Akamuona
anatuma jumbe kadhaa. Akatulia. “Willy?” Akamuita taratibu. “Hivi uliniambia
utakwenda kwenye Pikiniki?” “Sina uhakika kwenda huko kisiwani Pendo. Sioni
kama kutakuwa salama sana huko mbali na nchi kavu, halafu vijana wote walevi na
wavuta bangi watakuwepo huko! Nahisi itakuwa fujo tupu.” “Nilisikia waziri wa
starehe wa pale chuoni akisema kutakuwa na ulinzi mkali, na akaonya hata
wanaopanga kwenda kulipizana kisasi huko haitakuwa sehemu yake. Wamesema
wamelipia ulinzi mzuri. Nahisi kutakuwa salama.” Pendo akaweka ushawishi.
“Lakini nivizuri kusikiliza nafsi yako kile inachokwambia. Kweli itakuwa mbali
na nchi kavu, hutaki kwenda halafu ukajuta.” Pendo akarudisha macho kwenye
simu. Akamuona anaandika tena.
“Ulisema
utakuwa na kina Eva?” “Ndio nilikuwa na chat naye hapa. Mpenzi wake ameshanunua
tiketi zetu na za marafiki zake pia. Wanafahamiana vizuri na yule waziri wa
starehe wa pale chuoni kwetu. Eva alikuwa akiniambia tutakuwa wengi, nisiogope.
Maana na mimi niliogopa kwenda huko Mbudya. Niliona ni mbali, halafu wanakwenda
wengi mpaka wanafunzi wa Mlimani! Lakini ndio Eva ananiambia hapa wamehakikisha
itakuwa salama. Twende, tutakuwa wote Willy na mimi nitakununulia tiketi.”
Pendo akaongea kwa kubembeleza. Willy akacheka. “Au kina Kyande hawatakuwepo?”
“Naona Kyande ndio alikuwa wakwanza kununua tiketi! Anaimba hiyo safari mpaka
kero!” Wakacheka. “Nitaangalia.” Akajibu Willy. Pendo akaelewa anamipango yake
mingine. Na yeye akawa mstaarabu tu. “Sawa.” Akaitika na kurudisha mawazo
kwenye simu yake.
Pakatulia
kwa muda, kila mmoja akifanya lake. Lakini akili na mawazo ya Willy bado
yalikuwa kwa Chris na huyo Pendo. “Kesho ulitaka tuondoke hapa saa ngapi?”
Pendo akaweka simu chini, akafikiria kidogo. “Nafikiria mimi niwahi kidogo ili
nipate muda wakujitayarisha. Nakutana na Chris kwa chakula cha mchana, na
nywele zimeloa! Hazifai.” Willy akabaki akimtizama, Pendo akifikiria. “Nafikiri
niondoke kama kwenye saa tatu asubuhi. Nipitie saluni kwanza ndipo niende chuo.
Au itakuwa mapema sana nitakuamsha?” “Haina shida. Huo sio muda mbaya hata
kwangu. Naweza kusogea chuo nikawepo pale nikisubiria mtihani wangu wa mwisho.”
“Lakini mimi sitaelekea chuo kwanza Willy! Nitakwenda saluni kwanza, ndipo
niende chuo.” Willy akabaki kama hajui tena chakufanya na huyo mrembo.
“Hayo
yote ni maandalizi ya kukutana na Chris tu?” Pendo akababaika kidogo. “Huwa
Chris anapenda kwenda kula sehemu za hadhi ya juu, Willy. Sitaki nitokee kama
ambaye sijitambui.” Willy akanyamaza. “Nafanya kwa ajili yangu pia. Mvua
imeharibu nywele zangu, halafu usiku tutatoka wasichana wote wa darasani kwetu.
Tuliamua kwenda kupongezana kwa kumaliza mwaka pamoja. Hatujui nani atarudi
nani ataendelea. Tumeona tukafunge mwaka wa kwanza pamoja.” “Kwa maana nyingine
unayotaka kuniambia kesho ukiamka hapa hutahitaji usafiri wangu?” “Nashukuru,
lakini nitatumia daladala au hata taksii mpaka Kinondoni. Kuna dada huwa
anatutengeneza nywele vizuri.” “Sawa.” Willy akajibu, Pendo akafikiria kidogo
na kuendelea kuandika huku akiperuzi simu yake, Willy akimtizama tu.
Baada ya muda, akamuita tena.
“Willy, nataka kulala.” “Umeshachoka?” Pendo akacheka taratibu. “Nimezunguka
sana leo, karibu jua na joto lote leo limeniishia mwilini.” Pendo akasimama.
“Nikupe taulo dogo? Naona nywele bado zinatoa maji. Umelowa.” “Nitashukuru.
Nahisi nitalala na taulo kichwani.” “Njoo huku chumbani.” Chumba kilikuwa na
kitanda kikubwa tu, kimetandikwa vizuri. Pasafi, pakawaida. Akamtolea taulo.
“Geuka.” Pendo hakujua anataka afanye nini, akageuka. Akashangaa anamfuta
mgongoni na kwenye nywele. Pendo akacheka. “Una upendo Willy! Asante.” Willy
akacheka. “Kweli. Unakumbuka siku ile nilipoangushwa na Wema?” Willy akabaki akimsikiliza.
“Ulinifuata chumbani na kuniuliza ninaendeleaje! Unakumbuka?” “Nakumbuka hata
hukunikaribisha ndani!” Pendo akashituka sana na kugeuka.
“Nilikuwa nimetoka kuoga
Willy!” “Na ulikuwa na haraka yakujiandaa ili kumuwahi Chris.” Pendo akabaki
ameduaa. “Uliniambia hutanikaribisha ndani kwa kuwa unajiandaa, Chris anakuja
kukuchukua.” “Ukisema hivyo inasikika vibaya bwana!” Akalalamika Pendo, Willy
akacheka taratibu. “Lakini ndivyo ulivyoniambia.” “Si ulinielewa?” Pendo
akauliza kwa upendo. “Si ndio maana niliondoka kwa haraka!” Pendo akafikiria,
akashindwa azungumze nini tena juu ya hilo. Akataka kukaa. “Bado una maji. Njoo
kwanza.” “Mwenzio nimejisikia vibaya!” “Kwa nini tena?” Willy akauliza huku
akicheka. “Naona mimi nilikufukuza kwangu, ona jinsi wewe ulivyonikarimu
nyumbani kwako!” Willy akacheka sana.
“Acha
kufananisha kihivyo!” “Kweli Willy! Naomba nisamehe bwana. Nilikuwa tayari na
miahadi na Chris, na jambo jingine Chris hapendi kuchelewa. Akija, anataka
akikupigia kuwa amefika, na wewe utoke. Sikutaka tufike sehemu tuliyokuwa
tunakwenda tukiwa tumenuniana.” “Mimi naelewa Pendo. Wala usiwe na wasiwasi.
Geuka.” Pendo akageuka, Willy akaendelea kumkausha kichwa. “Hivyo
unavyonifanya, nitalala nikiwa nimesimama.” Willy akacheka. “Acha nikutolee
nguo nyingine yakubadili.” Akamtolea tisheti nyingine ndogo, akavaa palepale
Willy aligeuka pembeni tu. “Nimemaliza. Asante.” “Basi nipe hiyo mbichi.”
Akamuongezea blangeti jingine na taulo jingine Willy akatoka.
Baada
ya muda akasikia mlango unagongwa. “Karibu Willy.” Akawa amejifunga taulo
kichwani. “Unapendeza na kuvutia na kila kitu Pendo!” Pendo akacheka sana. “Kwa
hiyo hili taulo kichwani limenipendeza?” “Sana tu! Unautulivu na sura nzuri
sana. Kila kitu chako ni kizuri.” Pendo akacheka na kufikiria kidogo kisha
akamwimbia, “Asante Willy. Hata wewe ni mzuri.” Willy alicheka mpaka akainama.
“Acha utundu Pendo!” “Kwani hujui! Mpaka wanaume wenzio wanakusifia!”
“Haiwezekani!” Willy akazidi kucheka. Pendo akapanda kitandani. Radi ikapiga na
kufuatiwa na ngurumo. Pendo akakaa kwa haraka. “Usiniambie huwa unaogopa radi?”
Pendo akaanza kucheka. “Muulize Eva. Zikianza usiku, asubuhi anaamka nipo
kitandani kwake.” Wakacheka.
“Sipendi
radi, eti naona zitaingia ndani na kunipasua nikiwa peke yangu hapo kitandani.”
“Mkiwa wawili?” “Sina shida. Tena nyumbani ndio wanajua. Siku za mvua nilazima
nitalala na Nancy kama yupo nyumbani. Akiwa hayupo, nahamia chumbani kwa
msichana wa kazi.” “Haiwezekani Pendo!” “Hali ni mbaya. Mimi naomba tu uje
usomee hapa ndio nitalala. Lasivyo nakuja kulala pale kwenye kochi.” Willy
akazidi kucheka. “Tulale wote kwenye kochi?” “Kabisa Willy. Katika hilo wala
sitafikiria mara mbili. Lasivyo wote tutakesha hapa.” “Basi ngoja nikachukue
vitabu vyangu. Sasa utalala kweli na mwanga wa taa?” “Heri mwanga wa taa kuliko
radi.” Willy akacheka na kutoka akiwa na furaha vilivyo. Analazimishiwa kulala
kitanda kimoja na Pendo! Mungu ampe nini!
Wakati
anakusanya vitu vyake ili arudi chumbani alipokuwa amemuacha, akashitukia Pendo
ametoka kwa haraka. “Pendo!” “Naona hauji na radi zinaendelea!” Willy akazidi
kucheka. “Ndio hali mbaya hivyo!?” “Hapa nitakufuata mpaka chooni. Wewe niambie
nikusaidie nini, twende wote ndani.” Willy akaendelea kucheka huku akikusanya
vitu vyake. “Nataka kuzima taa.” “Wewe zima tu, mimi nakusubiria hapahapa.”
“Gizani!” “Giza ni bora kuliko hizo radi huko chumbani. Wewe twende tu.” Willy
akajua hali ni mbaya. Akawasha simu yake, akazima taa zote wakaongozana
chumbani huku wakicheka.
“Sasa
utanionea huruma hii hali inikute nipo kwa Chris au tupo safarini!” “Kwa nini?”
Willy akauliza taratibu. “Sijui nikwambia
nini juu ya Chris! Sijui ni mtu wa namna gani yule kiumbe! Anabadilika
badilika kama kinyonga! Ni ngumu kumtabiri. Halafu kama hivi ulivyonifunika
hapa vizuri, Chris huwa hawezi. Hawezi mambo ya kushikana shikana. Anasema yeye
hakulelewa kimayai, sijui mwenyewe anajielezea vipi! Lakini unaweza kukuta mpo
naye, mvua inanyesha na kuna radi. Anajua wazi mwenzie naogopa, kama
amekasirika, anaweza asikujali kabisa. Tena kama mpo hotelini, anaweza hata
kukuta anatoka. Anakwambia anafuata kitu upande wa baa. Sasa nikiwaga nyumbani
kwake, ninakuwa na kazi yakumfuata kila mahali, mpaka najikuta naamka kwenye
kochi, kumbe yeye aliniacha hapo kwenye kochi nilipomfuata, akarudi kitandani.”
“Kwa nini hakuamshi sasa ili mrudi naye kitandani!?” Willy akashangaa sana.
Pendo akafikiria.
“Aaah!
Sijui bwana. Sijui yukoje Chris! Lakini akiwa mwema, utafurahia.” Willy
akapanda kitandani na yeye. “Kama leo amekuwa mwema mpaka kesho umekubali
kutoka naye?” Willy akauliza kwa wivu kidogo, Pendo naye akacheka kidogo na
kunyamaza. Pakatulia. Akamsikia Willy anaanza kuperuzi vitabu vyake,
akajisogeza karibu naye, akalala.
Ijumaa.
P |
endo
aliamka akamkuta Willy akijisomea. “Ulilala vizuri?” Pendo akacheka na
kumgeukia. “Sana. Hata sijaota!” Wakacheka. Pendo akaangalia vitabu vya Willy
akakaa. “Nataka nioge, nitoke Willy.” “Bila kula!?” “Sitakula kwa kuwa najua
nitakula mlo mkubwa mchana. Mwenzio naogopa sana unene. Sili mara kwa mara.
Nina asili ya unene kweli! Nikijisahau tu, nakuwa kibonge. Na huwa sichelewi
kunenepa.” Willy akatabasamu tu akimtizama huyo Pendo anayeogopa unene. “Huyu
hata akiwa mnene au mwembamba atabaki akivutia hivihivi.” Akawaza Willy.
Pendo akatoka kitandani kuelekea bafuni. Akajisafi na kuvaa hukohuko nguo
ambazo alinunua bila kufua. Akatoka.
“Mbona
umetoka tofauti!” “Nanukia mitumba tu hapa. Hili gauni nililinunua jana.” “Umependeza.
Lakini naomba nikupeleke huko saluni.” Pendo akashangaa kidogo. “Usijali Willy!
Wewe endelea na kujitayarisha na mitihani!” “Nitaendelea kujisomea hata kwenye
gari wakati nakusubiria saluni ili turudi wote chuo.” Pendo akakaa. “Willy!”
“Sitaki kukuacha barabarani wakati nilikuahidi nitakufikisha chuoni. Usijali.
Nisubiri nijitayarishe, tutoke wote.” Ikamgusa sana Pendo. Akamsubiria.
Kweli
alimfikisha mpaka saluni. Kulikuwa na baa pembeni. Akamwambia atamsubiria hapo
akiwa anapata kifungua kinywa na kujisomea. Hapakuwa na watu wengi na bado
ilikuwa mapema tu. Pendo akashukuru na kuingia saluni. Alikausha tu nywele zake
alizokuwa ameshonea wiving ya rangi nyeusi tupu. Akamwambia aipige pasi tu, inyooke.
Akafanyiwa hivyo. Na rangi yake nyeupe, Pendo akapendeza sana. Akatoka kumfuata
Willy baa. Willy akatabasamu alipomuona. “Natamani hiyo bahati ya uwezo wa
kukupeleka sehemu yenye hadhi kwa chakula cha mchana ingekuwa yangu!” Pendo
akajisikia vibaya. “Lakini tupo wote na wewe hapa, na tumelala wote.”
“Hatujalala wote, ila tumelala pamoja.” Pendo akacheka na kuinama.
“Na
hapa hatupo kwa chakula, umenifuata tuondoke.” Pendo akafikiria kidogo.
“Nikwambie kitu Willy?” “Nakusikiliza.” “Nimekuwa na wakati mzuri sana pale
kwako. Wakati wakujaliwa kuliko ninavyokuwa na Chris kwenye mahoteli mazuri na
ya gharama. Kwa vyovyote vile, umenipa usiku mzuri. Nimefurahi.” Willy
akaridhika. “Kwa hiyo amani na furaha haipatikaniki kwenye vitu vya hadhi ila
kwa mtu mwenyewe. Umenijali vizuri. Umelala na mimi, upo hapa ukinisubiria, huo
ni upendo wa ajabu sana, sijapata kwa muda mrefu. Asante.” Ikamgusa Willy.
“Karibu.” Wakaangaliana na kucheka.
Wakati wapo njiani kuelekea chuo, Willy
akavunja ukimya. “Kwa hiyo leo na kesho utakuwa busy sana?” Pendo akacheka.
“Naamini hivyo. Eva ameniambia nijiandae haswa. Tutakula bata kwa mrija.” Willy
akacheka. “Unampenda sana Eva, eeh?” “Sana. Mbali na ule ukorofi wake, ni mtu
mzuri sana. Kwanza akiamua kukupenda, anakupenda haswa na ujue atasimama na
wewe katika kila hali. Nafikiri ndio maana mpenzi wake anampenda Eva.” Willy
akacheka na kumfikiria Eva. “Nimemuomba Kaka K aje anichukulie mizigo kesho
asubuhi. Ameniambia ataniambia muda atakao kuja. Kwa hiyo itabidi niwepo chuo
nikimsubiria.” “K ni nani?” “Kaka yetu mkubwa, anaitwa Kenton, halafu Nancy
ndio wakatikati kisha mimi mziwanda wao.” “Ndio maana unadeka Pendo!” Pendo
akacheka sana. “Wao ndio wananidekeza lakini mimi sinaga hata mpango!” Willy
akacheka sana. “Wewe hudeki?” “Sina mpango kabisa, lakini wao ndio wanataka
nideke.” Wakazidi kucheka.
Walipofika
karibu na chuo, Willy akamgeukia. “Sasa mimi nitakushusha getini, halafu
nakwenda kuegesha gari kwengine.” “Kwa nini huegeshi chuo wakati kunanafasi!?”
Pendo akashangaa kidogo. “Sipendi tu. Lakini wewe nitakusogeza mpaka getini, usijali.”
Pendo akajua ndio maana hakuwahi kumuona na usafiri. Hakutaka watu wajue kama
anausafiri. Hawakuwa mbali na hapo getini wakawa wameshafika. “Nakushukuru kwa
kila kitu Willy. Naamini hatutapotezana tena.” “Naamini hivyo.” Wakacheka
kidogo. “Mtihani mwema wa mwisho. Mungu akusaidie ufaulu sanaaa.” “Kwa hizo
baraka! Lazima nitafaulu tu.” Pendo akacheka na kushuka. Alipoondoka mbele ya
macho yake, ndipo Willy akakumbuka hakuomba namba ya simu. Akajilaumu sana.
Lakini akajiambia akitoka kwenye mtihani, Pendo atakuwa amerudi chuoni,
atamfuata tena chumbani kwake amuombe.
~~~~~~~~~~~~~~~~~
Willy
alibaki akisubiria mtihani mawazo kwa Pendo. Akakumbuka hiki na kile, akabaki
amekodolea macho anachotakiwa kusoma kabla ya mtihani. “Sasa hivi atakuwa
ameshafika kwa Chris wakipanga mipango ya safari.” Willy akawaza na kuumia
moyoni. Akabaki ametulia mpaka muda wa mtihani kukaribia, wenzake wakaanza
kuingia. “Kumbe umeshafika kaka!” Kyande akamsogelea. “Nipo hapa tokea saa saba
mchana. Vipi mtihani wa mwisho?” “Huu lazima nitengeneze msonge mwingine, kaka.
Nimekesha nao.” Wakazungumza kidogo akili za Willy zikarudi hapo, wakapitia mawili
matatu pamoja. Mtihani ukaanza. Willy akawa wa kwanza kumaliza. Hakuna
aliyeshangaa. Akatoka.
Moja
kwa moja chumbani kwa kina Pendo. Alimkuta msichana mwingine, akamwambia tokea
Pendo atoke, hajarudi. Akatamani kuuliza zaidi, lakini akashindwa. Moyo ukamuuma.
Akaangalia saa, ilikuwa saa 12 kasoro. “Chakula cha mchana gani hicho!
Itakuwa ameunganisha na kitu kingine.” Willy akazidi kujiumiza. Akarudi
kwenye gari yake. Akakaa mpaka kwenye saa moja usiku, akarudi tena. Safari hii
hata aliyemkuta mwanzo pale chumbani, hakumkuta. Aligonga na kugonga, kimya
zaidi akaona wasichana wanapita na vitaulo wakienda kuoga. Akaamua kuondoka tu.
“Pengine sasa hivi amelala kwa Chris! Mimi nahangaika tu.” Willy akawaza
na kuamua kurudi kwake. Akakumbuka mazungumzo kati ya Pendo na Chris, akajua
Chris amefanikiwa kumshinda.
Usiku
huo ukawa mgumu sana kwa Willy. Akatamani kurudi kwa Pendo kesho yake asubuhi,
lakini akakumbuka kaka yake atakwenda hapo chuoni kuchukua mizigo yake. “Labda
ndio ili awe huru kusafiri na Chris.” Willy akakumbuka habari za safari
zao, akakumbuka kuambiwa wanafikia kwenye mahoteli makubwa. Akaona ni heri tu
amuache aende. Hatamuweza Pendo.
Jumamosi ya
Pikiniki.
W |
illy aliamka
asubuhi hiyo akiwa mnyonge. Lakini akakataa siku yake kuisha hivyo. Akakimbilia
kwenye mazoezi. Akafanya hili na lile lakini moyo ukakataa. Mawazo kwa Pendo.
Mwishoe ikabidi ampigie simu Kyande kumtaarifu na yeye atakuwepo huko kwenye Pikiniki.
Alijua ndio njia pekee yakumuona Pendo. Akajiandaa na yeye vizuri ili kuvutia
zaidi. Akajua mida ya saa kumi wanachuo watakuwa wengi wakitaka kuvuka kwenda
huko kisiwani Mbudya. Akaona asubiri kwanza. Ilipofika mida ya saa 12 jioni na
yeye akawa amefika hapo wakakutana na kina Kyande kama walivyopanga. Wakakuta
kuna boti ambayo unaweza kukodi kwa bei ya juu zaidi, na mnakwenda wachache sio
wengi. Wakaona wakodi boti yao. Wakachangishana watu wa darasani kwao waliokuwa
karibu, wakaondoka kuelekea kisiwani. Mawazo ya Willy yakiwa kwa Pendo.
Walikuta
kumejaa na mziki ukisikika kwa sauti, kila mtu na mtu wake. Wengine
walishalewa. Lakini kweli kulikuwa na ulinzi mkali sana mpaka mbwa wa FFU
walikuwepo hapo. Hilo likampa tumaini Willy. Sasa wapi pakumpata Pendo! Hiyo
ndio ikabakia agenda. Kyande na wanzake wakakimbilia upande wa vinywaji, baa.
Willy akawaambia watawasiliana, yeye anazungukia kisiwa. Alizunguka Willy
karibia nusu saa ndipo akamuona Eva amekaa katikati ya watu, akajua na Pendo
atakuwepo hapo. Akasogelea lile kundi, na kweli akamuona Pendo amekaa katikati
yao lakini ametulia sana.
Akamsogelea
na kumgusa. Pendo akageuka. “Willy!” Akasimama kwa haraka. Willy akashangaa
amemkumbatia. Akacheka na yeye akamkumbatia vizuri. Wote wakawageukia. “Ndio
mmekuja au mlikuwa hapa muda mrefu?” “Hatujafika muda mrefu. Nimewaacha kina
Kyande upande ule wa baa. Nimekuja kukusalimia.” Pendo akacheka kinyonge. Willy
akamwangalia akajua kuna jambo halipo sawa. “Unataka tutembee kidogo?” Willy akauliza
kwa upendo, Pendo akakubali. Akamsogelea Eva na kumuaga. Wakaondoka.
Willy & Pendo
Kisiwani.
“Umependeza
sana Pendo. Lakini huonekani na furaha! Kuna nini?” “Nipo sawa Willy. Na wewe
umependeza. Na nimefurahi umekuja.” Willy akatafuta sehemu pembeni ya fujo.
“Itakuwa sawa kwako tukikaa hapa chini?”
“Hujaja na mtu wako?” “Unamaanisha msichana?” Pendo akacheka. “Willy!” “Ndivyo
ulivyomaanisha. Si ndivyo?” “Ndiyo.” Pendo akakubali kwa aibu na cheko.
“Hapana. Kwani nilikwambia nipo kwenye mahusiano!?” Willy akauliza kama anayejaribu
kuvuta kumbukumbu. “Hapana.” “Oooh! Nilifikiri nimeanza kuongopa!” Willy akavua
koti lake, akakaa chini akatandika koti pembeni yake ili Pendo akae. Akakaa
huku mguu mmoja amekunja goti. “Kaa hapa ili usichafue nguo yako.” “Asante.”
Pendo akavuta koti, akaliweka vizuri na kukaa. Willy akamuona anapenyeza miguu
yake yote miwili chini ya ule mguu wake aliokuwa amekunja goti, kisha kichwa
akakiegemeza kwenye goti la Willy. Hilo lilimfurahisha sana Willy. Akashangilia
moyoni. “Mungu anipe nini mimi!” Akawaza Willy na kuweka mkono mgongoni
kwake Pendo. Akatulia hapo kama kitoto cha paka. Watu wengine walikuwa wamekaa
mbele na pembeni yao makundi makundi hakuna mwenye habari na mtu.
“Za
tokea jana tulipoachana?” Willy akauliza kwa kujali huku akimwangalia Pendo
aliyekuwa ametulia gotini kwake. “Nzuri. Vipi mtihani?” “Sio mbaya. Nilirudi
kukutizama chumbani kwenu, nikaambiwa bado hujarudi.” Pendo akamgeukia vizuri
akiwa kama na mshangao kidogo. “Nilisahau kukuomba namba ya simu, Pendo.
Nilikuja kuomba namba. Nikarudi mara mbili hukuwa umerudi, nikajua bado upo
kwenye lunch.” Pendo akatulia kidogo kama anayefikiria. “Safari lini?”
Willy akaendelea kudodosa kutaka kujua kama bado Chris yupo kwenye picha. “Na
nani!?” Pendo akauliza. “Si safari yako na Chris!” “Nilifuata ushauri wako, nikaona
sio sawa kuendelea kumdanganya wakati ananiumiza. Nikamwambia ukweli, japo
amekiri hakukusudia kuniumiza. Akaahidi kujirekebisha.” Willy akaanza kukosa
raha.
“Kwa
hiyo mmetengeneza?” “Hapana Willy! Nimemwambia hakuwa akikosea kwa bahati
mbaya. Ndivyo alivyo, na hivyo alivyo, sina furaha yakuwa naye. Alikasirika
kidogo, lakini nashukuru alikubali kunipa vitu vyangu.” “Oooh, ndio maana
ulichelewa kuridi, kumbe ilibidi kurudi nyumbani kwake ili uchukue vitu vyako!”
“Hapana Willy! Vitu anavyoninunulia Chris, huwa anasema ni vya palepale
nyumbani kwake na kwa ajili yake. Nitumie pale kwake na niwe naacha ili nisiwe
na kwenda na vitu vyangu.” “Sijaelewa Pendo!” “Ni ngumu kumuelewa Chris, ndio
maana niliona nisipoteze muda. Nimuache tu. Lakini kuna kijibegi nilikiachaga
kwake ndicho kilikuwa na vitu vyangu, nilimuomba aniletee jana, nikijua
sitarudi tena kwake.” Hapo Willy akafurahi.
Lakini
akaingiwa tena na wasiwasi wa wivu, ikabidi aulize. “Na vitu vyako vingine, kwa
hiyo itabidi kufuata wakati mwingine tena?” “Hakuna kitu kingine nimeacha kwa
Chris, Willy. Nilikwambia Chris ni mtu wa hadhi. Ni wa hadhi kweli kweli.
Huwezi kuingiza hovyo hovyo tu vitu vyako nyumbani kwa Chris. Hata mswaki tu! Huwezi kupeleka hii miswaki
ya kawaida nyumbani kwake ukakaa kwenye sinki lake. Hatumii tu kila mswaki.
Anatumia miswaki ambayo mwenyewe anasema inafaa kwa meno na imepitia uchunguzi
wa madaktari wa meno. Huo ni mfano tu. Kwa hiyo huwezi kubeba takataka yako
ukaingiza kwenye nyumba ya Chris. Ananunua chochote unachotaka, vinakuwa
vyakutumia nyumbani kwake siku ukienda kwake. Kwa maana nyingine hata magauni
aliyokuwa akininunulia, alikuwa akiyapeleka dry cleaner yeye mwenyewe.
Yakisafishwa, anarudisha nyumbani kwake. Ninayatumia kwa shuguli zake yeye, na kurudisha
kwake. Si yangu.” Willy akashangaa sana.
“Hiyo
sijawahi kuona!” Pendo akacheka kinyonge. “Ndio maana umekosa raha? Usijali
tutanua mengine.” Pendo akacheka na kumpiga kidogo. “Hapana bwana! Mimi najua
kuridhika na vyangu. Hata hivyo tokea mwanzoni nilijua si vyangu. Yeye mwenyewe
alikuwa akiniambia kila akininunulia kitu au akinipa pesa nikanunue kwa ajili
ya shuguli zake. Alihakikisha naelewa ni cha pale kwake.” “Haiwezekani Pendo!”
Pendo akacheka. “Wewe hujawahi kukutana na kiumbe kama Chris. Na ndio maana
nilimtuma tu vitu vyangu. Kwanza nilijua angetupa kwa haraka sana baada ya
kuachana naye na kuvikuta kwenye stoo yake. Angeona ni uchafu.” “Sasa
unajisikiaje?” “Mbali yakumisi safari za hapa na pale na kulala kwenye 5 stars
hotel, nina amani na furaha yakutokuwa karibu na yule mwanadamu. Anachosha!
Hujui ni wakati gani au kitu gani kitamfurahisha au kumuudhi! Hicho kipengele
nishamaliza. Sirudi huko tena.” Willy akafurahia, akacheka taratibu.
“Sasa
kwa nini huna raha? Nimekukuta katikati ya kundi la watu wanaocheka na stori
nyingi lakini wewe umenyongea!” Pendo akanyamaza. “Pendo?” “Jana tulirudishiwa
baadhi ya mitihani yetu Willy.” Hapo hapo Willy akaelewa. “Imekuaje?”
“Nimeshikwa hesabu. Sikufanya vizuri mtihani wa mwisho na hata wastani pia haukuwa
mzuri tokea mwanzo tunaanza chuo.” Akaanza kulia. “Nikiwa
nawenzangu tu, nafeli! Sasa sasahivi nipo peke yangu ndio nitaweza kweli! Eva
hajakamatwa somo hata moja, Willy! Nitafanyaje?” Pendo akalalamika
akilia. Mwishoe akainamia kwenye goti la Willy tena na kuendelea kulia. Willy
akamsogeza nywele pembeni, mpaka akaacha uwazi kwenye shingo, akainama hapo
nakumbusu shingoni kama mara tatu huku akimpapasa.
“Niangalie
mimi Pendo.” Pendo akalia tena kidogo, akamgeuzia uso uliojaa machozi akiwa
bado amemuegemea gotini. Willy akamfuta. “Nitahakikisha unarudia huo mtihani,
na unapita. Na hutakaa ukakamatwa tena somo jingine. Sawa?” “Kweli Willy?” “Mimi ndio nakuahidi. Tutasoma
wote. Utajiandaa vizuri. Ukitulia na kujiamini, utarudia na utafanya vizuri
kabisa. Wala usikose raha kwa ajili ya hiyo.” “Kwahiyo,
hiyo ni ahadi?” “Na ninakusudia kuisimamia, endapo utasimama na mimi.”
Pendo akaona hilo sharti lakusimama na Willy ni zuri sana. Alishampenda Willy.
Kuwa naye na kufaulu shule, ni bahati ambayo alijiambia haitakaa ikatokea tena.
Akamuona ameridhika akajifuta machozi mwenyewe.
“Nilishaogopa
Willy! Nashukuru. Eva ameshaondoa mizigo yake yote chuoni na leo harudi tena
pale anaondoka na mpenzi wake!” “Nikikuomba turudi kwangu utakubali?” Pendo
akamwangalia na kucheka, akageuka pembeni kama anayefikiria. “Sio lazima. Ni
ombi tu. Ila namba ya simu naomba sasa hivi. Sitaki kurudia kosa.” Pendo
akacheka wakati Willy anatoa simu mfukoni kwa mkono mmoja mwingine ukiendelea
kupita mgongoni kwake Pendo, taratibu. Akamkabidhi Pendo simu. “Nikuwekee jina
gani? Nisije nikaweka Pendo, kumbe kuna kina Pendo wengine humu ndani.”
“Niwekee namba, jina nitakuja kuweka mwenyewe.” Pendo akacheka na kuandika
namba yake hapo. Akajipigia. “Tayari nimekuwekea namba yangu bila jina na mimi
nimechukua namba yako.” Akamrudishia. “Nashukuru.” Pendo akafikiria akawa kama
amegutuka.
“Mbona
huweki jina langu sasa hivi? Unataka ukaweke jina baya nini?” Willy akacheka
sana. “Unafikiria tanaka kuweka jina gani?” Willy akauliza huku akiendelea
kucheka. “Pendo mbaya asiyenikaribisha kwake, ila mimi namkaribisha kwangu bila
kinyongo.” Willy akacheka sana. “Hilo ni jina tu?” “Mimi nakuhisi hivyo bwana! Sasa
kwa nini hutaki kuweka jina mbele yangu?” “Kwa nini usifikirie nakutafutia jina
zuri.” Pendo akacheka huku akifikiria. Akamwangalia. Bado Willy alikuwa
akimbembeleza kwa kumpapasa upande wa mgongoni, akiwa amemuinamia kwenye goti
la ule mguu aliokuwa ameunyanyua.
“Kama
jina gani sasa?” Pendo akauliza. “Soulmate.” Pendo akashituka akabaki akimwangalia.
“Baya?” Willy akamuuliza. “Maana yake ndiyo nzito, Willy!” “Ndivyo
ninavyojisikia.” Pendo akamwangalia kama ambaye hajamuelewa. “Sijakurupuka
Pendo. Ndivyo ninavyojisikia kwako tokea tunaanza chuo.” Pendo akakunja uso
akimshangaa. “Sikudanganyi. Nakumbuka kila siku tulizokuwa tukikutana hata kama
hukuwa ukiniona au kunisalimia. Nakumbuka kuanzia nguo ulizokuwa ukivaa mpaka
aina ya nywele.” “Willy!” Pendo akashangaa taratibu. “Ni kwa vile nilivyokuwa
nikijisikia kwako Pendo. Na unajua ni kwa nini nilihama pale hosteli za chuo?”
Pendo akabaki kimya. “Kwa jili yako ili kukuthibitishia kwa vitendo kuwa sipo
na Wema. Niliona vile ulivyoamini na jinsi watu walivyoubebea bango ule ukweli
ambao sio kweli kati yangu na Wema. Nikajua neno ‘sio kweli’ pekee,
lisingekutosha kuniamini.” Pendo akabaki hajui aseme nini.
“Halafu
nikaona na vile Chris amejaa kwenye picha, hata siwezi kukaribishwa maji!”
Pendo akacheka sana. “Unanifanya nizidi kujisikia vibaya bwana Willy! Ulikuja
muda mbaya.” “Kweli ulikuwa mbaya.” Pendo akazidi kucheka. “Nikikuomba msamaha
itasaidia?” “Sijui! Jaribu.” Pendo akacheka. “Pole na samahani Willy.” “Ukiwa
hivyo natamani kukubusu tu.” Pendo akacheka taratibu akainama. “Jana
nilishindwa kuomba kwa kuwa bado Chris alikuwa kwenye picha. Lakini leo si
ruksa?” Pendo akatulia. “Sitakuchezea wala kukuumiza Pendo. Nakupenda na sijaanza
leo. Mimi ni mwaminifu wala hutahitaji kuwinda simu yangu. Nakuhakikishia
utakuwa peke yako kwangu.” “Kweli Willy?” “Nipe nafasi uone. Huna hata haraka
ya kunikubali, nitasubiri.” “Mimi nataka kuwa peke yangu.” Pendo akaongea kwa
deko akimpapasa Willy vinyweleo vya mkono. Willy akacheka taratibu. “Na ndivyo
itakavyokuwa. Nakuahidi Pendo. Na sitakubadilikia.” “Na mimi huwa sio muhuni
Willy.” Willy akacheka tena. “Basi tutakuwa sisi wawili tu.” Pendo akaonyesha
kurudhika akiendelea kumpapasa Willy vinyweleo vya mkono. Pendo akakumbuka
ahadi hizo walizopeana siku hiyo kisiwani. Akatulia akimfikiria Willy. Miaka
yote hiyo hakuwahi kumbadilikia hata mara moja! Alimdekeza wakati wote, imekua kama
kufumba na kufumbua, sasa hivi wanazungumzia talaka! Roho ikazidi kumuuma
Pendo.
Mawazo
yakamrudisha tena siku ile walipokuwa kisiwani. Akakumbuka jinsi Kyande alivyokuja
na kelele na kuingilia ule wakati mtulivu waliokuwa nao baada ya kupeana ahadi.
“Unakosa starehe kaka!” Akapiga kelele akiwasogelea. Alipowakuta wamekaa vile,
akapoa. “Huyu ni Pendo! Au macho ya kilevi tayari?” Pendo akasimama, na Willy
akasimama. “Samahani kuwaingilia. Sikujua kama umeshinda bingo, kaka.” Pendo
akacheka na kujirudisha nyuma ya Willy. “Nilijua unapitwa, lakini hapo kaka!
Acha mimi niombe msamaha wakuingilia. Naondoka kabisa, narudi kwenye mashindano
ya kunywa.” Willy na Pendo wakacheka, Kyande akaondoka akishangilia kilevi.
Willy akamgeukia Pendo akamvuta karibu na kumkumbatia. Akamnyanyua kichwa
vizuri kwa mkono mmoja shingoni akaanza kunyonya midomo ya Pendo. Kwa mara ya
kwanza kwa mwaka mzima wanaanza chuo mpaka wamemaliza mwaka ndio siku hiyo ndio
anafanikiwa hata kumshika.
Willy
akamvutia vizuri mwilini mwake, akamsikia nayeye Pendo akimkumbatia vizuri,
Willy akajua amefurahia. Hakuna kilichoendelea jioni hiyo hapo ufukweni ila
hayo mabusu. Wakarudi kukaa, wakakumbatiana tena na kuendelea kuzungumza kidogo
na mabusu mengi. “Nilikukaribisha nyumbani.” Pendo akacheka taratibu. “Asante.”
“Hiyo inamaana leo usiku tutakuwa wote?” “Bado nina vitu vyangu chuo.
Nimebakiza..” “Unataka twende tukavifuate kabla hatujaenda kwangu?” “Au
nikafungashe kila kitu ndipo nije kesho?” Willy akambusu tena na tena,
akimpapasa kwa heshima bila kufika mbali. “Nitakusubiri wakati ukifungasha.
Twende.” “Sasa hivi!?” Pendo akauliza kwa mshangao huku akicheka kidogo. “Kama
unapenda kuendelea kubaki hapa, sawa. Nitakusubiri.” “Hata tukitaka kuondoka,
tunaondokaje?” “Tutakodi boti iturudishe nchi kavu.” “Basi nisindikize nikamuage
Eva.” Hapo napo yakaendelea mabusu ya muda tu Willy akinogewa na midomo ya
Pendo, ndipo wakasimama.
Hata
Eva akamshangaa Pendo aliyerudi. “Unakwenda wapi wewe?” “Nitakwambia kesho. Ila
naondoka na Willy.” “Moja kwa moja!?” “Ndiyo. Naondoka na Willy, nilishakwambia
ananivutia. Na ametoka kunikisss.” Wakacheka sana. Willy yupo pembeni. “Pendo!”
“Nahisi nampenda. Anajali huyo! Ananipapasa kila wakati! Haachi kunishika.” Eva
akacheka kishabiki. “Ujue yule rafiki yake Chale, alikuwa anakusubiria?” “Akuu!
Simtaki, mimi naondoka na Willy.” Eva akacheka. Wakaagana. Wakati Pendo anaondoka,
rafiki wa mpenzi wake Eva, akamuita.
Pendo
akasimama. “Nimesikia Eva akisema unaondoka!” “Ndiyo.” “Daah! Nilijua tutakuwa
wote usiku wa leo.” “Yule pale ni mpenzi wangu, ndio amekuja kunichukua.” Wote
wakamgeukia Willy, wakakuta na Willy akiwatizama. “Oooh! Sikujua kama una mtu!”
Pendo akacheka kiuungwana na kuaga. “Twende.” Akamshika Willy, wakaondoka.
Wakakuta kuna baadhi ya watu nao wanaondoka. Wakapanda na kulipia, wakaondoka
kurudi nchi kavu. Walikuta gari ya Willy sehemu yakuegesha magari, wakapanda na
kuelekea chuo. “Nimefurahi umekubali kuwa na mimi.” Pendo akacheka bila kujibu.
Alichofanya
Pendo mara walipofika chuoni ni kukusanya vitu vyake vyote na kuweka kwenye
gari ya Willy. “Naomba usiogope ukadhani nahamia kwako moja kwa moja. Vyote
hivi vilitakiwa kurudi nyumbani ila nimepishana na kaka K, alipokuja kuvichuk...”
“Pendo!” Willy akamuita taratibu. “Sitaki uingiwe hofu.” “Hata ukihamia kwangu
moja kwa moja, sitajali. Ndio itakuwa furaha yangu. Unakumbuka nilikuomba
orodha ya vitu ambavyo ungehitaji pale kwangu?” Pendo akacheka. “Nilijua
unatania Willy!” “Hapana. Nakuhitaji Pendo. Nakupenda wewe. Sijawahi
kukaribisha mtu hata mmoja pale kwangu. Hakuna anayepafahamu pale ila wewe tu. Hata
Kyande hajui ninapoishi. Na nilikusudia hivyo ili tuwe na sehemu yetu sisi tu
wawili.” “Kweli Willy?” “Mimi nilikuwa nikikuwazia kwa muda mrefu sana. Naweza
nisiwe na uwezo wa kukupeleka kwenye mahoteli ya hadhi ya juu au nyumba ya
thamani kama Chris, lakini nakuhakikishia kukupenda na kukuthamini.” Ikamgusa
sana Pendo. Akamsogelea pale alipokuwa amesimama nyuma ya gari akipanga mizigo
yake, akambusu.
Walikuwa
wamesimama ndani ya geti la chuo, Pendo hakujali. Akamsogelea vizuri na
kuendelea kumbusu taratibu bila hata haraka wakati wanachuo wengine wakipita na
kuwaangalia. “Asante Willy.” “Asante na wewe.” Willy akashukuru kwa heshima ya
kumbusu mbele ya watu bila kificho. Wakamalizia kupakia vitu, nakuondoka hapo
chuoni mpaka nyumbani kwa Willy. “Naomba tusishushe vitu ili tena kesho
tusihangaike kupandisha.” “Unataka kuondoka kesho!?” “Ndiyo Willy. Kwani
ulitaka nikae mpaka lini?” “Isiwe kesho. Usiku mmoja tu! Nahisi mimi unanipunja
Pendo.” “Hapana Willy. Nyumbani wanajua nimeshamaliza mitihani!” “Ungefanyaje
kama ingekuwa unasafiri na Chris?” Pendo akapoa, akajua amekamatwa.
“Huwa
nilikuwa nikisafiri na Chris, inakuwa msimu wa chuo, Willy. Na safari hii
nilipanga kutosafiri naye tena au nilishaamua kutokuwa naye tena. Naweza
kukwambia nina muda mrefu hata kwake nimekuwa nikimkatalia kwenda. Nilishaona
haina hata maana ya kupata naye muda wa faragha! Kwanza alishanikera, hata
sikumbuki mara ya mwisho kumbusu Chris! Ni mnyanyasaji kuliko nitakavyokwambia.
Hisia zilishakufa kwake. Kama usingeniokoa kwa kuniambia nimwambie ukweli, nahisi
mpaka sasa hivi tungekuwa tukisumbuana naye tu.” Willy akabaki ametulia kama aliyeelewa
lakini bado anahisi kupunjwa.
Pendo
akapiga magoti kwenye kiti na kumbusu mara mbili tu. “Naomba tusifikirie
kuondoka kwangu wakati hata sijafika ndani.” “Nahisi ninahamu na wewe zaidi ya
haya masaa machache unayotaka kuyatumia kwangu.” Pendo akambusu tena bila
kumuachia, Willy akamshika vizuri akiwa amepiga magoti vile vile. “Naona kweli
twende tukatumie siku ya leo kwanza.” Willy akaongea sikioni, Pendo akacheka
taratibu na kumbusu tena. Akachukua kibegi kidogo ambacho alishakitenga tokea
chuo, chenye vitu alivyojua atatumia kwa Willy, akashuka. Willy akampokea na
kutangulia. Akafungua mlango, akampisha Pendo aingie. “Karibu.” “Asante.” Pendo
akapita.
Akamuona
Willy anapitiliza chumbani, na yeye akamfuata. “Naomba nioge kwanza Willy. Ndio
nitajisikia vizuri.” “Sawa.” “Kwani tutatoka tena?” “Hapana. Ulitaka tutoke?”
“Hapana. Niliuliza ili nijue nivae nini.” “Hatutatoka. Kama utakuwa na njaa,
kipo chakula na matunda.” “Sawa.” Pendo akaelekea bafuni na nguo za kulalia,
akaoga nakutoka akiwa amevaa nguo zake za kulalia, zikitamanisha haswa.
Akacheka wakati Willy akimtizama. Akang’ata mdomo wake wa chini kitu
kilichokuwa kikimchanganya sana Willy akifanya hivyo.
“Unavutia
hata kwenye nguo za kulalia Pendo!” “Asante.” Pendo mwenyewe alijijua ni mzuri.
Na vile Willy anavyomchukulia, ikamuongeza ujasiri sio kama Chris aliyekuwa
akimfanya ajisikie mnyonge mbele yake. Akamvutia karibu yake. “Nikwambie
ukweli?” “Mmmh!” “Nilishakupigia mahesabu humu ndani, nikaishia kukuweka
kitandani, taa ikikumulika.” Pendo alicheka mpaka akajifunika uso. “Willy
wewe!” “Hakika. Nilisema labda kwenye kochi. Nikajiambia kwenye kochi sitafaidi
kukuona vizuri mwili wako wakati nikikubusu kila mahali. Sehemu pekee niliyoona
nitatuliza nafsi yangu ni kitandani, tena ukiwa kama ulivyozaliwa, na taa zote
zikitumulika pale kitandani. Nitizame mapaja yako niliyoyaona siku Wema
aliposababisha uanguke!”
“We
Willy jamani!” “Yaani vile ulivyoanguka siku ile, nguo ikafunuka, ile picha ya
mapaja yako ipo akilini kama fomula za mahesabu. Ndio maana nilikimbia kukuinua
ili wengine wasije kuyaona. Nikajiambia siku ukija hapa kwangu, jinsi ya kuyaona
vizuri, niyashike na kuweka mdomo wangu hapo kwa uhuru, ni kitandani tu. Tena
na taa ikimulika. Nishakupigia mahesabu humu ndani, hakuna tutakapokaa usiku
huu kama sio pale kitandani, nikaridhika. Na ninataka nikushike kila
mahali. Midomo yangu ikiridhika kupita kote nilipokuwa nikipatamani huko
mwilini mwako, ndipo akili yangu itatulia.” “Mimi sijui nifanye nini sasa?”
“Sitaki ufanye chochote. Niruhusu nifanye kila kitu mwilini mwako. Hatua kwa
hatua kama nilivyopanga. Na nguo nikutoe mimi mwenyewe.” Pendo akafurahia sana.
“Nakuahidi
usiku wa leo utafurahia Pendo.” “Nimeshaanza kufurahia. Napenda unavyonishika
Willy. Nasikia raha!” “Basi niachie usiku wa leo nifanye kile nilichokuwa
nikitamani. Kuanzia kukuvua nguo zote mimi mwenyewe.” “Ila sasa nilipooga
sijavaa chupi tena!” “Nikikuomba uvae ili mimi mwenyewe ndio nikuvue itakuwa
nakusumbua?” Pendo hakutegemea. “Willy!” “Hakika Pendo. Naomba ukavae hapo
chumbani wakati nakusubiri hapa, halafu ukimaliza ndipo uniite.” Pendo akaenda
chumbani akicheka kama asiyeamini. “Halafu huyu Willy hata hakubadilika!
Wakati wote alipenda yeye ndio awe ananivua nguo na penzi iwe mwangani!”
Pendo akakumbuka hilo akiwa hapo chumbani kwao akimkumbuka mumewe. “Jamani maisha yananipokonya Willy wangu! Hakuna mwanaume
atakayeniwezea kama Willy mimi!” Pendo akakumbuka penzi la Willy na
kulia kwa uchungu sana akiwa peke yake hapo chumbani usiku huo akiwa ameachwa
na Willy.
Akakumbuka
mambo mazuri yaliyomfurahisha usiku huo ambayo hata Chris mwenyewe hakuwahi
kumfanyia kwa undani huo. Willy alionekana kufurahia kila anapopanyonya, tena
kwa muda mrefu kwa hisia bila papara wala kinyaa. Alifanya kama yeye ndiye
anayefaidi zaidi kumbe Pendo ndiye aliyekuwa akifikishwa kila mara wakati Willy
hajapata bao hata moja ila kuhangaika mwilini kwa Pendo. Usiku huo kwa mara ya
kwanza Willy akabahatika kumshika Pendo aliyekuwa akimtizama akiwa na nguo.
Sasa hivi yupo mikononi mwake, mtupu na ametulia kitandani kwake akitoa milio
iliyozidi kumfanya Willy apagawe na kila wakati alipokuwa akifika kileleni
alimuita Willy jina lake kitu kilichomfurahisha sana Willy na kuona kumbe Pendo
yupo pale wala hamfikirii mtu mwingine ila yeye!
Alipoamua
kuingia yeye sasa, kwa kuwa alishakuwa juu sana kwa kumpapasa Pendo kwa muda
mrefu, haikuchukua muda mrefu akapiga bao. Akajua Pendo atamdharau atamuona
hajui mchezo wa muda mrefu ndio maana alikazana na romance, akarudia raundi
ya pili iliyomtoa jasho Pendo. Alimgeuza kulia na kushoto safari hii akifaidi
Willy peke yake bila kupumzika na Pendo akiwa mwepesi hapo kitandani akimpa ushirikiano
kwa kila staili anayotaka kumfanyia, mpaka Willy akatosheka.
Wakati
anapumzika hiyo roundi ya pili, Pendo akaweka mkono chini ya kitovu chake na
kuanza kumchezea nywele za hapo taratibu na kumuamsha tena Willy. Willy
akamgeukia. “Nakufurahia Pendo!” “Na mimi pia.” “Basi naomba tuendelee tena.”
Pendo akacheka akijaribu kumfikia midomoni. “Una mwili mzuri Willy! Nasikia
raha ukinilalia.” Willy akacheka sana. “Mimi nilijua nakuumiza, lakini
nikashangaa mwenzangu ndio umepiga bao kwa haraka!” “Nasikia raha hicho kifua
chako kinavyonilalia, halafu huo mkono wako unavyokamata upande mmoja chini ya
hips kwa nguvu halafu ukiingia na kutoka, hapo nakuwa sijiwezi tena.” Willy
akawa ameshajua staili yake moja inayomfikisha kwa haraka, wakaanza tena penzi.
Pendo akakumbuka furaha aliyokuwa nayo
usiku ule, akimfaidi Willy akitamani asimalize anayomfanyia hapo kitandani.
Willy naye hakufanya mchezo ulio wakitoto kwani hakujua mwenzie aliyeachwa
alikuwa akifika wapi, kwa hiyo yeye akaongeza umakini akihakikisha hafupishi
safari na hakuna anakobakisha hapo mwilini kwa Pendo. Akamgeuza kulia na
kushoto, ilimradi wote wafurahi.
Asubuhi
ya siku inayofuata waliamka wakabaki kitandani. “Naomba na leo tubaki wote
Pendo. Umenionjesha tu.” “Hata mimi nataka tubaki wote Willy. Nimefurahia.
Nimeamini kweli unanithamini.” Pendo akaongea taratibu pembeni ya Willy. Willy
akaanza tena kumbusu. Kama apendavyo Willy akaanza kumtoa nguo Pendo. Walikuwa
wamelala hapohapo kitandani, midomo yake ikiendelea kumnyonya midomo yake huku
mikono ikimpandisha nguo ya kulalia. Kwani usiku baada ya purukushani zote
Pendo alirudi bafuni kuoga. Wakati Willy naye akioga, huku chumbani Pendo
akakumbuka zoezi la kuvuliwa nguo huku akipapaswa na kunyonywa mwili wake
vilivyo. Akavaa kwa haraka kabla Willy hajarudi hapo chumbani. Basi asubuhi
hiyo nayo zoezi la burudani la kuvuliwa nguo likaanza. Kwa hakika Pendo alimfurahia
Willy, akajiambia hataondoka hapo, liwalo na liwe huko nyumbani kwao. Atajua
chakudanganya baada ya kuridhishwa asubuhi hiyo. Mchezo ukazidi kunoga, akaona
uzito kuondoka hata kesho yake.
Akaona
atengeneza mazingira ya kukaa hapo zaidi. Akampigia simu baba yake ambaye
humsikiliza na kumkubalia kila jambo kwa haraka. Akajiliza kuwa amekamatwa somo
moja, tena hesabu. Anatafuta msaada hapo chuoni, na wote waliokamatwa wamebakia
chuo kwa muda wakijipanga. Walimjua ni muoga wa hesabu na huwa zinamsumbua.
Baba yake akampa pole na kumuhurumia sana. Pendo akajiliza kuwa amewamiss sana.
Akaahidi jumamosi jioni lazima arudi nyumbani japo awaone tu ndipo arudi kwa
wenzake kujisomea. Hilo likapita bila shida tena kwa upendo na akatumiwa pesa.
Willy alitoka kwenda kwenye kupokea mzigo wa mashuka na kuuza. Alipomuacha hapo
nyumbani, ndipo akapata nafasi ya kuwapanga wazazi.
Wakakubaliana
hiyo week ni ya kupumzika tu mpaka week ijayo ndipo watasoma. Alichofanya Willy
baada yakurudi na kuambiwa wazazi wameamini, na atakuwepo hapo week hiyo,
akashusha mizigo yote ya Pendo, wakaanza kupanga humo ndani, ikachukua picha ya
wao wawili. Pendo akajaa yeye na vitu vyake humo ndani ya nyumba ya Willy.
Wakabadilisha na kupaita kwao. Pendo alijawa furaha, na umbali aliofika Willy
kwenye mwili wake, hakuna kitu ungemwambia Pendo akaelewa zaidi na anachoambiwa
na Willy.
Siku
zikawa zikikimbi, jumamosi aliyoahidi wazazi angerudi kuwaona ikafika, ikabidi kurudi
nyumbani, lakini akawaendea na ratiba nzima ya jinsi ya kujisomea na wenzake,
kumbe ni Willy tu. Akadanganya nyumbani kuwa wenzake wamechukua chumba Kijitonyama,
wamefanya kempu hapo wanajisomea, wakijiandaa kwa kurudia mitihani. Akaongea
mengi ya uongo mpaka wazazi wakaamini na kutoa baraka zao. Pendo akaahidi kuwa
akiwa anarudi nyumbani siku za jumamosi jioni, analala hapo kwao lakini
jumatatu atakuwa akirudi kwenye kempu kujisomea na wenzake. Hilo
likapita kwa baraka zote. Lakini dada yake Nancy yeye akamwambia ukweli kuwa
amepata mwanaume anayempenda karibu kuchanganyikiwa, na kweli atamsaidia sana
hesabu. Sifa za Willy zikamvutia na Nancy, akaahidi kumfichia siri.
Maisha
kati ya Willy na Pendo yakaanzia hapo. Wawili hao wakaanza kuishi pamoja
kuanzia hapo. Willy akawa msaada mkubwa sana kimasomo kwa Pendo, wawili hao
wakawa wapenzi wa kutojificha. Likizo nzima Willy alikuwa na Pendo, chuo
kilipofungua Pendo hakuchukua chumba chuoni, maisha yakaendelea Kijitonyama kwa
Willy. Wanakwenda chuoni asubuhi, usiku wanarudi kwao. Wazazi wakitaka kwenda
kumtembelea hosteli, basi kitanda cha Eva ndicho kikawa kikionyeshwa ni cha
Pendo. Wazazi watakaribishwa chumbani kwa Eva, watazungumza kidogo. Wakiondoka,
na yeye anaondoka na Willy kurudi kwao.
Mwaka
huo wa pili katikati ikabidi Pendo amtambulishe rasmi Willy nyumbani kama ndiye
mume wala si mchumba. Akaweka msisitizo ndiye atakayemuoa lazima wampokee na
waonyeshe kumpenda. Mtoto huyo wa mama akaweka msisitizo, Willy akapokelewa
kama Kenton hapo nyumbani kwao. Pendo akiwepo nyumbani, basi ujue na Willy
atakuwepo hapo siku nzima wakifuatana kila mahali. Haikuwa tofauti na chuoni.
Kutengana muda wa vipindi tu. Lakini kama nikujisomea, utamkuta Pendo kwapani
kwa Willy. Hata kama mwenzake yupo kwenye kundi na wenzake wa uhasibu wakijisoma,
basi ujue Pendo atakuwa katikati ya hilo kundi la watu wa uhasibu, anajisomea
kivyake, wakati Willy anasoma na wenzake. Wakimaliza hata kama ni usiku,
wanarudi nyumbani kwao. Hakuna aliyejua wanapoishi, ila wao tu.
Hata
ungekuwa na mamilioni ya pesa, ukamtongoza Pendo, asingekubali kwa umbali
aliofika Willy kwenye maisha yake. Akilini na mwilini mwake alijaa Willy tu.
Uzuri wake na vile alivyo, alitongozwa kila kukicha, lakini akatulia kabisa kwa
Willy. Na Willy hivyo hivyo. Ukiwakuta chuoni wakitembea au kukaa, basi
wameshikana. Mabusu mbele ya watu kikawa kitu cha kawaida na watu wakawazoea.
Pendo akawa hajui tena maisha mengine bila Willy mpaka wanamalizia mwaka wa
tatu, Pendo hakushikwa tena somo hata moja na wakafaulu vizuri tu.
Kwa
kuwa biashara za Willy zilikuwa zikiendelea vizuri, hawakutaka kukimbilia ajira
japo Willy alipata makampuni mengi yakimtaka aanze kazi, lakini Pendo akamwambia
lazima wasome wote shahada ya uongozi pamoja. Hapo hata wazazi walishajua
wanaishi pamoja. Wakachumbiana na wazazi wakajua wakimaliza hiyo shahada ya
pili, walishanunua kiwanja, ndiyo hiyo nyumba aliyopo Pendo au aliyochukua
Pendo wakati wakuachana. Walianza kujenga wakiwa chuoni.
Usiku
huo Willy amemuacha Pendo hapo kitandani, Pendo akabaki akikumbuka hayo maisha
yake na Willy! Akakumbuka mapenzi yao, utulivu waliokuwa nao tokea wakiishi
pamoja wakiwa chuoni mpaka wakaja kufunga ndoa, miezi michache sana kabla ya
kifo cha mama yake ndio kidogo Pendo akaanza kukumbuka kumuona Willy
kubadilika, lakini alimtetea nafsini mwake akijua ni sababu ya kumuuguza mama
yake na Willy alipatana sana na mama yake, kumbe aliongezeka na Zelda! Pendo
akalia usiku huo akimkumbuka Willy wake huku akimuonea wivu Zelda, akijua
anafaidi maujuzi ya Willy. Akalia kwa uchungu mpaka akapitiwa na usingizi.
Talaka ya
Pendo na Willy.
K |
wa kuwa walikubaliana
kila kitu bila shida, Willy na Pendo waligawana mali zao kimya kimya bila
ugomvi. Kaka yake akaandaa talaka kwa haraka sana mpaka akamshangaza Willy. Ila
akajua ni kwa kuwa amekasirika. Alimjua Kenton jinsi anavyopenda dada zake,
zaidi Pendo. Tokea wapo wanasoma chuo, Kenton alimfanya Pendo kama mtoto mdogo.
Akajua uharaka ule ni hasira ya kutaka kumtoa kwenye maisha ya mdogo wake
asiendelee kumuumiza. Baada ya siku 5 tu tokea atoke nyumbani kwake, Willy na
Pendo wakakutana tena kwa mwanasheria kuweka saini zao kwenye hiyo talaka.
Pendo alitokea nyumbani kwenda kwenye hizo ofisi za huyo mwanasheria ambaye ni
rafiki wa Kenton. Aliwahi kidogo, akafika na kukaa. Akiwa amejiinamia Willy
akaingia. Moyo wa Pendo ukaanza kwenda mbio, asijue ni furaha au nini! Alishammiss
Willy kupita kiasi.
“Vipi?”
Akamsalimia na kuvuta kiti pembeni yake. “Safi. Pole na majukumu.” Pendo
akaongea kwa sauti ya chini na ya upendo kama kawaida yake. Willy akatabasamu
kidogo na kujibu huku akimwangalia. “Asante na wewe.” “Asante.” Wakamgeukia
mwanasheria wao aliyekuwa amekaa mbele yao. “Habari yako Willy?” “Nzuri na
samahani kuchelewa.” “Hamna shida, familia haijambo?” Willy akanyamaza kidogo,
Pendo akainama. “Haijambo tunamshukuru Mungu.” “Sawa sawa. Sasa kwa kuwa naona
mmeamua kumaliza mambo yenu kiuungwana, hatutachukua muda mrefu. Kama utataka
muda wakupitia makubaliano yenu tuliyoweka kwa maandishi, pitia tu. Pendo
alishapitia wakati akikusubiri. Hakuna haraka.” Willy akapokea zile karatasi.
Akasoma taratibu tu moja baada ya nyingine.
Kumbukumbu
za Pendo zikamrudisha siku waliposaini kwenye cheti cha ndoa. Harusi kubwa
yakifahari. Kulijawa shangwe kubwa, wapenzi hao siku wanakula kiapo kuwa mpaka
kifo ndio kitawatenganisha. Pendo akakumbuka ile hali ya furaha aliyokuwa nayo
siku ile kuolewa na mwanaume kama Willy. Akavuta pumzi kwa nguvu na kuinama.
Akachukia kutoshika mimba mapema. Akajichukia kusababisha kuvunjika kwa ndoa
ambayo wengi waliitamani! Akatamani kama ingekuwa vinginevyo! Lakini akajiambia
maji yameshamwagika. Willy si wake peke yake tena kama alivyomuahidi miaka hiyo
hata kabla ya ndoa, wakiwa wanachuo, kisiwani Mbudya. Yupo Zelda na ujauzito
unao msubiria Willy. Pendo akabaki ameinama.
~~~~~~~~~~~~~~~~~
0 Comments:
Post a Comment