Joshua
akatoka ndani ya gari kwa haraka akamkimbilia Malon kumrushia ngumi. Malon
mtoto wa mtaani alishaiona ile ngumi mapema sana, akakwepa. Naye Joshua kama
aliyejua angekwepa, akampiga ya kushitukiza kwa haraka za mbavuni mfululizo
kisha usoni. Wakazidi kupigana, Naya amesimama pembeni. Geb akatoka, alipomuona
Naya, Joshua na Malon, akakimbilia kule walipokuwepo na askari walipoona vile
bosi wao anakimbia, mmoja wao akatoka na kumfuata.
Badala
Geb agombanishie, akaanza na yeye kuchangia. Malon hakuzidiwa. Akaendelea
kupigana nao wote wawili. Mama G, Grace, Nanaa wanatoka, wanakuta hiyo fujo.
Naya analia pembeni, wanaume hao watatu wanapigana karibu kutoana roho. Joshua
na Geb wakamvamia kwa pamoja ndipo wakaweza kumuangusha chini. Wakaanza kumpiga
mateke kwa pamoja mfululizo.
“Geb
Magesa!” Sauti ya mama G ikasikika kwa juu na ukali ndipo Geb akawa kama
amezinduka. Akasimama. “Unafanya nini!?” Mama G akamuuliza. “Huyu ni Malon,
mama. Anatufuata mpaka nyumbani kwangu! Hapana mama. Hiyo ni dharau.” Joshua
alikuwa akiendelea kupiga mateke pale chini kama aliyepagawa. “Na wewe Joshua, inatosha.
Acha hivyo sasa.” “Nimemkuta anataka kumchukua tena Naya! Huyu ni mshenzi mama.
Ameona tumemnyamazia, ndio anaona sisi ni wajinga.” “Inatosha Joshua.
Acha hivyo. Mwache huyu askari amfunge pingu apelekwe polisi, vyombo vya sheria
viamue. Toka hapo Joshua kabla hajakuharibia maisha yako, ukafia
jela kwa kumuua.” Askari akamuweka pingu na kumnyanyua pale kwa nguvu.
“Unanifunga
kwa kosa gani wakati mimi nimesimama hapa kwenye eneo la nje, la uma! Sijaingia
kwenye eneo la mtu yeyote yule? Huo si ujinga tu!” Malon akaongea akitema mate
yenye damu huku akicheka. Na alikuwa sahihi. Pale ni nje ya uzio, sio ndani ya
mpaka wa Geb. Geb akamsogelea na kumpiga ngumi ya tumbo kwa nguvu mpaka
akainama. “Geb Magesa!” Mama yake alishituka nusu aruke. “Huyu ni mshenzi
mama.” “Sasa nimekwambia acha. Unanisikia Geb?” Geb akanyanyua mikono
juu kama aliyesalimu amri kwa mama yake na kurudi nyuma. Nanaa alikuwa
ameshangaa, amepigwa na butwaa, mdomo wazi karibu mate kumdondoka. Hakuwahi
kumuona Geb akimpiga mtu vile.
Akamsogelea
Malon karibu. “Sura yako ikionekana tena kwenye hili eneo ambalo anaishi mama
yangu, mke wangu na watoto wangu, nakupiga risasi. Na sikutishi. Usinijaribu.”
Akamgeukia yule askari. “Piga simu ofisini kwenu, ita gari ije imchukue huyu
jambazi.” Malon akacheka sana akiwadharau. Geb akawa kama amekumbuka kitu.
“Hivi ni nani aliyemfungulia mlango Naya na kumruhusu atoke nje bila idhini
yangu na mimi niliwaambia Naya asitoke ndani na wala asiruhusiwe kuingia mtu
ndani bila kuulizwa?” Geb akauliza na wote wakamgeukia yule mlinzi vizuri.
Joshua
akamsogelea Naya karibu. Bado alikuwa akilia kwa hofu. “Naya, niangalie mimi ni
Joshua, na upo salama. Hakuna wa kukuchukua tena wala kukuumiza.” Naya alikuwa
amepatwa hofu ya ajabu, anatetemeka kama aliyekuwa amewekwa kwenye barafu! “Unakumbuka
nilikuahidi nitahakikisha hata wakikusogelea hawatakuchuku tena?” Naya
akakubali akilia. “Basi jua upo salama. Naomba utulie na usiogope.” Joshua
akamvuta karibu zaidi, akamkumbatia vizuri. Akaendelea kumbembeleza akimsugua
taratibu.
“Ni
Chalo. Anasema alikuwa akifanya kazi na huyu jamaa zamani, kwenye kampuni
hiihii. Akasema wanafahamiana sana na ni mtu wa Mungu sana. Alishajua kama
anaye mwanamke wake anaitwa Naya tokea wakifanya naye kazi. Kwa hiyo alipoomba
aitiwe mkewe, akisema yeye hataki kuingia ila atoke tu wazungumze hapa nje,
ndipo nikamruhusu Chalo akamuite.” Wakamuona Geb anatoa simu. “Nakutaka ufike
hapa na walinzi wengine watakaonilindia kwa leo wakati nikitafuta kampuni
nyingine ya ulinzi.” Kabla hajajibu, Geb akakata.
“Hatukujua..”
“Mnachotakiwa kujua ni maagizo ninayotoa mimi na si vinginevyo. Nenda kaweke
silaha chini, subiri gari ije, ili haya unayoeleza hapa, ukaeleze polisi, ndio
wao waamue kama sio kushiriki njama ya kumtorosha mke wa mtu.” Hapohapo Geb
akatengeneza kesi. “Samahani sana ila..” “Hapo ndio unaharibu kabisa. Wewe
ondoka kabisa hapa. Nenda kasubiri pale kibandani. Hicho unachotaka kukifanya
nikumpandisha hasira zaidi. Wewe nenda, uje kuzungumza na kiongozi wenu, yeye
ndio atazungumza na wewe.” Grace akamkatisha na kumwambia hivyo yule mlinzi.
“Nataka kuomba tu msamaha.” “Sasa mimi ndio nakwambia muache sasa hivi, huna
utakachozungumza ukatengeneza ila kuharibu zaidi. Kama huamini, basi wewe
endelea kutofuata maelekezo yake.” Grace akamtahadharisha. Akaondoka na Malon akiwa
amefungwa pingu.
Mama G
akamgeukia Joshua. “Samahani sana Joshua. Ni kitendo cha muda mfupi mpaka
nahisi ni kama waliokuwa wakimvizia abakie peke yake maana wote tulikuwa nje
tukifanya kazi kwenye meza za wageni. Sasa tukamuacha akigawa pipi kwenye hizo
meza. Tukasema tumuache kama kumpa nafasi afanye kwa uhuru tena akigawa kwa
kuhesabu.” “Nashukuru mama, lakini bado Naya hajafika kwenye uwezo wa kuwa peke
yake. Naomba tumpe muda zaidi.” Joshua akawa kama analaumu.
“Maana
ningechelewa kidogo tu, angefanikiwa kumuingiza kwenye gari yake na kuondoka
naye tena! Bado Naya hana nguvu ya kushindana na mtu. Alikuwa akimvuta kikatili
sana huku akilia!” “Samahani baba. Naomba tusamemehe.” “Na mimi nisamehe Joshua
kwa kuwa nilikuahidi nitakuwa naye kila mahali. Samahani.” Nanaa naye
akaongeza. Joshua alikuwa na hasira. Akatamani aondoke lakini Magesa ndio
alikuwa akimtegemea yeye ampigie kinanda ili aimbe.
Bila
kuchelewa wakiwa bado kwenye ile taharuki, walifika walinzi wengine wawili na
kiongozi wao wakiwa na gari. Wakawapakia wale walinzi wawili pamoja na Malon
kuelekea kituo cha polisi. Geb, Joshua na Naya wakafuata na gari ya Geb. Nao
wakafika kituoni, wakaandikisha maelezo, wale askari nao pia wakawekwa ndani,
Joshua alishaita dereva wake akitaka aletewe gari ingine na gari yake
aliyotumia kugonga gari ya Malon ichukuliwe. Mpaka wanarudi nyumbani kwa Geb,
hata gari ya Malon haikuwepo nje ya uzio wa kina Magesa, Geb alisema hataki
aikute tena pale.
Akaomba
chumba ambacho anaweza kumtuliza Naya. Akampa dawa ya maumivu na kubaki naye
kitandani, Naya akiwa amemng’ang’ania shati pande za mbavuni, Joshua amejilaza
chali ameegemea mto. Alipohisi anaachia mikono, akajua ameshalala. Ndipo
akatoka hapo kitandani na kwenda kujisafisha, Geb akampa tisheti yake, akavaa.
Muda wa
shuguli ukawa umeshafika. Wakaamua kuanza keki kwanza. Joshua akakaa sehemu
maalumu iliyotayarishwa kwa kupiga kinanda ambacho kilikuwa cha Magesa
mwenyewe, ila kimetolewa nje kwa ajili ya hiyo shuguli ya siku hiyo akitaka
amuimbie dada yake. Tangia aone kinanda nyumbani kwa Joshua na kupenda, basi
wazazi wake wakamnunulia na yeye Magesa hicho kinanda na akawa ameshatafutiwa
mwalimu wa kuja hapo na kumfundisha kukitumia. Kwa hiyo hata hapo Joshua
alikuwa akitumia kinanda chake.
Akaanza
kumpigia ili Magesa aanze kuimba. Naya akatoka akimtafuta Joshua. Akamuona.
Akawa anajisogeza alipokuwa akipiga kinanda huku akimwangalia yeye tu. Watu
wote wakimsindikiza kwa macho, akawapita wote akaenda kukaa chini kabisa
majanini pembeni ya kiti alichokuwa amekalia Joshua ambaye na yeye alikuwa
akiendelea kupiga bila kuacha huku na yeye akimsindikiza kwa macho mpaka pale
alipokaa. Akajiegemeza kwenye kiti alichokalia Joshua na kuinamia magoti yake.
Joshua akamchungulia pale alipokaa kama kumwambia anamuona na ni sawa. Akatulia
kabisa.
Magesa
akaimba vizuri sana, wageni wengine nao wakamsaidia kuimba alipowaruhusu yeye,
wakamuimbia Liv ndipo wakaja kumuimbia na yeye Magesa sasa wakiongozwa na
Joshua akiwapigia kinanda na kuimba. Aliimba vizuri sana lakini walijua Joshua
hayupo sawa. Akaimba mpaka akamaliza ndipo akamgeukia Naya pale chini alipokuwa
amekaa ameegemea kitu chake. “Twende.” Akamsaidia kusimama. “Unaenda kazini
tena?” Wakamsikia akimuuliza Joshua kwa sauti ya chini lakini iliyoweza
kusikika na wasiwasi kidogo kama asiyetaka kuachwa tena. “Hapana. Twende
ukapumzike.” Wakatoka hapo kuelekea ndani.
“Bado
naogopa Joshua! Ujue kama ungechelewa, angenichukua!” “Unakumbuka tulimuomba
Mungu pamoja?” Akakubali kwa kutingisha kichwa. Wakakaa kwenye kochi ndani
wakati watu wote wapo nje. “Basi Mungu amekulinda na mimi nitaongeza umakini
Naya. Sitakuacha tena sehemu ambayo hakuna uangalizi mzuri. Nitahakikisha
wakati wote unakuwa sehemu salama.” Naya akapandisha miguu juu, akaikunja akiwa
kama amelala lakini akamlalia tena upande wa kushoto wa ubavuni kwake,
akapitisha nikono mbavuni kwake, akajilaza akiwa ameficha uso akiangalia kochi
nyumba ya Joshua wala si mbele.
Mama G
akawa ni kama aliyekuwa akiwapa muda wakae hapo ndani na watulie, muda mfupi
sana akaingia. “Vipi Naya?” Joshua akamchungulia kule alikokuwa amejificha.
“Naya?” Mama G akamuita kwa upendo lakini Naya akabaki kimya. “Au amekwisha
lala tayari?” Joshua alikuwa akimsikia jinsi vidole vyake vikipita huko mwilini
mwake kwa nyuma karibu ya mgongo, akajua hajalala. “Naona ameingiwa tu na hofu
na amechoka. Naomba mniruhusu akapumzike.” “Hamtakula!? Naomba msubiri tule
pamoja, Joshua mwanangu. Najua tumekuangusha kwa kuwa ulituamini na kama
tumeshindwa, lakini utusamehe baba. Usamehe kabisa. Naomba hili la watoto
liishe, ndipo muondoke. Itawauma sana watoto kuona mnaondoka hata hawajawalisha
keki!” “Basi tutasubiri.” Naya hata hakunyanyua uso kumtizama anayezungumza,
akabakia vilevile alivyokuwa amejilaza. Ila wakasubiri mpaka mwisho na Joshua
naye akatoa zawadi yake akimuakilisha na mkewe pia, ndipo wakaondoka.
Ndoa Na Iheshimiwe Na Watu Wote.
![]() |
maliwatoni na hivyohivyo ukiwa maliwatoni, unaweza kuona mtu aliyepo chumbani. Japo upande wa choo, kuliwekwa faraga. Kulizungushiwa kioo kizito na kikawekwa giza lililovutia hata kuingia humo chooni. Ila mtu wa ndani ya choo anaweza muona mtu aliyepo hapo maliwatoni ila ukiwa nje huoni ndani.
Alipokaa
tu, Joshua akakaa pembeni yake. “Kuna kitu najua unaweza usikikumbuke Naya.
Lakini kuna ahadi nilikupa mpenzi wangu. Tena kabla ya ndoa. Naomba niirudie
tena.” Naya akawa ametulia tu amejiinamia. “Unataka kusikia tena au umechoka?”
“Naogopa. Naogopa sana. Unajua ungechelewa kidogo tu, angenichua? Tena
alinikataza hata kukimbia, alisema ataniumiza vibaya sana. Sasa sijui
alimaanisha nini! Ungechelewa je! Naogopa sana Joshua, naona kama sipo salama!”
Naya akaongea kwa wasiwasi akisikika anaelewa anachozungumza.
“Nakuelewa.
Na usifikiri niliwahi pale kwa bahati tu! Ni Mungu alisaidia Naya. Kama
alisaidia leo, naomba amini pamoja na mimi kuwa na siku ingine atasaidia kwa
sababu nimemuomba Mungu tena na tena anisaidie kwenye ile ahadi niliyokuwa
nimekupa hata kabla ya ndoa yetu.” Naya akamwangalia kama anayetaka kumsikia
zaidi. “Unataka kujua?” Akatingisha kichwa kukubali.
“Uliniahidi
nini?” Naya akauliza taratibu tu. “Nilikwambia hivi, ‘Nitakulinda,
na kukupigania mpaka kifo changu. Wewe ni wangu. Na hutarudi kwa Malon.’ Najua
unaweza usikumbuke. Lakini nilikuahidi tukiwa pamoja tena uliniomba wewe
mwenyewe kuwa nikuahidi kukung’ang’ania wewe tu.” “Kwa hiyo ulishaniahidi
hivyo?!” “Kabisa. Kwa kuwa mbinu zake za kutaka kukumiliki hazijaanza leo.
Alikuwa ndio mwanaume wako wa kwanza, mkaachana ndipo tukaanza mahusiano mimi
na wewe, kisha akataka kukurudia tena. Lakini Naya, ulikusudia kabisa kuwa na
mimi. Na kwa kadiri alivyokuwa akitusumbua kwenye mahusiano yetu, ukahofia
ningekuacha. Ndipo ukaomba nikuapie kama sitakuacha. Ndipo nikakupa hicho
kiapo. Na ninakusudia kukisimamia daima.”
“Niambie
tena Joshua. Niambie tena, ili hofu ipungue. Naogopa sana. Anaonekana si mtu
mzuri. Sitaki anichukue.” “Unaweza kunipa muda mfupi nijipake losheni na kuvaa
nguo za kulalia?” “Unataka nikusubirie hapo nje?” “Hapana. Wewe ni mke wangu
Naya. Sina chakujificha kwako.” Naya akatulia akiwa ameinama akifikiria. Joshua
akambusu shavuni na kusimama.
Akafanya
yote hapohapo chumbani Naya akiwa ametulia tu kitandani. “Joshua!” Akamuita
tena taratibu. “Niambie.” “Nilipenda tulivyolala wote jana. Nililala vizuri,
kwa kwa kuwa ulikuwa ukinibembeleza.” Joshua akacheka. “Wewe ni mtu mzuri
Joshua. Unanisubiri mpaka nilale!” “Nakupenda sana Naya. Sana.” “Kama
hujachoka, naomba na leo tulale wote. Naogopa!” “Hata usipoogopa, unatakiwa
kulala na mimi. Na hapana, sitakuchoka Naya. Nimeomba Mungu anisaidie.”
Naya akatulia. Joshua akamuona anaanza kukosa raha, akajua anajaribu kukumbuka.
“Niangalie
Naya. Niangalie mimi na uache kukunja uso na kufunga macho kwa nguvu.
Utasababisha kichwa kuanza kuuma tena na hutakuwa na jinsi ya kukituliza kwa
kuwa si muda wa dawa.” “Sikumbuki Joshua! Kwa nini mimi sikukumbuki?”
“Sikuhitaji ukumbuke chochote.” Joshua akaenda kukaa pembani yake. “Tulia kisha
niangalie.” Naya akafungua macho. “Unataka tulale hapa ambapo ndio chumbani
kwetu au unataka turudi kule?” “Wewe unapenda wapi?” Naya akauliza kwa upole na
kuendelea.
“Mimi
nataka kuwa na wewe tu Joshua. Na hata ukitoka, uwe unaniacha hapahapa. Naomba
kwa sasa niwe na wewe tu. Najua umezoeana na kina Magesa, lakini mimi siwakumbuki
kabisa! Tafadhali usinipeleke na kuniacha huko. Hata kama unahitaji kutoka,
naomba nikusubirie hapa.” “Samahani kama nililazimishia uende kwa kina Magesa,
mpenzi wangu. Nilifikiri ingekusaidi! Ila sitarudia tena, mpaka wewe mwenyewe
utakapokuwa tayari.” “Sio sasa hivi.” “Sawa. Basi nikiwa nakwenda kazini,
utakuwa ukibaki hapa. Ukitaka kitu utakuwa ukiniambia mimi mwenyewe.” Hapo
akaridhia.
Kitanda Cha Ndoa Tena.
“Basi
naomba turudi kulala wote kwenye kitanda chetu cha ndoa.” Naya
akakubali. Wakaweka mambo sawa ndipo wakapanda kitandani. “Utaniahidi tena?”
Joshua akacheka. “Naona kumbukumbu zako zipo sawa.” “Nakumbuka mpaka pale tulipokutana
tena Joshua. Vile ulivyokuwa ukinibembeleza unisaidie.” “Kumbe
unakumbuka!” “Nakumbuka Joshua. Lakini pale nilikuwa kwenye maumivu makali
sana, hata kufikiria sikuwa naweza. Ila nakushukuru kunilazimisha.” “Kwa
kuwa niliweka ahadi kwako na mbele za Mungu kuwa, nitakulinda, na kukupigania
mpaka kifo changu. Katika uzima. Maradhi. Shida na raha. Wewe ni wangu Naya. Na
ndipo ninapoomba utulie na uanze kupata amani kuwa, nitafanya kila niwezalo,
usirudi kwa Malon. Na Mungu anisaidie.” “Asante Joshua. Sasa hivyo
ulivyonishika usiniachie mpaka nilale kabisa.”
“Unajua
hivi ndivyo ulivyokuwa ukilala tokea tumeona? Na hapa ndio kitanda na sehemu
yetu ya kwanza kuanza mapenzi mimi na wewe.” Naya akajivuta zaidi kana kwamba
alikuwa mbali. “Eti Joshua? Mimi nilikuwa mtu mzuri kwako?” Naya akamuuliza.
“Na usinidanganye.” “Ulikuwa mzuri sana Naya. Sana. Tulikuwa na wakati
mzuri mno. Nakwambia tulikuwa tukifanya mapenzi mimi na wewe hatukinahiwi ila
tu kuchoka. Hujawahi kutosheka na mimi Naya. Na hukuwa ukinidanganya. Nikweli
ulikuwa ukinifurahia na ukinijali sana. Uliniahidi utabaki kuwa wangu daima.”
“Nikikwambia tena itakuwa sawa au kwa kuwa sikumbuki zamani, haitaleta
maana?” “Sitachoka kukusikia mpenzi wangu. Na sijali ni wakati
gani utakao kuwa ukiniambia.” Joshua akayaongea hayo kwa sauti nzuri, karibu
kabisa na uso wa Naya.
“Ila
kabla hujaniambia chochote, naomba nirudishe zile pete nilizokuwa nimeweka
kidoleni mwako. Unaona hii?” Joshua akamuonyesha mkono wake wa kushoto. Naya
akageuka vizuri. “Hii pete yako ni nzuri sana, Joshua! Kama vitu vyako vyote!”
Joshua akacheka. “Asante. Lakini hii ni pete yangu ya ndoa, na ni wewe
ulinivalisha. Na nilizokuvalisha mimi, mbili. Moja ya uchumba, ingine ya ndoa,
zote zipo hapa. Zilibakishwa kwenye gari siku ulipopotea. Itakuwa sawa
nikizirudisha kidoleni ndipo uniambie unachotaka kuniambia au unaona haupo
tayari?” “Nataka univalishe wewe Joshua. Nitafurahi na mimi kuwa na pete zako
kidoleni kwangu.” Joshua akacheka kwa furaha, moyoni akisema, “wewe
ni Mungu, na badala yako hakuna mwingine.” Akatoka kitandani kwa
haraka kwenda kufuata hizo pete.
Akarudi
kitandani, Naya akakaa kabisa akionyesha utayari. Akampa na mkono. Joshua
akamvalisha moja baada ya nyingine Naya akimuangalia mpaka akamaliza. Na yeye
akajiangalia kidole chake. “Wewe Joshua unapenda vitu vizuri tupu! Hata hizi
pete ulizonivalisha ni nzuri sana!” “Na ulizipenda sana. Nitakuja kukuonyesha
picha ulizokuwa ukijipiga kila wakati halafu unaniringishia kuwa kidole chako
kimependeza kuliko changu.” Naya akacheka sana akijiangalia yeye kisha akavuta
mkono wa Joshua, akaangalia tena kama kuhakikisha. “Lakini kweli bwana! Naona
sikukosea, zangu zimenipendeza zaidi.” “Sawa Naya.” Kwa mara ingine tena
wakarudisha kicheko cha kweli ndani ya hicho chumba. Wakacheka na kurudi
kujilaza kama mwanzo ila safari hii Naya akijiangalia mkono wake uliokuwa na
hizo pete, akigeuza kila pande. Taa ikiwamulika hapo kitandani.
“Joshua!”
Akamuita taratibu. Joshua akaitika kwa busu pembeni ya kichwa sehemu iliyokuwa
karibu na uso wake Joshua, wakati Naya macho bado yapo kwenye mkono wake
akifurahia bado pete zake kana kwamba ndio anakutana nazo kwa mara
ya kwanza. Naya akamgeukia vizuri, akamwangalia.
“Nataka
mimi nibakie kuwa wako wewe tu, mpaka kifo.” Joshua akambusu mara kadhaa juu ya
midomo ambayo ilikuwa karibu sana na uso wake. Alipoona ameridhia, akamnyanyua
uso vizuri akaanza kunyonya midomo yake, mikono ikipanda mapajani taratibu.
Akamuona
anafurahia akanyanyua mguu mmoja juu yake zaidi. Joshua akapitisha mkono mpaka ndani
ya chupi aliyokuwa amevaa, akaweza kumshika makalio yake vilivyo. Naya akaanza
kujisogeza zaidi. Mkono wa Joshua ndani ya chupi ya mkewe ukaanza kuzunguka mle
ndani mpaka katikati ya matako akitaka kufika mbele, Naya akijitahidi
kujinyanyua kama anayetaka aendelee. Akaona ile chupi inamnyima uhuru. Bila
kutoa midomo ya Naya kinywani mwake, Joshua aliyekuwa na uchu na mkewe, hakuwa
amemsahau, wala hakuhitaji juhudi nyingi zifanyike ili kupandisha hisia za
mapenzi kama kwa Naya aliporudi amemsahau, akaanza kuivua ile chupi huku
akimminya vizuri, Naya naye akazidi kumng’ang’ania mpaka akamsaidia kutoa chupi
yake mwenyewe, pale alipoona Joshua anamchelewesha kwani mikono iliyokuwa
ikitembea katikati ya mapaja yake kutokea nyuma mpaka mbele, Naya hakutaka ipotee
kwa muda mrefu huko. Akaona amsaidie ili Joshua arudie kufanya alichokuwa
akimtendea na kumuamsha hisia zote.
Bila
kupoteza muda, Joshua naye akaanza kutoa nguo yake ya juu ya kulalia huku Naya
sasa akitembeza kucha na vidole sehemu ya juu iliyokuwa tupu, zaidi kwenye
kifua cha Joshua kilichokuwa na nywele, huku akiendelea kumnyonyo na yeye
midomo yake kwa uchu. Joshua akashangaa japokuwa Naya alisahau kila kitu,
lakini utundu wake wa kucha, na umaridadi wa mikono yake kila anapogusa na
kuminya, akichua taratibu, ulibaki vilevile kama zamani. Ikabidi Joshua
aharakishe kutoa nguo kwani mkono mmoja wa Naya ulishakuwa ndani ya pensi hiyo
laini, yenye lastiki kiunoni, kitambaa cha silki, safi kwa kulalia.
Joshua
akaendelea kufurahia kila kunakopitishwa kucha na anaposhika mkewe akimchua
taratibu. Mpaka Joshua anamalizia kutoa hiyo pensi, nguo ya chini, Naya
alishafika mbali sana. Midomo yake ilikuwa ikitembea mwilini kwa Joshua na
kumuacha Joshua hoi.
Alipokuwa
akirudisha midomo kifuani, napo alikitendea haki kifua cha mumewe. Alikuwa
akipitisha ulimi kwenye kifua cha Joshua na kuvuta kwa midomo zile nywele za
kifuani, taratibu na kumsisimua Joshua zaidi. Na anaporudisha midomo hapo
kifuani, mikono alibakisha kwenye uume wa mumewe akimchezea kwa utulivu, akimchua
mumewe taratibu bila papara. Ikawa sasa yeye ndio anacheza na mwili wa mumewe
zaidi bila kuchoka tena bila papara. “Naya hajasahau utundu wake
kitandani!” Joshua akashangazwa mawazoni, akifurahia midomo ya
Naya mwilini mwake.
“Nakupenda
Joshua.” Hilo neno lilisikika kwa nguvu na msisimko wa ajabu sana masikioni kwa
Joshua. Akapata nguvu kama aliyejiongezea nguvu za kiume. Shauku na tamaa kwa
mkewe ikaongezeka. Hamu na mwili wa mkewe ikaongezeka akataka amuingilie
tu afurahie joto lake. “Nitakuwa makini, nisikuumize.” Akamwambia akibembeleza
akiwa anamgeuza mkewe, akimtoa mwilini mwake, amuone mtupu akiwa amelala chali
pale kitandani. Akaanza yeye sasa kunyonya na kugusa huo mwili wa Naya. Yaani
kabla hata Joshua hajamuingilia mkewe, Naya alishamaliza safari ya kwanza.
Alipomuona ananogewa, anataka kwenda mara ya pili, ndipo Joshua akamkumbatia
vizuri. Matiti ya Naya yakaenea kifuani kwa mumewe. Akadaka midomo yake, Joshua
kwa mara nyingine tena, usiku huo akafanya mapenzi na mkewe akiwa
amemkumbatia kwa furaha zote.
Wawili
hao wakaendeleza penzi la haja. Kama alivyosema Joshua, Naya akashindwa
kutosheka mpaka yeye mwenyewe akasalimu amri. “Nikumbatie tena, nilale.” Joshua
akajua amelemewa. Yeye mwenyewe akamsafisha hapohapo kitandani akiwa anasinzia,
aliporidhika msafi, akajirudisha na yeye hapo, akamuweka kifuani, kwa mara
nyingine tena, Naya akarudi kulala kifuani kwa mumewe akiwa mtupu kabisa, na
Joshua akimpapasa kwa uhuru wote akimshukuru Mungu wake kwa kuuweka na huo usiku
wa siku hiyo hapa duniani. Siku hiyo iliharibiwa na kutaka kuisha vibaya,
ila wakaimaliza vizuri sana.
Jumapili.
Siku ya
jumapili nayo hawakutaka mgeni. Kwanza hata kina Magesa walionelea wawaache kwa
vile Naya alivyoondoka kwao akikataa hata kuwatizama ila kujificha ubavuni kwa
Joshua wakati wote. Mikono ya Joshua ndiyo iliyomtoa usingizini akimpapasa
taratibu. Akafungua macho akiwa mwanzoni amedhani ni ndoto. Akamkuta Joshua
akimtizama. “Joshua!” Akaita taratibu. “Umeamka salama?” akatulia kwanza kabla
ya kujibu akakaa na kuangaza chumba kizima kisha akajiangalia kwa wasiwasi
mpaka akamtia hofu Joshua akiogopa asije dhani amembaka.
Akajikuta
yupo uchi. Akavuta shuka taratibu na kujifunika Joshua akimwangalia kwa hofu,
hakutaka kuongea chochote ili amsikie yeye kumbukumbu zake zinamwambia nini, na
anafikirije juu ya mapenzi waliyofanya usiku uliopita. Kisha akamgeukia baada
ya kujivuta mwisho kabisa ya kitanda. Joshua kimya akimsihi Mungu amrehemu Naya
asimbadilikie. “Nilifikiri nimeota!” “Juu ya nini?” Akatulia kidogo kama hilo
swali limemtia wasiwasi. Akaegemea magoti kama anayejaribu kukumbuka na kupingana
na anachokumbuka.
“Naya?” Joshua
akamuita taratibu kumtuliza. “Abee.” “Naomba niambie unachofikiria. Na usigope.”
“Sijui ni ndoto?” “Juu ya nini?” “Kwamba usiku tulipata wakati mzuri?” akaongea
kwa kutojiamini. “Inawezekana ni mawazo tu.” “Ni kweli Naya. Na naomba
usijitilie mashaka. Wewe si mjinga hata kidogo ila uliumia sehemu ya kumbukumbu
za nyuma. Chochote unachokumbuka usikitilie mashaka. Nishirikishe ukijua mimi
ni wewe na nipo pamoja na wewe katika kila hatua. Kwa hiyo usiniogope kabisa. Na
ni kweli tulipata wakati mzuri sana. Ulinitoa simanzi yote. Na ukalipa ile
ahadi yako uliniahidi siku ile kabla hujapotea.” Akacheka. “Kweli ulinifurahia?”
“Sana Naya.” “Mimi mwenyewe nilifurahia sana. Unajua kunishika vizuri na napenda
unafanya mapenzi na mimi. Taratibu ukijali mwili wangu bila kutaka kuniumiza. Halafu
huna kinyaa!” Joshua akacheka sana.
“Kweli! Mimi
umenishangaza Joshua. Hata katikati ya mapenzi bado unatumia midomo yako kunilainisha!
Au sio kweli?” “Nimekwambia huna tatizo la kumbukumbu. Ni zile za zamani tu.” “Joshua
wewe unanipenda! Japokuwa nilikuwa nikikushangaa lakini vile ilikuwa
ikinisisimua sana na kunifanya nitake kuendelea kila wakati.” “Mpaka ukalemewa
na kulala kabisaa, ukaniachia kila kitu.” Naya akacheka na kujifunika. “Nilijua
ungechoka tu. Nilikosa kiasi. Nilikuwa na hamu na wewe Naya!” “Nimerudi Joshua.
Hakikisha hawanichukui tena.” “Nitajitahidi na Mungu nisaidie.” Ikawa ahadi
iliyochanganyikana na maombi.
“Asante
Joshua. Basi acha mimi nikaoge. Nililala mchafu.” “Nilikusafisha.” Naya
akacheka na kujifunika shuka. “Kila mahali?” akauliza akicheka ndani ya shuka. Joshua
akajivuta mpaka katikati ya miguu yake ndani ya shuka. Naya akazidi kucheka alipomuona
humo ndani. Akaiachanisha miguu yake mpaka amafika juu mapajani. Alipofikisha ulimi,
ikabidi Naya ajiegemeze kwenye mto vizuri akiwa amekaa, mkono wa Joshua
ukafikia matiti yake. Basi siku hiyo nayo ya jumapili, ikawa ni penzi
mfululizo. Naya akimfuata Joshua kila mahali akitaka kuchoka mzinga kama nyuki.
Naye Joshua akijua amebakia mwenyewe kwenye maisha ya Naya, hakutaka kufanya
kosa, alitumia nafasi yake vizuri akimpumbaza kwa hili na lile ili huko kichwani
kwa Naya abakie yeye tu.
J.3
Kurekebisha makosa.
Wakiwa
ofisini, Nanaa akijaribu kutafuta jinsi ya kujirudi kwa Joshua ili kuwa karibu tena
na Naya, maana Joshua aliomba siku ya jumapili wao wasiende nyumbani kwao kwa
chakula cha mchana baada ya ibada, ili abakie na Naya aliyeonekana bado yupo
kwenye mshituko. Wakajua wanawakwepa tu kwa kosa la kumuacha Naya karibu
kuchukuliwa tena na Malon.
Sekretari
wa Geb akamwambia anaye mgeni. Alipojua kama ni Bale na akamwambia amefika pale
ili kupunguza deni la baba yake, Geb akamwambia sekretari amwambie asubirie
chumba cha mkutano. Akamuita Joshua ili awe shahidi wao na yule mwanasheria.
Akaamuru Bale apewe anachotaka wakati akisubiria hao watu wawili wafike. Baada
ya lisaa watu wote wakawasili. Ndipo wakajongea chumba cha mkutano.
“Sitaki
fujo na mtu, ila kutaka kulipa pesa mnayomdai marehemu baba yangu.”
Akatoa hizo pesa. Kila mtu akashangaa. Bale alikuwa akilipia karibu nusu ya
deni la baba yake. Pesa nyingi maana ni deni la kuanzia ujenzi wa gala la
kisasa baba yake alijenga kwa hiyo pesa aliyowekeza Geb. Na Garama za barabara
ya vitofali iliyowekwa upya kuzunguka nyumba nzima mpaka galani kurahisisha
kuingizwa kwa bidhaa. Garama ya kubadili mfumo mzima wa umeme na kuwekwa mzuri
kuweza kusambaa kwenye nyumba waliyokuwa wakiishi na galani. Ndipo deni
likaongezwa na mazao sasa aliyokuwa akichukua kwa kina Magesa bila kulipa ila
kurudisha hiyo pesa kila akiuza. Japokuwa Naya alipewa na Joshua pesa ya kulipia
sehemu ya kiwanja walichonunua kutoka kwa jirani yao, lakini bado deni la
ujenzi mzima na mazoa lilikuwa juu. Ndio Bale akafika kulipa nusu!
Wakaandikishana mpaka wakamaliza.
“Labda
mimi nikuulize Bale, unalipa deni lote hili ili iweje?” Geb akauliza. “Nataka
kufanya kile baba yangu alitaka kufanya tokea mwanzo.” Wote wakawa wametulia
wakimsikiliza Bale aliyerudi safari hii akimtamka baba yake kwa heshima! “Baba
alitaka kiwanja kiwe cha Naya, kitabaki kwa jina la Naya, ila nitamsaidia
kukiendeleza kisibakie vile kilivyo. Nataka kulipia chote. Mumpe Naya hati yake
kisha tujenge kwetu. Na sisi tuwe na kwetu. Najua mimi na Naya
hatutashindwana.” Wote wakamshangaa vile alivyobadilika.
“Ngoja
nikuulize Bale. Kwamba sasa hivi upo tayari ujenge pale na bado kiwanja kibakie
kuwa cha Naya!?” Joshua akamuuliza. “Kabisa.” Wote wakawa kama hawamuamini.
“Acha nikuulize zaidi Bale, japokuwa najua mimi unanichukia sana. Hutaki niwe
na dada yako, japo unajua wazi ni mke wangu.” “Mimi sijasema nakuchukia! Ila
ukweli mimi na wewe hatuendani, Joshua. Ninachoamini na harakati zangu za
maisha, sio kama wewe. Ndio nikaamini mimi nitaendana na Malon.” “Ndio ukaamua
kumtoa Naya kwangu, na kwenda kumkabidhisha kwa Malon mpaka akamfanya ndugu
yako awe kama mjinga!? Kana kwamba haitoshi bado unamuelekeza Malon aje
amchukue tena! Kweli unajenga urafiki na Malon kwa kiasi cha kumdhuru dada yako
kwa kiasi hiki, Bale!?” “Subiri kwanza Joshua. Inamaana Malon amerudi tena
huku?!” Bale akawa kama haamini.
Wakamsimulia
kilichotokea siku ya jumamosi. Wakamuona kama amekasirika. “Hivi nyinyi mnamjua
Malon nyinyi? Hakuna jela yakumfunga yule mtu. Nina uhakika leo atarudi tu
uraiani. Na mimi sikuwa nikimjua kama vile alivyokuwa akisema Naya, ni mpaka
nilipoishi naye. Malon alinidanganya na moja ya sharti la kunitoa jela
na kuniweka huru uraiani bila kesi, yani kesi yangu mbaya iliyokuwa
ikinikabili aliniahidi itafutwa kabisa, endapo nitamsaidia kumpata Naya.
Na mimi nilikuwa na hali mbaya jamani. Nipo rumande kwa zile tuhuma. Sikujua
kama nitapata tena msaada maana alinisikilizisha majibu ya kila mmoja wenu
wakati akiwaambia mnisaidie kutoka jela. Alichonisikilizisha ukweli
kiliniogopesha sana, nikaona sina jinsi isipokuwa kuwa na yeye tu na kumsaidia
kile anachokitaka. Naya.” Bale akawasimulia mwanzo akiwa amefungwa mpaka
mwisho.
“Siku ile
Nanaa aliponiambia juu ya baba kuugua kwa ajili yangu, ilibidi kwenda kusaka
ukweli Tunduma, kwa kuwa sivyo Malon alivyokuwa ameniaminisha! Sikuwa
nikijua hata kama mlifika kule kunitafuta! Yaani baada ya kutoka Tunduma, na
kurudi kwake na kunitisha sana nimrudishie Naya lasivyo atanirudisha tena jela.
Mimi nikaondoka kwake nikimwaminisha nakuja huku kumfuata Naya ili nimrudishe tena
kwake. Lakini sikuwa hata na mpango wa kumrudisha kwake kwa kuwa kwanza
nilishagundua alimtesa sana Naya, na nikachukia kuona ametumia ujinga wangu,
kunifitinisha na Naya mtu ambaye sikuwahi kumuumiza kwa kiasi hicho!”
“Lakini
niliporudi nilipokuwa nimemuacha Malon na Naya, ili kumchukua Naya nimlete hapa
kama wewe Geb ulivyosema kama ni moja la sharti lako kabla yakutoa hati yetu,
Malon akaniambia Naya anajifanya vile makusudi ili kunidhulumu. Na mimi kwa
kuwa tayari nilishakuwa na uchungu, chuki kwake nikijua ananifanyia makusudi
kwa kuwa hanipendi, na mimi ikabidi kupambana naye bila kujua kama kweli Naya
hayupo sawa.”
“Nafikiri
alimpiga vibaya sana au sijui ni nini kilitokea, ila vipimo vilionyesha
amegongwa mpaka ameviba sehemu ya ubongo ndio maana hakumbuki! Kwanza alikuwa
amevilia damu mwili mzima kwa kipigo mlichokuwa mkimpa.” Bale
akaumia sana. “Mimi sikumpiga sana. Ni siku ile tu nilipokwenda kumchukua. Tena
ni makofi tu. Itakuwa ni Malon ndiye aliyekuwa akimpiga sana. Na ndio maana
hata safari hii alipotaka nimsaidie kumrudishia Naya, nilimkubalia tu lakini
sikuwa na nia ya kumrudisha. Nia ilikuwa ni kumtuliza wakati nakusanya hii pesa
na kujipanga kisheria, kabla hajanirudisha tena polisi. Ndio nikaja huku Dar
nikimwambia nimekuja kumfuata Naya.” Bale akaendelea kujieleza akisikika yupo
tayari kutoa ushirikiano kwa kina Joshua.
“Sasa
huwa nikiwa huku, naishi nyumbani kwake Kunduchi. Nilipofika sasa nikiwa
nimeshajua amenidanganya kwenye mengi, ikabidi sasa nianze kusaka ukweli.
Katika kufanya uchunguzi wangu, nikakuta ameficha chumbani kwake moja ya laptop
yake aliyotumia kutengeneza kile alichotaka nikisikie. Ndipo nilipochanganya
ukweli wa kule Tunduma na mazungumzo yote aliyowarikodi nyinyi wote mkimjibu
akitoa ushauri wa kupatikana kwangu, mpaka majibu ya marehemu baba. Malon amenitenda
unyama mpaka kusababisha kifo cha baba yangu!” Bale akaendelea.
Bale Atoa Ukweli.
Wote
wakashituka ila wakatulia kumsikiliza wakijua ameanza kujutia. “Kuna kitu
nataka kuwaambia, lakini naombeni msinipeleke polisi wala msinirikodi. Ila mjue
nitalipiza kisasi kama nilivyomlipisha Mbabe.” Wote wakataka kusikia,
wakajiweka sawa. “Nipo kutengeneza nilipoharibu na Malon ndiye aliyeniponza.
Kama nilivyowaambia, yeye ndiye aliyenitoa jela, kwa kutumia askari kabisa.
Wakanificha mpaka alipofika mwenyewe na kuniaminisha kile alichojua ningeweza
kuamini kwa haraka. Ukweli nilijawa sana chuki. Akaniambia lazima kuwakumbusha
kule nyumbani zaidi baba na Naya vile yeye alivyomuhimu kwenye familia, kwa kuwarudisha
chini kabisa. Na akaniambia kwa vile alivyonitoa jela, malipo ni kumrudishia
Naya.” Bale akaendelea.
“Ukweli
Malon ni mtoto wa mtaani anayejua afanye nini ili kupata chochote anachokitaka.
Tena kwa urahisi mpaka huwa ananishangaza! Kwa mfano maswala yako wewe Joshua
na Benadina.” Joshua akashituka sana. “Wewe ulimjuaje Benadina!?” Joshua
akauliza. “Mimi nilikuwa najua tu jina lake moja, tena kusikia kutoka kwa Naya
alipokuwa akimsimulia baba juu ya historia yako ya maisha zaidi upande wa
uwaminifu kwamba huna mambo ya kupenda wanawake ila huyo Benadina tu. Na
nilimsikia Naya akimwambia baba kwamba mlipoachana na Benadina, hukutafuta
mwingine tena.”
“Sasa
wakati nilipokuwa na Malon, mwanzoni tu hata kabla sijaondoka na kwake kwa mara
ya kwanza, na yeye alitaka kukufahamu zaidi ili kuweza kukugombanisha na Naya,
akuone na wewe ni muhuni tu, amrudie yeye. Sasa aliponihoji juu yako nikamwambi
kile nilichosikia kuhusu wewe na Benadina. Akaamini kwa kuwa hukuwa na mwanamke
mwingine baada ya Benadina, basi ulimpenda sana, kwa hiyo haitakuwa shida
kurudisha majeshi endapo Benadina akirudi pichani. Sasa alipotaka kumfahamu
zaidi, sikuwa na taarifa zenu zaidi ila nilijua shule mliyokuwa mkisoma naye.
Kwa taarifa hizo tu, Malon akaniambia ameshampata. Sikuamini, nikacheka tu!”
Joshua akashangaa sana.
“Ni kweli
alimpata, akampa namba zangu za simu na kunitafuta. Ila siku ileile ya kwanza
Benadina aliponipigia simu mimi nilimshitukia. Tena ndio siku tulikuwa kwenye
mshituko wa baba yako kutekwa nyara huko Tunduma akiwa anaomba na Naya.
Alinipigia nikiwa ndio nimerudi Kiluvya kuwa na Naya, pamoja na Zayoni sababu
ndio walikuwa kwenye huo mshituko, baba Naya ndio ametoka kutekwa muda mfupi
sana. Sikutaka hata kuzungumza naye ila nilimgombesha sana Benadina na kumuonya
asijewahi kurudia kunitafuta.” “Ndio maana wewe Malon amekushindwa!”
Akawa kama huyo Bale anasadiki mawazoni kwake.
“Na ndio
maana hapo alikwama. Lakini ninachotaka kukwambia ni kuwa Malon anauwezo
wa kupata chochote anachotaka. Zaidi akiamua. Ila nina uhakika wewe unamtisha
sana Malon. Mpaka sasa hakuwa akijua ni jinsi gani atakuweza, kitu
kinachompandisha sana hasira na kumfanya mwenye chuki zaidi kwako. Ila turudi
kwa kitu nilichotaka kuwaambia juu ya alichonisababisha nifanye huyu Malon.”
Bale akaendelea akisikika na mengi, na yeye Joshua akatulia maana majibu ya
maswali yake yaliyokuwa yakimuumiza na kumchanganya, yalikuwa yakijibiwa siku
hiyo.
“Malon
anajuana sana na walinzi au tuseme anajua tabia nyingi za walinzi kwa kuwa
alishakuwa na yeye mlinzi kipindi Naya alipomtoa jela. Akasema tabia za walinzi
wengi wanapenda bangi. Ili kuwafanya marafiki basi nikuanza kuwapa bangi. Ndipo
tukaanza sasa kuwa karibu na wale walinzi wa pale nyumbani. Wakawa
wakipitishiwa bangi kila wakati, bila kulipa. Walipoona ni deni kubwa ndipo
sasa tukauliza ratiba za pale nyumbani kujua siku gani kunakuaga na mzigo. Ili
sasa kuchoma gala zima.” Joshua akaumia sana.
“Mimi
sikujua kama atachoma na baba yangu na Zayoni, pamoja na bibi!” “Hudhani kama
ilikuwa bahati mbaya?” Wakamtega kwa swali. “Kwa jinsi ninavyomjua Malon sasa
hivi, haikuwa bahati mbaya hata kidogo. Kilichotokea kwa Naya juzi ndio ulikuwa
mpango wake tokea zamani, mimi sikuwa nikijua! Kumtoa baba duniani, aliyejua
anampenda sana Joshua sio yeye tena, ili Naya abakiwe peke yake, ammiliki yeye
bila kipingamizi. Alijua akiondoka baba, yeye atakuwa huru na Naya.
Sitashangaa hata nyumbani kwako Joshua, au kwako wewe Magesa, ametumia mbinu
ileile kuwa karibu na walinzi wenu ili kumsaidia kujua kinachoendelea majumbani
kwenu ili amtoe Naya.” Hapo akawashitua zaidi na kuanza kuamini.
“Kwa kuwa
jinsi anavyofanya nao urafiki, hata akikuomba kitu kwanza hutaona kama ni jambo
la hatari, na pili huwezi kumkatalia. Ninauhakika na hichi ninachosema maana
ndivyo tulivyofanya pale Kiluvya. Sasa kinachoniuma ni kule kuvuka mpaka mpaka kuua
watu wa nyumbani kwetu! Hakika atalipa.” Wote wakabaki kimya kwa muda.
“Mimi
nashauri uache sheria ichukue mkondo wake.” Mungai, wakili wa Magesa na baba
Naya akashauri. “Malon hajasoma shule ya darasani ila amefudhu ya mtaani.
Anajua kucheza na askari kupita nitakavyokwambia. Ninapokuhakikishia
kuwa leo anarudi mtaani, niamini atarudi mtaani. Na huwa hakubali
kushindwa kwenye mambo yake aliyokusudia. Ndio maana amefanikiwa sana kiuchumi
kitu kilichonivuta kwake zaidi. Na hatatulia mpaka amrudishe Naya kwenye
himaya yake. Na kinachoniuma ni sijui ni nini amemfanya Naya mpaka akawa vile!
Mimi aliniambia Naya anajidai tu, ila ni mzima ndio maana na mimi nikiwa kwenye
hasira, nikawa mkali kwa Naya kumbe ni kusudi tu ili kuendeleza kumsadia kwenye
mipango yake miovu. Alinipandikiza chuki bila sababu mpaka kudhuru watu wa
nyumbani kwangu! Sasa mimi mwenyewe nitamuwekea kikomo.” “Nashauri
usijiingize kwenye vita na Malon, Bale. Mmebakia nyinyi wawili
tu, acha..” “Hakutakuwa na kutulia kati yenu mpaka Malon adhibitiwe.
Si mmesema amekuja mpaka nyumbani kwenu nyinyi kina Magesa?” Kimya.
“Sasa
ndio mjue hana mipaka kwa analolitaka. Ana jinsi yake
ya kupata anachokitaka. Na hajui jibu la hapana wala hajui
kushindwa na jambo ndio maana anafanikiwa katika mambo yake. Hataacha hata
kwa kudhuru watu mpaka apate anachokitaka, Naya.” Hapo akagusa pabaya. Kimya
kila mtu akiwaza lake na hofu ikaanza kuwaingia juu ya Malon aliyejithibitisha
ni katili wa kupindukia kwa alama alizoacha mwilini kwa Naya mpaka
kumfanya tahira na teja. Na asiyekuwa na mipaka. Alishafanikiwa kuingia
mpaka kwenye ua ya Joshua kwa kupitia marehemu bibi!
“Magesa, nitarudi na pesa yako nimalizie deni
lako na ndipo niendeleze kwetu.” Bale akasimama. “Naomba msaada wako Bale.
Unajua ni aina gani ya madawa waliyokuwa wakimpa Naya? Maana wamegundua ni
madawa ya kulevya.” Bale akaumia zaidi. “Ni mshenzi yule. Amekataa kabisa
kuniambia. Mimi alinidanganya kama ni dawa tu za usingizi. Ila hakuniambia kama
ni dawa za kulevya! Hata nilipomsihi aniambie, akawa mkali. Ndio sasa najua ni
kwa nini alikuwa mkali kwangu! Alitumia ukali kama silaha tu ya kuficha ukweli
kwa kuwa yeye Malon mwenyewe hatumii madawa ya kulevya, ila bangi tu.
Asingethubutu kuniambia eti ampe Naya madawa ya kulevya!”
“Na si
hivyo tu Bale. Naya amepoteza kumbukumbu sababu yakuumizwa kichwa. Mimi sijui mlikuwa
mkimpigaje mke wangu, lakini mmemumiza kichwa vibaya sana mpaka amekutwa
nauvimbe kichwani, kama nilivyokwisha kukwambia! Kwamba amepigwa sana
kichwani.” “Itakuwa tu ni Malon. Mimi ndio siku ile nilimpiga, tena makofi tu!
Hakika nitamuwekea kikomo.” Bale akajitetea tu hivyo na kutoka. Lakini wakawa
wamemaliza upelezi hata wa kesi ya Kiluvya, ila hofu kwa walinzi wa majumbani
kwao ikaongezeka.
Chalo Naye Aeleza Ukweli.
Wakatoka
hapo kuelekea polisi walikokuwa wameshikiliwa wale walinzi wa Magesa walio mtoa
Naya ndani kumpeleka kwa Malon. Na kweli Malon alishakuwa ametoka kwa
dhamana. Wakaeleza janja ya Malon kuwahonga bangi. Wale walinzi walipobanwa,
Chalo aliyekwishafanya kazi na Malon, na ndiye aliyeenda kumuita Naya ndani,
kumbe kweli alipewa hongo ya pesa nyingi na Malon siku ile, akamuomba awe
anamfuatilia Naya mpaka atakapoachwa peke yake ndipo amuite. Ila
alimuhakikishia ni mkewe. “Anaonekana alimfuatilia tokea mbali, maana ni kama
alifika naye pale nyumbani. Akaishia baa ya kule nyuma baada ya kujua
alipofikishwa huyo Naya aliyeniambia mimi nimkewe. Aliponiwekea
salio na kuomba niwasiliane naye punde Naya atakapokuwa peke yake ndipo asogee.
Nilipomjulisha kuwa ameachwa peke yake pale nje, ndipo akaniambia ili kumuamini
yeye, nimwambie tu ni mumewe. Hivyo tu, basi atatoka. Na kweli, nilipomwambia
hivyo Naya, akatoka kwa haraka, mimi sikuwa na wasiwasi.” “Naya ameniambia
ulipomuita na kumwambia hivyo, kuwa mume wake anamuita, kwa kuwa alikuwa
akinisubiria mimi, yeye moja kwa moja akajua ni mimi.” Joshua akaongeza
ila kwa wasiwasi akijua kwa namna yeyote ile na walinzi wake wamefikiwa.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Wanafanyaje? Endelea kufuatilia.
0 Comments:
Post a Comment