~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Huku kwa
James naye akawa akisubiria Jema atoke kazini wakutane kwa chakula cha usiku na
kumalizia mazungumzo yao juu ya agano jipya waliloweka kwa simu. Kumu
alipotoka tu, Jema akampigia simu James kuashiria siku ya kazi ndiyo imeisha. Nanaa
akampigia lakini hakupokea simu yake ila akamtumia ujumbe kumwambia
atamrudishia simu baadaye. Nanaa akashangaa sana. “Nini?” Geb akamuuliza mkewe.
“Sielewi! Unajua jana kaka alisema hataweza kufika kwa chakula cha mchana, ila
angepita jioni. Hakuja wala hakusema chochote. Sasa hivi nampigia, hajapokea
ila amenitumia ujumbe kuwa atanirudishia simu baadaye!” Geb kimya. Nanaa
akamuangalia mumewe akahisi kuna jambo anafichwa.
“Wewe
unajua kinachoendelea?” Geb hakutaka kuwa msemaji wa James, akaamua kujiweka
pembeni. “Pengine ana kazi zake. Amesema atakurudishia simu, subiri mama.” “Si
kawaida yake! Mimi huwa simu zangu kwa kaka hazisubiri!” Geb akakumbuka hilo.
Akajua kazi itakuwepo. Kwa mara ya kwanza James ataanza kugonganisha magari.
Geb akanyamaza.
James
anamtumia ujumbe dada yake yupo kwenye simu na Jema. Hakuwa hata akimaanisha
anachomwandikia Nanaa. Akazungumza na Jema mpaka akafika hapo ofisini kwake.
James akamsogelea garini akamfungulia mlango. “Kwa hiyo mimi ni mchumba wa
James?” Jema akamfanya James acheke sana. “Niambie bwana ili nizidi kufurahi!
Ona maua yangu haya.” “Nakupenda Jema. Na kama utakuwa tayari na mimi, hakuna
kuchelewa tena.” “Ukimaanisha nini?” “Acha gari yako hapa, tutairudia.
Unisindikize mahali kwanza huku tunazungumza kwenye gari ndipo tukale.” Jema
akashuka na pochi tu. Akahamia kwenye gari ya James.
“Usinichoke
lakini.” “Kwa nini tena?” “Nina biashara ya kuosha magari pia. Sasa kuna kifaa
kiliharibika, ndio nilimtuma fundi akarekebishe. Na kuna kitu niliboresha. Ndio
nataka nikaangalie. Huwa huko siendi mara kwa mara kwa kuwa ni biashara ambayo
si rahisi kuibiwa.” “Kivipi?” “Mimi na Geb tuliweka mfumo ambao kila gari
inayoingia pale kuoshwa, inajirikodi na
mimi naweza kuangalia nikiwa popote. Kwa hiyo si ya kuifuata sana nyuma.
Inajiendesha au naweza kuindesha kwa simu.” “James umejijenga wewe mpaka
unatisha!” “Niliamua Jema. Wakati wengine wanatumia kipindi tunaanza tu kazi,
mimi nilikusudia kuwekeza. Na sio kote nilikoanza kulifanikiwa! Vingine
vilishindikana ndio nimebakiwa na hizo biashara mbili tu. Ya vifaa na hiyo
yakuosha magari.” “Hongera sana.” “Asante.” James akajibu na tabasamu.
Akamuona
amepotelea mawazoni. “Usiniache sasa hapa garini peke yangu! Rudi huko
ulikokimbilia.” Jema akacheka taratibu na kurudisha macho kwake. “Ninaposema
hakuna kusubiri tena, namaanisha naomba tusisubiri tena Jema.” Jema akatulia tu
akimsikiliza. “Sisi wote si watoto. Nataka tuanzishe familia kwa haraka tu. Au
wewe unasababu ya kusubiri?” Jema akatulia kidogo akitafakari.
“Eti
Jema?” “Unauhakika James?” “Juu ya nini?” “Naona tusiharakishe! Tupeane muda.”
“Hizo ni hatua za wasio juana Jema. Au niseme ni hatua za wajaribishao. Mimi
sijaribishi. Nitakubeba hivyohivyo na wewe naomba ujifunze kuishi na mimi
tukiwa wote. Halafu acha nikwambie ukweli ambao pengine unaweza ukakushangaza.”
Jema akamwangalia.
“Sijui ni
kwa nini, tokea nimeanza kukufuatilia, kwa mara ya kwanza hisia za kimapenzi
zimeanza kunisumbua.” Jema akainama. “Tokea nakua ni hisia nilizokuwa hata
siziruhusu lakini safari hii imenishinda Jema. Nakutaka wewe, na nataka
na mimi kuwa na mpenzi wangu. Mke kabisa. Sijui kama naleta maana?”
“Nimekuelewa.” Jema akajibu akiwa ameinama na tabasamu.
“Najiona
ndio hicho tu kinapungua kwangu. Sasa sitaki kuendelea kujipunja. Labda
uniambie wewe haupo tayari na mimi.” “Nakupenda James.” “Basi naomba tusisubiri
zaidi, tafadhali.” “Ndio tunafanyaje?” “Tuanze taratibu za kuoana kwa haraka.”
“James!” Jema akashangaa sana. “Hakika sikutanii Jema. Na kwa kuwa nimejiambia hata
kama nitazidiwa vipi, kwa jinsi tulivyojitunza mpaka ukubwani, sitakugusa mpaka
siku ya fungate yetu. Tuanze kwa baraka za Mungu. Ila si kwamba hata sasa hivi
sitamani! Natamani sana. Sasa kwa nini tujitese, au wewe haupo tayari?” Jema
aliona aibu sana. Maana James aliongea kwa wazi mno.
“Eti Jema?
Au unaona navuka mipaka?” Jema akajifunika uso akicheka. “Unisamehe pengine
nimekua muwazi sana, tena kwa haraka.” “Sio kosa, ila sikutegemea bwana!” James
akacheka sana. “Basi naacha. Ila ujue mimi nipo tayari na wewe.” “Nakupenda
James.” Hilo Jema akalirudia. “Na naamini hatutashindwana.” Hilo likamfurahisha
sana James. “Nikuulize swali gumu?” “Subiri papoe kwanza bwana!” James alicheka
mpaka machozi.
“Nishatibua
hali ya hewa?” “Sana!” Jema akajibu akicheka huku ameinama. “Mtu akikuangalia
kwa haraka, anaweza kusema wewe ni wale wasichana wa mjini walio kubuhu!”
“Kweli James!?” “Hakika. Nisingeusikia huo kweli kwenye mazungumzo yako, hakika
ningejua ulishakuwa kwenye mapenzi kwa muda mrefu tu.” “Na bado ungenioa?” “Ooh
yeah! Nisingejali. Mimi nilisubiri kwa sababu zangu binafsi, siwezi nikataka
kila mtu aishi kama mimi.” “Sasa haukuwa ukiteseka?” James alicheka sana.
“Naona
kumeshatulia, unataka tuendelee.” “Hapana James bwana! Sio ujibu kwa undani!”
“Ila nikisema asubuhi ndio zaidi. Ni sawa?” “Haaaa!” Jema alishituka, akajifunika
na pochi yake kwa haraka. James akazidi kucheka kama mazuri. “Sikumaanisha
hivyo bwana James!” James akazidi kumcheka. “Nakuandaa ujue una mume wa namna
gani. Si ndio tunafahamiana?” “Bwana taratibu!” “Wakati mimi nataka kuoa
haraka? Unataka tuingie kwenye ndoa hujui wajibu wa asubuhi?” Jema
alicheka sana akiwa amejificha. “Basi Jema. Siongei tena. Itoshe kwa leo.”
“Wewe umeshaanza malizia tu.” James akacheka sana.
“Nishatumbua
jipu?” “Kumbe! Sasa hilo swali gumu ni lipi tena?” James akamwangalia kisha
akaanza kucheka tena. “Basi usiulize tena bwana!” “Hutaki tena?” “Nakuhisi
vibaya.” “Mimi tena?” “Kabisa. Tubadili mazungumzo bwana!” “Hata hivyo
tunakaribia kufika. Tukitoka hapo, kuna mahali nakupeleka kula, kusherehekea,
‘NDIYO’ zetu.” “Halafu ndio utaniuliza?” “Na kukuomba juu.” James akamalizia
nakumfanya Jema akunje uso.
Wakafika
hapo, Jema akashangaa sana. “James hapa ni kwako?!” “Kwani ulishawahi kuja?”
“Zaidi ya mara moja! Nikawa najiambia huyu mtu aliyefanya hivi atakuwa ameona
mambo ya Ulaya.” “Kumu huyo. Ndiye aliyenipa hili wazo. Alisema aliona
alipokwenda Marekani kumtembelea jamaa yake. Akajiambia kama angekuwa ni mtu wa
biashara, angefanya. Basi aliponipa wazo na kuniunganisha na jamaa yake wa
huko, na yeye akawa mwema. Akaniunganisha na huyo mmiliki ambaye walipita
kuosha gari yake akiwa na Kumu. Akanielekeza na kuniambia alipogiza vifaa
vyake, ndipo na mimi nikafungua.” “Aisee nimekukubali James!” “Mbona hilo
nalijua.” Jema akacheka sana.
“Bwana si
kwa hivyo!” “Mimi kukubaliwa kwa namna yeyote ile, sichagui. Tena na wewe!” “Eeehee?”
“Nikubali vyovyote tu.” Jema akazidi kucheka wakiwa wameegesha gari sehemu ya
ofisi zilipo. “Kama umechoka unaweza kunisubiria kwenye gari. Sitachukua muda
mrefu.” “Naomba nikashangae zaidi ndani.” “Karibu.” Wakashuka garini.
Huku Kwa Joshua.
![]() |
“Naya!” “Umependa? Nimekuta kwenye moja ya mizigo yangu iliyoonyesha ni sanduku tulilokwenda nalo honeymoon.” “Nimeikumbuka, na niliipenda sana mwilini mwako. Naya wewe ni mzuri na una umbo zuri sana mpenzi wangu.” Baada ya hizo sifa Naya akapata ujasiri, akamsogelea karibu akiwa nusu uchi na hiyo lingerie iliyomuacha uchi kabisa ila kufunika matiti yake tu na kufunika mbele ya uuke.
![]() |
“Nimekuletea
zawadi Naya.” “Acha isubiri.” Naya akaongea akitaka kurudi midomoni. “Naomba
nipokee basi!” Joshua akaongea kwa msisitizo akimkwepa kidogo. Naya akashituka sana
akajua amekosea. “Samahani, sikujua kama upo nayo mkononi.” Akamuachia kila
mahali. Joshua akajuta. “Usingeachia huku chini!” “Nilifikiri unataka
nikupokee! Au nimeshindwa kuelewa tena?” Ile hali ikawatoa kwenye dimbwi zito
la mapenzi aliyoanzisha Naya, ikawa ni kama amemkatili. Joshua akamuona ameingiwa
hofu ya ajabu. Ikabidi ajirudi kwa haraka “Nilikuletea maua.” Akamkabidhi. Akamuona
mpaka mikono imeanza kutetemeka kwa hofu. “Nashukuru. Asante.” Naya akashukuru
macho kwenye maua lakini si kwa furaha kama alivyotarajia Joshua.
Joshua akajua hakumbuki na ameshaharibu. “Asante.” Akashukuru tena bila ya kumtizama na kugeuka kuelekea upande wa pili wa hicho chumba, sehemu kilichopo
![]() |
“Samahani
Naya.” “Hamna neno. Naona alishapika. Chakula kipo tayari. Nakwenda chini kwenye
kile chumba chenye vifaa vyangu, nitarudi baadaye kidogo.” Akatoka bila ya
kusubiri jibu. Joshua akanywea kabisa. Mwili ukawa kama umemwagiwa maji baridi.
Akahisi amefanya haraka kulazimishia hayo maua. Akajichukia na hata kuchukia
hayo maua.
Ukweli
Naya hakuwa akikumbuka kabisa. Akarudi kwenye hicho chumba na kujifungia.
Akaanza kutafuta sehemu alizokuwa ameandika zamani kusoma kama aliandika habari
za maua. Joshua akabaki akifikiria, akaona amfuate. Akashuka kwa haraka,
akakuta mlango umefungwa kwa ndani na funguo. Akagonga. “Kuna kitu nafanya. Ni
sawa nikiendelea? Nitakuja kulala baadaye. Naomba utangulie tu.” “Chakula?”
“Nilikula mida ya jioni. Bado nimeshiba. Nikisikia njaa kabla yakulala,
nitakula ndipo nije kulala. Na kwa kuwa nilishaoga, sitakusumbua.” “Hunisumbui
Naya!” “Basi nitakuja kulala.” Joshua ndio akajua haruhusiwi kuingia humo
ndani, na yeye ndio hatoki tena.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Alifanya
kila kitu bado Naya hakuwa amerudi hapo chumbani. Akaoga mpaka akamaliza. Akaamua
kujisomea kidogo akiwa kitandani wakati akimsubiri, mpaka akaanza kusinzia bado
hapakuwa na dalili yake kurudi hapo. Akaamua amfuate. Naya bado alikuwa
akitumia dawa. Akagonga taratibu, kimya. Akaita tena na tena, kimya. Akahisi
atakuwa amekunya dawa na kupitiwa na usingizi kwani hizo dawa ndio kitu cha
mwisho kunywa kwa kuwa zinamfanya alale sana. Akaenda kuchukua funguo ingine, ili
kufungua. Ikaanza kazi ya kuangusha funguo ya ndani kwanza. Akahangaika mpaka
akafanikiwa. Akafungua na kumkuta amelala sakafuni na diary mkononi, maua
pembeni.
Akaivuta
taratibu na kuifungua. Ilikuwa ya zamani. Akaanza kusoma aliyokuwa ameandika
humo. Akakutana na sifa zake kibao. Akifananishwa na wanaume wote waliopita kwenye
maisha yake na kuwaona kwenye mahusiano. Joshua akakuta yeye ameandikwa kwa
kupambwa kwelikweli. Kuwa amezidi hata zaidi ya maombi yake na mifano ya wengi
waliopo kwenye mahusiano. Chini akaandika shukurani zake kwa baba Naya,
kumuombea bila kukata tamaa mpaka kumpata huyo Joshua. “Nimemkatili Naya
wangu! Joshua aliyemsoma humu na kutaka kumridhisha leo japo hamkumbuki imekua
tofauti kabisa!” Akajilaumu akimwangalia vile alivyolala pale chini sakafuni
na kuzidi kuumia. Akagundua aliyoyasoma ndiyo yaliyompelekea mpaka kukumbuka
sanduku la fungate na kwenda kusaka vitu vya kumfurahisha.
Akakuta
pembeni daftari kabisa. Akalivuta. Akashituka sana aliposoma ndani. “WOSIA WA
BABA NAYA.” Moyo wa Joshua ukashituka. Akakuta ndani anaandika kila siku na
tarehe za hayo mambo anayoandika. Aliposoma, kwa hakika alisikia sauti ya baba
Naya kabisa. Na Naya naye akawa akiandika vile anavyojiwa na hayo maneno. Hapo
Joshua akapoa kabisa akabaki akimwangalia. “Ni nini hiki! Na kwa nini
hajaniambia kama amemkumbuka baba Naya?” Akawaza, asijue hata yeye ndio
siku hiyo amegundua ni maneno aliyokuwa akihusiwa na baba yake. Kwa muda mrefu
siku hiyo ndio kwa mara ya kwanza ameweza kujua ni nani alimwambia hayo maneno
yanayojirudia akiwa usingizini. Akafurahi sana na ndipo siku hiyo
akaandika hicho kichwa cha habari kuwa ni wosia wa baba Naya.
Akabaki akiwaza
na kusoma mpaka akamaliza. Akarudishia kila kitu kama kilivyo akambeba. Wakati
anatembea naye kumtoa hapo chumbani akashituka. “Samahani nilipitiwa na
usingizi.” Akateremka. “Usiwe unaomba msamaha Naya! Unanifanya nijisikie
vibaya.” Akatoa tabasamu la usingizi. “Naenda kulala. Najisikia kuchoka.”
“Umeshameza dawa?” “Ndiyo.” Akajibu. Wakarudi chumbani. Akaelekea chumba cha
kubadili nguo, Joshua akamfuata akakuta akitoa ile lingerie, kisha
akavaa nguo ya kulalia, Joshua asiamini kama ndio amekosa utamu wa usiku
huo.
“Kama ni
sawa, naomba nitangulie kulala, kichwa kimekua kizito!” “Hata mimi nalala,
nilikuwa nikikusubiria tu wewe.” “Pole. Nilipitiwa na usingizi.” Akatangulia
kitandani. Joshua akamuwahi. “Nisamehe mke wangu, nimekukatili.” “Hapana.
Mimi ndio najisikia vibaya. Sikumbuki kabisa. Najitahidi hata kusoma vitu vya
nyuma ili kukumbuka, lakini sikumbuki. Nakuhurumia naona unaishi na mtu ambaye
siye Joshua.” Akaanza kulia taratibu. “Hapana Naya.” “Nikweli.
Najua na wewe unamatarajio yako kwangu, mimi sijui! Kuna vitu vingine nafanya
nikijua ni sawa, kumbe nakosea.” “Mimi ndio nimekosa Naya. I
pushed you too hard! Sikutakiwa kufanya hivyo. Hapakuwa na ulazima wa maua
kwa wakati ule. Ila nilijua pengine ungekumbuka, na kukuongezea hamasa, kumbe
nimeharibu! Tafadhali unisamehe.” “Ni sawa Joshua. Usiku
mwema.” Hapohapo akageuka na kupitiwa na usingizi.
Ilimuuma
sana Joshua. “Hizi sio kumbukumbu nataka azitunze. Kabla hajakumbuka vizuri,
anakutana na mume wa namna hii!” Akajilaumu sana, nakushindwa kulala kwa
haraka, akajisalimisha kwa Mungu. Akatoka kitandani kabisa na kupiga magoti. “Nimekosa Baba yangu. Naomba unisamehe na unisaidie.
Naomba amani iliyokuwepo kati yangu na mke wangu. Nisaidie hekima yakuishi naye
kipindi hiki anachohitaji muongozo sahihi, asisikie kuumizwa hisia zake.”
Akaomba hapo Joshua, ndipo akalala.
Kwa James&Jema.
Wakati
huku wengine wamemaliza siku wanalala, huku kwao walichukua muda mrefu hapo
zaidi walivyotarajia. James akajikuta anatakiwa atengeneze hiki na kile zaidi
kwenye kompyuta hata akili kwa dada yake haikuwepo tena ila kumuhurumia Jema
aliyemuweka hapo akimsubiria usiku huo. Mpaka James anamaliza hapo kurekebisha
system nzima tayari ni saa nne na nusu usiku, Jema naye usingizi. “Samahani sana
aisee! Kumbe ni bora ungechukua tu gari yako!” “Tungekosa muda wa pamoja
barabarani.” “Kwa hiyo huoni kama umepoteza?” “Hata kidogo. Hivyo vyakula vipo
tu. Tutakula wakati mwingine. Acha mimi nikapumzike, jumanne ni siku za vikao
kuanzia saa moja asubuhi ratiba ya Kumu ndio naianzisha mpaka jioni ndio tunatulia.”
“Basi acha tuondoke.” Wakatoka hapo, kimya.
Jema
akajivuta nyuma ya kiti, akatulia James akaendelea kuendesha. Jema akakumbuka
na kumgeukia. “Ulitaka kuniuliza nini?” James mwenyewe akaanza kucheka. “Kama
ndio hivyo usiulize James.” “Mbona sikuelewi sasa?” “Mimi nahisi hilo swali sio
zuri bwana! Kwa nini likuchekeshe wewe mwenyewe?” James akazidi kucheka. “Basi
acha nikuulize wakati mwingine, usije shindwa kulala bure!” Jema akabaki kama
anaye tafakari.
“Nini?”
“Nahisi sitaweza kulala. Wewe niulize tu. Ni juu ya nini?” “Kukiss.” Jema
alishituka mpaka akapaliwa mate. “Kunywa maji.” James aliongea akiendelea
kucheka. Jema akakohoa mara kadhaa mpaka akatulia. “Ila bado sijauliza swali.”
“Nyie James jamani!” Jema akashangaa sana. “Pagumu pameshapita sasahivi ni
muendelezo tu kutaka kujua.” “Nini sasa?” “Nashukuru kwa utayari wako. Kwamba
tunaweza kuanza sasahivi, na kwa umbali gani?” “James!” “Ni kwa nia nzuri tu,
ili tukubaliane. Kwamba kwa sasa tuanze kwa busu la kama baba kwa binti yake,
au kaka kwa dada, au wapenzi?” “Mimi naona kwa leo kweli tuache.” James
alicheka mpaka machozi.
“Hutaki
tena?” “Sitaki.” “Sasa utalala kweli?” “Acha nikajue mbele ya safari.”
James akaendelea kucheka sana. “Sasa hapo unacheka nini, James?” “Aisee
nimemfahamu Jema ambaye nina uhakika watu wengi sana hawamfahamu! Kumbe unaabu
hivyo! Mtu akikuona..” “Naomba tusikilize radio, James. Tafadhali sana.” Bila
kubisha James akawasha CD ya nyimbo za dini huku akicheka. “Mimi sijui kuimba.”
James akajisalimisha. “Bora uimbe hata kama ni vibaya, ili usiwaze mambo magumu!”
Hapo James alicheka sana mpaka wakafika.
Akamfungulia
mlango. “Sasa hapa sijui natoa busu gani!” Akawa kama anayejiuliza. “Acha bwana
James!” Jema akalalamika. “Hutaki hata la baba kwa binti yake!” “Wewe sio baba
yangu.” Jema akajibu. James akatulia kidogo akamwangalia. Akaelewa ndio
amekaribishwa busu la mpenzi. Jema akajibaraguza kama anayefunga tena
pochi yake. James akamsogelea kupata mdomo. Jema asijue James alishajiandaa na
hilo busu tokea hajamfuata kazini. Alishajua nini afanye ili kufanya midomo
yake itoe ladha nzuri, kwani alimsikia Joshua na Geb wakiambizana ni nini wao
wanatumia kabla ya kupeana midomo na wake zao. Wote wakagundua wanatumia vitu
vinavyofanana kasoro tu flavour tofauti. Hapo ndipo James akajua kumbe kuna
matayarisho kabla ya kupata ndimi za mwanamke! Kwa kuwa hakuwa akijua ni wapi atapata,
akanunua pipi kifua na kuzitunza kwani na hizo alisikia wakiambiana wasipokuwa
na mouth freshener karibu, wanatumia hizo.
Usiku huo
akirekebisha mitambo ya kwenye biashara yake, Jema akisubiria, kwa kuwa hakuwa
amepiga mswaki jioni hiyo, akatafuna kwanza gum/BigG. Kutoa chochote
kilichokwama kwenye meno. Wakati wanatoka akaenda chooni na kusafisha kinywa
kwa kusukutua, kisha akajipaka mafuta ya midomo ili tu kulainisha midomo yake,
isiwe imekakamaa/mikavu. Kisha akaweka pipi kifua yenye ladha ya mint, ili
kufanya kinywa kiwe fresh ndipo akatoka hapo ofisini.
Hapo
anamsogezea mdomo Jema, anajiamini na atakachokutana nacho. Jema akampokea
taratibu na kushangazwa na utamu wa hiyo midomo. James akamuhisi anamsogelea
zaidi, akajua amependa. James akamsogeza karibu yake zaidi na kuendeleza kupata
midomo yake. Ikawa kwa mara ya kwanza James kupata denda. Na akalitendea
haki bila papara. Akawa na kiasi kabla hajapitiliza. Jema akacheka. “Midomo
yako mitamu!” akasifia. “Umenogewa?” Lile swali likamfanya Jema aanze kuondoka
na kumfanya James azidi kucheka. “Usikimbie.” “Nawahi kulala. Wewe mchokozi
James.” Jema akazidi kuongeza mwendo
mpaka kwenye mlango wa gari yake.
“Acha
nikufungulie mama. Usikimbie.” Akapunguza mwendo, James akampita, akamfungulia
ila akashangaa ameegemea gari. Jema akataka kumpita akamvutia kwake akawa
amemshika kiunoni akamvutia kwake, akaanza tena kumnyonya midomo yake. Jema
akajituliza akipewa denda mpaka akamuhisi mzee amesimama. Akamcheka James
nafsini mwake maana alizidi kumng’ang’ania. Baada ya muda akajinusuru nafsi
yake na kumuachia. “Nimefurahia Jema. Asante.” “Na mimi nimefurahi. Asante
James. Halafu unajua kukiss!” Akaona ampe sifa yake tu. James akacheka
akimtizama. Akainama.
“Naomba
unisamehe nimekufanya usile.” “Ila umenikumbatia, nimefurahi. Wewe ni mzuri na
umetulia James.” James alicheka mbele yake mpaka akainama. “Jema!” “Kweli. Mimi
nafurahia kuwa na wewe. Hata sijali kutokula.” “Kesho tutaanza kula ndipo mambo
mengine yaanze.” Wakaagana, Jema akapanda garini, akamfungia mlango, akaondoka.
Hapo James alikuwa amejawa furaha hata hakumkumbuka dada yake tena. Na yeye
akarudi kwenye gari yake safari ya kurudi kwake akapumzike ikaanza. Akawa akiendesha
huku akiendelea kulamba midomo. Akamkumbuka Jema alipokuwa mikononi mwake,
akampigia. Wakawa wanasindikizana.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
v
Nini Kitaendelea kwenye mahusiano hayo mapya ambayo Nanaa ni
kama kwa mara ya kwanza anasahauliwa na kaka yake!?
v
Mapenzi aliyokuwa akililia Jema, amepata?
v
Amani
kati yake na mkewe aliyotangaza Kumu hata kwa Bale, itaendelea kuwepo au Kumu aliongea kwenye sikio
la shetani?
§
Usipitwe.
0 Comments:
Post a Comment