![]() |
A |
kiwa
hata hajui anaanzia wapi kumsaka huyo
Gabriel. Lakini akili yake, hisia zake zilimwambia lazima ampate tu, ikawa kama
yeye ndio amebeba mjibu yake yote. Tunda anamtaka kwa hali na mali. Akiwa njiani kurudi Dar, akaanza kumsaka kwenye
mitandao ya kijamii ili kupata habari
zake kamili. Kumfahamu kwa undani zaidi.
Angalau kujua chanzo cha pesa yake.
Akaperuzi jina lake mpaka kwenye
magazeti. Kila mahali aliandika jina
lake kamili. Kwa kuwa alikuwa na pesa,
habari zikawa zinamfikia Tunda kwenye
kiganja cha mkono wake na kuzisoma kwa
makini sana bila kupuuza chochote.
Mpaka anatua uwanja wa ndege wa jijini Dar, akawa
ameshamfahamu Gabriel kwa asilimia kubwa
tu. Kuwa ni mtu ambaye yupo busy sana
kwa kuwa anamiliki biashara mpya na
ngeni ya chakula kimoja kikubwa nchini,
burger ya aina hiyo aliyoanzisha yeye.
Alisambaza migahawa yake nchini
kwa aina hiyo moja ya chakula. Burger G ndio jina la hiko
chakula kilichoonekana kupata walaji wengi sana. Kuanzia ladha na ufungwaji
wake kama hutaila hiyo burger pamoja na chips zilizokuwa zikikatwa kwa muundo
wa kipekee, kwenye moja ya hiyo migahawa yake.
Wengine walipenda na aina hiyo mpya ya
chakula cha onion rings pamoja na aina
za wings yaani vipapatio vya kuku vilivyokuwa vikitengenezwa kwa ladha
tofautitofauti. Hayo yote Tunda akayapata kwa kina na kushangazwa sana. “Alijificha wapi huyu
kiumbe hadimu!?”
Akajiuliza Tunda wakati akiendelea
kumsoma. Akagundua pia huwa
haendi bar wala kumbi za starehe. Mtu
aliyeshika dini sana. Na habari
iliyopamba vichwa vya habari vingi ni
ile tabia ya siku za jumapili migahawa yake yote kufungwa na wafanyakazi
wake wote wanatakiwa kupumzika siku nzima,
kwa ajili ya kumwabudu Mungu. Na yeye mwenyewe Gabriel siku zote za jumapili lazima awepo kanisani na familia yake. “Ndio maana!” Tunda akacheka.
Tunda hakuwahi
kuingia kanisani hata mara moja.
Aliweza kuingia kila mahali, lakini sio
kanisani labda kipindi ni mtoto, akiwa
anaishi na mama yake mzazi. Baba Tom alikuwa akilazimisha, lakini alipomzoea, aliweza kumkatalia
kwenda nao kanisani. Akawa anabaki
tu nyumbani siku za jumapili wakati
familia ya mama yake wakienda
kanisani. Hakuja kurudi tena huko
kanisani. “Nampataje
huyu kiumbe hadimu hapa mjini?” Swali lililomsumbua
Tunda ambaye muda haukuwa upande
wake.
Mteja wake wa Arusha alikuwa akimsubiria arudi jijini Arusha baada ya siku tatu. Na alijiambia hawezi kurudi bila kumnasa Gabriel ambaye wengi
walimtabiria huko kwenye mitandao ya
kijamii kuwa hatafika mbali, atafilisika
tu kwa tabia yake hiyo ya kufunga biashara zake
siku hizo ambazo wafanyabiashara
wengi hutegemea kuingiza pesa yeye alifunga sababu ya kumuabudu Mungu!
Chakushangaza wengine walitoa tathimini ambayo Tunda hakujua kama ni ya kweli
au uongo, ilielezwa yeye ndio
mfanyabiasha wakwanza wa migahawa
anayeingiza pesa nyingi zaidi tena akiwa
ametoa hiyo siku moja ya jumapili, kwa
juma. “Sasa kabla hajafilisika, na
mimi ninufaike.” Tunda akajisemea.
Atafutaye
Hachoki.
Tunda aliamka siku inayofuata akaenda kubadilisha aina ya nywele kichwani mwake, na kuweka nywele ambayo alijua wanaume wengi huvutiwa nayo. Ilikuwa wiving ndefu ya mawimbi. Alipendeza na hiyo nywele na alikuwa ameinunua kwa pesa nyingi haswa.
Akiiweka kichwani, utafikiri ni yake.
Na alimpata dada aliyejulia kichwa
chake, hakuwa akibadilisha mtu
wakumtengeneza ila yeye tu. Aliporidhika kuwa amependeza, ndipo akaweka mkakati wakumsaka huyo Gabriel.
Aliamua kwenda ofisini kwake akiwa
ameshamjua kwa asilimia kubwa.
Bado biashara kubwa aliyokuwa akijua Tunda anafanya huyo Gabriel ni hiyo ya chakula aina hiyo ya burger. Akajua watu
husifia chips, onion rings na wings walizokuwa
wakiuza kwenye migahawa yake. Na
wengine walisifia aina za juisi na
icecream za kwenye hiyo migahawa
yake pia. Walisema ilikuwa tofauti kabisa na sehemu nyingine. Basi Tunda akaona anazo habari zakumtosha kuanzia kumtega huyo mfanyabishara mcha Mungu, Gabriel.
Alifika ofisini kwa Gabriel, lakini sekretari wake alimkatalia katakata kuonana naye akamwambia nilazima awe na miahadi naye. “Unaweza kuja juma lijalo siku ya jumatano, saa nane mchana, atakuwa na nafasi
na mimi nakuweka wewe wa kwanza.” Yule
sekretari aliongeza huku akiangalia
ratiba ya bosi wake. “Naomba ukamwambie Nancy
anashida yakumuona, tafadhali. Akikataa nitaondoka bila kukusumbua.” Yule sekretari
akakubali kwa shingo upande huku
akihofia isije kuwa mtu muhimu sana
kwa bosi wake, akaja kujua baadaye
kama amemkatalia hata kufikisha ujumbe, akaingia matatizoni.
Akaamua kwenda kumwambia kama Tunda alivyomtuma.
Akiwa hajaelewa bado huyo Nancy ni nani,
akaonelea kutaka kwenda kumuona ilipengine sura imkumbushe. Gabriel kijana
huyo mwenye majukumu mazito, alitoka ofisini. Akakutana na huyo Nancy. Macho
yakagongana na Tunda. Akatulia kidogo Gabriel, mwishoe akaamua kuuliza. “Sijui tumeshaonana kabla?” Gabriel aliuliza akiwa na uso wenye maswali kidogo. “Huwa unaongea na watu unaowafahamu
tu?” Tunda akauliza na uso wa tabasamu,
uliojaa kujiamini. “Hapana, samahani. Nipo
kwenye kitu cha msingi sana.”
“Sitachukua
muda wako leo, naomba uniambie ni
siku gani tunaweza kuonana,
tukaongea vizuri.” Gabriel alifikiria
kidogo kisha akaonelea kuuliza tu.
“Ni juu ya mambo ya kazi au?”“Naomba nijibu hilo
siku tutakayokutana.”
Akiwa na
mshangao mbele ya sekretari wake na
binti huyo mrembo wa kuvutia,
aliyemsimamia mbele yake ilibidi Gabriel
au Gab kama wengi wa marafiki
wakaribu walivyozoea kumwita, akubali
kuonana naye siku inayofuata jioni.
“Sijui saa kumi na mbili jioni itakuwa
sawa kwako? Maana naona nitakuwa
busy sana. Nikifikiria ni muda gani
nikupenyeze kwenye ratiba yangu, ni
huo muda baada ya kazi.” Gabriel akamalizia huku akimtizama kwa makini.
“Wapi?” “Hapa hapa ofisini.”
“Sawa.”
Tunda
alihakikisha anaondoka Gabriel akiwa anamtizama. Alibaki amemkodolea macho Tunda mpaka alipotoka kabisa nje ya mlango. “Samahani.
Sijalipata vizuri jina lako.” Gabriel
alimkimbilia Tunda mara alipotoka nje. Tunda akatabasamu na kumgeukia vizuri. “Gafla kasahau jina!” Tunda akawaza. “Naitwa Nancy.” Akajitambulisha na kumpa
mkono. Gabriel akaupokea mkono laini
wa Tunda. “Nafurahi kukufahamu
Nancy, naitwa Gabriel lakini marafiki
zangu wengi wananiita Gab. Hapa
ndipo ilipo ofisi yangu kubwa,
nyingine zipo..” Gabriel akaendelea
kujieleza kama aliyechanganyikiwa huku Tunda
akimwangalia kwa macho yake matulivu. Kulikuwa na kitu cha tofauti sana kwa Tunda, alikuwa kama na sumaku kwa wanaume. Alijua wazi mwanaume akishakubali kumsikiliza tu, hataweza kuchomoa, hasa akiamua yeye.
Mwishowe Gabriel akaamua kunyamaza. Akamuachia mkono, akawa kama amejishtukia. “Nimefurahi
kukufahamu Gab.” “Asante sana kwa kuja
kuniona. Kwa hiyo umesema leo saa kumi
na mbili ndio utakuja?”
Gab
akajichanganya. “Nilifikiri ulisema kesho!”
Tunda aliongea kwa upole na tabasamu. “Nina mambo fulani ninafanya sasa hivi,
lakini huwa sekretari wangu anatoka saa
kumi na nusu jioni, na hapo ndio naacha
kupokea simu kabisa. Unaweza kurudi
jioni?” Gab akauliza kwa kubabaika sana.
Tunda akamzuga kwa kufikiria kidogo huku
akiangalia kalenda ya simu yake na
kumjibu. “Naweza kutengeneza muda kwa
ajili yako Gab.” Gabriel alianza
kuchekacheka.
“Samahani sana kwa usumbufu, najua hii nenda rudi, sio
kitu kizuri. Lakini naamini jioni
tutapata muda mzuri.” “Hamna
shida.” “Nikuitie taksii.” “Hapana Gab. Nipo na usafiri wangu. Asante tutaonana
jioni.” Tunda akaondoka,
asiamini kilichomtokea. Alitegemea ugumu mkubwa sana kwa Gabriel. Alishajaribisha kuzungumza na huyo Gabriel mbele ya kioo cha chumbani kwake. Akaona amekosea. Akajaribisha kioo cha bafuni kwake. Akajaribisha tena jinsi ya kuzungumza naye kabla hajatoka nyumbani kwake akiwa sebuleni. Akajaribu tena na tena mpaka
akaridhika, ndipo akaita Uber. Kuja
kukutana na Gabriel mwenyewe ndiye anayemuomba msamaha kwa usumbufu!
Akapunguza mukari kabisa.
“Naweza kula toto ya kanisani, mchana kweupee.” Tunda akajisemea na kucheka akiwa kwenye taksii iliyokuwa ikimrudisha Mlimani city.
Ile taksii hakutaka imfikishe kwake,
kwa kuwa aliichukua palepale nje ya
ofisi ya Gabriel. Hakutaka kufanya
kosa. Kama kawaida, akashushwa na
hiyo taksii hapo, akazunguka kidogo
pale Mlimani city, akatoka kabisa pale
kwenda kutafuta usafiri mwingine nje kabisa ya viwanja vya Mlimani City,
wakumrudisha nyumbani kwake.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Ilipofika jioni ya saa 12 Tunda alirudi ofisini kwa Gabriel, na kumkuta Gabriel peke yake pale ofisini. “Mbona upo peke yako?” Tunda akauliza wakati anaingia kwenye ofisi ya Gabriel. “Mfanyakazi wa mwisho huwa anatoka saa kumi na moja kamili.
Huwa napenda kubaki
peke yangu ili kumalizia kazi zangu
bila usumbufu. Na ndio muda wangu
wakufikiria na kujipangia ratiba ya
kesho. Karibu.”
Akamkaribisha Tunda. “Asante.”
“Utapenda
kunywa nini?” “Red wine.” “Oooh! Hapa kwangu siweki pombe kabisa.”
“Kwa nini?” “Sipendi pombe.”
“Basi naomba
fanta orange.” Tunda alivaa gauni lililomfika magotini na
lilikuwa na rangi angavu kidogo.
Kwa hiyo kukaa
kwake kwenye kochi kulisababisha lile
gauni liwe kwenye mapaja na zile
rangi zilivutia kuangalia juu ya mwili
ule Mungu aliouweka rangi nzuri
nyeusi halafu Tunda akaifanya ile
rangi kuwa ya kipekee. Hayo mapaja
yalikuwa yakifanyiwa Waxing.
Usingekuta kipele wala kinyweleo.
Safi wakati wote kama mtoto
mchanga. Na ili kuhakikisha Gabriel
anaona alichomkusudia, hakuacha
kulivuta chini hilo gauni huku akihangaika pale kwenye kochi. Gabriel
alijitahidi macho yake yasishuke chini
ya uso wa Tunda aliyejitambulisha kwa
jina la Nancy.
Alimsogezea
soda akammiminia kwenye glasi na kumkabidhi Tunda. Wakati Tunda anaipokea aliipindua ile glasi
kwa kusudi, soda yote ilimmwagikia
kuanzia juu mpaka chini kwenye lile
gauni zuri alilokuwa amevaa. “Ooh
my goodness! Nitafanyaje? Nitatokaje hapa? Ona nilivyoloa mwili mzima!” Tunda aliongea kwa sauti ya kulalamika na imejaa deko, tena kwa lugha ya kingereza kizuri sana. “Samahani sana Nancy, sijui nimeshikaje hii glasi! Labda
uingie hapo chooni kwangu ujaribu
kujisafisha.” Tunda aliingia hapo chooni ndani ya hiyo hiyo ofisi na kuvua lile gauni kabisa. Mbali na chupi hakuwa amevaa kitu kingine ndani.
“Sijui hata
kama litafaa jamani!” Gabriel
alimsikia Tunda akilalamika huko
chooni. “Samahani sana.” “Hivi una taulo? Nataka nijisafishe kidogo, mwili mzima
unanata kwa sukari ya soda!” “Vipo vitaulo vidogo vya kukaushia
mikono. Sijui vitafaa?”
“Itabidi tu.
Viko wapi?” “Huwa wanavipanga hapo kwenye kabati la juu.”
Tunda alifungua kabati na kukuta vitu vingine humo ndani, akijua kabisa silo kabati aliloelekezwa aliangusha zile chupa mle ndani
makusudi tu. Akajilalamisha kama
aliyejiumiza tena. “Aiii!”
Gab akakimbilia huko ndani alipokuwa Tunda, akamkuta
amevaa chupi tu, akilalamika maumivu yakujigonga huku akijaribu kuokota vitu
alivyodondosha sakafuni. Gab alipigwa na
butwaa, akabaki amekodoa macho. “Mbona hunisaidii jamani!?” Tunda akajilalamisha. “Samahani sana.”
Gab aliinama
na kuanza kuokota vile vitu alivyoangusha Tunda chini huku Tunda
ameshikilia kipanda uso chake.
“Vipi, umeumia?” “Hiyo chupa imenigonga
hapa.” “Tuone.” Gabriel akasogea, huku akitetemeka. Tunda alikuwa
uchi, matiti yake
ameyashikilia kwa mkono mmoja, kitu
alichotamani kama angeachia tu ili
afaidi kote. “Pole sana. Kuna uvimbe
kidogo. Twende ukalale pale kwenye
kochi nikuwekee barafu hapo kichwani.”
Tunda alicheka moyoni alijua Gabriel
ameshanasa, kwani hakuwa wala
amejigonga na kitu chochote. Alidanganya tu.
“Gauni lenyewe wala
halijatakata!” “Usijali, nitakusaidia kulisuuza. Tangulia ukapumzike pale kwenye kochi, mimi nikusafishie.” Tunda alienda
akajilaza kwenye kochi akiwa na chupi tu, tena chupi yenyewe ilificha mbele na
nyuma tu. Pembeni vimikanda vyembamba.
Hiyo hips hapo pembeni na ulaini wa
muonekano wa hilo paja. Usingeacha
kutizama. Rangi moja mwili mzima.
Ofisini ni maeneo yake
yakujidai pia. Alishatumiwa huko
na baba Tom, kuanzia mtoto mpaka
utuuzima. Hana asichojua kufanya endapo
akitakiwa kutumika hata hapo ofisini.
Iwe mezani, kwenye kiti cha ofisi au
hata kwenye makochi hayo. Alilala hapo
akimfikiria Gabriel aliyekuwa akimfulia hilo gauni huko bafuni. “Nimuweke wapi huyu kiumbe?”Akajiuliza Tunda
akiwa amejilaza na chupi tu pale
kwenye kochi.
Baada ya muda Gabriel alitoka na kitaulo kidogo na barafu kwenye kikombe. Akamkuta vile vile Tunda amejilaza. Akaenda kupiga magoti pembeni yake na kuanza kumkanda Tunda usoni. “Aaauu!” Tunda akajilalamisha
maumivu. “Pooo.” Gab alisafisha koo baada ya kupaliwa na mate. “Pole sana.” Tunda alimuona jinsi hali yake ilivyokuwa mbaya, lakini alimuacha mpaka yeye mwenyewe aanzishe. Akaendelea kumkanda hapo kwenye kipanda uso huku anazidi kutafuta jinsi ya kuweka mkono mwingine maana alianza kutumia mkono mmoja wakulia tu. Wakushoto ukawa unahangaika. Mara juu kichwani, mara pembeni ya kochi. Tunda alikuwa pale kwenye kochi akili zimezama kwenye maumivu yake.
Mlio wa taratibu akitetemeka ule ubaridi wa
barafu uliendelea taratibu. “Aaaa,
baridi!” “Pole.” Akajidai anamsugua
mabegani kupunguza baribi. “Asante.” Tunda akashukuru
taratibu. Macho yakagongana. Gab
akazubaa hapo kidogo. “Karibu.” Akajibu kwa sauti yakulemewa na mrembo huyo. Alishagonga hayo matiti mara kadhaa wakati akimkanda hapo kwenye kipanda uso. Alishaona hicho kiuno chenye
cheni, chembamba kilichoshikiwa na hayo mapaja. Taratibu kule kumsugua mabegani na mkononi kumpa joto, kukaongezeka.
Alipoona ameanza kumpapasa, Tunda alijua tayari. Ilikuwa ni mwiko kwake kulala na mwanaume bila kondomu. Alikaa taratibu na kumsogelea pale alipokuwa amepiga na magoti
kumuashiria yeye ndio alale. Bila kujielewa, Gabriel alipanda yeye kwenye kochi, Tunda alitumia utundu wote kumridhisha bila kufanya naye tendo
la ndoa. Alikusudia
kumchelewesha kumfikisha, makusudi
tu ili kuendelea kumchezea kwa muda
kidogo.
Kwanza Gabriel mwenyewe alikuwa akivutia. Tunda alishavutiwa naye. Gabriel alikuwa ni miongoni mwa vijana wachache Tunda aliovutiwa na maumbile
yao. Kuanzia nje mpaka ndani. Kwanza
alikuwa akinukia vizuri, mwili mzuri wa
kiume, msafi mpaka ndani. Halafu pesa
huwa inamtindo wakuongeza ladha
yake kwa mtu. Tunda mwenyewe
aliyekuwa akimchezea, akajikuta
akinogewa yeye mwenyewe, mpaka
akatamani kulegeza masharti,
lakini akakaza roho. Muonekano wake pale
kwenye kochi, Tunda alimfurahia.
Gabriel
alikuwa akionekana kufurahia sana
alichokuwa akifanyiwa na Tunda.
Miguno ya kulalama ilipozidi kama
anayeomba rehema za Tunda, ndipo
Tunda alipomuhurumia, akamfikisha.
Alipomaliza kabisa, ndipo Tunda
akamwachia na kukaa pembeni. Na
ndipo akili yake Gabriel ilipomrudia na
kuanza kubabaika pale kwenye kochi. “Sijui
imetokea nini! Lakini mimi ni mtu
ninayejiheshimu sana, Nancy. Usifikiri
ni mtu ninayelala hovyo na kila
mwanamke. Nampenda sana mke wangu. Nina..”
Gabriel alianza kujitetea na kuongea
mfululizo huku Tunda akimtizama
kwa utulivu bila kuongeza neno.
Mwishoe Tunda akasimama. Akaenda kuvaa
nguo yake ikiwa vile vile mbichi,
nakutoka ofisini kwake.
“Mbona unaondoka sasa?” Gabriel alisimama na
kumkimbilia. “Ulitaka
nifanyaje sasa? Naona unaongea
habari za mkeo tu, na kulalamika kwa
kitendo ulichofanya wewe mwenyewe! Ulitaka kuniingilia lakini
nikakataa, nimekusaidia, naona
unanitupia mimi lawama! Hujajua nini
kimenileta hapa, na wala hatujazungumza!” Tunda akamgeuzia yeye kibao
na kumuongezea hukumu. “Samahani Nancy. Nahisi
nimepaniki. Unajua tokea nimeoa,
sijawahi kulala na mwanamke mwingine isipokuwa
mke wangu tu. Nahisi ni hukumu tu ndiyo inanisumbua. Kuona nimeweza kukuvulia nguo, tena wewe mwanamke mgeni kabisa! Naomba usinielewe vibaya kabisa. Hii siyo tabia yangu,
nimeruhusu tamaa ini..”“Usijali
Gabriel. Mimi ni mtu mzima, naelewa.
Tutaonana wakati mwingine.”
“Mazungumzo yetu?”
Gabriel
akauliza na wasiwasi usoni. “Naomba utulie kwanza. Naona bado upo kwenye mshtuko. Nakuachia namba yangu ya simu, utanipigia utakapoona upo tayari kwa mazungumzo.” Tunda aliandika namba yake kwenye kikaratasi alichokuwa amekiona pale kwenye meza ya
mapokezi, akaondoka asiamini wepesi
aliokutana nao kwa Gabriel. Hakutegemea
kumvua nguo kwa haraka kwa kiasi kile! “Daaah! Nimejikubali.” Tunda alijipongeza na kucheka akiwa anarudi nyumbani kwake na gauni hilo bichi.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Kesho yake asubuhi, Tunda akapanda ndege kurudi jijini Arusha kumalizana na mteja wake. Hakutaka kuwa muongo kwa mteja yeyote yule. Alikuwa mwaminifu wa muda na maneno
yake pia. Na hilo
nalo walimpendea. Mteja wa safari hii alikuwa ni mtumzima kidogo, mwenye asili ya kiasia, anahusika na mambo ya madini. Alipotua tu uwanja wa ndege akampigia simu kuwa anaelekea hotelini. Akamwambia atamkuta akimsubiria. Alipofika tu, Tunda akamtuliza kwa mchezo wa raundi kama mbili, akatulia na kusamehe kumuacha kwa siku hizo. Wakaendelea kuwepo naye hapo hotelini huku akisubiria simu kutoka kwa Gabriel.
Alipoona kimya, akaanza kujilaumu akihisi hakutumia ujuzi wake ipasavyo kwa Gabriel. Alirudi Arusha na yule mteja
wake akawa amemaliza
kilichompeleka hapo, siku ya tatu yake wakarudi Dar. Ilikuwa jioni.
Alimlipa pesa nzuri sana. Tunda
mwenyewe akashangaa. Hakutegemea, tena
ni mteja aliyemdharau tu.
Alimtongoza akiwa hayupo hata
mawindoni. Alikuwa anakula tu mgahawani,
na yeye akaenda kukaa pembeni yake. Tunda akamtizama na kumpuuza. Kwanza hakuwa na asili ya Kitanzania. Tunda hakuwahi kufikiri kuja kulala na watu nje ya watanzania. Akajiongelesha kwa muda huku Tunda akila.
Alipomaliza, muhudumu alipomletea bili, akaomba alipie yeye. Tunda akacheka. Akamwambia yeye ni mgeni hapo
Dar, anatafuta mwenyeji. Aliongea
kingereza chenye lafudhi ya kiasia.
Tunda akacheka na kumwambia kwa kuwa
amekuwa mwema kwake, yeye
atamzungusha mjini kidogo.
Na kweli, walitoka na Tunda, wakaanza kutembea. Akamsindikiza sehemu mbili tatu, kisha akamuomba warudi naye kwenye hoteli aliyofikia. Tunda hakujua hata kama anayo pesa. Bado hakuwa amemwambia ni nini anafanya pale nchini na kama kawaida ya
Tunda, hakutaka kujua
yasiyomuhusu, akaona amzungushe tu.
Akimdharau wala hakumpa umaana anaostahili. Kwanza alikuwa mkubwa kwa umri na kwa kuwa hakuwa amevaa chochote cha thamani, Tunda akaona aende naye tu, akaonje yakigeni huku
akijua anampeleka sehemu ya hovyo. Alishangaa hoteli aliyofikia. Ilikuwa nzuri na ya pesa nyingi. Kidogo Tunda akaanza kumtizama kwa jicho la pili. Kuja sasa kuingia humo ndani ya hicho chumba alichokodi, Tunda akamshangaa na kucheka. Hakuamini kama anaendana na yale mazingira mle ndani.
Akamwambia huwa anafanya vile ili kuwa huru kuzunguka ugenini na kuweza kuzungumza na yeyote bila kuvutia wezi. Alimwambia wakati mwingine, ‘tajiri hana tofauti na mtumwa’. Kwa hiyo akamwambia wakati mwingine huwa anajishusha ili kuweza kuwa huru na kupokelewa na yeyote kirahisi.
Walikaa humo ndani wakizungumza machache na Tunda, mwishoe akamuomba penzi kiustarabu. Tunda akampa mchezo aliovutiwa nao na kumuomba wasafiri siku inayofuata. Walilala usiku huo, kesho yake Tunda akarudi nyumbani kwake kuchukua nguo za kuvaa huko Arusha na baadhi ya vitu. Ndipo jioni yake wakasafiri pamoja kwenda jijini Arusha na kumuona Gabriel. Waliachana na Tunda palepale uwanja wa ndege wa Dar siku hiyo waliporudi, akimwambia kesho yake anarudi nchini kwake.
Gabriel!
Tunda akarudi kwake akiwa amefurahia pesa aliyoingiza, lakini ukimya wa Gabriel ukaanza kumchanganya. Akiwa ndio amepanda tu kitandani siku hiyo hiyo ametokea Arusha, amejilaza kitandani kwake, usiku. Akaona ujumbe unaingia kwenye simu yake. ‘Nimepata safari ya gafla nipo Mwanza. Nikirudi nitakutafuta.’ Tunda akajua ni
Gabriel. Alifurahi mpaka akakaa. Akafikiria kwa haraka akaamua kumjibu. ‘Hata mimi
nipo Mwanza. Ukipata nafasi naweza
kukufuata ulipo.’ Baada ya muda simu ya Tunda ilianza kuita.
Tunda alicheka kisha akapokea. “Kama sasa hivi nipo tu hapa hotelini.
Nimerudi kama lisaa limoja lililopita.
Na sina mpango wa kutoka tena. Unaweza
kuja tukaongea?”
“Kuna mtu naonana naye usiku huu, Gab. Sijui tutachukua muda gani.
Na ndiye aliyenifanya nije huku Mwanza.
Nikimkosa leo sitampata tena. Yuko busy
sana. Tunaweza kuonana kesho au kesho kutwa
kama utakuwa una nafasi bado. Mimi nitakuwepo huku Mwanza kwa kama juma moja hivi.” Tunda akadanganya.
“Basi naomba tuonane kesho, Nancy. Sipendi kuingilia mipango yako.” Tunda akacheka
kidogo. “Mzima lakini? Mbona unasikika kinyonge hivyo?” “Aaah! Dunia hii, inamambo
kweli! Wewe acha tu.” “Nina kama dakika ishirini ndipo nionane
na mwenyeji wangu, tunaweza kuongea tu.”
Tunda aliongeza kwa sauti ya
kumuhurumia. Kwa sauti tulivu ya
Tunda, Gabriel akajikuta akieleza mambo
mengi mwishowe akaishia kueleza
mikwaruzano aliyonayo kwenye ndoa yake na jinsi
alivyomvumilia mkewe.
“Kwa nini usitafute msaada wa wazee?” “Siwezi hata kumwambia mtu.
Sisi ni viongozi pale kanisani. Ndoa
yetu ndio mfano wakuigwa mbele ya watu.
Yaani tunatolewa mifano kata kwenye
mahubiri. Leo tunawaambia vipi watu tuna
matatizo? Si tutawavunja moyo washirika
wengine?” “Pole sana Gab!” Tunda alimliwaza Gabriel mpaka akatulia. Waliagana Gabriel akiwa anacheka. Kwa mara ya
kwanza, Tunda akajikuta amevunja sharti
lake yeye mwenyewe. Kupokea simu ya mteja na kusikiliza matatizo yake kwa muda mrefu na kumliwaza. Lakini alishavutiwa naye.
Mwanzo wa
Mengi, Jijini Mwanza.
Tunda&Gab.
S |
iku
inayofuata asubuhi na mapema, Tunda
alipanda ndege kueleka jiji Mwanza
kumfuata Gabriel. Alipotua tu uwanja wa
ndege wa jijini Mwanza, akampigia simu.“Vipi Gab, unaendeleaje?” “Kwanza nataka kukushukuru
Nancy, umekuwa msaada wangu mkubwa.
Umenifanya nilale vizuri sana jana usiku.” Tunda akacheka kwa pozi.
“Afadhali kama uliweza kulala.
Wakati wowote ukiwa na shida unaweza
kunipigia. Umekula sasa?” “Kuna kitu
namalizia hapa, halafu kuna watu
watakuja tufanye kikao kifupi, wakitoka tu nitakutafuta ili twende
tukale.” Tunda
alitamani kuruka kwa furaha.
Akatafuta mgahawa akakaa hapo akisubiria simu ya
Gabriel. Ilipofika saa 9 mchana, Gabriel
akampigia nakumwambia yeye anafahamika sana. Hawezi kuonekana hadharani na mwanamke mwingine mbali na mkewe, akaomba amfuate hotelini kwake, ili wale chakula chumbani kwake. Lilikuwa ni kosa kubwa sana. “Una
uhakika Gab? Kama itakuletea matatizo,
sio lazima tukaonana. Tunaweza kuongea
kwa simu tu.” Tunda akamringia
kidogo. “Hapana. Hamna shida kabisa. Nitafurahi kukuona Nancy. Tafadhali
usiache kuja.” “Basi kwa kuwa wewe unafahamika.
Na wameshakuona upo hapo hotelini peke
yako, sidhani kama ni sawa wakiona na mimi naingia chumbani kwako. Kwa nini usinifuate
mimi hapa hotelini kwangu? Nafikiri itakuwa
salama.” Wazo
likawa zuri sana. Akamkubalia kwa haraka
sana.
Tunda alimwambia wakutane baada ya dakika 45 ,
angempigia simu atakapofika hapo hotelini kwa kuwa alikuwa mbali kidogo na kwenye hiyo hoteli
aliyokuwa amefikia. Akamdanganya alikuwa ametoka kikazi hapo hotelini tokea asubuhi. Gabriel akakubali. Kwa kuwa Mwanza ni kama uwanja wa nyumbani tu kwa Tunda,
hakupata shida kupata hoteli.
Alishafikishwa huko na wanaume
mbali mbali. Alijua hoteli ipi unaweza
kujificha na mtu wa mtu, na
usikamatwe.
Kwa haraka bila kupoteza muda, Tunda akachukua taksii mpaka kwenye moja ya hoteli aliyojua akienda huko hatakamatwa. Nia ilikuwa na
kumlinda Gabriel mwenyewe pia.
Alishamjua Gabriel ni kuku mgeni. Sio
mwizi. Akaona wakikamatwa kabla ya hajamuweka sawa, anaweza kumkosa moja kwa moja.
Akataka akamkoloze kwanza, akimuachia awe anajua njia yakurudia.
Alifika kwenye hoteli hiyo tulivu, pembezoni kabisa ya ziwa. Mandhari na umbali uliopo, lazima uwe na shuguli maalumu kukupeleka huko kama sio siku ya weekend wengi wanapoenda
kuogelea. Uzuri ilikuwa ni siku katikati ya juma. Nani wa kuwafuata huko! Bei
yakulipia tu usiku mmoja hapo, alijua
watu wa hali ya chini hawafiki huko
vyumbani. Akajua hata kama watafika, ni
weekend tena sehemu ya kuogelea tu. Sio
huko vyumbani. Akajiambia
akimfungia huko Gabriel siku mbili tu,
na kumuachia, yeye mwenyewe ataanza kumtafuta kama mwehu. Alichagua chumba kinachoangalia ziwa. Kizuri. Ndipo akampigia tena Gab, kumwelekeza upande uliopo hiyo gorofa alipokokodi hicho chumba na sehemu zilizopo ngazi za kuelekea huko juu gorofani kwenye chumba moja kwa moja. Akamuelekeza na upande chumba chenyewe kilipo pindi atakapofika kwenye hiyo gorofa. Alimwambia anampunguzia kupita mapokezi au kuuliza kwa yeyote.
Alitaka apite moja kwa moja, asishangae shangae hapo mpaka watu wakamuona na kumtambua kama ni yeye yuko pale. Gabriel akaelewa na kufurahia
vile anavyolindwa na Tunda. Hapo hapo
Tunda akaanza kupanga vitu vyake kwenye
meza na droo za hapo chumbani, ili
kumuonyesha Gabriel alikuwepo hapo tokea
zamani huku akimpigia mahesabu jinsi
ya kumbana mpaka usiku ule alale
naye pale, asiondoke. Swala lakumchomoa pesa akajiambia litasubiri. Akajiambia ni kama anawekeza kwanza kwake mpaka atakapomkoleza amchomoe pesa atakavyo.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Baada ya muda Gabriel aliingia pale, akakuta Tunda ameshanunua vyakula. “Sijui
nimekosea kukuchagulia chakula cha kula?” Tunda akauliza na tabasamu
zuri, huku akimrembulia. “Hamna shida
kabisa. Hivyo ndio nimefurahi. Nachukia
swali la ‘ungepeda kula nini! Huwa
nalikwepa sana.” Tunda akacheka.
Akaingia bafuni, akaosha mikono akarudi
kukaa kwenye meza. Gabriel alianza
kwa maombi, kitu kilichomfanya
Tunda acheke moyoni. Aliombea chakula
na mazungumzo yake na Tunda. Tunda naye alifunga macho akimtafakari Gab. Alipomaliza kuomba wakaanza kula taratibu wakiongea hili na kucheka lile pale sehemu ya mezani.
Taratibu Geb alianza kumlalamikia tena mkewe. Walihamia kwenye kochi baada ya kumaliza kula. Tunda akaanza
kumfariji tena huku
akimtizama kwa macho yake matulivu,
akimuhurumia. Kama kawaida yake,
muda wote huo anakuwa mtulivu sana.
Msikilizaji
mkubwa asiyeingilia. Na usipokuwa
makini, unaweza kuongea mpaka ya ndani
sana. Yeye kimya akikusikiliza kwa
utulivu. Alipoona hamalizi habari zake
na mkewe, akaona afupishe mambo. “Hebu jinyooshe kwanza hapa kwenye kochi. Vua viatu, unaweza kubaki na soksi tu.” Gabriel akavua bila swali au kubisha.
Tunda alinyanyua miguu yake nakuanza kuichua taratibu huku Geb akiendelea kuongea kama yupo kwa mshauri wa ndoa. Kwa utulivu ule wa Tunda, Geb alijikuta akiongea mengi tena ya ndani akiwa amejinyosha kwenye kochi na miguu yake ipo mapajani kwa Tunda akionyesha
uso wa kumuhurumia huku moyoni akitamani
amalize lakini Gab aliendelea kulalamika.
“Tuliza mawazo Gab, naamini kila kitu kitakuwa sawa. Jaribu kutumia njia nyingine kwa mkeo.” “Kama nini Nancy?
Nimejaribu..” Tunda aliendelea
kucheza na miguu ya Gabriel mpaka
alipomuona maneno yanapungua, safari za
chooni haziishi. Mara ya mwisho alirudi
amevua soksi. Akajirudisha kwenye kochi na miguu akaipandisha tena mapajani kwa Tunda. “Nashukuru naona masaji unayonifanyia, inanisaidia kutulia.” “Unataka ya mwili mzima?”Gab akasita kidogo.
“Usiwe na wasiwasi, nia yangu nataka utulie. Siwezi kukuruhusu ufanye kitu kibaya. Unakumbuka pale ofisini ulipotaka tu..” “Usinikumbushe ule
ujinga Nancy. Najutia sana” Tunda
alimsogeza miguu yake taratibu kutoka
mapajani kwake. “Nini tena?” “Sipendi kukusababishia majuto Gab. Naomba
uondoke.” “Hapana Nancy,
usinielewe vibaya.” Tunda
akanyanyuka kabisa akaenda bafuni kuoga.
Alitoka na nguo nyepesi sana zakulalia ambazo zilionyesha mwili wake wote kwa kuwa hakuwa amevaa kitu chochote ndani. Na ile nguo ilikuwa kama chandarua chepesi. Akajidai kushtuka “Kumbe bado upo!
Nilijua umeshaondoka. Naomba
uondoke nataka kulala Gab.” Tunda
alijiweka kitandani taratibu tena baada
ya kufanya mizunguko kadhaa kama anayeweka
kitanda sawa kabla hajapanda. Alijua wazi anamtesa kwani alikuwa akimsindikiza kila anakopita.
Mara kuchomoa shuka huku, kupanga mito
hivi. Kupunguza baadhi ya mito hiyo iliyokuwa imepangwa vizuri kitandani hapo na kuiweka
kwenye kochi.
Aliporidhika na maonyesho yake ndipo Tunda
akapanda kitandani.
~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~
Gabriel kijana wa kanisani, mtegoni.
Anatoka vipi kwa Tunda aliyeshindwa kujitoa wakiwa ofisini? Cha nini kwa mke wa
Gab, nakipataje kwa Tunda...
Usipitwe na muendelezo huu wa kusisimua.
0 Comments:
Post a Comment