“Ndio katika mambo niliyotaka tuzungumze jana,
lakini uliondoka.” Nanaa akahisi kizunguzungu. “Nilimuoa ndoa ya mahakamani ili
ili, na nihii…” Akamgeukia Geb, aliyenyanyua kikombe chake cha uji kwa mkono wa
kushoto akanywa, huku amembeba mwanae kwa mkono wa kulia, kisha akabaki
akimtizama na yeye Zac. Akacheka. Geb alikuwa akimtizama Zac kwa dharau. “Hivi
unajua jana uliniliza wewe? Nikajua nimepata mpinzani wangu! Kumbe ni wewe
tapeli wa mapenzi tu!” “Mimi sio tapeli wa mapenzi Geb. Nilimuoa Ndina, baada
ya Nanaa kuniacha, na sasa narudi kwa Nanaa, baada ya kuachana na Ndina.”
“Umeruka kipengele kimoja Zac. Ulikuwa na mahusiano ya kimapenzi ya siri na
Ndina, wakati ulipokuwa na Nanaa.” Geb akaongeza na kuzidi kumshangaza Nanaa na
kumuumiza.
“Kumbe mlikuwa wapenzi!?” Nanaa akauliza
akionyesha kuchanganywa zaidi. “Wakati ule tulipokuwa na wewe, hatukuwa
wapenzi, ila tulishakuwa na mahusiano naye tulipokuwa mwaka wa kwanza,
tukaachana kabisa. Na yeye akapata mchumba wake, na mimi ndio nikakupata wewe.”
Zac akajitetea, asijue kuwa ndio anaharibu zaidi. Nanaa aliinama huku amefunika
uso wake akilia.
“Niliwezaje kuwa mjinga kiasi kile
nikashindwa kuwagundua!?”
“Kwa kuwa sikuwa na mahusiano naye tena! Nilikuwa na wewe tu Nanaa. Nakupenda
wewe. Nipe nafasi unisikilize. Twende mahali tukazungumze.” “Hutaondoka na
Nanaa hapa, mpaka umwambie ukweli wote, Zac. Na ninakuonya, usimdanganye. Kwa
kuwa sitakuruhusu uendelee kumdanganya. Madhara yakukiuka huu ushauri wangu,
utayapata wewe na Ndina mzazi mwenzako.
Sikutanii.” Geb alisisitiza. Asijue anazidi kumchanganya Nanaa zaidi. “Umezaa na Ndina!?” Nanaa akauliza akionyesha
kuzidi kuchanganyikiwa zaidi ya mwanzo. “Wewe Geb
umemfahamuje Ndina?” Geb akamgeukia Nanaa. “Naomba usikie kutoka kwa Zac
mwenyewe, ila ujue hivi tunavyozungumza, Ndina ni mfanyakazi wangu.” Geb
akajibu na kunyanyua tena kikombe cha uji. Alikuwa amekaa wakati Nanaa na Zac
wakiwa wamesimama.
“Nakupenda Nanaa.” Zac akaongeza. “Hayo ndiyo
maneno unayojua Nanaa anapenda kuyasikia. Kwa hiyo unayatumia kwa wingi ili
kupumbaza akili zake, ashindwe kufikiria. Naomba acha kumdanganya Nanaa,
mwambie ukweli.” Geb aliendelea kusisitiza. “Kama unaona haupo tayari
kuzungumza na Nanaa, uniambie, nimtume dereva amlete Ndina sasa hivi. Ili yeye
ndio ampe ukweli wote Nanaa. Ujinga na umalaya uliokuwa ukiufanya huko nchini
Malaysia. Vile ulivyomtelekeza yeye na mtoto baada ya kufika huko. Yote hayo
nitataka Nanaa ayafahamu, ili akujue vile ulivyo Zac. Na ajue kwenye hiyo
mikono inayomkumbatia sasa hivi, ina uzoefu wa kuliwaza wanawake kama yeye, na
hiyo midomo inayombusu sasa hivi, ajue ina uzoefu wa kudanganya na imepita kwa
wanawake wengi tu, na wala yeye hatakuwa wa mwisho, kwa kuwa ndivyo ulivyo.
Hawakuiti player kwa makosa. Ni kwa kuwa una uzoefu wa wanawake. Unajua
kucheza na akili zao na fikra.” Geb akaendelea, akisikika ameanza kukasirika.
Nanaa akajua.
“Kwa masaa ambayo hata hayajatimia 24, tokea
ukutane na Nanaa, umefanikiwa kuingia kwenye akili zake, yupo tayari kuniacha
mimi na mtoto anayempenda kuliko nafsi yake, ili awe na wewe! Umempa njia
rahisi sana yakumuwezesha kuwa mbali na sisi, ili tu uwe naye kwa muda. Nanaa
amepata familia ya watu wanaompenda, Zac. Hakuna hata mmoja kati yetu
asiyetambua thamani ya Nanaa. Ndio maana leo hii siku ya kazi, mimi, Geb,
ninayemuweka mjini mkeo na mtoto wako, nipo hapa sasa hivi na Nanaa. Unajua ni
pesa kiasi gani napoteza kila saa ninayokaa hapa?” Geb akagomba.
“Tena nikiwa na wewe unayeniharibia siku yangu
ninayolipia garama kubwa sana! Siku ya leo ilikuwa yangu, Nanaa na Liv.
Nimekubali mambo yote yasimame kwa ajili ya hawa watu wawili, lakini umevuruga.
Mama yangu amepika vyakula vyote vile sio kwa kuwa hana mambo mengine
yakufanya, au Nanaa hawezi, nikutaka Nanaa atulie, apate muda wakufikiria mtoto
na mimi tu, lakini wewe mvurugaji umeingia. Umeacha kidonda kikubwa sana moyoni
kwa Nanaa. Kimeharibu moyo wa Nanaa, haamini tena kama anaweza kupendwa kwa
dhati.” Geb akaendelea.
“Haamini wanaume wote. Haamini kama wapo wanaume
tunaweza tukawa na hamu yakufanya mapenzi, lakini tukamudu kutawala hisia zetu.
Haamini, kwa ajili yako.” Geb akaendelea kuharibu zaidi. “Nanaa anajua kama
yupo mwanamke wakiarabu unayeishi naye sasa hivi, tena ndiye anayekuweka hapa
mjini? Umemwambia kama hizo zawadi unazotaka kumpa sasa hivi, zinatoka kwenye
pesa anayotolea jasho mwanamke mwenzie?” “Nitamuacha kama Nanaa akinikubali.”
Zac alijibu bila wasiwasi na kumshangaza Nanaa.
“Naomba uondoke Zac. Tafadhali
sana, naomba ondoka.”
Geb alishamaliza uji wake kwenye kile kikombe kidogo, akabaki akiwatizama. “Ondoka na zawadi zako.”
Nanaa akasisitiza. “Nashauri uweke nguvu kwa mtoto wako, kama
umeshindwana na Ndina. Yupo katika wakati mgumu sana. Mtoto wako mgonjwa, na
Ndina anasema hutaki kuzungumza naye. Ni wakati ambao mtoto wako anakuhitaji
sana, kwani ugonjwa alionao, unahitaji uangalizi wakaribu wa mama yake, na yeye
anashindwa kuwa naye wakati wote, kwa kuwa anahitajika awepo kazini, atengeneze
pesa. Mtafute Ndina, ujue habari za mtoto wenu. Haya, naomba uondoke kama
alivyokuomba Nanaa.” Geb akasisitiza.
Kisha akamgeukia Nanaa. “Kama huyu ndiye Zac
uliyekuwa ukinisimulia, hastahili hata tone la chozi lako. Nakuhakikishia
Nanaa. Zac unayemfikiria na kumzungumzia wewe, siye huyu hata kidogo. Hastahili
umlilie. Na ninakushauri usipokee vitu vyake. Ana mtoto mgonjwa, ambaye hataki
kumuhudumia, anazunguka na wanawake tu mjini. Mwanae anahitaji msaada wa Zac, kuliko hivyo anavyopoteza pesa kukununulia
wewe zawadi huko Kariakoo, halafu anakudanganya amenunua nje ya nchi. Amerudi
nchini muda mrefu sana. Hawezi kuwa alikununulia zawadi muda wote huo,
akazitunza wakati yeye mwenyewe anatunzwa na mwanamke.” Bila kuongeza neno, Zac
akatoka akiwa na mfuko wake mkononi, akamuacha Nanaa amesimama anakausha
machozi huku ameinama. Aibu! Mbio za sakafuni zikaishia ukingoni.
~~~~~~~~~~~~~~~
Geb akasimama, akaenda kuchukua mizigo yote pale
mapokezi, akarudi kwa Nanaa, twende ukale. Wakaanza kuongozana kurudi kwao, Geb
akiwa amembeba Liv na vyakula, huku Nanaa akifuata nyuma taratibu. Hakujua
aseme nini kwa Geb. Samahani halikuwa neno sahihi. Kwani hakuona kosa kuwa na
Zac. Labda Asante, kwa kumfungua macho au kumuokoa kutoka kwenye hatari
yakutapeliwa tena. Aibu ilimuingia, akaanza kujichukia. “Nina tatizo gani mimi? Kwa nini nakuwa mjinga wa kupitiliza? Naona
swala la mwanaume limeshindikana, heri nitengeneze kwangu.” Nanaa
akaendelea kuwaza wakati wanaingia ndani.
“Naona anasinzia huyu. Naomba nisubiri kwanza
nibadili hizi nguo, na nioge kabisa kutoa mkosi wa Zac, kabla mwanangu
hajanigusa.” Nanaa aliongea mara tu walipoingia ndani, akapitiliza bafuni. Geb
alitamani kucheka alipokuwa akimsikia akioga kweli. Akabaki akicheza na mwanae
kwa kumrusha rusha ili asilale. “Nanaa fanya haraka. Liv amelemewa.” Nanaa
alitoka kwa haraka akiwa na khanga tu. “Nimeona mpaka nivae, nitamchelewa
zaidi. Na akilala sasa hivi huyo, hataamka mpaka jioni. Na hata nikimuamsha
hapo katikati, hatanyonya vizuri.” Geb akamwangalia. Mwili wa Nanaa ulikuwa
mtupuuu. Umefunikwa na khanga tu. Geb akavuta pumzi kwa nguvu kama kujiweka
sawa. “Muone anavyorembua!a Anaonekana atalala sasa hivi.” Akamchukua nakuingia
naye chumbani. “Nyonya kidogo kabla hujalala Liv mwanangu. Usingizi gani huo
hauishi mama! Eti?” Alimsikia Nanaa akizungumza na mwanae huko chumbani.
Akambadilisha diaper na nguo nyepesi ya kulalia,
akamuweka kwenye ziwa. Akavuta maziwa kidogo tu akaanza kulala. Nanaa alibaki akimkuna
miguu ili aamke anyonye. Alifanya hivyo kwa muda. Liv anaamka, anavuta maziwa
kidogo, anarudi kulala. Hivyo hivyo mpaka alipopotelea usingizini kabisa. Nanaa
akacheka. “Yaani Liv wewe! Sijui umekuaje? Wala hatuzungumzi tena kama zamani!
Muone. Umelala kama umetoka kulima shamba!” Akamuweka kitandani kwake.
Alipohakikisha amemfunika mwanae vizuri, ndipo
akaanza kujipaka tena mafuta mwilini mwake. Akavaa kigauni kilichochanua chini,
lakini kifupi kiliishia juu kidogo ya magoti. Akachana tena nywele zake,
akatoka.
~~~~~~~~~~~~~~~
Alimkuta Geb amekaa sebuleni ametulia. “Geb!” Geb
akamgeukia. “Kama hutatoka, naomba nitoke kidogo, nikakamilishe mambo yangu ya
chumba. Nitajitahidi kuwahi kurudi.” “Nilifikiri ulimaliza jana!” Geb
akashangaa kidogo. “Hatua ya kwanza nimefanikiwa, namshukuru Mungu.” “Kwani
kuna hatua ngapi?” Nanaa alifikiria kidogo, akamsogelea. “Sina kitu chochote
pale kwangu. Nimeweka maboksi ya vitabu, na vitu vyangu vyote chini sakafuni.
Na sakafu yenyewe sio nzuri, nahofia maboksi yanaweza kupata unyevu, nikaharibu
kila kitu. Mapazia yenyewe niliyoning’iniza ni yale yale niliyokuwa nikitumia
chuoni. Madogo sana, ni kama yapo nusu dirisha. Nilifikiria kununua kwanza
kabati la vitabu, lakini naona nirudi kwenye wazo la kununua kwanza kitanda,
ili ikitokea..” Nanaa akanyamaza akaenda kukaa kwenye kochi la pembeni ya Geb.
Ile gauni ilifika katikati ya mapaja, ikaacha
mapaja yake nje. Akaanza kuhangaika kuvuta chini kana kwamba hakuwa akijua kama
alivaa nguo fupi. Asijue ndio anavuta macho ya Geb zaidi kumtizama.
“Nitajitahidi nisichelewe. Nataka nitoke mara moja nikanunue kapeti hata ya
plastiki tu, ya kutandika sakafuni, na kitanda. Sitakawia. Nimeona vinauzwa
palepale, karibu na kwenye chumba changu.” “Sitawahi kuja kuthubutu kukufukuza
tena Nanaa. Najua huniamini tena, lakini haitakaa ikatokea nakufukuza. Hata
iweje.” Nanaa alibaki kimya huku ameinama. Tayari machozi yalishakuwa kama
mvua.
Akaanza kujifuta. “Naomba nipe nafasi
nikuhakikishie nimebadilika. Hata yale masharti niliyoweka nimetoa. Upo huru
kufanya lolote, kwa huyo mtoto na pale nyumbani. Ila naomba tu tuwe
tunawasiliana.” Nanaa akanyamaza huku akifuta machozi.
Penzi Halitaki Kiburi.
K |
imya
cha muda mrefu kikatanda, Nanaa akiwa ameinama. Alipoona halii tena, Geb
akaendelea. “Eti Nanaa?” “Nashukuru.”
“Nanaa! Acha kunipa jibu la jumla la kunitoa njiani.” “Nimekushukuru kwa
kuniamini tena. Kunipa uhuru na mtoto.”
“Mbona kama unanikwepa Nanaa?” “Sikukwepi!” “Mazungumzo yote yanayotuhusu mimi
na wewe, unayakwepa!” Nanaa akanyamaza. “Umeniambia umenisamehe, lakini mbona
hivyo!? Kila nikikuuliza hali yako wewe, unaniambia mambo ya mtoto! Jana
nilikwambia nimeacha kwenda kazini, nataka kubaki na wewe na Liv, umeamka
asubuhi unajiandaa kuniacha hapa na Liv ili uende kwa Zac! Sasa hivi nakuomba
nafasi nyingine, tuwe kama zamani, unaniambia unashukuru! Ni kwamba umeamua
kuninyima mimi nafasi ya pili ambayo ulikuwa tayari kwenda kumpa Zac, mwanaume
aliyekuwa amekusaliti?” Geb aliongea kwa kulalamika.
“Hapana Geb! Hata jana nilikwambia nakwenda
kumsikiliza kwanza ndipo nitaamua. Zac alinionyesha kunihitaji, lakini wewe
ulinionyesha kwa maneno na vitendo hunihitaji, Geb. Leo tumekaa hapa kwa sababu
ya Liv tu. Kama Liv angekukubalia maziwa ya kopo na kutonihitaji mimi, nina
uhakika, usingenitafuta tena, Geb. Nilikuomba msamaha zaidi ya mara tatu,
lakini ulishindwa kunisamehe. Hata uliponiruhusu niishi pale kwako, bado
ulinionyesha wazi hunihitaji.” “Sio kweli Nanaa.” “Kweli Geb. Unafikiri ni kwa
nini nilikuwa tayari kurudi kwa Zac, kama si kunitamkia hunihitaji?” Nanaa
alihisi Geb hajui au hakumbuki mambo aliyomfanyia.
“Nanaa, nilikupenda na kuamua kukufanya uwe wangu
kabla ya Oliva. Oliva ndio njia yangu pekee ya kukumiliki. Sema nimekwenda
umbali ambao hata mimi sikutegemea, nikakuumiza zaidi. Lakini mapenzi
niliyokwambia siku ile tukiwa Morogoro, hayajabadilika Nanaa. Bado
nakupenda kuliko nafsi yangu.” Nanaa akamwangalia
kama haamini.
“Hivi unajua nimekuwa na Liz kwa muda mrefu sana
kuliko wewe?” Nanaa akanyamaza. “Unafikiri kwa nini wewe tumekuwa kwenye
mahusiano ya muda mfupi sana, lakini ukawa umeshika mimba yangu?” Nanaa akashindwa
kujibu. “Kwa kuwa mimi ndio nilitaka unizalie watoto Nanaa. Haikuwa mimba ya
bahati mbaya kama ulivyosema, kuwa mama yako alifanya kosa, na wewe ulifanya
kosa kushika mimba bila makubaliano au ndoa. Sio na mimi labda mwanaume
mwingine. Mimi huwa sikosei, Nanaa. Silali na msichana bila kondom. Lasivyo sasa
hivi ungekuta Liz ana watoto wangu kwa
kuwa alitamani sana tuzae naye mtoto wa kiume na wakike, lakini niliamua Liz
hatakuwepo kwenye maisha yangu kwa muda mrefu. Ndio maana ulipokuja tu,
nikakusoma haraka, niliporidhika na wewe, ikabidi kutafuta vitu vitakavyokuweka
kwenye maisha yangu mpaka kifo. Kwanza nilijua huwa huna tabia ya kuwa na
mahusiano ya muda mrefu, ni mwepesi kujitoa kwenye mahusiano, kwa sababu zozote
zile, na huwa hurudii matapishi. Mwanaume akikuumiza huwa humrudii hata iweje.
Yaani kama hichi unachonifanyia mimi sasa hivi.” “Sio
kweli Geb. Ni kwa kuwa sikubahatika tu kupata mwanaume wa kuwa na mimi muda
mrefu.” Nanaa akajitetea huku akifuta machozi.
“Inawezekana ni kweli umebadilika Nanaa. Nimeona
ulitaka kuvunja rekodi kwa Zac.” Nanaa akainama kwa aibu. “Hivi unakumbuka
uliniacha bila kutaka kunisikiliza? Hata nilipokubembeleza ubaki nijieleze,
hukutaka, ukanitukana na kuondoka! Ulibadili namba ya simu ishara ya
kuthibitisha kile ulichonitamkia, hutaki nikutafute tena. Hukutaka kurudi tena
kwangu, ukakubali kubaki na ujauzito wangu ukaamua kumlea mtoto wangu kwa
garama yeyote ile bila mimi! Tena ukijua nakupenda Nanaa. Nikiwa nimekutamkia
nilikuwa na wewe usiku kuchwa wakati mgonjwa. Nilikuwa najiiba kuja kulala na
wewe usiku ili kukuuguza. Si hospitalini si nyumbani kwa Antii, nilikuwa na
wewe. Sikupitisha hata siku moja, nilikuwa na wewe usiku kwa kuwa mchana James
alikuwepo na alitupiga marufuku tusikusogelee tena. Kwa kosa la kukusahau nje
ya ukumbi. Kama ningekuwa na mapenzi na Liz, au tupo kwenye mahusiano na Liz,
si huo ndio ungekuwa wakati wa mimi kuwa na Liz?”
“Wala sikuwa najua Geb. Nilikuona
mara moja tu. Na wala sikujua kama ilikuwa ndoto au la! Kwa kuwa nilipokuwa
nikiamka sikuwa nakukuta! Sikufahamu kama ulikuwa na mimi wakati mgonjwa Geb.
Nilijua ulinisusa.”
“Lakini nilikwambia Nanaa. Nilikupigia simu nikiwa safari. Nikakuomba rudi
nyumbani. Angalau nikuone. Ukalalamika sikupendi. Nikajaribu kukuelezea ukweli.
Ukaja kunikuta na Liz, ukasahau kabisa nilichokwambia. Kwa haraka sana bila
kufikiria ukanitukana na kunitoroka kama ulivyofanya Marangu. Nilijua Liz
angekuwepo Marangu. Unafikiri ni kwa nini nilitaka na wewe uwepo? Au hata
kwenye harusi. Kama nilitaka mapenzi ya wizi, kwa nini basi nikubembeleze uje
kwenye harusi ambayo najua nitasimamia na Liz, tena kwa style yakushikana
mikono?” Hapo ndipo akili ya Nanaa
ikaanza kufikiria vizuri sasa.
“Eti Nanaa? Kama kweli mimi ni mwizi wa kiasi
hicho kwako, kwa nini nitake na wewe uwepo kushuhudia wizi wangu?” “Mimi sijui Geb? Sielewi!” “Kwa nini huniulizi?”
Kimya. “Hivi unakumbuka tulipokuwa Morogoro uliniambia ni kwa mara ya kwanza
unajisikia kupenda. Ulikuwa ni ukweli au ni katika kunifurahisha tu?” “Sijawahi
kukudanganya Geb.” “Sasa mbona huishi kile unachokisema Nanaa? Kwa nini unanikatia
tamaa mapema hivyo? Nilikubembeleza twende wote Marangu. Liz akakutingisha
kidogo tu, ukaniacha Marangu. Unanikuta uchi nimetoka kuoga na Liz yupo
kitandani, unanitukana na kuniacha bila kunipa nafasi ya kunisikiliza. Unajua
kwa nini jana nililia?” Nanaa kimya.
“Niliona unampa nafasi Zac, ambayo na mimi
nilikuomba Nanaa. Ulikuwa tayari kuniacha mimi na Liv, uende ukamsikilize Zac.
Kwa haraka na yeye alikuwa na kosa kama langu tu. Lakini mwenzangu ulikuwa
tayari kwenda kumsikiliza, mimi ukanipuuza.” “Lakini Geb, nilikupa nafasi hiyo
zaidi ya mara 3. Tena mimi ndiye nilikuwa nikikuomba msamaha. Nikitaka yaishe.
Ukanikatalia. Zac alirudi, akiniomba msamaha na kunitaka tena. Sasa
ningefanyaje tena kama sio kumpa yeye nafasi?” Nanaa akajitetea.
“Si nilikuomba msamaha siku niliyokufuata na
Oliva kule hotelini? Nikarudia tena na tena. Ukaniahidi umenisamehe. Leo
unanipa mpango wa kuniacha mimi na Oliva, uje uwe nasi kama mfanyakazi wangu
halafu jioni unarudi kwa Zac! Kweli Nanaa?” “Sikujua
kama unanihitaji tena, Geb. Uliniambia nipo huru kwenda kwa mabwana zangu. Ila
nirudi kunyonyesha mtoto. Ni kweli uliomba msamaha. Lakini nilijua ni msamaha
wa kunifukuza siku ile kama ‘paka mwizi’. Sio vinginevyo.” “Kama
kweli wewe ulikuwa na mapenzi ya dhati kwangu, kwa nini hukutaka kuhangaikia
hiyo ‘vinginevyo’? Kwa nini
ulikubali kwenda kuanzisha mahusiano au kufufua hivyo ‘vinginevyo’ kwa Zac, ukaniacha mimi unayekiri unanipenda? Au ni
mimi tu ndio nawajibika na ‘vinginevyo’?
Ikitokea mimi naacha, ndio inakuwa basi?” Hapo Nanaa akaishiwa jibu.
“Sasa kwa kuwa mimi nina mapenzi ya dhati na wewe
Nanaa. Na nilitaka uwe kwenye maisha yangu mpaka kifo, ikabidi kukusoma zaidi
ili nijue ni kitu gani kinaweza kukufunga kwangu usinikimbie hata iweje? Ndipo
nikagundua siri ambayo nimeitumia, japo nakiri nimefika mbali.” “Siri gani?” Nanaa akauliza kwa upole. “Nilijua
kwa makuzi uliyokuwa wewe, kwa namna yeyote ile hata iweje, ukija kupata mtoto,
utataka kumtunza huyo mtoto kwa garama yeyote ile. Kwa hiyo nikajifunza
mzunguko wako wa hedhi kwa haraka sana, ili kabla hujanitoroka uwe unamtoto
wangu.” Nanaa akashangaa sana.
“Geb wewe!” “Ningefanyaje Nanaa na mimi
nakupenda? Na ndio maana nilimchukua Liv tokea upo chuoni, nikijua utamfuata
tu. Ulipotaka kutoroka naye, nilijua ukifanikiwa kutoka pale, sitakuona tena
maishani. Ndio maana nilikuwekea masharti magumu nikimuweka Liv kama chambo
yangu nikijua alipo Liv, ndipo utakapo kuwepo daima. Nakiri nilifika mbali kwa
hasira kama unavyonifahamu, lakini naomba uniamini Nanaa, ni kwa kuwa nakupenda
na ninakutaka uishi na mimi. Ni mpango niliopanga kabla ya Liv hajaja duniani.
Nilikuchagua wewe uje kuwa mke wangu.” Zilikuwa ni habari ambazo Nanaa
angetamani angeambiwa mapema sana.
“Sikuwa na
haraka ya mtoto hata kidogo. Kama wewe ungekuwa ni mwanamke mvumilivu, unatulia
kwenye mahusiano, ningekuoa baada ya kumaliza tu chuo, halafu baada ya kama
miaka miwili ndipo tungefikiria swala la mtoto. Lakini niliamua kulipa garama
ya kuzaa kipindi hiki kigumu, ambacho nilishakipigia mahesabu nikajua ni
kipindi ambacho kitakuwa kina mambo mengi sana yatakayonifanya nisilale, wala
kutoweza kulea, lakini nilikubali yote hayo ili tu wewe uwepo kwenye maisha
yangu.” Geb akaendelea.
“Huu sio wakati ambao ningetaka hekaheka za
watoto, Nanaa. Mimi huwa napanga mambo yangu kwa makini. Yale ambayo yapo ndani
ya uwezo wangu, huwa napanga ni nini kitatokea kwa kipindi gani. Kwa hiyo kama
sijaenda kinyume na mipango ya Mungu, huwa najua lini nitafanya nini. Nakuwa
pia nimeshapigia mahesabu matokeo ya hicho nitakachofanya, garama ya kulipa, na
huwa najiandaa kabisa. Nilikuchagua wewe tokea zamani.” Nanaa hakujua aongeze
nini katika hilo.
“Ni nini kinakufanya usilale?” Nanaa akauliza kwa
upole. “Mwaka huo uliopita au kipindi hichi cha sasa hivi, nilikipanga kwa muda
mrefu kuwa ni kipindi cha mabadiliko ya maisha yangu. Nilipanga kuacha kazi
ambayo ilikuwa ikiniingizia pesa bila kuwaza itakuwaje, na kujiajiri mwenyewe
kama baba yangu. Nilipenda vile baba yangu alivyokuwa akifanya kazi kwa bidii
na nikaona amefanikiwa sana. Aliniambia juhudi huwa haimtupi mtu. Kwa hiyo tokea
nakuwa, baba alikuwa akija kunichukua na kunipeleka kwenye miradi yake,
nilikuwa nikimwangalia vile anavyofanya kazi kwa bidii tena bila kuchoka wala
kulalamika. Nikawa namtamania mafanikio yake. Alikuwa akinifundisha kwa maneno
na vitendo” Kidogo Nanaa akakumbuka stori ya Mama G. Historia yake na Magesa.
Aliishia wakina Geb wakati wanazaliwa, walikuwa wakiishi na baba yao. “Inawezekana alirudi kwa mkewe!” Nanaa
akawaza. “Lazima nitengeneze mazingira
ya mama kunimalizia ile stori. Inaonekana
ina mwisho mgumu.” Nanaa akaendelea
kuwaza.
Akakumbuka anazungumza na Geb. Akamwangalia ili
kuendelea kujua kinachomsibu. Geb akaendelea.“Sasa nilipanga kuanzia mwaka jana
na miaka miwili mbeleni, yaani miaka 3, iwe ni miaka ya mabadiliko ya maisha
yangu. Nijikite kwenye biashara tu. Nilijiwekea ni muda ambao tutafanya kazi
mchana na usiku bila kupumzika na pengine bila kupata faida kubwa au kutokupata
faida kabisa mpaka nifanikiwe na biashara ikue, kisha ifike kipindi ambacho
nitatafuta mtu mwaminifu nitakayemwamini na kunisaidia, halafu pengine wakati
huo biashara itakuwa imekomaa, na kuanza kujiendesha yenyewe bila uangalizi
wetu mkubwa, ndipo sasa tuanze kufikiria swala la watoto.” “Unamaanisha na
mimi!?” Nanaa akauliza kwa upole huku akimtizama Geb, na kumuomba Mungu aseme
ndiyo. Geb akacheka tu bila kutoa jibu.
“Sasa, sasahivi unaendeleaje na mipango
yako?”“Mbona unabadilisha mazungumzo yetu Nanaa? Bado unanikwepa.” “Sikukwepi
Geb?” “Sasa kwa nini unataka tuzungumzie mambo ambayo sio ya msingi kwetu?” “Ni
msingi Geb. Kutokulala kwako wewe, kunaniathiri na mimi.” “Kivipi wakati
hunitaki mimi wala vitu vyangu?” Nanaa akanyamaza. “Unanikataa mbele ya watu
Nanaa!” “Hapana Geb.” “Ni kweli. Ulikubali kumsamehe Zac uondoke uniache mimi
na mtoto, ili uwe na yeye!” Nanaa akajisikia hukumu moyoni akaegemea magoti,
nakuanza kulia tena.
“Mama amekuomba uweke vile vitu nyumbani, lakini
umemkatalia kwa sababu zile zile ulizonipa mimi nilipokuomba usikodishe chumba,
uvilete vitu nyumbani.” “Ulinionyesha hunihitaji
tena Geb. Ulinifukuza kwako, ningefanyaje? Sitaki kuhangaika maisha yangu yote
Geb. Wewe unajua ninavyoogopa kuwa peke yangu maishani. Ndio maana nilikuwa
nipo radhi kumsamehe Zac, ili nisiwe peke yangu!” “Nilikosa Nanaa, na
nikakuomba msamaha. Umenipa jibu la jumla kuwa umesamehe huku ukinionyesha wazi
hupo radhi kunirudia kama mpenzi. Hapo ulipo unatengeneza sehemu ya kukimbilia
siku nitakapo kukosea tena, au niseme umenithibitishia wazi kuwa muda na wakati
wowote utatuacha mimi na mtoto wangu. Si ndio hivyo Nanaa?” Nanaa alibaki kimya
akilia.
“Eti
Nanaa? Hivi umeshajiuliza ni lini na wewe utakuwa na kwako, au mtu wako ambaye
utamlinda na kumpigania hata iweje?” Kimya. “Uwe na nyumba utakayoilipia garama
kama hivyo ulivyohangaika kukutana na dalali. Dalali akakupeleka mpaka kwenye
hicho chumba, ukakuta kicho chumba kina watu wengine wawili ambao nao
wanakitaka. Ukahangaika kumtafuta mwenye nyumba. Ukahangaika kumfuata nyumbani
kwake ili tu kuzungumza naye na kumshawishi akupe wewe hicho chumba.
Ukahangaika mpaka ukachelewa kurudi nyumbani kuhakikisha unakipata hicho chumba
na kukimiliki.” Nanaa akaendelea kulia bila kujibu.
“Au kwa utayari uliokuwa nao wa kutuacha sisi ili
ukaishi na Zac, mwanaume aliyekusaliti! Ukawa tayari kwenda kuanza upya.
Kujenga ambako uliamini tu, si kwa kuwa ulikuwa na uhakika na Zac ila Imani tu.
Sasa umeshafikiria kujenga nyumba yako? Namaanisha sio jengo, namaanisha nyumba
utakayoijenga wewe, yenye mume na watoto. Utakayoilipia garama kama hiyo
kuhakikisha una nyumba, yaani watu. Kwa kuwa nyumba sio majengo Nanaa. Kama
ingekuwa hivyo mimi nisingehangaika na wewe. Sasa hivi ninayo majengo zaidi ya
matatu, tena majengo mazuri na ya gharama. Lakini yote hayakaliki bila wewe na
Liv. Zaidi wewe Nanaa.” Nanaa akazidi kulia.
“Muda huu, ningekuwa kwenye moja ya jengo langu
linalosifika pale Ubungo. Kila mtu anamtafuta mmiliki wake, amuone. Lakini nipo
hapa na wewe, Nanaa. Na ni juzi tu usiku nimeshindwa kulala kwenye jengo
jingine kule Tabata. Lenye kitanda kizuri na mashuka ya thamani kuliko haya
ninayolalia hapa sasa hivi, ili tu niwe na wewe hapa! Kwa kukubaliana na mimi
katika hilo, kuwa nyumba sio jengo. Ndio nakuuliza Nanaa, ni lini na wewe
utahangaikia kujenga nyumba yako, na kuacha kukimbia hovyo kwa kila sababu?
Yaani ukawa mwanamke wakutegemewa. Mtu anajua hata iweje, ‘Nanaa ni kimbilio langu. Nanaa atakuwepo
kunisitiri. Hata kama nimekosa, nakimbilia nyumbani kwa Nanaa, atakuwepo
kunisitiri, kuniliwaza na kunisaidia.’ Eti Nanaa?” Ulikuwa ni ukweli uliokuwa
ukimuumiza sana Nanaa. Akabaki akilia bila kujibu.
Ukimya wa muda ukapita, Geb akajirudisha kwenye
kochi akajiegemeza vizuri, akabaki akiangalia dari. “Geb!”
Nanaa alihama kochi, akaenda kukaa pembeni ya Geb. “Nitabadilika.”
Geb alibaki akimwangalia. “Kweli
nitabadilika.” Nanaa akarudia huku akifuta machozi. “Nakusikiliza.” “Tokea uliponiambia habari za Zac, nikakusudia kutoka
moyoni kubadilika. Nitaacha kukimbia, na kwa kuwa nimejua naweza kuwepo kwenye
maisha yako, basi nitahakikisha katika
kila mpango ninaouweka na wewe upo.” “Safi sana. Sasa naomba tuanzie
kwenye chumba ulichochukua.” Nanaa akaishiwa nguvu. “Kwa
nini nisikitunze tu? Kitakuwa kama stoo.” “Nilifikiri umesema katika
kila mpango na mimi nitakuwepo!” “Ndiyo, upo.” “Mbona
sasa kauli zako za ‘nita’ haziishi?”
Nanaa akatulia kidogo akajiweka sawa kama anayefikiria chakuzungumza.
Mwishowe akaamua kuzungumza, maana Geb alibaki akimtizama.
“Basi naomba kile chumba nilichokodi, tukitunze kiwe kama stoo.” “HAPANA.” Geb alijibu kwa haraka na
kumfanya Nanaa ashangae. “Huwezi kushika huku na kule Nanaa. Unakuwa ni kama
mtu usiyejua nini unataka! Au huna uhakika na unachokitaka. Kama umeamua kuwa
na mimi, basi ujue kuna garama ya kulipa, ambayo nikuambatana na mimi katika
kila hali. Mvua inyeshe, jua litoke tutakuwa pamoja” Nanaa alitamani
kuchanganyikiwa.
“Geb please! Ni chumba tu!” “Hapana Nanaa. Sio chumba
tu. Kile chumba ndio level ya commitment yako kwangu. Ni kipimo cha
utayari wako kwangu.” Nanaa aliendelea kulia. “Pale tunapoishi tu, kuna vyumba
ambavyo hata havitumiki. Nyuma ya ukuta wa ile nyumba, kuna nyumba nyingine
kubwa zaidi ya ile tunayoishi na unajua kuwa ni yangu. Kama kweli umeamua kuwa
na mimi, na kujenga nyumba yetu, anza kwa kuweka Imani kwangu. Ukishindwa hapo
tu, ujue haupo tayari na sitakulazimisha Nanaa. Amua vile unavyotaka. Ila ujue
nakupenda, na ninakuhitaji wewe kama Nanaa wala si kama mama yake Oliva.” Nanaa
aliinama na kuanza kulia tena.
Kwa mara ya kwanza maishani ndio amefikia ndoto
zake. Kitu alichokuwa akikitamani sana tokea zamani. Awe na kwake kunakojulikana
ni nyumbani kwake. Uchungu ulimuingia kila alipofikiria kupaachia sababu ya Geb
ambaye amemkuta na kila kitu chake! Anaanzia wapi kujiona ni mmiliki mwenzake?
Alitamani awe na kwake. “Geb! Naomba nikibakishe tu
kile chumba. Tafadhali Geb.” Nanaa aliongea kwa uchungu huku akitamani
Geb amuhurumie akubaliane naye katika hilo.
“Inamaana hilo ndilo jibu lako kwangu kuwa
hunitaki tena?” Nanaa akazidi kulia kwa muda, ikasikika sauti yake tu akilia.
“Eti Nanaa? Huu ndio mwisho wetu?” Geb akauliza. “Basi
nitaenda kuvitoa hivyo vitu.” Nanaa akajibu huku akiendelea kulia kama
aliyelazimishwa kujibu. “Unauhakika?” “Lakini ujue
nafanya nikiwa nimejawa hofu, Geb. Naogopa sana.” “Na mimi najua Nanaa.
Na ninakuahidi hutajuta.” “Kweli?” Nanaa
akauliza akionyesha wasiwasi. Geb akamsogelea akumbusu huku akimpapasa.
Hakutaka kwenda mbali sana lakini alihakikisha anaamsha hisia zote kwa Nanaa,
kisha akamuachia akiwa ametulia kabisa.
“Kwa hiyo umeamua kujenga nyumba yetu?” Geb
akauliza huku akimtizama kwa karibu. “Si na wewe utanisaidia?” “Kabisa.” Nanaa
akavuta pumzi kwa nguvu na kutoa tabasamu. “Sitakimbia tena. Nitakung’ang’ania
hata iweje, na mimi nitakulinda.” Geb akacheka. “Hapo umekamilisha furaha
yangu.” “Na mimi nimefurahi kujua unanihitaji, Geb. Nilijua hunitaki tena,
unamtaka mtoto wako tu.” “Liv ndio chambo yangu. Nakupenda Nanaa, na ninajua
wewe ndio utaweza kuishi na mimi, na mimi nikayafurahia maisha. Ila lazima
tujiwekee utaratibu wa kuzungumza. Hata iweje, tafadhali hakikisha
unanisikiliza.” “Nitafanya hivyo Geb. Asante na samahani katika swala la Zac.”
Geb akambusu midomo yake. Aliinyonya kwa taratibu. Kwa kiu aliyokuwa nayo
Nanaa, alitamani amvue nguo, lakini akamuachia.
“Sasa turudi kwenye lile swali lako.” “Lipi!?”
“Uliniuliza biashara inaendeleaje.” Nanaa akacheka. “Kweli una akili ya
kutokusahau!” “Kwa kuwa mwenzio nakuweka kwenye mipango yangu yote, tena tokea
zamani. Na ndio maana nilikuwa nikisafiri na wewe na kukueleza kila kitu. Jinsi
ninavyofanya biashara zangu, hasara ninazoingia na faida ninazoingiza. Nilikuwa
nikikushirikisha kwa wazi nikitaka uelewe. Kwa hiyo kwa kujibu swali lako,
biashara zinaendelea vizuri, ila bado nipo kwenye hatua ambayo ninahitajika
sana. Kuwa karibu ili kuhakikisha baada ya muda mfupi zinakuwa na uwezo
wakujiendesha zenyewe, au hata nikimuachia mtu, najua nini chakutegemea.” Geb
akaendelea.
“Nipo kwenye kuweka mfumo ambao utanisaidia
kuendesha hiyo biashara bila kutumia jasho jingi kama sasa.” “Ungependa
nikusaidie nini?” “Swali zuri sana. Cha kwanza, naomba amani kati yetu. Kukiwa
na utulivu nyumbani, itanisaidia kutulia na akili zangu zitaweza kufanya kazi
vizuri. Najua naweza nikawa na majukumu mengi sana huko kazini, ukajikuta muda
mwingi upo nyumbani peke yako, naomba univumilie. Naamini ni kwa muda mfupi tu.
Nikiweka mambo sawa, hata ulezi wa watoto nitakusaidia.” “Mtoto mwenyewe mmoja
tu, na nipo na mama, sitashindwa.” “Sasa hivi mtoto ni mmoja, watakuja wenzake
karibuni tu, halafu mama anakazi zake. Ni vile anakupenda tu ndio maana ameacha
majukumu yake, na kuamua kuwa na wewe. Lakini mama anabiashara zake kubwa tu,
zinazomtegemea. Najua hivi karibuni ataanza kwenda kazini, utajikuta upo peke
yako na mtoto.” “Usijali Geb. Mimi nitakuwa sawa tu. Labda kama kuna kitu
kingine unachotaka nifanye, ila kama ni hayo tu, nitajitahidi.” Nanaa alijibu
akiwa ameonekana akili yake imerudi likizo. Inafanya kazi kama mama ambaye yupo
tayari kwa majukumu.
“Kingine ambacho kilimshinda Liz, naona labda
nijaribishe na kwako, sijui kama utakubali.” “Nini?” “Swala la mama.” Nanaa
hakuwa ameelewa. “Mama amefanyaje?” Akamuona Geb anasita kidogo. “Ni nini?”
Nanaa akauliza kwa upendo. “Nataka kuishi na mama.” “Unamaanisha huyu mama
yangu mimi, Mama G au mama gani!?” Geb akacheka sana. “Basi Nanaa. Ombi langu
najua limepita.” “Mbona huyo hata akikataa kuishi na sisi tutamfuata huko
anakokwenda! Kimbilio langu yule.” “Asante Nanaa. Unajua aliuza mali zake zote
kwa ajili yangu?” “Uliniambia. Lakini hata kama angekuwa hajauza, mimi mwenyewe
namuhitaji sana Mama G. Ndio mwalimu wangu kwenye kila kitu. Kuanzia mtoto
mpaka kwako. Simuachi popote. Kwa hiyo wewe lete hitaji lako jingine.” Geb
akacheka.
“Ni hilo tu. Na kesho anapokuja kukuletea
chakula, mwambie akusindikize ukachukue mizigo yako kule ulikoiacha, arudi nayo
nyumbani, wewe akuache hapa.” Nanaa akacheka. “Ulivyokazania! Husahau?”
“Nahesabu ni kushindwa kwa hali ya juu. Yaani hangaika yote hii, halafu
nishindwe kukupatia sehemu ya kuishi! Naona nahangaika bure! Hata Grace na mama
wananisema sana. Mama jana amekuacha wewe hapa nyumbani, akanipigia simu na
kuanza kunisema sana. Mama anakupenda Nanaa! Amenigeuka mimi, amekufanya wewe
kama kiziwanda wake! Umechukua nafasi yangu Nanaa.” Nanaa akacheka sana.
“Unaona wivu?” “Sijazoea. Alinizoesha kunisifia
kwa kila jambo. Mimi nilikuwa malaika kwake. Lakini sasa hivi amenibadilikia,
kama hanijui! Mama anakutetea sana. Huna kosa kwake.” “Kweli mimi ni mtu mzuri
sana. Sina hatia.” Geb akacheka. “Sawa Nanaa. Lakini kufunga kile chumba, na
kuonyesha kuwa umerudi nyumbani moja kwa moja, itakuwa nafuu kwangu. Ujue hata
Grace alininunia?” “Grace!?” “Ndiyo Grace, dada yangu.” “Kwa nini tena? Mbona
mimi sijaonana naye karibia mwaka!” “Mama alinisemelea kwake. Sijawahi kumuona
Grace akiwa mkorofi vile. Lakini amechukia sana kitendo nilichokufanyia,
kukufungia nje.” “Jamani mimi napendwa!” Nanaa alimfanya Geb acheke sana.
“Kumbe sina hata haja yakujigombania! Ninao
watetezi wangu tayari.” Nanaa alimfanya Geb azidi kucheka. “Hapa
tunapozungumza, mama yupo anafanya kazi zangu, ofisini kwangu sio kwake, ili
niwe na wewe hapa.” Ilimgusa sana Nanaa. “Ni kweli nimepata familia
inayonipenda, Geb. Nashukuru.” Hapo mikono
ya Geb ilikuwa juu ya mapaja ya Nanaa. “Nakushukuru kuniokoa kwenye mikono ya
Zac. Ningekimbilia kwenye mikono ya hatari ile, nikaacha nyuma upendo mkubwa
hivi! Asante Geb.” “Nisingekubali kushindwa Nanaa. Niliamua kubaki leo ili
tuzungumze mpaka tukubaliane. Najua unanipenda.”
“Kumbe unajua kama nakupenda?” “Nafahamu. Uliniambia
kuwa kwa mara ya kwanza maishani, umejisikia kupenda. Umesahau?” “Nakumbuka Geb, nilijua umesahau!” “Hata kidogo.
Siwezi kusahau kitu kama hicho. Iliniongezea upendo na uhakika wa kutaka uwe
mke wangu. Kumbuka mwenzio nilianza kukupigia mahesabu hata kabla sijakuona. Na
nikaachana na Liz kwa Imani ya wewe kuja kunikubali niwe mpenzi wako.
Ulipomkataa Zinda kwa sababu zinazoeleweka, nikaingiwa hofu kuwa unaweza
usinikubali. Sasa kuja kuona nakubaliwa busu, halafu ukaniambia umeanza
kunipenda, nikaja kukubaliwa sex! Ndio kabisaa.” Nanaa akacheka na kujificha
uso.
“Geb, naomba nikuulize. Lakini naomba usinielewe
vibaya. Nataka kujua tu ukweli.” “Juu ya Zac?” Nanaa akainama. “Hamna shida na
wala sio vibaya. Hata mimi ningetaka kujua ukweli.” Kidogo Nanaa akatulia
akitaka kujua Geb asiyekwenda kumbi za starehe wala asiyeweza kujichanganya,
amemfahamu vipi mtu kama Zac kwa undani hivyo!
Historia
Ya Zac.
“Kipindi
kile nafanya kazi BOT, nilikuwa karibu na kaka yake Ndina. Nilimwajiri. Ni
mfanyakazi wangu mpaka sasa. Anaitwa Jeri. Alinifuata akaniambia anaomba
nimsaidie kutafuta bank statement yenye pesa nyingi ili ampe mdogo wake,
aondoke hapa nchini kwa haraka, yeye na mwanaume wake, kama kuficha aibu. Yaani
hiyo bank statement iwe na uwezo wa kuonyesha inaweza kutunza watu
wawili huko ugenini.” Nanaa akaanza kuumia.
“Ndipo nikamwambia kama anazungumzia bank
statement yangu, nilazima anipe maelezo zaidi, juu ya hao watakao kwenda
kuitumia. Ndipo akanipa kisa cha Ndina na Zac. Kuwa Ndina alikuwa na mahusiano
ya siri na Zac huku akiwa na mchumba wake. Baada yakumaliza chuo pia
waliendelea mpaka mchumba wa Ndina alipogundua. Alipombana Ndina, akakiri na
kusema tayari yupo mjamzito.” “Sasa huyo mchumba au Ndina mwenyewe alijuaje
kama mimba ni ya Zac?” “Swali zuri sana, maana hata mimi niliuliza.” Geb
akajiweka sawa.
Kisha akaendelea kusimulia. “Ndina ametokea
kwenye familia ya wacha Mungu. Nikikwambia wacha Mungu, ni wale watu ambao
ukiwaangalia kwa macho unajua ni watu wanao mpenda Mungu. Ndivyo alivyo huyo
kaka yake, Jeri. Nimfanyakazi wangu wa muda mrefu tu, kwa hiyo namfahamu vizuri
sana. Ni wale watu ambao hata ukimzidishia shilingi moja, akaja kujua akiwa
kwake, atatumia elfu moja, kukupigia simu ili kukujulisha na kesho yake
atairudisha. Kwa hiyo hata huyo mchumba aliyekuwa amemchumbia Ndina, alikuwa
mlokole yule wa kweli na ni rafiki wa Jeri. Kwa kifupi, hakuwahi kumgusa Ndina
kimapenzi.” “Oooh!” Nanaa akacheka na kuinama.
“Sasa baada ya Ndina kuona ameingia aibu, hawezi
kuwaambia wazazi na kanisani kwao atatengwa au atajulikana kama alikuwa
mzinifu, akaamua aondoke nchini na Zac aliyekuwa amepanga kuendelea kusoma. Kwa
kuwa naheshimiana sana na Jeri, na ninamuamini, nikakusudia kumsaidia. Lakini
nilitaka kukutana na hao wapenzi wawili kwanza. Nikamwambia Jeri awalete pale
ofisini kwangu. Kule ulikokuwa na wewe ukifanya kazi.” Nanaa akakumbuka
zilipokuwepo ofisi zake za zamani maeneo ya Fire, na mama G alishamwambia kuwa
walihama pale amenunua jengo maeneo ya Ubungo.
“Hongera Geb. Mama aliniambia umenunua jengo maeneo ya Ubungo.” Geb
akacheka kidogo. “Asante.” Akajibu na kufikiria kidogo kisha akaendelea.
“Basi, wakafika kuniona. Alikuwa Zac, Ndina na
Jeri. Nikazungumza nao, wakaniambia ilibidi kufunga ndoa ya harakaharaka
mahakamani ili kutuliza wazazi baada ya kugundulika hayo mahusiano yao. Na Zac
akasema nilazima waondoke pamoja kwa kuwa Ndina ni mjamzito. Kwa hiyo
wakaniambia nikiwapa hiyo bank statement yenye hicho kiasi cha pesa,
hawawezi kukosa Visa. Basi, kwa kuwa naheshimiana sana na kaka yake Ndina,
nikawapa ile bank statement, wakaondoka, wala sikuwafuatilia tena.”
Nanaa alizidi kuumia. Alimuacha Zac amepiga magoti nje ya daladala akimsihi
arudi wazungumze, lakini kumbe alirudi kuendeleza mahusiano na Ndina! Maigizo gani haya jamani! Hata Nanaa
alijiuliza.
“Sasa miezi mitano iliyopita kaka yake Ndina
akarudi tena kwangu na stori nyingine kuwa anaomba nimpe kazi dada yake, Ndina.
Kwanza nilisita kwa kuwa huwa sipendi kuajiri ndugu wawili, na yeye anajua.
Akanihakikishia hapatatokea tatizo. Nikamuuliza shule iliisha? Akasema hapana.
Akasema walipofika huko, Ndina akazaa mtoto mwenye matatizo, mlemavu. Akawa
anahangaika na mtoto peke yake, Zac anafanya umalaya tu. Mambo yalipomzidia,
ndipo ikabidi amtafute tena kaka yake, kaka yake akamtumia nauli akarudi
nchini. Lakini mtoto akawa anahitajika matibabu na matunzo. Ndina akawa hana
kazi na hana msaada wowote kutoka kwa Zac. Akawa yupo tu nyumbani anategemea
wazazi yeye na mtoto wake.” Nanaa alimsikitikia sana Ndina. Alimfahamu kama
binti mtulivu, kumbe alikuwa na mambo ya chini chini yaliyokuja kumuweka
mwangani!
“Sasa kaka
yake ndio akaniambia wamehangaika sana kutafuta kazi bila mafanikio. Akaniambia
nikimwajiri Ndina ni kama nitakuwa nimemsaidia
huyo mtoto mlemavu pia. Basi, nikamwajiri na Ndina. Akaanza kazi hapo
kwenye kampuni yangu. Tena anajitahidi sana kazini. Lakini Zac alikuja kukata
mawasiliano na Ndina kabisa. Siku tatu zilizopita niliwakuta Ndina na kaka yake
wakizungumza, Ndina alikuwa akilia sana. Sikutaka kuuliza kulikoni kwa kuwa
kwanza ulikuwa muda wa kazi, na wao wapo wanaongea mambo ambayo nilijua ni ya kifamilia,
kitu nilichokuwa nikikikwepa tokea mwanzoni na yeye kaka mtu anajua. Nikaingia
ofisini kwangu na kuendelea na kazi, ndipo kaka yake akanifuata kuniomba
msamaha na kunieleza kuwa anafikiria kumshitaki Zac, kwa kumtelekeza mkewe na
mtoto. Kwani alimaliza shule yake, amerudi nchini na Ndina ameambiwa anaishi na
mwanamke wa kiarabu. Ndina alimfuata na kumwambia hali ya mtoto wao sio nzuri,
lakini Zac akamfukuza kwa ahadi ya kuja kumtafuta baadaye.” Geb aliguna huku
anatingisha kichwa.
“Mama alinipigia simu akiwa amekasirika kweli
kweli. Ananitukana kama hanijui! Huku ananiambia yupo mwanaume anaitwa Zac,
anampenda Nanaa na kumuonyesha mapenzi kuliko mimi! Mama akaniwakia kuwa yupo
tayari kumuoza mwanae Nanaa kwa Zac, kama naendelea kuleta mchezo. Sasa leo
kuja kumuona huyo Zac mwenyewe, ndio nikamkumbuka kabisa. Si unajua mimi
sisahau? Nikakumbuka mpaka alivyokuwa amevaa siku alipoletwa ofisini
kwangu na Jeri, yeye na Ndina.” Nanaa
alishakuwa ameinama.
Akafikiri kwa muda, “Nisamehe Geb. Nilikuwa
kwenye hali ya kutangatanga.” “Lakini sasa hivi si nimebaki mimi peke yangu?”
Nanaa akacheka nakujifunika uso kwa aibu. “Eti Nanaa? Ahadi ya kunipigania si
bado ipo?” “Na kukung’angania pia.” Geb akacheka. “Yameisha bwana.” “Kweli
yameisha au utakuja kunikumbushia tena baadaye? Maana wewe husahau Geb.”
“Nitajitahidi, nisikukumbushie tena kama kukuumiza. Nakuhakikishia yameisha.”
Nanaa akatulia kidogo.
“Najifunza Geb. Naomba nivumilie. Mambo mengine
najifunza ‘in a hard way’. Mengine ndio hivyo.
Sikuwahi kupata mtu wakunikalisha chini na kunifundisha hivi kama mama yako.
Sijapata uongozi mzuri. Nilishazoea kukosolewa katika kila jambo. Hata yale
niliyoyaona ni mazuri, bado nilikosolewa. Nahisi ndipo nilipojenga tabia mbaya ya
kujihami. Najikuta nakimbia kimbia kila wakati. Sijui kujitetea. Hata kama
najua ni haki yangu, nakimbia na kuachia watu wengine wachukue kile ninachojua
nastahili. Nitaanza kujifunza kukusikiliza kama ninavyomsikiliza mama, ili
unisaidie. Usichoke na ninaomba unisaidie kuto kunikumbushia udhaifu wangu mara
kwa mara. Itanisaidia kunijengea roho ya kukuamini kama vile kwa kaka James.
Najua huwa namkosea, sana tu. Lakini nafikiri huwa ananivumilia na kunipa
nafasi tena na tena. Ndio maana amebakia yeye kuwa kimbilio langu wakati wote.
Naamini nitabadilika Geb.” “Nitakuwa na wewe Nanaa. Usiogope.” Nanaa akaridhika
na kutulia kidogo. Geb akabaki akimtizama kwa uchu. Ule mkono pale juu ya yale
mapaja akaanza kutembea taratibu.
Kabla hajaharibu mazungumzo, Nanaa akamuwahi.
“Nina wazo Geb. Sijui kama utakubali?” “Wazo gani?” “Ili kuleta amani tufanye
hivi. Nirudishe ile mizigo nyumbani, halafu nimpikie chakula kizuri Grace na
familia yake, tuwakaribishe nyumbani.” “Hapo utakuwa umeniokoa.” “Lini sasa
tunarudi nyumbani kwetu?” Nanaa akauliza akijijumuisha na yeye. Geb alifurahi
sana. “Kweli umeamua.” “Sitaki mchezo. Nipo kwenye ujenzi mwenzio!” Geb
akacheka kwa sauti. “Nakuona Nanaa.” “Kwa hiyo usinicheleweshe.” Geb akazidi
kucheka huku akimtizama Nanaa aliyevaa sura ya kazi. “Sitakuchelewesha. Ila
naomba unipe siku kama mbili au tatu
nyingine mbele.” “Kwani kuna nini huko nyumbani, mbona hutaki hata
nirudi kuchukua vitu?” “Kuna kitu kizuri nakutengenezea. Kikikamilika hicho ndio
nitakurudisha.” “Unanitengenezea mimi!?” Nanaa aliuliza na tabasamu usoni.
“Sina mwingine Nanaa, ni wewe.” Nanaa alifurahi sana, akaanza kumbusu na yeye
Geb.
Alifanya kama vile Geb anavyomfanyia kumnyonya
midomo yake, lakini yeye alivuka mipaka. “Tokea jana sijala zaidi ya kile
kikombe cha uji nilichokunywa pale mgahawani. Chakula kilikuwa hakipiti kwa
hofu.” “Pole mpenzi wangu. Basi wewe tulia nikushukuru. Kazi yote nitafanya
mimi mwenyewe, wewe furahia tu.” Geb akacheka. Nanaa alikuwa mtundu kuliko
alivyodhani Geb. Na kweli, alicheza na mwili wa Geb akiwa amemvua nguo zake
zote palepale kwenye kochi. Alimchezea mpaka Geb alipofanikiwa kupata goli la
shukurani.
“Daah! Hii ya aina yake.” Geb akasifia.
“Umefurahia?” “Sana.” “Basi tukae, tule, ukishiba, unilipe.” Geb akacheka.
“Mimi nilifikiri unanishukuru, kumbe utakuja kunidai?” “Si ndio na wewe
unatakiwa kunishukuru, kwa kukushukuru!” Geb akacheka sana. “Sawa mama.
Nitakushukuru, kwa kunishukuru. Nilikuwa na hamu na wewe Nanaa! Acha nile
haraka nishibe, halafu nifanye mapenzi na wewe. Tangia siku ya kwanza unaondoka
nyumbani nilikuwa nikikuwaza, huku nikihofia unaweza kutimiza yale maneno yako
ya kutafuta mwanaume mwingine. Halafu nikawa sina uhakika kama ulishika mimba
au la. Nikajiambia hata kama ilishika, itakuwa ilitoka. Nilijikatisha tamaa.
Nikajiambia kwa upasuliwaji ule, na madawa uliyokuwa ukitumia, Liv asingeweza
kuishi.” “King’ang’anizi huyo! Ndio maana niliamua kumkatisha jina nimwite tu
Liv. Amestahimili mengi kweli.” Nanaa
aliongeza.
“Ndio maana nitamuenzi sana huyu mtoto. Amenisaidia
kujipatia mke.” Nanaa akacheka sana. “Ujue Geb unatakiwa uniombe radhi wewe?”
Geb akacheka. “Kweli tena. Yaani unapanga mipango yote hiyo halafu mwenzio
hunishirikishi!” “Nilijua nikikwambia swala la mtoto, wakati ule ungekataa.
Maana uliniambia hutaki kitu chochote kiingilie shule yako.” “Wala hujakosea.
Nisingekubali. Tena ningeanza kukukwepa.” “Usingeweza Nanaa.” Nanaa akacheka
kwa aibu. “Unatabia mbaya Geb wewe! Ulikuwa unanichanganya kwenye mapenzi
makusudi ili niwe nakufuata nyuma kama mjinga!” “Lakini si umeona nilivyokuwa
nafanikiwa? Ulikuwa unaning’angania kweli kitandani.” Nanaa akacheka akajificha
uso na mto wa makochi.
“Hata mimi
naridhika sana kufanya mapenzi na wewe, Nanaa. Nakufurahia kwa kila namna.
Zaidi mwangani nikiwa nakuona mwili wako.” Geb alishaanza kumvua nguo Nanaa.
“Napenda kubusu midomo yako. Napenda kufanya mapenzi na wewe huku nikikutazama
sura yako. Napenda mlio unaotoa kila unapokuwa mikononi mwangu nikifanya
mapenzi na wewe. Nakupenda Nanaa.” Geb alimuweka Nanaa kwenye kochi na kusahau
swala la chakula.
“Ule kwanza Geb.” Nanaa aliongea taratibu akiwa
uchi kabisa pale kwenye kochi huku Geb akimbusu mwili wake. “Siwezi kusubiri
tena.” Nana akatabasamu akiashiria kumruhusu kufanya anachokitaka mwilini
mwake. Hata yeye alikuwa na kiu kali ambayo ni Geb pekee alijua ndiye mwanaume
anayeweza kukata kiu ile vizuri. Yalikuwa mapenzi mazuri, yaliyojaa uchu,
msamaha na furaha. Nanaa alimng’ang’ania Geb pale kwenye kochi, wakajikuta
wamehamia chini kwenye kapeti, nakujisahau kabisa. Waligeuzana huku midomo yao
ikigoma kuachiana. Yalikuwa mabusu ya kung’ang’aniana. Ilishapita miezi 8 bila
wawili hao hata kugusana kitu ambacho wote kilikuwa kikiwatesa sana.
“Liv amenikatili bwana!” Geb akalalamika. “Kwa
nini tena?” “Anamiliki starehe yangu ya kufungia magoli. Ona! Nashindwa
kunyonya.” Nanaa akacheka sana huku akijiziba matiti yake. “Geb wewe! Chakula
cha mtoto hiki!” “Namsamehe tu kwa kuwa amekuwa mvumilivu. Hata sasa hivi
ametulia kimya, baba yake nakula raha. Watoto wengine sasa hivi wangeshaharibu
kwa kujiliza!” Nanaa akazidi kucheka.
~~~~~~~~~~~~~~~
Mabusu mengine ya haja yakaanza. Nanaa hakupoteza
muda, akachangamkia penzi, akafikishwa alikotaka, na Geb naye akafanikiwa.
“Daah! Nahisi ndio maana nilikuwa kama mwehu! Ulishanizoesha vibaya Nanaa.” Geb
alishamaliza raundi kama mbili za harakaharaka, na yeye akajilaza pembeni ya
Nanaa, alimvuta mpaka kifuani kwake, akabaki akimwangalia. “Umeniumiza sana Geb!” Nanaa akaanza kulia.
“Najua, Nanaa. Najua sasa hivi itakuwa ngumu kuja kuniamini tena. Eti Nanaa?”
Nanaa akanyamaza, akageukia pembeni na kuendelea kulia.
“Ulinisukuma kikatili sana, na
kunifungia nje.” Geb
aliumia na kujutia sana. “Naona hata
shida kusema samahani Nanaa. Naona haitasaidia. Ndio maana umenirudishia na
pesa zote.” “Sijawahi kutamani mali maishani Geb.
Najua hata mimi nikihangaika naweza kuwa nazo. Unakumbuka nilikwambia shauku na
kiu yangu, iliyokuwa ikinipelekea kutafuta wanaume?” “Nakumbuka Nanaa. ‘Sense of belonging and Security’.” “Ambavyo umenihakikishia huwezi kunipa Geb. Unanipa kitu
kirahisi sana, ambacho hata mama yako anaweza kunipa, pesa. Lakini
umenipokonya tumaini kubwa sana ambalo ni wewe peke yako ulifanikiwa kunipa.”
“Umenirudisha kwenye hofu kitu
ambacho ulishakitoa zamani! Najiuliza hivi kweli nikikukosea tena, utakuja
kunisamehe kweli? Mapenzi haya yatadumu kwa muda gani? Nakuwa naogopa!” “Nisamehe Nanaa. Nakiri
nilikosea sana. Naomba nisamehe. Kwanza mimi mwenyewe niliteseka. Wala
usifikiri ilinipa furaha. Na bado inanitesa mpaka leo.” Nanaa akanyamaza.
“Naomba safari hii nisitoe tena ahadi, ila niombe
kitu.” “Nini?” Nanaa akamgeukia. “Tujenge kisiwa chetu pamoja ambacho hakuna
mmoja wetu ataweza kumfukuza mwenzake. Kisiwa hicho itakuwa ni mimi na wewe tu,
wengine wataongezeka. Kiwe ni kisiwa ambacho hakitawahi kuvunjika kwa namna
yeyote ile, ila kifo. Isiwe ni kazi ya mikono ya mwanadamu, ili isiharibike kwa
rahisi. Tafadhali Nanaa.” Nanaa alianza kumbusu tena. Kisha akamwangalia
vizuri.
“Kwa hiyo niwe na uhakika kuwa haitakaa ikatokea
tena maishani unanifukuza?” “Hata iweje, sitathubutu kukufukuza popote.” “Kwa
hiyo niwe na uhakika nimepata mtu wangu wa kudumu?” “Mpaka kifo, ni mimi na
wewe tu.” Walirudi kitandani baada ya kuoga, na kutumia muda mrefu huko bafuni,
wakishikana na kufanya mapenzi. Ni kama Mungu alituma malaika wa kumlea Oliva
siku hiyo. Walijisahau hata kama wanamtoto! Nanaa hakumuamsha ili anyonye,
akaachwa alale na njaa yake mpaka usiku.
“Narudi chumbani kwetu na Liv.” “Haitakaa
nikalala mbali na wewe tena Nanaa. Nikisafiri tunasafiri wote na mtoto.
Usinipokonye tonge mdomoni bwana! Acha nikufurahie.” Nanaa alifurahia, akarudia
kumbusu. “Itakuaje sasa?” “Twende tumuamshe mtoto, anyonye, akilala tunamuweka
kitandani kwake, sisi tunaendelea.” “Sijamuogesha leo.” “Muachie hiyo kazi bibi
yake, atakuja kesho.” “Nashukuru kwa kubaki na sisi leo. Nilikuwa na hamu na
wewe Geb!” “Hata mimi Nanaa. Nimefurahia
wazo lakubaki.” Nanaa alikuwa ameshatoka ndani ya shuka, akijitayarisha kutoka
hapo chumbani, akajikuta anarudi mwilini mwa Geb, alimpokea wakaanza tena.
Milio ya huba ndio aliyokuwa akitoa Nanaa na
kuamsha hisia za Geb zaidi. Kwa kuwa alishindwa kunyonya matiti yake. Ile style
ya kumpakata akifanya naye mapenzi, akaibadilisha. Badala ya kunyonya matiti,
chakula cha Liv, akabaki amemkumbatia Nanaa, aliyekuwa akitoa sauti tamu
nakumfanya Geb azidi kupagawa, mpaka alipofanikiwa tena. “Daah! Utaniua Nanaa.
Mwenzio sitosheki!” Nanaa akacheka. “Hata mimi nafurahia sana. Unanifanya
siumii. Japokuwa tunafanya kwa muda mrefu, lakini sichubuki! Napenda jinsi
unavyonilainisha ukinihisi nipo mkavu.” “Vipi?” Nanaa akaruka pale kitandani.
“Hamna tena Geb. Twende tukamlishe kwanza mtoto.” Geb akacheka akanyanyuka.
Walitoka hapo kwa pamoja, wakarudi bafuni. Safari
hii walioga kweli na kutoka. Geb alikwenda kutafuta chakula alichokileta mama
yake tokea asubuhi. Nanaa akaingia kunyonyesha. Wakati ananyonyesha, Geb
akaingia na chakula alichokuwa amepasha moto. Akawa anakula, huku anamlisha
Nanaa aliyekuwa ananyonyesha. “Mimi sijashiba Geb.” Geb akacheka. “Hivi unajua
asilimia kubwa ya hiki chakula umemaliza wewe Nanaa!?” “Basi ulipakua kidogo.
Safari hii nenda kaweke kingi.” Geb alinyanyuka huku akitingisha kichwa.
“Nanyonyesha bwana.” “Mmmh! Acha kumsingizia mwanangu. Tokea nakufahamu, ulaji
wako ni huo huo.” Nanaa akacheka.
Geb akarudi na chakula kingine akamlisha Nanaa
mpaka akamaliza. “Angalau sasa hivi.” “Nanaa wewe! Angalau au umeshiba?”
“Angalau.” “Basi naenda kukuletea kingine.” “Hapana bwana. Nitaamka usiku nile
tena.” “Na wewe hushindwi!” Nanaa akacheka. Kwa uchovu wa mapenzi ya siku nzima
na vilio vya hapa na pale, walijikuta wanalala kwenye chumba hicho chenye
kitanda kidogo. Oliva alilala ukutani, Nanaa katikati, Geb mgongoni kwa Nanaa
kama kawaida yake.
~~~~~~~~~~~~~~~
Waliamka asubuhi wote wakabaki wanacheza na mtoto
kitandani. “Huendi kazini?” Nanaa akauliza. Maana Geb alionekana hana haraka.
“Baadaye nitatoka kidogo, kisha nitarudi. Bado najiona kama nakuhitaji!” Nanaa
akacheka. “Ila nimemwambia mama alete chakula nakuendelea na shuguli zake.
Baadaye nitakwenda mwenyewe ofisini kwangu.” “Mtoto hajaoga Geb! Ungemuacha
mama aje amuogeshe.” Geb akamnyanyua Liv. “Eti Liv? Unataka kuoga? Kwanza mtoto
mwenyewe bado ananukia kabisa huyu. Kesho bibi yake anakuja.” “Jana ulisema
hivyo hivyo!” “Acha bwana nipumzike Nanaa. Nahangaika sana mwenzio. Acha na leo
nijipe likizo tulivu bila kuingiliwa. Najua mama akija hapa utakuwa busy na
mama, mimi nitaachwa. Nataka muda na wewe. Au umeshanichoka?” “Hapana Geb
mpenzi wangu. Nakuhitaji mnoo. Nitamfuta tu Liv, atakuwa sawa.” Geb akambusu na
yeye Nanaa, kisha akaendelea kucheza na mtoto wake.
Ilipofika mchana wakati Nanaa amepitiwa na
usingizi kitandani kwa Geb, Geb aliamka baada ya usingizi mfupi walioamua
kulala baada ya kupata kifungua kinywa na penzi la haja. Akatoka. Nanaa alilala
karibia siku nzima. Alikuja kuamshwa na Geb mida ya saa 12 jioni akiwa amembeba
Liv. “Mungu wangu Geb! Amelia sana?” Nanaa akashituka na kukaa. “Nilipitiwa na
usingizi.” Akajaribu kujitetea. “Acha
kupaniki! Nahisi mimi ndio nimemuamsha wakati namuwekea zawadi zake kitandani.”
Nanaa akatulia. Kisha akagutuka kama aliyekumbuka kitu.
“Sasa mbona mimi sina zawadi!?” Geb akacheka tu.
“Acha upendeleo Geb! Na mimi nataka zawadi.” “Mimi ndio zawadi yako!” “Mmmh!
Zawadi hiyo ukiwa umesimama na nguo zako hivyo, mimi wala sitaki.” Geb alicheka
mpaka akakaa. “Nanaa wewe ni mtundu wakupitiliza.” “Njoo mwaya Liv. Pole mama.
Nilipitiwa usingizi.” Nanaa akampokea mtoto wake na kuanza kumbusu huku
akimuongelesha. “Nyonya kwanza halafu ukanionyeshe zawadi alizokuletea dad.”
Nanaa akaanza kunyonyesha huku wakizungumza na Geb na kucheka.
Liv alipolala, wakabaki
wao wawili hapo kitandani wakizungumza na kufanya mapenzi. Geb alikuwa
amemletea Ice cream. Wakawa wakila hapo kitandani. Mara ampake Geb kifuani
nakuila kwa kulamba kifua cha Geb. Kule kupiga kelele kwa baridi ya ile ice
cream aliyoimwaga Nanaa, ilifuata na kukumbatiwa na kupewa joto na Nanaa. Na
hivi walilala mchana, ikawa fujo tupu hapo kitandani. Huyu anyonye hiki ashike
hapa, afanye vile, ilimradi kusherehekea kupatana. Wakalala hoi. Kwa mapenzi ya
siku mbili mfululizo.
Chanda Chema,…!
S |
iku
ya tatu Geb alimka na nguvu mpya. Akili iliyotulia hata usoni alionyesha yake
yanamuendea sawa. Alitoka kitandani akamuacha Nanaa bado amelala. Alimbusu mara
kadhaa, akamfunika vizuri, akaondoka. Hodi ya Mama G ndio iliyomtoa kitandani.
Nanaa alikurupuka na kwenda kufungua mlango. Akampokea Mama G vyakula, ndipo
wote wakagundua kidoleni kwa Nanaa kuna pete nzuri sana ya uchumba. Nanaa akabaki
ametoa macho. “Wala sikujua kama amenivalisha hii pete! Itakuwa amenivalisha
usiku tulipokuwa tumelala!” Bado Nanaa alikuwa kwenye mshangao. “Nzuri kweli
kweli! Ndio anakuoa?” Mama G akauliza huku akicheka. “Sijui mama!” “Kwani
hajakwambia?” “Kanivalisha nikiwa nimelala! Yaani sasa hivi na mimi ndio
naiona. Ila nimejawa furaha ya ajabu mama yangu.” “Nakuona, hata usoni
umebadilika!” Acha Nanaa aanze kuruka ruka. Alicheza kama mwehu huku Mama G
anacheka.
Kidogo kama akakumbuka kitu, akatulia. “Sijui
ndio atanioa!?” Nanaa akauliza huku akitaka kujua kama na Mama G atampokea.
“Hana mwingine atakayeweza kuishi naye yule. Namjua Geb. Wewe ndio mwanamke
utakayemfaa.” “Yeeeeyyyy! Mke wa Geb mieee!” Nanaa aliendelea kuruka ruka. Mama
G alikuwa akimtizama huku anacheka. “Hongera mwanangu Nanaa. Naona umepata
mume.” “Mume haswaa. Si mchezo! Kama karata, nimelamba DUME.” Mama G akaanguka
kicheko.
“Chizi wewe!” “Acha mchezo mama. Na mimi nitaitwa
Magesa! Siamini mama yangu.” “Nakuona mama Magesa. Hongera.” “Asante mama
yangu. Nimefurahi sana umenipokea mimi kama mke wa Geb. Nimefurahi mnoo.” Nanaa
alikuwa akihema kwa kucheza.
“Sasa
sijui nimuulize kama atanioa au nisubiri tu nimuone?” Nanaa aliuliza huku
akiangalia kidole chake. Mama G alikuwa akimwangalia huku anacheka. “Eti mama?”
“Wewe akipiga simu, mshukuru kwanza kwa hiyo pete. Halafu muache.” “Basi
nampigia.” “Huwezi kusubiri!?” “Siwezi mama. Acha tu nimpigie. Nilivyokuwa
ninahamu ya kuwa na mtu wangu hapa duniani! Mwanaume anayenipenda na
kunithamini kama Geb!” “Mmmh! Naona umemsamehe kabisaa.” “Mama naye kwa kuweka
visasi! Mambo gani hayaishi!?” Mama G alicheka sana.
“Gafla mimi ndio wakuweka visasi, Nanaa mwanangu?
Sio wewe uliyejidai unataka uanze maisha yako!” “Mama na wewe! Mambo ya zamani
hivyo!” “Si ni juzi tu!?” “Bwana mimi sikumbuki! Kwanza twende tukachukue
mizigo yangu, urudi nayo nyumbani.” “Pale kwenye ile nyumba yakupanga, wote
tutaonekana machizi. Si uviache hata mwezi uishe?” “Wee! Unataka
kunicheleweshea ndoa! Acha tu huyo Geb anione nimekusudia kutulia hapo kwake,
anitangazie ndoa.” Mama G alicheka sana.
“Naona umepania?” “Sio kidogo.” Nanaa alijibu kwa
kujiamini. “Ujue nakushukuru sana mama yangu! Asante sana kwa kunifundisha
kutulia na kuwa mvumilivu. Naanza kuona matunda yake.” “Karibu mwanangu. Mungu
awasaidieni nyumba yenye amani na utulivu. Mpate watoto kadiri mtakavyo.” “Si
na wewe utakuwepo?” “Ukinihitaji nitakuwepo.” “Nakuhitaji sana mama yangu. Tena
sana. Ujue najifunza sana kutoka kwako? Wewe ni mfano wa malezi ambayo sikuwahi
kuwa nayo kabla. Najifunza kweli. Nataka tuishi wote ili niendelee kujifunza.”
Mama G alifurahia sana kusikia hata Nanaa anamuhitaji.
Japokuwa alikuwa na uwezo
wa kuwa na nyumbani kwake, lakini ameishi na Geb maisha yao yote. Ni mtoto
ambaye hakuwa tayari kumuachia kirahisi. Sasa kuona Nanaa amemkubalia kuendelea
kuwepo kwenye maisha ya mwanae, ilimgusa zaidi na kuongeza upendo kwa Nanaa.
~~~~~~~~~~~~~~~
Nanaa Amechumbiwa Na Geb. Je Ndio
Ndoa? Usikose Kujua Yatakayojiri Huku Wamekusudia Kuzika Ya Zamani. Yapi Yanazikika,
Yepi Yatawafuata?
Usikose Kuwa Nao Kwenye Penzi Zito La Geb & Nanaa.
0 Comments:
Post a Comment