Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com MAKOSA! – SEHEMU YA 70. - Naomi Simulizi

MAKOSA! – SEHEMU YA 70.

Sabrina akaanza kumsihi Mungu aingilie kati ile hali nzima. Wasirudi kwenye mafarakano na hata hilo likiisha, basi ndoa yake ibaki imesimama. Akabaki ameinama akimsihi Mungu huku akimsikiliza mzee Msindai. “Sasa ninawaonya.” Akanyanyua uso kumuangalia mzee Msindai anavyotoa onyo. Mwenyewe alijawa aibu yakupitiliza. Huyo mzee aliwabana wote, yeye na wazazi wake wakaishiwa nguvu, wakabaki wamenywea.  “Na zaidi mama Sabina. Nakuonya, acha ndoa ya Jackson na Sabrina. Kwa sababu wakati nyinyi na Tino mmemtelekeza Sabrina, hamuoni uthamani wake, sisi kina Msindai, tuliitambua dhahabu udongoni, tukaienzi. Tangia anaingia kwenye familia yetu, hajawahi kutelekezwa hata mara moja.” Mzee akaendelea.

“Iwe mwisho kurudi kwa huyu mganga, na mganga mwingine yeyote yule kwa ajili ya Jackson Msindai. Chochote kitakachompata Jackson, sitakusamehe. Unanitangazia vita kwa muda mrefu sana, lakini nilinyamaza kwa heshima ya binti yenu. Lakini unavuka mipaka. Nahofia dawa unazomfanyia Jackson, siku moja zinaweza kumpata.” “Wala hazitampata baba. Hata ahangaike mpaka achoke, hakuna silaha itakayonyanyuka kinyume yangu, mume wangu na watoto wangu, itafanikiwa mama. Nilimtuma baba kwako, kuwa, unapigana vita mbaya sana, na wala hushindani na mimi ila Mungu aliye hai.” Jackson akawa haelewi mkewe ameyajuaje hayo.

“Uhai wangu, watoto wangu na mume wangu umefichwa ndani ya Kristo Yesu. Si mimi ninayeishi, bali Kristo ndani yangu. Ndio maana muda wote unahangaika kutuloga mimi na Jack, hufanikiwi mama. Acha, kwakuwa yupo Simba wa kabila la Yuda, ambaye halali akihakisha ananiombea kwa Mungu bila kuchoka. Lipo jeshi la malaika hapa kwangu, wanazunguka mchana na usiku wakifanya makao. Hakuna uchawi utafanikiwa hapa kwetu. Nakuhakikishia mama, hutakaa ukafanikiwa. Wewe endelea kuhangaika tu, ila ujue unamaliziwa pesa yako.” “Hana nafasi nyingine ya kujaribu. Huko alipotolewa jioni hii kwa huyu mganga akiloga, namuonya hapa mbele yako Sabrina, ili usije kunichukia baadaye binti yangu, isiwahi kurudiwa tena.” Hapo Mzee Msindai akaweka msisitizo.

“Linapofika swala la kulinda kina Msindai, huwa sizembei na Tino nimemwambia. Asichanganywe na rangi ya hawa watoto wawili. Hawa ni wakina Msindai. Hakuna, narudia tena, HAKUNA, atakayenipokonya. Mlijaribu kwa uchochezi, mlishindwa. Mkaja kisheria, pia mmeshindwa. Mmehamia kwenye uchawi ndio leo naweka kikomo. Huna nafasi ingine ya kukosea kwa kina Msindai, mama Sabina. Umezimaliza zote. Kama umeshindwa kuona hii ndoa ikiendelea, kaa mbali mama. Hii ndoa imeunganishwa na Mungu, kwa nini mnacheza na mipango ya Mungu!?” Kimya.

“Baba Sabina, kwa muda wako, mkumbushe mkeo, nimeshaandikisha shitaka kituo cha polisi. Ninao ukiri wa huyu jamaa. Kupokea pesa kutoka kwa mama Sabina, akitaka kumuangamiza Jackson. Mengine sitasema. Lakini nataka ujue huku kurudi kwake mkeo hii leo kwa huyu mganga, ni mtego nilimuwekea ili niweze kumpa nafasi ya mwisho ya kujitoa mwenyewe. Niliwaambia wamuache, akishindwa kujitoa yeye mwenyewe ndipo nimkamate kama hivi. Nikawaambia wamwambie huyu jamaa, amtajie mahitaji magumu, na pesa nyingi akimtaka ayalete ndipo amfanyie uchawi wake. Kwa asilimia nyingi sana, nilijifariji pengine ataamua kuachana na ubaya wake, atahesabu garama ya kuangamiza ni kubwa kuliko kuacha mtoto wangu, lakini bado mama Sabina umeng’ang’ania tu! Umesaka kila kitu kwa garama kubwa sana ili kumpatia mganga amuangamize kijana wangu! Hiyo ni dhuluma ambayo SIKUBALI.” Sabrina akaumia sana.

“Kuna swali lolote kabla sijaondoka, ili baadaye kusijekuwa na kutoelewana zadi?” “Mimi nimeelewa mzee Msindai, na naomba nikuombe radhi kwa yote. Kuanzia kwa Sabina mpaka mama yake. Kuna ambayo yalikuwa yakiendelea, hata mimi sikuwa nikiyajua, nimekuja kuyasikia kutoka kwa Tino alipokuwa akizungumza na mimi pamoja na mama Sabina hapa.” “Hata hayo mazungumzo yenu ninayo.” Baba Sabina akashituka sana kama wengine wote pale ndani. Sabrina ndio alitamani aridhi ifunguke hapohapo mbele ya huyo mzee, apotee na hao wazazi wake.

“Kwamba huamini?” Mzee Msindai akauliza, wakabaki kama mabubu. “Si Tino amewakataa nyinyi na kusema hataki hawa wajukuu zangu waje kwenu ni bora wakabi kwangu mimi ninayewapigania kwa upendo lakini si kutaka kujinufaisha nao?” Wakazidi kuogopa. “Hakuna sehemu ndani ya hii nchi jina la Msindai likatajwa kwa hila, nisisikie. Nina masikio kila mahali. Kwa hiyo nakuonya mama Sabina. TULIA. Turudishe mahusiano yale ya kwanza kabisa. Ila hiki unachofanya, ni hatari mno, kwa kuwa hutataka kuwa vitani na mimi. Ni mbaya mno, kwa kuwa huwa mimi sijui kushindwa.” Kimya.

“Nimemaliza. Sasa usafiri wa kuwarudisha Chalinze na Bagamoyo kwa huyu mganga upo. Kwa kuwa mimi ndio nimewaleta hapa, nyinyi wawili lazima tuondoke wote kasoro baba Sabina niliyemkuta hapa. Mtakuja kupanga safari ya kurudi hapa kwa wakati wenu, vinginevyo Sabrina aseme tofauti.” “Mimi nataka kurudishwa kwangu.” Akajibu mama Sabrina na kumuumiza sana Sabrina. “Basi, maadamu kuna usafiri wa bure, acha na mimi niende mama. Nyinyi mpumzike.” Akaaga baba Sabina. Sabrina akabaki ameinama. Baba yake akarudi chumbani, akachukua vitu vyake na kutoka. Mzee Msindai akabaki wa mwisho kuhakikisha wote wametoka hapo ndani, ndipo na yeye akaaga na kutoka. Wakabaki Sabrina na mumewe, kimya wote wamepigwa na butwaa.

~~~~~~~~~~~~~~

“Aibu gani hii jamani! Kushikwa uchawi na baba mkwe!” Mwishoe Sabrina akajikuta akiongea mawazo yake kwa sauti huku akisimama. Jack naye akasimama kama mshale. “Wewe Sabrina vipi bwana! Mbona hupati picha kubwa!? Mama yako anataka kuniua!” Sabrina akamwangalia na kuondoka, akamfuata nyuma. “Sabrina, au wewe hujaelewa vizuri?” “Acha woga bwana!” “Naachaje kuogopa? Au anataka nife urudi kwa Tino?” “Labda.” Sabrina akajibu akiendelea kutembea, Jack akamvuta kwa nguvu. Akageuka. “Utaniangusha bwana Jack!” “Mbona huna wasiwasi na kufa kwangu au unaona bora nife tu!?” “Hufi bwana Jack acha kupaniki.”

“Kweli Sabrina wewe hunipendi! Umesikia natafutwa kuuwawa halafu wewe...” “Tulia kwanza bwana Jack, halafu nifikirie mimi na aibu niliyoingia.” “Sabrina! Kweli unazungumzia aibu na sio kifo changu!” “Sasa wewe umekufa hapo ulipo?” “Nitakufa.” “Hufi bwana acha kupaniki. Hakuna uchawi utakuuwa wewe Jack. Tulia.” Sabrina akaingia chumbani, Jack akamkimbilia.

“Sabrina!” “Jackson Msindai, nakuhakikishia hakuna uchawi utakuua, tulia bwana. Mbona imani yako ipo hivyo? Fikiria langu. Baba mkwe amethibitisha aliyokuwa akiyasema mama Msindai wakati wote.” Jack akafikiria kidogo, akasimama. “Kaa bwana.” “Tuanze kwanza langu Sabrina, ndio tuje matatizo yako. Wewe ulijua kama mama yako ananiloga?” “Nimejua jioni hii. Ndicho baba alichokuja kuniambia.” Jack akashituka sana.

“Sasa mbona wewe huna wasiwasi!?” “Kwa sababu najua kwa hakika kama lilivyo jina langu kuwa hakuna silaha itakayoinuka juu yangu mimi, wewe na watoto wetu, ikafanikiwa Jack. Nina uhakika kwa asilimia zote wala si 100. Tunalindwa sisi kuliko ulinzi wowote ule unaoujua hapa duniani. Na hata baba nimemwambia asiogope.” “Unauhakika gani?” “Kwa kuwa kama ulimsikiliza baba kwa kutulia, mama hajaanza kukuloga leo alipotolewa kwa huyo mganga wake. Na baba amesema ameanza muda tu tokea Sabina akamatwe. Baba amesema ameuza mali zao nyingi tu akitaka afanikishe uchawi wake bila mafanikio. Sasa unafikiri ni nani ametulinda mpaka sasa kama sio ulinzi wa ki Mungu juu yetu?” Jack akatulia.

“Na ndio maana wewe ulipotoka tu na kuhamia huko kwenye kambi ya shetani, amekuadhibu vibaya sana.” Jack akamwangalia mkewe. “Kwani wanaume wangapi wanafanya kama wewe na hawayapati kama yako? Ona ulivyozua balaa kwa ndugu zako na familia nzima? Upo mtandaoni mpaka leo kwa starehe uliyokubali kupokea kutoka kwa shetani. Alikuwa akikutafuta bila mafanikio, kwa kuwa ulikuwa ndani ya ulinzi wa ki Mungu. Ulipotoka tu, akakuonyesha zawadi, na wewe ukapokea kwa haraka sana. Ona anavyokuadhibu wewe na familia nzima ya Msindai! Phina mwenyewe yupo matatizoni sababu yako. Shetani hana zawadi ya bure, Jackson. Na alikuwa akikusaka, mpaka wewe mwenyewe ulipoenda kujisalimisha kwake, akakupokea kwa mikono yote miwili. Ndio maafa hayo.” Jack akapoa kabisa.

“Turudi kwangu.” “Sasa wewe unashida gani, kwani wewe ndio umeshikwa na uchawi bwana!? Baba sio mkurupukaji. Anafanya mambo yake kwa uchunguzi. Anakujua wewe ni nani. Na kwa taarifa yako tu, kama hujajua, mzee Msindai anakupenda na kukuheshimu sana Sabrina. Amekubali kunipa nafasi nyingine ya kunitafutia video ya Uswiz, kwa ajili yako. Kwa hiyo usiwe na wasiwasi. Baba anakujua. Ila ongeza umakini kwenye maamuzi yako. Kama hujaelewa, umeshakosa mara mbili na amekwambia kupitia mazungumzo yake na mama yako. Ulipojifungua Brayan uliondoka na watoto bila kuaga wakati yeye alikuwa akija kukuona  kila siku pale kwa Pendo.” “Na mimi nilielewa pale. Nitakuja kumuomba msamaha.”

“Hilo ni moja na kubadilisha wajukuu zake majina bila idhini hata yangu!” “Nilishamuomba msamaha na wewe Jack, mbona kama unataka kuanzisha jambo jingine?” “Ni hilohilo tu. Ulifanya maamuzi yako bila hata kumshirikisha hata yeye ambaye alionekana yupo upande wako tokea mwanzo!” “Nilishakupa sababu.” “Ya kuwasogeza watoto kwa Tino, sawa. Ila mpaka kubadili majina, Brina!” “Sasa wangesafiri vipi au wangetengenezewa vipi hat…” Akasita. Akafikiria na kuona anyamaze tu ni kama anaharibu zaidi. Akabadilisha alichotaka kusema.

“Kwako nilishakwambia sababu Jack. Ulizini, ukaficha mpaka siri yako ilivyojulikana. Ukapotea, nakuja kukutana na wewe siku mama yako anatangaza kupokea mtoto wa Phina na si wangu ambao…” “Mimi najua unajua kama ulikosa Sabrina. Hata ukijitetea, unajua ukweli kutoka ndani ya moyo wako, unaujua ukweli wa mambo ila ukatenda ulichokitenda. Basi.” Jack akasimama nakutoka.

Sabrina akakaa hapo akifikiria akajitetea kwa hili na lile mwishoe akaona amfuate tu. Akamkuta amekaa sebuleni, amejiinamia kama kawaida yake akikasirika au jambo likiwa halijamuendea sawa huko kichwani mwake. “Sasa umekasirika nini Jack?” “Wewe hunipendi kama ninavyokupenda mimi Sabrina. Kuna mambo unanifanyia, mimi siwezi kukufanyia.” “Jackson Msinda! Kweli wewe unaongea hivyo au ni kwa kuwa sasahivi umevurugwa na taarifa nyingi?” “Mimi nakupenda Brina. Lakini wewe una…” “Kabla hujaendelea sana, naomba tulia na ufikirie kila neno linalotoka kinywani mwako Jack. Inawezekana nilipitiliza kwenye kuwatafutia watoto msaada, lakini hata kama ungekuwa wewe usingefanya tofauti. Mimi nimekataa kufa kijinga, kuacha watoto wakiteseka wakati wanaweza kupata msaada hata kama sisi hatupo. Unakumbuka habari za Hezekia yule aliyeandikwa kwenye kitabu cha Isaya mlango wa 38?” Jack akanyamaza.

“Yule aliyekuwa mfamle wa Yuda, Jack?” Jack akakunja uso kuashiria bado hajakumbuka vizuri. “Yeye alikuwa mfamle mzuri sio muovu kama wafamle wengine waliopita kuongoza Yuda. Ninachotaka kukwambia ni katika swala lake yeye alipougua na kukaribia kufa. Nabii Isaya alitumwa kwake na Mungu. Unakumbuka ujumbe aliokuwa ametumwa?” Kimya. “Sio atubu. Mungu hakumtuma Nabii Isaya akamwambie tubu kwa kuwa utakufa, aliambiwa Bwana anasema hivi, ‘Tengeneza mambo ya nyumba yako, kwa sababu utakufa, hutapona’. Hakupewa ujumbe mwingine wowote ila huo tu. Ila unakumbuka ndio baadaye akamuomba Mungu kwa uchungu akimkumbusha mema aliyotenda hapa duniani, ndipo Mungu akamwambia atamuongezea miaka mingine 15 na kumuokoa kutoka kwa mfamle wa Ashuru, na ahadi ya kuulinda mji. Ila ninachotaka kusema, kutengeneza mambo ya nyumbani kwetu kabla hatujafa ni mpango wa Mungu, Jack. Sio kitu kibaya.” Jack akapoa na kurudi kuinama.

“Naomba twende tukalale Jack.” “Mimi nimekasirika.” “Sasa umekasirika nini!? Nafikiri mimi ndio natakiwa kukasirika Jackson. Na ukumbuke kesho una kikao kinachosubiriwa majibu na mzee Msindai. Naomba twende ukalale, uamke mwenye akili safi.” “Unanichanganya Brina. Tulianza vizuri. Mimi na wewe tu, lakini naona sasahivi tupo wengi kwenye hii ndoa. Mara Tino awepo, mara umtoe. Sijui baada ya miezi 6 aliyokupa baba, mtaamua nini! Kama watoto ni wangu au..” “Si umeshasikia watoto ni wa Msindai!” “Kwa hiyo?” Jack akaendelea kuuliza.

“Kama mimi na wewe hatupo, basi ni wa Jacinta. Na Junior ameambiwa na wao ni warithi wa mali za Msindai. Sasa wewe wasiwasi wako ni wa nini? Maana mimi mwenzio sina tena wasiwasi. Nishajua hata nisipokuwepo, wanangu watakufa matajiri. Mali yote hiyo ya Msindai!” “Acha kucheka bwana Brina!” “Wewe unataka kujiudhi bure Jack, mume wangu.” “Ukiniita hivyo ndio inakuwa afadhali.” “Muone!” “Basi twende tukalale wote, Brina!” “Tangulia. Acha mimi nikanyonyeshe raundi ya mwisho ndio nije kulala.” “Acha nikusubirie, labda usiku wa leo unaweza kunihurumia, angalau nikalala na mke wangu, kesho nikaamka akili imetulia kabisa.” Sabrina akamwangalia na kuondoka. Jack akamfuata mbio.

“Sasa tutakaa hivihivi mpaka lini, Brina wangu! Hasira haziishi tu ukanitamani mumeo?” “Acha kelele Jack!” “Sawa, kwani wewe huna hamu na mimi? Mwenzio nakutamani. Nikimuona vile Brandon anavyokunyonya nakuwa…” “Naomba kanisubirie chumbani Jack!” Jack akaanza kucheka. “Au tuanzie chumbani ndio ukanyonyeshe wakati mimi nalala kwa ajili ya kikao kesho?” “Hapana Jack. Mimi mwenzio akili zitakua hazijatulia.” “Yessss!” Jack akashangilia mpaka akaruka kwa Sabrina kukubali penzi. “Unapiga kelele Jack! Unataka mpaka watoto wote waamke tuanze tena kazi ya kubembeleza!” “Hakika watasubiri. Bora hawana njaa, wala hawaumwi, watanisubiri kwa kweli. Na mimi nakuhitaji! Haaa! Wanakuganda wakati wote mpaka mimi nasahauliwa!” “Haya naomba nenda basi chumbani.” Jack akaenda chumbani kwa furaha zote.

Alichokiunganisha Mungu.

H

ata Sabrina alikuwa na hamu na mumewe. Tokea siku wanaagana asubuhi ya Sabrina kwenda kufanyiwa upasuaji wa huyo Brandon, hakuwa amefanya mapenzi na mumewe tena. Akanyonyesha harakaharaka hata kabla mwanae hajatoa nyonyo mdomoni kuashiria ameshiba, akamrudisha kitandani na kutoka hapo kwa haraka asije mkuta Jack amelala. Akamkuta anachagua nguo zakuvaa kesho yake akamdaka. “Acha nioge kwanza. Wewe chagua tai na mengineyo nakuja sasahivi.” “Nikuulize Brina?” Sabrina akamwangalia wakati akivua nguo. “Nini?” “Kwani na wewe ulikuwa na hamu na mimi?” “Sana Jack! Kwa nini?” “Mbona sasa siku ile tulivyotoka kwenye harusi palikuwa na mazingira yote yakufanya mapenzi lakini ukataka tulale tu? Mimi nikajua hunitaki tena!” “Mambo mengi yalikuwa yakiendelea, Jack. Akili ilikuwa haijatulia. Lakini bado nakupenda Jack wangu.” “Eti nimefurahi kusikia hivyo!” Sabrina akacheka na kuingia bafuni.

Ulikuwa usiku wa kukata na shoka kwa Jack hata Sabrina mwenyewe. Kila mmoja alisikika kutoridhika na mwenzie kwa haraka kitu kilichowatuliza wote. Kwa Sabrina akafurahi kuona bado mumewe anamfurahia japo alipita mrembo Phina hapo katikati yao. Na kwa Jack akafurahia kuona wala Sabrina hamuonei kinyaa kwamba anaona uchafu kwa kuwa alilala na mwanamke mwingine. Aliyokuwa akimfanyia kabla, hata usiku huo alimfanyia tena kwa kina na furaha zote. Jinsi alivyombana kwa mdomo, Jack alikaribia kumalizia mdomoni ila Sabrina akamuwahi na kumkalia kwa haraka akiwa Jack amelala chali mpaka hiyo safari wakaimaliza.

Na Japokuwa hakuweza kunyonya matiti ya mkewe na Sabrina kupata starehe ya ulimi wa mumewe kwenye chuchu zake, lakini aliipata midomo ya mumewe sawia na kufika kileleni akiwa anasikilizia midomo ya mumewe inavyomnyonya kwa uchu wote kana kwamba anavuta kitu kitamu. Jack alipita taratibu na kwa haraka akimchezea kwa ulimi huku ndevu zikiamsha kamasa vilivyo, mpaka alipotulia akiwa anamnyonya vizuri huku akikipekecha mdomoni mwake kwa ulimi mpaka Sabrina akamalizia safari yake ya mwisho kwa furaha zote. Walilala kama waliotoka shamba kwa kuchoka kwa penzi la kukata kiu.

Mbele Ya Kaisari.

A

subuhi hiyo Jack akaamka jasiri kama simba. Na hivi mkewe amemsamehe! Huna kosa utakalomkumbusha Jackson ukamuumiza. Alitoka hapo mapema sana akiwa amependeza vilivyo. Hakuwa amevaa tu koti la suti. Lakini shati jeupe safi na alifunga tai yake. Tena lilikuwa miongoni mwa mashati ambayo Sabrina aliyatoa dry cliner. Safi. Linawaka na kung’aa kwa weupe. Koti alilining’iniza nyuma ya gari akitaka kulivaa wakati akiingia ofisini kwa bosi wake, kaka yake akiwepo. Njia nzima alikuwa akipiga miluzi.

Saa nne kasoro 10 akapata simu kutoka kwa sekretari wake kuwa anaitwa ofisini kwa Waziri wa Fedha. Akatoka akiangalia saa maana alifikiri ingekuwa saa nne kamili. Tokea yupo nje, akamsikia kaka yake akicheka na Waziri wa Fedha ndani. Sekretari wa Waziri akamwambia aingie. Ile hali aliyoikuta mle ndani, ikabidi tu atulie na hofu imuishe. Hakutaka kujikaribisha wala kuingilia, akabaki amesimama. “Naona mzee hataki mchezo! Ametuma video mapema kweli, nimekutana nayo mlangoni!” Akaongea bosi wake akimgeuzia kompyuta na yeye aone. Jack akajisogeza karibu. “Naona ni sauti tu ndio hamna. Lakini kwa sura anaonekana vizuri kabisa. Unaweza kurudisha kuanzia mwanzo.” Jack hakuwa akiamini jinsi baba yake alivyofanya mambo kwa haraka. Wamezungumza jana yake tu, asubuhi hiyo video imeshaingia nchini! Akamsogezea laptop yake, yeye akarudi kuzungumza na Junior wakicheka. Jack akajivutia laptop karibu.

Ya Nchini Uswiz.

J

ack akarudisha hiyo video kuanzia mwanzo. Akaonekana Phina anatoka chumbani kwake. Akaelekea kwenye lift huku akijitengeneza vizuri. Lift ikamchukua mpaka gorofa aliyokuwepo Jackson Msindai. Kweli akaonekana amegonga kwa muda. Kisha akaonekana anazungumza akiwa bado amesimama nje ya mlango uliokuwa bado umefungwa, akasubirishwa kidogo. Akaonekana anasubiria nje ya mlango huku akitengeneza matiti yake kuyafanya yaonekane vizuri kwa nje, na kuweka nywele vizuri wakati akisubiria. Bada ya muda Jack akamfungulia akionekana anachungulia sio kutoka kabisa. Wakazungumza kidogo. Japokuwa maneno hayakusikika, lakini akaonekana Jack kurudi tena ndani. Hapo kukawa na kusubiria tena. Phina akaonekana nje ya mlango kuendelea kujiweka sawa. Akarekebisha matiti yake tena na tena akiyanyanyua juu zaidi. Akayachungulia mara ya kwanza, akaonekana kutoridhika. Akasogea pembeni ya mlango. Akayapanga tena mpaka akaridhika ndipo akarudi tena mbele ya mlango. Akaweka sawa nywele zake, akasubiria tena, ndipo mlango ukafunguliwa. Safari hii Jackson hakuonekana hata kuchungulia ila Phina akaingia ndani. Mapigo ya moyo ya Jack yakaanza kwenda kasi. Akatazama muda tokea Phina alipoingia. Akaandika kwenye kikaratasi. Akabaki pale akisubiria kuona muda aliotoka Phina, kana kwamba hakuwepo huko nchini Uswiz siku hiyo na sio yeye aliyemfungulia mlango.

~~~~~~~~~~~~~~

CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment