Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com Ni Wangu! – Sehemu ya 58. - Naomi Simulizi

Ni Wangu! – Sehemu ya 58.

Man alimuona amepotelea mawazoni. “Naamini tutakuwa na wakati mzuri huko.” Akamtoa kwenye mawazo wakiwa njiani. Walikaa nyuma, wao wawili tu. Grace akamwangalia akatabasamu na kurudisha macho dirishani. “Grace!” Grace akageuka. “Unawaza nini?” Kwa asili Grace alikuwa mtulivu wa bila kujisingizia. Aliweza kukaa kimya bila kuzungumza neno na isimsumbue hata kidogo. Akacheka. “Wewe ni mkimya sana Grace! Niambie hapo unawaza nini?” “Mambo mengi mchanganyiko.” Grace akajibu taratibu.

“Unamuwaza Danny?” Man akauliza. Grace akavuta pumzi taratibu. Akatulia kwa muda. “Hata yeye namfikiria. Nafikiria hatima yetu. Nini chakufanya nikitoka huko mbugani! Wapi niende! Kwa muda gani! Je nipo tayari kuja kuishi maisha mengine bila wao! Nini nilikosea kwake? Kama kuna kitu kibaya kilimpata, kwa nini nimemuombea na akashindwa kubadilika? Kwa nini moyo wangu umekata tamaa mapema? Nilishawahi kumpenda yeye kama Danny au nilipenda aliyokuwa akinifanyia nikashindwa kufikiria, kama Geb alivyoniambia?” Grace akafikiria tena.

Akaongeza kwa upole. “Nataka kujilaumu kama anavyonilaumu Geb, lakini najirudi.” “Geb anakulaumu nini?” Grace akatulia kidogo. “Mwezi mmoja kabla ya kufunga ndoa na Danny, nilipata muda wa mazungumzo naye. Nilimwambia vile ninavyomchukia Danny. Na mambo mengine mengi. Unakumbuka nilikwambia aliondoka pale tulipokuwa tukiishi naye kabla ya ndoa, baada ya mimi kuleta nyumbani mwanaume mwingine anioe?” “Nakumbuka.” Man akajibu.

“Sasa hayo yote Geb ananiambia ni kama Danny alinifunika kitambaa kwa mambo mengi aliyokuwa akinifanyia. Kwa hiyo alipoondoka niliharakisha kumkimbilia. Nikitaka arudi aendelee kunifanyia aliyokuwa akinifanyia, nikasahau upande wa mapenzi. Sasa najiuliza, kwani mapenzi ni nini? Mapenzi si pamoja na mtu kukujali! Kukufanyia mambo mazuri?” Man akanyamaza.

“Niambie Man. Mtu ukimpenda si utamfanyia mambo mazuri?” “Umesema sahihi kabisa. Kuwa mapenzi ni pamoja na kumjali mtu Grace. Yapo mambo mengi yanabeba penzi. Halafu pia kuna watu wanafanya mambo mengi kwa sababu tofauti tofauti. Ni ngumu kujua kwa nini mtu anakutendea jambo hili au lile. Ila ninachojua upendo wa kweli huwa umebeba sifa nyingi, Grace. Mtu unayempenda ni lazima utamsitiri. Huwezi kumuanika nje, kwa kile ulichokikuta ndani. Tena sirini! Upendo huwa hautafuti mambo yake wenyewe. Upendo unavumilia. Upendo hauhesabu wingi wa dhambi. Hata kukiwa na sababu. Watu tunakasirika, lakini huwa kunakujirudi sababu ya ule upendo.” Grace akafuta machozi.

“Unafikiri na mimi nimekosa upendo? Nimeshindwa kuvumilia?” Grace akauliza. “Swali gumu sana hilo, Grace. Ni ngumu kujibu kwa haraka kwa kuwa ni wewe na Danny peke yenu mmepita mlikopita na mnapita hapo mlipo. Ila sijui inakuaje pale mwenza wako anapokukataa na kutafuta mwanamke mwingine! Hapo sijui inatakiwa kufanya nini kwa wewe unayebaki. Ila kama akijirudi, akatubu, hilo nalo nafafikiri ni swala jingine. Japokuwa bibilia imeruhusu kuachana kwa kosa la uzinzi, lakini kuna kipengele cha kusamehe saba mara sabini.” Man alimueleza taratibu.

“Ni ngumu sana. Ni ngumu mno Man. Kuna matusi ananitukana akiwa na Sara. Sara anakuja kuyarudia mbele yangu na mbele ya msichana wangu wa kazi. Vile Danny anavyonilinganisha mimi na yeye, Sara huko kitandani. Ni aibu mno. Naumia nashindwa kata kumsimulia mama yangu mzazi, kwa aibu. Nabaki nayo nikiumia sana. Nashinda hata kuwa mama kwenye nyumba niliyojenga mwenyewe, kwa fedheha! Aibu kwa wafanyakazi wangu ninaowalipa mshahara! Nashindwa hata kuwaongelesha kwa vile ninavyoanikwa vibaya. Si kijana wa maua, si walinzi getini. Wote wanajua mapungufu yangu ya ndani kabisa.” Grace akaendelea kulia. Wakajisahau walipo.

“Nyumba ni yangu mwenyewe, lakini naogopa hata kurudi, Man. Nafikiria narudije tena pale? Naogopa mpaka nakosa raha! Halafu kwa kawaida mimi nimuoga sana wakuwa peke yangu. Nafikiria labda nikija kurudi, niende nikaishi na mama. Lakini napo najihisi aibu zaidi. Jamii itaniona nimeshindwa na mtoto mdogo! Lakini najua wazi sina nguvu za kupambana, na hata Mungu akinijalia nguvu, sipo tayari kupambana tena. Nimekinahiwa Man. Sitaki tena. Nafikiria narudije kwa mwanaume aliyeanika mwili wangu nje kwa kiasi hiki!? Tena kwa kunitukana sana. Naweza kusamehe  hata kabla sijaombwa msamaha, lakini narudije kumvulia nguo mwanaume kama Danny!?” Grace alilia kwa uchungu sana. Kila alipopata nafasi, alitoa dukuduku lake.

“Njoo hapa karibu yangu.” Grace akajisogeza. Akamshika mkono. “Naomba nikuombe kitu. Jaribu kutulia. Unakumbuka jana uliniambia unahisi umetengeneza rafiki?” Grace akatingisha kichwa kukubali. “Basi naomba ujue unaye rafiki wa kweli. Katika shida na raha tutakuwa wote Grace. Muda na wakati wowote utakaonihitaji nitakuwepo na wewe. Naomba ujue haupo peke yako tena. Tukifika, tutapata muda wakupanga mambo vizuri. Ili usiishi kwa shida tena.” “Na likizo yangu ikiisha nikatakiwa kuondoka?” Grace akauliza.

“Nimekwambia nitakuwa na wewe wakati wote.” “Wewe maisha yako, yako huku Man. Mimi maisha yangu yako Dar. Huko ndiko naogopa hata kurudi. Sasa tukiachana itakuaje?” “Nimekwambia tutapata muda wa mazungumzo Grace. Nimepita hapo ulipo. Tena mimi nikiwa sina mtu wakunishika mkono kama hivi. Au hata mtu wakuzungumza naye, ila kutendwa mabaya tu. Hatutashindwa kupata njia. Kuwa mvumilivu.” Grace akatulia. 

Man akajiegemeza kwenye kiti, akamsogeza karibu. Grace akarudia kumkumbatia kama jana yake usiku. Sema safari hii walikuwa kwenye gari akihema karibu sana na shingo yake, kwa kuwa alikuwa amekaa. Man akaanza kumpapasa taratibu. “Is gonna be okay, Grace. I promise.” Alimnong’oneza na kumbusu akimwakikishia kila kitu kitakuwa sawa. Grace akajivuta kwake zaidi. “Asante.” Grace akashukuru. 

Ukisema Cha Nini,…

          Grace mwanamke anayependa kupendwa na kubembelezwa tokea mtoto. Mikononi ndio sehemu zake zakujidai. Baba yake ndiye aliyemwanzishia hilo. Alikuwa mikononi mwa baba yake mpaka kifo chake. Hajui maisha mengine ila kukumbatiwa na watu wamuonyeshe wanamuhitaji. Danny amempitisha kwenye wakati mgumu ambao hakuwahi hata kudhania kwa uzuri uliokuwa ukisifiwa na kila amtizamaye, gafla Danny anatangaza kukinahiwa! Ametoka Dar akiwa mnyonge, ametua kwenye mikono ya Man! Mwanaume aliyekuwa na yeye akitafuta penzi! Mungu awape nini? 

Man alishachezea nywele za kizungu kwa muda mrefu. Hakushindwa kumtuliza Grace kifuani na kumpa yakizungu. Mabusu ya hapa na pale, bila kuvuka mipaka, yaliendelea huku wamekumbatiana, dereva akiendelea kukanyaga mafuta. Mara kadhaa Grace alinyanyua uso kumtizama Man wakati wanazungumza. Napo hapo Man akabusu kipanda uso, huku akiweka sawa nyusi nyingi za Grace na kumtuliza. 

Grace alitulia kama kitoto cha paka, mikononi mwa Man, akiendelea kuchezewa nywele huku akiliwazwa kwa sauti tulivu bila kelele kama Danny. Wote walishakuwa kwenye ndoa. Wote walisalitiwa. Ila Man yeye tokea mwanzo aliingia kwenye ndoa aliyotegwa. Tena akiwa mtoto mdogo. Akafungiwa ndani na huyo mama wa kizungu. Akageuzwa yaya kisha kuhamishiwa jela alikotendwa unyama. Alitua nchini, hana hamu ya mapenzi. 

          Akashangaa imekuaje kwa Grace! Tena kwa haraka vile. Malisa ndiye aliyepeleka mambo kwa haraka. Lakini alikusudia kumvuta Grace taratibu huku akisubiria kujua hatima yake na Danny, ili na yeye ajipenyeze kwenye moyo wake. Lakini anajikuta Grace yupo kifuani. Anafurahia kifua chake kama yeye anavyofurahia kifua chake kulaliwa. Anatamani historia za kilio cha Grace kiendelee ili apate sababu ya kumuweka kifuani. Mwanamke mtulivu, asiye na papara hata na maneno yake. Leo Danny anatangaza kukinahiwa! Mungu amjalie yeye hiyo nafasi. Ndio ombi lililobaki kwa Man.

Mambo Ya Mbugani.

Wallifika hotelini, dereva akaegesha gari mbele ya hoteli, lakini hakuna aliyetamani kushuka. Wakabaki wakiangaliana huku wamekumbatiana. Wote walijua wameshawashiana tamaa njia nzima. Dereva akaamua ashuke na kuondoka kama kumpa nafasi bosi wake. Man alirudia kumbusu Grace kwenye kipanda uso mara kadhaa huku akimpapasa. Lakini safari hii aliongeza nguvu kidogo mpaka Grace akahisi mikono ya kiume ikipita mwilini mwake.

Ni miezi zaidi ya 6 sasa tokea Grace ashikwe vile na mwanaume kimapenzi. Hata hivyo mbali na Danny hakuwa akimjua mwanaume mwingine. Mwili mzima ulikuwa ukipiga kelele ukimtaka Man asaidie kutuliza. Man naye ni miaka mingi. Hakuwa hata akikumbuka ni lini aliweza kuwa na mwanamke kitandani. Akatoa ujuzi wake wa kiume, akamfurahisha mwanamke. Hisia alizokuja kuamsha Grace mwilini mwake, zilikuwa zimefukiwa muda mrefu sana.

“Watakuwa wanakusubiria. Ngoja na mimi nishuke nikaangalie chumba nitakachokuwa nimetafutiwa na Beka.” Grace alianza kujitoa taratibu. “Na hapa pia nina chumba kama kile ulichompisha Malisa na familia yake. Tunaweza kutumia wote.” Grace akacheka kidogo, akainama kama ambaye hajui aseme nini. “Ukishindwa, mimi nitalala kwenye makochi. Usiogope.” Man akaongeza kwa upendo huku akimtengeneza nywele zake. “Sawa.” Grace alikubali kwa sauti ya upole huku akitabasamu. Wakatoka.

Hawakuwa na haja ya kwenda mapokezi. Man alikwenda kwenye chumba chake moja kwa moja. Kalikuwa kajumba kadogo kanacho jitegemea. Vinyumba vingine vilionekana vina milango miwili. Kuashiria wanaweza kukaa wageni wawili, tofauti bila kuingiliana. Ila kutumia baraza pamoja. Palikuwa pazuri na patulivu. Grace akaanza kujisikia vizuri. “Mmejitahidi kuwekeza kweli!” Grace akasifia wakati Man anafungua mlango. Alikuwa amebeba mizigo yote ya Grace. Yeye alisema vitu vyake vyote vipo hapo kama ilivyo kule. Walipofungua, chumba kilikuwa kisafi sana. Kimetengenezwa na kuwekwa vitu vizuri.

“Inamaana vyumba vyote vipo hivi!?” Grace akauliza. “Nimejitahidi kuwa hivyo. Lakini hapa ni zaidi kwa kuwa ni kama nyumbani kwangu. Sina maisha mengine ila hapa na Arusha. Nikiwa Dar, nakuwa kwa mama na baba.” “Tena nilitaka kukuuliza wazazi wako wapi.” “Kwa hiyo umepata jibu. Wote wako wanaishi Dar. Kasoro tu mimi ndio ninaishi huku.” “Unapapenda?” Grace akauliza. Man akafikiria kidogo.

“Mwanzoni ilikuwa kama inanilazimu. Sikuwa na namna. Nilipoanza kuzoea, nikaona patanisaidia kufukia mawazo yangu hapa. Nikajichimbia kwenye kazi tu mpaka imefanyika kwangu. Hata hivyo sikuwa na sababu yakuchagua niishi wapi hapa Tanzania. Ilikuwa popote.” Grace akakaa kwenye kochi. “Unataka ukazunguke kidogo sasa hivi, au leo unataka kutulia tu ndani mpaka kesho?” “Nimependa wazo la pili. Leo nikae tu humu ndani, nipumzike. Kesho ndio nitoke.” Man akaenda kukaa pembeni yake.

“Basi nitarudi baadaye kidogo. Ngoja nipite niangalie kama mambo yamekaa sawa. Nitarudi na chakula.” “Sawa.” Grace akaitikia. “Kuna kitu chochote maalumu unataka kula?” Grace akafikiria kidogo. “Hapana. Chagua chochote tu.” Akabaki akimwangalia. Grace akashangaa hasimami tena. Akacheka. “Nimefurahi upo hapa na mimi Grace. Naamini tutakuwa na wakati mzuri.” “Hata mimi. Nimefurahia mikono yako. Mwenzio napenda kubembelezwa.” Man akacheka sana.  “Usinicheke bwana!” “Nilikuona tokea siku ya kwanza. Nikajiambia jamaa atakuwa anafaidi! Umekaa kama mtu wakushika wakati wote. Na unatia raka ukiwa mikononi. Unautulivu fulani ambao unaambukiza mtu anayekushika.” “Kwa hiyo na leo usiku utanikumbatia?” Grace akauliza huku amefunika macho akicheka.

Man alizidi kucheka. “Ila usinifikirie vibaya. Mbali ya Danny, wewe ndio mtu wa pili kumruhusu anikumbatie na kunishika hivyo. Sio kila mtu nakuwa namruhusu.” Grace akajitetea.

“Mimi sijui mambo ya nyuma. Ninachojua, Mungu wangu amenirehemu.” Grace akacheka sana. “Usije ukajuta na wewe kama Danny.” “Huwa siongozwi na hisia Grace. Ingekuwa hivyo sasa hivi ningekuwa na msururu wa watoto na wanawake.” “Sasa unaongozwa na nini?” Grace akauliza. “Nitakuja kukwambia nikirudi.” “Kwa hiyo nisilale nikusubirie uje unikumbatie huo usiku?” Man akacheka tena. “Kwani natakiwa kusubiri mpaka usiku?” “Sasa si ndio utakuwa umemaliza kazi zote? Tunakaa kitandani, tunatulia. Hamna kutoka tena.” Man akacheka.

Akamsogelea. Kwa mara ya kwanza akambusu mdomoni, lakini kidogo tu. “Nitakuja kukukumbatia.” Grace akacheka huku ameshika midomo yake kwa vidole. “Asante.” Akashukuru taratibu. Macho ya Grace yalikuwa ni ngumu kumruhusu mwanaume amwache hivi hivi hasa akiwa amekukaribisha. Akambusu tena kwa haraka mdomoni. Grace akacheka kwa deko. Man akaona arudie tena, ila safari hii apunguze haraka. Akambusu midomo ya nje kwa muda kidogo huku amemshika shingoni. “Asante Man.” Grace akashukuru tena wakati Man akimwachia.  

“Nimepatwa na uzito wa kutoka. Natamani kubaki hapa na wewe.” “Usiwe na wasiwasi. Mimi nipo hapa nakusubiri.” Grace aliongea kwa  upendo, akibembeleza. Hata yeye alionekana anahali mbaya. Man akafunga macho nakujiegemeza kwenye kochi. Grace akajisogeza kifuani. Akamkumbatia tena. Man akavuta pumzi kwa nguvu akafungua macho. Wakabaki wameangaliana. Kwenda ameshindwa, kuendelea ameshindwa.

“Hali yangu mbaya Grace. Sijafanya mapenzi zaidi ya miaka 8. Na sijafanya mapenzi nikaridhika zaidi ya miaka kumi.” “Pole.” Grace akamuhurumia. “Natamani nibaki na wewe hapa ndani hata siku tatu tu. Unafikiri tutakuwa tumeharakisha sana, pengine ungehitaji muda zaidi? Samahani Grace. Najikuta nakuwa muwazi sana kwako mpaka naogopa.” “Lakini hivyo ndio nafurahi Man. Asante. Ila nashauri ukaweke mambo sawa, ili tukiamua kujifungia humu ndani isiwe usumbufu tena.” Bado Grace alikuwa amemkumbatia. 

“Naomba basi nikubusu hata kwa dakika mbili tu ndio nitoke.” Grace akatoa tabasamu la kukubali. “Lakini nataka nikubusu kwa uhuru wote, Grace.” “Ndio unatakaje?” “Nikuweke kitandani, nikubusu nikiwa nimetulia na kwenye nafasi.” “Okay.” Grace akajibu kwa upole. Wakatoka pale kwenye makochi, wakahamia kitandani.

Grace akavuta mto akajilaza. “Lakini Grace, mimi huwa si busu tu midomo. Napenda kuwa huru.” “Okay.” Grace aliendelea kukubali taratibu huku akifikiria aina gani ya busu anayotaka kupewa. Tayari mwili wake ulikuwa ukichemka. Man akaanza utundu wake pale. Alinyonya midomo ya Grace, akaja shingoni. Masikioni. Akarudi midomoni. Shingoni kuelekea kifuani ambako alishuka taratibu huku akiminya minya mwili wa Grace taratibu. Miguno na mihemo ya Grace ikaanza kuchanganya. Aliharibu alipofikisha midomo yake kwenye sehemu juu ya matiti ya Grace, ambayo yalikuwa bado kwenye shati, ndani ya sidiria. Grace alianza kuhangaika. Man akajua anataka amfungue. 

Akarudi midomoni nashingoni wakati akimtoa nguo taratibu. Alirudisha macho kifuani wakati amemalizia kumfungua sidiria nyuma ya mgongo. “Waw!” Man akapagawa baada ya macho yake kutua kwenye matiti ya Grace. Ilimchukua zaidi ya dakika mbili kutoka kifuani kwa Grace. Alihama titi moja hadi jingine. Kulia na kushoto kama mtoto mwenye njaa kali, mpaka akasahau midomo.

~~~~~~~~~~~~~

Kwa kuwa walishakuwa wamewashana tamaa tokea njiani, hakuna jinsi angemuacha Grace vile, eti Man akatoka kwenda kusimamia kazi. Usiku uliopita walijikaza, wakalala wakiwa wamekumbatiana. Miili imegusana kwa karibu vile! Man alishamtamani huyo Grace tokea anamwona kwa mara ya kwanza. Alitamani kugusa huo mwili mara nyingi tu. Grace naye alishamtamani Man. Alishapagawishwa na umbile lake. Ni kama alikuwa mwanaume wa ndoto zake. Kinachowazuia ni nini!? Grace akasahau kabisa maombi ya kufunga na kuomba juu ya Danny.

~~~~~~~~~~~~~

Ndani ya muda mfupi sana, wakawa kama walivyozaliwa pale kitandani. Man akigugumia na yeye. Kila aliposhika, macho yake yaliitwa na pengine. Man akabaki kama amechanganyikiwa na Grace pale kitandani. Akaona ili asionekane mjinga, kwa umbile lile alilofanikiwa kuliona kwa macho, aingie tu ili roho yake itulie. Alikwenda kumkumbatia Grace kwa mkono mmoja huku akipenya taratibu. Alishamlainisha kwa mabusu ya kila mahali na unyonywaji ambao Grace hakuwahi kufanyiwa hivyo tokea anazaliwa. Danny ni mtu wa kinyaa na Grace alikuwa mwanamke wake wa kwanza. Mtoto aliyelelewa na mapadri, hakuwa na mengi. Sasa huo mwili ukakutana na Man. Mtoto wa uzunguni! Alinyonya huo mwili kana kwamba anakula ice cream. Grace mkimya sio huyu kitandani kwa Man. Man aliutenda huo mwili wa Grace, akabaki akilia nakuomba rehema ya Man.

Kwa mara ya kwanza baada ya miaka mingi, Man anamwingilia mwanamke. Tena mweusi wa rangi anayoipenda yeye! Alitua ndani huku roho yake imejawa hamasa. Alijitahidi kutulia huku akisugua meno, akawa anapanda na kushuka taratibu bila papara. Alikuwa amemkumbatia Grace kwa mkono mmoja huku akimsugua taratibu. Kilio alichokuwa akikitoa Grace, Man akajua anachokifanya mwilini mwa mwanadada huyo, kinapokelewa. Mara kadhaa aliinama kunyonya midomo yake, shingo na masikio huku akifanya naye mapenzi. Alikuwa akitoka midomoni kwenda shingoni na masikioni huku akiendelea kufanya naye mapenzi taratibu na kwa hisia zote. Mkono ule mwingine ulikuwa na kazi ya kutembea mwilini mwa Grace.

Alishika kiuno, huku akimnya minya hips zake kwa uchu. Grace aliendelea kunung’unika kwa huba pale kitandani. Man aliongeza nguvu kwa kadiri ya uhitaji wao. Baada ya muda wakutosha wa mapenzi, Man alipomfikisha Grace kileleni, akaridhika kuwa ameridhika ndipo na yeye akamkamata kwa nguvu, Grace akahisi ameongeza nguvu si kawaida maana hata kalio alilokuwa amekamata, alilishikila haswa akiwa juu yake mpaka akamalizia. Wote wakawa wamekata kiu kwa muda huo. Man akamvutia kifuani, wakabaki wanahema.

Grace alimbusu mara kadhaa kifuani akimshukuru. “Asante.” “Karibu. Na mimi nakushukuru Grace. Asante sana. Naomba usiondoke hapa kifuani, nilale kidogo.” “Okay.” Grace akajivuta karibu zaidi. Man akambusu midomoni. Hapo hapo akalala. Grace akabaki amelala kifuani kwake, amejawa na furaha. Akafurahia vile alivyoweza kuenea pale kifuani kwa Man. Akafurahia ile hali ya utulivu. Aina ya mapenzi aliyofanya naye. Grace aliyejua aina ya mapenzi ya Danny tu, akaonjeshwa penzi jingine lisilo na kinyaa. Man hakumpa hata style za ajabu. Moja tu, lakini alimtenda vilivyo.

Hapakuwa na papara wala kinyaa. Alimtuliza hapo kitandani. Akatembeza midomo kila mahali na kumuacha Grace hajitambui. Alijawa na furaha. Hakuna jinsi ungemwambia kuondoka kwa Danny si uamuzi sahihi, akakuelewa. Hata kama ingekuwa malaika ametumwa kumwambia hivyo, asingesadiki tena

~~~~~~~~~~~~~

Zilipita siku tatu mfululizo, Man na Grace wakihudumiwa humo ndani bila kutoa hata mguu nje. Kwa muda mrefu sana tokea aanze hiyo kazi au apokee majukumu kutoka kwa baba yake, Man aliweza kumwachia kijana mwingine majukumu yote nakutaka aachwe kabisa apumzike. Familia yake wote walijua yupo na Grace kitu kilichomfurahisha zaidi Grace kujua amepokelewa vile alivyo na kwamba ni mama, lakini halikuwa tatizo kwao. 

“Sasa kama huyo sio Mungu amejibu maombi yangu ni nini?” Grace aliwaza asubuhi hiyo akiwa na Man pale chumbani, akimsomea ujumbe kutoka kwa mama yake. Alituma ujumbe wa kuwatakia mapumziko mema. Hakuna jinsi yakueleza furaha ya Grace. Ilionekana mpaka usoni. Muda wote alikuwa mikononi kwa Man, akipapaswa. Mabusu ya hapa na pale ndio yalikuwa hayahesabiki kwani walianza na kumaliza kila wakati.

Damu Nzito,..

Ilikuwa siku ya ijumaa, mida ya saa nane mchana, Grace na Man wakiwa  katikati ya mapenzi, simu ya chumbani kwa Man iliita. Man alikasirika sana. “Ni nani anapiga na wakati nimeshawaambia labda iwe muhimu sana?” Grace akacheka. “Pokea. Labda ni muhimu.” Man akanyoosha mkono akapokea. “Kuna nini?” “Ni simu ya Grace. Kuna mtu amesema ni lazima azungumze naye.” Man akakunja uso, akamwangalia Grace. “Nini?” Grace akauliza. “Simu yako.” Man alionekana kuishiwa nguvu kabisa.

Grace akavuta shuka, akajifunika vizuri, akasogelea simu. Akaivuta karibu. “Halow!” Grace aliitika kwa upole. “Subiri.” Muhudumu akamjibu. “Grace!” Akasikia sauti ya Geb. “Umenishitua bwana!” Grace akalalamika. “Wewe ndio unanitia wasiwasi G. Kwa nini unafanya hivyo? Uliniahidi nini?” Geb alilalamika na yeye. “Samahani. Nilisahau!” “Wewe sio msahaulifu G. Umepuuza.” Grace akacheka. “Usicheke bwana! Mama pia anawasiwasi.” “Msiwe na wasiwasi mimi nipo salama. Kwanza nimepitisha siku..” Grace akanyamaza. Akakumbuka alitakiwa ampige simu siku ya jumatano.

“Samahani Geb. Basi kesho nitapiga.” “Upo salama?” Geb akauliza. “Nipo salama. Vipi wewe na watoto?” “Tunaendelea vizuri.” Geb akajibu. “Na Nanaa?” Grace akauliza tena. “Namshukuru Mungu hajambo.” Geb akajibu. “Umeshamuomba umuoe?” Grace akauliza. “Hata akikubali nitataka muda wa kwenda naye kwenye fungate. Nani nitamuachia kazi?” “Hapana Geb. Hiyo isiwe sababu. Kwanza tumeweka mfumo mzuri sana ambao mimi au wewe tunaweza kufuatilia mambo ya kazini tukiwa mbali. Sio lazima tuwepo hapo.” “Sasa unataka niwepo kwenye fungate huku nafuatilia mambo ya ofisini? Ungekuwepo hapo sawa. Lakini hata kupiga simu kutujulisha kuwa upo salama, inakuwa shida!” “Ni mara moja tu Geb na wewe! Na nimekuomba msamaha kaka yangu. Kwani hujanisamehe?” Kimya. 

“Geb jamani! Utaanza kuninyima raha.” “Basi Grace. Usije ukaanza kulia. Nahisi nimekuwa na hamu na wewe.” Grace akacheka. “Hata mimi nina hamu na wewe.” “Si urudi sasa?” “Bado nataka muda Geb.” “Mbona unasikika kama huna matatizo?” Grace alicheka sana. “Hukuondoka na kicheko hicho Grace! Naona umeshapumzika inatosha. Njoo bwana na mimi nioe.” Grace na Geb, ni watu waliozoea kuwa karibu wakati wote. Japokuwa usingewakuta wakiongea sana, lakini kila mmoja alithamini uwepo wa mwenzake.

“Wewe zungumza na Nanaa. Akikubali hata kesho, mimi nitarudi kwenye harusi yenu na nitachukua vitu vyote vitakavyonisaidia kuendesha mambo ya ofisini ili wewe utulie huko kwenye fungate. Unajua siwezi kukutupa kipindi unachonihitaji Geb. Nitakuunga mkono kwa kila hali. Lakini sipo tayari kurudi kwa sasa. Nimekusudia kuwa mbali na hapo kwa hizo siku 30. Acha nione nini kitatokea baada ya hapo. Naomba niunge mkono katika hili.” “Sawa.” Geb akaitikia.

“Sasa utamuomba Nanaa?” Grace akauliza. “Natamani sana kumuoa kabla hajajifungua.” “Sasa kinachokuzuia ni nini Geb? Unampenda sana huyo mtoto.” Geb akanyamaza. “Huwezi kuishi bila Nanaa. Nakujua Geb. Heri umfanye awe mkeo kihalali, mmalize hilo mtulie.” “Tatizo sio mimi Grace. Ni yeye. Anajihisi kama sio msafi kwa kuwa amebeba mtoto wa Malii!” Geb akaongea kwa uchungu kidogo.

“Huu ndio wakati wa wewe kumuonyesha kuwa hata aweje, wewe bado unampenda na kumuhitaji. Hakuna kitu atafurahia kama akiona unamuoa vile alivyo. Mwambie hujali kama amebeba mtoto wa Malii au vipi. Unamtaka yeye.” “Nimemwambia G!” “Hapana Geb bwana! Acha ku sound kama umekata tamaa tayari, wakati mimi nakujua wewe ni mtu ambaye hushindwi na jambo! Acha kukata tamaa na kukubali Nanaa ambaye yupo katika hali hiyo ndio awe muamuzi wa maisha yenu wote na watoto! You always manage to stay on top of all games. Inakuaje sasa?” Geb akanyamaza.

“Unanisikia Geb? Na ukute wakati mwingine anakujaribu kujua upo tayari kwenda naye umbali gani. Lazima umuonyeshe hata kama maji yana kina kirefu kiasi gani, upo tayari kuzama naye. Unanisikiliza lakini.” “Nakusikia. Sasa akikubali, utakuja? Maana sitaki kuwa peke yangu siku hiyo.” “Nakuahidi nitakuja Geb. Nitaanza kwa kumuomba msamaha hata kwa ujumbe, halafu nisubiri nione atajibu nini. Akisamehe na kunifungulia mlango, nitakuja hata kusaidia kumtafutia nguo za harusi. Mkikamilisha jambo lenu, na mimi nitarudi mapumzikoni.” “Asante G. Basi nitazungumza naye.” “Nakuombea ufanikiwe Geb.” “Asante.” Wakakata simu.

 ~~~~~~~~~~~~~

Man alikuwa akimsikiliza jinsi anavyozungumza na kaka yake. “Mnaonekana mpo karibu sana na Geb!” Grace akacheka. “Ni pacha mwenzangu. Na ananipenda sana Geb. Hawezi kuniona nalia. Tokea tupo watoto. Anaweza kufanya chochote kwa ajili yangu. Ni kama baba kwangu.” Man akacheka. “Kwa nini anakutafuta?” Grace akamsimulia makubaliano yao ya kumpigia simu mara moja, kila baada ya siku tatu. Man akacheka.

“Hivi anajua kama wewe ni dada yake?” “Anachukia hiyo kitu! Kwanza hataki hata nimkumbushe hivyo au mama amkumbushe. Hataki hata kuzungumzia udogo wake kwangu. Anatamani mimi ndio ningekuwa mdogo.” Wakacheka. “Ni vizuri kupata watu wanao kufuatilia kuliko ungekuwa peke yako kwenye kipindi hiki kigumu.” “Lakini hata awe karibu yangu kwa kiasi gani, unajua siwezi kumwambia yeye kila kitu. Na mama ndio kabisa. Namlaumu kwa kumleta Sara kwenye maisha yetu. Najua na yeye anajutia, lakini amenitenganisha mimi na wanangu.” Wakaanza kuongea.

Grace alisimulia mambo mengi. Huku akilia, kulaumu na kusononeka. “Lakini mimi naona unamlaumu mama bure Grace. Mbona Geb aliyeletewa huyo mwanamke asimchukue, halafu Danny kwa kumuona tu akamchukua?” Grace akafikiria. “Inamaana kama asingekuwa Sara, basi angekuwa Jamila au Jane au Yusta! Imekuwa Sara, kwa kuwa alikuwa karibu na yeye alikuwa  kwenye mawindo.” Man akaendelea. “Unasema mama alimfukuza Sara. Umeshajua ilikuaje Danny yeye akampata huyo Sara? Inamaana walitafutana. Na Danny akakubali kumpokea yeye.” Man akasisitiza.

“Usitake kuniambia eti leo ugomvi wa Malisa na mumewe, halafu mama Ole akaingilia, kumtetea mtoto wake Malisa, eti  wewe leo ukufanye uanze kutafuta mahusiano mengine mbali na mimi kwa sababu mimi nilijua, halafu sikuongea kitu! Useme unawaadhibu ndugu zangu kwa kupitia mimi! Kweli Grace? Wewe inakuingia akilini au alikutafutia tu sababu?” Man ikabidi awe muwazi. Grace akabaki akifikiria.

“Imekuaje sasa Geb na Nanaa tena wako pamoja?” Man akahoji na kumtoa Grace kwenye mawazo. “Sijawahi ona Geb akipenda, kama alivyompenda huyu mtoto.” Man akacheka. “Ukisema mtoto, unamaanisha nini?” “Nanaa ni mdogo sana kwetu. Halafu kazuri kama katoto. Hata watoto anaomzalia Geb, utapenda kuwaangalia tu. Wazuri sana.” Man akacheka. “Ndio maana Geb hawezi kuishi bila yeye?” “Sio hivyo tu. Katika watu wanaomjulia Geb, ni Nanaa. Anamjulia sana, hata mimi huwa sijui anawezaje. Yaani kipindi cha miezi mitano waliyokuwa wametengana, Geb akiwa amemkasirikia Nanaa, Geb alikonda akawa kama babu mzee. Ungemuona, ungesema ana upungufu wa kinga mwilini. Ni kwa kuwa Nanaa hakuwepo kwenye maisha yake.” Akamsimulia Man mwanzo mpaka mwisho wa mahusiano ya Geb na Nanaa. 

“Hawezi kulala usingizi mzuri, wa masaa mengi mbali na yule mtoto. Yaani Nanaa akiumwa akalazwa, Geb anahama nyumbani, anahamia hospitalini. Unaweza kufika asubuhi kumuona mgonjwa, ukamkuta Nanaa amemkumbatia yeye Geb, kwenye kitanda hapo hospitalini, amelala utafikiri yeye ndio mgonjwa!” “Haiwezekani Grace! Yaani analala wodini?” “Ili asikatazwe na mtu, au asiingie aibu, inamlazimu kumpeleka Nanaa hospitali zile za ghali, tena atake alazwe chumba cha peke yake. Ili na yeye aponee hapo hapo.” Man alicheka sana. “Haiwezekani Grace!” “Sisi wenyewe tulikuwa tunashangaa, mpaka tukawazoea.” Walitumia muda mwingi kufahamiana. Man alimueleza mambo ya kwao na yeye Grace akamueleza kila kitu cha kwao. 

Geb na Nanaa.

Geb akapiga simu kwa Nanaa mara baada ya kuagana na Grace.  “Hivi nilipoondoka nilikwambia nakupenda?” Nanaa akacheka sana kisha akajibu. “Mimi hata sikumbuki!” “Basi nakupenda Nanaa.” “Asante Geb.” Kimya. “Kweli Nana?” “Nimesema asante, hujasikia?” “Hayo ni majibu ya jumla sana bwana.” “Ukija, nitakupa jibu jingine. Usichelewe kurudi sasa.” “Utanifanya nirudi sasa hivi.” Nanaa akacheka sana. “Fanya kazi dad. Eti Liv?” Nanaa akampa simu Liv. “Bye dady!” “Mbona ananiaga kabla ya salamu?” Geb akauliza Nanaa akacheka.

“Anamfundisha Magesa kupanga blocks. Nimemchoza makusudi kwa kuwa wamenitenga.” Geb akacheka. “Na asivyopenda kusumbuliwa akiwa na mambo yake huyo!” “Kamkaba Magesa wangu! Mwanangu hana raha! Kila akiondoka, anamfuata anamwambia lazima ajifunze. Sasa unamjua Magesa alivyo na mambo mengi. Mambo ya msingi na yeye, vitu viwili tofauti. Raha yake yeye ashike kila mahali, sio akae chini afanye jambo moja.” Wakacheka.

“Mnafanyaje sasa?” Geb akauliza. “Tupo tu. Wametoka sasa hivi kusafisha humu ndani, ikabidi kuwatoa watoto nje. Dada akiwa na pajama zake hivyo hivyo. Wamecheza hapo kwenye mabembea. Hapa nasubiri amalize shule yake kwa Magesa, akaoge. Maana kila nikimwambia twende tukaoge, ananiambia ‘subiri kwanza mama!’ zaidi ya dakika 20 sasa. Mwenzie nilishamuogesha tokea asubuhi, yeye kachelewa kuamka kama kawaida yake. Anataka amueleweshe Magesa, Magesa anaona anapotezewa muda, basi hawamalizi.” Geb akacheka. 

“Nawatamania.” “Lazima. Kwa nyimbo hizi za ABCs zinazoimbwa kuanzia dada akimka mpaka tukilala! Lazima utamani kuwepo humu ndani.” Geb akazidi kucheka. “Hapa kichwa kimejaa nyimbo za akina Diego.” Geb akaongeza. “Mwenzio naimba za Sofia bila kutarajia. Kila mdomo ukifunguka naimba ‘Sofia the Great!’.” Wakazidi kucheka. Kila Liv alipokuwa akiamka, alihakikisha kila tv ya humo ndani inawashwa cartoon zake. Hakuna kinachoendelea ila mambo ya kitoto tu. Wakaendelea kuzungumza huku wakicheka.

~~~~~~~~~~~~~

Japokuwa hawakurudi kufanya mapenzi, lakini walilala pamoja. Amani na furaha vilitawala kati yao. Geb akawa mtulivu sana, hata Nanaa akawa akishangaa jinsi alivyobadilika asijue na yeye alishaonjeshwa joto ya jiwe akajifunza, hasira hasara. Mungu alimrudishia utulivu hata na kwa watoto wake pia. Aliweza kurudi kwenye mazingira aliyokuwa akiyafurahia hakuna sababu asiwe mtulivu. Kama kawaida yake, Nanaa alikuwa akienda kumpokea kila alipotoka kazini. Kila akishuka kwenye gari, alikutana na mapokezi ya kufurahisha na kumfanya awe anatamani kurudi nyumbani kila anapochoka na majukumu ya siku.

 Nanaa na  wanae wanakuwa wakimsubiria na akafanya tukio la kumpokea ‘dad’ ni kitu cha kufurahisha sana mpaka wanae wakawa wakisubiria kwa hamu. Akishafika Geb basi watamshangilia kwa furaha, watapata mabusu kutoka kwa baba yao. Nanaa atabeba chochote alichokuja nacho Geb, yeye Geb anabeba watoto.

Anaweza kurudi nao kwenye mabembea ya hapohapo kwenye apartment wacheze tena kidogo. Au kama hajachelewa au hajachoka, basi anaweza kuwapeleka sehemu nyingine kama kwenye mgahawa mzuri wenye sehemu ya kuchezea watoto, wakati Nanaa akila kama kawaida yake haishiwi na njaa kama mwanae Magesa. Au mara nyingine humpeleka kumfundisha kuendesha gari uwanjani. Inategemea muda atakaorudi nyumbani na hali yake, au watoto wao. 

Upendo wa kweli ulionekana katikati yao. Ila Nanaa alijua wazi Geb anateseka kuwa mbali na mama yake. Japokuwa alimchagua yeye, lakini alijua wazi analipa garama ya kuwa mbali na mama yake. Hakujua wanaonana wakati gani, ila akaacha kuchukua watoto na kwenda nao kwa bibi yao. Hakuwa akiaga kama anakwenda, ila alijua wanaonana na kuwasiliana tu.

Ni kweli Nanaa alikuwa amemkasirikia sana mama G. Lakini ni mtu ambaye walikuwa naye karibu sana. Mama G alimpenda Nanaa, hakuwahi kumuonyesha ubaya mpaka kwenye tukio la ubakwaji wake. Tokea anahamia kwao, mpaka anamuita amsaidie maswala ya Liv wakati amezaliwa na yeye ana mitihani, mama G amekuwa upande wake tu bila unafiki ila upendo usio na hila. Mpaka Malii alipoingiza roho chafu sana siku ile usiku. Roho chafu iliyomwingia kila mmoja wao aliyekuwepo pale, nakuwaacha hawajitambui ila kusambaratika vibaya sana.

~~~~~~~~~~~~~

Bado James hakuwa amemtafuta Nanaa, huo ulikuwa mwezi wa sita tayari wanatafuta wa saba kitu ambacho si kawaida yao. James hakuwahi kuacha kumtafuta Nanaa tokea analetwa nyumbani kwao ni kachanga kabisa.

Haya, alivunja ndoa na mahusiano ambayo hayakutegemea kuvunjika kamwe. Grace na Danny. Ndoa yao haikuwa ya ajabu sana. Kulikuwa na mapungufu yao, lakini ni kama kila mmoja wao alishajiamulia ni mpaka kifo. Hata Grace hakuwa hata na wazo la kumuacha Danny japo alimuona na mapungufu mengi aliyoyajua yeye. Japokuwa alijua kuna mambo fulani watu hufanya kwenye mapenzi, Danny hakuta kuyafanya kwa kinyaa akishangaa ni kwa nini watu wawe wanafanya mambo kama hayo, akiona ni uchafu, Grace ambaye hakuwahi kufanyiwa hivyo maishani, akakubaliana na mumewe, ndoa ikaendelea bila shida. Mpaka alipokuja Malii na kumwaga hiyo roho chafu, iliingilia hiyo ndoa yao pia. Ilivunjika hata usingeweza amini kama ni wale ambao walipenda kukaa pamoja kila wakati.

Hiyo roho chafu ilipenya mpaka nafsini kwa Danny kiasi cha kumfanya kutilia mashaka kila kitu. Yale mazuri yote aliyokuwa akijisifia kwa watu juu ya mkewe, ndiyo hayo hayo akayatumia kumchafua nayo.

Upande wa kuvunjika urafiki na wema wa Nanaa wote ukaweza kusahaulika kwa usiku mmoja tu ambao Malii alitoa siri ya kuwa alishamvulia nguo. Ilikuwa ni kama neno la ajabu sana. Likatiwa nguvu ya ufitini, ubaya uliopita kiasi, uuwaji ndipo hiyo roho ikamwingia na mama G, na kumtibua nafsi yake kupita kawaida na kumchukia Nanaa kupita kiasi. Hata akaamua kumtafutia mwanae, mwanamke mwingine ambaye hata hakumchunguza. Akaamua kumuunganisha na Geb, aliyezaa na Nanaa ambaye alikuwa akimpenda na kumpongeza kwa kumzalia wajukuu wawili. Alisahau kabisa maneno yake yeye mwenyewe. Alipomkaripia Geb na kumwambia mwanae kwa kinywa chake mwenyewe kuwa, hakuna mwanamke mwingine atakayekuja kuishi naye mle ndani isipokuwa Nanaa. Yote hayo mama G aliyasahau, akamkimbia Nanaa.

Haikumuacha salama na Nanaa mwenyewe aliyetendwa ubaya. Baada ya yote hayo, Nanaa akamchukia kabisa mama G. Akasahau yooote ambayo alishawahi kumtendea. Akabakiwa na kosa la kumnyang’anya watoto na kumtafutia Geb mke. Gafla yeye ndio akawa ameshika makali. Mama G akaachwa kwenye nyumba peke yake. Bila Geb, wala wajukuu ila lawama pande zote.

Grace akimlaumu kwa kumtafutia mumewe mke. Danny akimlaumu kwa kupokonya watoto wa Nanaa. Japokuwa Geb hakumwambia mama yake, ila alijua wazi na yeye anayo malalamiko yake juu yake. Akajua mpaka muda huo anajua kwamba alificha barua ya Nanaa. Na japokuwa hakurudia kuzungumzia tena wala kumlaumu tena ila alishamwambia anajua alikuwa akizuia Nanaa asishike wanae. Geb alizungumzi mara moja tu, hakurudia tena kulaumu.

Hata watoto hawakuachwa salama. Mahusiano ya watoto wa Grace na mama yao yalivunjwa kiajabu sana. Urafiki wa Fili na Liv ulivunjika pia. Hawakuwa wakionana tena. Na hata walipokuwa wakikutanishwa, Liv anakuwa akimlilia mama yake, hawezi hata kumtizama Fili. Ikajengeka chuki kwa Liv hakuwa akimtaka tena bibi aliyekuwa akimlea kwa upendo sana, sababu alimchapa akiwa amechoka na kuwaona wanaishi nao bila mama yao ambaye wakati wote walipokuwa wakikutanishwa, waliachana na mama yao akiwa analia. Moja kwa moja Liv akajua wao ndio wanahusika na kumtenganisha na mama yao. Akawachukia mpaka baba mtu alipomrudisha kwa mama yake, hapo urafiki ukarudi. Magesa naye ameshaonja mikono ya mama yake, akajua utamu wa mikono ya mama, gafla akamkataa bibi yake aliyemlea toka anazaliwa. Ikawa mahusiano ambayo hayakuwahi kufikiriwa kuvunjika, yakavunjwa kwa dhambi moja tu iliyoingia kati kati yao.

~~~~~~~~~~~~~

Jioni hiyo Geb akarudi, akamkuta Nanaa amepooza tofauti na utani waliokuwa wakitaniana asubuhi kwenye simu. Akaanza kuwaza ni nini amekosea tena! Ahadi ya kuja kuambiwa kama anapendwa tena, mbona imegeuka kuwa huzuni! Geb akaanza kujiwinda kila anachoongea ili asiharibu zaidi. Alichelewa kidogo kutoka kazini. Akafika watoto ndio wanaandaliwa kwenda kulala. Akasaidia kwa juhudi zote huku akimsihi apumzike.

          “Leo nimechelewa kidogo, kulikuwa kuna kitu narekebisha. Nilitaka kusimamia mimi mwenyewe ili nihakikishe wanamaliza.” “Pole.” Nanaa akajibu kifupi wakiwa wamebaki wao wawili tu hapo chumbani. “Inabidi uanze kutembelea miradi yote Nanaa. Ili ujue ni nini tunamiliki. Kwa mfano leo nilikuwa kwenye ile bohari kubwa, nikisimamia ukarabati. Hasa umeme. Niliona bili imeongezeka. Kumbe ni nyaya tu ndio zimechakaa. Nikaamua kupaweka nyaya mpya, ili nione kama kutakuwa na mabadiliko yeyote.” Geb aliendelea kujiongelesha huku amejilaza kwenye mto, Nanaa amejiegemeza kwenye kitanda akimchezea nywele.

“Sijui hata kama amesikia nilivyosema miradi yetu! Yaani na  yeye nimemuweka.” Geb akawaza wakati akimwangalia Nanaa, alipokuwa akipitisha kidole kwenye nyusi zake nyingi huku akifikiria. Alionekana kuna jambo anafikiria.

“Nanaa!” “Pole sana.” “Acha kunidanganya bwana. Wala ulikuwa hunisikilizi.” Nanaa akaanza kucheka. “Unawaza nini?” Nanaa akatulia. “Eti mpenzi wangu?” Gafla akamuona machozi yanatoka akajifuta. “Vipi? Ni nini nimekosea?” “Hivi unajua karibia watoto wangu wote ni mama yako ndio amenisaidia tokea wanazaliwa?” Geb akanyamaza asijue anapoelekea. “Nakumbuka alivyonisaidia kipindi cha Liv. Leo nimekumbuka vile nilivyokuwa nikiogopa na nilikuwa sina msaada, akaja kunisaidia mpaka nikamaliza mitihani. Unajua alikuwa halali anahangaika na Liv tu! Mpaka nilikuwa nikimuhurumia. Asubuhi na mapema alikuwa anakuja kukaa na sisi mpaka usiku.” Nanaa akaendelea kuongea.

“Unakumbuka uliponifukuza ukanifungia nje? Nilikuwa nimejaa damu. Mama akanisafisha tena bila kinyaa! Alinilea vizuri sana. Aliishi na mimi kwa upendo sana.” Nanaa akaendelea. “Unakumbuka kipindi alipozaliwa Magesa vile alivyokuwa akinipongeza kwa kumzalia Magesa? Akamlea mtoto wangu mimi nikiwa mgonjwa. Akawa ananiletea wanangu asubuhi na jioni bila kuchoka.” Geb kimya. Aliogopa hata kupenyeza neno asije kuharibu.

“Sijui alipatwa na nini!? Akanigeuka kwa kosa lakutomwambia kama eti nilimvulia nguo Malii! Ni kama mtu aliyekuwa akinitafutia sababu yakunifukuza.” Hapo Geb akaanza kuona anataka kurudi kwenye mabaya. Akatamani akumbuke kitu kingine kizuri. “Lakini Geb, kila nikifikiria maisha yangu na mama. Vile tulivyoishi naye kwa upendo. Ni kama alikuwa zaidi ya rafiki. Tulikuwa tukicheka kila tukionana. Unakumbuka vile alivyokuwa akihangaika kuleta vyakula kule hospitalini hata kabla sijajifungua?” Nanaa akauliza tena.

“Wewe hukumbuki?” Kimya. “Au ni mimi tu kwa kuwa nimemmiss?” Alivyosikia tu hivyo akadakia. “Nakumbuka sana. Nakumbuka.” Nanaa akazidi kulia. “Nina hamu naye, japo ameniudhi sana.” Geb akatamani kumwambia amtafute lakini akaona ni heri anyamaze kwanza. “Na ninachoogopa ni kumkaribisha sasa hivi tena kwenye maisha yangu. Alinipokonya wanangu. Asije kurudia tena. Nahisi kwa kuwa aliwalea tokea wanazaliwa ndio anaona ana amri nao. Hapana. Heri kumuacha tu. Nyinyi endeleeni na maisha yenu, mimi niendelee na wanangu.” Mpaka hapo ombi la ndoa likawa gumu. Mwisho haukuwa mzuri hata kidogo.

“Naomba utulie Nanaa. Mimi nipo hapa na wewe. Na nilikwambia nilishagundua kosa langu. Nikashindwa kusimama kwenye nafasi yangu kama baba na mume kwako. Siwezi kuruhusu hilo litokee tena. Kwanza kwa faida ya wanangu. Siwezi kuondoa hiyo furaha ninayoiona kwa sasa hivi. Sithubutu. Nitakuwa nawakatili mno. Kwa garama yeyote ile, nimejiapia kuwapa wanangu hiyo furaha. Pili, nimekusudia kusimama na wewe Nanaa. Jua litoke, mvua inyeshe. Nimekuchagua wewe Nanaa, kwa kuwa nakutaka wewe. Sina maisha bila wewe.” Nanaa akajisikia vibaya sana. Akaona vile Geb alivyojitoa kwake.

“Asante Geb. Kweli umeamua kuwa na mimi. Nimeona mpenzi wangu. Nakushukuru.” Geb akajiweka sawa. “Uliniambia nikija utaniambia kitu.” Nanaa akacheka na kufuta machozi. “Nilitaka kukwambia na mimi nakupenda Geb. Na ninakushukuru kuacha kila kitu kuwa na mimi hapa kwenye kipindi hichi kigumu. Unanifariji. Unaniombea. Na usiku ninapo ogopa au kuwa na ndoto mbaya, unakuwa na mimi unanisubiri mpaka nilale. Na nimeona hata ndoto mbaya zimeanza kuisha. Siku hizi naweza kulala mpaka asubuhi na naona Jimmy alikuelewa. Amebadili muda wa kucheza.” “Anamsikiliza baba yake je! Jimmy atakuwa mtoto mzuri sana. Msikivu, naona kuliko wote.” Nanaa hakuamini.

          Unamtambua Jimmy kama mtoto wako!?” “Kama nakutambua wewe kama mke wangu, sasa Jimmy atakuwa nani? Tutamlea kama Liv na Magesa. Hapatakuwa na tofauti. Au madaraja kwao. Kile Mungu atakachotujalia, ndicho tutakachompa.” “Nakushukuru Geb. Umenitia shauku ya kujifungua salama, tuje kulea wote hawa watoto. Lakini…” Nanaa akasita.

“Lakini nini?” Geb akauliza. “Itakuaje kama nikifa wakati najifungua?”  “Nitafanya kile utakachotaka nifanye na huyo mtoto. Ukinipa nimlee kama Magesa, ujue nitafanya hivyo. Chochote kile, mimi nitafanya. Lakini nimezungumza na Mungu wangu, nimemuomba akupe miaka mingi sana. Uje unizike mimi na si vinginevyo.” Nanaa alilia sana.

“Nakupenda Geb. Na asante kwa upendo wako.” “Kama kweli unanipenda Nanaa, kwa nini hutaki tuhalalishe ndoa yetu?” “Sio kwamba sitaki. Kuna mambo mengi yalikuwa yakinifanya nisite. Kubwa umeshalijibu sasa hivi.” “Juu ya Jimmy?” “Ndiyo. Unafikiri ningeleaje watoto wa baba wawili sehemu moja? Kama wewe huna shida ya huyu mtoto kulelewa hapa, angalau imenipunguzia mzigo.” Geb akambusu.

“Naomba unyamaze kulia, kisha uniambie kikwazo kingine.” Nanaa akatulia. “Familia yako?” Nanaa akajibu. “Imefanyaje?” “Bado sitaki kuwa nao karibu.” Geb akanyamaza. “Hilo ndilo tatizo. Najua unataka ndugu zako, na mimi siwataki.” “Hilo sitaki kuliingilia Nanaa. Nakuachia wewe. Ila nataka ujue, wakati baba anakufa, aliniomba rasmi nimtunzie mkewe na Grace. Ni ombi ambalo alinisisitiza sana. Tena akiniambia nisisahau kama mama ni yatima. Mimi ndio niwe ndugu ambaye awe na uhakika hatapoteza. Ndio maana nilifurahi sana kuona nyinyi wawili mnaelewana na mnapendana. Nikajua haitaniwia ngumu kuwa na nyinyi wote. Ndio maana nilikuomba tokea mwanzoni kama tunaweza kuishi na mama.” Geb akaendelea.

“Lakini Nanaa, mimi ndiye niliharibu. Namjua mama. Najua udhaifu wake wa kupaniki kipindi cha matatizo. Nafikiri hata wewe nilikwambia. Sio mtu wakumtegemea kutoa maamuzi yenye hekima kukiwa kuna tatizo kubwa. Siku ile asubuhi wakati tunaondoka na watoto, nilikuwa na hasira sana. Sikujua hata kama alikutamkia maneno mabaya. Ni kweli nilikusudia kuondoka na watoto. Lakini uwe unaletewa jioni na asubuhi. Mbaya zaidi sikufuatilia utekelezwaji wa hilo, sababu ya kujitupia kazini ili kujaribu kupunguza hasira. Sikutaka hata kuwa na watoto karibu ili wasinione vile nilivyokuwa nimekasirika.” Geb akaendelea kwa makini asije kuharibu.

“Nikamuachia mama majukumu yote ya watoto. Majuzi nilienda kumuuliza mama kwa nini alimpa maagizo Jeri asikukubalie watoto au hata asiruhusu wewe ushike watoto, akatuambia mimi na Grace. Tena Grace aliumia sana. Mama akasema alikuwa na nia nzuri. Malii ni Malaya sana. Halafu ulikuwa ukinyonyesha watoto wote wawili. Akasema aliingiwa na hofu, pengine ungekuwa amekuambukiza magonjwa ambayo jamii ilikuwa ikisema Malii anayo, halafu na wewe ukaambukiza watoto. Kwa kuwa ni kweli Malii alishatembea na mama mmoja ambaye alikuja kufa kwa UKIMWI. Akaona ni heri tuje kumlaumu yeye lakini aokoe watoto.” Nanaa akalia sana. Geb akamvuta nakumlaza vizuri, akamkumbatia. 

“Naomba tulale Nanaa. Inatosha kwa leo. Mambo mengine hayana majibu kwa haraka. Naomba tumuachie Mungu” Geb akaona asiibue mengine. “Tuombe.” Geb akaanza kuomba. Akamuombea Nanaa hekima na afya nje. Akamuombea utulivu, furaha na usingizi mzuri. Akazungumza kidogo na Jimmy. Wakalala.

~~~~~~~~~~~~~

Geb aliinua hukumu moyoni kwa Nanaa. Inamaana mpaka hapo ni yeye tu ndiye amebeba majibu ya mambo mengi sana. Kujenga familia hiyo ya Magesa. Anajenga na nani na nani anamuacha? Akubali kuingia kwenye ndoa wakati haelewani na mama G, ambaye ndio kiungo kikubwa sana cha hiyo familia? Ni kweli alimudhi sana. Kitendo cha kumnyang’anya watoto wake na kumtafutia Geb mke! Nanaa alishindwa kusamehe. Hata kama alipata sababu nzuri na ya msingi ya kumnyang’anya watoto na kumkataza asinyonyese wanae, lakini si kwa matusi makali vile, na si kwa kumtafutia mwanae mke. Nanaa alizidi kupata sababu yakumchukia yule mama.

Lakini katika muda wote alioishi na yule mama, alihisi upendo mkubwa sana. Zile kumbukumbu za mambo yule mama aliyokuwa akimtendea, zikaanza kumrudia. Zilikuwa zikija moja hadi nyingine huku zikimuonyesha yule mama hakuwa na sababu yakufanya hivyo. Lakini alifanya hata pale Geb alipomuonyesha yupo kinyume naye, lakini mama yake alisimama kumtetea yeye, Nanaa. Japokuwa alikuwa akiendelea kujipa sababu ya kumchukia, lakini wema ukazidi ubaya.

~~~~~~~~~~~~~

Asubuhi siku ya jumamosi ambayo Geb aliahidi hatakwenda kazini, alikuwepo tu hapo na familia yake. Tokea asubuhi anazunguka na Nanaa humo ndani. Wameacha gorofa, wanaishi kwenye apartment ya vyumba viwili tu, na watoto wao. Liv aliamka akitaka kumfundisha kaka yake kujenga nyumba kwa matofali ya mbao. Mchezo aliokuwa amenunuliwa na baba yake. Magesa hakuwa na huo muda. Alitaka kuzunguka na kufanya shuguli nyingi kwa wakati mmoja. Nanaa alimwambia Geb, wanyamaze waone mwisho wake.

Liv alihangaika naye, mpaka akachoka. Kila alivyojenga kabla yakufika mwisho, Magesa alipiga ngumi nakucheka sana. Nyumba nzima ilikuwa ikianguka kitu ambacho kilikuwa kikimsababisha Liv, aanze upya kila mara. Mwishowe akamvuta mpaka kwa mama yake. “Kaa hapa, usije tena kule.” Geb na Nanaa wakacheka. “Mwanao kafukuzwa. Nilikwambia Liv hapendi shuguli nyingi. Anataka akianza jambo lake moja, amalize. Kama Grace.” “Njoo mwaya mwanangu. Magesa wangu yeye anataka kucheza sio mambo ya msingi.” Magesa akawa anamchekea mama yake huku anamfuata.

“Yuko wapi Fili?” Liv akamkumbuka rafiki yake kipenzi. “Unamtaka Fili?” “Magesa anaharibu. Namtaka Fili.” “Basi ngoja nimpigie mama yake Fili tumuombe Fili aje acheze na Liv. Wakikubali, Dad ataenda kumchukua. Sawa?” “Nampenda mama.” “Hata mimi nampenda Liv wangu.” Liv akacheka akawa anasubiria mama yake apige simu. Geb akataka kumkataza, lakini Nanaa alishanyanyua simu na kupiga wakati Liv anachekacheka mbele ya mama yake, akisubiria. Geb akanyamaza.

Kuliko Ungua Mpini.

“Simu ya Grace imezimwa.” Nanaa akaongea. “Amekataa?” Liv akauliza kwa masikitiko. “Hapana Liv. Subiri.” Akampigia simu Danny bila kusema anapiga wapi.

Geb akabaki kimya anawaangalia. “Halow! Ni mimi Nanaa.” “Upo? Habari za siku?” Danny akauliza. “Nzuri kabisa. Vipi wewe na familia?” “Mimi maisha yangu na wanangu yanaendelea vizuri. Mungu amenipumzisha na kina Magesa.” Nanaa akashangaa. “Unamaanisha nini!?” “Kwani hujasikia?” “Juu ya nini?” Nanaa akahoji. “Unajua yale mangurue pori?” Nanaa hakuwa ameelewa. “Yanakuwa manene meusi hivi. Basi nimeamua kuachana na ngurue pori na ukoo wake wote. Wachawi, roho zao mbaya kuliko shetani. Unakumbuka walichokufanya?” Nanaa alikuwa bado hajaelewa.

“Sasa walipokufukuza wewe tu na kukupokonya watoto, na mimi nikawageukia. Nilichukia sana walivyokunyanyasa wewe mtoto yatima. Kama walivyokupokonya watoto wako, na mimi nilihakikisha nimewapokonya watoto. Sitaki hata Magesa mmoja ashike mtoto wangu.” Danny aliongea maneno mengi machafu akimtukana Grace.

Nanaa aliona machozi yanamwagika. “Dude zito kama gunia! Linakuweka roho juujuu kila wakati lisije likalalwa na wanaume wengine likakuu kwa magonjwa! Unakazi ya kulilinda tu! Watu wanataka kulivua nguo kuliangalia kuna nini ndani, kumbe hamna kitu. Bure kabisa. Maji matupu.” “Danny! Danny!” Nanaa alimwita huku akilia. “Nimejitafutia kasichana kazuri. Nalala bila presha. Unanyanyua popote. Una..” “DANNY!” Nanaa akaita kwa ukali.

“Subiri kwanza. Hapo unamuongelea Grace!? Nanaa akauliza kwa upole huku akilia taratibu. “Kumbe nani? Majitu makatili kuliko shetani. Hapa nimeshatayarisha hati zangu za talaka. Amekimbia nyumba. Namsaka. Nikimpata tu, nataka aweke saini nioe, mtoto mchangaa.” Nanaa aliumia sana.

“Kweli Danny? Matatizo yangu na Geb yamekufanya umesahau alipokutoa Grace wewe? Leo unamtukana hivyo!” “Sasa ngoja nikwambie ukweli wote, Nanaa. Grace alinifuata yeye mwenyewe kwa kuwa alitumwa na familia yake wanichukue mimi kuniweka kama kafara yao. Waligundua nyota yangu ipo juu, ndio maana walitaka kuniweka kwenye maisha yao ili wanitumie kujipatia utajiri. Ndio maana mara tu baada yakumkubalia Grace kurudi naye huku Dar kutoka Tabora, mama yake akahakikisha namuoa kwa haraka.” Nanaa aliendelea kusikiliza.

“Na ukipiga mahesabu, ni baada ya kuniingiza tu kwao. Mimi kuingia kwenye agano na Grace, ndio pacha wake akaanza kufanikiwa. Kama ukichunguza vizuri, ni wao tu wawili ndio wanamiliki kampuni ambayo hatetereki hapa nchini. Hata uchumi uwe mgumu vipi, wao wanafanikiwa tu. Hata umwambie Grace kuna ofisi itamchukua kwa mshahara watakao mlipa mara mbili wa anaolipwa na kaka yake, hakubali. Anataka tu kufanya hapo hapo kwenye hiyo kampuni. Geb anafanikiwa, kwa agano la mimi nililoweka na Grace. Grace na Geb wanashiriki nyota. Kwa hiyo agano nililoweka mimi ni kama nimeweka na Geb pia. Wote wananufaika kwa kupitia mimi. Nimeambiwa ndio maana wananiweka karibu. Ndio maana hawataki kunikorofisha. Unaambiwa nikiondoka kwenye maisha yao hao, hawana kitu.” Nanaa alikuwa haamini anachoongea Danny.

“Sasa unaambiwa mambo hayo alianza mama yao. Mama yao ni mshirikina sana. Alitukusanya watoto wengi sana. Tukawa tunakuja hapo kwao. Geb anajidai sisi ni marafiki zake, kumbe anatafuta janja yakutuweka karibu na mama yake atusome nyota. Alipoona nyota yangu inafaa kuliko vijana wengine wote, ndio wakaanza kunilisha mambo ya ajabu. Ndio kisa cha mimi kuwa kama nimechanganyikiwa kwa Grace. Usifikiri yalikuwa mapenzi yale! Unaambiwa walinichezea sana. Ndio nikawa kama nimechanganyikiwa. Namtaka Grace tu. Kumbe ni madawa waliyokuwa wamenilisha  yakunifanya nioe kwao, wachume pesa. Mimi ndio nawaletea utajiri.” Danny akaendelea.

“Sasa vijana wote wameshawajua tabia zao hao. Wakawa wanatafuta jinsi yakuniokoa mimi na wewe. Malii alipokuja siku ile alituambia kwa kiasi. Lakini aliponitoa pale ndani akaenda kunitupa njiani, alinieleza kila kitu kwa kina. Ndio nikawekwa sawa na wenzangu mtaani. Sasa walipoona mimi nawakimbia, si ndio wakamtafuta sasa mwanamke mwingine mwenye nyota kali. Mama yao akamtafutia Geb mwanamke ili amuoe, ili hata mimi nikimuacha Grace, wapate nyota ya mtu mwingine. Lakini ujue hapo ni baada ya kuhangaika sana na mimi kutaka kunirudisha kwenye familia yao, nakuona nimewagundua. Nakwambia niliwaambia machoni hivi. Wakashindwa hata kubisha. Wakabaki kimya kabisa.” Danny aliendelea kuzungumza kijasiri.

“Mimi ndiye niliyemshitua Sara, mwanamke waliyekuwa wamemtafutia Geb. Ili wamtoe na yeye tambiko. Hapa ninapokwambia nipo naishi na Sara. Mapenzi ya ukweli. Nimetulia, sio kama nilivyokuwa na Grace. Yaani najisikia nipo mimi kama Danny wa miaka iliyopita. Nimepandishwa cheo kazini. Maisha yangu mimi na Sara yapo raha mstarehe. Ila nimeapa kumsaka Grace mchana na usiku, kutoa kiapo changu kwenye maisha yake. Nimetangaza kuvunja agano nao. Huko sirudi tena. Kwa hiyo Nanaa, shukuru Mungu aliyekutoa mapema. Ila ombea wanao. Nasikia wanatoa watoto wao pia kafara. Jaribu kujiiba hata ukaone wanao. Vimebaki mifupa mitupu, na wote wapo wanawaangalia bila huruma. Kumbe watoto wapo kwenye dawa kuwaletea pesa. Nimepiga marufuku wasiwasogelee wanangu kabisaaa.” Daany akawa ameshika kasi.

“Mimi sijui kilichokupata Danny. Lakini hivi tunavyozungumza nipo na wanangu hapa. Naishi na watoto wangu na Geb. Na Mungu akipenda tutafunga ndoa.” “Mungu wangu Nanaa! Hao watu wamekuloga!” Danny akashituka sana. “Danny! Ni nini kimekupata wewe!?” Nanaa alikuwa haamini. “Kama unafikiri mimi nimechanganyikiwa, kwa nini hushangai kuwa kwa nini bado Geb anataka kufunga ndoa na wewe? Geb ni mkororfi sana. Hawezi kukubali akuoe baada yakubakwa na Malii. Kuna jambo ambalo ananufaika na wewe. Ukute ni hao watoto aliowatoa kafara pia. Ameona walikuwa wanakaribia kufa, ndio amekurudisha, umsaidie kuwalea hao watoto ili wazidi kuwaletea pesa kwenye familia yao” Danny akasisitiza.

“Naomba kuongea neno la mwisho Danny. Maana nimejua hakuna jinsi nikabadilisha unachoamini sasa. Ila ujue kabisa, Grace alikua mkeo. Na iwe kwa hila au la, mliingia agano mbele ya Mungu. Wakati wote Mungu anaangalia agano lake ili alitimize.” “Agano lenyewe…” “Subiri kwanza Danny. Mimi nimekusikiliza tokea mwanzo mpaka mwisho. Naomba nisikilize na mimi.” “Sawa.” Danny akakubali.

“Mungu anaangalia agano lake, na hatakubali mtu yeyote yule asimame kwenye agano aliloahidi ataweka mkono wake. Kuwa sana makini. Ndoa yako na Grace ni ya kanisani. Mimi nakujua kwa sehemu Danny. Ila nimekujua ukiwa na hasira, huwa huna uwezo wakufikiri kabisa kaka yangu.” “Unanivunjia heshima Nanaa.” “Hapana Danny. Naomba unisikilize. Nimekusikiliza muda wote ukitukana viungo vya kike vya Grace, ukumbuke na mimi ni mwanamke. Natokwa damu na maji kama Grace. Kuna siku nakuwa na joto na kuna siku nakuwa baridi kama Grace. Uliza wataalamu wa afya watakufundisha juu ya joto  la mwili wa mwanamke utaelewa au mzunguko wa mwili wa mwanamke. Nimevumilia kukusikiliza mpaka ukamaliza. Naomba na mimi nisikilize.” Nanaa akasisitiza.

“Mbona naishi na Sara hayupo hivyo?” “Unajidanganya Danny. Unaongelea Sara mtoto wa mjini huyo!? Mtoto ambaye hajui hata kusukuma mtoto mmoja leba! Mtoto ambae kama amefanikiwa kubeba mtoto akakaa tumboni kwake si zaidi ya miezi miwili, akamtoa. Unamlinganisha na Grace aliyekuzalia watoto watatu! Anawanyonyesha mpaka wamefika hapo unaponiambia umewapokonya na kuzurula nao! Amewafundisha kujisaidia na kukaa! Unamlinganisha na Sara ambaye anaweka madawa huko kwenye uchi ili kila mwanaume anayelala naye amtoe bikra iliyokwisha tolewa tokea yupo mtoto!” Nanaa alishachukia.

“Sio Sara.” Danny akapinga. “Humfahamu Sara kama ninavyomfahamu mimi, Danny. Mimi nilikuwa napewa habari zake na mtu aliyekuwa karibu naye na aliyekuwa akimuona akinunua hizo dawa za shabuu ili kuziweka huko kwenye sehemu za kike ili kufunge. Niambie tu ukweli Danny, hukumtoa bikra Sara?” Nanaa akauliza. “Mbona hata na Grace nilimtoa?” “Sijui juu ya Grace, ila mimi ninauhakika na bikra uliyotoa ya Sara.” Nanaa akajisahau hata kama Geb yupo pale. Aliongea kwa machungu sana.

“Bikra ya Sara sio yenyewe, Danny. Anaziweka kutokana na anayetaka kumfurahisha. Hata uliyotoa wewe ni yakuweka. Tena nina uhakika alikuwekea baada ya kufukuzwa kwa kina Magesa. Kwa kuwa aliyokuwa amemuwekea Geb, alikuwa akilalamika mbele ya huyo mtu kuwa Geb anamchelewesha kumtoa ili aendelee na maisha yake. Alipoona Geb haitoi, na wanaume zake wanamsumbua, akaenda kutolewa na mwanaume mwingine, ili aendelee na wanaume zake mtaani. Hapo kabla hata hajafukuzwa kwa kina Geb au hata hajaja kwenu.” Nanaa akaongea kwa hasira.

“Huyo anayekuletea habari za Sara, ni muongo.” Danny akapinga. “Sawa Danny. Lakini nakwambia kabisa, Sara atakuua kwa magonjwa. Sio muhuni. Huyo msichana ni Malaya wakutafuta wanaume walale naye.” “Huna utakachoniambia juu ya Sara nikaamini. Sara amekuwa baraka kwangu. Maisha yangu yamebadilika. Ninapesa. Tena yakulipwa kwa jasho langu. Na hayo yote hayo nimeyapata baada ya kuachana tu na Grace.” Nanaa hakuamini.

          “Danny wewe! Umepatwa na nini!? Hivi hujui kuwa sasa hivi wewe na Sara, mnakula matunda ya Grace!? Mnavuna alikopanda Grace! Hakika Mungu hatawaacha Danny. Ipo laana ya mke. Itakushika tu.” “Kwanza ujue Grace sikumuoa kwa akili yangu. Kwa hiyo hakuna agano kati yangu na Grace. Pili, wewe ni mtoto sana kwangu Nanaa. Nayajua maisha kuliko wewe. Namjua Mungu kwa kulelewa kanisani. Najua mambo ya mjini kuliko wewe kwa kuwa wakati wewe uko migombani unabadilishwa nguo, wenzio tulikuwa tumeshafika mjini.” “Sawa Danny kaka yangu. Na samahani pale nilipokuvunjia heshima.” Simu ikakatwa.

~~~~~~~~~~~~~

Nanaa alikuwa kwenye mshituko akabaki ameduaa. Akagundua Liv alishaondoka pale mbele yake yupo chumbani anacheza na mdogo wake. Geb ametulia pale pembeni yake kwenye kochi ameinamia simu yake. Nanaa akamtizama. “Wewe Geb!” Geb akamtizama. “Wewe unajua haya yote?” “Nafahamu Nanaa. Najua kila neno alilokwambia. Tena kutoka kwa Danny mwenyewe. Nilimfuata kujaribu kuzungumza naye juu ya familia yake. Hatima yake na Grace. Tena baada ya Grace kuondoka.” “Subiri kwanza Geb.” Nanaa akawa ameshachanganywa.

Ndipo Geb ikabidi na yeye amuelezee kila kitu. “Danny amemtukana dada yangu, mbele ya macho yangu! Huo uchafu anaokwambia juu ya Grace, ameniambia na mimi. Bila hofu, wala aibu, au huruma. Anamchafua Grace na sisi huko mtaani! Hakuna tulichobakiza Nanaa. Mama ndio anaitwa mchawi. Na hivi amebaki peke yake, utamuhurumia. Vijana wote wanamsema vibaya. Wale wote waliokuwa wakija kula na kunywa pale nyumbani, wanamtishia kumfanyia mambo mabaya. Wanasema kuwa alikuwa akiwaroga walipokuwa wakija pale ili mimi nifanikiwe. Wanasema mama ameiba nyota zao wote, amenitengenezea mimi ili nitajirike. Na ndio maana nimefanikiwa kuliko wote.” Nanaa akaumia sana.

“Kwa hofu ya kuja kumdhuru mama, kuanzia jumatatu nimeamua kumfungia ndani na kuongeza ulinzi. Kuna waliokuwa wamemfuata na wake zao na watoto kule kazini kwake, wanaomba wawafungue watoto wao.” “Kivipi!?” Nanaa akauliza huku akilia kwa uchungu sana. “Si unajua waliokuwa wameoa, kila walipokuwa wakijifungua mama alikuwa akiwahudumia wake zao na watoto? Tokea wanazaliwa mpaka sasa. Sasa wake zao wanakuja kusema sijui mama aliiba vitomvu vya watoto wao.” “Mungu wangu Geb!” Nanaa alizidi kusikitika.

“Kama vile alivyokuwa akisafisha kitomvu cha Liv wakati mchanga?” Nanaa akauliza. “Ehee! Sasa wanasema kila vile vitomvu vilipokuwa vikianguka, mama alikuwa akiviiba, anaficha ili aje afanyie uchawi. Ilikuwa ugomvi mkubwa. Wale wanawake wanamtukana mama, kama hawamfahamu! Ndio mfanyakazi mmoja wa mama akanipigia simu. Ikabidi kukimbia kwenda. Kufika nikakuta mama anahali mbaya. Wamemzunguka. Wanamdai vitomvu vya watoto wao. Na mambo mengi sana. Niliumia Nanaa! Niliumia sana.” “Pole Geb.” Nanaa alizidi kuumia. 

          “Sasa ukafanyaje?”“Sikusema kitu Nanaa. Nilimchukua mama na kumrudisha nyumbani. Alikuwa kwenye hali mbaya sana. Nikakaa naye mpaka jioni niliporudi hapa.” “Kwa nini hukuniambia Geb?” “Nikwambie nini Nanaa kwa yote tuliyokufanyia? Mama anaamini anastahili hayo yote kwa aliyokufanyia. Unakumbuka ulipowaambia umewaacha juu ya madhabahu ya bwana?” “Ni hasira tu Geb!” “Basi mwenzio anaamini ndivyo Mungu anavyomlipa kwa mabaya aliyokutendea.” “Hapana Geb. Mimi niliongea kwa hasira tu.” Nanaa akazidi kuumia.

“Sasa Grace anasemaje?” Nanaa akazidi kuhoji. “Aliamua kwenda kupumzika. Alishindwa. Alijitahidi kuvumilia, akiomba na kujaribu kubaki na watoto, lakini kama ulivyomsikia Danny. Alikuwa akisema Grace anamtaka warudiane kwa ajili ya kuendelea kumfanyia mambo ya kishirikina. Grace alituambia walikuwa wakifanya mapenzi na Sara kwa sauti kama kumuumiza.” “Mungu wa mbinguni Geb! Ni nini kinatokea?” Nanaa hakuamini.

“Sasa mbona sijampata Grace kwenye simu?” “Alizima simu yake kabisa. Amechoshwa na picha za Danny na Sara alizokuwa akitumiwa na watu. Wengine walijidai wanakosea namba. Lakini ilikuwa makusudi tu kumfikishia ujumbe wa matusi yaliyosambaa mtaani kutoka kwa Danny.” “Pole mpenzi wangu. Poleni sana.” “Nashukuru Nanaa. Ila najua Mungu ataturehemu tu. Tulipokosa, atatusamehe. Yataisha siku moja.” Nanaa akabaki amenyamaza kama aliyepigwa na bumbuazi.

~~~~~~~~~~~~~

          Muda wote Geb amekuwa akirudi nyumbani akionekana ametulia bila kumuonyesha Nanaa kile kinachoendelea. Alimchukulia kwa upendo, kumbe anakabiliwa na matatizo makubwa sana. Alibaki Nanaa akiwaza. Akakumbuka usiku uliopita jinsi alivyomwambia Geb juu ya ndugu zake kuwa hawataki kuwa nao karibu. Akamuhurumia Geb. Katika yote hayo, bado amemchagua yeye! Anakuja nyumbani kwa wakati. Anajitahidi kuwa naye bila kulalamika! Amemuonyesha upendo wa ajabu sana. Amempokea yeye na mtoto wake! Nanaa alizidi kuumia akihukumiwa.

~~~~~~~~~~~~~

“Kwa hiyo mama yupo peke yake?” Nanaa akauliza kwa uchungu sana. “Awe na nani tena? Grace aliondoka akiwa anamlaumu kuwa amemtafutia mumewe mke. Mimi nipo hapa na familia yangu. Sasa unafikiri anabaki na nani? Halafu naogopa Nanaa. Kwa fujo walizomfanyia kazini kwake, siwezi hata kuruhusu mtu afike pale nyumbani. Nimeongeza ulinzi. Nimemwambia asitoke pale. Maana wanaweza kuwa wanamuwinda nje. Nataka asubiri kwanza kwa muda mpaka patulie.” “Kweli Geb unanipenda! Umekubali kuwa hapa na mimi ukamuacha mama yako peke yake!” Nanaa akazidi kuumia. Geb akanyamaza.

“Mimi nimesamehe Geb. Nimesamehe kabisa mpenzi wangu. Niambie jinsi yeyote unayotaka nikusaidi katika hili. Nimechagua kusimama na wewe kama vile wewe ulivyosimama na mimi.” “Nakushukuru Nanaa. Lakini narudisha ombi langu lile lile. Naomba urudie tena kujenga nyumba yetu. Sio jengo. Maana hata wewe umekuwa shahidi. Tumeacha nyumba kubwa ya thamani. Tena iliyonigarimu pesa nyingi sana, tupo hapa tumejibana kwenye apartment ya vyumba viwili. Inawezekana kabisa na mimi nilichangia kuharibu nyumba ya kwanza tuliyojenga. Lakini naomba usichoke. Naomba anza upya. Pata muda fikiria ni jinsi gani yakufanya.” “Wewe unataka nini?” Nanaa akauliza.

“Ni zamu yako mpenzi wangu. Naomba ufikirie. Nimeshakwambia nini nataka. Naomba wewe fanya kile ambacho unajua hakitakufanya ujute baadaye. Panga matofali yako vizuri, ili nyumba isije kutuangukia tena baadaye.” “Naomba nianze kwa kuwa mkweli. Sina tena kitu ambacho nimekuficha Geb. Mungu wangu nishahidi. Hata mazungumzo yangu ya mwisho na Malii, nimekwambia. Sasa kama aliendelea kuwasiliana, sijui. Mimi nili mblock na nilikwambia nilimkabidhi dada Fifi kila kitu na pia karibu na siku za kujifungua pia nitamkabidhi simu yangu na nitafungulia mawasiliano ya Malii ili yamsaidie yeye baadaye.” Nanaa akaona awe muwazi zaidi.

“Nashukuru kwa hilo. Ila sijisikii vizuri vile ulivyomwamini Fifi kuliko mimi.” “Kwa kuwa hatukuwa wote Geb!” “Sasa hivi tupo pamoja Nanaa. Na nimekuahidi kusimama na wewe wakati wote hata atakapozaliwa Jimmy. Au umeshindwa kurudisha Imani yako kwangu kwa mabaya niliyokuwa nikikutendea, tena kwa kurudia rudia. Huniamini tena na Jimmy?” “Ninakuamini Geb. Na mimi nimekwambia nimeamua kusimama na wewe.Tumesha sameheana. Huko tumepita. Nitaenda kuchukua kila kitu nikukabidhi wewe.” “Hapo sawa.” Nanaa akacheka. “Una wivu Geb wewe!” “Sio wivu Nanaa. Hata Fifi mwenyewe atakuwa hatuelewi. Tunatuma ujumbe mbaya sana kwenye jamii. Na mimi nafahamika hata na nisiowajua!” “Basi mpenzi wangu. Hilo tumeshalimaliza.” Wakatulia.

“Unaenda kumuona mama saa ngapi?” “Leo na kesho nilimwambia siwezi kwenda kwa kuwa nitakuwa na nyinyi. Kwa hiyo mpaka jumatatu.” Nanaa akamuhurumia. “Ni sawa tukaenda wote?” Geb akamtizama kama kutaka uhakika. “Kama unaona sio sawa, basi. Ila nashauri uende ukamwangalie. Usimwache peke yake hasa baada ya hayo matatizo.” “Hapana. Nataka uwe na uhakika Nanaa. Sitaki ujisikie kama unalazimika.” “Wewe unafikiri atafurahi kuniona na hii hali niliyonayo?” “Hali gani?” “Mjamzito na mjukuu ambaye sio wake?” Geb akafikiria kidogo.

“Mimi naona nisubiri mpaka nitakapojifungua Geb. Tuache tu.” “Hapana. Kama unajisikia kwenda, twende. Inawezekana huu ndio ukawa wakati wa bwana. Usimzuie Roho wa Mungu kufanya kile anachotaka kufanya. Kuhusu anajisikiaje juu ya ujauzito wako, naweza nisiwe na majibu yote. Ila amekuwa akituma salamu kwako na watoto. Amekuwa akisema nikusalimu. Na Grace ameomba nikusalimu, nikwambie anakupenda na anakuombea Mungu akurejeshee miaka yote uliyopoteza na wanao.” Nanaa akazidi kuumia na kuwahurumia.

Ilikuwa ni familia ya watoto watatu tu. Mama na watoto wake wawili mapacha. Upande wa baba walishawakataa kuwatambua tokea uhai wa baba yao. Mama yao ni yatima. Kwa hiyo kila mjukuu na mkwe aliyekuwa akiongezeka kwao, ndio familia pekee waliyoitegemea. Na walikuwa wakijitoa kwa moyo wote kupenda na kusaidia watu bila ubaguzi.

Ukipanda Mema, Utavuna Kwa Wakati..

Geb arudi kwa mama yake akiwa na familia yake yote. Hata yeye hakuwa akiamini. Lakini kwa  kuwa alikuwa akimuomba sana Mungu, akajua maombi yake yameanza kujibiwa. Kila wakati Nanaa alikuwa akimtizama, asiamini ukimya ule ulikuwa umebeba mazito ya kiasi kile. Geb aliegesha gari mbele ya nyumba. Akafungua watoto wake. “Twende Liv.” Mama yake ilibidi amuite baada yakumuona amesita baada yakushuka. “Twende mama yangu. Twende ukamsalimie bibi.” “Hapana mama. Bibi chapa.” Nanaa akasimama na kumwangalia vizuri.

Moyo wa Geb ukapasuka. Akajua tayari mambo yameharibika tena. Alishakuwa amefika karibu na geti dogo la kuingilia ndani. Akasimama akiwa amembeba Magesa. “Bibi alikuchapa!?” Nanaa akauliza kwa mshangao. “Chapa hapa.” Liv akamuonyeshea kwenye matako. Akamtizama Geb, Geb kimya kama kawaida yake. Akarudisha macho kwa Liv. 

~~~~~~~~~~~~~

v Haya tena, wanandoa hawa wameanzisha penzi jipya. Kila mmoja ni kama amepata mwenza wa ndoto zake. Grace aliyekuwa akilia, sasa anafutwa machozi kwa herufi kubwa na Man. Danny anaimba kupata kimwana. Laini, mweupe, rahisi kunyanyua popote, Sara. Anakula vitu FRESH sio makapi.

LAKINI, ‘Alicho kiunganisha Mungu, Mwanadamu asikitenganishe.’

v Nanaa ameamua kurudi kwa mama G. Liv naye anaanzisha jambo jingine. 

Nanaa aliwaacha wahukumu wake madhabahuni mwa Bwana.

-       Je, bado Mungu anapatiliza mabaya?

-       Bado Mungu analipa kisasi?

-       Ubaya wao utawafuata mpaka wapi?

v Mama G amejikuta yupo kifungoni. Imebidi mwanae Geb kumfungia ili wasimdhuru. Ni kama Nanaa amebeba hatima ya yote. Amesimama nje ya mlango. Ataingia?

v Nini kitaendelea kwa mapacha hawa wa mama G, waliofanikiwa kielimu, kiuchumi lakini kwenye mahusiano imekuwa shida.

-       Ndoa ya Grace itaishia wapi?

-       Geb anataka kumuoa Nanaa katikati ya mvurugiko huo, mwisho ni nini? 

Usikose Muendelezo.

 

CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment