“Hapana. Nguo namvua mwenyewe.
Huyu nataka kumvua taratibu. Nifaidi kuanzia macho mpaka mzee akiingia ndani
kabisa, nisikilizie raha yake.” Akamkataza huyo kijana wake. Nanaa alilia kama
anayechinjwa. “Naomba usinifanyie unyama huu
mbele za watu, hasa kaka yangu. Tafadhali Malii.” “Nilijua ndipo ulipochagua! Haya ongoza njia mpaka chumbani
kwa Mzee G E B.” Malii alidhihaki. Wakamfungua mikono, Nanaa akatoka pale
kwenye kochi huku akilia. “Kaka nisaidie. Niokoe kaka yangu.” Nanaa
alikuwa akilia huku akimtizama kaka yake. “Hawezi kukusaidia huyo. Hana shida
ya wewe kulalwa na wanaume. Haimsumbui hata kidogo. Ndio maana anakuacha hapa
bila shida akijua Geb anakulala bila heshima.”Malii akacheka kwa kudhihaki tena.
“Eti gafla James anajidai
amesahau kuwa Geb alikuwa akilala na Liz nyumba ambayo na wewe ulikuwepo! Anajidai
amesahau kuwa Geb alikuacha nje ya ukumbi siku ya harusi yangu wakati yeye Geb,
anapeana mabusu na Liz ndani, na James akiona! Eti leo gafla James anajidai
amesahau kabisa, anatoa baraka zake uzalishwe humu ndani ya familia hii
wasaliti! Wanafiki wakiongozwa na mama yao anayejidai mcha Mungu. Mtoto
wake analala na wanawake ndani ya nyumba hiyo hiyo ambayo na yeye yupo,
lakini hana shida! Sidhani kama ataumia nikilala na wewe hapa na yeye akiwepo.
Eti mama Lao?” Akamgeukia mama G, akiwa vilevile uchi.
“Utaumia na mimi nikiendelea
kwa Nanaa? Maana Geb alitoka kulala na Liz, akaja kulala na Nanaa, na bado mama
unatoa baraka zako tu. Naamini hatakuwa na shida hata na wewe ukitoka kulala na
Geb, ukaja kulala na mimi pia sasa hivi. Au mama G, unabisha!?” Malii akauliza
kwa kejeli akijua wote wamefungwa midomo hawawezi kuongea.
“Si nilikwambia Nanaa? Hamna
mwenye shida na sisi tukiendelea. Twende zetu wangu. Tukale vitu vyetu
taratibuuuu. Bila jasho. Kipupwe kikitupuliza chumbani kwa Geb.” Wote
walifungwa mikono, miguu na midomo. Wakabaki wamekaa wamenyoosha miguu huku
wamesimamiwa na risasi. James alikuwa akisikika akilia sana. Aliinama muda wote
akilia.
Akamshika Nanaa kwa nguvu, kutoka
pale alipokuwa akilia pembeni ya kochi. “Umeona uroho wa pesa unavyo kuponza?
Leo unaweza kukosa vyote.” Malii akacheka huku wakipandisha ngazi akimvuta na
Nanaa na kijana mmoja wao akiwasindikiza. “Ulikataa kulala na mimi ili Geb
asijue akakufukuza kwake. Sasa leo mbele yake, nakutia mpaka nichoke. Si
alijidai hataki niwe karibu na wewe nisiwasimamie harusi! Sasa leo nakukula
kitandani kwake, huku AC yake inanipuliza. Kwanza hataumia, hakupendi. Heri
mimi ninaenda kukulala na ninakupenda.” Alisikika Nanaa akilia tu.
Walifika mpaka mlangoni mwa
chumba. “Waungwana eeh! Tusisumbuane. Nataka kula vitu vyangu kwa nafasi.
Taratibu mpaka niridhike.” Malii aliongea kwa sauti ili wakina Geb wasikie.
Wakaingia chumbani. Malii alimvua Nanaa nguo zote, yule kijana akamfunga pale
kitandani. “Naomba usimfunge mdomo. Nataka nimsikie sauti yake wakati
nikimfaidi. Ndio itaniongezea molali.” Malii aliongea huku akimtizama Nanaa
pale kitandani.
Alimfunga mpaka akamaliza. “Naomba
sasa utupishe.” Yule kijana akatoka. Nanaa akazidi kulia. Ilisikika sauti ya
Nanaa tu akilia. Baada ya muda, Malii akatoka akiwa vile vile uchi. “Nimeshamaliza
raundi ya kwanza. Nataka kinywaji baridiii ili niendelee.” Malii alikuwa
akiongea huku anashuka ngazi, akiwa mtupu kabisa kama alivyozaliwa. Akaelekea
jikoni na kutoka na jagi la juisi. “Mpaka hii iishe yote, nitakuwa nimekata kiu
zote.” Malii aliongea kwa kujigamba huku akipandisha ngazi kurudi chumbani kwa
Geb alikokuwa amemuacha Nanaa akilia. Aliendelea kunywa ile juisi bila kutumia
glasi. Alikunywa hivyo hivyo kutokea kwenye jagi. Uchi kama alivyozaliwa. Nanaa
alisikika akilia kwa uchungu sana. Malii akaingia na kufunga mlango.
“Yaani nikikuona tu mwili wako,
akili inavurugika. Hakika Nanaa wewe ni mzuri na mtamu.” Malii aliendelea. “Uwiiiii!
Heri mama yangu alinizaa mwanaume jamani! Starehe hii ningepata wapi mimi?”
Malii alisikika akishangilia huko chumbani, Nanaa akilia sana.
Baada ya kama lisaa tena ndipo
Malii akatoka. “Jamani nawashukuru kwa ushirikiano wenu.” Malii aliendelea
kuzungumza nao huku akivaa. “Nimeoga kabisa. Nahisi nimefutia taulo lako Geb.
Taulo kama sufu!” Malii aliendelea kukejeli huku akiendelea kuvaa pale pale
mbele yao. “Nimekuwa maskini, lakini sijutii. Kwa niliyoyapata huko juu! Si
mchezo. Sasa Geb una baraka zangu zote. Na wewe endelea kuchezea tu. Hata
ukimwaga mipesa pale kwa Nanaa, mimi naelewa kabisa kaka.” Akamgeukia James.
“James! Dada yako mtamu! Si
mchezo kaka. Kama walikuwa wanakupa vijipesa visivyoeleweka, anza kumchuna
kubwa kubwa. Unastahili ndugu yangu. Si kwa utamu ule wa Nanaa! Eeh bwana eeh!
Kaka heshima zako. Umekuza, na mimi leo nimefaidi matunda yako. Mtoto mtamu
kuanzia machoni mkapa ndani!” Malii akamaliza kuvaa.
“Sasa jamani, kilichotuleta
kimekamilika. Tuondokeni, nisizidi kuchelewa. Nanaa nishamfunga huko juu.
Mchukueni huyo mke mdogo wa Geb, Danny. Ameolewa na kaka mtu na mdogo
wake. Basi jamaa hapa kafika. Na yeye anataka aitwe Danny Magesa. Huyo
tutaondoka naye. Mkijitahidi kujifungua na kupiga simu polisi, mjue mmemuua
Danny. Danny ndio tiketi yangu yakunitoa hapa salama. Ukiita polisi tu, sisi
tunamuua Danny, halafu tunamtupa. Tukijiridhisha kua tupo salama, tutamwachia
ili arudi kuwafungua. Sasa uwamuzi ni wako Geb, Grace,
James, Gozi na mamaa ya busara. Mnamtaka Danny au
kuingilia penzi langu na Nanaa? Maana kwangu mimi Nanaa ana penzi la kweli,
kwenu nyinyi wanawachuna tu. Wachanga wawili wamehamia jijini. Biashara
zimewashinda, James kaamua kumtumia mdogo wake ajinufaishe mjini. Sasa Grace
kazi kwako wewe uliyezalishwa kama panya. Vidume vitatu bila baba, au yangoswe
umuachie ngoswe.” Malii aliongea bila wasiwasi.
“Haya, Danny twende. Aga mkeo
kabisa. Maana wewe yatima ndugu yangu. Wanaweza kukutoa kafara. Nawajua hawa
watatu. Tena mama yao ndio kiongozi wao. Wabinafsi kweli. Watu wa maana na
wathamani ni wao watatu tu. Mama na mapacha wake hao wawili. Hawakawii kukutoa
muhanga mtoto yatima. Twende baba.” Danny akanyanyuliwa pale chini. “Ukiwahi
kurudi mkuu, wewe ndio utawafungua wote.” Malii akaongeza.
“Ila Nanaa aoge jamani. Geb,
usiguse kabla hajaoga. Niushauri tu kaka, na kukujali kwa ule umbali tuliotoka
mimi na wewe. Nimemwaga kila kitu humo humo. Na si kwa ukame niliokuwa nao.
Kama bahari vile. Utaenda kujionea mwenyewe. Mtoto kawa mwekunduuu kwa
shuguli.” Malii akacheka nakuongeza. “Bwana leo ndio ujue pesa si kila kitu
na ni kila kitu pia. Leo pesa yako imeshindwa kukulinda wewe na mama
yako ambaye ndio Mungu mtu kwako. Ndani ya mjengo wako, nimefanya kila kitu kwa
pesa yangu mimi ambayo huwa unaiona chache, huku pesa yako nyingi umeifungia
benki. Ningetaka kukuua ningekuua kirahisi tu. Wewe na mama yako mwanadamu
pekee unayemthamini hapa duniani.” Malii akacheka tena.
“Halafu naomba niongeze kwenye
pesa ni kila kitu. Kwanza nitakuwa mchoyo wa fadhila kama nisipotambua
juhudi zako Geb. Umenipa kitanda kizuri. Mashuka safi. Hewa nzuri. Nimemlala
Nanaa bila kutokwa jasho. Nimeoga maji mazuri. Bafu safi. Taulo lako zuri.
Nakushukuru milionea wetu. Pesa yako imenitunzia Nanaa mpaka na mimi
nimemfaidi. Nimemfaidi humuhumu kwenye nyumba yako. Iliyozungukwa na walinzi na
ukuta mkubwaaa. Eti mwenye kisu kikali ndio mla nyama! Usemi wa kishenzi
huo. Tena Zinda anasema ni usemi aliombiwa na mama yako. Akijinadi kuwa wewe
ndio mwenye kisu kikali, wengine hatuwezi kumpata huyo Nanaa. Sasa mama,
nakutaarifu kabisa. Haikuwa shuguli ndogo. Nimepiga kisawa sawa. Gozi fikisha
ujumbe kwa wote. Mwambie Zinda, leo na yeye nimemlia. Geb! Baba, nimekula.
Nimekula haswaaa! Haaaa!” Malii alianza kucheka na kushangilia. “Uuuuuu!!
Ibarikiwe siku ya leo jamani. Twendeni ndugu zangu. Inatosha.” Wakatoka huku
wakimvuta Danny.
~~~~~~~~~~~~~~
“Huyu Danny ndio kafara yao.
Mwekee kabisa risasi ya tumbo. Ukiona chochote usichokielewa, fyatua tu. Hamna
hasara yeyote. Kwanza hapo alipo sio binadamu. Anatembea kama mzimu tu. Wamemfanyia
uchawi. Ndio maana mnamuona hapo kawa kama fala. Hao wote kina Magesa, wamemuoa
huyo. Na yeye wanamlisha kama mtoto wao au kama Nanaa. Basi Geb na dada yake
wanavuna mipesa tu kwa zindiko walilomtoa huyu. Unaambiwa walishamzika muda
mrefu sana. Ndio maana wanapesa nyingi
yeye yupo kama fala tu. Hajitambui.” Malii akaendelea kumwaga sumu na kuibua
kitu cha tofauti kwa Danny.
“Unaambiwa mama yao mchawi
kweli kweli. Anakijiduka kidogo tu, lakini weee! Anamijihela hatari. Watu
wanajiuliza, kiduka kile na pesa zote hizo, wapi na wapi!? Ipo namna tu. Sasa
unaambiwa kila mwezi lazima Geb aende Iringa kwa mganga wao. Huyu Danny ndio chuma
ulete wao. Wamemfanya kama jinga! Hajijui tu. Lipo kama toto la kike! ”
Walimsikia Malii akiongea huku wakielekea kwenye gari. Baada ya muda wakasikia
gari likiondoka.
~~~~~~~~~~~~~~
Vilijaa vilio vya miguno
yataratibu na sauti ya uchungu ya Nanaa ilisikika kutoka juu chumbani kwa Geb.
Hakuna aliyeweza kumtizama mwenzake. Mlio wakufunguliwa geti kwa nguvu,
ulimwamsha mmoja wa mlinzi getini. Akajaribu kuangalia kamera, akaona ni gari
aliyoingia nayo Malii. “Kwa nini atoke
kwa kasi hivyo!?” Mlinzi akajiuliza. Akaamua kwenda ndani kujua kama ni
salama. Asijue alishachelewa.
Alikuta mlango wazi. Akaingia.
Alishituka sana kukuta ile hali. Alipigwa nabutwaa, asijue afanye nini. “Samahani nililala kidogo.” Akaomba msamaha
huku akitetemeka, asijue kama alilala zaidi ya lisaa. Bosi yupo chini sakafuni.
Plasta mdomoni, mkononi na miguuni, huku akilia kama mtoto. Alikuta hali
iliyomchanganya sana. Kwa kuchanganyikwa akawaacha wa pale chini, akakimbilia
chumbani kwa Nanaa.
Alimkuta na hali mbaya sana.
Kwanza mke wa bosi wake, halafu yupo uchi nyang’anyanga pale kitandani.
Akamfunika kwanza ndipo akamfungua huku akiendelea kulia. Nanaa hakutoka pale
kitandani. Aliendelea kulia kwa uchungu mnooo. Mlinzi akawa ameshajua
kilichotokea.
Akarudi tena kuwafungua James,
Gozi, Geb, mama G na Grace. Mlinzi mwenyewe akaanza kulia kwa hofu. “Ngoja nipige simu polisi.” “Hapana. Usithubutu. Watamuua mume wangu.
Wewe acha kama ilivyo. Mmeshindwa kulinda, acha na wala usimwambie mtu yeyote.
Umenisikia?” Grace akauliza kwa hasira huku akilia. “Hata walinzi wenzio usiwaambie. Sisi tupo sawa tu. Wamemchukua mume
wangu. Ukisema chochote, watamuua Danny. Ondoka na kaa kimya.” “Sawa mama.” Mlinzi akajibu, nakutoka huku anatetemeka.
Hakuna aliyeweza hata
kunyanyuka. Walikaa pale mpaka Danny akarudi huku anakimbia. Grace alisimama na
kumkumbatia huku analia. “Hawajakuumiza?” “Hapana. Nani
amewafungua?” Danny akauliza huku akitetemeka. “Mlinzi.
Lakini tumemwambia asimwambie mtu ili wasikudhuru. Hawajakuumiza?” Grace
akarudia tena huku akimwangalia mumewe kila mahali. “Walinifungua na kunishusha
katikati ya kwenye mataa ya hapo Buguruni. Nusura kugongwa!” Danny aliongea
huku akionekana amepaniki.
“Naomba tuondoke Grace. Tukachukue
watoto tuondoke sasa hivi. Sitaki kuendelea kukaa hapa. Twende.” Grace na Danny
wakaenda kuchukua watoto wao, wakaondoka. James akatoka hapo kimya kimya, huku
akivuta kamasi. Na Gozi akafuata nyuma. Akabaki Geb na mama yake. Geb na
yeye akatoka. Hakurudi tena, mama yake
alikesha akilia.
Asubuhi
Ya Baada Ya Balaa.
Nanaa alilia usiku kucha bila kunyamaza wala wakumbembeleza.
Ikabidi tu aamke. Ilishakuwa asubuhi, mtoto wake alishaanza kulia. Akajua ni
njaa tu. Akakimbilia bafuni kuoga huku akiendelea kulia. Akavaa haraharaka
akatoka bila hata kupaka mafuta. Magesa alianza kwa sauti ya chini. Mpaka Nanaa
anamaliza kuoga, tayari nyumba ilijaa
kilio chake. Akakimbilia chumbani kwa mama G, alipokuwa analala na watoto wake.
Akasita mlangoni. Lakini akajikaza. Akafuta machozi, akaingia kama ananyata.
“Unaenda wapi?” Hilo ndilo
lilikuwa swali lililomshangaza Nanaa. “Nakuja
kumnyonyesha mtoto wangu.” “Huna aibu wala huruma wewe Nanaa!?
Umeyaharibu maisha ya Geb, sasa hivi unataka umuharibu mtoto wake! Unamauchafu
ya mwanaume mwingine, unataka umnyonyeshe nayo mtoto! Unataka kumuharibu awe
mlemavu na tahira? Umenyimwa aibu wewe mtoto! Nguvu ya kukutoa juu mpaka hapa
unatoa awapi?” “Nimeoga mama!” Nanaa alijibu huku
machozi yakimtoka. Midomo ilikuwa kitetemeka sana.
“Ila sikushangai. Ndio kawaida
yako. Umeshazoea kuwahudumia wanaume kwa siri, halafu unarudi hapa nyumbani
unajidai, Mama! Mama! Huku unajichekesha. Mnafiki mkubwa wewe. Unawavulia nguo
kina Malii, halafu unarudi kwangu unajidai unajiliza unampenda Geb!
Ukatuaminisha kuwa wewe ni binti mzuri. Tukamshawishi Geb kuwa wewe ni mke
wakuoa! Mwanangu akazaa na wewe, kumbe wewe ni Malaya, huna shida kuvulia nguo
wanaume wengine! Unachotaka ni pesa tu kutoka kwa mwanangu! Umaskini gani huo
uliokutoa utu na kututapeli kwa kiasi hicho? Umechanganya kundi zima la
marafiki. Unamvulia nguo huyu, unalala na huyu. Jana ulitaka kusababisha kifo
cha Geb sababu ya umalaya wako. Nimechanwa mdomo kwa ajili yako!” Nanaa alikuwa
haamini.
Geb akarudi. Akaingia na vijana
wawili. Nanaa akashangaa wale vijana wanapandisha juu chumbani kwao. Geb
akampita Nanaa. “Nimbembe yupi? Liv bado anaonekana amelala.” Geb akamuuliza
mama yake bila kumtizama Nanaa. “Mnaenda wapi na
wanangu?” Nanaa akauliza. “Tumegundua hila zako. Na hazitafanikiwa
Nanaa. Labda usubiri mimi nife, ndio utacheza na wanangu na wajukuu zangu.
Twende Geb.” Mama G alionekana ameshajitayarisha.
Shilingi Yatumbukia
Chooni.
“Geb please!” Nanaa akapiga magoti,
akatambaa mpaka alipo Geb akamshika. “Usiwahi kunishika tena Nanaa. Wewe ni
muongo na muuwaji. How could you that!? Eti Nanaa? Umewezaje kunifanyia mimi
hivyo? Ni siku ngapi nilikuwa na wewe pale hospitalini? Sikukuomba unieleze
ukweli wote juu yako na Malii, ukanidanganya?” “Sikukudanganya Geb. Sikutaka kukuumiza. Tafadhali nielewe.” Nanaa aliendelea kulia.
“Nimekuelewa. Tena nimekuelewa
vizuri sana Nanaa. Hutawahi kuja kubadilika. Japokuwa nilikuomba usije
kunidanganya. Nikakuomba uwe unaniambi ukweli hata kama unajua utaniumiza.
Nilikurudia zaidi ya mara tano. Ndio kitu pekee nilichowahi kukuomba kwa
kurudia rudia. Lakini uliamua kunidanganya. Tena umefanya na rafiki yangu!
Nimekaa na wewe hospitalini Nanaa. Nikiteseka kwa ajili yako! Muda wote nipo
pale. Nalala kwenye kiti! Ili tu kuwa na wewe. Nimeacha shuguli zangu zote ili
niwe na wewe, lakini umenilipa ubaya wa ajabu sana. Tena huku ukiniangalia
machoni! Unawasiliana na Malii, huku ukilala na mimi! Anakuomba penzi na
kuzungumza maswala ya mapenzi, huku unalala na mimi. Umemfanyia yale yale
unayonifanyia mimi! Je ni wanaume wangapi unawafanyia kama unavyotufanyia mimi
na Malii, tena ukirudi kwangu ukijidai unanipenda?” Geb aliongea kwa uchungu
sana.
“Ulitaka nikupe nini ili
uridhike Nanaa? Ulitaka nikuoe ili uje umiliki mali zangu halafu ndipo ufungue
makucha yako? Kwa kuwa mimi sikutoshi kwa chochote, kwa hiyo upo hapa kwa ajili
ya mali yangu tu? Sasa, kwa kuwa kwa bahati mbaya sana, umezaa watoto wa pekee
ninaohitaji hapa duniani, sina jinsi ya kukufukuza. Kwa kuwa najua ipo siku
Magesa atanilaumu sana, nakuachia hii nyumba. Sio kwamba nakupa. Umeshaichafua
vyakutosha. Si mimi, watoto wangu wala mama yangu wanaweza kuishi tena humu.
Umeinajisi kwa kiwango kikubwa mpaka Mungu aliponihurumia, ndipo akaja
kukuadhibu mbele za watu na kunifungua macho. Ulikuwa ukienda kwa wanaume zako,
unaenda kufanya unayoyafanya kisha unarudi hapa. Unadanganya kila mtu!” Geb
alikuwa mkali na muongeaji, Nanaa hajawahi kumuona.
“Utaishi hapa, kwa vile
unavyotaka wewe. Lakini huruhusiwi kuleta wanaume zako humu ndani. Nenda
kaendelee kulala nao huko huko nje. Siku ambayo utaleta mwanaume hapa ndani,
ujue ndio mwisho wako wakuishi humu ndani. Usithubutu kunitafuta kwa la kheri
wala la shari. Leo ndio mwisho hata wa kuiona sura yako.” “Geb usiniache!” Nanaa akaendelea kulia.
“Watoto watakuwa wanaletwa
hapa. Dereva akikukosa, ujue ndio basi. Hawaruhusiwi kulala hapa. Utawaona kwa
muda mfupi kisha, watarudishwa kwa mama. Wataletwa kwa muda na wakati mama
atakaoona unafaa.” Nanaa hakuwa akiamini.
“Mama!” Geb akamgeukia mama
yake aliyekuwa akimnyonyesha Magesa maziwa ya chupa. “Huna sababu yakubeba
chochote humu ndani. Tutaanza upya mimi na wewe. Mungu atatusaidia tu.” Geb
akambeba mtoto wake wa kike, akatoka. Nanaa alibaki amepiga magoti akilia.
Baada ya muda Mama G naye akasimama nakutoka. “Mnafiki mkubwa wewe!” Alimsikia
mama G akiongea kwa hasira.
Msiba
wa Nanaa.
“Mungu uliyeniumba nisaidie mimi! Mungu wangu nisaidie
jamani.” Nanaa alibakishwa pale chini
kwenye sakafu ya chumba alichokuwa wakilala wanae na mama G. Aligaragara akilia
bila kunyamaza. “Mungu nisaidie! Mungu wangu nisaidie. Mungu njoo nisaidie.” Nanaa
aliendelea kulia. “Nimekosa nisaidie. Nimekosa nisamehe Mungu. Na wewe usiniache.
Nisaidie Mungu wangu.” Nanaa aliendelea kulia bila kunyamaza.
Hakuwa akijua wameenda wapi na
watoto wake. Hakujua ni lini atarudishiwa hao watoto. Mtoto aliyeteseka naye
hospitalini karibia kufa, anatenganishwa naye akiwa hata hamfahamu mama yake
vizuri. Hakuwahi kumuogesha, wala kumvalisha! Hajawahi kukaa naye hata zaidi ya
masaa 5 wakafahamiana na mtoto akajua joto la mama yake! Joto analolifahamu
Magesa ni la bibi yake tu. Nanaa aliendelea kulia kila akimkumbuka Magesa mtoto
ambaye ni kama amemzalia mama G. Alimtoa pale hospitalini na kummiliki kama
wake.
Kila alipomkumbuka Liv mtoto
wake, alizidi kuomboleza asiamini kama ndio ametenganishwa na mtoto aliyembeba
kwa shida akiwa chuoni. Alibakishwa pale peke yake akilia mchana na usiku.
~~~~~~~~~~~~~
Baada ya siku tatu, mchana, akasikia simu kutoka
getini. Anatakiwa kutoka, anamgeni. Alikuta gari ya Geb nje. Akajua ameletewa
watoto. Akakimbia mpaka kwenye gari. Jeri ambaye ni dereva akashuka. “Nimeambiwa
nimlete mtoto.” “Magesa yuko wapi?” Nanaa
akauliza huku analia. “Nimeambiwa nimlete huyu tu.” Nanaa akapiga magoti nje ya
gari akazidi kulia.
Alijua muda mfupi atakao kuwa
akiletewa hao watoto, angalau Magesa atamfahamu. Alilia mpaka Liv na yeye ndani
ya gari akaanza kulia. Akasimama kwa haraka na kufungua mlango ili amchukue
mtoto. Jeri akamuwahi. “Nimeambiwa haruhusiwi kunyonya wala kuingia ndani.” “Sasa hapa nijuani. Nitasimamaje na mtoto hapa!?” Nanaa
kauliza. “Nimeambiwa pia asitolewe ndani ya gari.” “Haiwezekani jamani! Huku nikumwadhibu mwanangu. Ona mtoto
anavyonililia. Mimi namtoa.” “Hapana dada. Nimekatazwa kabisa.” Jeri
akamzuia kabisa. Nanaa alizidi kulia kama amefiwa. Liv analia, mama yake naye
analia.
“Naomba umuondoe
hapa. Huku nikumtesa mtoto wangu tu. Mwambie Geb, Mungu anamuona. Waache
kuwaadhibu wanangu kwa kosa nililolifanya mimi.” “Lakini kuna kitabu
hiki. Natakiwa mimi nikifika hapa nikiweke saini, na wewe uweke saini kuwa
umeona watoto.” “Sitafanya hivyo.” Nanaa
akajibu kwa jeuri huku akilia. “Nimeambiwa ukikataa nikwambie hawa watoto
hawatarudi tena.” Nanaa akazidi kulia. Akaweka saini.
“Unarudi tena
lini?” “Sijui dada yangu. Ni mpaka nitumwe.” “Naomba wakikutuma tena uniletee watoto, hakikisha unakuja na Magesa.” “Unajua
siwezi dada yangu. Nafanya kile ninachotumwa.” Liv alikuwa akilia sana akimtaka
mama yake. Mikono yote ilikuwa juu. Analia akiita mama, mpaka akawa mwekundu
kabisa.
“Kama hutaniruhusu kumshika mwanangu, naomba mtoe hapa.” Bila
kuongeza. Akapanda kwenye gari, akaondoka huku Liv analia sana.
~~~~~~~~~~~~~
Nanaa akarudi ndani huku akilia
asiamini ukatili anaoendelea kufanyiwa. “Mungu! Usiruhusu
wanangu wapitie nilikopita mimi. Kama unapatiliza dhambi ya mama yangu, natubu.
Natubu Mungu wangu msamehe mama yangu, nisamehe mimi na wanangu. Tusamehe baba.
Warehemu wanangu kama unavyowarehemu watoto wengine. Hawakuchagua kuzaliwa na
mimi! Wewe ndio umewachagulia watokee kwangu. Kama nikuchagua kuzaliwa, basi
wangechagua wazazi wanaopendana na wenye ndoa nzuri. Lakini Mungu, usiwahesabie
hatia wanangu. Kumbuka rehema Baba yangu. Wakumbuke wanangu.” Nanaa
aliomba siku nzima akilia kwa uchungu sana.
Hiyo siku ikapita, na kesho
yake pia. Baada ya siku tatu tena, Nanaa akaletewa watoto wote, lakini wakiwa
wamelala kabisa. “Kwa nini wananifanyia kusudi jamani? Hawataki
niwashike wanangu! Halafu wanawaleta wamelala! Ndio natakiwa kufanya nini?” “Saini
hapa.” Jeri alishashuka na kukaa upande aliokuwepo Nanaa ili asije kufungua
mlango. “Hakika sita saini. Kawaambie nimekataa. Labda
waniruhusu nishike wanangu. Nina saini ujinga tu. Hapana.” Yule dereva akarudi ndani ya gari. “Hivi Jeri una watoto wewe!” Nanaa akamuwahi kabla hajaondoa gari. Akauliza huku akilia
kwa kwikwi. Jeri akanyamaza. “Nijibu tu.” “Ninao dada.” “Sasa unafikiri
hivi wanavyowafanyia watoto wangu ni sawa?” Kimya. “Hata kama mimi ningekuwa mbaya wa namna gani, wangeniadhibu mimi.
Lakini sio watoto wangu.” “Lakini nilimwambia bibi kuwa Liv anamtaka mama yake.
Akasema..” “Sitaki kujua alichokujibu. Ila hivi sio sawa
kabisa.” “Naomba niondoke dada yangu. Wanasubiriwa hawa watoto.” “Naomba nisaidie namba yako ya simu.” Nanaa akamuwahi tena.
Jeri akaindika mahali, akamkabidhi Nanaa. Akaondoka.
Nanaa akarudi ndani akilia
sana. Alilia Nanaa bila kujua chakufanya. Kwa muonekano wa Magesa, alionekana
amelishwa vizuri na ameshiba. Alikuwa akivutia. Wazi alionekana anatunzwa
vizuri. “Huyu
mtoto hatakaa anijue kama mimi ni mama yake.” Nanaa
alizidi kulia. “Liv wangu jamani mimi! Mungu nisaidie.” Nanaa
akaendelea kuomboleza.
~~~~~~~~~~~~~
Zilipita siku saba Nanaa akilia
bila kuletewa watoto. Akakata tamaa. Akakumbuka hakusaini lile daftari kuwa
aliona watoto, na aliambiwa asipoweka saini yake, ajue ndio hatakaa aone watoto
wake tena. Akajua ndio basi tena. Kwenye chumba chake na Geb hakuwahi kurudi
kulala tena. Aliishia kulala kwenye makochi huku akishindwa kupata usingizi.
Kila akifunga macho, alimuona Malii anamfanyia hiki au kile. Akaishia kukesha.
Pengine kusinzia kidogo hapo hapo kwenye makochi lakini sio kulala vizuri.
~~~~~~~~~~~~~
Njaa nayo ikaanza kumsumbua.
Hakuna wakumpikia. Inabidi ajipikie mwenyewe. Akajua maisha mapya yameanza.
Maziwa yalikuwa yamejaa sana. Alishakamua mpaka akajaza kila chombo humo ndani
akawa anaweka kwenye friji, hana wakumpa au kuyanywa. Akaamua kutoka kwenda
duka la madawa, kuulizia kama kuna dawa yakukausha maziwa. Hakupewa jibu
lililomfurahisha sana, kwani walimwambia ayaache tu. Asikamue tena mpaka
yakauke yenyewe.
Kwa asili Nanaa alijaliwa
maziwa mengi sana. Yalikuwa yamejaa, yanamuuma kama majipu. Ikawa kama bahati
tu, akakutana na mwanaume, sio mtumzima sana, alikuwepo hapo pembeni, akadakia
kwa kumpa ushauri wa kiasili tu wala si kidaktari. Akamwambia awe anaweka
maganda ya kabichi, yabaridi kwenye matiti yake. Akamtupia huo ushauri kuwa
ayaweke maganda hayo ya kabichi kwenye friji mpaka yapate baridi ndipo ayaweke
kwenye matiti yake yakiwa vile vile ya baridi.
Nanaa akaondoka hapo kwa uchungu sana akiumizwa na wazo kuwa mwanae
anapewa maziwa ya kopo wakati yake yapo tu! Aliumia sana.
~~~~~~~~~~~~~
Mwisho wa mwezi ulikuwa umepita
kama siku mbili. Geb alikuwa ana mtindo wakumuwekea pesa kwenye akaunti yake.
Akaamua kupitia kwenye ATM, akangalie na huko nako kukoje na achukue pesa
baadhi. Akakuta hapajawekwa pesa mwezi huo. Akajua safari hiyo Geb amemuamulia
kweli kweli. Akapanda daladala yakurudi kwake akiwa na pesa kidogo yakumsaidia
matumizi yake endapo atataka kitu.
Akatembea taratibu mpaka
getini. Mlinzi akamwambia watoto waliletwa, lakini hawakukaa sana kwa kuwa
hakuwepo. Nanaa alianguka chini nakuanza kulia pale mbele ya yule mlinzi. Yule
mzee akamuhurumia. Akamshika mkono nakumwingiza ndani huku akilia sana.
Alipotulia akaamua kumpigia
simu Jeri, dereva wao. “Nilisharudisha
watoto. Hapa nimetumwa maziwa ya mtoto.” Nanaa
akazidi kulia. Akajua ni maziwa ya Magesa. “Unaweza kuwaleta? Nimerudi.” “Sidhani
dada. Baba yao ametupa glasi kwa hasira baada yakumwambia haupo nyumbani.
Sidhani kama watarudishwa tena.”
“Waambie nilienda duka la madawa tu.
Nimerudi.” “Acha nikwambie
ukweli dada, hakuna anayekusema vizuri pale. Hasa bibi. Anakulalamikia vibaya
sana. Na leo ameapa kumtafutia mwanae mke, aoe, ili alee hao watoto. Wakufute
kabisa kwenye maisha yao.” Nanaa alihisi
kuchanganyikiwa.
~~~~~~~~~~~~~
Presha nayo haikukawia
kutibuka. Nanaa akaanza kujisikia vibaya. Akajua wazi pressure ipo juu.
Alihofia kutoka tena pale asije kuwakosa tena wanae pindi watakapoamua
kuwarudisha tena. Akavumilia tena siku tatu mbele, akaona kimya lakini hali
ikawa inazidi kuwa mbaya. Wakati mwingine hakuwa akiweza hata kutoka pale
alipokuwa amelala kwenye kochi.
Akaona kwa ile hali hata
akibaki pale akaletewa watoto awapakate, hataweza. Akajiamulia kurudi
hospitalini akaonane na yule daktari aliyekuwa akimtibu. Dokta Lyamu. Alimtafuta
kwenye simu. Akamwambia kwa wakati ule hana pesa. Wakashauriana wakutane
hospitali ya taifa ya Muhimbili ambako haitamgarimu sana, kama kule alikomuona
kwa mara ya pili kwenye hospitali ya kulipia, ambako Geb ndiye aliyekuwa
akigarimia matibabu hayo. Akaona wazo zuri.
Alitoka pale akiwa na hali
mbaya sana. Akatembea kwa shida mpaka kwenye kituo cha daladala. Akiwa ndani ya
daladala yakuelekea muhimbili akaanza kutokwa jasho jingii. Akaomba apishwe
kwenye kiti. Akakaa. Daladala iliposimama tu, akashuka na kuchukua taksii. “Naomba
nikimbize hospitali ya taifa ya Muhimbili. Najisikia vibaya sana baba yangu.”
Yule Mzee, dereva taksii akaondoa gari. Nanaa akajilaza kiti cha nyuma.
Alimfikisha mpaka mbele ya dokta
Lyamu huku amemshikilia mkono. “Vipi?” Akauliza mara alipomuona anakuja huku
ameshikiliwa. Na yeye alikuwa akitoka. “Najisikia vibaya sana.” Nanaa akajibu
huku akitetemeka. Dokta Lyamu akampokea. “Na mimi natoka mara moja, nitarudi
baada ya muda mfupi sana. Nesi atakupima vipimo vya awali. Kisha nitakuja
kuendelea.” Nanaa akatingisha kichwa kukubali.
Akaingizwa kwenye chumba cha
pembeni. Akaanza kufanyiwa vipimo. “Unakaribia kupata stroke, dada. Pressure
yako ipo juu sana!” Yule nesi aliongea akionekana ameshapaniki. Hapo hapo
akampigia simu dokta Lyamu. Akarudi kwa haraka sana. Nanaa akapewa huduma ya
kwanza na kupelekwa wodini. Sababu ya mawazo mengi, walisumbuka sana kushusha
pressure yake. Aliishia kuchomwa sindano za usingizi ili kumfanya alale.
Msiba
Na Mwenzie.
Alijikuta mwezi ukiisha akiwa
bado hospitalini. Akajua kwa uhakika hatapata tena watoto wake. Kila alipokuwa
macho, alikuwa akilia. Si mchana si usiku. Matibabu yaliendelea huku presha
nayo ikiendelea kuwa vile vile bila kushuka hapo alipokuwa amelazwa wodini. Sio
kwenye chumba cha peke yake kama alivyozoeshwa na Geb kuwekwa chumba cha peke
yake, tena kwenye hospitali za garama sana, na za huduma za hali ya juu. Hicho
hakikumsumbua hata kidogo. Hakuwa hata na mtu wakumtembelea. Hilo nalo
alilitegemea. Alijua kaka yake James atakuwa hana uwezo hata wakumtizama tena machoni.
Siku zilizidi kwenda akiwa bado
hospitalini, ikabidi aanze kujishauri mwenyewe. “Nimerudi sifuri kabisa!” Nanaa akajiwazia. “Lazima niwe imara. Leo wamefanikiwa kunipokonya watoto wangu. Lakini
ipo siku wanangu watanitafuta tu. Mungu yupo. Sasa wasije kupatwa na akili,
wanataka kumjua mama yao, na mimi nimekufa! Lazima nitoke hapa nilikojificha.”
Nanaa akajishauri.
“Uzuri nilisoma. Naweza nikahangaika kupata kazi, lakini nitafanikiwa
tu. Mungu wangu upo.” Nanaa akawaza na kujitahidi kutulia. Geb
alikuwa akimuwekea pesa yakutosha. Kwa hiyo hata akaunti yake ilisoma vizuri.
Akaanza kupiga mahesabu pesa aliyonayo. Akajua anamwanzo mzuri kabisa. Wapi
pakuishi. Ndio ukawa mtihani. “Siwezi
kuendelea kuishi pale. Nitajitesa tu. Heri nikatafute kwangu.” Nanaa
akakusudia. Akaamua akitoka pale, akaanze maisha yake sehemu nyingine. Angalau
akaanza kulala vizuri. Na vilio vikakoma. Ikawa inaendelea mikakati tu kichwani
mwake. Anawaza hili na kupanga lile, ilimradi maisha yasije simama mara baada
yakutoka pale.
~~~~~~~~~~~~~
Mwanamke wa jirani yake
akamuona ameanza hata kuchangamka. “Habari za asubuhi?” Nanaa akasalimia wakati
anaelekea msalani. Yule dada akaitikia. Nanaa akapita. Aliporudi yule dada
akamsemesha. “Naona leo umeamka na nguvu!” Nanaa akamwangalia tu, nakunyamaza. “Unajisikiaje?”
Akaendelea kumuhoji. Akamfananisha yule dada na mama G. Alimuanza kwa upendo
lakini mwishowe akampokonya na watoto. Akapanda kitandani akajilaza bila
kujibu.
“Na mimi nilikuwa nikilia hivyo
hivyo! Tena mimi nilimkasirikia mpaka Mungu. Basi kufa hufi, unabaki unajitesa
tu mwenyewe. Nilikaa kwenye hali hiyo mpaka nikaamua kujifariji tu. Maana wakunifariji pia sina!
Mtu uliyekuwa na mume na watoto, gafla unabaki peke yako! Maisha ni kitu
kingine!” Kidogo akaanza kumgusa Nanaa.
“Una watoto wa ngapi?” Nanaa
akamuuliza. “Wakike wawili.” Nanaa akanyamaza. “Unataka kuona picha zao?”
Akamuuliza tena Nanaa. Akamtizama kwa muda, akamuona analia bila kujibu. Huo
ndio ukawa mwanzo wakufahamiana kwa yule dada na Nanaa. Siku nzima Nanaa na
yule dada wakawa wakizungumza. Nakufahamiana.
Yule dada akamueleza historia
ya pressure aliyonayo. Nanaa akamuhurumia sana. “Pole.” Ndicho kitu pekee
alichoweza kusema baada yakumsikiliza kwa muda mrefu nakumuhurumia. “Nitafanya
chochote humu duniani kupata hata dakika tano tu nyingine na mume wangu na
wanangu. Nakwambia chochote. Niliumwa karibu kufa. Hawa wauguzi wote
wameshanizoea hapa. Vikitibuka tu, nakaa nao hapa mpaka wananichoka.” Nanaa
aliendelea kumsikiliza.
“Pole sana.” “Ndio maisha mdogo
wangu. Wakati mwingine unapata hiki, kile kinaondoka. Tulipokuwa tumefika na
mwenzangu, nilikuwa sidhani kama kuna kitu nitataka tena hapa duniani. Siwezi
kusema tulianza chini sana, kwa kuwa wote tulitoka kwenye familia zenye
aghueni. Lakini mtaji wetu mkubwa ilikuwa penzi. Acha dada yangu. Mimi
nilipendwa! Tena penzi la dhati, achana na haya mapenzi ya kwenye tv. Penzi la
haja! Lakini Mungu alinipokonya mchana kweupe!” Yule dada aliendelea.
“Ilikuaje? Kwani wewe hukuwepo
kwenye hiyo safari?” Nanaa akauliza tena. Maana yule dada alikuwa akisimulia
kama Nanaa anafahamu kila kitu ila anarudia tu. “Si ndio nilikwambia
tulikubaliana mimi nibaki. Nipokee mzigo, halafu nimfuate baada ya siku mbili.
Nikishaweka mambo sawa, basi nimfuate. Sasa kaka yake ndio anasema anahisi
alipata hiyo ajali baada ya kumpigia simu na kumwambia mama yao amefariki huko
hospitalini. Kwa hiyo asiende moja kwa moja hospitalini kama alivyokuwa
amesema, aende tu nyumbani. Sasa mume wangu alikuwa kipenzi cha mama yake.
Nahisi ndio kuchanganyikiwa na kupata ajali.” Yule dada aliongeza.
“Yaani Dada! Pale pale, wote
wanne na mtoto wa shangazi yake tuliyekuwa tukiishi naye. Alikuwa kijana ambaye
tunashirikiana naye sana kwenye biashara zetu. Yaani tulishibana na yule kijana
kama yeye ndio alikuwa mdogo wangu mimi. Mungu aliwachukua siku moja! Kufunga
na kufungua nikajikuta sina mume wala watoto. Kijana ambaye labda ungesema
angebakishwa tusaidiane, na yeye hapo hapo akafariki. Tulizika watu watano kwa
siku moja. Mama mkwe ambaye ndio alikuwa mgonjwa, wakawa ndio wanakwenda
kumwangalia, mume wangu, binti zangu hao wawili na huyo kijana!” “Pole sana.”
Nanaa aliishia kusema hivyo tu.
“Tena nilizaa watoto wanaakili
dada! Asikwambie mtu. Namba moja tokea wanaanza shule mpaka kifo. Mmoja alikuwa
ndio amemaliza la saba, mwingine ndio alikuwa la tano. Nazunguka na picha za
hao watoto kama mwehu! Utafikiri wapo nyumbani wananisubiri.” “Pole sana.”
Nanaa akaongeza.
“Nimeachiwa mali na nyumba.
Lakini asikwambie mtu, nyumba ni watu. Na watu mnaopendana. Hata ukiwa na
gorofa 3, na kila kitu ndani halafu uliowapenda hawapo, havina ladha.” Nanaa
akajihisi anamsema yeye. “Lakini ndio
maisha bwana! Nimekuwa kama mwehu. Wakati mwingine hata mimi nahisi
nimechanganyikiwa. Nikaacha kila kitu, nipo hapa kama unavyoniona. Vikitibuka
nakuja kukaa nao hapa. Wakitaka kuniruhusu wakati mwingine nakataa. Naona heri
nikae hapa kidogo. Haya, ukikaa hapa, ukisikia matatizo ya wengine, wakikupa na
vijidawa vya usingizi, unajsikia vizuri. Unaona matatizo yako sio makubwa kama
wengine. Basi siku zinasogea. Au unasemaje?” Nanaa akacheka nafsi mwake.
“Huko nikujidanganya.” “Heri
kujidanganya kuliko ukweli wa dunia.” Nanaa aliropoka tu. Hakumaanisha. “Sasa
utajificha hapa mpaka lini? Ni heri ukakae hata kwenu.” “Kwenu, huna pesa!? Hujakutana
na ndugu zangu wewe. Walinipa pesa ya mtaji nianze biashara. Halafu nikajidai
naomboleza nikapoteza mali zote. Hakuna anayetaka kuniona tena. Wakiniona tu
wanajua nataka kuwakopa.” Nanaa akashangaa.
“Kwani imekuaje kwenye hizo
biashara zako?” “Ipi!? Biashara gani!? Nani afanye? Kwa kichwa kipi kwa mfano
hapa? Nakwambia kuna wakati hata moja jumlisha na moja sina jibu! Nilipoteza
kila kitu. Nimebakiwa na nyumba tu. Ndipo hapo ninapoishi kama sipo hapa.”
Nanaa akamtizama.
“Unanishangaa?” Akamuuliza Nanaa.
“Na huyu mwanaume anayekuja kukuangalia wakati mwingine?” “Ndugu wa mume wangu.
Tena undugu wa mbalii. Ndiye nimebakiwa naye. Tena ukimuona kaja hapa, ujue
mkewe hafahamu.” “Kwa nini!?” Nanaa akauliza tena.
“Wivu tena! Anahisi kama
nitamuibia mumewe. Eti kwa kuwa mimi
sina mume.” “Kwani mume wako amefariki lini?” Ikabidi Nanaa kuuliza maana huyo
dada ni mzungumzaji haswa ikabidi amkatize kwa swali. “Juzi ya juzi tu! Kama
miaka miwili iliyopita.” Nanaa akakaa vizuri kwa mashangao “Miaka miwili!?”
“Acha tu mdogo wangu!” Nanaa akabaki akimtizama. Gafla akaona matatizo yake sio
kama ya huyo dada. Yaani yule dada anahitaji msaada wa haraka sana kutoka hapo
kuliko yeye. Gafla akaona amsaidie.
Akamuhurumia na kuamua kumpa historia yake. Akamsimulia historia nzima ya maisha
yake mpaka kufikia hapo alipo. “Kilichonisaidia pekee mpaka unaniona hapa
wodini na wewe, nikusimama na kuchukua hatua.” “Pole sana. Kumbe na wewe
yamekukuta!” “Hakuna na wala hakuna atakayekuhurumia kama hutasimama wewe
mwenyewe. Leo napata pole yako, kwakuwa nilitoka pale kwenye kochi nikaja hapa
nikiwa nakaribia kupata stroke. Sijui kama unanielewa?” Nanaa alishabadilika.
“Umeniona hapa nalia,
ukashangaa. Nilikuwa nalia kuanzia siku nabakwa mpaka natoka pale getini. Tena
kwa sauti ya juu. Nilipohisi nitakufa, ndio nikajiona vile nilivyomjinga.
Nitakufa niwaache wanangu. Ndugu zao wanapesa sana. Watawapa kila kitu.
Watawapeleka wanangu kokote. Baba yao ataoa mwanamke yeyote yule. Hata kama
huyo mwanamke atakuwa anawaka kama nyota, lakini na pesa zao zote, hawawezi
kuwapa wanangu mama mzazi. Ipo siku watanitafuta tu. Sikutaka waje waonyeshwe
kaburi. Nilitaka waje kukutana na mimi mwenyewe. Ndio maana nipo hapa.” Nanaa
aliongea kwa ujasiri kama sio yeye.
“Leo nimeamka tofauti kwa kuwa
nimeamua kuacha kujiliza na kujionea huruma. Itakula kwangu mazima! Nina
mpango wakutoka hapa na kutafuta pakuishi nikaanze maisha. Nimekataa kuwatesa
wanangu. Au mwanangu mkubwa. Akiniona analia sana. Anataka nimshike, na mimi
siruhusiwi.” “Lakini ni washenzi sana hao watu!” Yule dada akapandwa na hasira.
“Hapana dada yangu. Acha
wakasirike tu. Wana haki. Lakini najua hawajui kama wanawaadhibu watoto. Wale
watu walijitoa sana kwangu. Yule mwanaume alikuwa akilala na mimi hospitalini.
Kuanzia siku naingia mpaka natoka hospitalini. Haniachi. Alinipa mapenzi ya
kweli. Mimi mwenyewe nimeharibu. Nimesikia wanamtafutia mwanamke aoe. Naumia
sana. Lakini lazima nifanye kitu dada yangu. Kama nilivyokwambia historia
yangu, sina mama mimi, wala baba. Na ninajua kaka hataki tena kuniona. Kwanza
nimemwaibisha mnoo. Hakutegemea. Tokea ametoka pale, hajarudi tena wala
hajanitafuta tena. Na yeye alishaniulizia kuhusu huyo mwanaume aliyenibaka,
ambaye alikuwa rafiki yake kama nilivyokwambia, lakini sikumwambia ukweli au
niseme nilinyamaza. Sasa hebu niambie, nikijilaza hapa nakulia, mwisho wake
nini?” Yule dada akabaki kimya.
“Angalau wewe una hata shemeji
wakuja kukutizama. Mimi nikikaa hapa, ndio kila kitu kimelala. Nataka dokta
akipita, nimwambie aniandikie dawa, niondoke.” “Basi naona na mimi niondoke tu.”
“Kumbe! Tena angalau wewe unahata pakuweka kichwa.” “Sina hata shilingi!” Yule
dada akalalamika. Nanaa akajua ndio maana watu wanamkimbia kwa kuomba pesa.
“Wewe si una nyumba? Anza
kuipangisha. Pangisha vyumba baadhi, bakisha hata kimoja upate pesa.” “Yaani
nikaishi na watu!? Sijawahi mwenzio.” “Kwa hiyo ni heri hivyo unavyotangatanga
ukiomba? Jiwekee muda wakujiweka sawa. Kubali kuishi na watu, ili upate pesa
Ukianza biashara, ikichanganya, unawatoa wapangaji wako, unaendelea kuishi peke
yako.” Kama mwanga ukamulika kichwa chake.
“Umenifungua dada yangu. Maana
ndugu zangu waliniambia niuze.” “Hapo ndipo utakapochemka mara 100. Nyumba ni
kitu ambacho hakishuki thamani. Usiuze. Pangisha. Na mimi nitakuwa mteja wako
wa kwanza.” Wote wakacheka. “Sikutanii. Si nimekwambia natafuta pakuishi? Ndio
niwekee chumba.” “Tena umenipa wazo zuri hivyo! Wewe nakupa chumba chenye bafu
na choo chake kabisa. Cha nje, ujitegemee.” “Hayo ndio maneno.” Nanaa
akachangamka, tumaini jipya likachipua.
Yule dada naye akamshukuru
Nanaa, wakabadilishana namba za simu na kupeana sasa majina. Akamwambia anaitwa
Fridah, lakini watu wamezoea kumuita Fifi. Wakakubaliana kuishi pamoja,
wakitoka pale. Waliruhusiwa siku moja. Nanaa akamwambia atahamia kwake siku
inayofuata.
Kuliko Ungua Mpini.
Zilishapita siku zaidi ya 35
tokea Nanaa atoke hapo nyumbani. Alirudi akiwa na nguvu sio kama alivyoondoka.
Akapita ndani pale getini kusalimia walinzi. “Sisi tulijua umeondoka dada.”
Nanaa akacheka kinyonge. “Nilikuwa hospitalini. Mna ujumbe wowote wa kwangu?”
“Walileta watoto mara mbili, naona baada ya kukukosa. Wameacha.” “Haya.
Asanteni.” Nanaa akataka kupita. “Kulifungwa. Tukaambiwa tukae na fungua kama
utakuja kurudi. Ziko hapa.” Nanaa akarudi kuzichukua akaelekea ndani.
Akaingia stoo. Akatoa vitu vyake
vyote na kuviweka sebuleni. Akaanza kufungasha taratibu. Madaftari kuanzia yupo
chuo mwaka wa kwanza, yalikuwepo hapo. Akacheka. “Kweli shule ndio utakuwa mkombozi wangu. Sasa hivi ni muda wa kuingia
kazini.” Aliviambia vyeti vyake. Akakusanya kila kitu chake. Hakuacha hata
kimoja.
Vyote alivyokuwa amenunuliwa na
Geb, akabeba. Akachukua na mabegi ya Geb aliyokuwa akisafiria. Akapanga vitu
vyake humo. Akaingia chumba alichokuwa akilala mama G na wanae. Akachukua nguo
moja moja za watoto wake. Nazo akabeba. Usiku kucha alikuwa na kazi yakupanga,
kusafisha na kuchoma moto vitu ambavyo hakuvihitaji tena.
Wakati panapambazuka, akawa
amemaliza. Kila kitu chake kikawa kipo mlangoni. Akaingia kuoga, akatoka akawa
amekaa anawaza. Akaamua kumuandikia ujumbe Geb.
Barua Kwa
Geb.
“Geb mpenzi wangu,
nimekukosea sana. Najua hakuna jinsi unaweza hata kunisikiliza tena, lakini
naamini ipo siku Mungu atakupa rehema yakunisamehe. Nashukuru kwa kuniruhusu
kuendelea kuishi hapa, lakini Geb, kumbuka hii nyumba tulihamia mimi na wewe.
Wote wawili ndio ilikuwa mara yetu ya kwanza kuhamia hapa. Nakumbuka usiku wetu
wa kwanza chumbani kwetu, ulinisistiza na kuniomba nikutengenezee ‘home’.
Ukasema hili jengo halina maana kama sisi wote hatutakuwepo humu ndani na kama
hakutakuwa na amani. Nakiri kuivunja hii nyumba kwa mikono yangu mimi mwenyewe.
Sina chakujitetea. Nakutetea hata mbele za Mungu, ulifanya kwa nafasi yako.
Tena kiuaminifu sana. Sijawahi pata mapenzi kama uliyonipa Geb. Nakiri, na
ninakutetea mbele za Mungu, hata mbele za watoto wetu hapo baadaye. Hakika huna
hatia Geb. Upo sahihi kuniacha.
Nimeshindwa kutimiza jambo kubwa nililokuwa nimekuahidi Geb,
lakini nakuahidi kukuombea. Nimetubu. Na nitaendelea kutubu kwa kutokukwambia
ukweli wote na kuishia kukuumiza mpenzi wangu. Najua Mungu atanisamehe na
kunisikiliza. Nimeambiwa unatafutiwa mke ili uoe. Nakuahidi kukuombea
mpenzi.
Nitakuombea bila
kuchoka ili Mungu akupe mwanamke atakayekupa yale yote niliyoshindwa mimi
kukupa. Na asikuumize kama nilivyokuumiza mimi. Nakuombea faraja na amani ile ipitayo
fahamu zote, ikufunike Geb. Najua unaweza ukaona haitawezekana kwa yale
niliyokusababishia. Lakini Geb, Mungu yupo. Jipe muda tu, ipo siku Mungu
atarejesha furaha yako kwa upya.
Hili jengo na vitu vyote vilivyomo humu ndani ni vya thamani
sana. Lakini haviwezi kukamilika kama wewe na watoto hampo humu ndani. Sitaweza
kuishi humu ndani peke yangu. Hata hivyo naona itakuwa mateso makali zaidi kwa
Liv. Analia sana akiniona. Anataka nimshike, wakati umeweka masharti magumu
sana kati yangu na wanangu, Geb.
Ni heri niondoke wazoee kuwa hawana mama, kuliko hivyo
wanavyolia nakushindwa kuwabembeleza wanangu. Inaniuma kuliko nitakavyokueleza.
Unajua jinsi nilivyokuwa nikiwazaa kwa shida. Ilikuwa kufa na kupona
ili wao wazaliwe. Sikubahatika kuwa na mama. Ningependa wanangu wanione. Lakini
sio kwa mateso kwa kiasi hicho Geb. Sitaki wanangu walipe garama ya kosa langu.
Ni heri niondoke tu. Naamini Mungu atawasaidia kwa namna nyingine.
Sitarudi tena hapa. Kuwa huru kuuza tu. Najua hutaweza kuja
kuishi tena humu kwa yale yaliyotokea humu ndani. Hata mimi sijaweza kupata
usingizi tangu usiku ule. Imekuwa mateso matupu. Kwa hiyo kuwa huru kufanya
chochote na hii nyumba yako. Mimi nakwenda kuanza upya, sehemu nyingine. Hakika
nakushukuru Geb. Asante kwa mapenzi ya kweli uliyonipa. Nakuombea kila la
kheri. Mungu akujalie hekima ya kuwalea watoto wetu vizuri. Mungu azidi
kukufanikisha katika kila eneo la maisha yako.
Nanaa.
~~~~~~~~~~~~~
Machozi yalikuwa yakimtoka
Nanaa. Simu ya Fifi ndio iliyomtoa kwenye majonzi wakati anarudia kusoma barua
yake. “Unalia tena?
Mbona ni kama tuliwekeana mikakati yakutokulia tena!?”
Nanaa akacheka kidogo. “Shikamoo
dada Fifi.” “Marahaba mdogo wangu. Sasa ndio kumekucha. Inakuaje?” “Nishamaliza
kuweka kila kitu. Hapa nataka nikaite taksii ije inichukue mimi na mizigo
yangu. Inilete kwako. Ushanitayarishia chumba?” Nanaa akamuuliza. “Ndio ilikuwa kazi ya usiku kucha. Ujue ni
chumba alichokuwa akiishi yule kijana! Sijawahi kukifungua tokea tuwazike. Mama
yake alikuja akachukua vitu vyake, nikakifunga.” Nanaa akatulia asijue asema pole au afadhali.
“Wewe Nanaa?” “Nipo nakusikiliza dada yangu.” “Sasa usafiri
utapata wapi? Maana mwenzio tokea mume wangu apate ajali, sijarudi kuendesha.
Nina gari liko hapa. Nina kazi ya kulipasha moto tu lisiharibike. Kuna kijana
anakuja kulichukua, analiendesha kidogo, na kulirudisha.” “Bwana njoo unichukue
dada Fifi, acha mambo yako!” “Nimeingiwa hofu mwenzio. Sitaki kuendesha.”
“Tulizungumza nini na wewe unafanya nini sasa?” “Hatua ndogo ndogo kama za
mtoto mchanga, Nanaa mdogo wangu! Ni jana tu umenitoa kule hospitalini. Leo
unataka kuniingiza barabarani!” “Acha kujilalamisha dada Fifi bwana! Njoo unichukue.
Nitakulipa. Badala nimlipe dereva taksii si heri nikulipe wewe usie na pesa.”
Akamsikia anacheka.
“Unakuja?” “Nanaa akianza jambo! Basi nakuja. Lakini ujue
mwendo wangu utakuwa kama kinyonga!” “Wewe hata ukifika usiku wa kesho. Wewe
njoo tu.” “Haya ndio mambo. Basi nisubiri.” Wakaagana.
~~~~~~~~~~~~~
Akaendelea kuweka kila kitu kwa
usafi ili asipaache pachafu. Alishafua mashuka ya kitandani kwao. Akaacha
chumba kisafi lakini hakina nguo zake wala za Geb. Geb alishahamisha vitu vyake
siku ile ile alipokuja kuchukua watoto wake.
Baada ya kama lisaa, Fifi akampigia simu amuelekeze nyumba
ilipo. Alikuwa karibu tu. akamuelekeza mpaka akafika pale. Alimkuta Nanaa
getini akimsubiria. Akaomba afunguliwe Geti. Fifi alitoa macho baada yakufika
pale.
“Acha utundu dada Fifi!” “Kumbe
ulikuwa unaishi ikulu!?” Nanaa akacheka. “Twende ukanisaidie kutoa mizigo.
Halafu unagari nzuri hivi! Lazima kulifanyia kazi.” “Yaani tumelinunua mwaka
ule ule aliokufa mume wangu! Lilikuwa bado jipyaa! Utaona ndani.” “Basi huyo
mumeo huko atakuwa anasikitika sana!” “Usiseme hivyo Nanaa! Kwanza kwa nini?”
“Si umemvunja moyo! Yaani amekuacha pazuri, ukajigeuza omba omba! Aibu zako
dada Fifi.” “Kufiwa kubaya Nanaa wewe.” “Pole dada yangu. Mimi nakuchangamsha
tu.” Wakasaidiana kupakia mizigo ya Nanaa ndani ya gari mpaka wakamaliza.
“Nisubiria hapo nje getini.
Nataka kuzungumza na hao walinzi kabla sijaondoka.” Nanaa aliongea huku
akifunga milango. “Lakini nataka uhakika Nanaa. Kweli unatoka kwenye nyumba
kama hii unahamia kwenye chumba kimoja! Kweli!” “Hapa si kwangu dada. Na mimi
nilipakuta, na kupashangaa hivyo kama unavyoshangaa wewe. Halafu sijaweza
kulala humu ndani tokea nifanyiwe ule unyama. Silali dada. Nakesha nikizunguka
humo ndani kwa hofu. Sitapaweza. Uzuri huo ni wa macho tu. Nikiendelea kulala
hapo, nitakufa siku si zangu. Acha nikaanze upya dada. Ipo siku na mimi
nitakuwa na kwangu. Hata hivyo nimechelewa tu. Nilitakiwa niwe nimeshafika
mbali.” “Bado mdogo sana Nanaa. Utafanikiwa tu.” “Amina dada.” Fifi akatoka.
Nanaa akarudi getini.
Akawakabidhi funguo. “Naomba niwashukuru kwa heshima mliyonionyesha tokea
nahamia hapa mpaka leo. Naona sina kitu chakufanya hapa. Nimeamua kuondoka.”
“Unaacha jumba lote hili dada!” Nanaa akacheka. “Tumeambiwa tukulinde.” “Sina
chathamani chakulindwa baba yangu. Nimepoteza kila kitu. Acha nikaanze upya.”
“Nakuombea heri mama. Mungu awe nawe.” “Amina baba yangu.” Wakazungumza kidogo
tena. Nanaa akaacha funguo na barua akatoka, akijua wote wanajua yaliyompata.
Maana mmoja wao ndio alikuja kumfungua siku aliyobakwa. Akajua japokuwa
wanabadilishana, lakini lazima habari zimeenea. Akaondoka.
~~~~~~~~~~~~~
Haikuwa nyumba kama ya Geb,
lakini si pabaya hata kidogo. Walijenga nyumba yao mitaa ya Kawe, njia ya
kwenda Mbezi. Ilionekana bado ni nyumba mpya tu. Lakini hapakuwa hata na ua
moja wala ukoka hapo nje. Nyumbani kwa Geb palikuwa kijani haswaa. “Heee! Mbona
pakame hivi kama jangwani? Huna maji?” “Tulichimba kisima. Nina maji mpaka
yanatoka kwenye shawa. Utaoga mpaka uchoke.” Nanaa akacheka.
Wakaingia ndani kwenye geti. Nyumba
ilizungushiwa uzio mzuri tu, lakini mfupi. Uliweza kuona kila kinachoendelea
ndani. Nanaa akapelekwa mpaka kwenye hicho kinyumba cha nyuma ya hiyo nyumba
kubwa. “Na huo upande mwingine nani anaishi?” “Nakwambia hamna mtu.” “Na pako kama
hapa?” Nanaa akaendelea hukoji baada ya kuonyeshwa sehemu yake. “Kama
unavyopaona hapa, ndivyo huko navyo kulivyo.” Nanaa akaweka mizigo yake yote
ndani.
“Njoo kwanza dada yangu.” Fifi
akasogea. “Japokuwa sijajua utanidai kiasi gani, lakini naomba nikushukuru.
Asante. Naona mwanzo wangu si mbaya.” Wakacheka. “Au utanipokonya kitanda?” Nanaa
akauliza. “Nipeleke wapi mdogo wangu? Hapa nataka kukwambia uchambue kile
kitakacho kufaa, usivyotaka tutoe nje.” “Mbona nakushukuru. Basi naomba
tumshukuru Mungu kwa mwanzo wetu mzuri.” Fifi akabaki amekodoa macho.
“Wewe unamwamini Mungu!?”
“Nisingefika hapa bila Mungu. Alikonitoa huyu Mungu! Huwezi amini.”
“Umenisimulia. Sasa lakini alikuwa wapi wakati unabakwa?” Fifi akauliza. “Pale
pale alipokuwepo wakati namdanganya Geb. Alikuwa pale pale wakati
akinisisitiza nimwambie Geb ukweli wote nikashindwa. Alikuwa pale pale alipo
wakati napanda gari na kwenda kwa Malii. Nikamvulia nguo huku nikijua
wazi nazini. Hajawahi kuhama. Mungu wangu yupo pale pale dada yangu.
Yote niliyoyapata, yananistahili kabisa. Sina hata wakumlaumu dada Fifi. Hakika
sina. Hujui ni kwa kiasi gani nilisukumwa kumwambia Geb ukweli wote, lakini nikapinga.
Nimetubu. Naamini nitasamehewa tu.” Fifi alilia.
“Ninaadhibu watoto wangu kwa
kushindwa kumtii Mungu. Dada Fifi, mimi namjua Mungu kwa kumuona
akinitendea mambo ya ajabu. Namfahamu Mungu si kwa kumsoma tu. Amejidhihirisha
kwangu mara kadhaa. Ameniokoa mara kadhaa kwenye shimo la mauti. Leo nipo hapa
kwako, si kwa bahati mbaya, ni kwakuwa nimekaidi, dada. Wanangu wanalia
kwa sababu mimi nilikaidi. Nimemuumiza mwanaume mwenye mapenzi ya kweli, kwa
kuwa mimi nilikaidi dada. Kwa hiyo, usiwe na wasiwasi juu ya uwepo wa Mungu
wangu. Yupo.” Nanaa aliongea taratibu lakini kwa uchungu sana.
“Hata kukutana na
wewe, si kwa bahati mbaya dada. Najua alikuandaa makusudi kwa ajili yangu.
Unaweza usielewe, lakini nina uhakika nipo sehemu sahihi. Acha nimshukuru kwa
kuwa najua hajaniacha.” Nanaa akafuta machozi.
Ilikuwa bado ni asubuhi tu, wakati wanashikana mikono na
kuomba pamoja. Fifi alimsikia Nanaa akiomba sala fupi tu. Lakini alishukuru kwa
machozi, huku akiombea watoto wake na Geb. “Warehemu watoto
wangu ewe Mungu wangu. Nawaombea faraja, wao na baba yao. Sijui utafanyaje,
lakini ile faraja inayopita fahamu zetu, ndio ikawe juu yao. Watunze, mfariji
Geb wangu. Mpe hata yale ambayo hajui kama anayahitaji.” Nanaa
akaendelea kidogo. Akamuombea na Fifi, wakamaliza.
“Mmmh! Mpaka umenisisimua!” Nanaa akacheka. “Sasa
mwenzio nataka kuandika.” “Unaandika nini tena?” Fifi akauliza na kujirusha
kitandani. Palikuwa hata hapajatandikwa. “Naanza kuandika barua za kuomba kazi.
Lakini dada, nina wazo.” “Lete mawazo yako. Nimeshaanza kukuogopa Nanaa.” “Acha
hizo bwana!” Wakataniana kidogo, Nanaa akaendelea.
“Mwenzio ni mjuzi sana
wakupika.” “Unataka tufungue hoteli?” Fifi akamdaka. Nanaa akacheka sana. “Kwanza
nimefurahi ulivyojiweka na wewe. Naona akili imetoka likizo.”
“Nilijichetua tu, mdogo wangu. Lakini mimi muhangaikaji sana Nanaa. Usinione
hivi.” “Basi kama ndio hivyo mbona tushafanikiwa? Tutafute mahali tufungue
sehemu yetu. Jumatatu mpaka ijumaa. Siku za jumamosi na jumapili, tuwe
tunatafuta tenda, tunafanya catering.” Fifi akakaa.
“Wewe mtoto kabila gani?”
“Bwana dada Fifi acha utani! Nataka kutengeneza pesa ili niweze kulipa kodi.
Sitaki niwe nakukimbia.” Wakacheka. “Wazo zuri sana. Lakini shida ipo kwenye
mambo mawili. Mimi si mpishi mzuri. Zaidi yakusonga ugali na kupika wali, hamna
ninalojua.” Nanaa akacheka.
“Sikutanii Nanaa! Mume wangu
alikuwa anapika vizuri kunishinda mimi. Mwenzio nilitoka kwenye familia
yakusoma tu. Kazi za ndani tulikuwa hatufanyi.” “Wewe usiwe na wasi wasi
utajifunza tu. Ni rahisi sana. Haya nipe tatizo jingine.” “Pesa. Mwenzio si
nimekwambia sina hela?” Fifi akajitetea.
“Kwanza nakulipa kodi yako ya
miezi 6. Hata leo ukitaka twende kwenye ATM, au nakurushia. Halafu kabla
hatujaweka vikwazo vingiii, tutafute eneo. Tujue garama zote. Au tunaweza
kuanza kwa kufanya catering. Tukaanza kupika humu humu ndani, tunapeleka kwenye
shuguli za watu. Hasa kitchen paty ndio wengi wanapenda vitafunwa. Tuandike.”
Nanaa akavuta karatasi.
“Sambusa, vitumbua, chapati,
bajia, kalumati, kachori na maandazi.” “Vyote hivyo unaweza kuvipika!?” “Ndiyo.
Na wewe nitakufundisha. Halafu wateja wetu wa kwanza ni wale wale wateja wako
uliokuwa ukiwasambazia vifaranga wewe na mumeo. Leo utawapigia simu wote,
utawaambia umebadili biashara. Sasa hivi unafanya Catering. Usisahau hao ndugu
zako wasomi.” “Sasa wakisema wanataka tuwapelekee sample?” “Mbona unakuwa na
vipingamizi vingi hivyo?” “Nauliza tu
mdogo wangu! Tusije tukatangaza, halafu tukaishia kuonekana wote machizi.”
“Basi anza kutuma ujumbe sasa hivi tukusanye oda. Halafu tupike, waambie kesho
tutawapelekea maofisini wakaonje.” Fifi akabaki amemtolea macho Nanaa.
“Mbona unaniogopesha Nanaa wewe!
Umechangamka!” Nanaa akacheka. “Sasa ujumbe usemeje?” Nanaa akavuta karatasi,
akaandika. ‘Tunatoa huduma ya
kusambaza bites. {Sambusa, bajia, maandazi, chapati, kachori, kalumati na egg
chop}. Kwa ajili ya sherehe kubwa na ndogo. Tutatoa chai na kahawa pia.
Tunaweza kukuletea ofisini, kwa mlo wa kila siku au hata kwenye vikao na
majumbani. Tutakuletea popote ulipo kwa oda kuanzia elfu 50 na kuendelea.”
Akamsogezea
ile karatasi Fifi. Hebu soma. Halafu uongeze na wewe. Fifi akasoma nakumtizama
Nanaa. “Una friji?” Nanaa akamuuliza. “Ndiyo. Lakini chafu.” Fifi akajibu. “Haya
twende tukaioshe, wakati unapigia watu simu na kusambaza ujumbe. Ukimaliza,
tunaenda kununua vitu.” Fifi na Nanaa, wakachangamka kweli kweli. Matumaini
yakawajia. Mpaka inafika jioni, walikuwa na tenda zakupeleka kesho yake
maofisini.
“Nanaa wewe!” “Lazima
kuchangamka dada. Mimi nimeona jinsi watu wazima wanavyomuheshimu yule baba
watoto wangu. Kijana mdogo lakini akiongea watu wanamsikiliza. Akikaa mahali,
utajua pesa ipo. Kwa kuwaza tu. Akanifundisha kuchukua hatua pia. Anasema yeye
kila wazo analifanyia kazi. Sikudanganyi dada Fifi, yule kaka anapesa. Kuna
mahali nilienda naye, wafanyakazi wa benki, wanao zijua akaunti zake,
walisimama wanaume wale wakawa kama wajinga mbele yake. Na usifikiri anafanya
mambo ya ajabu! Ni kuwa makini tu. Sasa tuanze kazi dada yangu. Heshima
haiombwi mjini.” Wakacheka. “Mbona
nakushukuru mdogo wangu! Mwenzio watu walikuwa wananikimbia.” Usiku huo huo
wakaanza kazi wakiwa wameshanunua kila kitu, mpaka lunch boxes zakufungia
vitafunio hiyo kesho yake.
Huku Nyuma
Nyumbani Kwa Geb.
Jeri alipita tena kuleta watoto. Lakini mlinzi akamwambia
akiwa pale pale getini. Kuwa Nanaa ameondoka rasmi. Na ameacha barua.
Akakabidhiwa hiyo barua aliyokuwa amemwandikia Geb, na kugeuza baada ya
kuzungumza kidogo, wakiteta. Wala Geb hakuhamia mbali. Walirudi kuishi pale
walipokuwa wakiishi zamani na mama yake.
Muda huo huo wakamuona
anarudisha tena watoto. Bibi yao akatoka. “Hajarudi tu!?” Akauliza baada
yakuwafikia kwenye gari. “Wamesema ameondoka moja kwa moja. Amewaaga kuwa
hatakaa arudi tena pale. Kumbe ule mwezi aliopotea pale, hakuwa kwa wanaume
bibi. Alikuwa hospitalini amelazwa.” Mama G akatulia kidogo kama anayefikiria. “Ameacha
na barua hii hapa, amesema apewe baba yao hawa.” “Nipe mimi hiyo barua. Halafu
niachie mimi nitazungumza kila kitu na baba yao. Wewe usimwambie chochote.
Nimemtafutia mwanangu binti mzuri. Ametulia na atamfaa tu. Mwache aende zake,
kwanza Geb hamtaki tena.” “Sawa.” Jeri akamkabidhi hiyo barua, akasaidia
kushusha watoto, akaondoka zake.
Geb alirudi kutoka kazini. Akamkuta Liv amekaa kwenye kochi
ametulia kama anaangalia tv. Akamgeukia baba yake, akarudisha macho kwenye tv.
Wala hakuchangamka. “Walipelekwa kwa mama yao?” “Na leo pia hawakumkuta.” Mama
G akajibu kwa ufupi tu akificha ukweli wote. Geb akanyamaza. Akaenda kukaa pembeni
ya Liv. Akaendelea kuangalia cartoon na mtoto wake.
~~~~~~~~~~~~~
Mrembo aliyekuwa ameletwa hapo
na mama G, kama msaidizi wa watoto, Sara, akatoka na glasi ya juisi. “Pole na
kazi.” Akatoa salamu kwa Geb. “Asante.” Geb akajibu huku macho yako kwenye luninga.
Akavuta stuli, na kumwekea ile juisi. “Karibu.” “Huyu anakula nini? Mbona kama
amekaa tu hapa?” Geba akauliza akimaanisha
Liv. “Anavyoringa huyo mwanao! Haambiliki. Anataka tufanye vile
anavyotaka yeye.” Moyo ulimpasuka Geb, akamtizama Sara. Ni Liv wake!
Mama G aliposikia lile jibu,
akatoka kwa haraka kule jikoni. “Ameshakunywa maziwa, natengeneza chakula chao
cha usiku.” Akamuwahi Geb kabla yule msichana hajaendelea. “Wala hakuyanywa!
Karudisha chupa jikoni.” Sara akamalizia nakurudi jikoni. “Atakula chakula cha
usiku. Atakuwa sawa tu.” Mama G akajaribu kupoozesha.
“Liv!” Geb akamuita. “Unataka
kula nini?” Akamwangalia baba yake, nakurudisha macho kwenye luninga. “Unataka
nikupakate?” Geb akaendelea kumuuliza taratibu. Liv akasimama, nakwenda
kumkalia baba yake. Akalala muda ule ule akiwa ameshikilia mtandio aliozoea
kujifunika ili anyonye kwa mama yake.
Geb akamwangalia. Akamuweka sawa, akavuta rimoti akabadili
channel ya tv. Kutoka pale walipokuwa wamemuwekea Liv, akahamisha kwenye mpira.
Wakabaki kimya pale kwenye kochi. Mama yake akatoka. “Kunywa hiyo juisi.” “Huyu
amelala. Alikula kweli mchana?” Geb akauliza. “Amekula vizuri tu.” Sara naye
akatoka jikoni, akajibu yeye.
“Naomba nikamlaze chumbani.”
“Mwache kidogo.” Geb akajibu huku akimwangalia mtoto wake kama anayetaka muda
naye zaidi. “Ameking’ang’ania hicho kimtandio, kama nini sijui! Kila
anapokwenda anacho. Na ukitaka alie, mpokonye.” Sara akaongea kama utani huku
akikaa kochi la pembeni. “Angalia nisije nikaunguza.” Mama G alimkatisha
nakumtaka arudi jikoni. Alishaona anakoelekea ni kumtibua Geb “Na unavyopika
vyakula vingi, kama hotelini!” Sara akasimama kurudi jikoni. Hakuna
aliyejibu.
~~~~~~~~~~~~~
Kalikuwa kabinti kazuri sana
kwa muonekano. Ndio alikuwa amemaliza chuo kikuu cha Mzumbe, mjini Morogoro.
Aliitwa Sara. Mzuri. Msafi wa mwili wake. Alikuwa mdogo kidogo kwa Nanaa. Bado
alionekana ni binti mchanga. Mwili haujapitishwa kwenye uzazi wala majukumu
mazito. Mama G alifahamiana na shangazi yake. Alipomweleza balaa la Nanaa,
ndipo shangazi mtu akamuelekeza kwa huyo mtoto wa kaka yake.
Akamwambia ni binti aliyetulia
na yupo tu nyumbani anasubiri matokeo yake. Anaishi na wazazi wanaoeleweka na
wana uwezo mzuri tu. Kwa hiyo huo ndio muda wa kuwaunganisha vijana wao. Aende
pale kama kuwalea watoto, huku wakisomana tabia na Geb. Ndipo mama G akamtuma
aletwe.
Ilishapita week moja tokea
aletwe hapo wakati Nanaa amepotea, hajulikani alipo. Kumbe yupo hospitalini.
Geb alimkuta humo ndani, hakuuliza. Mama G akamtambulisha kwa Geb nakumwambia
yupo pale kumsaidia swala la watoto. Naye Sara akasema anapenda sana watoto.
Huwa ni kitu anafanya kwa furaha zote. Geb akasikiliza, nakunyamaza tu. Sara
alianza kwa mbwembwe zote, lakini akakutana na Liv. Kichwa kama ya baba yake!
Hapo ndipo Sara alipoanza kuchoka.
~~~~~~~~~~~~~
Mama G akamfuata jikoni.
Akamsaidia kutayarisha vyakula, akavitoa pale. Wakati anatoka na vyakula, Geb
naye akawa anasimama na mtoto wake. “Mbona unaondoka na chakula tayari?” Sara
akamuuliza Geb. “Au utarudi? Maana kishaiva.” Kimya. “Ungekula kwanza ndio
ukalale. Usilale bila kula.” Geb akamtizama bila yakumjibu kitu, akapitiliza
chumbani kwa mama yake. Alimbadilisha nguo mtoto wake, akamlaza kitandani. Mama
yake akamfuata. “Naona huyu hataamka tena mpaka kesho.” Geb akaongea huku
akimfunika vizuri binti yake. “Chakula kipo tayari.” Mama yake akaongeza.
“Nilikuwa na kikao na mtu
sehemu wanayouza chakula. Nikala. Kwa hiyo nipo sawa tu.” Geb akajibu na
kuuliza. “Magesa ataamka tena?” “Amekula ndio akalala. Hapo tena mpaka usiku,
ndio ataamka tena, anywe maziwa, arudi kulala mpaka asubuhi.” Mama G akajibu. “Vipi
maziwa hayo uliyombadilishia? Anayapenda?” Geb akauliza. “Sana tu. Yaani huyo
mdogo anakula bila shida. Akianza kuvuta chupa yake, kama mchwa! Lakini si huyo
dada mtu. Anafanya anachotaka yeye, na anakula akitaka. Kama leo nzima alikuwa
kisirani! Bibi yake akasema labda apelekwe kwa mama yake. Ndio kumkosa mama
yao, akarudi nakujiweka kwenye kochi mpaka kapitiwa na usingizi. Lakini watoto
wanabadilika. Nikumpa tu muda. Bado mdogo huyo. Atasahau tu mateso ya mama
yake.” Sara aliingia na kujiweka kitandani kwa mama G huku akiongea. Wote
wakanyamaza.
“Sasa mimi naenda kula chakula
changu chumbani. Kuna tamthilia yangu huwa naifuatilia. Ndio mida yake hii.
Nitakula huko huko na kulala. Nitaosha vyombo kesho. Leo siwezi tena. Kwanza
nimechoka.” Sara akasimama nakutoka pale chumbani. “Atakuwa kweli amechoka.
Anajituma kweli!” Mama G aliongea, akionekana hata hoja yake haina nguvu. Geb
hakujibu kitu.
Maisha Ya Nanaa.
Biashara ikamchanganyia Nanaa.
Akawa busy, hana hata muda wakupumzika. Akimaliza kupika usiku na kutayarisha
vitu vya kumalizia kupika asubuhi yake, anakuwa amechoka sana. Hoi kitandani
tayari kwa asubuhi kumalizia kupika ili wakasambaze maofisini kabla muda wa
kunywa chai kupita. Pesa ndogo zikawa haziwapigi tena chenga, yeye na Fifi kitu
kilichomuongezea morali Fifi, kwani alifanikiwa kuacha kukopa hovyo hovyo.
Hakuna aliyekuwa akimsikia kwa shida ila kuwauzia vitafunwa.
Urafiki kati yake na Nanaa
ukanoga. Hakuacha kuomba na Nanaa. Mwezi wa pili akiwa anaishi na Nanaa,
akaamua kuhama nyumba kama alivyoshauriwa na Nanaa. Akaikodisha nyumba kubwa,
akahamia nyumba ya uwani pembeni ya Nanaa. Huko ndiko walipokuwa wakikesha kwa
kufunga sambusa na kuongea.
Hakuna
Msiba Usiokuwa Na Mwenzie.
“Nikwambie kitu d ada
Fifi?” “Niambie tu.” “Lakini usianze kushituka kama kawaida yako.” Fifi
akacheka. “Sema bwana. Tumepata dili nyingine nini? Maana mtoto wewe kwa pesa!”
Nanaa akacheka kinyonge. “Unajua huu ni mwezi wa tatu tokea nikwambie
nimebakwa?” Fifi akatoa macho. “Usiniambie una mimba!!” “Acha tu dada yangu.
Sijui nitafanyaje. Nilijihisi tokea mwezi wa pili. Lakini nikajipa muda.
Unakumbuka leo wakati tunatoka posta kupeleka mzigo?” “Pale uliponiambia
tusimame duka la madawa ndio ulikuwa unanunua kipimo!?” Nanaa akacheka.
“Dada Fifi unaakili ya haraka
yakufikiria! Mpaka unaniogopesha.” “Mtoto mbaya wewe! Sasa ulikuwa ukinificha
nini? Ndio maana nimekuona tokea asubuhi huna raha!” “Naogopa dada.” “Wala
usiogope mdogo wangu. Atakua tu.” “Hilo sina wasiwasi nalo. Ila sikutaka mtoto
wakubakwa dada. Au niseme sikutaka kuzaa na yule mwanaume. Halafu mimba yangu
ya mwisho ilikuja na presha mbaya sana. Ilinibidi kulazwa mpaka nilipojifungua.
Sasa nafikiria, sijui itakuaje?” “Hapo nakuelewa. Lakini Nanaa, huko usiwaze.
Wewe si unamwamini Mungu? Basi amini na hilo liko ndani ya mapenzi yake.
Atakupigania tu.”
“Angalau umenituliza. Lakini
nimekuwa nikisita kweli kwenda kuangalia afya yangu. Malii alikuwa mchafu sana.
Hakuna mwanamke anampita.” “Wewe usijipe presha buree. Ukaanza kuugua. Tulia.
Ukianza kliniki, utajua yote.Watakupima kila kitu. Hatua moja umeshaifanya.
Ushajua mtoto yupo. Yaliyobaki mwachie Mungu.” Nanaa akanyamaza. “Tena unaweza
kuta huyo mtoto ndio akawa faraja yako.” “Mmmh dada!” “Kweli tena. Si unasema
umepokonywa watoto wewe? Basi huyo atakufaa.” Nanaa akaamua anyamaze.
~~~~~~~~~~~~~
Hakuna siku iliyopita asiache
kuwakumbuka wanae na kuwaombea. Tayari hofu ya kuzaa na Malii ikawa imemkamata
kupita kiasi. Hakuwa akiweza kulala vizuri. Lakini hakutaka kumuonyesha Fifi.
Ila alimuona wazi amebadilika. Muda mwingi alimkuta akifikiria. Vicheko
vilipungua kabisa kati yao. Nanaa akawa mtulivu wakupita kawaida yake. Akili
ilikuwa imemvurugika asijue tena chakufanya. Mipango yote aliyokuwa amejiwekea,
akaanza kuona hamna tena tumaini. Anazaa na Malii! Hicho ndicho kilikuwa
kikimuumiza. Heri angekuwa amebeba mtoto wa Geb. Hakukumbuka hata kuomba kazi
kwenye ofisi yeyote ile. Akabaki akipika vitafunywa. Nakusambaza maofisini huku
akiwa hajui hatima yake.
~~~~~~~~~~~~~
Mambo yanazidi kumuharibikia Nanaa. Mama G
amembadilikia kabisa na ameshamtafutia mwanae binti mchangaa! Alishajisifia wanae
hufanya kile anachotaka yeye.
Sasa Je, Safari hii ndoa kwa Geb
itafanikiwa baada ya kushindwa kwa Nanaa.
Nanaa yu mjamzito tena. Mori wote wa
maendeleo umemuisha.
Nini kitaendelea?
0 Comments:
Post a Comment