Ujauzito Wa Olivia
Nanaa
na Geb wakaendelea kula wakiwa hapo hapo kwenye makochi. “Umependa huo ugali?”
Nanaa akamuuliza. “Nimependa. Naona kweli wameupika sasa hivi. Bado laini.” Geb
akaendelea kula, huku Nanaa akiendelea na yeye kula kwa mara ya pili.
“Nimefurahi unakula tena.” “Nahisi nilikuwa nimekasirika tu. Sasa hivi naona
hali imerudi ileile! Na mpaka nijifungue, nahisi nitanenepa mpaka nitapasuka.”
Geb akacheka. “Kwani kwenye mimba ya
Liv hukuwa ukila? Nilikuona ulikuwa
umekonda sana.” “Kipindi cha ujauzito wa Liv kilikuwa kigumu sana kwangu Geb.
Nilijitahidi kupambana kwa kadiri ya uwezo wangu. Kipindi kile mambo mengi
yalikuwa yakiendelea kwenye maisha yangu. Sikuwa nimetulia, ingekuwa ngumu
kunenepa.” Nanaa akatulia kidogo.
“Kwanza sikuwa na pesa ya kutosha. Au niseme
nilikuwa nikibania pesa ili Liv akizaliwa asipate shida. Halafu nilikuwa
nikijitahidi kula vyakula vya kunijenga afya yangu zaidi. Kwa hofu nisijekuwa
dhaifu nikashindwa kujifungua. Nikaishia kufa mimi au mtoto. Kwa hiyo sikuwa na
uhuru wa kujichagulia. Nilikuwa napika vitu ninavyojua mwili unahitaji huku
nikinywa dawa za virutubisho kwangu na kwa mtoto. Nyingine nilikuwa nikinunua
gali! Ni hizi za GNL za kina mama wajawazito. Lakini nilifanya makusudi ya
kuingia garama ili nisipatwe maradhi.” Nanaa akatulia kidogo, kisha akaendelea.
“Halafu ukumbuke nilikuwa nimebeba mimba ya Liv
nikiwa najua nimefanya kosa kama alilofanya mama yangu. Kuzaa bila makubaliano.
Kwa hiyo nilikuwa najilaumu huku nikijua umerudiana na Liz. Sikujua kama
utakuja kumkubali Liv. Kwa hiyo nilijawa wivu na majuto ya kupita kiasi.
Nilikuwa silali vizuri. Wakati mwingine nilikuwa nakuota labda unanibusu
shingoni nikiwa nimelala. Kama hivi nilivyozoea nikilala ubavu ubavu huwa
unanibusu huku shingoni au vile unavyokuwa ukinichora mgongoni taratibu. Basi
nilikuwa nikiota unanifanyia hivyo, nashituka kutoka usingizini, nashindwa hata
kulala tena. Kwa hiyo sikupata wakati mtulivu wakujifikiria sana. Nilikuwa
nakula chakula kama dawa kwa ajili ya mtoto.” Nanaa akaendelea.
“Na ukumbuke ndio nilikuwa mwaka wa mwisho.
Napambana angalau nimrudishie kaka cheti kizuri ili asione juhudi zake zilikuwa
bure. Niliogopa nisije kurudi na mtoto tu, tena asiye na maelezo yakutosha,
badala ya kumpelekea cheti kizuri. Kwa hiyo nilikuwa nikipambana kufa na kupona
na masomo huku nikijitahidi kumfariji Liv huko tumboni asihisi hayupo sehemu
sahihi. Wakati wote nilikuwa nikizungumza naye na kumwambia namsubiria kwa
hamu. Wakati hata sikuwa nikijua kama ni wakike au wakiume! Jina sikuwa nalo!
Wala sikuwa nikijua pa kumuweka baada ya kuzaliwa. Nilijiambia kila kitu
nitakitatua kila kinapojitokeza. Sikutaka kuanza kujipanikisha nikashindwa
kufanya mambo yanayonikabili kwa wakati ule. Kwa hiyo kwa kujibu swali lako,
sijui hata mimba ya kwanza ilikuwaje. Sikuruhusu sijui vile viugonjwa vya mimba
vijitokeze au sijui nataka kula sijui nini! Sijui nina hamu ya nini! Hapana.
Kile nilichojua kitamfaa mwanangu, kililazimishwa kupita mdomoni na kukaa
tumboni bila kutapika.” “Pole. Lakini nashukuru Mungu umenizalia binti mzuri
sana. Oliva ni mtoto wa ajabu sana. Huwa natamani muda wa kumuweka kifuani
kwangu ufike. Halafu ajifiche kwenye shingo yangu huku amenikumbatia na
vimikono vyake!” Nanaa akacheka.
“Yaani Nanaa, sijawahi kupata hiyo furaha moyoni.
Mtoto mtamu bwana! Asikwambie mtu.” “Tena umelea mwenyewe!” Nanaa akaongeza.
“Bwana mtoto huyu akaniita na kunitafuta baba yake mapemaaa. Yaani alipozaliwa
tu, akaona amtafute baba yake. Nikamfuata mpaka Mlimani kule! Hakuna jinsi
nikamweleza mtu furaha Mungu aliyonipa, akaelewa. Ni zaidi ya utajiri au ni
zaidi ya chochote Mungu alichowahi kunibariki nacho. Mbali na wewe lakini.”
“Nilikuwa nakusikiliza tu.” Wote wakacheka.
“Lakini Nanaa. Kesho lazima turudi nyumbani. Nina
mambo muhimu sana yakufanya ofisini.” Kimya. “Si tunarudi wote?” Geb akauliza.
Nanaa akabaki kimya kama anawaza kitu. “Naomba turudi nyumbani Nanaa. Tafadhali
sana. Twende tukapambane tukiwa pamoja.” “Tutarudi wote Geb. Kwanza wewe
mwenyewe umeshuhudia kuwa siwezi kuishi tena bila wewe. Mtu anagonga mlango tu,
nakupigia wewe simu!” Geb akacheka. “Kweli tena. Najiona sitayaweza tena maisha
bila wewe Geb. Ila nafikiria mahusiano yetu pale nyumbani. Naona yamevurugwa!
Zamani ilikuwa inatia raha kusikia unarudi nyumbani. Lakini sasa hivi! Sijui
itakuaje? Moyo unakuwa mzito kweli.” “Wewe ndio kiungo muhimu sana pale
nyumbani. Ukiamua wewe, utaweza kuwaunganisha tena wote. Au unaweza kuwavuta
tena pamoja. Sasa hivi wote wanaishi katika hukumu. Wanajua wamekusaliti. Au
wamesababisha kutofanikiwa kwa harusi yetu. Inawauma sana.” Nanaa akavuta pumzi
kwa nguvu akifikiria.
“Naomba simu nimpigie mama. Naona nianzie hapo
kwanza. Au unafikiri atakuwa amelala, ni usumbufu?” “Najua atafurahi sana
kukusikia. Ni wazo zuri sana. Na ninakushukuru Nanaa.” Nanaa akacheka kidogo. “Kweli.
Unafikiri wewe ukinuniana na mama G, mimi nitakuwa kwenye nafasi gani?”
“Yameisha Geb. Na nimekuelewa. Hata hivyo namuhitaji sana mama. Ona hapa
nilipo. Najua ningekuwa nimezungumza na mama wakati ule aliponipigia Mira, sasa
hivi tusingekuwa hapa. Najua angenishauri vinginevyo. Nimekimbia nyumba kwa
hofu tu. Mama ni mshauri wangu mzuri sana. Namuhitaji. ” Geb akampa simu yake.
Ukipenda Boga, Penda Na Ua Lake.
Nanaa
akampigia mama G. “Pole mama. Nimekuamsha?” “Hapa natamani
kuruka ruka. Sikutegemea kukusikia.” Nanaa akacheka. “Nilikununia hivyo ujue!” “Mbona hilo nalijua. Sasa hasira zimeisha?” Nanaa akacheka. “Nina hamu na
wewe ndio maana.” Mama G akaanza kucheka. “Kwanza asante kwa blangeti na mtori. Liv alikuwa anatetemeka kwa
baridi mpaka nikaogopa!” “Pole mwanangu. Naomba nisamehe.” “Yameisha mama
yangu. Hapa nilipo nina mambo kibao ya kukwambia. Naona hiyo kesho mbali.”
“Kwani mnarudi kesho!?” Mama G akauliza kwa mshangao.
Alijua labda Geb angekaa hapo kidogo na familia yake ili kumtuliza Nanaa.
“Geb ana kitu
cha muhimu kesho ofisini. Anataka kesho asubuhi tuwe tumeshafika Dar.” “Basi
nitakuja kuwapokea.” “Asante mama. Tutaongea zaidi tukionana.” “Haya mwananngu
Nanaa. Mungu azidi kuwatunza na kuwabariki.” “Amina mama yangu. Nikupe Geb?” Nanaa akauliza. “Nipe tu.” Nanaa
akamkabidhi simu Geb. “Pole na safari.” “Asante. Mambo
yote yakienda sawa, tutakuwepo hapo uwanja wa ndege wa Dar, saa tatu na nusu asubuhi.” “Sasa na
huyo mpenda usingizi!?” Mama G akauliza akimaanisha
mjukuu wake. “Itabidi kumuamsha tu. Atalala
tukifika nyumbani. Kuna mtu nakutana naye saa sita mchana. Lazima niwahi.”
“Basi mtakuta nikiwasubiri hapo uwanjani.” “Asante mama.” Geb akashukuru. “Karibu. Wewe na familia yako muwe na usiku mwema.” “Na wewe pia mama.” Wakakata simu.
Hakuna Deni.
“Kitu cha mwisho na chamsingi kabla hatujaenda
kulala.” Nanaa akamgeukia Geb kwa utulivu na umakini. “Naomba ujue sasa hivi hauishi
na mimi kwa kuwa nilimlipa mama mkubwa ile pesa.” Nanaa akainama.
“Ninapokuangalia wewe Nanaa, siioni ile pesa. Sifanyi mapenzi na wewe kwa kuwa najifidia
ile pesa. Hata kidogo.” Nanaa alipooza, akashindwa hata kuongeza neno. “Sikudai
na wala sitakuja kukudai wewe wala mtu yeyote yule. Naomba tusije wahi
kuizungumzua tena hiyo pesa. Maishani mwetu kote. Naomba isitajwe tena.
Ninapokutaka kimapenzi naomba uwe huru, kubali au kataa. Usifanye mapenzi na
mimi ukijidhania wewe ni mtumwa wangu. Sinunui penzi kwako Nanaa. Nakupenda.
Nataka uwe wangu wa milele. Si kwa pesa ila upendo wa dhati. Sijui kama
umenielewa?” “Nimeelewa na samahani.” “Basi. Ni hilo tu.” Geb akasimama. Nanaa
alimjua huwa hawezi kuweka kitu moyoni. Huongea. Akabaki ameinama pale kwenye
kochi.
~~~~~~~~~~~~~~~~
“Sasa leo itabidi kulala na Olivia. Hatujabeba
kitanda chake. Tukimuacha pale kitandani peke yake, tutamkuta chini ya uvungu.”
Nanaa akamgeukia mwanae aliyekuwa amelala ndani ya blangeti lililokuwa likimpa
joto. “Nikuulize kitu Geb?” Geb akageuka. “Uliza tu.” Nanaa na yeye akasogea
pale alipokuwa Geb, karibu na kitanda alicholala Liv. “Ulimwambia kaka?” “Ilibidi
Nanaa. Nilijua umekimbilia kwake.” Nanaa akanyamaza kwa muda.
“Hata
Grace na Danny wanajua. Nilikuwa nimechanganyikiwa. Ilibidi na wenyewe
kuwapigia simu. Nilijua ndio umenitoroka moja kwa moja. Hata hivyo sikutegemea
kama ungenipigia.” Nanaa akamtizama kwa mshangao. “Ni kweli Nanaa. Sikujua ni
nini alichokuwa amekwambia Mira! Sikujua
umeamini kwa kiasi gani! Nilijua utakuwa umenikasirikia kwa kukuficha.
Nikajiambia na hivi unayo pesa ya kutosha, itachukua muda mrefu sana
kunitafuta. Hakika sikutegemea kukusiki kwa mapema hivi. Eti unanifikiria mimi
niliyekukosea! Eti kunitoa tena wasiwasi! Sikutegemea. Nilishakuwa nimekata
tamaa.” “Nakupenda Geb.” Nanaa akaongea kwa upendo.
“Hilo nimelithibisha Nanaa. Na ndilo
nililokuwa nikilitafuta maishani mwangu kote kabla yako. Wengi wananipenda kwa
sababu moja au nyingine. Nafikiri nilikwambia. Kama sio pesa zangu, basi
watataka kuzaa na mimi ili wapate watoto kama mimi. Hakuna anayeweza
kunifikiria mimi kama wewe. Hata niwe nimekukosea vipi, wakati wote inapokuja
swala langu, unaweka hasira pembeni kwanza. Unahakikisha nipo sawa, ndipo
unaendelea. Nakushukuru kwa kunijali. Asante.” Nanaa akajisikia vizuri. Akatoa
tabasamu la mwito wa mapenzi.
Geb
hakumchelewesha. Hapo hapo wakahamia kitanda cha pembeni. Baada ya kufanya
mapenzi ya nguvu, Nanaa akalala hapo hapo kitandani. Usingizi mzito wa mimba,
ukamchukua. Hata hivyo alikuwa na siku ndefu iliyojaa hofu na vitisho. Mapenzi
aliyofanya na Geb mara alipofika na wakati huo, yalimtosha kulala usingizi
mzito. Geb akambusu mara kadhaa, kisha akamfunika vizuri. Yeye akahamia kitandani kwa mtoto wao ili
asianguke. Alibaki akimtizama Liv vile alivyolala vizuri. Akajikuta akicheka.
Hakusahau, akashuka kitandani, akapiga magoti na kuanza kumshukuru Mungu wake.
Akaomba kwa muda ndipo akarudi kulala.
~~~~~~~~~~~~~~~~
Olivia
alifungua macho, akamkuta baba yake akimwangalia. Akaanza kucheka. “Hata mimi
nilikuwa na hamu na wewe Liv.” Geb akambusu akiwa amelala pale pale kitandani.
“Pole nimekuamsha mama yangu. Lakini lazima tuondoke. Utalala vizuri nyumbani.
Sawa eeh?” Liv alicheka tena akiwa anaonyesha wazi bado ana usingizi. Ilibidi
baba yake amwamshe ili waondoke. Nanaa alikuwa akipata kifungua kinywa kwa
haraka. Alimka asubuhi na kuanza kulalamika njaa. Geb akamuagizia kifungua
kinywa wakati anakusanya vitu. Oliva ndio alikuwa wamwisho.
Waliondoka
jijini Arusha, kurudi jijini Dar. Geb akiwa amejawa shukurani kwa Mungu wake
kuwa amemrudishia familia yake. Hata hilo jaribu la shetani alilokusudia
kumuangamiza nalo, wamevuka. Mungu amewashindia. Tena wanarudi nyumbani
wakiwa wamejawa furaha na amani.
Kulikoungua Mpini, Kukabaki Shoka.
Walitua
jijini, Mama G akiwa anawasubiria. Walipotoka tu, akamkimbilia Oliva.
Alimchukua kutoka mikononi kwa baba yake, akamkumbatia kwa muda mrefu,
wakamuona machozi yanamtoka. “Asante
kwa kurudi Nanaa. Mungu wangu akubariki mwanangu. Nahisi ningekufa siku si
nyingi kwa upweke.” Mama G aliongea huku akifuta
machozi. Nanaa akajisikia kuhukumiwa zaidi. Liv alikuwa akimchekea bibi yake.
“Samahani mama. Haitatokea tena. Sasa hivi ukiniudhi nitakuwa nakununia
huku tunaongea.” Wakacheka na kuelekea kwenye gari.
Geb
alifika tu nyumbani, akala na kutoka kwa haraka. Alimuaga Nanaa na kumwambia
hatakawia kurudi nyumbani. Baada ya kutoka tu, Nanaa akamgeukia mama G. “Sasa
nafanyaje na Danny? Naona amekosa kweli raha!” Mama G akaguna. “Tuongee wakati
namlisha huyu dada. Tumbo naona limeingia ndani!” “Utamlisha nini sasa?” Nanaa
akauliza. “Nilisha mpikia ndizi, nikatupia hapo mboga kibao na samaki.” “Asante
mama.” Nanaa akashukuru, wakaelekea jikoni.
Mahusiano Hujengwa.
Baada
ya kumuwekea Oliva chakula chake na kuanza kumlisha, mama G akaanza. “Kwanza ujue
Danny yupo kwenye machungu mengi. Anajiona amempoteza Zinda. Mtu aliyemchukulia
kama kaka yake wa damu. Hakutegemea kama Zinda anaweza kwenda umbali aliofika
kwa ajili ya kitu ambacho anajua fika, Geb alikuwa akikupenda wewe tokea wapo
sekondari. Na wote walikuwa wakijua. Lile kundi lao lote la vijana, walikuwa
wakijua juu ya hisia za Geb juu yako. Sasa Danny yupo kwenye mshituko.
Hakutegemea kama Zinda anaweza kutenda ukatili wote huo. Alijua angekasirika,
lakini sio kwa kiwango hicho. Imekuwa ni kama mtu aliyekuwa amebeba mambo mengi
moyoni. Akionyesha kuna amani, kumbe yeye ana lake moyoni.” Mama G akaendelea.
“Kingine
anajilaumu na kuona aibu. Aibu kama vile ulivyosema. Yalikuwa mambo ya ndani
sana, ya kwetu tu. Aliwezaje kuyatoa nje!?” “Najuta mama! Ningejua nisingesema
vile. Wala sikuwa na wazo kama ni yeye ndio alikuwa akimwambia Zinda.
Nimejisikia vibaya!” “Wala sio kosa lako Nanaa. Ni kweli Danny amekosea.
Hakutakiwa kuongea vile. Wakati wote mimi huwa nawaambia wanangu, kuna mambo ya
familia yale mazito. Hayo hayatolewi nje hata iweje. Halafu kuna mambo ya
kawaida ambayo unajua hata yakizungumzwa hayataleta madhara yeyote. Hivyo hivyo
kwenye ndoa. Japokuwa Grace anazungumza na mimi sana juu yake na Danny, najua
kuna mambo mengine hawezi kuniambia. Ni yake na Danny tu. Na siwezi kuvuka
mpaka, kumdodosa kutaka kuyajua zaidi. Kwa kuwa mimi ndiye nimemfundisha.”
Nanaa akabaki akiwaza.
“Nitafanyaje
mama? Sitaki hili nalo litutenganishe.” “Na hilo ndilo la msingi Nanaa
mwanangu. Kosa limeshatokea. Lakini kutengana ndio litakuwa anguko kubwa sana.
Alimwambia Grace ni lazima warudi kwao. Hawezi hata kumtizama tena Geb. Anasema
kama isingekuwa yeye, mwezi huu mngefunga ndoa yenu. Lakini yeye ndio
anakwamisha. Hataki tena kuwa karibu na watu. Grace anasema hata kuzungumza
hawazungumzi. Anamuhofia anaweza kuugua kwa mawazo.” “Itabidi mimi na Geb
tuzungumze naye. Sitaki tuje kutengana sababu ya chuki za nje.” “Labda hivyo
itasaidia.” Waliendelea kuongea wawili hao. Wakasahau hata kama kulikuwa na
tatizo kati yao. Geb aliporudi jioni, akakuta vimejaa vicheko na kutaniana.
Moyoni akapumua.
Zinda Na Chuki Yake.
Katika
kuhangaika kumuangamiza Geb na Nanaa, Zinda alipata wazo la kwenda kwa mama
yake mkubwa Nanaa. Akiwa anaifahamu hiyo familia ndani na nje, hakupata shida
ya kuwaweka mama yake James na wanae hao wawili upande wake. Pesa tu ndio
ilifanya kazi. Zinda alichukua mkopo wa pesa maalumu kwa ajili ya kulipiza
kisasi cha kunyang’anywa Nanaa. Alikusudia kumtesa zaidi Geb aliyekuwa akimuona
hakustahili utajiri wote aliokuwa ameupata kwa haraka zaidi yao.
Geb
alifika nchini kutokea masomoni nchini India, wengi wa marafiki zake
walishakuwa wameanza kazi. Akiwepo Zinda. Wakati Geb anahangaika mtaani
akitafuta kazi na hana pesa ya kutosha, tayari kina Zinda walishakuwa na
viwanja. Tena kama Zinda alishakuwa amemaliza msingi. Alishakuwa anamiliki gari
kabla hata ya Geb na Danny.
Enzi
Geb anahangaika na kutafuta pesa, ndio zilikuwa enzi za Zinda kula starehe bar
na wanawake anaowataka. Kwa asili Zinda alizipenda pombe. Yeye ndio alikuwa
akiongoza kwenye kundi lao kwa mshahara unao eleweka. Wakati huo Danny bado
yupo chuo akisoma shahada yake ya pili. Na ndio wakati huo hata familia ya mama
G ndio walikuwa wakiishi kwa maombi ya kufunga na kuomba ya huyo mama, huku
wakiishi wote kwenye kajumba kadogo.
Haikuwa
kufumba na kufumbua kama wao walivyodhani, kwa Geb kumiliki thamani nyingi. Ilimgarimu
haswa, na pia ni kweli mkono wa Mungu ulijionyesha dhahiri juu yake. Kijana
huyo alijaliwa akili ya kufikiria kwa haraka. Na kwa kuwa aliachiwa ramani na
baba yake juu ya maisha, Geb ambaye alijaliwa kutosahau mambo, akaanza
kupambana jijini.
Mshahara
wake wa kwanza alioupata kutoka hapo BOT, alihakikisha wanahama pale walipokuwa
wakiishi. Mama yake alimng’ang’ania kumpa asilimia kumi ya huo mshahara wa
kwanza. Kila Geb alipoingia na kutoka, mama G alidai hiyo asilimia 10.
“Nimeweka agano na Mungu wangu Geb. Nataka hiyo asilimia 10 nikatoe sadaka
kanisani. Lazima nitoe hiyo nadhiri.” Geb alimpa mama yake hiyo pesa. Mama G
akaenda kuitoa sadaka kama alivyokuwa amemuahidi Mungu wake wakati akimuombea
mwanae.
Wazo
la gari halikumjia kwa kwanza. Akaamua kuwekeza kwa haraka. Kwa hiyo alianza
kazi na biashara ni kama kwa wakati mmoja. Alipoanza kupata faida, ndipo
akamnunulia mama yake gari. Wakati mwingine alikuwa akipelekwa kazini na mama
yake, na wakati mwingine alipanda daladala. Mida ya jioni kutoka kazini, hapo
ndipo alipotafuta marafiki walio karibu yake kumsogeza pengine karibu na kwao
au alipanda tena daladala. Wengi walikuwa wakimshangaa. Hasa marafiki zake.
Walikuwa wakimwambia huo ndio wakati wa kustarehe. Lakini haikuwa hivyo kwa
Geb. Ule ndio ulikuwa wakati wa kuwekeza. Alikuwa akiweka mipango bila kuchoka.
Asilimia kubwa ya mshahara wake iliingizwa kwenye biashara.
Kipindi
cha mwanzoni hakupata faida. Wakati mwingine malori aliyokuwa akikodi kwenda
kuchukua mazao, yaliharibika njiani na kuharibu kila kitu. Na kuishia kupata
hasara kwa asilimia yote. Mshahara unapotea, na biashara inakuwa imekufa. Mzigo
wa kwanza ulikuwa wa matunda. Aliyatoa Lushoto kwa nia ya kuyafikisha jijini
Dar. Tena akiwa amepata soko tayari kutoka kwenye kampuni yakutengenezea juisi
hapo hapo jijini. Kabla hata lori hilo halijatoka Lushoto, kukiwa na mvua kali.
Likakwama mlimani. Mpaka kukauka kwa barabara na kuweza kutoa lori hilo
barabarani, matunda yote yalikuwa yameoza. Geb akaingia hasara. Lakini hakukata
tamaa.
Akakusanya
tena pesa, akaamua kuagiza vitunguu kutokea mkoani Singida. Lori hilo ambalo
alilikodi, dereva wake hakuwa amelifunika vizuri. Mvua ikanyesha tena na
kuozesha vitunguu karibia vyote. Ni vichache sana alivyoweza kuuza kwenye
masoko. Tena kwa wauzaji wadogo wadogo. Hakurudisha hata nusu ya pesa
aliyowekeza. Mama yake alimshauri kuachana na hiyo biashara na kufikiria
nyingine, lakini Geb hakukata tamaa.
Akahamisha
akili kwenye tikiti maji. Safari hii alihakikisha anatuma lori huko Bagamoyo na
yeye mwenyewe akaenda kusaidia upakiwaji. Alirudi nao mpaka alipohakikisha
yanashushwa salama kwenye kiwanda kilichokuwa kikinunua matikiti hayo. Na
baadhi kwa wateja, wauzaji wa matunda wenye masoko madogo madogo. Hapo ndipo
alipoanza kuingiza pesa.
~~~~~Lockheg martl~~~~~~~~~~~
Ilikuwa
mida ya jioni wakati alipompigia mama yake James simu na kutaka kuzungumza
naye. Akiwa ana milioni 30 ya kwanza aliyokuwa amelipwa na Geb, mama huyo
mchaga alishakuwa amerudi Dar na harakati za kuwekeza pesa hiyo ulishaanza.
Hakutaka kubadilisha maisha yake na wanae kwa haraka. Akachukua chumba. Akawa
anaishi hapo yeye na watoto wake wakike wawili na mjukuu. Aliondoka nyumbani
akiwa amegombana kabisa na baba James. Alimlaumu kuendelea kuzunguka na mabinti
hao bila kuwaongoza kwenye kujitegemea.
Bado
binti hao wakubwa walikuwa wakitegemea kupewa kila kitu mpaka sabuni zao za
kuogea. Angalau Viola alikuwa akipokea pesa kiasi kwa ajili ya mtoto wake
kutoka kwa mzazi mwenzake, Alex. Lakini Vai yeye alitaka kupewa mpaka pesa ya
wanja na lipstik. Aliamka muda anaotaka na alilala usiku mwingi sababu ya
kuangalia tv. Walipotoka nyumbani kwa James wakiwa wamekimbia mahari ya Nanaa
na kurudi nyumbani kwao mjini Moshi, baba yao aliumia sana alipouliza kama
waliweza hata kusoma kozi fupi tu za kuongeza elimu na kupata jibu la hapana.
Si Viola wala mdogo wake hata walioongeza ujuzi wowote. Walirudi warembo na
kiswahili cha jijini tu.
~~~~~~~~~~~~~~~
Alipoelekezwa
wanapoishi hapo jijini, Zinda hakutaka kuchezea bahati. Alinunua kuku wawili wa
kuchoma, ndizi na chips. Soda kreti zima akabeba na chupa za bia kwa kuwa
alijua mama yake James ni mnywaji. Alipokelewa kwa heshima sana. Wakaanza kula
na kunywa. Alipoeleza tu shida yake, hapo ndipo alipojua atafanikiwa. Akaanza
kupewa mawazo ya nini cha kufanya kuhakikisha anamuangaiza kabisa Nanaa. Yeye
akiwa na nia ya kumkomoa tu Geb, akakutana na mahasimu wa Nanaa.
Zinda
alipewa njia nyingi sana. Akapewa madhaifu mengi sana ya Nanaa. Huku akimwagiwa
yeye sifa kuwa ni mwanaume mzuri. Akaambiwa Nanaa hajatulia au hawezi kutulia
na mwanaume mmoja ndio maana ameshindwa kukubali kujifunga kwake tu. Akaambiwa
huwa anakimbilia wanaume wenye pesa, ndio maana huwa haoni wanaume wazuri kama
yeye Zinda. Akapewa faraja ambayo hakutarajia. Mvua za sifa zikamlowesha Zinda.
Alisifiwa kwa kupokezana. Kuanzia uzuri wake wa nje mpaka roho yake. Bia
zilizokuwa zimeshaingia ndani yake kabla hajafika hapo, zilimsaidia kufurahia
sifa hizo. Matumaini ya kufanikisha lengo lake la kumkomoa Geb na Nanaa,
iliongezwa mara dufu. Alitoka hapo ndani, Zinda akiwa na tumaini jipya. Aliagwa
kama mfalme na shukurani kede kede kutoka kwa mama James na wanae.
Ugomvi
ukaanza mara tu baada ya kurudi ndani baada ya kumsindikiza na kugundua Zinda
ana usafiri. Aliacha gari nje. Tena sio gari mbaya. Ni gari ya kawaida tu,
yakueleweka. Na alishasema anamalizia kujenga nyumba nzuri sana na yakifahari
ambayo hiyo ndio alitaka ahamie na Nanaa. Viola na Vai wakaanza kutukanana
mwishowe ngumi zikaanza. Kila mmoja wao akawa anamtaka Zinda. Wakajaza watu kwa
kupigana mpaka kuvuana nguo hapo chumbani kwao. Huku mama yao akishindwa
kuingilia kabisa.
Vichaa, Wamepewa Rungu.
Mashindano
yakaanza. Zinda akaanza kuthaminiwa kama mfamle. Akifika hapo, walishindana
kumtayarishia na kumuhudumia kwa maneno mazuri. Kila mmoja alijitahidi kwa
nafasi yake. Zinda akiwa amefika hapo kuzungumza na mama yao na kuhakikisha
wapo ukurasa mmoja, lakini akajikuta hali ya uanaume aliyoona Nanaa ameipuuza,
warembo hao wawili wameitambua. Hakuna jinsi ungemwambia Zinda asirudi kwenye
hiyo nyumba akakubali. Aliagwa huku akibembelezwa arudi tena kesho yake.
“Kwanza unaishi peke yako. Sitaki ulale njaa bwana. Ukitoka kazini njoo ule
ndipo ukalale.” Hayo ni maneno ya Vai asiyejua hata kupika uji, akiwa amesimama
dirishani mwa gari la Zinda akiwa anamuaga. Viola alipitwa. Alimpeleka mtoto
wake chooni.
Safari
za hapo zikaanza kuwa nyingi. Kila akitoka kazini, basi alipita nyumbani kwa
mama James na binti zake. Wakati mwingine hakuwa akimkuta mama yao sababu ya
kuhangaika kutafuta jinsi ya kuwekeza mjini. Mama huyo muhangaikaji aliyetoka
kwake na kumuacha mumewe kwa kishindo huku akimtambia atamsikia kwenye vyombo
vya habari tu, akiwa amefanikiwa sana. Na kweli hakutaka mchezo. Alihangaika
kwa kadiri ya uwezo wake kuwekeza pesa aliyolipwa na Geb.
Zinda
naye akalipa tena mahari ya Nanaa kwa pesa tu. Maana mama huyo alimwambia
akitaka amsaidie, alipe na yeye hiyo mahari. Bila kipingamizi, huku ikifahamika
wazi kuwa mahari za Kichaga huwa hazimalizwi, lakini mama James alitaka alipwe
pesa yote, na Zinda naye akamlipa pesa yote. Na Zinda ndiye aliyempa wazo mama
James la kumdai tena Geb pesa.
Alimwakikishia kuwa Geb anapesa sana. Kwa kulipwa tu milioni 30 ni kama
kujidhalilisha. Zinda alimsifia yule mama kwa malezi ya Nanaa huku akimuonyesha
kumuhurumia kwa kazi ngumu. Akamtia moyo, wakakubaliana kwenda kusimamisha hiyo
harusi ya Geb na Nanaa. Ndipo usemi wa ‘umoja ni nguvu’, ulipotimia siku ile kanisani. Wakafanikisha nia
zao. Mama James akapata pesa, Zinda yeye akafurahia kusimamishwa kwa harusi.
~~~~~~~~~~~~~~~
Akiwa
na pesa yakueleweka, Mama huyo wa kichaga anayeifahamu pesa na akili ya
kuzalisha, akaanza kusugua kichwa. Nyumbani akawa hapatikani sana. Binti hao
wawili waliozoea kuhudumiwa na hawawezi kazi, hawakutaka kuhangaika na mama
yao. Wao walikuwa wakibaki tu nyumbani. Kwa hiyo mara nyingi Zinda akajikuta
anabaki nao hapo nyumbani.
Viola
mwenye mtoto au jukumu la mtoto, mara nyingi mtoto alimfanya akose nafasi ya
kumganda Zinda ipasavyo. Hapo ndipo Viola alipomjutia yule mtoto. Chuki kwa
mwanae pia ikaanza. Aliona anamzuia kwenye mambo yake. Alianza kumpiga bila
kosa. Hakuruhusiwa kumwita mama yake pale Zinda anapoingia mle ndani ili na
yeye apate muda na Zinda.
Mama
James alipata eneo ambalo kwa akili yake ya haraka akajua akipakarabati hapo,
anaweza kufungua baa. Ilikuwa ni nyumba ya mzee ambaye alifariki akaachia
watoto wake waliokuwa wakipigania hiyo nyuma. Alipokuja mama James akitaka
kupakarabati na kupakodisha, wakamkubalia. Mama James mchapa kazi. Anaamka
asubuhi kuelekea huko Msimbazi Centre kwenye ujenzi wa baa yake, kurudi usiku
sana amechoka. Hajui linaloendelea kwa mjukuu wake wala bintize.
Siku
hiyo Zinda akiwa ndio ameingia tu pale, ndio Viola naye alikuwa ametoka
kumchapa sana mtoto wake, alikuwa akilia. Vai akamdaka Zinda na kumuomba watoke
pale kwa sababu ya kelele. Zinda hakukataa. Akaona ni kweli Viola anahitaji
muda wa kumtuliza mwanae. Walipoingia tu kwenye gari, Vai hakuchelewa.
Akamshauri warudi nyumbani kwake, apike yeye, wale. Zinda hakubisha. Hata yeye
aliona ndio utakuwa mwanya wa kumpata Vai kimapenzi, kitu alichokuwa
akikitamani tokea Vai alipokuwa akijitongozesha.
Vai Nyumbani Kwa Zinda.
Alipoingia tu ndani, uvuaji wa viatu wa Vai
ulimfanya Zinda aliyekuwa nyuma yake ashindwe hata kusogea. Hali yake
ikaharibika kabisa. Vai alikuwa amevaa sketi ya kuchanua fupi. Ndani alikuwa na
chupi yenye mikanda kila mahali. Alipoinama vile, mabaja yote yalikuwa wazi
mbele ya macho ya Zinda. Aliendelea kuvua viatu hivyo kichokozi mpaka
akahakikisha Zinda anaona kila kitu.
Akiwa amejawa uchu, Zinda hakupoteza muda. Badala
ya kumuonyesha jikoni kama Vai alivyokuwa akisisitiza njiani akiwa amekaa
pembeni yake na nusu ya mapaja yake nje akijaribu kuyafunika ili kuhakikisha
Zinda anayaona, Zinda alimwingiza chumbani. Vai mtoto wa mahaba. Aliyejua
wanaume tokea utoto, hakufanya mchezo mdogo. Alihakikisha anampagawisha Zinda
kiasi cha kumuacha hajielewi.
Akajituma vilivyo bila kuchoka huku akimgeuza kulia
na kushoto bila kujali hisia zake mwenyewe, ila Zinda. Nyumba hiyo ndogo
yakupanga ambayo haikuwa na kiyoyonzi, au AC siku hiyo Zinda alitamani ingekuwa
tofauti. Vai alimtoa jasho kwa purukushani hapo kitandani, akaishia kuhema na
hushukuru kama mpumbavu. Vai alimuamulia siku hiyo ili kumdhibiti asimfikie
tena Nanaa wala Viola.
Zinda
alipoona mchezo umekolea, akamtumia ujumbe kijana wake aliyozoea kumtuma hapo
mtaani, alete chips kuku na bia. Vai hakuwa mnywaji hata kidogo. Akaletewa
soda. Wakala. Zinda akaona usiku umeingia akaamua kumrudisha Vai nyumbani kwao.
Vai akiwa amekusudia kulala, hakubisha. Akaingia kuoga, akatoka akiwa
anajikausha. Mtoto wa kike kama alivyozaliwa. Akaanza fujo pale chumbani. Zinda
akiwa ameshalewa, akajiambia amfurahie binti huyo tena kidogo, kisha
atamrudisha baada ya hapo.
Alikuja kuamshwa na alam ya kumtaka ajiandae kwenda
kazini. Kwa purukushani nyingi za usiku uliopita, Zinda aliamka kichwa kizito,
mbio bafuni kuwahi kibaruani. Alimuaga Vai akimuahidi kuwasiliana baadaye. Na
akamwambia akiwa tayari kuondoka kurudi kwao, amtaarifu ili amuelekeze wapi
pakuacha funguo za nyumba yake.
Mpaka anatoka jioni, hakuwa amepata simu yeyote ile
kutoka kwa Vai na wala Vai hakuwa akipatikanika. Akaamua kuanzia nyumbani
kwake. Akamkuta Vai ametulia tuli kochini. “Mbona sikupati kwa simu!” Zinda akahoji
akiwa haelewi kinachoendelea. “Simu iliishiwa chaji tokea jana. Nimeshindwa
kuondoka kwa kuwa sijui jinsi ya kufunga mlango.” Vai alijibu na kusimama.
Binti huyu aliyefahamika hana nidhamu, kumbe alijua kujituma.
Akasimama
kumpokea Zinda. Alimpa busu la kutulia, lakini mkono ulishakuwa umefika kwenye
zipu ya suruali. Tayari akili za Zinda zikaanza kuvurugika. Akaona achangamkie
kwa haraka kabla hajamrudisha kwao. Mabusu yale yakawapeleka kitandani, Zinda
akihema hovyo anadai angalau roundi moja ndipo waondoke. Walipotua tu kitandani
akiwa amepagawa, Vai akasimama. “Naona unirudishe tu nyumbani. Tusije chelewa
kama jana.” Aliongea kwa heshima zote huku akijiweka sawa na kuashiria utayari
wa kuondoka. “Naomba usiniache hivi Vai! Tafadhali sana.” “Unaonekana wewe
mwenyewe hufurahii kulala na mimi Zinda.” Vai akajilalamisha.
“Hapana Vai! Mbona mimi nafurahia sana tu. Ila.”
“Ila sifanani na Nanaa?” Vai akamkatisha maneno. “No no noooo. Namaanisha ila
sikutaka kukutia matatizoni kwa mama. Nimefurahia sana kuwa na wewe Vai.
Sijawahi kupata usiku mtulivu kama wa jana. Nimelala kama mtoto mchanga!” Vai
akacheka kwa huba. “Hata mimi sijawahi kufanya mapenzi na mwanaume kama wewe Zinda.
Ujue jana umeniliza wewe!” Sifa zikaanza. “Sijawahi kulala na mwanaume mwenye
maumbile kama yako Zinda. Yaani ukinishika nasikia kama kuchanganyikiwa.
Ukiingia humo ndani, ndio kabisa, sijiwezi. Lakini naogopa kunogewa halafu
ukakumbuka penzi lako kwa Nanaa. Ukaniacha nateseka.” Vai aliendelea kumtesa
Zinda aliyekuwa yupo juu zaidi ya mlima Kilimanjaro.
Hapo Vai anaongea huku titi moja lipo nje. Tena
titi ambalo halijawahi kunyonyesha mtoto hata mmoja. Weupe wa Vai kama wa kaka
yake James, wamechukua kwa mama yao. Macho ya Zinda yalikuwa yakiangalia chuchu
iliyokuwa ikikaribia rangi ya pinki kama ya mtoto wa kizungu. Mungu ampe nini
tena? Aliyokuwa akiyaona kwenye tv, leo yapo ndani ya chumba chake cha kulala!
Zinda akabaki akiangalia lile titi.
“Mimi naona niondoke tu Zinda.” Kosa akarudisha
lile titi ndani ya shati lililokuwa na vifungo mbele. “Tafadhali Vai. Naomba
usinitese. Nanaa hayupo hapa. Kwanza nataka nini kwa Nanaa ambacho wewe
utaninyima! Eti Vai? Au kuna unachotaka kuninyima?” “Hapana Zinda. Ila sitaki
ujute.” Zinda akasimama kwa haraka akaenda kumshika mikono yote miwili.
“Nakutaka wewe Vai.” “Sasa nikirudi hapo kitandani halafu ukanichanganya? Wewe
mwenyewe unajijua jinsi ulivyomtamu Zinda. Ukianza huwa sitaki kumaliza. Nataka
tuendelee tu. Na wewe unaonekana ni kama hupo huru na mimi.” “Mimi nipo huru.
Nilikuwa namuhofia mama tu. Lakini kama unasema mama hana neno, basi naomba
tubaki wote. Tafadhali Vai.” Vai akajifanya anafikiria kidogo.
Akajua
juhudi zake za jana zimezaa matunda. Akamsogelea karibu kabisa na sauti
akaishusha. “Unauhakika?” Akamuuliza na kupiga magoti mbele yake. Akamalizia
kumtoa ile suruali na kuanza kumchezea akiwa amepiga magoti vile vile. Alipoona
Zinda analalamika zaidi, akasimama. “Nimekuuliza kama una uhakika Zinda. Sio
tena unatoka hapa unaniacha nateseka mwenzio.” Zinda alitamani kulia. Alikuwa
anakaribia kupata goli la ushindi palepale alipokuwa amesimama.
Hapakuwa na kiapo alitakiwa atoe wakati ule
akashindwa. Hakuna neno alilotaka kulisikia Vai kwa muda ule asilitamke.
Ilimradi tu Vai amnusuru. Vai alimuachia akaenda kujirusha kitandani. Mapaja
yote yalikuwa nje. Zinda aliendelea kuteseka pale alipokuwa amesimama. Macho
mapajani, hana nguo. “Naweza kukupa muda wa kufikiria. Mimi nitakuwepo tu
nyumbani Zinda. Utanifuata wakati wowote utakapokuwa tayari.” “Mimi nipo
tayari. Nakutaka wewe Vai. Sidhani kama kuna mwanamke yeyote hapa duniani
anaweza kunipa unayonipa. Nakufurahia sana. Natamani usiondoke hapa.” Zinda akajitia
kitanzi yeye mwenyewe huku akimfuata kitandani akiwa amevaa shati tu.
“Kweli Zinda?” “Nakuapia Vai. Natamani usiondoke.
Nataka leo tupate usiku kama wa jana.” “Hata mimi Zinda. Napenda hivyo
unavyonikamata kwa nguvu wakati tunafanya mapenzi. Naridhika. Natamani uwe
wangu wa milele.” Tayari mkono wa Zinda ukatua mapajani. “Hivi kinachotuzuia ni
nini Vai? Eti mpenzi?” “Kweli upo tayari kuwa na mimi?” Vai akaanza tena utundu
wake. Alihakikisha anawasha taa, nakumvamia Zinda pale kitandani. Alimlaza
chali. Akamkalia juu. Macho ya Zinda yalikuwa yakitazama mwili uliokuwa ukiwaka
kama alumasi. Vai alijinyanyua juu na chini. Kata dakika tano hazikupita, Zinda
akakata kiu yake. Vai hakufanya haraka kujitoa pale kwa Zinda. Akabaki
amemwinamia huku akimbusu midomo, shingoni na masikioni.
“Kweli Zinda wewe mwanaume. Sijapata ona. Duuuh!
Yaani bila kuhangaika umenifikisha na mimi! Nakushukuru sana. Asante mpenzi.
Nakushukuru sana.” Vai hakuwa hata amesikia chochote kile wakati anafanya
mapenzi. Lakini alimuongopea tu ili kumfurahisha. “Daah! Nahisi Mungu amenifuta
machozi. Sikutegemea kupata mwanamke kumzidi Nanaa. Hakika umeniweza Vai.”
Zinda alishanogewa vyakupitiliza. “Tafadhali lala na mimi leo. Tumjulishe tu
mama kuwa uko kwangu.” “Sawa.” Vai akakubali kwa haraka sana.
~~~~~~~~~~~~~~~
Hapo walishakuwa wamesimamisha ndoa ya Geb na
Nanaa. Kazi ya Zinda ikabaki kujipongeza tu. Mungu amemfuta machozi. Akaletewa
kimwana kama Nanaa, ndani ya nyumba. Kwa rangi watoto wa mama James na Nanaa
hawakutofautiana kabisa. Wote walichukua weupe wa bibi yao. Hata mama mkubwa
alikuwa mweupe sana. Maumbile tu ndio walipishana na Nanaa. Lakini hata wao
walikuwa na maumbile mazuri ya kike, yakumvutia mwanaume yeyote yule. Viola na
Vai hawakuwa na vitu vilivyozidi sana mwilini mwao kama Nanaa, lakini wachaga
hawa, walikuwa wa namna yao. Usingechoka kuangalia. Kama ulifika nchini
ukaambiwa wachaga wana sura au umbile baya, basi ukikutana na ndugu hao, utajua
umedanganywa tu. Binti hao wote waliokuwa wamelelewa nyumba moja, walijuana
madhaifu yao na uzuri wao. Kwa hiyo haikusumbua kuangamizana.
Vai alitumia kipindi hicho vizuri sana kumliwaza
Zinda aliyekuwa akilalamika kusalitiwa na rafikize. Vai akageuka kuwa BFF wa
Zinda. Akatulizwa kimya nyumbani kwake. Kazini, nyumbani kwa Vai. Wakati wote
alipewa penzi la nguvu. Alikuta nyumba safi. Nguo zimefuliwa na chakula kipo
mezani, Vai kochini akimsubiria. Na salamu ya Vai ilimfanya Zinda kuwahi kurudi
nyumbani. Alihakikisha anarudi nyumbani peke yake bila rafiki. Na akiingia tu
anafunga mlango kwa nyuma tena kwa haraka, kwani Vai alikuwa akimvulia suruali
mlangoni. Mpaka Zinda anaenda kukaa kwenye kochi, na kuulizwa habari za kazini,
basi ameshajishindia bao moja la bila kutoa jasho.
Vai alikuwa akimwambia hiyo ndio ilikuwa pole
yake ya shuguli za siku nzima. Alimtaka asimame tu. Yeye anampa pole ya kazi
bila kujigusa. Basi hapo ndipo Vai alipomliza mtoto huyo wa kiume, nakujikuta
hajiwezi mbele ya Vai. Ni muda aliokuwa akiutamani ufike, arudi nyumbani apate
ukaribisho huo ambao Vai aliutendea haki.
Zinda alijitenga na kila mtu ambaye alijua
angemtaka siku za weekend wakutane au amjibu jumbe yeyote. Kwenye makundi ya
whatsapp akawa hasikiki tena. Bia anazikuta kwenye friji yake nyumbani.
Hapakuwa na sababu yakumtoa Zinda nyumbani kwake tena. Huwezi kumkuta Zinda na
simu akiwa na Vai. Vai alijua kumtawala na kuziteka fikra zake ipasavyo.
Wanawake aliokuwa akiwalipa baa ili afanye nao mapenzi, hakuwalinganisha na
Vai. Vai yupo nyumbani. Anamlilia mapenzi! Anapewa penzi muda na wakati wowote
ule. Hata wakati mwingine anaamshwa na mabusu mwilini. Vai anakuwa yupo tayari
akimlilia kuwa ameshindwa kulala, mpaka amtulize. Utamwambia nini Zinda?
Kwa Kina Nanaa.
Huku kwa Nanaa na Geb,
walishakubali kushindwa. Wakaendelea kuishi bila ndoa. Nanaa na Geb
wakajitahidi kurudisha amani kati yao. Walimtafuta Danny yeye peke yake
wakapata muda wa mazungumzo naye. Walijaribu kumfariji na kumuhakikishia yeye
sio sababu ya yote. Adui yao ni shetani. Geb akamwambia Danny, wakikubali
kutengana hapo ndipo kutakuwa kushindwa kwao. Walimpa maneno mengii ya
kumfariji Danny mpaka akaanza kurudisha ujasiri.
Furaha ikaanza kurejea kati yao. Lakini Grace na
familia yake hawakurudi tena kuishi pale. Ikawa kazi ya Nanaa na Liv kwenda
nyumbani kwa Grace. Geb na mama G wanapokuwa wakiaga kwenda kazini, Nanaa na
yeye anajifungasha na mwanae, nakuhamia kulala kwenye makochi ya nyumbani kwa
Grace. Kuanzia asubuhi anapofika hapo mpaka jioni. Mama G hakuwa akikaa kazini
siku nzima. Kwa hiyo alifanya kazi nusu siku. Tena inapolazimu na kumfuata
Nanaa nyumbani kwa Grace.
Grace alishapata mfanyakazi aliyekuwa akimsaidia
swala la watoto. Jeri, dereva wa muda mrefu sana wa Geb, ndiye aliyekuwa dereva
wa Nanaa na Liv, na ndiye aliyemtafutia Grace msichana wa kazi. Alikuwa binti
mzuri, mwaminifu na mchapa kazi kama Jeri. Aliwapenda hao watoto na kuwahudumia
bila kuchoka. Kwa hiyo muda mwingi Grace alijikuta wakipata muda na Nanaa.
Grace akimsaidia kumlea Liv. Kwani Nanaa alikuwa akilala kupita kiasi. Wakajua
mimba ya Nanaa imempenda Grace.
Akiamka tu asubuhi, anambeba mwanae hivyo hivyo na
nguo zake za kulalia, anahamia kwenye kochi nyumbani kwa Grace au kwenye chumba
alichopewa hapo nyumbani Grace. Atalala
hapo siku nzima, huku Grace akifanya kazi zake hapo pembeni yake, hapo hapo
nyumbani. Ni kama Grace alihamisha ofisi yake nyumbani. Basi Nanaa atalala hapo
mpaka muda anaojua Geb anakaribia kurudi nyumbani. Wakati mwingine alipika
chakula cha nyumbani kwake hapo hapo kwa Grace na kukibeba, au alimtaka Geb
apitie hapo nyumbani kwa Grace ale ndipo warudi kwao. Ukimtaka Nanaa, muulize
Grace.
“Huyu atakuwa na mimba ya mtoto wa kike. Naona
umenipokonya mapenzi yangu.” Grace akamcheka mama yake. “Mimi naona anataka
kuiona tu hii sura. Unafikiri hata akifika hapa ananiongelesha sana? Hata Danny
amchokoze vipi, atacheka kidogo tu, baada ya muda mtamsikia anakoroma hapo hapo
pembeni ya Danny.” Wakacheka. “Nasikia sana mnavyonisema!” Nanaa alitoka
usingizini akasikia Grace na mama yake wakimsengenya jikoni.
“Turudi nyumbani Nanaa! Ni nini unapendea hapa?”
“Wewe mwenyewe hutabiriki bwana mama. Mara uniambie unaenda kazini mara moja
unarudi, halafu sikuoni tena sijui mpaka masaa mangapi! Na mimi sitaki kukaa
pale peke yangu. Liv anataka tucheze wakati mimi nina usingizi. Naona heri aje
hapa achangamshwe na kina Fellius, wakati mimi nalala. Grace akila ugali,
amlishe wakati mimi nalala.” Nanaa akakaa. “Tumbo hilo limeshaanza kuwa kubwa
zaidi yako. Si ukubali tukaangalie jinsia ya mtoto?” “Bwana mama! Acha kuwa
kama Geb. Mbona hamna subira? Eti Grace?” “Mimi ndio huwa siwezi kusubiri
kabisaa. Naanza kuulizia jinsia pale tu nikijijua ni mjamzito.” “We Grace!”
“Ili nijue nilichobeba na kujiandaa.” Grace aliongeza. “Bwana mimi sitaki.
Nyinyi subirini mtoto mwingine anakuja.” “Mmmh! Kazi ipo.” Mama G akaongeza
huku akimtolea matango aliyokuwa amemtayarishia. Nanaa akakaa.
“Mmempikia Geb wangu?” Nanaa akauliza huku
akitafuna tango. “Ujue umenyimwa aibu Nanaa wewe?” Mama G akamfanya Nanaa
acheke. “Pika mwenyewe.” “Mimi na wewe mama yangu? Najua utakuwa umenisitiri
tu. Geb hawezi kutoka kazini asikute chakula.” Nanaa akaongea huku anacheka.
“Sasa leo atakula wali na mchuzi wa nyama.” “Hapo ndipo kuachika. Haya naomba
mnipishe hapo nianze kuchangamka. Akija hapa akute chakula.” “Si ukapikie kwako
Nanaa? Ni nini kung’ang’ania kwenye majumba ya watu!” “Mama naye kunifukuzia
mgeni! Wewe mwache.” Grace akalalamika. “Wala sio mgeni. Na kesho tena nitarudi
mwaya Grace. Haya twende mama kabla sijalala tena.” Wakacheka na kutoka.
~~~~~~~~~~~~~~~
Ilishakuwa miezi minne imepita tokea Zinda
asimamishe harusi ya Geb na Nanaa. Maisha kwa kila mmoja yalikuwa yakiendelea
kama kawaida. Hakuna aliyezungumzia swala la harusi kati ya Geb na Nanaa. Nanaa
ndio hakuwa tena na habari. Kazi yake kulala
na kula kuhu analea mimba. Oliva alishaanza kushika mahali na kutembea.
Mama yake James baa yake ikaanza kuchanganya kwa
pesa alizokuwa amelipwa na Geb. Alifungua baa ambayo iliuzwa vinywaji vya kila
namna, pamoja na chakula. Mama huyo alikuwa na shuguli kuliko maelezo.
Alidamkia baani kwake kuhakikisha kunakuwa na kifungua kinywa kizuri wateja
wasimkimbie. Na kwa kuwa alikuwa mzungumzaji, na bei yake haikuwa juu, alikuwa
na wateja wengi. Baa yake ilikuwa ikijaa kuanzia asubuhi mpaka usiku. Utani na
sifa kibao kwa wateja wake. Wote walimtaka wamkute pale baani.
Aliifanya
hiyo kazi kwa bidii zote kumuhakikishia mumewe na James, kuwa hata yeye
anayaweza maisha. Na Nanaa mbaye ndio mkosi wake, ameshamkata kwenye ukoo wake
ndio maana anafanikiwa. Ukweli kwa muda mfupi sana mama James alikuwa na pesa.
~~~~~~~~~~~~~~~
Vai nae ni kama alihama kabisa nyumbani kwao
wakajua anaishi kwa Zinda. Kilichokuwa kikimshangaza Viola na mama yake, ni
wanaishije au Vai anafanyaje. Kwa kuwa Zinda alikuwa akimsifia swala la usafi
na chakula kizuri. Vai anafahamika kuwa hajui kupika wala hawezi kujituma
kufanya chochote.
Maisha yakaendelea. Vai na Zinda. Furaha na mapenzi
mazito huku Vai akiomba Mungu afanye muujiza, ashike mimba amzalie mtoto Zinda
ili amuombe wafunge ndoa awe wake kihalali ili asije kurudi tena kuishi na mama
yake, Viola na mwanae. Wivu ulikuwa ukimsumbua sana Viola. Kwanza aliona Vai ni
kama amemuibia mwanaume wake kwani yeye ndio alimuwahi Zinda tokea siku ya
kwanza wakipigana. Alimwambia mama yake na Vai kuwa atahakikisha Zinda anamuoa
yeye. Lakini Vai akamwambia na yeye ameshamuwahi Zinda kuwa atakuwa wake. Ngumi
zikapigwa, na ndipo Vai akamuharibia kwa Zinda kwa kumwambia tayari Viola
anamtoto, na alizaa na mwanaume wa wizi. Akajitahidi kumchafua kwa kadiri ya
uwezo wake mpaka akamzidi mahesabu dada yake, yeye akaibuka mshindi.
Kila alipokuwa akienda kutembelea nyumbani kwao,
Vai alifika akiwa nadhifu. Tena alikwenda na Zinda wakiwa wanaendesha gari ya
Zinda. Vai alijitahidi kila akienda hapo nyumbani ana nguo mpya na pochi. Maringo
kwa dada yake yakaongezeka. Na alihakikisha Viola hapati hata dakika moja peke
yake na Zinda. Alimfahamu dada yake. Kila Viola alipotaka akaribishwe nyumbani
kwa Zinda na wao wakawatembelee, Vai alidakia kwa haraka, kuwa atatafuta siku
na kuja kuwachukua. Wawe wavumilivu.
Hayo yalikuwa majibu yake akiwepo Zinda. Lakini alipokuwa akimtanguliza
Zinda kwenye gari, yeye akibaki nyuma, alihakikisha anampiga mkwara dada yake
kuwa hamtaki nyumbani kwa Zinda. Nia yake ilikuwa ni mpaka ashike yeye mimba
ndipo amkaribishe Viola aliyekuwa akitumia kubeba mimba kama silaha ya kumpata
mwanaume yeyote anayemtaka yeye. Hata kama ni shemeji yake. Vai alishamshuhudia
akitoa mimba nyingi tu alizokuwa akiwabebea makusudi wanaume ili wasimkimbie.
Alipokuwa akiachwa na mimba zake, alizitoa. Ni mtoto wa Alex tu ndiye
aliyemtunza kwa kuwa Alex alikuwa akituma pesa na alimuahidi angemuoa.
Ukweli maisha ya Zinda yalibadilika. Alikuwa kwenye
mahusiano mazuri na matulivu. Vai alituliza mawazo, mambo ya kitoto akaweka
pembeni. Akakusudia kushika mimba atulie na Zinda aliyekuwa na muelekeo. Zinda
alikuwa akimalizia nyumba yake ili ahamie. Vai alishakusudia yeye ndio atakuwa
mama mwenye hiyo nyuma. Mvua inyeshe, jua litoke, yeye ndiye ataishi hapo na
Zinda.
Historia Ya Vai.
Miezi minne ilishapita tokea Vai aanze kuishi na
Zinda. Mapenzi ya mchana na usiku lakini hakuwahi kushika mimba hata mara moja.
Wasiwasi ukamwingia Vai. Akakumbuka mimba alizokuwa na yeye akitoa tokea yupo
shuleni sekondari. Nyingine hata mama yake hakuwa akijua. Alipokuwa kidato cha
pili, alitoa mimba mbili. Akiwa anaishi hapo hapo nyumbani, na mama yake
hakujua. Mimba ya mwisho ndio alikaribia kufa. Kwani alimtoa mtoto ambaye
tayari alishakuwa ameanza kucheza. Ilikuwa mimba kubwa kabisa.
Vai aliugua na kulazwa kwa muda mrefu. Wakiwa
wamehamia hapo jijini, Vai alipata mme wa mtu. Kwa kuwa alikuwa na gari na
alikuwa akimpa pesa, akaamua kufanya kama dada yake. Akambebea mimba ili
amuweke awe hata nyumba ndogo ili kuendeleza starehe na mgao wa pesa uongezeke.
Alikuwa akimpeleka kwenye mahoteli ya garama na kumnunulia vitu vya garama.
Lakini ikawa kinyume kabisa na matarajio yake. Alipomwambia
ni mjamzito, yule baba hakuonyesha kushituka. Akaendelea kukutana naye kwa
siri, lakini haikuwa kama zamani. Mimba ilipofikisha miezi mitano kwenda 6,
kukiwa kumeshaanza ugumu wa mawasiliano kati yao, yule baba akamwambia Vai
ameamua kusitisha mahusiano. Na amemwambia mkewe, mkewe amemsamehe. Ameamua
kutulia kwenye ndoa yake. Akampiga marufuku asimtafute tena, iwe mwisho.
Vai hakupoteza muda, akaenda kutoa mtoto mkubwa
kabisa. Alirudi nyumbani kimya kimya bila kumwambia mtu yeyote kile
alichokifanya. Siku zilidi kwenda, huku akiteseka kwa maumivu makali ya tumbo.
Harufu ya kama kitu kilichooza ilipoanza kusumbua kwenye chumba hicho
walichokuwa wakilala na mama yao, ndipo ikajulikana alitoa mimba. Vai alikuwa
na homa kali sana. Mama yake alimkimbiza hospitalini.
Vai alimweleza daktari waliyemkuta kuwa alikuwa
mjamzito, lakini mimba ilitoka. Mama yake na Viola walijua ni uongo. Ni kwamba
alimtoa mtoto. Tena vichochoroni ambako hakupewa huduma ya kueleweka. Ilibidi
kusafishwa kizazi na kutibiwa kwa majuma kadhaa akiwa alishapoteza damu nyingi
na infection ya kizazi.
Alipotoka
hapo, Vai alitulia kabisa mpaka alipokuja tena Zinda, akaamua kutulia na Zinda.
Alishaonjeshwa kifo. Alishatapeliwa na wanaume, basi akakusudia kuwa Zinda ndio
atakuwa wakuzikana. Alikuwa akimtetemekea huku akijipongeza kwa kufutwa
machozi. Akajiapia kutulia kabisaaa.
Kwanza anatafuta nini? Hajasoma na hana kazi. Lakini
Zinda anamtunza vilivyo. Ahadi zote kwa Nanaa, Zinda akazitimiza kwa Vai. Mungu
ampe nini tena? Hata ungekuwa na nini, kama ungekutana na Vai wa safari hii,
hata ungemtongoza asingekubali. Katulizwa na Zinda. Anapewa kila atakacho kwa
kadiri ya uwezo wa Zinda. Na Zinda hakuwa akimgasi kwa shule wala kazi.
Hakumtaka arudi shuleni wala atafute kazi. Alishamwambia mshahara wake
utawatosha. Basi, maisha yakaendelea.
Zinda.
Zinda mtoto wa kiume mkubwa kwenye familia yao.
Ndiye anayetegemewa kwao kwa mambo mengi sana japo bado baba yake
anajishugulisha kwa biashara ndogo ndogo. Danny aliongezeka kwenye familia
hiyo. Akawa msaada mkubwa sana. Alikuwa akituma pesa bila kumtaarifu hata Zinda
mwenyewe. Wadogo zake Zinda au wazazi wa Zinda walipokuwa na shida, hawakusita
kumpigia simu Danny na kumuomba msaada. Lakini baada ya kujihesabu amesalitiwa
na Danny kwa kumuunga mkono Geb kumchukua Nanaa, aliwapiga marufuku ndugu zake
wote wasiwahi kuwasiliana tena na Danny.
Hata wazazi wake aliwaambia mabaya mengi sana
yaliyowaumiza juu ya Danny. Alihakikisha amejenga uadui kati yao. Wazazi wa
Zinda hawakumtaka tena Danny. Si kwamba Danny mtoto yatima alipoteza tu kaka
ambaye ni Zinda, alipoteza na wazazi wa pekee aliojichagulia ukubwani.
Aliwapenda wazazi hao kama wake. Akisikia hata mmoja wao ni mgonjwa, basi Danny
atawasha gari na kukimbilia Tabora kuwaona.
Maombi ya mama yake Zinda ni aoe na apate watoto wa
kurithi. Mke wa Zinda alisubiriwa kwa hamu sana na familia nzima. Mama yake alishampa
majina ya wasichana wengi tu wa pale pale kijijini kwao, lakini Zinda
aliwakataa. Akampa baraka zote, alete atakayempenda yeye, ilimradi aoe.
Swala la kwamba kama Vai ataweza kuishi na ndugu
zake likaanza kuwa mtihani. Nia ya Zinda ni kuhamishia baadhi ya ndugu zake
pale jijini ili kuwasaidia. Wanaoweza kwenda shule waende na wanaoweza kufanya
biashara wafanye. Lakini wasihangaike mahali pakuishi. Yeye ndio awasaidie
malazi. Na ndio maana alijenga nyumba kubwa iliyokuwa ikimtoa mate Vai, japo
haikuwa ya kisasa sana, ila Zinda alijua itamtoshea yeye na nduguze.
Hamu ya mtoto ilikuwa ikimsumbua Zinda. Kelele za
kulinganishwa na rafiki zake hasa Danny ambaye tayari ana watoto watatu,
zilizidi kumtesa Zinda. Kila mara mama yake alimtolea mfano kwa mwenzie Danny.
Akamwambia anachelewa kuanzisha familia. Na ni kweli umri ulikuwa ukikimbia.
Zinda alijiona mtu mzima. Habari ya kuambiwa na Vai kuwa ameshika mimba,
aliisubiria kwa hamu sana bila mafanikio. Walikuwa wakikaribia kumaliza mwezi
wa tano tokea Vai aanze kuishi nae hapo.
~~~~~~~~~~~~~~~
Alijitahidi asionyeshe huo wasiwasi, lakini
uzalendo ukamshinda. “Hivi unatumia njia yeyote ya uzazi wa mpango?” Zinda
alirusha swali siku hiyo ya jumamosi walipokuwa wakipata kifungua kinywa
asubuhi. Hakuwa ameenda kazini. Waliamka kama mida ya saa nne hivi baada ya
kuchelewa sana kulala usiku uliopita. Alitoka kazini akamkuta Vai
amejitengeneza akimsubiria watoke. Zinda akiwa amechoka, akaona itakuwa ni
kumkatili tu Vai. Alishajitengeneza vizuri. Aliingia bafuni kuoga, akatoka kwa
haraka akiwa ameshavaa na yeye. Alimwambia anahamu ya kwenda kula samaki choma.
Zinda akaendesha gari mpaka mtaa wa Kawe, ambako alijua atapata samaki wazuri wakuchoma.
Madhari waliyokutana nayo huko, iliwatuliza na kuwafanya wakae hapo kwa muda
mrefu. Zinda akinywa pombe zake, Vai akinywa soda na chakula.
~~~~~~~~~~~~~~~
Vai alishituka sana. Hakujua swali hilo
linamakusudi gani. Kwamba hataki mtoto, kwa hiyo anamkumbushia kutumia kinga.
Au anataka mtoto lakini anamshangaa hashiki mimba kwa muda wote! Kichwa
kikamzunguka. Akakumbuka ni kweli hakuwa anatumia kinga yeyote ile. Sasa kwa
nini hajashika mimba muda wote huo!? Mawazo yakamrudisha siku ile alipokuwa
chumba cha upasuaji akisafishwa. Akakumbuka mazungumzo ya daktari aliyekuwa
akimuhudumia akiongea na wasaidizi wake huku yeye amelala kwenye meza hiyo.
Daktari alikuwa akisisitza kuwa amekuta uozo mkubwa humo ndani. Anajitahidi
kusafisha kwa makini kwa kadiri ya uwezo wake ili kumsaidia apone na asipoteze
kizazi. Maumivu makali aliyokuwa nayo wakati wakimsafisha, Vai hakujua hatima
ya kizazi chake. Alikuwa akilia kama anayechinjwa.
Alishamuomba mara kadhaa huyo daktari mchome
sindano ya kupunguza maumivu, lakini hakukumbuka hata kama alichomwa au la.
Waliishia kumuhoji maswali ya jinsia ya mtoto aliyekuwepo humo na umri wake
kabla hajatolewa. Kwa kuwa alikuwa na maumivu makali, hakuwa akijibu bali
aliendelea kulia.
~~~~~~~~~~~~~~~
“Vai!?”
Zinda akamtoa kwenye mawazo. “Kwa nini unaniuliza hivyo?” Vai akauliza na yeye
huku akinyanyua kikombe chake cha chai na tabasamu kumuashiria yupo sawa.
Lakini hofu ilishamwingia. “Nataka tu kujua.” Zinda akaongeza. “Unajua Viola
alifanya kosa maishani, sitaki na mimi kurudia kosa.” Vai akajitetea.
“Kosa gani?” Zinda akauliza. “Nilikwambia kuwa
alimpokonya mwanamme wa mtu akazaa naye akijua ataolewa. Yule kaka akamzalisha
Viola, akaishia kuoa mwanamke mwingine. Viola amebaki anahangaika na mtoto.
Anamtumia pesa za matumizi za mwanae tu. Lakini bado mzigo ni wake yeye. Mtoto
akiumwa anahangaika yeye peke yake. Mwanaume anafurahia na mwanamke mwingine.
Nimejiapia mimi kuzaa ni mpaka ndoa. Mwanaume anayekupenda kwa dhati,
hakuchezei tu. Anakuoa ndio mnazungumzia swala la watoto. Mambo ya watoto
kwanza, binafsi naona ni kwa wale wanaume wabinafsi.” Hapo Vai akamfunga mdomo
Zinda.
Walishaishi pale kwa muda wote huo, bila kumtamkia
ndoa. Akajua hapo anaambiwa yeye. Kwa ukweli hakuwa ameona mapungufu yeyote ya
ajabu sana kwa Vai. Kwa nini asimfanye mke? Akamkumbuka Nanaa. Nanaa alishakuwa
na sifa zote za kuwa mkewe. Alimuona jinsi alivyomudu kuishi na familia ya Geb
pale kwake bila shida yeyote wakati Liz alikuwa akilalamika akitaka waishi peke
yao, wengine waondoke au Geb awatafutie mahali pakuishi. Danny alishamwambia
sifa za Nanaa. Jinsi anavyopika vitafunio vizuri na vile anavyomjali Geb na
kila mtu pale ndani. Heshima na upendo kwao. Danny alishamwaga sifa nyingi tu
kwa Zinda. Kwa hiyo Zinda alikuwa akimtongoza Nanaa aliyekuwa akijua atamfaa
yeye na familia yake. Ndio maana tokea mwanzo kabisa, hakusita kumwambia Nanaa,
atahamisha ndugu zake mjini. “Nanaa ndio
angekuwa mke mzuri kwangu.” Zinda akawaza.
“Lakini hawana
tofauti sana. Hata Vai anafaa tu. Lakini atawaweza ndugu zangu kweli wakati
dada mmoja tu aliye naye amemshindwa! Kila akiongelea juu ya dada yake, anakuwa
akimuongelea vibaya! Sipendi jinsi anavyomjibu mama yake. Atamuweza kweli mama
yangu yule muongea kilugha wakati wote? Lakini kwangu ni mwema sana. Vai
anaweza kunifaa. Japo hatamfikia Nanaa. Nanaa..” Zinda aliendelea kuwaza. “Au wewe bado unahisia
za mapenzi kwa Nanaa?” Vai akarusha swali la haraka lililomfanya Zinda akaribie
kupaliwa. Ni kweli alikuwa akimuwaza Nanaa. Akakumbuka kiuno cha Nanaa
alichokuwa akikitamani hata kujitambia mbele ya kina Geb, Danny na James.
Akiapa siku akimkamata Nanaa kitandani, hatatoka. Alishasema atalipia mpaka
sauti ya Nanaa! “Yule mshenzi ndio
anafaidi sasa hivi! Mpaka mtoto amempa!” Zinda alizidi kuchukia moyoni.
“Eti Zinda? Maana tunaishi wote hapa. Sikusikii
hata ukizungumzia hatima yetu. Ndio nauliza bado upo na hisia za kimapenzi kwa
Nanaa?” Vai alisisitiza swali lake. “Kwa
nini ufikirie hivyo Vai? Huo ni ukurasa ambao nishafunga. Sina mpango naye hata
kidogo. Hata akirudi leo kwa magoti, simtaki. Wanini tena? Kwanza ni kama
umenikumbusha wewe sasa hivi kwa kumtaja jina lake. Sijawahi hata kumfkiria
mjinga yule. Nilishamfuta kwenye kumbukumbu zangu.” Zinda aliongea huku
amekunja uso.
“Sasa ili asikukere zaidi, mpe talaka yake muachane
moja kwa moja?” Hapo hapo Vai akamuwahi. Zinda akashangaa. “Kama kweli umemfuta
mawazoni basi muache kihalali.” Huo ulikuwa mtihani kwa Zinda. Ndio adhabu
aliyokuwa ameishikilia kwa Geb na familia yake na akaapa kuwaumiza ipasavyo.
Aliweka uthibiti wa cheti cha ndoa ambacho alikitafuta kwa shida sana,
akadanganya mpaka akapata hicho cheti cha ndoa yake na Nanaa. Akakiweka
hadharani ili hata ikitokea Geb anataka kufunga ndoa hata serikalini sio
kanisani tena, ashindwe.
“Mimi sioni sababu ya talaka. Kwanza ndoa yenyewe
ya magumashi. Waache walipe kwa ubaya walionitendea.” Zinda akazungusha. Vai
akambadilikia. “Kwa hiyo bado unaumwa na penzi la Nanaa!? Mimi nipo na wewe
hapa. Nakupa penzi langu. Leo unanitamkia Nanaa ni bora kuliko mimi!?”
“Sijasema hivyo Vai!” “Unamaanisha nini? Kama kweli huna hisia naye tena, kwa
nini kutaka kuendelea kulipiza kisasi kwa mtu asiyekuhusu? Inamaana bado
unampenda Nanaa!” “Hata kidogo. Sina mpango na yule Malaya.” Zinda aliongeza
msisitizo.
“Kinacho kushinda kumpa talaka sasa ni nini?” Vai
alishakuwa mwekundu. Mtoto huyo wa kichaga hakutaka ujinga. “Ndoa yenyewe ni ya
uongo Vai. Kwa nini tunagombana kwa ajili ya hilo? Kwanza ni wewe mwenyewe ndio
ulinipa hilo wazo mkisaidiana na Viola! Kwa nini sasa unataka kunigeuka?” “Sasa
kama mimi ndio nilikupa hilo wazo, ukakubali, ndio nakupa tena wazo jingine.
Kampe talaka, sisi tuendelee na maisha yetu. Maana sasa hivi yeye anashindwa
kuolewa kisheria kwa kuwa inajulikana ana ndoa na wewe kihalali, na wewe hutaweza kuoa kwa kuwa kisheria
unajulikana una ndoa naye halali. Labla uniambie unasikia wivu kuona Nanaa
anaolewa.” “Wivu wa nini sasa?” Zinda akaona amebanwa.
“Kama kweli huna mpango naye na huna wivu,
mwandikie talaka. Muachane kihalali ili maisha mengine yaendelee.” Zinda
akasimama bila kujibu. Akakusanya vyombo pale mezani akaingia jikoni. Vai
akamfuata.
“Kweli nimeamini ulikuwa ukinichezea. Sasa hapo
ndio ningeshika mimba! Si ungeniacha na mtoto wangu ukarudi kwa Nanaa?” “Naomba
punguza sauti na hasira Vai!” “Kwa nini?” Vai akauliza huku ameshika kiuno.
“Mwenzio maisha yake yanaendelea kama kawaida! Anaishi na mpenzi wake. Amezaa
naye mpaka mtoto. Eti wewe umebaki hapa unamsubiria! Kama sio ujinga huo ni
nini?” “Mimi simsubirii Nanaa. Kwanza wewe mwenyewe uliniambia Nanaa hajui
kupenda.
Anamwibia
tu huyo Geb. Sasa kwa nini leo unamtamka kama mpenzi wake?” Vai alitamani
kupasuka kwa hasira.
“Hivi unawazimu wewe Zinda? Yaani katika mazungumzo
yote hayo umesikia neno ‘mpenzi wake’
tu? Mambo yote hujasikia!? Sasa umeshanithibitishia unamtaka Nanaa kuliko
chochote hapa duniani. Yaani upo radhi ukose kuanzisha familia yako. Ya mke na
watoto, ilimradi uhakikishe Nanaa haolewi! Kwa hiyo unabaki vile vile kama
ulivyoapa mwanzoni kama wewe hutampata Nanaa, basi hakuna atakayempata?” “Sio
kweli Vai.” Zinda alijitetea kwa shida sana. Vai alimkaba vilivyo.
“Unajua mimi ndio kaka nategemewa nyumbani kwetu.
Natakiwa kuoa na kuwa na watoto. Siwezi kumuacha Nanaa akaharibu ndoto zangu na
familia yangu.” “Basi kama huna taarifa, ujue Nanaa amekukwamisha. Huwezi
kupenda wala kuwa na familia kwa ajili yake. Husogei wala hutasogea hapo.” “Sio
kweli Vai. Yote niliyofanya ni wewe ulinishauri! Sasa kwa nini kunigeuka?”
“Usinifanye mimi mtoto mdogo Zinda. Unarudia mambo tuliyokwisha ongea.
Nimekwambia kama ulinisikiliza mwanzoni, basi nisikilize na sasa hivi.
Kinachokushinda kufuata ushauri wangu tena sasa hivi ni nini, kama sio kuwa
unaona nakushauri kuwa mbali na Nanaa?” Vai alikuwa amemtolea macho akimuuliza
maswali ya kweli. Watoto wa mama James huwawezi kwa kuongea. Wakikuamulia,
huweki neno kama mama yao. Vai alimkaba Zinda, akabaki akirudia hoja.
“Sasa nisikilize Zinda. Endelea na maisha yako.
Tafuta mwanamke mwingine utakayeendelea kumchezea na kumtumia humu ndani kama
mimi. Umlale usiku kucha na asubuhi kabla ya kwenda kazini. Akufulie nguo zako
na kukupikia. Mwanamke atakayekuwa anakufikiria wewe wakati wote, wakati wewe
unamfikiria Nanaa. Kwa heri.” Vai akatoka pale jikoni kuelekea chumbani kufungasha.
~~~~~~~~~~~~~~~
Kwa Zinda kumewaka. Vita ya Wenyewe Kwa Wenyewe.
Wakati Nanaa na Geb wametulia. Maisha yanaendelea, Geb amesema wamuachie
Mungu na Nanaa ameridhia. Amani na umoja vimerejea kati yao. Hakuna hata anayekumbushia
ubaya wa watu walio watenda. Lakini kwa Zinda mambo yanatibuka. Zinda achague
leo. Kusuka au kunyoa. Vai ambaye hana uhakika kama anazaa lakini yupo hapo kwake
akimridhisha vilivyo. Penzi zito, ametulia ndani, au Nanaa ambaye anazidi
kumzalia Geb watoto?
Nani wa nani?
Usikose muendelezo kujua kitakacho jiri.
Safari hii Mungu Anatoa Muujiza Upi?
Wakati Mwingine Mungu Hutumia Hata Adui zako Kukufanikisha. Anaweza kutumia
hata jiwe, kujipatia utukufu!
Je, Ndilo atakalofanya kwenye hili pia?
Endelea kufuatili
0 Comments:
Post a Comment