Jumamosi ya kikao Cha Mwisho.
Atafutaye Asiyechoka.
Kilikuwa
kikao cha mwisho ili ianze kitchen party kisha send off ya Jema
ndipo Bigday, harusi. Wakapanga mengi ya mwisho, Jelini akapewa jukumu
la kuwahi ukumbini na kuhakikisha kumepambwa vizuri na vyakula vimewasili bila kukosekana
hata kimoja kama walivyolipia. Alipopata majukumu yake akamnong’oneza mama yake,
kisha mama yake akamuuliza. “Kwa hiyo usiporudi niwe na wasiwasi?” “Nipigie
kabisa. Sitachelewa. Na si umeona hata sijanywa hapa! Sikutaka nishindwe
kufikiria. Nitarudi.” Akachukua bodaboda na kuondoka kuelekea Kunduchi kwa
Doro.
Alifika
ni kama alikuta watu wengi hapo bustanini kwa Doro wakinywa, hakutegemea. Akaingia
kwa kujificha mpaka ndani sebuleni napo akakuta watu wengine! Doro alipomuona
tu ameingia hapo, akamkimbilia. “Mbona watu wengi hivyo!? Mimi nilijua
wachache!” “Walevi wote hao wameitana kukesha wakinywa hapa kwangu, wala
usihofu.” Jelini akaangaza macho. Akamuona anacheka. “Ni nini?” Doro akauliza. Mara
Kasa akasogea. “Yaani wewe ni msafi kila wakati na kila mahali!” Jelini
akampokea kwa hizo sifa kitu kilichomfurahisha sana Kasa. Amesifiwa na Jelini!
Hakutegemea.
“Na wewe
ni msafi Jelini.” “Asante.” Wakacheka Doro akiwatizama. “Sikujua kama
unafahamiana na dada Doro!” “Dunia ndogo.” Akajibu Kasa. “Kwa kweli. Ila
nimefurahi kukuona tena.” Akaongeza Jelini na kumshangaza zaidi Kasa. “Kweli au
unaongea tu? Maana si ulichokisema mara ya mwisho tulipokutana Jelini.” Jelini
akakunja uso. Doro akaona awapishe. “Kasa na Jelini, nyinyi karibuni. Mjisikie
huru popote. Na msisimame hapo. Jikoni pametulia hakuna mtu.” Jelini akacheka bado
na mshangao usoni kwa kile alichokisema Kasa, Doro akaondoka.
“Naomba
twende jikoni.” Jelini akaongoza njia Kasa akamfuata nyuma akicheka. “Niliongea
jambo baya kwako!?” Jelini akamgeukia na kumuuliza mara walipofika jikoni.
“Tena mbele za watu.” Kasa akajibu, akamuona ameshituka na kujifunga mdomo.
Kasa akabaki akitingisha kichwa kumuhakikishia alisema huku akimpa tabasamu.
“Naogopa hata kujua nilichozungumza. Ni kibaya sana?” “Mimi kiliniumiza Jelini.
Hukuwa ukinifahamu ila ukanichagua kati ya kundi zima kunishutumu.” Akafunga
macho. “Naomba nisamehe...” Akawa kama anayefikiria jina. “Kasa.” “Yeah, Kasa.
Nisamehe kaka yangu. Mwenzio Jema anasema eti mimi mropokaji. Halafu
nikishakunywa, nakua naongea sana. Ndio maana nataka kupunguza pombe.
Zinanifanya sifikirii vizuri na..” Akasita alichotaka kuzungumza.
Akaona
ombe msamaha tu. “Nisamehe Kasa. Sikukusudia kukuumiza. Mwenzio sipendi
kumuumiza mtu.” Kasa akafurahi sana, hakutegemea kukutana na Jelini wa namna
hii. “Yameisha.” Jelini akawa kama hajaridhika. “Niliongea neno baya sana?”
“Yameisha bwana. Kweli yameisha na nimefurahi kukusikia kuwa hukumaanisha.” “Ni
vile hujanizoea. Mwenzio naongea sana. Ila nakuahidi kubadilika. Nitakuwa
makini na maneno yangu. Na nimefurahi umenisamehe.” Kasa akacheka akimwangalia.
“Umekula
au ungependa nikutafutie kitu cha kula? Mimi hapa ni mwenyeji kidogo. Nilikuwa
nikilala hapa kwa dada Doro. Kwa hiyo ni mwenyeji.” “Ulikuwa ukilala, Kwa
hiyo umeacha?” “Nimeacha kupenda kwa watu.” Wakacheka. “Kwa hiyo umehamisha
kijiwe kwengine?” “Kwa mama Jema. Ndio hanichoki.” Kasa akavuta kiti na kukaa.
“Wengine wanakuchoka?” Jelini akacheka. “Niambie ungependa kula nini
nikutayarishie.” “Mimi nataka nikae na wewe tuzungumze tu, au unataka kwenda
kunywa nje na wenzenu?” “Leo narudi kwetu. Sitaki kunywa sana. Kwanza mtu kama wewe
unataka kuongea nini na mtu kama mimi!?” Akajishika kabisa kwa kushangaa.
“Wewe
ukoje na mimi nikoje?” “Wewe unaonekana unatokea kwenye daraja la juu sana
kwenye maisha. Mimi mwenzio hata sijasoma! Washikaji zangu ni walevi wa baa
ambao hatufikirii chakuongea. Kinachokujia kichwani ndio hichohicho unakitoa
mdomoni.” Jelini aliongea akicheka kama mazuri. Kasa akacheka na yeye. “Mimi na
wewe hatuwezi kufanya mazungumzo hata kwa dakika 10. Utachoka bure. Bora niende
kwa wale walevi kule nje tunaozungumza lugha moja.” “Unataka kurudi nyumbani
saa ngapi?” “Nikipata bia mbili tu, naondoka kabla sijazidisha.” “Unarudije
nyumbani?” “Bodaboda, daladala, bajaji, chochote kile sichagui ilimradi tu
kufika nyumbani.” “Hutaki nikusogeze?”
Jelini akacheka akifikiria.
“Vipi?” “Mwenzio
misaada ya watu naogopa. Watu wanapenda kukupa kitu halafu wanakuja
kukudai baadaye.” Kasa akabaki akimwangalia. “Kweli tena. Unakuta unapewa kitu
vizuri tu. Unakua na haraka yakupokea, kumbe mwenzio anakuwa na lengo jingine.
Sisemi kama ndio tabia yako! Lakini mimi mzito wa kupokea misaada hata kama ni
midogo kiasi gani.” “Nakupa lifti sio nakupeleka. Maana na mimi naondoka sio
kwamba nalala hapa. Kwa hiyo usihesabu kama ni msaada. Hesabu kuwa gari
inaondoka hapa ikiwa na nafasi.” “Sitaki kukusumbua au kukuchelewesha.”
“Nilifikiri hutachelewa!” “Stori zinaweza kuzidi, nikabaki kucheka.” “Hudhani
kama utapitisha maamuzi ya unywaji kwa usiku wa leo utakapo baki na wenzio
wakiendelea kunywa?” Hapo akamfanya afikirie.
“Basi
bora hata nile tu niondoke, dada Doro asijisikie vibaya. Anaweza dhani bado
nimemchukia kwa maneno mabaya aliyonipa.” “Maneno gani tena!?” “Acha
nisiyarudie kwa sababu nilishamwambia nimemsamehe. Ila acha anione hata
nimeshika sahani ya chakula, ataridhika.” “Utakwenda kula wapi?” Hilo swali
likamfanya Jelini acheke akifikiria. “Nataka kuwepo, ulipo.” Akaongea Kasa akibembeleza
kidogo na kumshangaza Jelini. “Kwani wewe hunywi?” “Bia hapana. Ladha yake
mdomoni imenishinda kabisa. Ila nakunywa vinywaji vingine.” Akacheka na kusimama. “Basi acha nikachukue
chakula, nakuja kula hapahapa. Maana najua hata waliopo hapo sebuleni
hawaendani na wewe. Na sijui kwa nini alikukaribisha katikati ya watu kama sisi!”
Akatoka.
Akarudi
na chakula mkononi. “Unauhakika hutaki kula kitu chochote?” “Umekuja kwa
kuchelewa Jelini. Mimi nilishakula mapema. Huwa ikizidi saa 12 jioni sili tena.
Kwa hiyo nilipofika tu nikala.” Jelini akamtizama na kunyamaza. “Mbona sasa
sikuoni na bia?” “Kwa kuwa wewe upo. Na nilishakukosea, sitaki kukunyima raha
na bia kitu ambacho si rafiki kwako.” Akamuona ana utu. “Lakini nisingejali.”
“Haina shida. Bia huwa zipo tu.” Akaendelea kula huku akimtafakari asiamini
kama amekaa naye na ametulia si mapepe kama alivyokutana naye mara ya kwanza.
Pakawa na
utulivu wa namna yake. Jelini akijiwinda na maneno yake. Akaingia Doro
akijihami. “Dada Doro chakula kizuri sana. Ila ni kawaida yako.” Akamgeukia
Kasa. “Dada Doro anapika sana. Akikutengenezea nyama ya foili, utakula mpaka
basi. Halafu usafi wake ni wa mpaka bafuni! Ndio maana napapenda kwake.” Kasa
akamtizama Doro kama kumkumbusha swali lake wakati akimsema Jelini. Kwamba, ‘Je
nikikaa na Jelini naye atakusema hivyohivyo kama wewe?’ Akakumbuka na
kujibaraguza. “Kawaida tu.” Akajibu Doro akimkwepa Kasa.
“Mimi
nikimaliza kula naondoka dada.” “Sasa si tulale tu leo? Gimo kaleta pombe kibao!”
“Acha ninywe siku nyingine dada yangu, leo nirudi tu nyumbani.” “Jelini naye!”
“Acha dada nikue kidogo. Nimezidisha michezo na nyinyi wenye maisha yenu wakati
mimi sina kitu kabisa! Nakimbizana tu na nyinyi! Kweli si sawa. Hata hivyo
naona nipunguze pombe, nianze kufikiria.” Doro akacheka. “Wewe nicheke
tu.” “Nakuaminia. Nimekuona siku mbili tatu hizi! Si mchezo! Basi nisubiri
nikurudishe nyumbani.” “Mimi nitamsogeza.” Hapo Kasa akatoa macho kwenye simu
na kumtizama Doro kwa amri. “Bora, ili asiwe peke yake na usiku huu.” Akajirudi
Doro kwa haraka. Jelini akawa hajaelewa ila akaona anyamaze.
Doro akataka
kutoka. “Dada Doro, naomba nikuage kabisa.” “Huji hata kuwasalimia kina Gimo?”
“Acha iwe wakati mwingine. Gimo ataanza kunichokoza ilimradi tu nikae tuanze
kelele, wakati mama Jema ananisubiria nyumbani. Tutawasiliana na nashukuru
kunikaribisha leo.” “Kwa ugeni gani wa hapa na wewe!?” “Wewe pokea shukurani
zangu. Ungeweza kutonialika na nisijue kama umealika watu hapa. Nimefurahi.”
Kasa kimya, Doro akacheka. Jelini asijue hiyo yote ni pesa ya Kasa na amefanya
kwa ajili yake.
Chai Rangi, Huwezi Tia Tui La Nazi.
Wakaondoka
kimya kimya watu hawakuwaona. “Nashukuru kwa ushauri wakutobweteka pale. Na kwa
jinsi ninavyojijua mimi, nisingeondoka leo pale.” Jelini akavunja ukimya mara
tu Kasa alipotoa gari hapo nyumbani kwa Doro. Kasa akacheka. “Kweli tena. Zile
kelele pale zote zinanihusu. Watu wangu sana. Dada Doro ndio kampani
yangu. Tukianza kunywa na kucheka, tunajisahau mpaka tunakuja kufukuzwa baa
inafungwa.” “Umemzoea sana Doro?” “Sana kuliko hata Jema. Mtu mzuri sana halafu
tunaendana sababu ya pombe. Jema dada yangu yule mtakatifu, halafu hawezi
kelele. Sasa dada Doro mshikaji wangu. Tukianza kucheka, hatumalizi mpaka wakati
mwingine tunajisahau tulichokuwa tukicheka. Ni dada mzuri sana.” Kasa
akanyamaza.
Akamuelekeza
kwao. “Jumapili huwa unafanya nini?” “Mimi ratiba ya jumatatu na jumapili
hazina tofauti na hazijulikani. Napenda sana kulala. Na nikipata kitanda kizuri
na upepo uliochujwa kama pale kwa dada Doro, ndio nalala siku nzima.” Kasa
akacheka akimtafakari Jelini ila akaona amchukulie taratibu. “Kanisani?” “Mimi
na mama yangu ni wakristo jina. Hatuendagi kanisani. Kwa hiyo kama hivi
nikimkuta macho, tunaanza stori mpaka tuchoke ndio tunakwenda kulala na bibi
pia yupo kwa hiyo stori haziishi. Kingine mama hafanyi kazi siku za jumapili.
Basi hapo ndio kuja kuamka ni mchana. Kula, stori, siku imeisha.”
“Nikikukaribisha kanisani kwetu utakuja?” Alicheka Jelini. Kisha akacheka sana.
Mpaka
Kasa akaanza kucheka. “Sasa unacheka nini?” “Mimi nahisi nikiingia kanisani,
malaika wote watatoka wanipishe mimi na Mungu.” Kasa alicheka sana. “Kwa nini?”
“Kiumbe cha ajabu ambacho hawajawahi kukiona!” Kasa akatingisha kichwa. “Hapana
bwana. Utakuwa sawa.” “Nashukuru, lakini hapana. Kwanza sitaki kwenda kanisani.
Sio sehemu hata nawaza kuja kwenda.” Kasa akashangaa sana.
“Ulikosana
nini na kanisa?” “Ni sehemu ambayo sina mazoea nayo kabisa. Hata hivyo kesho
nataka kuwepo tu nyumbani. Najisikia kutulia nyumbani.” Akajibu hivyo kwa
msimamo kama ambaye katika hilo hakaribishi tena nyongeza, kisha akamuona
ametulia. Kasa akabaki akimtafakari na kujaribu kufikiria jinsi ya kumchukulia!
Akapata wazo jingine akaona amjaribu. “Jioni ungependa nije kukuchukua tukapate
ice cream?” Jelini akashangazwa. Akamtizama kabisa. “Unakumbuka nilikwambia
nataka kuwepo ulipo?” “Huendani na mimi na wala masikani zangu. Kwa kukuangalia
tu, maisha yangu na yako ni tofauti kabisa Kasa. Hutanimudu mimi, bora
nikwambie mapema usijipotezee muda.” Jelini aliongea kwa wazi bila hata
kumficha. Kasa asiamini anaweza vipi kukataa ukaribisho rahisi vile kutoka kwa
mtu kama yeye! Gari yenyewe anayoendesha Kasa ilionekana ipo neema.
Kwamba ipo ahadi ya kunufaika kuwa karibu yake. Lakini haikuwa hivyo kwa
Jelini! Na hakuzungumza kama mtoto wa kike akitingisha kibiriti!
“Nakua mkweli
kwako, Kasa. Mimi najijua.” Akaumia, nakuhisi kukataliwa vibaya. Ni Kasa!
Warembo wanammezea mate! “Nikuulize kitu?” “Niulize tu.” Jelini akakubali kwa
utulivu tu. “Kwa hivi nilivyo na unavyonifikiria nipo. Kama kweli ningekuwa ni
mtu ambaye unataka kuwa naye karibu. Umempenda kabisa. Ungefanyaje?” Hapo
Jelini akanyamaza akifikiria. “Eti Jelini? Maana mimi nimekuwa mkweli kwako.”
“Hunijui kabisa mimi Kasa. Na ninauhakika kama ungekuwa ukinijua mimi, wala
usingenipa hata hii lifti.” “Nimekupa lifti kwa kuwa nakufahamu Jelini. Mwenzio
sikuishia tu siku ile nyumbani kwa James. Niliendelea kukufuatilia mpaka
nikahakikisha leo nakuona. Nilikuwa pale nikikusubiri wewe.” Jelini akashangaa
sana.
“Kasa!”
“Nataka kuwa ulipo Jelini. Na sitakuchukulia muda mrefu. Ilimradi tu kesho
nikuone.” “Mimi!?” “Wewe Jelini, ndiyo. Naomba nikuone kesho jioni kama
kanisani umenikatalia.” Jelini akacheka. “Bora ice cream kuliko kanisani.”
“Basi iwe jioni ya saa 11.” Wakakubaliana lakini Jelini akiwa na maswali mengi
sana juu ya Kasa. “Naomba nikuombe kitu cha mwisho Jelini?” Jelini akacheka
vile anavyobembelezwa. “Nini?” “Namba ya simu.” Akamuona kama anasita. “Unasita
nini?” “Usinielewe vibaya Kasa. Nimezungukwa na watu, mimi tabia zao nazijua.
Wengi hawaishii vizuri na mimi. Wanatakaga na kadhalika. Halafu
ukiwakatalia wanakuwa wakali mpaka kutaka kunidhuru.” “Nakuhakikishia mimi si
mtu wa namna hiyo na sitafanya kitu
ambacho hatujakubaliana. Huoni kanisani nilikuomba, ulipokataa si uliona
sikukulazimisha?” “Lakini kweli.” “Mimi nataka kampani kama unayompa Doro.”
Jelini akashangaa sana.
“Doro ni
mpweke. Hana mtu.” “Basi na mimi sina tofauti naye.” “Bwana Kasa unanidanganya!
Nilikukuta katikati ya marafiki. Na kwa hali yako lazima una watu wengi.”
“Nisingekuwa hapa kama kuna mtu mwingine. Si tutakuwa wote, utaona.” Jelini
akatulia, akamuona anamkabidhi simu yake. Naomba jipigie kwa kutumia simu
yangu.” Jelini akafanya kama alivyoombwa lakini kwa hakika Kasa alijua
amemlazimisha si kitu alichokifanya kwa moyo. “Tayari.” “Nashukuru.
Nitakushusha uliponiomba, ila naomba usipande bajaji ili usianguke. Panda
taksii ili ufike nyumbani salama, kesho tukutane kwa ice cream.” Jelini
akacheka tu na kunyamaza. Akamsogeza mpaka karibu na sehemu aliyojua angepata
usafiri. Akamlipa kabisa dereva, ndipo wakaagana.
Akiwa
ndani ya taksii akielekea kwao, mahela yakaingia kwenye simu yake. Akashituka
sana. Akabaki ametoa macho akiangalia simu. Mwishoe akaamua kumtumia ujumbe. ‘Unanitisha
bwana Kasa! Hii pesa ni nyingi sana.’ ‘Usijali. Kawaida tu.’
Akarudisha kwa haraka na ujumbe mwingine ukaingia. ‘Umeshafika
nyumbani?’ ‘Bado, lakini nakaribia. Asante kwa pesa.’ Akaona awe muugwana. ‘Karibu. Ukifika nijulishe ili nilale nikijua upo salama.’ Jelini akasikia kujaliwa kwa namna yake. Kutoka kupigwa
kibao cha usoni na Colins, kuja kubabaikiwa na Kasa, kidogo ikamrudishia
ujasiri. Akacheka nafsi kwake.
Alifika
kwake, Kasa amejawa tumaini. Jelini aliyekutana naye siku hiyo akawa tofauti
kabisa. Alitaka kumpata na kumlipiza kisasi kwa kumdhalilisha, lakini
akajikuta anatizamia kwa hamu kuja kumuona tena, wapate muda naye zaidi. Kadiri
alivyokuwa akimuwekea ngumu, ndivyo alivyoamsha hamasa kwa Kasa na kutaka
kumfahamu zaidi. Kasa hakuzoea kuhangaishwa. Walio mfahamu kama ni kijana
aliyetoka kwenye familia ya aina yake, walikuwa wakiomba hiyo nafasi anayoiringia
Jelini. Kwanza kupanda gari ya Kasa yenyewe ilikuwa ni bahari ya mtende. Jelini
aliringia! Akaibua kitu cha tofauti kwa Kasa. Akili ikamzunguka na kumfikiria
kwa tofauti na alivyomsikia. Msichana wa baa tu! Akabaki akisubiria
ujumbe mpaka akahisi amemsahau.
Akiwa
anakaribia kupotelea usingizini ujumbe ukaingia. ‘Samahani nilichelewa kukwambia
kuwa nilifika salama. Usiku mwema Kasa.’ ‘Na wewe Jelini.’ Jelini
akacheka na kutulia. Kasa wa viwango hasa anayethamini shule, akaanza kuingiwa
na Jelini moyoni. Aliyekuwa naye usiku huo alikuwa ametulia haswa. Akabaki
akimtafakari na kujigeuza kitandani akitamani ingekuwa tofauti. Angalau Jelini
atokee daraja hata la chini yake kidogo tu, lakini kumlinganisha Jelini na
aliko yeye, ni kama yeye yupo gorofa ya 102, halafu Jelini yupo gorofa ya 12.
Mtengano mkubwa sana. Akakwama hapo akitafakari. Aendelee kuweka msisitizo, au
kweli aachane naye! Akapotelea usingizini akiwa hajapata jibu.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Kama
kawaida yake, ratiba yake si ngumu. Kula kulala. Alishashiba usiku, basi
akalala hapo mpaka saa tano asubuhi. Akatoka kumsaka mama yake. Akamkuta
akipika na kufua. Bibi alikwenda kwa mama mkubwa kwa siku chache kabla ya
shuguli kuanza. Wakabaki wao tu watatu kama kawaida yao. Zikaanza stori. Yeye
amekaa tu ila kumchekesha mama yake. Akampigia mtu wa pikipiki waliyezoea
kumtuma hapo kwao ili alete mtori na chapati akataka na soda ya mwanae Fanta
orange. Mama yake akimwangalia tu. Vikaletwa vingi tu.
“Jema
amekupa hela?” “Mimi si mjinga mama. Usianze kunichota.” Akanyanyuka wakicheka.
“Naona umejaa!” “Na nguo zako zote za shuguli nakulipia mimi. Na kaka
namnunulia mashati ya shuguli zote.” “Sasa Jelini mwanangu kama unayo pesa yote
hiyo mama yangu, si uanze kufanya kitu kitakachokusaidia kukuingiza kipato?”
“Umeanza mama.” Akaondoka kabisa hapo. “Ila nashukuru kwa msaada wa nguo.” Hakujibu,
akajua ameshakasirika. Akamsikia akimuita mtoto wake akale.
Baada ya
muda alipomaliza kula na kujitayarisha akaondoka. “Utarudi?” Mama yake
akamuuliza wakati akitoka. “Siendi baa.” Akamjibu hivyo. “Sawa mama yangu,
nitakuwa nakusubiri.” Akajua mama yake anachomaanisha, haamini kama kweli
atarudi, wala hakumjibu, akatoka. Alikuwa amependeza sana, kama kawaida yake
hajikosei.
Kweli akaenda kumnunulia mwanae nguo. Zaidi
chupi. Hicho hakuwa akisahau. Jelini alipenda sana chupi. Akamnunulia nyingi
kama kawaida yake hanaga kuwaza kesho ila matumizi. Akajinunulia na yeye vitu
vyake. Akalipia kwa fundi nguo zake na za mama yake, akarudi nyumbani na kuku mzima
wa kuchoma na ndizi. Mama yake akimwangalia tu.
Akaoga
tena. Akabadili nguo, akajitengeneza na
kuaga. “Ndio safari ya baa sasa?” Akaanza kucheka. “Mama Jema siku hizi umekua
mwingi wa maswali wewe! Utakufa pressure bure! Wewe tulia.” “Kwa hiyo ni baa?”
“Siku hizi mambo ya baa napunguza.” “Pombe tena basi?” Akazidi kumdodosa
taratibu. “Si pombe ni ya kurithi jamani? Ukoo mzima wanakunywa, kwa nini na mimi
nisinywe?” “Wewe unarithi kunywa pombe tu, na mengine?” “Kuzaa pia nimekurithi
mama yangu. Wala si kimoja.” Mama yake akaguna kwa masikitiko. “Na wala sitachelewa,
usianze lile swali lako la kama narudi.” “Bora.” “Na nitakuletea bia mbili za
kulalia. Au unasemaje?” “Na mimi Fanta ingine.” Akaongeza Jeremy, mwanae.
“Msijali.” Akatoka.
“Tuone
vitu alivyokununulia.” Akaenda kumletea bibi yake na kushanganzwa sana. “Huyu
pesa kapata wapi?!” “Mwenzio nimefurahi!” Jeremy akamwambia bibi yake akirudia
kuangalia vitu vyake. “Basi hela yote itapata matumizi asifanye cha….” Akaona anyamaze tu.
Taka Cha Mvunguni.
Kasa
alikuwa akimsubiri barabara kuu. Alipomuona tu, akamfungulia akapanda.
“Umependeza Jelini!” Akacheka akifunga mkanda. “Asante. Na asante kwa hela.”
“Ulishashukuru jana, bwana! Vipi siku yako?” “Nzuri tu. Na wewe kanisani?” Kasa
akacheka. “Ibada ilikuwa nzuri tu.” Akatulia asije akazungumza neno baya kwa kuropoka.
Hawakwenda
mbali sana, ila sehemu ya hadhi kama kawaida yake Kasa. Wakaagiza ice cream,
wakaanza kula taratibu tu, Jelini kimya kama aliyejionywa na kama anayesubiria
kitu. Maana alijua kwa upewaji ule wa pesa, kuna kitakachofuata. Na Kasa naye
alishamsikia akisema watu wanapenda kumdai kila wakimpa kitu, akaona anyamaze.
Wakala ice cream taratibu tu.
“Vipi
maandalizi ya send off?” Akavunja ukimya. “Yanakwenda vizuri sana. Jema
anauungwaji mkono mkubwa mpaka mama ameshangaa. Hakujua kama ana watu wengi.
Tulijua tungefanya kitchen party ndogo, lakini kumbe anamarafiki wengi
sana. Kila mtu anatuma mchango. Tuliishiwa vikoi, ikabidi mama aagize tena.”
“Hata James amepata uungwaji mkono mkubwa sana. Ukishiriki mambo ya watu, na
watu watajituma kwako.”
“Wewe
umeoa?” Alishituka sana, hakutegemea hilo swali. Akacheka na kumuonyesha mkono
kwamba hauna pete. “Kujibu swali lako, hapana sijaoa.” Jelini akacheka
taratibu. Wakatulia. Akaona ni muda wa kuweka ombi lake mapema kutimiza azma
yake, kufunga midomo rafiki zake. “Siku ya harusi utakuwa na nani?” “Mama na
kina mama mdogo. Dada Doro pia atakuwepo.” Akajibu bila ya kufikiria, na Kasa
akajua. “Mbona unacheka?” Jelini akamuuliza. “Nikimaanisha mtu wako.” Jelini
akafikiria kidogo na kupata jibu. “Oooh!” Akaanza kucheka kama kawaida yake.
“Unamaanisha
mchumba?” Akauliza akicheka hana mbavu. “Au boyfriend.” Akaongeza Kasa kama
kupunguza uzito na hilo likamfanya azidi kucheka. “Jelini!” Kasa mwenyewe
akajikuta akicheka. “Mwenzio sitaki tena mambo hayo. Unakua unagandwa na mtu!
Huna raha wala uhuru na maisha yako, na mimi nataka kuwa huru sio simu zakuanza
kuulizwa upo wapi na unafanya nini!” “Hutaki?” “Akuuu! Yaani unajikuta gafla
eti mtu mmekutana naye tu, anaanza kutawala ratiba yako yote! Eti uwe wapi na
ufanye nini! Hapa hapafai! Pale panakufaa! Sasa unajiuliza huyu mtu vipi!
Umekutana naye tu, basi tayari eti anajua nini unataka! Au eti nini unatakiwa
kufanya! Halafu anaanza kukukataza bila kujali furaha yako!?”
“Wewe furaha yako nini?” Ikabidi Kasa aulize
akiwa amechoka kabisa. “Kuwa na washikaji baa, kucheka. Kila mtu
anahaiba yake. Ukikaa na wengi, unapata mengi. Siku inanoga. Sasa unakua na mtu
mmoja, pengine yeye mwenyewe kisirani. Mnajikuta wote mmekwama kwenye hasira
zake! Halafu maisha yako yanakuwa hayana raha! Akuu! Mimi hivyo sitaki.” Kasa
akacheka taratibu akitafakari alichozungumza.
Mwishoe
akasema akiwa mawazoni. “Mimi nafikiri mahusiano ni kuzungumza na makubaliano.”
“Huo mwanzo mzuri sana. Ila baada ya hapo, unajikuta ni yeye tu ndio anataka
mambo yake yafuatwe. Hakusikilizi tena. Kwa hiyo kwa kifupi mimi sina mchumba
wala boyfriend. Na sitaki hiyo adha. Kwa hiyo siku ya harusi nitakuwa na yeyote
atakayekuwepo karibu, na anayetaka kufurahia. Sio tena matatizo.” Kama kawaida
yake akajibu kirahisi, asitake kuchosha akili zake kuanza kufikiria jinsi ya
kujibu akiwa amewaza nini Kasa anamaanisha! Hapana. Alichokisikia ndicho
alichokijibu kirahisi tu. Kasa akatulia kabisa akiendelea kukubaliana na
utofauti wao kimaisha. Hata moyoni akaona kweli hatamuweza msichana kama Jelini
asiye na mipaka! Akaanza kujirudi na kukubaliana naye yeye mwenyewe na hata
Doro alipomwambia hatamuweza Jelini.
Wakamaliza,
akamuaga. “Narudi nyumbani.” “Leo baa huendi?” “Acha nikwambie ukweli Kasa.
Najua Doro ni rafiki yako, ila mimi ni kampani yangu kubwa. Ndio sababu ya kuwa
nakuwa baa kwa uhuru nikijua na yeye yupo. Sasa kwa sasa hatupo vizuri sana.
Kuna ukweli aliniambia. Sijui kwa nini umeniuma sana nashindwa kurudia
tulivyokuwa zamani. Sasa sijui kwa kuwa ni yeye aliyeniambia hivyo au jinsi
alivyoniambia kwa kunitusi! Sijui! Ila nahisi ni vile nilivyomtegemea kwangu na
kule tulikotoka.” “Mmetoka wapi na Doro?” Kasa akauliza.
“Mbali
sana. Kama utakuwa umemfahamu muda mrefu, utajua alikopita. Mimi ni mdogo sana
kwake, lakini nilisimama naye kwa karibu sana bila kinyongo wala kulalamika.
Sasa kuja kuniambia maneno makali, tena bila kosa! Imenivuruga kidogo hata hamu
ya baa imepungua. Nimeona nitulie tu nyumbani kwa muda.” Kasa akatumia akili
kumuuliza kijanja kujua sababu. “Mmegombana muda mrefu?” “Wala si kugombana,
maana mimi siwezi kutukanana. Alinipigia simu nikiwa nimelala nyumbani kwake,
yeye akiwa kazini, ndipo akaanza kuniporomoshea mvua ya matusi. Ila aliomba
msamaha akisema alikuwa na siku mbaya kazini. Nimemsamehe, lakini yale maneno
yananisumbua kweli! Ila kujibu swali lako, leo baa sitakwenda. Narudi tu
nyumbani.” Wakaondoka hapo kurudi garini.
Walipopanda
tu garini, Kasa uzalendo ukamshinda tena. Sitaki nataka. Ukweli Jelini anavutia
haswa. Anatamanisha kwa namna zote, kasoro tu hizo tabia zake. Na
mwenyewe hazifichi na wala haoni tatizo na alivyo. “Unafikiri tutakuja kuonana
lini tena?” Jelini akakunja uso akiwa anafikiria huku akijiweka sawa kitini.
“Eti Jelini?” “Hata sijui Kasa! Ila siku za harusi zimekaribia, vikao vitakuwa
vikifanywa karibu kila siku. Halafu mama anataka Jema arudi nyumbani apumzike
siku chache kabla ya harusi. Jema mkali sana kwangu sio kama mama. Hataki niwe
natoka hovyo. Kwa hiyo sijui.” “Basi niombe vitu viwili.” Jelini akamwangalia.
“Usikatae
kabla ya kufikiria.” Jelini akacheka. “Siku ya harusi uwe kampani yangu, tukae
wote. Na jumatano tutoke kwa chakula cha usiku.” Jelini akatulia. Ukweli
hakumpenda Kasa kimapenzi hata kidogo. Kuja kuwa naye harusini na haiba yake ya
ustaarabu, akaona atamnyima raha hata ya kunywa. Akapoa kabisa, akiwaza jinsi
ya kumkatalia.
“Jumatano
tunaweza kutoka. Ila harusi si nitakuwa upande wa bibi harusi wewe bwana
harusi?” “Hatutapanga viti kwa namna hiyo. Tumekusudia kupanga viti kwenye meza
za duara, watu 10.” “Kwa hiyo wewe hutakaa na wenzako?” “Unaweza kukaa na
sisi.” Hapo pakawa pagumu zaidi. Jelini anapenda uhuru wake kama ndege. Leo
kumuweka katikati ya wastaarabu, wanaohesabu na kufikiria maneno ya kuzungumza,
wengine kama Kasa wanaosema bia inayompa yeye kiu eti ina ladha mbaya mdomoni, nikumziba
pumzi.
“Mbona
unakua mzito hivyo Jelini!?” “Nikwambie ukweli lakini usikasirike?” “Niambie
tu.” “Hapana.” Kasa aliumia sana. Pesa yote aliyompa, hadhi yake, leo
anamkatalia! Ikamuuma sana mpaka akabadilika. “Labda niulize ni kwa nini?”
“Mimi na kina mamdogo tumepanga mipango yetu siku ya harusi. Wale wana fujo
kunizidi mimi. Hutaweza kumudu hiyo fujo na kelele zetu. Hutaweza kukaa kwenye
meza yetu na mimi najihisi nitajipunja sana kukaa na nyinyi. Hadhi yako ni
kubwa sana Kasa. Usiku wote nitakuwa nikijiwinda maneno. Acha siku hiyo
nifurahie na ndugu zangu.” Jelini aliyedhani ni malaya kwa kumtizama na
chakaramu tu, anamsimamo wake tena mgumu haswa.
“Tafadhali
usichukie. Mimi najijua mwenyewe.” “Nimeelewa, na nashukuru kuwa muwazi zaidi.
Kwa hiyo unafikiri hata hutanisalimia kabisa?” “Siwezi kutofanya hivyo. Nishakufahamu
kwa karibu hivi! Lazima kukutafuta kujua umekaa wapi. Kama utaniruhusu lakini.”
Hapo Kasa akaridhika sana. “Si ni sawa? “Kabisa tena ruksa.” Wakacheka, lakini
hilo likamfurahisha sana Kasa. Shida yake ni kurudisha heshima mbele ya rafiki
zake akionekana mtoto kama Jelini anamfahamu kwa karibu. Ila hata yeye
alishamuona si mtu ambaye wanaendana hata kidogo.
Kasa
alilelewa kwenye mazingira ya hadhi ya juu sana. Kwenye pesa ile yakutowaza
baada ya miaka mitano maisha yatakuaje. Baba yao alikuwa na pesa sana. Alikuwa
na vitega uchumi vya uhakika akitumia akili na nguvu kuhakikisha pesa haikauki
kwake. Kasa alikuwa akiingiza pesa kutoka kwa baba yake kila mwezi, kubwa
kuliko mshahara wake. Yaani kwa kumtizama tu kasa, ungejua ni samaki wa
kukaangwa. Amejaa mafuta. Ni mstaarabu wa asili sio wakujifunza ukubwani baada
ya kufanikiwa. Alizaliwa ustarabuni. Haitachukua hata dakika moja akimpeleka
Jelini katikati ya jamii ya kwao na kuonekana ni wa tofauti. Akamshusha
kituoni, akaondoka.
Chachandu Kuwekwa Pilipili.
Hilo juma
likawa kimya kati yao, Kasa naye akaona amuache tu maana Jelini hakukosea hata
kumtumia ujumbe wa kumjulia hali. Busy na yeye kwa maandalizi ya shuguli ya
dada yake. Jioni aliyoingia Jema hapo kwao ikawa furaha, mwali ameingia. Mama
zake wote na bibi walikuwepo hapo. Wao wanakunywa na kucheka bila kikomo. “Mimi
mwenzenu vyakukesha sitaviweza. Pombe sinywi, halafu tokea alfajiri nilikuwa
busy kazini kuweka mambo sawa ili kumsaidia bosi wangu kabla sijaondoka.” Jema
akataka kuingia chumbani alipoona shangwe haziishi. “Jema naye! Anajua kukata
watu stimu! Sasa kulala sasahivi wewe Jeremy?” Mama yao mdogo ambaye anamfuata
mama yao akalalamika. Ila huwa anapata nao sana hao watoto wa dada yake. Mlevi
ndio maana na Jelini anampenda. Tofauti yao ni yeye anaijua pesa mpaka
shilingi. Ana maduka ya nguo za jumla, Kariakoo na vipodozi duka ameweka Sinza.
Amejijenga haswa, kwa hiyo wakati mwingine walikuwa wakitafutana na Jelini kwenda
kunywa. Hakubahatika mtoto wala ndoa.
“Kaa basi
nikupe ya mjini.” “We Koma wee! Mbona umemkazania mwanangu!? Ulitaka kukesha
naye hapa ili umfanyaje?” Mama yake akaingilia. Na Jema alijua atamtetea tu.
Wote wakaanza kucheka. “Keshakwambia pombe hanywi, na amechoka. Unataka kesho
atokee mbele za watu kama kazee!?” “Nataka kumpa ya mjini na wewe dada!”
“Jelini huyo hapo mtaka ya mjini. Mwache Jema.” “Mimi yote nayajua mama yangu.
Twende Jema nikakuulize maswali ya msingi.” “Sasa na wewe Jelini usianze.” “Sasa
kwa taarifa yako mama, hata yeye atanishukuru huyo Jema. Msianze kunipinga. Hii
ndio zawadi yangu kwake.” Jema akacheka na kutaka kujua.
“Ndio
twende sasa kabla sijampigia simu mpenzi wangu, maana nikianza kuzungumza naye
sikati mpaka nilale.” “Sasa wewe nenda kamuage. Usizungumze sana maana nilikuwa
nakusubiri nikufundishe jambo zuri sana. Muage tu wakati mimi namalizia bia
yangu kutoa aibu.” Wakaanza kushangilia zaidi mama mdogo alishajua. “Mimi
mwenyewe nakuja.” “Sasa utamtia aibu Jema jamani! Mimi namjua dada yangu huyu.
Haya kwake mazito.” “Kwani mnaenda wapi?” Akauliza mama yake mkubwa.
“Kuna shule
hiyo, mamdogo aliniita, wakati shoga yake anaolewa. Yule mwali alikuwa dizaini
kama hivi za Jema. Akafungiwa ndani siku 20, huyo mama akawa anaenda. Ndio shoga
yangu huyu akaniita na mimi niende.” “Kukata mauno?!” Mama yao akashangaa sana.
“Sasa
dada wewe acha ubishi. Hapo hata mimi Jelini nampongeza maana nilisahau kabisa.
Bwana tulipewa shule ya nguvu!” “Sasa wewe badala umuite huyu kwenye mambo ya
maana, unakwenda kumuita kwenye kukata viuno! Mama unamsikia mziwanda wako?”
mama Jema akawa amekasirika. “Kila mtu kuna alichoandikiwa dada, bora mkono
uende kinywani. Kama yeye kachagua ya kitandani, si bora awe mjuzi kuliko
anazunguka kwenye vitanda vya watu akitia aibu!” Mamdogo alishalewa, na
walimjua kwa kupenda vitanda vya wanaume. Jelini anacheka mbavu hana.
“Wewe
unafikiri duka la Sinza lile nililifungua kwa pesa yangu?” “Waambie mamdogo.”
“Haki sidanganyi. Mimi sikutia uvivu. Nilijifunza kwa yule bibi, nikatoka hapo
nikamkamata mwenye nazo. Bwana yule mzee alikuwa akitoa hela bila kuombwa!”
Wakaanza kucheka. “Haki siongezi. Niliyokuwa nikimfanyia yule baba, akawa kama
mjinga! Jamani ipo siri kubwa sana ya kitandani. Mapenzi yapo sikatai.
Ni kama chachandu tu, lakini ikiwekwa pilipili, vyaongeza ladha.” “Tena
yule bibi alikuwa anasema chakula ni chakula. Lakini kisicho na chumvi na
chenye chumvi tofauti.” Wakazidi kushangilia wawili hao wakipokezana maneno.
Pombe ishaingia kichwani.
Ila hapo wakamgusa
Jema. Akakumbuka James anavyotizamia fungate, halafu hana ajualo! Akajirudi.
“Mimi nataka kujifunza, mama!” Jema kasema, wote wakaanza kushangilia pombe ikisaidia
kupiga kelele. “Wewe unataka ujifunze mambo ya kitandani kwa malaya hawa!
Utamuogopesha James.” “Sasa kwa taarifa yako Jema, ukitaka ndoa inoge, ukifika
chumbani kuwa malaya.” Jema alishituka sana. “Haaa! Mamdogo jamani!” “Basi ujue
malaya wa mjini watakusaidia. Hakuna ulokole kitandani Jema. Shauri zako,
utanikumbuka! Wakimshika mzungu wako yule, wakamuonjesha ya uswazi, huna
utakalofanya akarudi. Utanikumbuka, labda asije onjeshwa.” “Basi mamdogo na
wewe njoo.” Jema akafanya wazidi kucheka vile alivyoonekana ameingiwa hofu
anataka msaada kwa kila mtu. “Hutaki tena kumpigia simu mpenzi akubembeleze
ulale?” Jelini akamkejeli akicheka. “Nishaona nitatia aibu. Bora mje mnisaidie
kujiandaa.”
Wawili
hao wenye vichwa vinavyofanana waliohundhuria unyago wa bibi, wakamfuata Jema
nyuma tena kishabiki. “Pumu imepata mkohozi. Na Mode anavyopenda ushangingi
huyu!” “Watamtia ujinga hapoo!” Mama Jema akaongeza kwa dada yake wakiendelea
kunywa.
Mwali Hafundwi Hadharani.
“Kwanza
tupe staili zako ulizojiandaa nazo.” Akaanza Jelini. Hilo swali likawa gumu kwa
Jema. “Kwani kunatakiwa ziwe ngapi?” “Wewe tuonyeshe ulizo nazo.” Akaongeza
Mode, mama yao mdogo. Jema akaanza kubabaika. “Acha masihara Jema wewe! Kwamba
huna moja!? Kwani huwa mnafanyaje?” Wakazidi kumnyima raha. “Mimi na James
hatufanyi mapenzi.” Jema akajibu kwa aibu kidogo akionekana mnyonge mbele yao.
Bwana walicheka mpaka wakaaa chini.
“Nimeona
nije, kabla hamjamtia hofu akaona hataiweza ndoa.” Akaingia mama Jema na bia
yake mkononi wao wakiendelea kucheka ila kwa mshangao. “Hivi ujue mama Jema
bado ni bikra!” Mpaka mama yake akashangaa. “Sema kweli?!” Mpaka mama yake
ikawa ngumu kuamini. “Mama naye!” Jema akajichekesha. “Sasa na huyo James unamtulizaje?”
“Jamani si kila mwanaume ni mdhaifu kwenye hilo jambo. James anataka tusubiri
mpaka ndoa.” Walishangaa kama wameona chatu hapo chumbani.
“Kama
hamnifundishi, ondokeni, mwache kunishangaa.” “Mimi nitakufundisha dada yangu
wala usijali.” “Na mimi nitakuandalia begi zuri sana la fungate. Nguo za
uchokozi. Chupi za ukweli sio machupi yakizee. Utamkera mumeo.” Akaongeza Mode. “Wewe una kaumbo kazuri Jema,
lazima ujifunze kujiacha wazi mbele ya mumeo uvutie.” “Acha kunidanganya
Jelini. Wewe ndio una umbo zuri.” “Mimi najijua mzuri navutia.” “Pumu imepata
mkohozi.” “Kweli mama. Kwani uongo mamdogo?” “Aaah sana tu.” Kama kawaida yake
kumpa sifa Jelini shoga yake. “Lakini na wewe Jema mzuri. Tena unavutia kwa
namna yako dada yangu ndio maana James anakupenda wewe.” Jelini akamtia moyo
dada yake mpaka mama yake akafurahi.
“Kila
mwanamke ana uzuri wake. Wala usijifiche mbele ya mumeo, maana hutakaa ukawa
mimi na wala mimi sitakaa nikawa wewe. Tumia ulivyonavyo vizuri, tena kwa
ujasiri. Mimi kibonge, najua jinsi yakuweka mwili wangu mbele ya mwanaume, kwa
kunitizama tu, kabla hajanishika, mnara upo hewani. Lakini nikiwa mtupu na hizo
nguo za ndani alizokwambia mamdogo Mode.” Jema akawa anaona aibu. Mamkubwa naye
akaingia. “Mama ameenda kulala nikasema na mimi nije nipate shule.” “Sasa na
wewe usianze maneno mengi ukamfanya Jelini apotee pointi. Alikuwa akizungumza
naye vizuri tu hapa. Tafuta mahali, kaa.” Mama Jema akamwambia dada yake.
“Kwa hiyo
umesema ujasiri? Maana eti mimi sijioni kama navutia.” Jema akaongea kwa
wasiwasi. “Hakuna mwanamke asiyevutia mbele ya mwanaume dada yangu. Toa aibu,
jiamini. Mimi kila siku nasema biashara matangazo. Unavyojiuza kwa mwanaume,
ndivyo atakavyokuchukulia. Ukijiweka thamani, na yeye atakuthamini.” Wakaanza
kumshangilia Jelini, kidogo aibu ikaanza kutoka kwa Jema.
“Tuanze
na ukaaji kitandani. Mtoto wa kike hukai kitandani kama shuka au mto.”
Walicheka, ila Jelini akawa yupo serious. “Nakaaje sasa?” “Kwanza inategemea
unataka kufanya nini hapo kitandani. Kama unataka kuanza romansi. Kwamba umekaa
kichokozi ili usimame umtoe nguo au..” “Jelini wewe! Mimi ndio nimvue?!” Chumba
kizima walicheka mpaka mama yake. “Msinicheke bwana! Sasa si ataniona mimi nimek…”
“Tulikwambia nini wewe?” “Chumbani natakiwa kuwa malaya.” Akajibu Jema mwenyewe
na cheko.
“Ushawahi
ona malaya chumbani?” Jelini akamuuliza. “Hawana aibu ndio maana wanalala na
mabwana zenu wasomi, tena bila hofu. Halafu pesa yote ambayo ilitakiwa ije
kwako na watoto, inaishia mtaani. Sasa kwa nini utake mtu akamfanyie mumeo kitu
unachoweza kufanya mwenyewe.” “Haya basi nifundisheni.” Ikaanza shule ya
kwanza. Yeye Jema aweje kabla ya tendo. Jelini akamfundisha kwa vitendo kabisa.
“Na unayaweza!” Mama yake akamwambia. Akacheka na kuendelea.
“Na
unapotoka kitandani unamfuata kuanza romansi, sio tena unatembea kama unakwenda
migombani kwa bibi na jembe! Taratibu ili akuone vizuri ukiwa na lingerie yako
mwilini, zile nguo zako za uchokozi. Na sio ukifika midomoni tena umetulia tu
unanyonywa midomo, unakazi ya kuachia mate tu mpaka yadondoke! Hapana. Mdomo
msafi, ladha jitafutie mwenyewe hata pipi au spray za mdomo kwa harufu
utakayochagua. Zuia mate yasijae mdomoni, hiyo tena kero na kuleta kinyaa. Na
wakati wa denda, lainika Jema. Sio umekakamaa kama upo kwenye gwaride bwana!”
Jema akaanza kujifikiria alipokuwa akipewa denda alikuwa akifanyaje! Akahisi
alikuwa akikakamaa.
“Na
mwanamke ni multi tasks. Tuna uwezo wa kufanya mengi kwa wakati mmoja na
hatukosei. Ndio uwezo wa kipekee tumepewa sisi wanawake na Mungu. Sasa hiyo
zawadi unatumia hata kwenye mapenzi. Unapata denda huku mikono yako ya kike ikibarizi
mwilini mwake.” Jema aibu. “Mamdogo simama.” Mode akasimama, Jelini akamwambia
Jema aangalie. “Mpaka kushika huko!” Jema akashituka sana. “Hee kumbe! Tena sio
ushike kama andazi unataka kutozea kwenye chai! Koni inachezewa kabla ya
kulambwa.” Jelini alicheka mpaka akakaa chini. “Ndio je! Wewe Jema vipi bwana!
Tena kama amevaa suruali ili kumchanganya unafungua zipu tu, unachomoa mzigo
wote mpaka kengele zake halafu unamchezea huku ukila denda, unanyonya mpaka
masikio uone kama hajaivua suruali haraka akilia bila msiba!” Wakacheka mbavu
hawana.
“Wewe
unaenda haraka bwana mamdogo Mode! Huyo hajui hata jinsi ya kushika koni.”
Wakacheka na kugonga. “Malaya nyinyi!” Mama Jema akamwambia Jelini na Mode na
kuzidi kucheka. “Mpe mpaka shule za kengele za mumewe.” Wakacheka na kugonga.
“Zile kengele zina mistari.” “Mnamchanganya bwana! Hamjamaliza koni yenyewe.”
Jelini alicheka sana. “Kumbe mamkubwa unataka na wewe!” “Acha nijifunze bwana.
Hakuna kufudhu maishani. Kila siku ni kujifunza tu.” Basi hapo Jelini
akajiachia akamfundisha romansi tu. Akamuelekeza mengi hatua kwa hatua.
“Ulale
mwali, kesho romansi ya kumchanganya kama hutaki mambo mengi kitandani. Umechoka.
Unataka kumpa vya chapuchapu, ulale. Sasa unavyoandaa viungo, jinsi ya kukaanga
kabla hujatupia mhogo ndani mpaka kuivisha kwa tui. Taratiiibu bila yeye kujua kwa
wakati huo wewe hutaki, unahitimisha tu.” Wakacheka wenyewe kama waliokumbuka
jambo! “Halafu sasa staili za kutiana. Sio kutwa kitandani mpaka mchakaze
godoro!” “Au kuharibu chaga!” Mamdogo akaongeza na kugonga kwa Jelini. “Mwanamke
jua kutumia mazingira. Akijileta jikoni, unaye. Bafuni, unampa. Ukimkuta kwenye
kochi baada ya taarifa ya habari, unamkojoza taratibu.” “Akiingia ndani kutoka
kwenye shuguli zake unampokea zipu ya suruali sio mkoba tu.” Walicheka wawili
hao, kama mazuri.
“Mamdogo,
akiingia tu?” “Kumbe. Mkono mmoja mkoba, mwingine zipu ya surulia midomo
inamnyonya kama pipi tamu. Ukipiga goti mbele ya suruali, ukimaliza hapo,
anaacha pesa yote anarudi kwa mkewe mtupuuu.” “Jambazi huyu!” Mama Jema
akafanya wacheke. “Na lugha ya kufanya mapenzi, Jema. Nilitaka kusahau.” “Na
mihemo na sauti zake. Sio kujikaza mwenzio anahangaika, umetulia tuli kama
unachomwa sindano!” “Au gogo!” “Au kugugumia kama unatolewa mwiba!” Walicheka
mpaka basi. “Jemaaa!” Mama yake mkubwa alicheka sana vile alivyomuona Jema
ameshangaa. “Hivyo mtaninyima raha. Sitaweza vya milio au kuongea.” “Sasa
ukianza lugha za kwenye bibilia kitandani, utamkata stimu mumeo. Ongea jambo
mpaka limsisimue.”
“Au
unatoa mhemo ukilia kama unakunwa na ukakunika. Sauti nzuri, laini mpaka
ajipongeze anafanya jambo zuri. Sio tena kimya kama mpo kwenye kikao cha bunge,
unamsikiliza spika!” Wakazidi kucheka. “Kesho tunaendelea Jema dada yangu. Tutakufundisha
hema ya romansi. Na ya wakati umemwaga mchele, ukitaka atie mboga. Na wakati
akikwea mlima.” “Na akiwa chumvini.” Walicheka hao, kama mazuri, Jema
akajifunika uso. “Mnazidisha bwana!” “Haa! Wewe mama hujasikia wale wanawake
wananyonywa, wametulia kimya mpaka mwanaume anagairi!” Jelini akauliza bila
aibu. “Basi mimi napata stori zao baa kwa wale wanaume malaya. Mamdogo yupo
sahihi. Wanasema kuna wanawake wapo kama wanakamuliwa jipu! Onyesha kwamba ni tamu. Tena mwambie tamu, nataka tena.
Uone kama hujawa unapiga mabao kulia na kushoto.” “Haaa!” Jema akashangaa kwa
mshituko, akakimbilia kitandani na kujifunika na mto. Alifanya wacheke sana.
“Ila nimefurahi sana kunifikiria Jelini. Hakika ningetia aibu.” “Karibu, shule
nyingine kesho kabla ya kichen party na baada.” Wakatoka kumpisha apumzike.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
0 Comments:
Post a Comment