Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com Nilipotea! - Sehemu ya 17. - Naomi Simulizi

Nilipotea! - Sehemu ya 17.

 

G

abriel akajirudi kama ambaye hajui tena anachotaka. “Naomba  usikasirike  Nancy. Sikuongea kwa nia mbaya. Mke wangu  ndiye mwanamke niliyedumu naye kwa  muda mrefu sana. Hata sikumbuki ni  lini nilimvulia nguo mwanamke  mwingine. Labda zamani sana enzi za ujana huko chuoni. Tena sio hapa  nchini. Kile kitendo nilichokufanyia  pale ofisini kimenifanya nijione mjinga  sana. Nilikufanya ufanye kitendo  ambacho  najua  hata  wewe  hukutarajia.” Gab alijisogeza. 

Naelewa wewe ni binadamu Gab.  Siwezi kukuhukumu kwa lolote. Yale  yamepita. Nafikiri matatizo uliyonayo  na mkeo ndiyo yanakupelekesha.  Unaonekana haujatulia kimawazo hata kidogo,  umejawa wasiwasi kupita kiasi! Wakati kwa maongezi yako naona umefanikiwa  sana na kila kitu kinakuendea vizuri.  Kukwambia  nikufanyie  masaji, nikutaka kukusaidia  tu, sio vinginevyo.” Asante Nancy kwa  kunifikiria. Sasa bado ofa ya masaji  ipo au ndio nimeharibu?” Tunda  akacheka taratibu.  Nishabadili nguo sasa hivi, nimevaa  nguo za kulalia tu.” “Sasa zina shida  gani?

Hebu niangalie jinsi nilivyo,  Gab! Ni kama nipo uchi tu. Sitaki  unielewe vibaya na wewe ni mume wa  mtu.” Kule kuangalia ilikuwa kosa jingine. Gab alibaki amemkodolea  macho Tunda aliyekuwa amejifunua  kutoka kwenye shuka, akapiga magoti  pale kitandani ili kumuonyesha nguo  nyepesi aliyovaa. Tunda alivuta shuka  nakujifunika huku akicheka. Si umeona mwenyewe? Sio nguo za heshima.” Hamna bwana. Mbona upo sawa tu.  Wewe nifanyie tu.Tunda alijua wazi  hata afanyaje, Gab hana jeuri ya  kumuacha usiku ule. 

Kama  kondoo  anayeenda  machinjiaoni, Gab akasalimu amri.  Alivua nguo na kukimbilia kitandani  kwa masaji. Hakutoka pale kitandani  mpaka palipo pambazuka. Tunda  akaanza kutoka usingizini kabla  yakufungua  macho,  akakumbuka  amelala na Gabriel. Alifurahi sana. 

Akafungua macho taratibu akamkuta akimtizama. Akatoa tabasamu lililojaa usingizi. “Wewe mtoto utaniua.” Gab akalalamika. Tunda akacheka na  kujitoa kifuani kwake, akajilaza  kwenye mto. Mbona unanikimbia  sasa?” “Siumesema unawahi kikao  asubuhi hii?” “Nimeshawatumia ujumbe tutafanya mchana. Rudi hapa  kifuani bwana.” Tunda akacheka  wakati anarudi. Gabriel ulalaji wake  sio hata nusu ya Mbawala Juniour.  Gabriel alimuweka kifuani kwake,  akamchezea taratibu mpaka Tunda  akalala. Alifurahia mikononi kwa  Gabriel. Alipenda harufu yake.  Alitamani asitoke hapo kifuani. 

Hakuna kikao kilichofanyika siku hiyo  wala siku inayofuata. Tunda na  Gabriel walibakia hapo chumbani wakifurahiana. Alikuwa ni kama chui  aliyeona  nyama.  Lakini  alichomfurahisha Tunda ni ustaarabu.  Kumuomba na kumuuliza kama yupo  sawa au anataka kupumzika. Alijawa  shukurani kwa kila anachofanyiwa na  Tunda. Hakuacha kusema asante na  kutaka kujua kama yupo sawa. Hakuna kitu kidogo alichofanyiwa na Tunda  asitoe shukurani na kukielezea jinsi  alivyofurahia. Hilo Tunda alilipenda na kumfananisha kidogo na waziri Mbawala. Wengine wote hawakuwa na  tofauti. Walimtumia tu. 

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Baada ya kutoka hapo, Gabriel  akaanza kumganda sasa Tunda. Kila  safari anayosafiri alitaka awe naye.  Walisafiri nje na ndani ya nchi. Na  kwakuwa alikuwa akimpa mapesa  mengi, Tunda akaanza kupunguza  wateja waliokuwa wakimuhonga pesa  chache na sio wastaarabu. Wanaotumia  mwili wake vibaya. Kama Mbawala  Junior, akaanza kupuuza simu zake.  “Pengo lake limezibwa na Gab.” Akacheka Tunda wakati akisoma  jumbe za Mbawala Junior na kuzifuta.  Hata alipopiga simu, hakupokea tena.

Jeuri ikamjaa, akaanza kuringia  wateja wake wengine.  Pesa aliyokuwa akimwaga Gabriel,  ilimtosha sana tu. Bila kutegemea, Gabriel akawa zaidi ya Sadiki.  “Mungu amenifuta machozi.” Tunda akajisemea. Hapakuwa na kuloga,  wala kukesha makaburini. Gabriel  hakutaka habari za watoto wala  kumpekua Tunda. Penzi na starehe tu.  Wote walikuwa watu wa furaha. Hata  walipokuwa  jijini  Dar,  bado  walionana. Kituo chake kilekile.  Mlimani city. Hata kama ni jioni au  usiku  wakati  Gabriel  anarudi  nyumbani kwake, alisimama hapo.  Tunda alimfuata. Watatumia hata lisaa  kama akiwa na haraka au watakaa  hapo ndani ya gari kwa muda wa  Gabriel. Ndipo wanaachana.

Hazikuwa zikipita siku tatu bila wawili  hao kukutana. Ilikuwa ni kama Gabriel  hawezi kutoonana na Tunda tena.  Malalamishi juu ya mkewe yakaisha  kabisa. Gabriel akawa mtu mwenye  furaha tu. Tunda alishamfundisha kupuuza mambo  madogo madogo. Basi amani ikaendelea mpaka nyumbani. Kila mtu aliyaona mabadiliko ya Gabriel kitu  kilichoibua maswali hata kwa mkewe  ambaye walishazoea kujibizana kila  wanapokuwa pamoja. Akashangaa  ukimya na kunyamaza kwa mumewe.  Usingemkuta Gabriel akibishana naye  tena. Alitoka muda wa kawaida, na  kurudi nyumbani muda wa kawaida.  Tunda alishajiambia, ukila na kipofu,  humshiki mkono. Hakuiba kwa kelele,  ili asikamatwe  mapema na kupokonywa tonge mdomoni. Basi, akaendelea kunufaika na Gabriel na Gabriel akinufaika na Tunda. Maisha  ya amani na utulivu yakaendelea. 

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Gabriel alimtaarifu Tunda msiba mkubwa uliotokea kanisani kwao.  Rafiki wa mkewe Gabriel, Bethy  alifariki akiwa anajifungua. Aliacha  watoto wakiume wawili na bado walikuwa wadogo. Kwa ukaribu  aliokuwa nao huyo dada aliyefariki  gafla na Bethy mkewe Gabriel, ule  msiba ulikuwa kama wao. Walilala na  kushinda msibani kipindi chote hicho  cha msiba, mpaka walipohamisha  msiba huko kijijini kwao huyo  marehemu. Kwa hiyo hapakuwa na  kuonana tena. Tunda akaamua kutumia  muda ule na wateja wengine.   

Akiwa Dodoma na Naibu waziri wa ujenzi wa awamu hiyo ya utawala, hakuacha kuwasiliana na Gab. Gabriel alilalamika vile alivyo na  hamu naye, na pindi watakaporudi  mjini lazima waende kupumzika  Nairobi. ‘Hata mimi nipo mpweke sana Gab. Siku nikikukamata wewe! Utajuta.’ Gabriel alipiga simu huku akicheka sana. “Utanifanyaje?” Sitaki kukwambia. Lakini lazima utalipia huu upweke  ulionisababishia. Waliongea kwa muda  mrefu, Gabriel akiwa anajiambia  moyoni kuwa amepata mwanamke anayempenda   kwa dhati na  kumridhisha kuliko hata mkewe, huku Tunda naye akijiambia amepata mtu wake  wa kudumu. Lazima kumridhisha na  kumuweka karibu kwa garama yeyote  ile. Na kweli, linapofika swala la  Gabriel, kila mtu atasubiri. Na kila kitu  kitasimama. Gabriel kwanza.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Alirudi yule Naibu na kumwambia  watatoka jioni kwenda mziki, lakini  kabla ya hapo anakwenda kukutana na  mtu anayetaka sana tenda ya ujenzi wa barabara ya Nachingwea. “Bwana  kwani lazima ukaonane nae leo?” Tunda alilalamika. Inabidi Teddy! Ni  watu tunaoheshimiana nao sana. Na  walishajenga barabara ya Mpanda  bila shida. Tena mama yake ni mtu wa nyumbani kabisa. Ni kabila moja, ni mama  mzuri sana.” “Kwa nini asitufuate  klabu sasa?” “Hahahahah! Jamaa  mwenyewe hata pombe hagusi. Twende bwana hatutakaa sana.” Ikabidi akubali tu.  Tunda alivaa suruali iliyomshika  vizuri, na kiblauzi cha kung’aa, rangi za usiku. Ndogo nayo  ilimshika juu vizuri. Chini ya hiyo blauzi ilikuwa na muundo  wa VMbele na nyuma na vimikanda   

kama shimizi. Kwa kuwa ilikuwa jioni  na wanakwenda mziki, akavaa kiatu  kizuri cha juu chenye uwezo wa kumbeba muda mrefu bila kuchoka.  Hakika alipendeza Tunda. Alishikwa  vizuri juu mpaka chini. Kila kitu  kilimkaa vizuri. Na hapo alijulikana  kama Teddy.   

Net Naye Arudi Pichani.

K

wa mara ya kwanza tokea kwa Shangazi  yake, Tunda akiwa kwenye kuuza mwili  wake, akutana uso kwa uso na Net!  Alifika kwenye hiyo hoteli  na huyo Naibu Waziri, wakaelekea upande wa  mgahawani, wakamkuta Net  alishawasili, akisubiria tu hapo mgahawani. Tunda alishtuka sana.  Alitamani arudi kwenye gari lakini  yule Mheshimiwa alikuwa amemshika  mkono.  Net  alisimama  huku  akimwangalia Tunda.  “Umesubiri sana?” Hapana  kiongozi. Na mimi ndio nafika hapa. “Huyu anaitwa Teddy, niko naye hapa  kipindi hichi cha Bunge. Huwa  anakuja kusaidia saidia ili kazi ziende.” Kisha akamgeukia Tunda. “Teddy, huyu ni Nathaniel, ndio hao  wajenzi wa barabara yeye na mama  yake.” Tunda hakutaka hata kumpa mkono Net. Akawazunguka na  kutafuta meza na kukaa. Wakamfuata  na wao wakakaa hapo hapo kwenye  hiyo meza. 

Muda wote wa mazungumzo kati ya  Net na yule Mheshimiwa, Tunda  alikuwa ameinama akichezea simu  yake. Walipomaliza wakati yule  Mheshimiwa akiagana na Net, Tunda  akasimama na kuondoka bila hata  kuaga, akaelekea kwenye gari. Tunda  alibadilika kabisa mpaka yule Naibu  alimuona. “Vipi? Mbona kimya?” Kichwa kimeanza kuniuma gafla. Basi turudi hotelini.Walirudi  hotelini, akalala. Naibu asielewe  kulikoni. Akajua mambo ya wanawake  tu, atakuwa sawa. 

Basi aliamka kesho yake yupo sawa,  akafanya kilichompeleka Dodoma kwa  huyo Naibu bila shida wala kinyongo, akimfurahisha vilivyo. Akiwa kwenye  vikao vya Bunge, Tunda anazunguka  na kuwapa wengine huo mwili muda  huo wa mchana wakati Naibu yupo  kwenye vikao vya Bunge. Anarudi  kulala, tayari kumsubiri Naibu waendeleze mchezo huku akimsubiria  Gabriel amtafute.  Tunda akaendeleza mchezo wake huo,  huko jiji kuu la nchi ya Tanzania kama  kawaida. Akiwazungusha wabunge  kwa mawaziri. Wakubwa kwa vijana, mpaka Gabriel alipomtafuta kuwa amerudi Dar, na wamemaliza msiba.  Gabriel  huwa  hasubiri.  Tunda  alishakuwa ametengeneza pesa nzuri  tu, akafungasha vilivyo vyake, akarudi Dar kwa Gabriel kabla hata Bunge  halijaisha.   

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Ratiba  za  Tunda  zikaanza  kutegemeana na ratiba za Gabriel.  Hakutaka Gabriel amkose muda na  wakati wowote anaomtaka yeye. Hata  kama ni usiku wa manane, Gabriel  akimwita popote, alienda.  Simu yake ilikuwa haisubiri. Ilikuwa  na mlio wake maalumu. Akipiga muda  na wakati wowote. Hata akiwa na  mteja, huyo mteja atasubiri. Gabriel  kwanza. Alimchomoa pesa nyingi  sana, na Gabriel naye alikuwa  akizimwaga bila kufikiria mara mbili.  Kabla Tunda mwenyewe hajaomba,  alimpa. Tunda akawa na pesa, kama  yeye ndio mmiliki wa biashara za  Gabriel na Gabriel ndiye mfanyakazi  wake.  

Gabriel hakuongopa. Tunda alipotua tu  jijini, akakuta Gabriel anayo mipango  tayari. Alimwambia atasafiri tena na  mkewe. Lakini nilazima azungukie  biashara zake tena huko Mwanza  ndipo wasafiri na mkewe. Tunda alitua  jijini asubuhi, jioni akawa tena kwenye  ndege kuelekea Mwanza na Gabriel.  Walitumia siku tatu pamoja. Gabriel  akienda kuchungulia tu kwenye hiyo  migahawa yake, na kurudi hotelini  kwa Tunda. Baada ya hizo siku kuisha wakarudi Dar, Gabriel na mkewe  wakasafiri tena.  Tunda hakuuliza ni wapi anakwenda.  Alimuonyesha  Gabriel  kuwa  anaheshimu ratiba zake na mkewe.  Hana maswali na hata alipokuwa  mkewe akipiga simu na yeye yupo naye, basi  atanyanyuka hapo na kuondoka kumpa  nafasi yakuzungumza. Hilo alilipenda  sana Gabriel. Hakuwa msumbufu. 

Hakuwa akimtafuta Gabriel kwa simu  wala jumbe, alimpa yeye ruksa  kumtafuta muda na wakati wowote atakao,  lakini sio yeye. Alimwambia hataki kuja kumtia matatizoni. Hata namba  yake ya simu alimshauri ashike tu  kichwani. Penzi tamu la wizi likaendelea.

 ~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

     Gabriel aliposafiri tena na kumuacha, Tunda akarudi kuwa huru tena. Akaamua  kukumbushia wateja zake wengine. “Huwezi kujua kama akirudi atanitafuta au atabanwa na mkewe.  Heri kuzungukia makoloni yangu  mengine.” Akajiambia Tunda. Lakini  alikuwa amebakisha wateja wachache na wamuhimu tu ambao hawalii sana shida. Pesa ipo. Akabahatika  kumpata mfanyabiashara mmoja aliyemwambia  atamuhitaji kwa siku tatu. Tunda  akakubali akasafiri naye kurudi tena  Mwanza.  Huyo baba hakuwa akimpenda sanaa.  Ila ndiye aliyempata kwa wakati huo.  Tunda alimuona ni mbahili sana.  Alimuweka kwenye kundi la wateja  aliowaita wabahili. Honga yake na  yeye ilikuwa pesa ndogo ndogo, lakini  Tunda alifurahia hoteli alizokuwa  akienda naye. Na uhuru aliokuwa nao  wanapokuwa pamoja. Kwanza alikuwa  mlevi sana na pia hakuwa akimbana  Tunda.  Mara  nyingi  alikuwa  akimuacha Tunda hotelini siku nzima,  jioni akirudi ndio anatoka naye  kwenda kunywa mahali.

Walifanya starehe nyingi sana  alipokuwa na Tunda, tofauti na wateja  zake wengine waliokuwa wakipenda  kumfungia tu ndani. Na hapo aliweza  kupata wateja wengine wa muda  mfupi. Au hata marafiki zake huyo  huyo baba. Wakiwa kwenye kunywa  na kula huko kwenye starehe, akiona  ameshalewa, basi Tunda anaweza  kumtongoza mmoja wa rafiki zake, na  kupanga naye miahadi ya mchana.  Huyo baba akiwa ametoka kwenda  kwenye shuguli zake, basi hapo ndipo Tunda  atakutana na mwingine. Na uzuri wa  huyu baba kwa kuwa alikuwa mtu  mzima na mlevi, shuguli yake kwenye mapenzi haikuwa kubwa sana. Aliridhika kwa haraka kitu ambacho  hakikuwa kikimchosha Tunda. Basi  hapo ataingiza pesa kwa huyo na  wengineo. Atarudi kwake akiwa  amejaa.

Fumanizi Tena.

Siku ya tatu wakiwa Mwanza na yule  mteja  wake,  walikuwa  mahali  wakinywa na marafiki zake yule baba. Yaani wafanyabiashara wenzake. Pombe iliyokuwa ikinywewa hapo,  vyakula, ulikuwa utapanyaji mtupu.  Na karibu wote waliokuwa hapo  mezani, Tunda alishawadumia, ila  hawakuwa wakijuana. Kwa hiyo wote  walikuwa wakiiba kwa yule aliyekuja  nae Tunda, kwa wakati tofauti tofauti.  Tunda akawa akinufaika nao, wasijue.

 Wakiwa wamejawa vicheko vya kilevi hapo mezani, yule baba aliyekuwa  amekuja naye Tunda, akapokea simu  ilisikika ni ya kikazi. Walizungumza  kidogo kisha akamwelekeza yule mtu  aliyekuwa akizungumza naye kwenye simu pale alipo, na kumtaka afike hapo  kwa mazungumzo zaidi. Yule mtu alimwambia atakuwepo hapo kama  baada ya dakika 15 tu. Vicheko  vikaendelea.

Tunda alitamani ageuke upepo apotee,  pale Net alipowasogelea kwenye meza  yao. “Najua hupendi mazungumzo ya baa. Lakini sitakuweka sana.” Yule  baba alisimama kusalimiana na Net,  lakini  Tunda  hakutaka  hata  kumwangalia tena. Alimuona vile Net alivyokuwa akimwangalia.  “Samahani  bwana,  sijatoa  utambulisho. Akamgeukia Tunda, “Joy, huyu anaitwa Nathaniel yeye na mama  yake ni wateja wetu wakubwa. Tunawaingizia vifaa vyao vya ujenzi  hapa nchini. Tusema ndio watu  wanaochangia kutuweka mjini.” Yule mteja wa Tunda aliongea huku  akicheka. Hapana bwana!Net  alijibu kiuungwana kidogo. 

“Kweli kabisa. Unafikiri bila tenda  zenu, mjini pangekuaje? Haya huyu  anaitwa Joy, ni nini.. Siunajua kuna umri ukifika joto linapungua mwilini?  Hata bibilia imeshauri. Inabidi wazee tutafutiwe mabinti wadogo watupe joto  kama mfamle Daudi aliyependwa sana  na Mungu!” Yule Mzee alishakuwa  amelewa, alikuwa akiongea sana.  “Mabinti kama hawa ni hadimu sana  hapa duniani. Au unasemaje Bosi  wangu?” Yule Mzee alimuuliza Net huku akimpiga piga begani. Net  alitabasamu huku akimwangalia  Tunda. Tunda alishatoa simu yake  kwenye pochi akawa akiichezea bila  kunyanyua uso wake. Wakati mtumzima huyo akiendelea kuropoka.

“Sijui tutegemee lini huo mzigo?” Net  akauliza taratibu, ili kubadili  mazungumzo ya yule mzee aliyokuwa akimsifia Tunda tu badala ya biashara.  Alitoa sifa zake za uzuri wa Tunda  mpaka umbile lake, tena kwa undani  bila kunyamaza huku akiendelea kunywa. Tunda akasimama. “Vipi  tena?” Naenda msalani.Tunda  akaondoka. Hakurudi mpaka alipoona  Net ameondoka.

  ~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Aliporudi tu Dar, mteja mwingine akamtafuta. Naye pia ni miongoni  mwa wateja wake ambao Tunda  hakuwa akimpenda sana, kwani  alikuwa muoga sana ila bado anataka kuiba. Kitu alichokuwa akimkubalia tu ni pesa alizokuwa akimuhonga.  Alimpata kwa kumkonyeza akiwa  amekaa na mteja mwingine kwenye  baa. Alienda naye kwenye gari baada  ya kumuaga mteja aliyekuwa amekaa  naye siku ile na kwenda kumaliza haja za yule mteja aliyemkonyeza kwa  muda mfupi sana tena kwenye gari  kitu alichokifurahia sana na kufanya  kama mazoea.

Walikuwa  wakikutana  sehemu  zinazouzwa vyakula, tena muda wa  mchana, wakati anakwenda kwa  chakula cha mchana, na Tunda  alikuwa akimuhudumia kwenye gari yake. Kiti  cha nyuma ambako vioo vilikuwa giza.  Tunda anamchezea, baada ya muda  mfupi sana, anakuwa amemalizana  naye. Tunda anaondoka na yeye  anakwenda kuungana na rafiki zake kwa chakula cha mchana hapohapo  bila kuchelewa. Alimpenda sana  Tunda kwa umaridadi wake. Wepesi  na usanifu wa alichokuwa akimfayia.  Kila akipata tu pesa, basi lazima  atamtafuta Tunda. Na hakuwahi hata kuhisiwa na yeyote yule. Si marafiki  zake aliokuwa akitoka nao kwa  chakula cha mchana tu, hata mkewe  pia. Kwani alirudi nyumbani muda  wake wa kawaida bila kuchelewa na  wakati wote alikuwa ofisini au sehemu  husika ambayo hakuwahi kutiliwa  mashaka. 

Siku hiyo walikubaliana wakutane na Tunda  kwenye baa ambayo walikuwa  wakiuza mbuzi na ndizi za kuchoma  nzuri sana, karibu na ofisini kwake.  Tunda alikipenda sana chakula cha  pale. ‘Kama ni hapo ujue ni mpaka nile  kwanza. Siunajua ninavyopenda mbuzi wa pale?’ ‘Sio tuchelewe sasa, Maria! Siunajua  muda wangu?’ ‘Nishawahi kukuchelewesha  hata mara moja?’ Tunda akamtumia huo  ujumbe.  ‘Basi mama. Wewe tangulia uagize chakula,  mimi nikija sitakaa sana, tunakwenda kwenye gari.’ Wakakubaliana.

Tunda alivaa  vizuri kama kawaida yake. Na alivaa  kigauni kilichokuwa kikiendana na sehemu anayokwenda kufanya shuguli yake. Kigauni chepesi kilichochanua.  Na kiatu cha juu. Aliporidhika na  muonekano wake ndipo akatoka.  Alitoka mapema kidogo ili kupata  muda wa kula. Alijitengea muda wake  ili usiingiliane na muda wa mteja  wake. Bila kuchelewa, kwa kuwa  alijua anachotaka, alipofika tu  akaelekea jikoni moja kwa moja,  akaagiza chakula huku akiwasihi  wasimcheleweshe. Kisha akatafuta  sehemu akakaa.

Baada ya muda mfupi  tu, chakula na kinywaji vikawa  vimeshawasili hapo mezani kwake. Wakati akila na yule mteja wake  naye akawasili akiwa na faili mkononi.  “Sasa makaratasi ya nini na wewe!?” Kuna mtu anakuja kulichukua hili  faili.” “Si umesema una haraka wewe! Akichelewa?” “Jamaa mwenyewe mzungu, anatunza muda sana. Akikwambia  dakika kumi ni kumi. Atakuja sasa hivi,  wewe  malizia  hicho  chakula.  Tutaondoka sasa hivi.” Wakati  ameinama anakata nyama nyingine ili  aendelee kula, akasikia mtu akisalimia.  Aliponyanyua macho alikutana na Net.  Tunda alibaki kama amemwagiwa  maji ya baridi. Net alibaki akimtizama  Tunda. Akavuta pumzi kwa nguvu  kisha akaweka mikono yake juu ya kiti  kilichokuwa mbele ya macho ya Tunda  na kubaki wakitizamana na Tunda  aliyekuwa ameduaa. “Kumbe na wewe  unamfahamu Maria?” Yule mteja akamuuliza Net, lakini Net alibaki  akimtizama Tunda. 

Tunda aliinama akachukua pochi yake akasimama. “No no no nooo Maria!  Huwezi kuondoka. Lazima tumalizie mipango yetu.” Tunda alivuta kiti  nyuma na kuanza kuondoka. Yule  mteja wa Tunda alimkabidhi Net lile  faili  bila  maelezo  yeyote,  akamkimbilia Tunda. “Maria! Maria!  Kuna nini? Simama basi tuongee.” Tunda hakugeuka nyuma akaondoka. 

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Picha ya macho ya Net akiwa  anamwangalia kila alipokuwa  akimkuta na wateja wake, ilianza  kumsumbua sana Tunda. Hakujua kwa  nini. Alijifariji sana, na kujimbia hana  haja yakumjali Net, si kitu kwake, lakini moyo ulishindwa kupokea  kabisa zile taarifa zakumpuuzia Net.  Aliendelea kuteseka. Kila alipofunga  macho alimuona Net akimtizama.  Mara  nyingine  aliota  Net  amemfumania kabisa. “Kwani hata  akinifumania kuna nini!?” Tunda  alishtuka kutoka ndotoni nakuanza  kujishangaa.  “Hanihusu,  simuhusu.  Kwanza hata hanifahamu.” Tunda  aliendelea kujifariji. 

Hodi ya kijana wake wa kazi ndiyo  iliyomtoa  kitandani.  Alikwenda  kumfungulia mlango baada ya mlinzi  kumfungulia geti. “Leo kazi kubwa ni  usafi na kunyoosha nguo zangu.” Sawa dada.Tunda akaamua kurudi  tena chumbani kwake alikokuwa  amekaa muda wote akijifikiria baada  ya ile ndoto yakufumaniwa na Net,  akiwa katikati ya kufanya mapenzi na mteja wake mwingine.

 ~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Akiwa anakaribia mlango wa  chumbani kwake, akasikia simu yake  ikiita. Aliikimbilia akijua ni Gabriel tu,  kwani ndiye mtu pekee aliyekuwa  amebaki wakupiga simu. “Mbona  mapema leo?” Nimelala nakuota. Tunda  alianza kucheka. Na mimi nimekuota. Nafanya nini? Gabriel akauliza huku  akicheka.  “Mpaka tukikutana ndio nitakuonyesha kwa  vitendo.” Unapenda kunichanganya akili  wewe Nancy! Utafanya nishindwe kufanya  kazi siku nzima.” “Naweza kukufuta hata kazini.” “Kweli?” “Lini umeanza kunitilia  mashaka?” Njoo basi kwenye saa nane  mchana. Usiache Nancy, hali mbaya  mwenzio.” “Hali mbaya vipi wakati umeamka pembeni ya mkeo?” Sinilikwambia  sababu zake haziishi? Kama jana ameniambia  amechoka sana, nisimguse.” Pole Gab. Nishazoea. Gabriel alijibu kwa utulivu kidogo. Basi nitakuja saa nne. Usijali.”“Sawa.

Mtu pekee aliyemchanganya akili  Tunda ni Gabriel. Alianza  kujitengeneza kuanzia asubuhi hiyo.  Alibadili rangi za kucha zaidi ya mara  tatu huku akitoa kasoro kila nguo.  Mpaka alipopigiwa simu tena na  Gabriel. “Kazi haziendi huku Nancy. Njoo  uokoe jahazi.”Siumesema mpaka saa nane mchana?!” “Siwezi kufika saa nane.Tunda  alicheka sana.  Basi nakuja. Nipe kama lisaa.” Ilibidi  Tunda ajikubali tu ili asimchelewe  Gabriel ambaye alikuwa kama Mungu  mtu. Akatoka hapo kwake.

Alikwenda mpaka ofisini kwa Gabriel.  Sekretari aliambiwa simu na wageni  wote wasubiri. Wakajifungia na Tunda  humo ndani ofisini kwa Gabriel.  Ilikuwa saa sita mchana wakati Tunda  akiingia humo ndani.  Baada ya kama dakika 20 hivi,  sekretari akampigia simu kumwambia  BF anaondoka. Tunda alimuona  Gabriel amepaniki. “Kwa nini sasa  hukuniambia kama ameshafika? Subiri natoka  sasa hivi.” Waliingia chooni kwa  Gabriel, akajisafisha vizuri na kuvaa  harakaharaka kisha akatoka nje kabisa  kumfuata huyo mgeni ambaye Tunda alisikia jina moja tu, BF. Alimuacha  Tunda akijitengeneza huko huko  chooni ili atoke safi kama alivyoingia.

Tunda akiwa bado chooni, Gabriel  alirudi pale ofisini kwake na mgeni  wake. “Samahani sana. Nilikuwa na  kijidharula  kidogo.” Usijali.  Ninaharaka kidogo. Labda nikuwekee mafaili yote kwenye kompyuta yako,  baadaye ukipata muda wakuangalia  kila kitu na kuridhika, ndipo utanipigia  simu.” Hamna shida kabisa. Vipi  mama lakini?Wakati wameinamia  kompyuta Tunda naye akatoka kule  chooni akaingia pale ofisini ili  kuchukua pochi yake na viatu  alivyokuwa amevua katikati ya penzi,  aondoke.   

Fumanizi Baya, Lililomgarimu Tunda.

K

ule kufungua mlango wa chooni  kuliwafanya wote wanyanyue uso na  kumtizama Tunda. Uso kwa uso na  Net tena. Tunda alitamani kurudi  chooni lakini alikuwa ameshafunga mlango nyuma yake. Net alisimama  vizuri akamwangalia Tunda na  Gabriel.  “Umeanza lini Gab?” Net alimgeukia  Gabriel aliyeonekana kupaniki zaidi.  “Eti Gabriel?” “Nancy huyu ni Net, rafiki yangu sana tokea tupo wadogo  kabisa. Mpaka watu wametupa jina la  BF, Best Friend.” Gabriel na yeye  alisimama huku akitetemeka. Wazi  alionyesha ameingiwa hofu. Net  alimtizama Tunda kwa muda, kisha  akatoka bila kuaga.

Samahani sana Gabriel, sikukusudia.” Usijali Nancy, nimakosa yangu. Nilisahau  kama jamaa aliniambia atakuja saa sita na robo. Huwa anapenda kwenda  sana na muda. Kule kumuweka hapo  nje wakati nipo na wewe humu ndani  atakuwa amekasirika sana.Tunda  alitoka kimya kimya bila hata  kuongeza neno.  Akarudi kwake asijue kama lile ni  balaa au kuna mkosi unaomfuatilia.  Akakumbuka ndoto aliyoota usiku wa  kuamkia siku hiyo. Alitamani kulia.  Alipoteza wateja wengi sababu ya  Gabriel, hakuwa tayari kumpoteza  Gabriel, mteja aliyekuwa akimlipa  mapesa mengi sana. Ni kama yeye  ndio aliyekuwa akimlipia garama zote  kubwa za maisha. Wengine ni kama  chakula, mavazi na saluni.   

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Ulipita  kama  mwezi,  Tunda  amejifungia ndani asijue chakufanya.  Gabriel aliacha kupiga simu kabisa  tokea siku waliyofumaniwa na Net  pale ofisini. Alishapoteza wateja  karibu wote. Tena kwa kufanya juhudi  za makusudi, kuwaambia kabisa  wasimtafute  mpaka  yeye  takapowatafuta ili wasije kumtafuta au  hata kutuma ujumbe anapokuwa na  Gabriel. Halafu ikatokea kwa bahati  mbaya, Gab akaziona na kumfikiria ni  Malaya tu akamuacha.  Kwani mara nyingine walikuwa  wakicheza na Gabriel games zilizopo  kwenye simu yake.

 Na hakuishia hapo kwa hao wateja zake wangine, alikwenda umbali wakuwa block kabisa ili hata ujumbe  usije kuwa unaingia akiwa na Gabriel.  Pesa aliyokuwa akihongwa na Gabriel  ilikuwa ni sawa na kuhongwa karibu  na wanaume wengine wote waliokuwa wamebaki . Shida ndogo ndogo na  kubwa za Tunda zilikuwa zikimwisha  alipokuwa na Gabriel. 

Tunda aliendelea kuwaza juu ya  maisha  yake,  kwani  nyumba  aliyokuwa akiishi alikuwa akilipia  kodi kwa dolla. Aliishi maisha ya  kifahari sana. Pesa yake ilikuwa  ikiishia kwenye kuvaa vizuri na  kujinunulia vitu vya thamani kana  kwamba hakuna kesho. Alikuwa anajiambia mwili wake ndio  biashara yake. Lazima kuutunza vizuri.  Basi Tunda alikuwa akiutunza huo  mwili kama aliyeambiwa anaupungufu  wa kinga mwilini. Alikuwa akinywa  virutubisho vya huo mwili kwa gharama kubwa sana.

Alijiunga na kampuni iliyokuwa ikileta  virutubisho vya mwili vya asili nchini.  Basi  alikuwa  akinywa  hivyo virutubisho kila siku bila kukosa.  Hakuwahi kuishiwa. Kwa kumtizama  tu Tunda, ungejua huo mwili unatunza  vizuri. “Anayeendesha taksii, lazima atengeneze hiyo gari ya biashara mara kwa mara  kuvutia wateja wake. Kusafisha,  matengenezo mazuri, kubadilisha oil,  na kujaza mafuta kila inapokaribia  kuisha ili asizimikiwe njiani akiwa na  mteja. Basi na mwili wangu ndio hivyo hivyo.” Tunda alikuwa akijikumbusha hayo mara kwa mara juu ya kujijali. 

Basi ukimkuta ndani ya Sauna,  ametulia kimya. Na alithamini pia  muda wa masaji. Hoteli yeyote  aliyokuwa akienda na wateja zake,  ilikuwa ni lazima aulizie kama   

wanatoa hizo huduma. Na kama zipo,  atatumia ipasavyo. Hata kulala, alilala  kwenye kitanda cha garama kama  mfalme na hata mashuka yake  alijifunika mashuka mazuri sana. Na  alihakikisha kama hayupo kazini,  anapata muda wakutosha wa kulala.  Usingemkuta  anakula  takataka.  Chochote alichojua kitamnenepesha,  alikula kwa hamu, tena kidogo sana.  Kwanza alikuwa akila virutubisho  ambavyo vilimfanya hasikii njaa  hovyo. Na akila mlo mmoja mkubwa,  basi. 

Mara nyingi  hakuwa akipika chakula nyumbani  kwake. Isipokuwa vitu vidogo kama  kukaanga mayai tu na kuchemsha  maziwa. Vyakula vingine alikuwa  akila kwenye mahoteli. Tena ya maana  tu. Na kila alipokuwa akienda kwenye  biashara zake, alihakikisha anarudi  nyumbani na chakula chakula kesho  yake. Hakuwa akipenda kuwa karibu  na moto wa jikoni kwa muda mrefu.  Kwa muda wote huo alioishi peke  yake, baada yakutoka kwa shangazi  yake, Tunda alijipenda sana. Alikuwa  ni kama anajilipia miaka yote  aliyoteseka tokea anatolewa kwa bibi  yake akiwa bado binti mdogo.

Kwa  kumwangalia tu, ungejua mwili huo unashugulikiwa vizuri. Mwili mzima utafikiri  amepigwa msasa wa ukweli. Aina ya  lotion na mafuta ya nywele  yaliyokuwa yakiingia mwilini mwake,  ilikuwa pesa yakutosha. Yalimfanya  ang’ae kama nyoka juani.  Nywele ambayo sio 100% human hair,  haikuwa ikiingia tena kichwani  mwake. Saluni alizokuwa akienda  kutengenezwa Tunda, ni za wake wa  mamilionea wa mjini na kina mama  wanaoshika pesa nzuri.  Kwa hiyo, bili au garama zilizokuwa  zikimkabili kwa wiki tu, ili kumfanya  aendeshe maisha yake, ilikuwa juu  sana kama matumizi ya familia moja  kwa mwezi. Achilia mbali hiyo kodi  aliyokuwa akilipa kwa madola, kwa  mwezi.   

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

          Siku zikazidi kwenda, Gabriel  hamtafuti. Garama zote akaanza kulipa  yeye mwenyewe kwa kutumia akiba  aliyokuwa nayo. Kilichommaliza zaidi  hiyo kodi ya miezi mitatu. Na akajua  miezi mitatu huwa haikawii kuisha.  Atapata wapi pesa ingine ya kodi!?  Mwenye nyumba wake alikuwa  makini, hakuwa akitaka kupitishiwa  kodi yake zaidi ya juma moja.  Ikabidi kuanza kusaka wateja wake  wazamani bila mafanikio. Kwani na  hali ya uchumi wa Tanzania ikazidi  kuwa ngumu, kila mtu alilalamika pesa  hamna. Hata yale mabuzi aliyozoea  kuyashtukiza  yaliacha  kuhonga,  walianza kumkopa.   

Hali ikazidi kuwa mbaya. Wengi wa  wateja wake alipowafuata, waliishia  kumlisha, nakumtumia bila kumpa  pesa. Akaamua atulie, kwa kuwa pia  alikuwa akitumia taksii kumzungusha  kwa hao wanaume walioacha kumlipa.  Ikabidi  hata  masharti  aliyokuwa amemuwekea  yeye  mwenyewe Gabriel, kukiuka. Kutomtafuta yeye  mpaka Gabriel mwenyewe amtafute.  Tunda akaanza kutuma jumbe, bila  kupata majibu kabisa.  Siku zikazidi kwenda. Mwezi wa pili,  watatu, na wa nne tokea ukimya wa  Gabriel. Na muda wakulipa tena kodi  ukafika bila Tunda kukusanya pesa  hata nusu ya hiyo kodi.

Wasiwasi  ukazidi kumwingia. Ikambidi aingie  mtaani kusaka wateja kwa nguvu zote ili angalau kupata kodi tu. Akajiambia  mengine yanaweza kusubiri, ila sio kufukuzwa pale anapoishi.  Alihangaika mpaka alipokata tamaa.  Akaanza kumfuatilia tena Gabriel  kujua alipo. Kitendo cha kupita muda  wote huo wa miezi minne tokea  kumsikia na kumuona Gabriel kuliongeza wasiwasi usioweza kutamkika. Gabriel hakuwa  mtu wa kukaa kimya kwa muda mrefu  hivyo. 

Hofu aliyokuwa nayo Tunda, hakuwa  akiweza hata kupata usingizi. Alijawa  hofu ya nini chakufanya. Hakuwa na  tumaini tena na maisha yalikuwa  lazima yaendelee. Tena kwa haraka na  bili zilikuwa zikisubiri kulipwa. Akiba  yake aliyokuwa nayo alishalipia kodi  ya miezi ile ambayo Gabriel hakuwepo  nchini, aliposafiri na mkewe.   

Aliporudi Gabriel ndio ni kama  alikuwa akijikusanya tena na ndio Net  akaingilia. Akaja kulipa tena kodi  nyingine baadaye. Akajimaliza kabisa.  Sasa anafanyaje tena!  Hana ndugu wala rafiki wakumkopa  pesa au kumsitiri. Tunda alikuwa peke  yake hapa duniani. Hakuna hata  aliyejua anapoishi. Hana biashara  yoote anayojua na kuweza kuifanya  isipokuwa kuuza huo mwili ambao  umeanza kutumiwa kwa kukopwa.  Tunda alianza kuisha mwili kwa  wasiwasi.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Maji yalipofika shingoni, akaamua  kwenda ofisini kwa Gabriel.  Akaambiwa amesafiri kikazi yupo  jijini Arusha. Tunda alifurahi sana.  Kwani alishajua viwanja vyake vyote  Gab awapo jijini Arusha. Hakutaka hata  pakuche. Akarudi kwake, kufungasha  huku akiwa ameshampigia simu kijana  anayemsaidia kukata tiketi za ndege.  Akamsihi  afanye  juu  chini,  kuhakikisha anampatia tiketi ya  kumfikisha Arusha siku hiyo.  Akiwa nyumbani kwake anafungasha, yule kijana akamwambia amempatia  tiketi lakini akamtajia pesa kubwa kwa  makusudi akijua lazima atamlipa  sababu Tunda alimpigia akiwa  anambembeleza sana na kumuonyesha  ni muhimu. Hata hivyo alimjua Tunda  anayo pesa. Ni mteja wake wa muda  mrefu na huwa akimpatia tiketi, haachi  kumlipa za nyongeza kama shukurani.  Na kweli, Tunda hakumbishia.  Akamwambia anaitaka kwa bei yoyote  ile, amuwekee.

Akachukua taksii mpaka uwanja wa ndege. Pesa ndogo  aliyokuwa amebakiwa nayo kama  akiba, ndio hiyo hiyo aliyokuwa  akiitumia kwa garama zote hizo  kumfikisha Arusha akiwa na uhakika  itarudi tu punde Gabriel atakapoiona  sura yake.  Alifika Arusha kulikuwa na dalili ya  mvua. Akachukua taksii tena, moja  kwa moja kwenye hoteli aliyojua  lazima Gabriel atakuwepo. Hakuwa na  pesa yakutoshea kuchukua chumba  pale kwenye ile hoteli wala nauli  yakurudia. Hata pale alipokuwa akiishi  mwenye nyumba alishamwambia amepata ubalozi ambao unataka  kumkodishia mfanyakazi wao ile  nyumba kwa pesa kubwa zaidi ya ile  anayolipa Tunda kila baada ya miezi  mitatu. Alimwambia wao wapo tayari  kulipa kodi ya mwaka.

Kwa hiyo akamwambia inabidi aongeze kodi, na  baada ya week hiyo kuisha kama bado pesa yake haijaingia kwenye akaunti  yake, atatolewa vitu vyake nje, maana  ulishapita mwezi bila Tunda kulipa.  Kwa hiyo Gab pekee ndiye mkombozi  aliyebaki anayeweza kulipa mapesa  yote yale kwa mara moja.

Giza  lilikuwa limeshaingia, pale Tunda  alipokuwa akishushwa pale hotelini na  manyunyu  ya  mvua  yalianza  kudondoka moja moja. Alikwenda  mpaka mapokezi akamkuta muhudumu  anayefahamiana naye, akamwambia  Gabriel yupo upande wa bustanini  anakula. Tunda alifurahi sana.  Akaingia chooni akajitengeneza vizuri  ndipo akaelekea alipo Gabriel.   

Cha Mtu, Mavi.

A

limkuta Gab amekaa peke yake  pale mezani lakini kulikuwa na vinywaji vingine pale  mezani. Tunda alihisi hayupo peke  yake. “Gab!” Tunda aliita kwa upole  akitegemea Gabriel angefurahi sana  kumuona. Gabriel akasimama kama  mshale. Naomba uondoke Nancy,  hapa nipo na mke wangu. Maisha yetu  ya ndoa yanaendelea vizuri. Sitaki  uniharibie tafadhali. Nimetubu kwa  Mungu na mke wangu nimemwambia  mapungufu yake, amejirekebisha.  Ndoa yetu sasa hivi ina amani. Tena  hapa nipo na BF, mama yake na mke  wangu. Naomba uondoke kabla  hawajarudi.  Wameenda  msalani. Ondoka Nancy tafadhali.” Tunda  hakuwahi kumuona Gabriel huyu.  Alikuwa amehamaki. Mkali kama pilipili. 

Kwa shida alizokuwa nazo, ikabidi  ajikaze. “Nimeishiwa pesa, sina hata  shilingi! Nyumba yenyewe ninayoishi  wananifukuza. Pesa ya mwisho  niliyokuwa nayo ndio nimekata tiketi  ya kukufuata huku, hata pesa  yakuchukua chumba sasa hivi hapa  sina. Nitaenda wapi usiku huu na  ninaona mvua inaanza? Naomba  nisaidie.”Akiwa kwenye mshtuko wa  kufukuzwa vibaya vile, Tunda  alijikaza na kubembeleza kwa sauti ya  chini tu. Lakini wazi alisikika kama  anayetaka kulia. 

“Kwa nini uje bila taarifa Nancy!? Hilo sio tatizo langu. Naomba uondoke  tafadhali. Toka kabla sijakupiga.” Tunda aliumia sana, akajikuta akilia  nakushindwa kujizuia pale mbele ya Gabriel. Alikumbuka alivyofukuzwa  na mama yake bila baba Tom  kumtafuta tena. Gabriel hakuwa na  tofauti ya shukurani kwa Tunda kama  baba Tom. Wote walijua kumpamba  wawapo kitandani. Aliinama na kuficha  uso wake akilia mbele ya Gabriel,  asijue  anakwenda wapi usiku ule, huko arusha!? Manyunyu yakazidi kuongezeka.

“Nimekwambia ondoka Nancy. Na  usije kunitafuta tena.” Gabriel  aliongea kwa ukali zaidi huku akimsogelea Tunda kwa hasira kali  sana usoni. Tunda alishtuka sana  hakuamini kama Gabriel anaweza kupiga mwili huohuo aliokuwa  akiusifia  na  kumshukuru  kwa  kumtuliza akiwa na matatizo yake!  Akasogea huku anaficha uso zaidi asije  akampiga usoni huku akilia na kutetemeka. Tunda alikuwa kwenye  mshtuko mkubwa sana. Alitetemeka  mpaka mwili ulionekana ukitetemeka.  Kitu kilikuwa kimemkaba Tunda,  alishindwa hata kuongea tena ila  kujinusuru asije kuishia kupigwa pale. 

Akaamua aondoke tu. Wakati  anageuka ili aondoke alimuona Net  amesimama  pembeni  yao  akiwasikiliza.  Hakutaka  hata  kumsalimia, kwani hakujua amesikia  mangapi. Akaondoka pale akilia kwa  uchungu na aibu.  Akabaki  Net  na  Gabriel  wakiangaliana.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

v  Haya, historia inajirudia tena kwa Tunda.  Kama alivyoondoka vibaya nyumbani kwa  bibi na babu yake, baba yake mzazi, baba  Tom, Shangazi yake, ndivyo anavyofukuzwa tena na Gabriel aliyebaki tegemeo lake pekee. 

v  Anakaribia kufukuzwa kwenye hiyo nyumba  aliyokuwa akiishi kwa kulipa kodi kwa dola,  ambako hapajulikani. Tena nyumba yenyewe  imejaa vitu vya thamani vitupu! Hana ndugu,  hana rafiki wala sehemu si ya kuhifadhi hivyo  vitu vyake tu, hata yeye mwenyewe. Hana shule kichwani, hana biashara yeyote  inayoweza kumwingizia kipato, na mbaya  zaidi safari hii hana hata pesa ya kuanza  chochote. 

v  Akiwa hospitalini baada ya kufukuzwa kwa  shangazi yake nusu mfu, baba yake mzazi alimuachia pesa hospitalini iliyomsaidia  kumkutanisha na Sadiki. 

Sadiki amekufa, akamuachia hivyo vitu vyote  vya thamani na pesa iliyomkutanisha na  Kinny. Sasa safari hii Tunda yupo peke yake  kwenye jiji la ugenini. Hauziki tena.  Safari hii Tunda atafanyaje? 

Usikose mwendelezo wakusisimua zaidi. Ndio mambo yanazidi kupamba moto. Endelea kuwa na Tunda. 

CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment