe kunaniongoza vizuri. Hivi unajua tukiendaga mziki tunakaa mpaka kunakaribia kupambazuka! Nikitoka hapo nimechoka, nalala siku nzima, kisha baa. Sina muda na mwanangu, nipo kama mgeni kwenye maisha yake! Siku mbili tu nimekua na wewe, angalau najua maendeleo ya mwanangu! Wewe ni bane kwa kadiri ya uwezo wako. Tena ukiona jambo hulipendi, wewe niambie tu kama Jema.” “Ukinipa ruhusa hiyo sawa. Njoo basi nyumbani. Halafu uniambie kilichokuwa kikikuliza.” “Husahau!” “Siwezi. Kwa kuwa sitaki ulie.” Akafurahi Jelini, akaanza kujiandaa.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Akamuita mwanae chumbani. “Pole Jeremy.” “Asante.” “Lakini bibi alivyokushauri ndio vizuri. Ukikimbia ile shule, ujue hutapata elimu nzuri. Wewe hutaki kuwa kama wao?” “Ila mimi sitakuwa na roho mbaya ya kutenga watu.” Jelini akamuhurumia. “Basi ndio ukazane, ili uwapite, lakini ubakie kuwa mwema. Akija mtoto mwingine mgeni, akutane na wewe, halafu umpokee vizuri.” “Kwa hiyo nikazane si kwa ajili yangu tu? Na watoto wengine na wewe pia mama. Mimi nikiwa na hela nitakuwa nikikusaidia sanaaa.” Jelini akacheka na machozi.

“Hutanikimbia?” “Mimi sitakukimbia. Nitakutunza wewe na bibi Jeremy.” Mpaka mama Jema akacheka. “Bora uje ututunze Jeremy.” Akatoka kumfuata bibi yake. “Mimi nitakutunza bibi. Ukizeeka sana nitakuwa nakushika mkono mimi mwenyewe na kukuvalisha manguo mzuri kama ulivyokuwa ukininunulia.” Mama Jema alifurahi sana. “Basi uanze kwa kutokimbia elimu nzuri. Pambana palepale mpaka uwapite wote. Ukifanikiwa hapo, ndio ujue unaweka msingi mzuri wa kuja kutukomboa mimi na mama yako.” “Basi bibi. Sikimbii tena. Na hata kesho wakinicheka, silii tena.” “Hayo ndio maneno. Haya tuanze kusoma.” Jelini akawaacha wakisoma pamoja, bibi yake akimsaidia maneno magumu.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Gari ilimchukua na kwenda mpaka kwa Zenda. Gari ilipokuwa ikiingia getini, akamuona Zenda anatoka ndani kwenda kumpokea. “Daaah! Naona wewe mzee kakupenda. Mpaka anatoka kukupokea!” Devi ambaye ni dereva akaropoka na kuinua maswali kwa Jelini. Akatumia akili ya haraka. Akacheka. “Wengine huwa hatoki kuwapokea?” “Hivi wewe unamjua huyu mzee au unamsikia?” Jelini akacheka tu nakuona amuweke kiporo aje amdodose baadaye. Walipofika tu, akamfungulia mlango.

“Mimi napenda unavyokuja kunipokea.” Zenda akacheka. “Kwa kuwa nakua nakusubiria kwa hamu.” Jelini akacheka na kushuka garini, Devi kichwa mbele kama hayupo. Mzee Kasa alipofunga tu mlango, akaondoka kabisa pale. Jelini akamdaka midomo. Wakapata kisi zakutosha ndipo wakaingia ndani. Na walipofika ndani, kwa kuwa Zenda alikuwa amevaa suruali kama track, Jelini akaivuta na kupiga magoti mbele yake, akaanza kumnyonya. Suruali na boxer vikabaki magotini, mikono ikizunguka mpaka nyuma akimchezea mpaka kurudi mbele kwenye kokwa. Akamchezea wakiwa wamesimama hapo sebuleni, kisha akamsukumia kwenye kochi, akakaa.

Akaanza kujitoa nguo mbele yake, ndipo Zenda akamalizia zake akiwa amekaa akimwangalia. “Ugeuke pia.” Jelini akawa anacheka huku anajitoa nguo taratibu mpaka akamaliza. “Yaani hivyo kukuangalia tu, naweza nikajikuta napiga bao.” Jelini alicheka sana. “Geuka tena Jelini.” Akamgeuzia mgongo na kwenda kumkalia akiwa amegeukia mbele amempa mgonga. Akajinyanyua mpaka akafanikiwa kujipenyezea. Akaanza kujinyanyua taratibu na kushuka akimnyongea ndani. Zenda mwenyewe akawa anababaika hajui ashike kiuno au tako. Jelini akamfanyia taratibu, alipomuona anamng’ang’ania, akajua anamalizia, akambana kwa nguvu. Zenda alipiga kelele akimaliza. Hakufanya haraka kusimama, akasubiria mpaka tone la mwisho akiwa amemlalia kifuani kwa mgongo wake mpaka akamaliza, ndipo akamgeukia na kumlalia kifuani, matiti yakigusa kifua chake akihema.

“Hii ngeni.” “Umependa?” “Sana! Jelini unajua mapenzi wewe!” Akacheka taratibu akiwa ameweka uso shingoni kwake. Akamkumbatia vizuri, akamuacha mpaka akahema na kutulia. “Unapenda kwenda mziki?” Jelini akajua bado anasumbuliwa na ujumbe wa Doro. “Nafikiri pia na kampani. Lakini si kitu ambacho nakaa nakukimisi.” “Pengine ni kwa sababu ulikuwa ukienda mara kwa mara.” Akamjaribu. “Mimi nakuchagua wewe Zenda. Tafadhali niunge mkono. Usinisaidie kuhesabu ninayokosa huko nje, ila hiki ninachokipata hapa. Sijawahi pata mwanaume wa kunituliza kifuani kwake kama hivi wewe. Unanibembeleza na kunifanyia mapenzi vizuri.” Zenda akacheka. “Hiki nilichonacho hapa, huwezi linganisha na mziki bwana! Naomba toa mawazo huko kwa Doro, uwe na mimi hapa.” “Sitaki ujihisi upo kifungoni!” “Kama hiki ni kifungo, basi acha kiwe cha maisha.” Hilo likamnyamazisha kabisa Zenda akiwa amefurahishwa sana moyoni.

“Nikuulize kitu Zenda?” “Juu ya nini?” “Na uniahidi utaniambia ukweli.” Akanyamaza, Jelini akakaa vizuri na kumtizama. “Mbona hujibu sasa?” “Unanitisha.” “Wewe sema ukweli wala usitishike.” Akabaki akimwangalia. “Hiki unachokifanya kwangu. Tokea mwanzo. Kunipima, kunitumia dereva na kunileta hapa, tunafanya mapenzi, na kuondoka, unakifanya hivi kwa wanawake wangapi, na mara ngapi?” Akatulia akifikiria.

“Kwamba ndio tupo wengi hivyo?!” Jelini akashituka sana. “Hapana. Amebaki mmoja ambaye nitazungumza naye, napo nitafanya kwa ajili yako. Siwezi kusema yeye ni kama wewe. Yeye alijua wazi ni swala la mapenzi tu, na yeye namsaidia shida zake nyingine. Na sio mtu ambaye tulikuwa tukiwasiliana kama hivi wewe. Sikumfungulia huo mlango. Alikuwa akitumika kwa kusudi hilo tu, basi. Halafu nafikiri nilishawahi kukwambia, ni kisirani sana. Anakiburi cha elimu.” Jelini akakosa raha.

“Kujibu swali lako, nilishajaribisha kwa wanawake wawili au watatu kabla yake huyu. Nikahisi watakuja kuniua. Sikuwa na amani nao. Wao walikuwa wakubwa kwako halafu wadokozi sana. Kama wewe vile ulivyoingia kule chumbani kwangu ukashangaa na kutoka, wao walikuwa wakiondoka na vitu pia. Walikuwa wezi na tamaa zisizo na msingi. Nilikuwa nikiwapa pesa, lakini pia wakiondoka lazima wataondoka na kitu.” Jelini akashangaa sana.

“Lakini huyu niliyebaki naye tumekua naye zaidi ya miaka miwili nafikiri. Ametulia, si mwizi ila ni jeuri. Na kwa shule aliyonayo na wadhifa wake, nafikiri ndio maana vijana wenzake wanamuogopa. Ni mkorofi wakumuona usoni. Kwa hiyo nilikuwa nikimuita ninapomuhitaji.” Jelini akakosa raha. “Sasa mbona unakosa raha na umeniomba mwenyewe niwe mkweli?” “Kwa hiyo hapa ni kama nyumba ya kulala na wanawake zako!?” Zenda akatulia kidogo kama ambaye amemfanya afikirie.

Jelini akasimama. “Unakwenda wapi sasa!?” Akaokota nguo zake zote na kuzidi kuchanganya Zenda jinsi alivyokuwa akiokota. “Jelini?” Akajificha matiti na katikati ya uchi tu. Hips zote pembeni zinaonekana halafu amesimama mbele yake, Zenda hali ikawa imeshabadilika. “Kuvaa nguo, nahisi nakuondoka kabisa. Hapa mimi sitapaweza Zenda. Hii haina tofauti na nyumba ya kulala wageni. Inamaana muda na wakati wowote ule  wanawake zako wanaweza kuja hapa na kunikuta mimi uchi. Maana wewe wameshazoea kukuona uchi. Mimi mwenzio sijionyeshi kwa kila mtu. Na sio mpelekwa mahotelini kufanywa mapenzi, kama malaya. HAPANA Zenda.”

“Jelini umekasirika na unanifanyia si haki. Mimi nimekua mkweli kwako. Na sijawahi kugonganisha magari. Nilikuwa nikianzana na huyu, nikiona nimeshindwa, nahitimisha, naanza na mwingine. Sijawahi kugonganisha magari humu ndani. Na sifanyi umalaya.” “Kasoro huyu mwanamke wa mwisho, hajui kama mimi nipo!” “Kuwa mkweli Jelini. Mimi na wewe tumeanza jana tu! Ulitaka nifanyaje?” “Ndio maana navaa ili nisijekutwa na mwanamke wako.” “Sio wangu. Na jana nilikwambia kabisa nitamuacha kwa ajili yako. Au umesahau?” Jelini akatulia.

“Kuwa mkweli Jelini. Sikusema hivyo?” “Sasa mbona mpaka sasa hajui? Akiwa na shida na wewe, halafu akaja hapa?” “Nipe basi muda mama. Nipe nafasi ya kurekebisha. Halafu hata kama mimi ni malaya wa kiasi gani Jelini, kweli kwa yote haya bado nitafute mwanamke mwingine! Anipe nini tena?” “Mimi sijui bwana!” “Sitakusaliti, usiwe na wasiwasi. Kwanza wala si kwa sababu yako. Yangu mwenyewe. Mimi mwenyewe naogopa magonjwa. Naomba uniamini.” Akabaki amesimama na nguo zake sehemu anazojua wazi zinamtesa mwenzie akawa kama anayejishauri.

“Mimi sijatosheka.” Akamwambia kwa kumbembeleza. “Nakutaka zaidi Jelini wangu. Tutumie muda wetu vizuri sio kulumbana. Mimi napenda unavyonichezea. Nakaa siku nzima nakumbuka mikono yako mwilini mwangu. Hakuna mwanamke amewahi kunifanyia unayonifanyia Jelini wangu. Mimi nakutaka wewe, wala sirudii makapi.” Akasimama na kumsogelea. Hapo Jelini kichwa kinataka kupasuka kwa sifa. Kabla hajamshika akamuwahi. “Nataka kujisafisha kwanza.” Akahakikisha anamuwahi midomo. Akamkisi taratibu, kisha akamgeuza mbele. Akaanza kupapasa matiti huku akimnyonya sehemu za shingo, mwenyewe akaachia nguo. Zenda akampapasa huku akimuongoza njia mpaka bafuni.

Akamuachia na kuanza kufuta mashine ya Zenda kwa taulo. Nyumba ilikuwa na baridi, huwezi kutokwa jasho. Kwa hiyo akawa akimfuta na maji ya vuguvugu mpaka akaridhika ametakata. “Nenda kanisubiria kitandani.” “Hutaki na mimi nikusafishe?” “Hapana bwana Zenda! Sio mashindano.” Akatokaa akicheka sana. Mtoto wa kike akajisafi mpaka akaridhika.

Akatoka, alipofika tu chumbani Zenda akamuwahi. “Nakupa gari kabisa uwe huru kuja kunifumania utakavyo.” “Mimi sitaki gari ya kukufumania Zenda. Sitaki hata kuhisi kama nitakuja kukufumania. Kwa sababu najua siku nikikufumania huo ndio utakuwa mwisho wetu, na mimi sitaki kuachana na wewe. Kwa hiyo kaa tu na gari yako, ila tafadhali uwe muaminifu. Watu wanasema na jamii imeshozoea kusema hakuna cha peke yako. Mimi hivyo sikubali na sitaki. Ndio maana umenikuta peke yangu, kwa kuwa sikupata mwanaume anayeamini ninachoamini. Nikaamua kusubiri. Naomba uwe ni wewe Zenda.” Hakutegemea. Alimshangaza sana.

“Jelini! Nakupa gari!” “Nahitaji usafiri wa kukufikia popote ulipo, lakini sio kukufumania Zenda. Mimi hivyo sitaki. Nakutaka wewe Zenda. Gari ya kukufumania HAPANA.” “Basi mama. Nabadili lugha.” Jelini akapanda kitandani na kuanza kumchezea mwili kuanzia miguuni wala asizungumzie maswala ya gari tena. Akazidi kumshangaza Zenda. Utafikiri hapo alipo ana magari 20, Zenda anataka kumuongezea jingine! Kumbe hana hata moja. Wala kwao hawajawahi kumiliki gari. Jema ndiye mtu wa kwanza kuwa na gari kwenye familia yao. Yeye na mama yake, usafiri ni wa kudunduliza tu.

Wakati akimtafakari huyo mtoto, yeye Jelini aliendelea  kucheza na mwili wake taratibu. “Zenda wewe ni mzuri! Kila kitu chako kizuri.” Akaendelea kumsifia. “Napenda rangi yako na Zenda mwenyewe. Huyu naweza kulala usiku kucha nikimnyonya tu.” Zenda alicheka sana. “Tulia bwana Zenda, unanitingisha!” “Sawa mama.” Akaanza kumchezea kengele na kumchua uume wake kwa utulivu mpaka akamuona amelemewa, akahamisha mdomoni. Akaanza kumnyonya mpaka akakojoa. Chozi lilikuwa likimtoka Zenda, bila msiba, maana Jelini hakumuachia hata alipokuwa akikojoa, aliendelea naye tena akimkaba kwa nguvu zote mpaka mwisho. Anamaliza bado mzee amesimama.

“Nikajisafishe nisikuchefue?” Jelini hakumjibu, akamlalia nakuanza kumnyonya masikio taratibu akiweka ulimi. Zenda akaanza kupagawa tena akiwa amelala vilevile chali. Akajiona anakua mpumbavu akajitahidi kuhamisha mikono kwenye matako yake, akaanza kumkamata kwa nguvu, Jelini akajinyanyua na kujiingizia machine, Zenda analalamika kupita kiasi. Akamkalia kisha akahamisha mikono yake na kuiweka kwenye matiti yake, Zenda akawa akiyachezea, Jelini anamkatikia akimfinyia ndani. Akazidi kuweweseka mpaka akashindwa kuvumilia, akamgeuza haraka. Akamuweka Jelini chali, miguu juu. Akahamia kwenye K ya Jelini. Akaanza kunyonya mpaka Jelini akalainika kabisa.

Akampa ya kwao. Katerero. Acha Jelini aanze kupiga mayoe. Kichwa tu ndio kinamchezea kisime. Aliloa Jelini, akamvutia kwake akimuomba aingie, akamnynyua miguu, akapiga magoti katikati ya mapaja ya Jelini, mchezo ukaanza. Taratibu akimsikia Zenda akisugua meno. Akajua amekolea haswa. Akaendelea taratibu ila kwa nguvu haswa, Jelini alimsikia. Alichopenda ni jinsi alivyomshika. Mkono mmoja kwenye hips, mwingine tako akiliminya kwa hisia zote. Jelini alikuwa akisimkwa, hajiwezi. Lakini hakusahau kumbana na kukatika kutokana na mwendo wake. Alikuwa akilalama akimuita Zenda taratibu, Zenda akazidi kupagawa kila akisikia jina lake likitamkwa na Jelini aliyeonekana amekolea haswa hapo kitandani.

Mchezo ukaendelea kila mmoja akifurahia kivyake. Zenda alipogusa G spot ya huko ndani, akaharibu ustaaarabu wote, Jelini akajiachia akilia haswa, hakuna cha kukatika tena wala kumbana, ila kufurahia. Zenda akazidi kuongeza nguvu akijua amempatia. Ilikuwa mara yake ya kwanza kufika kileleni na mwanamke, wakati anafika, akiongeza nguvu kumbe ndio alikuwa akimfikisha na Jelini, Zenda alifurahi sana. Jelini alimkamua mpaka akaridhika yupo sawa, akashusha miguu.

Zenda akajitupa pembeni yake akihema kama Jelini tu. “Utanifanya nishindwe kufikiria vitu vingine Jelini. Niwe nikikufikiria wewe tu.” “Mwenzio nakupenda Zenda. Nakupenda sana. Natamani niwe na wewe tu.” “Nimeelewa Jelini. Nakuhakikishia sitakusaliti. Tutabaki peke yetu.” Akatoka kitandani. Akaenda kuleta kitaulo chenye maji ya vuguvugu, akamsafisha asijue anavyomshangaza. Hajazoea hayo kabisa. Alishazoea akimaliza na hao wanawake zake, ni kwenda kuoga, anawapa pesa, mchezo umeisha. Jelini naye akajisafi, akarudi.

“Njoo ulale kifuani kwangu.” Jelini anavyopenda kupendwa, akafurahi. Akarukia kitandani. Akamfunika akiwa amejilaza kifuani kwake. Akamkumbatia vizuri. “Nikwambie kitu ambacho sijakisema muda mrefu?” Jelini akamdaka midomo. Akapata kisi. Kila alivyotaka kumuachia, Jelini akamng’ang’ania akimnyonya ulimi taratibu huku akimchezea sikio. Akatulia hapo akiendelea kumchezea kisha akamuachia na kufungua macho. “Nakupenda Zenda. Nakupenda sana.” “Na mimi kwa mara ya kwanza, nimesikia upendo wa kweli Jelini. Kwa umri wangu huu, na utajiri unaonizunguka, sikujua kama naweza kuja kupendwa hivi. Nakushukuru kunipenda mimi kama Alexendar.” Jelini akarudi midomoni. Wakaendeleza kisi, wakinyonyana midomo kwa muda kisha akamuachia na kutulia. Wakapitiwa usingizi.

Akiwa usingizini akasikia mikono ikimpapasa kisha kunyonywa maziwa. Akacheka na kufungua macho. “Zenda!” Akaita akiwa usingizini. “Nakuamsha huamki!” “Nilikuwa nimefurahia ulivyokuwa umenishika.” Akambusu. “Twende nikakuonyeshe kitu.” Akaingia bafuni kusuuza uso na kinywa. Akachukua pipi kwenye pochi yake akaanza kumumunya. “Tunatoka nje?” “Hapana. Chini ya hii nyumba. Kwa ndani.” Achukua shati la Zenda akavaa.” Zenda akacheka na kumshika mkono. Wakaelekea mlango uliokuwepo karibu ya jikoni lakini kumbe unashuka ngazi. “Wewe nyumba yako ya ajabu Zenda!” akacheka. “Ila pazuri sana.” Wakashuka kama mizunguko miwili, akafungua mlango kwa kubonyeza namba. “Alam?” Jelini akamuuliza wakacheka wakikumbuka jinsi walivyokutana kwa mwanae.

Jelini akapokolewa na magari masafi sana. Mengine yamefunikwa na mifuko yake. Jelini akashangaa. “Unafanya biashara ya magari pia!?” “Hapana. Sasa, kasoro lile pale dogo la mwisho, ambalo najua hutapenda, niambie katika haya, lipi umependa.” Jelini akakunja uso akiyasogelea. Akamsadia kuyafungua mpaka ndani. Jelini akayaangalia, akamuona anacheka.

“Nini kimekufurahisha huko kichwani mwako?” “Hili gari zuri sana na napenda muundo wake.” “Ni Range spot. Very expensive. Umeipenda?” “Sana tu. Lakini nilikuwa najicheka nasema nikija kumiliki gari kama hii, nitakuwa nalala macho nikiilinda. Na hivi pale kwetu hakuna geti la maana! Watakuja kuliiba mchana kweupee. Ndipo nitageuka mlinzi.” Zenda akacheka.

“Basi tutaanza kuzungushia ukuta na geti la maana kwa ulinzi, ndipo ulichukue. Ni lako.” Jelini akamwangalia kama ambaye hajamuelewa. “Nakupa hili gari likusaidie kukufikisha nilipo.” Akarudia maneno yake. “Nitaliweka wapi mimi, Zenda!? Kwetu hapako hivi, mlinzi wetu wa…” “Acha vipingamizi Jelini. Naomba upokee kwanza.” Akaangalia kisha akashangaa anaanza kulia.

“Acha hizo Jelini bwana!” Akajifunika kabisa akazidi kulia, Zenda hakutegemea. “Ndio umefurahi?” Akakubali kwa kichwa. Zenda akaanza kumcheka. “Usinicheke bwana! Sasa mimi gari kama hili ningepata wapi?” “Kwangu.” “Kaa hapo kiti cha nyuma Zenda.” “Unataka unipeleke wapi?” “Nakuendesha kwenye gari yangu, mpenzi wangu amenipa. Nataka wewe uwe abiria wangu wa kwanza.” “Sasa mbona nakaa nyuma tena?” “Wewe unapewa lifti kwenye gari ya watu, na masharti!? Ukoje Zenda! Panda bwana acha ubishi.” Akapanda kiti cha nyuma.

“Mbona huulizi funguo.” “Funguo zangu zote ninazo.” Zenda akaanza kucheka akawa kama ameelewa. Jelini akamfuata hapo nyuma, akaanza romansi akivuta pensi nyeupe laini aliyokuwa amevaa. Akainamia koni. Ananyonya huku akimchezea vinyweleo vya mapaja. Zenda alikuwa akiweweseka, kisha akamtoa nguo ya juu akiwa ametoa mdomo kwa mzee, akaweka mkono akimchua, mdomo unamlamba bila kuacha mate, akipanda juu akiwa amekaza ulimi. Zenda alikuwa akitetemeka baada yakufikia chuchu zake. Chuchu za kiume zikaanza kuchezewa. Kisha akamkalia akiwa anajiingizia.

“Hutaki nikuandae?” “Mwenzio nikikuona hivi Zenda, na kukunyonya, naloa. Hapa nipo tayari.” “Kweli Jelini?!” “Nakupenda Zenda.” Akamwambia sikioni na kumbusu. Akatoa shati la Zenda alilokuwa amelivaa na kulitupia kiti cha mbele. Akabaki uchi akiwa amepakatwa miguu ametuliza kwenye kiti, mzee yupo ndani. Akachukua mikono yake, akamshikisha kwenye matako yake, ziwa akamuwekea mdomoni, akaanza kujivuta juu akiwa anakwenda mbele na nyuma huku akikatika. Alifanya hivyo mpaka akamuona mtu mzima anatokwa na machozi. Jelini taratibu huku vidole vikimchezea masikio. Alishajua hajiwezi akishikwa masikio.

Hakuchukua muda, akamwaga chuzi lote, Jelini akiendelea kumbana akizunguka hapohapo bila kunyanyuka asije akachomoa akiwa anamalizia. Alipotoa ziwa mdomoni na kujificha katikati ya matiti, akajua amemaliza. Akabaki akipitisha vidole kichwani kwake taratibu akamuacha atulie kabisa, akamwangalia. “Asante.” Jelini akacheka na kumbusu akataka kutoka. “Subiri kwanza.” Akajirudisha kukaa vizuri na kujivuta akiegamia pembeni ya kiti cha mbele.” “Kesho kuna kijana anaitwa Zilo, atakupeleka kubadili jina la hii gari, uwe na vitambulisho vyako, iwe kwa jina lako.”

“Nashukuru Zenda. Lakini sitakuwa na pakuliweka!” “Nimekwambia tutatengeneza uzio na kuweka ulinzi wa maana.” “Nimekusikia Zenda. Ila ujue mwenzio nina mama wa kichaga. Kila pesa ikiingia mkononi mwake, anafikiria kuzalisha sio kujenga ukuta wa kulinda gari.” Zenda akacheka sana. “Hakika atanikimbiza kama mjinga. Hapa nilipo nina biashara ambayo ilikuwa tufanye naye, tumekwama mtaji. Nikienda na pesa ya kujenga ukuta wa kulinda gari, atahisi nimegonga kichwa mahali, wala si bangi. Hawezi kunielewa. Nashukuru, lakini acha nianze taratibu mpenzi wangu.” “Vyote vinaweza kwenda pamoja. Usijali. Nitumie mchakato wa biashara na garama zake. Kuna mtu nitamtaka aupitie mchakato mzima, halafu tujue tathimini yake. Ni mtu wangu, namuamini kwenye maswala la mipango. Wewe nitumie mchakato mzima, ila kwa maandishi tafadhali. Nikikamilisha, nitarudi kwako.” Jelini hakuamini.

“Nashukuru Zenda. Asante mpenzi wangu.” “Sasa ukianza biashara tutapata wapi muda wa pamoja?” Ikawa kama analalamika tena. “Huyohuyo mama. Anaakili sana ya biashara.” “Unamuamini?” “SANA. Namuamini na mwanangu, ije kuwa pesa!” Hilo likamgusa sana Zenda. Kwamba cha thamani kwake ni Jeremy kuliko hata mamilioni ya pesa! Akazidi kuvutiwa naye kuona si limbukeni wa pesa kama wanawake zake wote aliokwisha kuwa nao na wanao mzunguka.

“Naamini hakuna chakututenga Zenda. Si ndiyo?” “Usije kufanikiwa sana ukanisahau Jelini!” “Mafanikio yangu ni kuwa na wewe Zenda. Mimi mwenzio nakupenda, kuliko kila kitu. Hata usiponisaidia chochote wala sitajali ilimradi niwe tu na wewe. Nimeona watu wenye pesa, tulikuwa tukishinda nao kule baa na wanamanyumba kama haya yako. Lakini nyumbani hapakaliki. Ukisikia historia zao ndio utachoka kabisa. Ndio maana mimi nikatulia, nikisubiria mtu wangu. Sina haraka za mali, kama mahusiano. Sijawahi lala njaa. Mama yetu anahangaika kweli ili tusije wahi lala njaa. Kwahiyo naweza nisiwe na mali nyingi au msomi, lakini mimi napenda mahusiano yaliyojengwa kwenye mapenzi ya kweli na si pesa.” Zenda akafurahi kusikia hivyo.

“Kwa hiyo niwe na uhakika na wewe?” “Kabisa Zenda! Mwenzio mimi sina tamaa za wanaume. Ni hivyo hunijui tu. Mimi sio malaya.” “Hapo nimeridhika.” Wakarudi juu. Usiku huo Zenda akahakikisha Jelini anakula ndipo wakaagana.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Hatimaye Kwa Umri Wake Zenda Anakutana Na Binti Mdogoo, Anayemuonyesha Penzi Zito Na La Kweli.

Jelini Amesimamia Penzi Lisilolemewa Na Pesa.

So Good To Be True. Right?

Nini Kitaendelea?

CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment