“Umesahau Phina tulikuwa
naye chuoni na mimi ndiye niliyemsaidia kutafuta kazi aliyo nayo?” Kimya. “Kwa
maana nyingine, nilijua Phina yupo, ila nikakuoa wewe. Na kama ningekuwa nataka
mwanamke mnene, basi Pam uliyenikuta naye kule Singida sasahivi angekuwa mke
wangu au hata huyo Phina mwenyewe. Lakini mbona nilikuoa wewe? Tuwe wakweli
Sabrina, wakati wote mimi ninaokurudia, unakuwa matatizoni na unakuwa umekonda
sana tu!” “Mmmh! Naona leo umeniamulia.” “Nakwambia ukweli ili urudishe mawazo
kwenye mahusiano yetu. Najua umekasirika, lakini pia najua unajua kama nakupenda
Brina. Sijakosea kukuoa wewe. Nakupenda vile ulivyo mke wangu. Sema nimekosa. Nimejikwaa
ambako sikutegemea. Naomba unisamehe. Na tafadhali kesho naomba nifichie aibu
yangu. Nisindikize harusini. Angalau baba anione nipo na wewe pengine anaweza
hata kupokea salamu yangu vizuri.” Hilo likamshitua kidogo Sabrina.
“Kwani na mzee Msindai
atakuwepo!?” “Familia nzima inatakiwa kuwepo. Ni mtoto ambaye baba alimsimamia
ubatizo. Kwa hiyo mzee Msindai ni baba wa ubatizo na alikuwa akimtibu wakati
mtoto mpaka amekua. Kwa hiyo ndio naomba tuongozane.” Sabrina akanyamaza. “Na
swala la wembamba, nilikuoa hivyohivyo ila sema sasahivi umepungia zaidi, tena
ni kidogo tu. Wala haina tofauti na unavyokuaga.” “Mimi sijaelewa aina hii ya
msamaha jamani!” Angalau wakaanza kucheka.
“Naona unataka kujipa
sifa zisizo zako mama. Mimi nakupenda hivyo ulivyo. Nabeba na kuhamisha
nitakapo bila kutokwa jasho ila kufaidi tu. Halafu asilimia kubwa ya tutakao
wakuta pale walikuwepo kwenye harusi yetu, na wanamjua Sabrina wangu alikuwa mwembamba
tokea mwanzo. Hao wa mitandaoni achana nao. Hawatujui. Ni mashabiki tu, kazi
yao kuniharibia.” “Umeharibu wewe mwenyewe, wala si watu! Nani..” “Basi mama. Basi.
Huko unapokwenda ni kurudi nyuma. Utapandisha hasira halafu tutaanza upyaaa. Acha
tuendelee hapahapa. Kwa hiyo?” “Tutakwenda lakini kwa mashariti.” “Gani tena!?”
“Sitakwenda after party.” “Hata kama Jacinta atakuwepo na Junior?” Hapo
Sabrina akatulia kidogo na kuanza kushawishika. “Si unajuaga inavyokuwa nzuri?
Tena..” “Mwenzio nina watoto wadogo, Jack. Nitawahi kurudi ninyonyeshe. Wewe
nenda tu. Uwe na amani. Kafurahie na wenzio.” “Basi tutarudi wote. Wakatulia.
Sabrina akageukia upande mwingine akalala. Jack aliogopa hata kumgusa asije
haribu. Akajisogeza pembeni kabisa na yeye akalala.
Jumamosi.
Sabrina alimuacha Jack
kitandani akiwa amelala hana habari. Akamuelewa maana na yeye alikuwa amechoka
akili, hakuwa akipumzika kwa mawazo akijua Phina na mwanae wameingilia ndoa
yake. Hata akilala alikuwa akilala usingizi wa mang’amung’amu. Usiku aliompa
Jacinta, alilala kama mtoto mchanga. Akajua ndio anachokipata mumewe. Mazungumzo
waliyoyafanya, yamempa pumziko la akili. Akamuacha apumzike na kutaka kila mtu
awe kimya humo ndani ili alale.
Akiwa chumbani kwa wanae
wakiume, ametoka kumuogesha na Brayan, Jack akaingia. Ilishakuwa saa nne
asubuhi. “Huyu mbona yupo uchi? Si umuite Pina akusaidie?” “Michezo mingi! Ila
namtafutia nguo, nitamvalisha sasahivi.” “Natoka. Sitakawia kurudi.” “Na mimi
nitatoka baadaye kidogo niende saluni nikatengenezwe kwa harusi.” “Nahisi
nitakukuta. Sitakawia. Mzee Msindai anataka nikaache damu hospitali ya Usalama
wa Taifa. Sikawii maana wananisubiri.” Sabrina akashangaa. “Damu ya nini
tena?!” Akajiuliza ila akaona anyamaze tu. Jack akatoka.
Ndoa Na
Iheshimiwe Na Watu Wote.
J |
ack na mkewe wao hawakwenda kanisani. Waliamua
kwenda ukumbini tu. Ulipofika muda wa kwenda ukumbini, wakatoka. Sabrina
alipendeza sana. Walimtengeneza vizuri, hata kule kukonda kukampendeza. Na Jack
alivaa suti nyeusi nzuri. Akapendeza maana alipitia kufanyiwa na usafi wa kichwa. Kwa
hiyo wote wakatoka wasafi. Ungejua yapo mafanikio kwao. Walinukia neema tupu.
Jack akatoka kama Naibu Waziri kwelikweli na mkewe. Walifika ukumbini
wakatafuta meza ya Msindai. Jacinta alifurahi sana kumuona Sabrina. “Hapa Jack
asipoangalia ataporwa mjini! Umependeza sana Sabrina, wifi yangu! Upo kama
kabinti kasikokuwa na mtoto hata mmoja! Kama mwana mitindo ulioshushwa kutokea Los
Angeles!” Sabrina alicheka sana. “Asante wifi yangu. Shikamooni.” Akasalimia
wengine hapo mezani. “Bi mdogo naona mambo yako si mabaya.” “Na wewe umependeza
Joy. Na shem pia. Wote mmependeza.” Junior akaitikia. Jack kimya.
“Baba na mama wako wapi?”
Akauliza Sabrina. “Mzee Msindai yule kule mbele kwenye meza ya wazazi, naona
hajaja na mkewe.” Akajibu Jacinta na kuendelea kunywa. Hata Jena hakuwepo.
Stori zikaendelea hapo mezani. Jack na mkewe kimya. Maharusi wakaingia, sherehe
ikaanza rasmi. Kila mtu kula na kunywa na MC mcheshi basi kukawa na kucheka.
Ila Sabrina akawa amepoa tu. “Unasikia baridi?” Jack akamuuliza kwa
kumnong’oneza sikioni. “Naona hapa ukumbini wamewasha AC kali!” Sabrina
akalalamika. Jack akasimama akavua koti lake kisha akamfunika vizuri. “Asante.
Lakini si na wewe utasikia baridi?” “Nipo sawa.” Akavuta kiti cha Sabrina
karibu na kiti chake. Kisha akampitishia
mkono juu. Sabrina hakukataa. Akajisogeza karibu, akawa kama amemuegemea
mumewee upande mmoja, Jack akamkumbatia vizuri. Wakatulia. Ila Sabrina
akasikika kuvuta pumzi kwa nguvu kisha akatulia. Wao wawili wakawa wala si
wazungumzaji, ila watizamaji tu. Kimya.
Kilipofika
kipindi cha waalikwa kucheza, baada ya maharusi kufungua kwa mziki wa taratibu,
Junior akasimama na kumshika mkono mkewe na kumuongoza njia pale mbele ili
wacheze na maharusi. Junior akamshika mkewe vizuri, Joy akamkumbatia mumewe, wakaendelea
kucheza. Wakatulia wakiwaangalia wanao cheza. Jack akambusu mkewe sikio ambalo lilikuwa
upande wake mpaka Sabrina akasisimkwa, akacheka na kumwangalia. Hakutegemea! “Twende
na sisi tukacheze.” Sabrina akajishauri akisikiliza huo wimbo, ukamvutia.
Akatingisha kichwa kukubali. Jacinta kimya akiendelea kunywa taratibu.
Akatoa koti la mumewe,
Jack akalivaa na yeye akamungoza njia mpaka pale mbele. Sabrina hakujivunga, akamzungushia
mikono yote juu ya shingo, Jack alifurahi akatamani kumuuliza baba yake kama
anaona! Akamkumbatia na yeye vizuri, wakaanza kucheza. Kweli walipendeza. Alivaa
gauni lililomkaa vizuri sana na likaenda na mwili wake. Walionyesha hadhi
waliyonayo kwa wkati ule. Sabrina alivaa nadhifu sana kama mumewe. Pendo huwa
ananunua nguo kwa mwanamke anayetoa nguo, viatu na vitu vingine kutoka nje ya
nchi. Alimuunganisha na Sabrina na yeye akawa mteja mzuri sana wa huyo mama. Kwani
na wao huwa wananunua bila kukopa, hulipa siku wanapochukua kitu wanachokipenda
kutoka kwa huyo mama. Basi kila anapoingiza mzigo mpya nchini Pendo na Sabrina wanakuwa miongoni mwa wateja
wake wa kwanza kuwaambia ili wachague wao kwanza kabla ya wengine. Kwa hiyo
hiyo nguo Sabrina aliinunua tu na kuiweka kabatini ikisubria siku ya
kuvaliwa
maana alimuitia mzigo mpya na hilo gauni akamwambia alimchukulia maalumu kwa
ajili ya kamwili kake kadogo. Ndipo Sabrina akalilipia na kuliweka tu kabatini.
Siku hiyo alilivaa na
kiatu cha juu. Nywele ikatengenezwa vizuri. Sabrina alipendeza sana. Jinsi Jack
alivyokuwa amemkumbatia, mpaka Sabrina akajilaza kifuani wakati wakiendelea
kucheza.
Mzee Msindai akaenda
kumchukua Jacinta wakacheze naye. Na wao wakaenda kucheza palepale pembeni yao.
Wakacheza nyimbo nyingine mbili ukiwepo wa ‘It wasn’t easy, but it’s worthy’
uliopigwa na mwimbaji mashuhuri wa nyimbo za injili nchini Marekani, mwanamama
Cece Winans. Mzuri sana, aliuimba kama Yesu akiongelea kazi nzima ya msalaba,
lakini ukaendana kabisa na wanachopitia Jack na Sabrina. Kwamba, ‘Haikuwa Rahisi, Lakini Inastahili’. Ukisikiliza kwa
haraka bila kusikiliza maneno yake unaweza usielewe kama ni wa Mungu unasikika kama
wimbo wa taratibu tu kama nyimbo nyingine za kimapenzi, lakini ulibeba
maana kubwa na nzito, ulifanya wasikilizaji maneno kwenye nyimbo kutulia
na kutafari zaidi.
Don't think
for a moment, I never felt the pain, You can't imagine, The hurt and the shame, They
put the nails through my hands, Pierced my side, please, understand
It wasn't
easy, but it was worth it, It wasn't easy, it wasn't easy, It wasn't easy, but
it was worth it, It wasn't easy, it wasn't easy, It wasn't easy, but it was worth
it, I didn't have to do it, But I did it anyway
'Cause I
really love you, So much I took your place, I died for your sins, Yes, I'm the
one, Don't take it lightly what I've done, It wasn't easy, but it was worth it,
oh, It wasn't easy, it wasn't easy, It wasn't easy, but it was worth it, It wasn't
easy, it wasn't easy, It wasn't easy, but it was worth it
I left my
throne, My purpose was the cross, Shed innocent blood, I paid the cost
It wasn't
easy, it wasn't easy, It wasn't easy, but it was worth it (but it was worth it),
It wasn't easy, it wasn't easy, It wasn't easy, but it was worth it, It wasn't
easy, it wasn't easy, It wasn't easy, but it was worth it, It wasn't easy, it
wasn't easy (it was worth it, yes it was), It wasn't easy, but it was worth it
It was
worth it, ooh, No, it wasn't easy, no, it wasn't easy
But it was
worth it, Ooh-oh
Wakaucheza huo wimbo
vizuri na kufuatisha maneno mpaka ulipoisha. Ilipoanza Twist, Sabrina akajitoa
mikononi kwa Jack, wakaondoka hapo sehemu ya kucheza wakicheka, kwamba wamesalimu
amri, wawaachie wawezaji. Wazazi wengi wakasimama kuingia kucheza kwa furaha
zote. Enzi zimerudishwa! Wakarudi kukaa “Naomba urudi kukaa kama vile ulivyokaa
mwanzo.” Jack akamsihi mkewe. Sabrina akamgeukia. “Sasahivi sisikii joto. Nipo
tu sawa.” Sabrina akajivunga. Jack akamwangalia, Sabrina akatoa tu tabasamu na
kurudi kuangalia waliokuwa wakicheza. Akamsikia Jack amejivuta mpaka kwenye
bega lake, akamuegamia yeye. Akamchungulia pale alipojiegemeza. “Nakupenda
Brina.” “Najua.” Jack akamvuta mkono akaanza kuchezea pete zake, wakatulia.
Sabrina akageuka na kumbusu kichwani maana bado alikuwa amemuegemea. “Nashukuru
mama.” Sabrina akacheka, wakatulia.
Wakashitukia mzee Msindai
amewasimamia. Wote wakasimama kama watoto wa shule ya msingi waliofumaniwa.
“Shikamoo baba.” “Marahaba mama. Umekula vizuri?” “Naona nimezidisha.” Mzee
Msindai akacheka. “Nakusanya maziwa ya kaka mdogo.” “Unajuhudi ya kunyonyesha!
Lakini hiyo ni nzuri sana.” “Asante baba yangu. Naona na wale kuku wa kienyeji
ulioniletea wanasaidia kuongeza maziwa. Asante sana.” “Karibu. Wewe Twist hujui
kucheza?” “Hata kidogo. Naweza kuanguka kabisa! Umependeza sana baba.” “Asante.
Suti hii zawadi kutoka kwa Jacinta. Naipenda sana. Huwa navaa kwenye vitu
muhimu kama hivi.” “Basi acha na mimi nije kukununulia ingine. Ziongezeke.”
“Afadhali nipate nzuri ingine ya kubadilisha.” Wakacheka kidogo, Jack kimya. “Tutembee
kidogo.” Jack akajua ni yeye anaambiwa atoke wakazungumze nje. “Nitarudi,
Sabrina.” Akavua koti lake na kumvalisha mkewe, baba yake akatangulia nje.
Wakamuacha Sabrina hapo mezani peke yake, wengine wote wakicheza mbele. Jack na
baba yake nje kabisa ya ukumbi. Sabrina kimya akijiangalizia tu.
Baada ya muda Jack akarudi
akiwa amepoa haswa. Akajua mazungumzo kati yao bado hayaendi vizuri. Akarudi na
kutulia kupita kawaida. Sabrina akamuona mzee Msindai anapita kurudi alipokuwa
amekaa. Sabrina naye akamuacha tu.
Kila Kosa Na Garama Yake. Hata Kama Mungu Amesamehe, Huwezi Kuepuka Kulipa Garama.
Wakati wapo njiani kurudi
nyumbani baada ya harusi kuisha, akatoa bahasha na kumkabidhi Sabrina. “Asubuhi
nilikwenda kupimwa. Baba alitaka niende nikaangalie afya yangu.” Hilo halikuwa
jambo baya, hata Sabrina hapo akafurahia. “Mbona umepoa sasa? Umepata matokeo
mabaya!?” “Fungua usome.” Sabrina akaingiwa hofu akafungua na kusoma. Akaona
kila kitu kipo Negative kwamba hana
ugonjwa wowote. “Sasa mbona umekosa raha kwenye majibu mazuri hivi!?” “Phina
amerudi. Safari hii anamadai mengine.” “Ni nini tena!?” Sabrina akamuuliza
akiwa na wasiwasi.
“Amemtafuta Jena mpaka
kazini kwake. Amemwambia anampango wa kunishitaki mimi kuwa natumia madaraka
niliyopewa na Raisi, vibaya. Narubuni wanawake kwa kutumia cheo nilichopewa.
Nikishalala nao, nawatelekeza. Ananishitaki kwa kumtelekeza yeye akiwa mjamzito,
mpaka akaugua na kumpoteza mtoto wetu. Anasema japokuwa ushahidi ulipotezwa,
yeye Jena atabaki kuwa shahidi wake maana alishamfuata. Akakubali kuwa mtoto ni
wa Msindai. Akamuahidi yeye na mama kumfanyia babyshower na kumkaribisha
ramsi kwenye familia. Anasema anao mashahidi waliosoma comment ya Jena,
na ku like post yake ya babyshower kuashiria kweli alikuwa
mjamzito wa mtoto wangu.” Sabrina akashituka sana. Akatulia kwa muda
akifikiria.
Mwishoe akaona aulize tu.
“Sasa baba ameshaurije?” “Daah!” Jack akasika kuumia zaidi. “Niambie tu.” “Hivi
tunavyozungumza, Ibra na Phina wamerudi
kuwa timu moja. Maana mwanzo..” Ikabidi Jack amuelezee Sabrina sasa kuanzia
mwanzo walipoungana na kumfuata nyumbani mpaka mwisho jinsi walivyofuta
ushahidi kwenye simu zao na kuchukua hata nakala za picha walizokuwa
wamechapisha. Sabrina akazidi kuwaogopa hao kina Msindai. Ikabidi akae sawa
asikilize zaidi.
“Sasa kama ulivyosikia
siku ile pale nyumbani, simu yangu ilibadilishwa, na inafuatiliwa. Sasa
nafikiri katika yote hayo, kupoteza mtoto na kuhamishwa kituo cha kazi,
inavyosemekana Phina akaanza kunitafuta bila mafanikio. Nasikia ijumaa alikuja
mpaka pale ofisini, akaambiwa hawezi kuniona mpaka miahadi. Ndipo nasikia
akamtafuta tena Ibra ili aungane naye kuendeleza mipango yake ile ya kwanza. Safari
hii nasikia Phina amemuahidi Ibra kumpa ushirikiano wote.” “Naomba nikuulize
kitu Jack. Na naomba uwe mkweli.” “Niulize tu.” Sabrina akamwangalia kwa muda,
mpaka ikabidi Jack atoe macho barabarani na yeye amwangalie.
“Niulize tu Brina. Na
nakuahidi sitakudanganya kama najua jibu lake.” “Ni nini ulimuahidi Phina huko
mlipolala?” “Acha nikwambie ukweli Sabrina. Hapakuwa na kutongozana, wala
mazungumzo. Mpaka nahisi Phina alinitega jamani! Maana unajua yeye alikuwa
miongoni mwa watu wanaoandaa safari za Wizara. Alijua kama tutasafiri mimi na
wenzangu. Wao walitangulia huko kuanza kuweka mipango. Kwa hiyo alijua nani
atalala wapi.” “Wewe ulijua kama yuko huko?” “Mungu wangu nishahidi Sabrina.
Sikuwa nikijua kama yuko huko na hata kama alihusika na mipango ya malazi yetu
huko.”
“Anyways.
Tulipofika kesho yake tulikwenda kwenye mkutano kama kawaida, nikarudi chumbani
baada ya kukaa na wenzangu baa. Mimi nikachoka, kwa sababu mimi sinywi. Nikala,
nikaamua kwenda kulala. Wakati nishavua nguo kabisa, nipo kitandani, Phina
akaja kunigongea. Kwanza nilishituka. Sikutegemea kama angekuwepo kule maana
waliokuwa wameongozana nao nilishakutana nao wote. Akasema kuna sehemu yeye na
mwingine walikwenda kama matembezi ndio maana wakati sisi tukisalimiana na wenzake,
sikumuona. Basi, akasema kuna kitu anaomba azungumze na mimi. Tena Mungu
nishahidi. Nikamwambia kabisa sipo vizuri, kwa kuwa nilishapanda kitandani
kulala. Akasema hatanichukulia muda mrefu. Nikamwambia asubiri hapo mlangoni.
Nikarudi kuvaa pensi, nikamkaribisha.”
“Siwezi kukwambia
aliyoniambia, lakini nikaja kushitukia nimeshalala naye. Nikamwambia kabisa,
nimefanya kosa, sikutakiwa kulala naye. Nikamwambia mke wangu ni mwaminifu sana
na ananipenda, sikutakiwa kumfanyia hivyo. Nikamuomba avae, atoke. Unajua ni
ile aina ya milango ukitoka, huna haja yakufunga tena kwa ndani. Inajifunga tu
yenyewe ila kuingia ndio mpaka mtu wa ndani akufungulie, au utumie kadi.
Kwahiyo nikamuacha akivaa ili atoke, nafikiri nikapitiwa na usingizi. Nilikuwa
nimechoka Sabrina. Siku ilikuwa ndefu.” “Na umetoka kufanya mapenzi.” Sabrina
akamalizia. Hapo Jack hakutaka kuchangia kabisa ili papite kwa haraka. Akaendelea
kwa haraka.
“Basi nafikiri alipoona
nimelala ndipo akanipiga picha.” “Kwa hiyo si kwamba mlilala mpaka asubuhi!?”
“Hapana! Tena hata yeye nilimuuliza ni kwa nini anatangaza kana kwamba nililala
naye usiku kuchwa? Ni kama hakunipa jibu la kueleweka. Ila kama nilivyokwambia,
sikutaka kumbana sana, nikitaka atulie, awe upande wangu, ili kufuta hizo picha
na kumtuliza. Sasa sasahivi ndio nasikia wapo na Ibra. Wameshafikia magazeti
zaidi ya matatu.” “Mmmh!” Sabrina akaishia kuguna.
“Sasa baba anasema
amefanikiwa kufuta hiyo habari kwenye magazeti makubwa, ila ya Udaku
imeshindikana, ndio maana ameniomba nizungumze na wewe mapema. Ujue kesho hiyo
habari itakuwa imeenea.” “Sasa baba anataka mimi nifanyaje?” “Kwanza ujue ili
isikushitue kama walivyokushitukiza mwanzo, wote tukapaniki.” Sabrina akapoa,
akakumbuka jinsi ilivyoingiwa hofu mwanzoni.
“Anasema mambo mengi
yanaweza kuchimbuliwa. Mengi mno. Yangu, yako mpaka watoto pia. Anachosema
tunaweza kuja kujaribiwa kumjibu yeyote yule. Ameomba kama utaweza, unyamaze
kabisa. Hata usijaribiwe kujibu hata kwa hekima. Halafu tuache tuone
watasababisha madhara makubwa kiasi gani. Anasema tunaweza kutumia nguvu kubwa
kupambana na hili, kumbe madhara yake yanaweza yasiwe makubwa sana. Kwa sababu
sasahivi hawana tena ushahidi. Watakachoweza ni kunichafua na mengine ambayo hatujui.”
Sabrina akanyamaza. Akajivuta mwisho kabisa wa kiti, akatulia.
“Najutia Sabrina. Najutia
sana.” “Najua Jack. Na pole.” Jack hakuamini. Akamwangalia. “Namaanisha. Najua
hata kama wewe ni malaya wa kiasi gani, lakini najua usingekuwa mjinga,
kukubali kuingiza familia nzima matatizoni kwa kiasi hiki.” Jack akaumia sana.
“Kwa hiyo wewe unaamini mimi ni malaya?” “Samahani imetoka mdomoni vibaya,
Jack. Lakini najua unaelewa namaanisha nini. Kuwa wewe si mjinga kujiingiza
matatizoni kwa kiasi hiki.” Wakatulia.
“Najua sasahivi ndio
unaweza kurudi Singida kabisa! Maana kuanzia kesho, mjini hapa patachafuka
kwelikweli.” Jack akawa kama anamjaribu tu kujua atasema nini. Sabrina
hakujibu. “Maana nasikia amesema hana chakupoteza tena. Kumbe mwanzoni hakutaka
Ibra aseme si kama alivyoniambia akiniaminisha anataka asiniharibie mimi, kumbe
alikuwa akijilinda na yeye kikazi na kujua nitazaa naye. Sasa nasikia amesema
kwa kuwa na kazi pia amepoteza, hataogopa hata akiitwa kwenye kuhojiwa popote
kule, atakwenda kuongea yote.” “Ameamua kutokwenda huko Lindi?” “Unajua yupo na
Ibra ambaye na yeye aligoma kutoka hapa mjini. Kwa hiyo atakuwa amemshauri tu
asiende, atafute kazi hapa mjini.” Sabrina akatulia mpaka nyumbani.
Alipofika tu, wakina Pina
wakatoka mbio. “Tukupokee dada?” “Mna njaa zisizowaisha nyinyi! Na safari hii
sijaleta kitu. Nimetoka kwenye harusi.” “Dada naye! Si ungebeba hata kipande
cha keki!” “Songa ugali ule wewe mtoto. Acha njaa zisizoisha.” Sabrina
akapitiliza chumbani kwake. Akaenda kuoga, kazi ya ulezi ikaanza. Kunyonyesha
na kukamua. Jack akamfuata tena. “Naomba safari hii usikaukwe maziwa kwa
mshituko, Sabrina.” “Hapana. Nashukuru kuniambia mapema. Kwanza imenisaidia kujua moyo wako na
kunituliza. Mwanzo ulinikimbia Jack, ikanichanganya zaidi nikijua umekusudia
kurudiana na Phina! Na nikajua ulianzisha tabia ya kulala na wanawake huko nje.”
“Huo udhaifu wa kukimbia na kuingiwa hofu, najua nilikuahidi nitabadilika,
lakini nafikiri niongeze juhudi kuweza kukukabili kipindi cha matatizo tuwe
tunazungumza nisiwe nakuacha ukiwa huna taarifa kamili.”
“Nilikuwa nikitaka kukwambia
safari hii sitapata mshituko kama mwanzo mpaka kukaukiwa maziwa kwa kuwa sasahivi
ni kama akili imeshajindaa kupokea chochote, maana nishafikiria mabaya zaidi.
Akili imejiandaa na mpaka ambayo wewe hujayasema pale garini, mimi nishayafikiria
na akili imeyapokea. Kwa hiyo hakuna kitakachonishitua tena.” Ikabidi Jack aingie
na kukaa hapohapo chumbani kwa watoto wao wakiume.
“Kama nini tena
ulichofikiria!?” “Kuvuliwa madaraka!” “Umefikiria mbali! Maana na hilo baba
ameniambia nijiandae nalo endapo itakuwa skendo kubwa. Sema nilikuwa naogopa
kukwambia.” Sabrina akanyamaza na kuendelea kunyonyesha mtoto aliyekuwa amelala
huku akivuta. “Nimekuangusha eeh?” “Nafikiri zaidi Mungu aliyekuamini.” Sabrina
akajibu na kunyamaza. Jack naye akabaki ameinamia magoti anawaza. Kimya.
~~~~~~~~~~~~~~
Akasubiri mpaka mkewe
akamaliza shuguli zake hapo chumbani, akawa na kazi ya kumfuata mpaka jikoni
alipokuwa akisafisha vifaa alivyotumia kukamulia maziwa. Anamfuata nyumanyuma
ila kimya. Sabrina akamuacha tu mpaka akamaliza na wakahamia chumbani. Kimya
tu. Akaweka mambo yake sawa, Jack yupo tu. “Naomba lala Jack.” “Nakusubiria
wewe.” “Mimi namalizia kujisafisha, nitoe harufu ya maziwa, ndio nije tulale.”
“Nimefurahi ulivyosema hivyo.” Sabrina akamwangalia na kuelekea bafuni.
Akatoka bado yupo.
Akapanda kitandani. “Utarudi Singida?” “Kwani huko ndio hakuna magazeti?”
“Lakini kweli. Kwa hiyo utafanyaje?” Akavuta pumzi kwa nguvu na kubaki
akifikiria. “Unazidi kunichukia eeh?” “Hapana Jack. Umenifanya nikumbuke hapo
ulipo. Mimi nimeshakua hapo Jack. Mara mbili. Ila hapo ulipo sasahivi, ndio
panafanana na Dodoma kabisa, kule chuoni. Kila anayekutizama, unahisi anakuona
upo uchi.” “Kweli aisee! Au anakuhukumu! Mpaka hao wasichana wako wa kazi naona
hata wanavyoniangalia sio kama zamani. Sasa sijui ni kweli au mawazo tu!”
“Inaweza kuwa kweli au ni hofu tu.”
“Sasa ulifanyaje?” “Ni
wewe Jack! Huoni jinsi nilivyojirudi kwa haraka? Ulinitoa mavumbini. Chini
kabisa. Ndani ya masaa 24 ukanirudisha juu kabisa na ukabadilisha historia
yangu pale chuoni. Haikuniondolea ile aibu ya kukataliwa na Emma vibaya vile,
lakini angalau nikaonekana ni wathamani. Kwamba hata kama Emma amenidharau, lakini
bado mtu kama wewe unaniona wa thamani. Ilinisaidia sana.”
“Hata mimi umenisaidia
sana jinsi ulivyokuja na mimi kwenye harusi. Nimeona hata jinsi baba
alivyozungumza na mimi safari hii imekua kwa heshima. Imekua kama aliyekuwa akinitaarifu
kinachoendelea bila ule ukali na uchungu kuona nimemuangusha, na kushindwa hata
kunitizama. Nakushukuru Brina.” “Na mimi nimepata wakati mzuri, Jack.
Nilikumiss mpenzi wangu. Mwenzio nilijua nimeshakupoteza huko kwa Phina!”
“Tafadhali nisamehe Sabrina. Nisamehe.”
“Wewe niambie kile unachotaka nifanye.
Nitafanya tu.” “Usiende Singida. Nimejiambia hata kama nitapoteza hii kazi,
nitatafuta kazi hapahapa Dar, tutaishi tu. Au unaogopa?” “Hata kidogo Jack. Mimi
tena! Nitakuwa muongo eti kwa hapa tulipo ndio nijidai eti naogopa maisha!
Nimetoka pabaya sana, na wewe unanijua. Hapa nilipo ni bora mno. Hata kama
tutashuka wakichukua hayo majukumu ya Unaibu waziri, lakini najua hatutashindwa
maisha.”
“Halafu acha nikusaidie
jambo. Hapo ulipo sasahivi, acha kufikiria mambo mengii ukijiogopesha. Ushafika
mwisho wa baya zaidi. Kufukuzwa kazi.” “Hilo wala halikuwa baya la mwisho,
Brina. Baya langu la mwisho ni wewe. Kazi hainisumbui hata kidogo. Nimesoma
mimi Sabrina, eti! Halafu nimeshakuwa na uzoefu wa kazi. Siwezi kukosa kazi.
Wala siogopi ila nasikitika tu, maana tulifika mbali haswa! Nachukia kuanza
upya! Tena nikiwa nimeshajiingiza doa ambalo mtu anaweza kulitumia hata kisiasa
kuwaambia watu wasinichague kwa sababu hiyo, kutumia mali ya umma vibaya
nikirubuni wanawake!” “Naomba tulale Jack. Acha mengine yajijibu yenyewe. Kuna
garama ya kulipa, hiyo huwezi kukwepa. Jiandae tu. Ni kwa namna na jinsi gani, muda
utajibu hayo. Sasa hivi acha tulale, mwenzio nina kachanga. Sasahivi ataamka
anataka kunyonya. Acha nipumzike kidogo.”
“Nashukuru Brina. Asante
kukubali kusimama na mimi.” “Sasa wewe ulifikiri nitakukimbia?” “Sijui!”
“Nilikwambia naogopa utaniua kwa magonjwa. Sasa ungeniua kwa magonjwa vipi kama
nilikuwa na mpango wa kukuacha? Ni kwa kuwa sikuwa na uhakika na wewe Jack,
ndio maana nilikuwa nikijiandaa hata kwa binti zangu. Lakini mimi sijui
kumkimbia mtu wakati wa matatizo, mpaka ungenifukuza mwenyewe kama alivyofanya
Tino na Emma. Ila ni kweli nilikuwa sijui itakuaje kwenye aina ile ya ndoa! Na
mtoto! Ndio maana nikaona ni bora niende Singida, nikupishe ufikirie.” “Wewe
siwezi kukuacha hata iweje.” Sabrina akanyamaza. Wakalala.
Jumapili.
A |
lipoamka na kuweka mambo sawa, akaanza kupiga
simu. Akaanza kwa Joy. “Bi mdogo hujambo?” “Njooni basi
kwangu leo kwa chakula cha jioni. Mkija mnakuta kipo tayari mnakula ili muwahi
kuondoka kwa ajili ya kuwahi usingizi wa Claire.” Joy akaanza kucheka. “Shida yangu ni shem, Joy. Najua nikimuomba yeye peke yake
ndio aje sitakuwa nikimtendea haki. Nilimsikia jana akimwambia baba, leo
anataka kupumzima tu nyumbani na familia, hatoki.” Joy akabaki akifikiria.
“Mbona unapatwa uzito?” “Kwa kuwa leo tulipanga
tusitoke kabisa, hapa bado tupo kitandani.” Sabrina akafikiria kwa
haraka, akasema basi niruhusu mimi nije nizungumze naye hapohapo kwako. “Hapo nitakupenda. Nilishaanza kujisikia vibaya kukukatalia.”
“Usijali. Wewe wangu. Muda gani mzuri ataweza kupokea wageni? Nitakuja peke
yangu wala siji na timu yangu.” “Kama ni hivyo kuanzia saa 10 sio mbaya.”
Akamuaga Joy na kuangalia muda. Akajua mzee Msindai atakuwa ameshaamka.
~~~~~~~~~~~~~~
Akampigia na kupokea kwa
haraka tu. Akasalimia. Akamuuliza habari za watoto, akamjibu. “Leo mnakwenda ibada ya saa ngapi?” “Kama kawaida yangu,
mama. Ulitakaje?” “Basi nimepatia. Hapa naandaa timu yangu yote, leo tutakuja
kuabudu huko na nyinyi. Ila shida yangu baada ya hapo nataka kuzungumza na wewe
pamoja na wifi Jacinta, najua shem alisema leo hatakuja kanisani naona yeye
nitamfuata nyumbani nikazungumze naye. Sitachukua muda wenu mrefu. Ni mazungumzo
mafupi tu.” “Ni kweli najua Jacinta atakuja kanisani, ila Junior alisema leo
hawatakuja. Ila ili haya mazungumzo yawe mazuri, tukitoka twende tukale sehemu.
Wajukuu wacheze wakati sisi tukizungumza.” Hilo likakaa sawa.
Kitu ambacho hakujua
Sabrina, alitengeneza mazingira ambayo Jacinta na baba yake walikuwa hawajui ni
jinsi gani kuyafanya yawe hivyo. Angalau familia yao ionekane pamoja.
~~~~~~~~~~~~~~
Hapohapo mzee Msindai
akampigia Junior. “Naomba kwa leo tu, nikuombe ubadili mipango
yako. Najua ungetamani kupumzika, lakini hili ni la muhimu. Sabrina, yeye
mwenyewe amenipigia simu akiomba akutane na mimi pamoja na Jacinta. Lakini wewe
alipanga kukufuata nyumbani. Nilipomuomba tutoke kwa chakula baada ya ibada,
anaonekana amelifurahia hilo. Nilitaka angalau tuwe pamoja wote kujaribu
kuponya kulikoharibika.” Junior akaelewa kuwa angalau waonekane kama
familia moja ili hata kama shutuma mbaya zimesambaa, basi jamii ione maisha yao
yanaendelea kama kawaida.
“Ametoka
kuzungumza na Joy, ila akampa mipango yetu ya leo. Hatukupanga kutoka baba.
Nimekuwa na mambo mengi, sijatulia na familia yangu, ndio leo nilitaka kupata
nao muda.” “Inaeleweka kabisa. Basi nikuache upumzike.” Mzee Msindai akakata
simu.
~~~~~~~~~~~~~~
Sabrina na Jack
walikwenda kanisani ambako anasali mzee Msindai, mkewe, Jena, pamoja na Jacinta.
Ila mama Msindai hakuwepo wala Jena. Ni Jacinta na baba yake tu. Wakaungana nao
hapo kanisani na familia ya Jack. Baada ya ibada ndipo wakaenda kula ambako
walikutana na familia ya Junior. Hata iweje, Junior hawezi kumkatalia jambo
baba yake. Japokuwa hawakwenda kanisani, lakini waliwakuta sehemu ya chakula. Wakaunganisha
meza, wakaa.
Yalikuwepo mazungumzo ya
kawaida tu tena Sabrina aligundua ni mazito kama kila mtu anatafuta chakuongea wakati
wakisubiria chakula. Sabrina akamuomba Jack kwa kumnong’oneza kuwa, aende na
watoto upande wa baharini wachezee maji wakati wakisubiria chakula. Jack
akashangaa kidogo. Kwa nini yeye ndio aondolewe hapo! Ila akatii, hata hivyo
kuwa katikati yao ni kitu ambacho ilishakuwa ni kama adhabu. Aliogopa watu wa
nyumbani kwao kupita kiasi.
~~~~~~~~~~~~~~
Walipojikuta peke yao
Sabrina akaanza. “Samahani baba yangu, imekua kama nimewaitisha kikao bila
idhini yako.” “Usiwe na wasiwasi. Kwanza ni kama hiki kikao mimi ndiye niliyeitisha
ili kukusikiliza. Karibu.” “Nashukuru.” Mapigo ya moyo yakaanza kwenda kasi
baada ya kujikuta watu wazima hao na nyadhifa zao wakimsikiliza yeye. Akacheka
kidogo kwa wasiwasi kujituliza. “Ongea mama Msindai, tunakusikiliza. Usiwe na
wasiwasi.” Jacinta akamtia moyo, angalau wote wakacheka.
“Labda nianze kwa kuomba
msamaha kwa niaba ya Jack.” Wote wakashangaa, hawakutegemea. “Jack amekosa.
Amekosa sana na ametushangaza sisi wote na kuumiza familia. Lakini baba, shem
na wifi yangu, Jack anajutia sana. Ana wakati mgumu ambao tusipomsaidia, ataharibikiwa
kabisa. Ameingiwa hofu yakupita kiasi. Nafikiri ni kwa kuwa Jack si mkosaji.”
Wote kimya. “Najua nyinyi mnamjua Jack, lakini mimi namfahamu Jackson kwa
mahusiano ambayo nyinyi hamtakaa mkamfahamu. Na hiyo ni tokea chuoni. Ukweli
alichokifanya Jack si kawaida yake hata kidogo. Sasa hivi yupo kama alivyo kwa
sababu si mzoefu wa hiki alichokifanya, na nafikiri shetani alipata mwanya
hapo, akaona atumie huo mwanya kumuangamiza Jack na kutuvuruga.” Sabrina
akaendelea. Wote kimya wakimsikiliza.
“Tulipokuwa chuoni,
Jackson alikuwa akililiwa na kupiganiwa na wasichana wazuri sana zaidi ya
Phina. Mchana na usiku walikuwa wakimtaka. Na walikuwa tayari kulala naye
kabisa. Lakini Jack alikuwa na msimamo katika hilo mpaka akampata Phina, na
kuanza naye mahusiano. Akatulia na Phina tu. Na hilo ndilo lililokuwa
likimtofautisha Jack na wanaume wengi pale chuoni ila zaidi yeye kwa kuwa
alikuwa ametokea kwenye familia yenu hii. Jina kubwa. Pesa na usafiri mzuri
ambao pia ulimtofautisha na kila mtu pale chuoni, lakini Jackson akabaki akijiheshimu,
hajajichafua kwa mambo ya wanawake. Hata alipokuwa na Phina, mpaka mimi
namaliza chuo, sikuwahi kumsikia amefanya alichokifanya. Alitulia na Phina tu
japo wanawake wengine waliendelea kumjaribu. Si kwa kuhisi ni kwa kusikia wasichana
wa pale chuoni wenyewe walivyokuwa wakimpangia mbinu mbalimbali za jinsi ya
kumtega Jackson Msindai, lakini walishindwa.” Sabrina akaendelea.
“Jackson sio muhuni, ni
muadilifu. Hata Ibra anajua hilo sema amepanga kumchafua tu. Na hata Phina
mwenyewe anamjua Jackson si mtu anafanya alichokifanya kwake kwa sababu hata
alipokuwa na yeye, mimi nilikuwepo
karibu na Jack akinisaidia kwa hali na mali, na kila mtu alijua kama Jack
ananipenda mimi, lakini baba, mimi ni shahidi wa Jack. Japokuwa alinipenda sana,
nikarudi kwake, Jackson hajawahi kumkosea Phina na wengi walitegemea kwamba
kile ndio kipindi pengine Jackson anaweza kuendesha mahusiano ya aina mbili au kumsaliti Phina. Lakini hakufanya hivyo.”
“Na Singida hivyohivyo.
Alikuwa na Pam, mimi nikiishi naye nyumba moja, lakini hakuwahi hata kukosea
kunijaribisha kimapenzi japo nilionekana nipo huru. Jackson hajawahi kuharibu
hata kwa bahati mbaya huko Singida. Alikuwa na mwanamke mmoja tu, Pam. Na hiyo
si kwa kuambiwa na Jack, ni kwa sifa nilizozikuta Chamani. Jack hajui, wala hajawahi
kufanya hiki alichokifanya. Ndio maana mimi nilipaniki na mimi nikakosea,
nikijua ameamua kurudiana na Phina na kuanzisha familia ingine, ndio maana
nilikuwa radhi kuondoka kurudi Singida ili kumpa nafasi yeye binafsi na mimi
kujiponya nafsi yangu. Nisishuhudie kuwa mwanamke wa kwanza kuachwa na Jackson
Msindai katikati ya mahusiano. Najua ni ubinafsi, nilikosea niliyoyafanya,
naomba msamaha.” “Pole sana mama.” “Nashukuru baba. Ila.” Akamgeukia Junior.
“Nakusihi shem msamehe
Jack. Huko kunyamaza, ni adhabu inayomuumiza kupita kiasi.” “Kama naweza kujibu
katika hili.” “Karibu shem.” “Asante Sabrina. Mimi nimejifunza kutoka kwa baba,
na imefanyika kuwa tabia yangu. Kama sina kitu sahihi chakusema, au kama sijui
kitu, siwezi kusema, ni bora kunyamaza. Na baba nilimwambia, kwa mara ya
kwanza, sijui nizungumze nini na Jack.
Pengine bado nipo kwenye mshituko! Sijui! Lakini nimekosa kitu chakuzungumza
naye kabisa. Na ukumbuke na mimi nina kijana mkubwa tu Sabrina. Anazungukwa na
jamii hiihiii. Ni kiasi cha muda tu, atakuja kujua. Muulize baba huyu kama
sikumpigia simu kumuomba ushauri nizungumze vipi na CJ endapo atasikia na
kutaka kujua ni nini kilitokea kwa anko wake! Kwa hiyo nipo kwenye wakati ambao
na mimi sijui chakusema!” Sabrina akatulia kidogo. Pakatulia.
“Pengine nikuombe shem,
wifi na baba, mumsikilize.” Kimya. “Tafadhalini msikilizeni tu. Na yeye
msikie upande wake, pengine itamsaidia yeye na nyinyi kujua mumsaidiaje. Nyinyi
ndio watu muhimu sana kwa Jack. Nimeishi naye, nimemuona. Anaweza asiwaambie,
lakini Shem na wifi, Jack anawaangalia na kuwaheshimu sana. Kipimo chake cha
ukamilifu kwenye mambo yake ni nyinyi. Ndoto za Jack sio kuwa kitu kingine ila
kuwa kama wewe, shem. Anajua amekosa sana. Na mimi najua amekosa na ameniumiza,
lakini naombeni mumsamehe mume wangu. Mtizameni kama zamani. Naomba mumfungulie
mlango wa mazungumzo. Najua mpo busy, lakini hii itamsaidia.” Sabrina
akaendelea kumbembelezea mumewe.
“Jack ana majukumu mazito
ambayo hajawahi kuharibu. Ni mchapa kazi tokea tupo Singida au niseme chuo.
Ukimpa jukumu yule, hajui kuharibu. Nahofia shetani asije akaendelea kujipati
utukufu katika hili ambalo wengi wanamuangalia. Nimeweza kumtizama na
kuzungumza naye kwa kumpa muda aongee, yupo kwenye hali mbaya. Kichwa chake
hakipo sawa. Tusipo msaidia sisi sasahivi, Jack ataharibu na kazini. Amejawa
hofu na wasiwasi kupita kiasi. Kwa kichwa kama kile hakiwezi kufanya kazi ngumu
kama anazozifanya, akafanikiwa.”
“Labda mimi nikuulize swali Sabrina. Mumeo amekwambia kinachoendelea sasahivi? Nikimaanisha unajua kinachoendelea hata asubuhi hii?” “Najua wifi.” Hilo jibu likawashangaza na Sabrina akawaona kama ambao hawamsadiki kama anajua kwa undani huo. “Naweza nisiwe na taarifa kamili, lakini imebidi kuanza kumfuatilia Phina huko Istagram. Amefungua akaunti mpya ambayo ametangaza kuwa hiyo inalindwa kitaalamu hakuna mtu anaweza kumfutia tena vitu vyake. Asubuhi hii amepost tena huko Ista na nimesoma gazeti lililoweza kurusha malalamiko yake yeye kama mtoto wa kike akigandamizwa kwenye jamii. Nimeona na post zake zote na jinsi watu wanavyomuunga mkono katika malalamiko yake. Nimeona wifi yangu. Nimesoma na safari hii ninafuatilia kwa karibu sana.” Bado wakahisi anamtetea Jack akiwa hajapata lalamiko jipya aliloazisha Phina huko mtandaoni, analolisimamia na kupatwa uungwaji mkono zaidi wakimchafua Jack, ambalo hilo ndilo limeumiza zaidi familia yake, zaidi mzee Msindai.
.~~~~~~~~~~~~~~
Ni Nini Kitaendelea?
0 Comments:
Post a Comment