Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com NILIPOTEA! – SEHEMU YA 15. - Naomi Simulizi

NILIPOTEA! – SEHEMU YA 15.


T

unda akajikaza na kumjibu taratibu tu. “Nataka nioge  kwanza ili niwahi kulala,  ndege yangu inaondoka kesho asubuhi.” Mbawala akakaa kwa mshtuko na  mshangao Nilifikiri tunaondoka muda mmoja, jioni! “Nimebadilisha tiketi.” “Bila kuniambia!?Akauliza Mbawala kwa hasira kidogo. Tunda akamwangalia na kushindwa  kujibu. “Doris!?” Kimya. Tumekuwa na  wakati mzuri sana mimi na wewe. Kwa  nini unanikimbia bila taarifa? Nimetoka kukwambia Mbawala! “Kwa hiyo wewe ndio mtu wa namna hiyo? Unabadilika badilika kutokana  na unavyojisikia?Kimya.

Labda  niulize ni sababu gani inayokupelekea kushindwa kusubiri kwa masaa  machache ili turudi wote?” Kimya.  Au ni kwa kuwa nimekwambia wewe sio Doris na kutaka kujua ukweli  zaidi?” Tunda akamwangalia kidogo, maana alikuwa ameinama kama  anayefikiria.  “Mimi ni waziri, tena wa mambo ya  nje. Nakuja huku kuzungumzia mambo  mazito sana. Kweli ulitegemea nisafiri  tu na mtu nisiyemfahamu, tena baada  ya kukataa mimi nisikate tiketi!?” Tunda akashtuka sana. Hakujua vile  alivyomkatalia yeye kukata tiketi  kungeibua maswali kwake kwa haraka  kwa kiasi kile. Kwanza hakujua hata  kama kwake inamaana. Tunda  alimkatalia kijanja, akimzuga kwa  penzi zito, asijue mwenzie hakuwa  waziri kwa awamu ya uongozi makini  kama huo na kushika nyadhifa kubwa  kwenye awamu za maraisi wengine  kwa  bahati  mbaya. 

Mbawala alishakuwa  balozi  akiwakilisha  Tanzania kwenye nchi za ulaya kwa  muda mrefu sana, tena bila kuvuruga.  Inamaana akili ipo. Na yupo makini.  Huwezi kumdanganya kitoto.  “Nina maadui, ndani na nje ya nchi.  Kuna watu wanatuma wasichana  wengi tu kuniwinda kwa mapenzi ili  kunitega. Lazima kujua nipo na nani  na  kuwa  makini  na  kila  ninachokifanya.”Alizidi kumtisha  Tunda.

Baada ya kukataa tiketi ya  bure kutoka kwangu, tena kwa safari  niliyoomba mimi, ikabidi kujiuliza na kukufanyia utafiti. Nisingeweza kuwa  hapa  na  wewe,  bila  hata  kukuchunguza!?” Mwili mzima wa  Tunda ulikuwa ukitetemeka, asijue  ajibu nini.   

“Lilitafutwa hilo jina la Doris bila  kuleta  majibu  yanayoeleweka.  Wasiwasi ukazidi kuniingia kwa kuwa tulishakuwa wote kwenye gari pale Mlimani city lakini ilikuwa gizani  kisha ukapotea tu pale Mlimani city.  Hata mlinzi wangu alipojaribu  kukufuatilia, ukawa kama umempotea. Yeye akasema jinsi ulivyompotea, ni  kama mtaalamu. Yeye akakuchukulia  kama mpelelezi. Akasema msichana  wa kawaida asingeweza kumpotea  vile.” Tunda akashtuka zaidi. 

Ndio huyo mlinzi wangu ikabidi  kutoa wazo la kupata picha yako  mwangani ili kukuchunguza zaidi.  Sikujua kama umetumwa na nani, kwa  sababu hata namba ya simu  uliyoitumia kunipata mimi, ni ya siri.  Siwapi watu hovyo. Anayo raisi wetu,    watoto wangu, mke wangu na watu  wasiozidi hata 7 mbali na hao  niliokutajia. Tena nao ni viongozi wa  juu sana kwenye nchi zao. Ambao simu  zao huwa hazisubiri. Popote pale  nikiona mtu anapiga kwa namba hiyo,  lazima  nipokee.  Hata  wewe  nilikwambia.” Tunda alishtuka sana. Akatamani hata kupotea pale. Lakini na yeye akafikiria kwa haraka.

Kitu kikamshtua na kumuumiza. Akaona aulize. “Subiri kwanza Mbawala. Usiniambie kuwepo kwako  pale uwanja wa ndege siku ile ilikuwa  njia yakunipata ili watu wako wanipige picha ili unichunguze  zaidi!?” Tunda akauliza huku midomo  ikimtetemeka. Ningefanya nini wakati uli....Dont. Machozi  yakaanza kumtoka Tunda.  Akamnyamazisha kwa haraka, na  kumwacha waziri haelewi. Tafadhali acha tu.” Tunda akaendelea kumsihi  huku akilia.  Nilifurahi sana kukuta ukinisubiria  pale, Mbawala! Ulinyanyua kitu ndani  yangu ambacho sikuwahi kukipata kwa  yoyote yule ila kwako wewe pekee. Nilikuja huku kwa furaha, nikashindwa  hata kutoka nje, nikikutaka tu wewe.  Ndio maana nilikuwa sichoki kila  unaponigusa au ninapokutizama kwa  kile  nilichofikiri  ni  uthamani  uliouweka kwangu. Kumbe ulikuwa  umenifuata uwanja wa ndege kama  muwindaji ili walinzi wako wanipige  picha, na sio upendo!” Tunda alisikika  akiwa ameumia sana. Doris! Tafadhali usiongee  chochote  Mbawala. Please. Tunda akatoka  pale chumbani.

Tunda alitoka nje kabisa ya lile jengo  akaanza kulia kwa uchungu sana hata  asijue ni kwa nini. Mbawala  alimpokonya  tumaini  kubwa  alilolijenga ndani ya siku chache sana tokea wakutane. Alilia sana. Gafla akakumbuka analo tatizo kubwa zaidi ya kuumizwa hizo hisia zake. Hofu  ikamwingia asijue yule baba amejua  nini juu yake. Mambo mengi yalipita  kwa wakati mmoja kichwani kwake,  yakavuruga tumbo lake zaidi. Akaanza  kutapika tena. Safari hii yalikuwa mate tu yanayotoka. Mwishoe akatafuta  sehemu akakaa. Nje tu. Tena akakaa  chini kabisa kwenye kijiukuta kidogo  kilichojengewa  kama  urembo  membeni ya maua. 

“Nini amegundua juu yangu? Amejua kama mimi nafahamiana na  mwanae?”Akajiuliza kwa hofu. Au amejua kama niliiba namba yake ya  simu kwenye simu ya mtoto wake?” Tunda akajiuliza huku akitetemeka na machozi yakimtoka  huko ugenini. “Lakini kama  tena  angekuwa amekumbana na kitu  asichopenda, asingenifuata huku na  kukaa naye siku zote hizi. Na  asingeniuliza ni nani ninayemuhofia  kuonekana naye. Angemtaja tu.” Kidogo hilo likamtuliza. 

Akakumbuka alivyokuwa akimfurahia  kitandani.  “Wote  wananifurahia  kwenye mapenzi, halafu wanakuja  kunigeuka. Niache kujidanganya.” Akakanusha ile furaha aliyomuona  nayo Mbawala wakiwa naye. Akakataa  kujiweka kwamba yeye ndio sababu.  “Anajua kama mimi ni Tunda?  Amenichunguza wapi? Walifanikiwa baadaye kuja kufika kwangu ili  kunichunguza zaidi? Nini wamejua juu yangu!? Wanaweza kuwa  wametumia simu yangu mimi  mwenyewe kufika kwangu. Labda  kwa kufuata gps!” Tunda akazidi  kuingiwa hofu na kushindwa hata  kutembea. Alikaa pale bila kujua muda  unazidi kwenda. 

Akatamani abadilishe yale maisha.  Naanzia wapi tena? Akajiuliza  huku akihesabu garama za maisha  zinazomkabili. Halafu nije kuishi  kama Tunda tena!?” Hapo machozi  yakaanza kumtoka tena kwa upya.  Tunda ni mtu wa mwisho kabisa hata  yeye hakutaka kumuona. Akaanza  kukumbuka maisha aliyoishi zamani  kama Tunda. Kuanzia mtoto mpaka  mkubwa. Alivyosalitiwa na kufukuzwa  kwenye majumba ya watu. Chuki ikajaa. Maana alikumbuka tukio moja  hadi jingine nakuzidi kumchukia  Tunda. Hakutamani Tunda aje aishi  tena duniani. “Tunda ni jeusi, baya  jitu la kutumiwa mwili wake bila  huruma wala heshima. Linatukanwa  na kufanywa vile mtu anachopenda.  Halijasoma. Namchukia Tunda.  Kwanza sitaweza hata kulala nikiwa  Tunda.” Tunda akazidi kulia peke  yake. Akiwaza hili na kujiogopesha  kwa lile. Mpaka akatulia mwenyewe. 

Hapakuwa na jinsi. Hawezi kutoroka  kwenda popote. Yupo ugenini na vitu  vyake vipo hotelini. “Heri nirudi tu.  Yule baba analindwa. Ukute hata  hapa walinzi wake wananiona.” Alipoangalia saa yake, akashtuka sana.  Ilishakuwa ni saa nane na nusu usiku.  Akasimama kwa haraka, akaamua kurudi hotelini. Hakuwa amefika  mbali. 

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Alimkuta Mbawala amelala.  Hakuwasha taa. Aliingia kuoga,  akaamua kulala sehemu ya makochi.  Akajilaza taratibu kama asiyetaka  kumsumbua Mbawala. “Njoo ulale  kitandani.” Akasikia  sauti  ya  Mbawala. Akabaki kimya. Akamuona  amesimama anamfuata. Akawasha taa.  Twende ukalale kitandani. Akasisitiza huku akimshika mkono.  Wakarudi kitandani. Mbawala akamfunika vizuri, akalala nyuma yake,  alikuwa amempa mgongo.  Wakatulia kwa muda.

“Ndege yako  inaondoka saa ngapi?” Waziri  Mbawala akamuuliza taratibu. Saa  nne na nusu.”“Utafikaje uwanja wa ndege?” Nitatumia shuttle ya hoteli.  Wamesema watanipeleka.Tunda  akajibu taratibu. “Nina kikao saa tatu  asubuhi, najua nitakuacha ukiwa  umelala. Kwa kuwa nitaondoka mapema kidogo ili nikaweke mambo  sawa. Mimi ndio mzungumzaji kesho. Inabidi kuwahi kuwapelekea vitu ambavyo nitahitaji wavionyeshe kwenye projector.  Kwa hiyo  nitaondoka kama kwenye saa moja na  nusu.” Tunda akatulia akiwa anamsikiliza, hakujibu kitu.

Wakatulia tena kidogo. Nimekuwa na  wakati mzuri. Asante.Waziri  aliongea taratibu. Tunda akavuta  pumzi na kutulia tu asimuelewe  anataka kumfikishia ujumbe gani.  Kuwa ameridhika na uchunguzi  walioufanya juu yake au! “Unafikiri nitakuja kukuona tena?” Tunda  akatingisha kichwa kukataa. Mbawala  akambusu  shingoni.  Naomba ukibadili mawazo unitafute tena.” Tunda akajikuta anaanza kutokwa na  machozi. Nilijua ulikuja uwanja wa  ndege kuniaga Mbawala. Sio kuniweka  mwangani kwa  walinzi wako! Nimeumia sana. Umenipokonya kitu  kikubwa  sana.  Hata  natamani  usingeniambia. Ukaendelea  kunidanganya kwa muda.” Tunda akalalamika kwa kuumia sana.

Naomba  unielewe.Hilo ndilo tatizo linaloniumiza Mbawala. Nimeelewa.  Natamani ingekuwa vinginevyo. Tunda akaendelea kulia taratibu.  Naomba  niangalie.  Tafadhali. Tunda akamgeuka taratibu. Akawasha  taa ya pembeni ya kitanda. “Naomba  unielewe mama. Sijui nani nimwamini.  Nazungukwa na watu wabaya watupu. Nawindwa kuliko nitakavyokwambia.  Watu wanawinda roho yangu kwa kila  namna sababu ya majukumu yangu.  Wanatumia mpaka watu wakaribu  yangu kuniangamiza. Inanilazimu  kuwa makini sana.” Tunda alimsikia  akiongea kwa kukubembeleza kama  anayejutia. Kidogo ikampa moyo. 

Uliniogopesha kidogo uliponitumia ujumbe kwenye simu yenye ile namba.  Ndio maana nikakupigia kwa haraka. Sauti yako ikanivutia, nikataka  kukuona. Kumbuka wewe ndiye uliyependekeza mpaka eneo la kukutania. Nikaingiwa kidogo hofu.  Lakini ukawa tena kama unanilinda  nisionekane na watu. Ikawa nafuu tena. Nikakukubalia. Kuja kukuona  upo mtulivu tu, na mapenzi yale,  nikafurahia. Lakini ulipokataa tiketi, nikajua moja kwa moja unakitu  unaficha. Ni nini! Ndio nikajua hutaki  nijue jina lako kamili. Nikaingiwa tena  na hofu. Nikakumbuka mara kadhaa  pale tulipokuwa kwenye gari, ulikuwa ukiingia kwenye pochi yako tena katikati ya mapenzi.” Nilikuwa  nikibadili kondom, Mbawala. Hapo  Tunda akajitetea. 

Hata hilo wazo halikunijia. Maana unayo jinsi yako, ni ngumu kuelewa  unapokuwa unabadili. Ni hapa hotelini  ndipo nilielewa kuwa huwa unabadili  kondom hata katikati ya mapenzi,  nikiwa hata sijafika. Ikaniongezea  ujasiri wakujua kuwa nipo salama pia.  Lakini wakati ule hata sikufikiria.  Nafikiri  ni  sababu  ya  hofu.  Nikajiambia labda unarikodi au sijui. Lakini ukumbuke ulianza kwa kuniita waziri Mbawala. Nikakwambia tukiwa wote usiniite waziri. Unakumbuka?” Tunda akakumbuka. Lakini mimi  sikujua kama ni kwa kujihami,  Mbawala! Nazidi kuumia kuona  nilikuelewa vibaya na kujiwekea tumaini ambalo hata halikuwepo.”

Tafadhali usiumie, ila nielewe  tafadhali. Nimesalitiwa sana.  Nimeumizwa, ndio maana umekutana  na Mbawala huyu aliyekuumiza na  wewe. Ila sikukusudia kukuumiza kwa namna hii.Akambusu mara kadhaa  juu ya kipanda uso na kumfuta  machozi.  Tunda alimuwekea hukumu moyoni.  Alilia kwa kumaanisha kutoka moyoni.  “Unajua baada ya kukubali kuja huku,  na walipokuchunguza na kukosa  sababu. Wakaniambia sio mtu  hatarishi, basi nikajiambia labda umefurahia tu kampani yangu.  Unataka kunitumia kama wengine. Nikajiambia basi na mimi nifurahie huu muda. Ndio nikakufuata hapa.  Kwa muda wote tumekuwa hapa,  nimekufurahia  sana.  Nikazidi  kukusoma nakukuamini sio mtu  hatarishi kwangu. Umetulia. Huna papara. Unanifurahia kila ukiniona.  Ila nimegundua kuna mambo au jambo  unanificha, ndio maana nilikwambia  ili kama utaniamini, basi ufunguke ili  kuendelea  kufahamiana  zaidi.  Natamani hapa isiwe mwisho.” Tunda  akavuta pumzi kwa nguvu. Hakujua  anatakiwa aombe msamaha au aseme  nini! Kuomba msamaha, inamaana  aeleze ukweli wake wote.  Amwambie amelala na mtoto wake!  Hatataka hata kuja kumuona tena. 

“Kwanza atanishangaa nimewezaje kulala nao wote wawili! Ataniona ni  mchafu wa kupindukia.” Tunda  akapinga hilo wazo. Je, ajibu hata hilo  la wapi amepata hiyo namba yake ya  simu! Amwambie aliiba namba yake  ya simu kwa mwanae! Sithubutu.  Atahisi na yeye nimemwibia mambo  yake kwenye laptop yake au simu  yake. Na hivi alisema anamajukumu  mazito, ndio mwanzo wakuishia jela  wanifunge.” Tunda akaona bora nusu  shari. 

Unataka uwahi kulala ili kesho  usiamke na uchovu?” “Sio kikao cha  muda mrefu. Kama hapatakuwa na  kingine kitakachojitokeza huko kwa  wenyeji wetu, kikao kikiisha naweza  kurudi kupumzika mpaka jioni  nitakapokuwa nikiondoka.” Wakatulia  kidogo. Mbawala akiwa amepata jibu lake. Hataki kuwa muwazi kwake. Tunda akitamani kama ingekuwa  tofauti. Alivutiwa sana na waziri  Mbawala.  “Naomba uniage.” Tunda akaongea  taratibu na kwa upendo. Mbawala  akachangamkia penzi. Safari hii ikawa tofauti. Wawili hawa wanaagana kutokuonana tena wakiwa  walisharidhishana sana haswa kitabia.  Tunda alishamwambia hatamtafuta  tena. Kila mmoja alijawa nguvu na  huzuni ya kuagana ila wasijue kile  kinachoendelea kichwani  kwa  mwenzie.

Kwa Tunda huzuni ya  kumpoteza aliyejua ni Sadiki  mwingine. Tena bora zaidi. Kwa  Waziri Mbawala alipata dogo dogo wa  kumtuliza na kumliwaza popote tena  kwa wepesi, alijua atajaza pengo  kubwa la mapenzi alilonalo nyuma ya pazia, mbele ya umati akijulikana  anayo ndoa swafi. 

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Alamu ya simu ilikuja kumuamsha saa  mbili kasoro. Alipoangalia pale  chumbani, hakumkuta Mbawala.  Akajua alishaondoka. Akaingia kuoga  alipotoka akiwa anavaa na  kujitengeneza mbele ya meza ndogo aliyokuwa ameweka vipodozi vyake,  akaona bahasha. Akajua ni pesa tu  kutoka kwa Mbawala. Kwa haraka  akaifungua. Alikuta dola nyingi,  mpaka  akakaa. “Huyu  Mzee  amenifikiriaje  kutokana  na  alichokigundua kwangu!? Pesa yote  hii!” Mpaka mikono ikaanza kutoa  jasho. Akaiweka chini ile bahasha  akabaki akiitazama.

Tunda akatamani ingekuwa tofauti  pengine angemtafuta tena. Lakini  moyo wake ulishageuka hapo, akashidwa chakufanya. “Siwezi kuja kumtafuta tena. Ananichunguza!  Nitaharibu kila kitu. Atakuja kufufua  mengi mabaya yanayoweza kuja  kuniingiza matatizoni. Mwishoe aje  amfufue  na  Tunda  ambaye  nilishamzika muda mrefu sana.  Hapana.” Tunda akawaza akiumia, akijua wazi inampasa kurudi nchini na kuendeleza biashara ya ngono kwa asiowajua ili aweze kuishi mjini. 

Akavuta Note pad na kalamu  vilivyokuwa  hapo  pembeni,  vimewekwa na hotel, akaamua kumuandikia. Mbawala, asante kwa wakati  mzuri sana na waheshima ulionipa. Asante kwa pesa. Nakushukuru sana. ASANTE. Nakutakia kila la kheri.’ Hivyo tu, akakiacha hicho kikaratasi  kwenye kona ya kioo. Kwamba lazima angerudi, angeikuta. Bado aliacha vitu  vyake vya thamani humo ndani.

Tunda alichukua vitu vyake tu, na kuondoka  pale hotelini. Usafiri wa hotelini ndio  alioutumia kumfikisha uwanja wa  ndege.  Kama kawaida yake, aliwahi kabla  hata ya muda wa abiria wa kimataifa  wanavyohitajika kufika uwanja wa  ndege. Aliondoka nchini Afrika ya  kusini akiwa ameumia tofauti na  alivyofika hapo. Anamuacha Waziri  Mbawala ambaye alishaanza kuvutiwa  naye! Akajisikia ni kama amempoteza  kwa kifo kama alivyompoteza Sadiki  kwa  gafla  akiwa  ameshaanza  kunufaika. Waziri Mbawala peke yake,  kwa hongo ya kwanza tu, alionyesha  anao uwezo wa kumuweka jijini bila  kuhangaika na wengine.

Akiwa kwenye ndege akaendelea  kujifikiria. Hasira kwa ndugu zake zikamjia. Akachukia kila mtu. “Wote ni wasaliti. Wangenitunza  hata  kimasikini tu kama vile zamani kwa bibi, nisingefika kote huku.” Tunda  akazidi kuumia na hasira kupanda.  “Nitaanza na Mihayo. Nikimpata yeye, nitalipa kisasi kwa watu wanne  kwa mpigo.” Jazba ikazidi kumpanda.    

Kisasi.

A

lipotua tu uwanja wa  ndege wa Mwalimu Nyerere,Dar akampigia simu Tewele.  “Nilikuwa nakuwaza sasa hivi! Ila ikabidi  niwe mstaarabu kwa kuwa uliniambia  utanitafuta.” Vipi,kwema? Tunda akauliza huku akicheka taratibu.  “Kwema. Nina safari ila sio ile niliyokwambia. Ile Mihayo ameninyima  bwana. Nasikia anakwenda mwenyewe. Ila  kuna kikao cha siku mbili tu Bagamoyo, na  mimi nimo kwenye orodha ya watu wachache aliochagua yeye tuhudhurue. Na yeye atakuwepo. Ameita  viongozi wote wa bandari. Ngazi za juu tu. Tanga, Zanziber na hapa. Sio siku nyingi,  lakini naona zitatufaa. Na hivyo ulivyo  mtulivu, nikakufikiria wewe wakuzitumia hizo siku chache pamoja kwa utulivu.” Tunda  akacheka kidogo.

“Sasa si utakuwa kwenye  mkutano?” Tunda akamuuliza kama hataki wakati alitamani kuruka kwa  furaha yakwenda kukutanishwa na  Mihayo.  Hujaelewa mama. Tuna siku mbili ambazo  ni zetu peke yetu. Usiku kucha tupo wawili tu.  Hakuna haraka yakuwahi nyumbani. Mimi  na wewe. Nakupa ruhusa unipagawishe  utakavyo!” Tunda akacheka sana. Lakini usiku mmoja lazima uutumie na Mihayo, au  atakuwa na mwanamke wake? Tunda  aliuliza makusudi ili kujipanga.  Sidhani. Si unakumbuka nilikwambia aliacha kazi? Hawezi kuja kujitokeza mbele ya wafanyakazi, tena ngazi ya juu wa bandari!” Basi ndio kujipanga vizuri. Tukiwa huko tutazungumza zaidi.Wakazungumza  zaidi na kukubaliana hiyo alhamisi juma lijalo atampitia Mlimani City, waelekee Bagamoyo pamoja. 

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Tunda akajiambia anazo siku zakupumzika mpaka hiyo alhamisi. Ilikuwa ijumaa aliporudi nchini. Lakini  alikuwa  amechoka  na  kusafiri. Akamtumia ujumbe Mbawala Junior,  mtoto wa waziri. ‘Kesho yako ikoje? Naweza kuwa na nafasi.’ Hapo hapo  akampigia. “Nakuja mama. Jumamosi yote na jumapili nakupa wewe.” Tunda  akacheka.  Ukifika hotelini utanijulisha basi, ili  nikufuate.” “Ngoja niangalie tiketi ya kesho asubuhi.  Si ni sawa?” Sawa. Lakini asubuhi ya saa nne siku ya jumapili, itabidi niondoke, nina  miahadi ya saa 6 mchana. Tunda akadanganya.  Asingethubutu kumpa siku mbili. Aliijua shuguli yake. Hiyo siku ya jumamosi tuliyoipata, tutaitumia ipasavyo.” Tunda alicheka kumridhisha, lakini  alijua hatanii. Hayupo hata nusu ya  baba yake. Yupo rafu! Akajisemea  moyoni. Lakini kwa kuwa alijua kutoa  pesa nzuri kama baba yake, hakutaka  kumpoteza na yeye kwa kumsubirisha  muda mrefu, mpaka akakata tamaa na  kumfungia mlango.  “Asije tafuta  msichana mwingine bure. Acha  nimuweke karibu hivyo hivyo.”

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

     Alifika kwake na kujitupa kwa uchovu na mawazo. Alimpoteza Waziri kitu kilichobaki kikimuuma. Alilala siku nzima kwa ushovu  wa safari lakini zaidi penzi la Waziri.  Alipoamka usiku alikula na kurudi  kulala. Asubuhi kabla hajakwenda kwa  Mbawala mtoto, akaenda kwenye  masaji kufanya mwili wake utulie.  Akatengeneza na kucha. Nywele zilikuwa kwenye muonekano mzuri,  akaona aziache, lasivyo angemchelewa Mbawala ambaye alimtegemea kufika  hapo wakati wowote.

Kwa Mbawala Junior.

I

liposika saa tano na robo,  Mbawala akapiga simu  kumtaarifu kuwa ameshatua jijini na yupo hotelini anamsubiria. Akamtajia namba ya chumba na kumwelekeza alipo. “Nitakuwa hapo  baada ya dakika 40 kuanzia sasa.” Nakusubiri kwa  hamu. Tunda alijua kazi imeshaanza.  Alishajiambia mapumziko ni mpaka kesho yake watakapo achana. Mpaka akamuhisi anatumia dawa kumuongezea nguvu! Lakini  alilala usiku kucha na mchana  alipofika kutoka Sauzi. “Nipo tayari  kumkabili.” Akajipa moyo huku  akikumbuka ule muda wa kupumzika  katikati ya mapenzi. Akapumua  kidogo. Hapo naweza kupumzika  hata kulala na mimi kidogo. Lakini  akakumbuka Mbawala nayeye huwa analala tena kwa kukoroma sana.  Akachoka gafla kabla hata hajaanza kazi yenyewe. Lakini akajiambia ni  kwa siku moja tu, atakwenda  kupumzika nyumbani kwake. 

Alifika hotelini mpaka kwenye  chumba alichomuelekeza. Akagonga.  Mbawala alifungua mlango akiwa  anaongea na simu. Akamuonyeshea  ishara aingie tu. Tunda akaingia. Akapomkea na busu. Kama kawaida alikwepesha mdomo, akamkumbatia,  akampa la sikio. Mbawala akacheka.  Mtu wa kwenye simu bado alikuwa  akiongea. “Kwa nini usimuache tu, baba?” Tunda akachutuka baada ya kusikia  hivyo. Akajua anazungumza na baba  yake.  Uwamuzi ni wako baba. Wewe amua vile  unavyotaka. Lakini kuwa makini kwa wadhifa wako na hayo mambo yakienea,  yanaweza kukuharibia mipango yako yote. Hutaki kujitia doa sasa hivi.”Akamsikia  baba yake akijibu. Hapana dad. Huo ni ushauri wangu tu. Unaweza kuuchukua au  kuuacha. Ila ninachotaka kukwambia ni  kuwa, nakuunga mkono kwa kile  utakachoamua.”Akatulia kidogo kama  anayesikiliza.

Dad!? Akamsikia  akiuliza kwa mshangao mpaka usoni.  She is my mom! Ulitegemea nisimjulie hali! Akasikia baba yake akiongea kwa sauti ya ukali. Dad Please! Mbawala Junior  akasikika akimsihi baba yake. Mzee  akaendelea kuongea kwa jazba. Bado  Tunda  alikuwa  hajaelewa  kinachoendelea juu ya huyo mke wa  waziri na familia yake. Akaona atulie  asikilize.  “Naomba nikupigie kesho dad. Tafadhali. Am  in the middle of something.” Baada ya  muda wakusikiliza, akamsikia Junior  akimuomba baba yake akate simu.Kimya. “Dad?” Akamuona anaangalia  simu yake.

Amenikatia simu! Akaweka simu pembeni akilalamika kidogo. Kwema? Tunda akauliza taratibu. Daah! Wazee hawa  wanatuchanganya kweli! Hatujui hata  jinsi ya kuwasaidia.” Nini tena? Mbawala akasita. Daah! Ndoa zina  mambo yake Fina! Naomba tuyaache tu, tuendelee na yetu.Akajibu, na  kuanza kumchangamkia. Tunda akajua hataki kuzungumzia hilo. Akakubali  kutumika tu. 

Wakiwa katikati ya mchezo huo  aliokuwa akiuendesha Junior kwa uchu  wote, simu yake ikaanza kuita  mfululizo. Kila alipojaribu kupuuza,  ikaendelea kuita tena na tena. Alitoka pale kitandani kwa hasira. “Ni nini  jamani!?” Akapokea huku akilalamika. Sauti ya kike ikasikika upande wa pili. “Come on!” Junior akasikika akishangaa kwa sauti. Sijamkatia simu, yeye ndiye amenikatia simu! Ila nimemwambia siwezi kuacha  kumpigia simu mama, labda ndio maana  amekasirika.” Mbawala akasikiliza. No  way T! This is my mom we are talking about  here! Akabisha na kuendelea kusikiliza. Tunda akajua  anazungumza na dada yake Taffy.  Akamuona ni kama aliyekubali yaishe. Mwishowe akajibu,  “Fine. Mbawala akajibu na kusikiliza  tena kidogo. “Si nimesema sawa! Ama!?” Akajibu kwa  hasira  kidogo. 

Nakuendelea kusikiliza zaidi.  Nitakuja kesho mchana. Sio leo. Leo nina  kitu cha muhimu nafanya na siwezi kuahirisha  kwa matatizo ambayo sina uwezo wa kuyatatua.  Mama ameamua kuendelea na maisha yake, kwa  nini na wewe usimshauri dad aendelee na  maisha yake amwache tu, watu tupumzike! Kwa vikao hivi vya kila siku unafikiri itasaidia  nini?” Hapo Tunda akaelewa kwa kiasi.  Akamuona Junior anasikiliza tena  kidogo. “Nimesema nitakuja kesho, na wewe  zungumza na dad. Tafadhali Taffy. Huu ni  usumbufu, na ni kama adhabu ambayo  hatustahili. Dad is smart than this. Na wote  tunamjua mama anamsimamo wake. Akisema  hapana ni hapana. Hawezi kurudi, na siwezi  kuacha kuwasiliana naye kwa wao kushindwa  kuelewana!” 

Akatulia  kama anayesikiliza. Basi kama ni hivyo, atakuwa amenichagua  mimi wakunimalizia hasira zake. Akamsikia akijibu. Naomba nikuage,  nitawaona kesho tafadhali. Nakata simu. Sasa  sio na wewe uje kusema nimekukatia.  Nimekuaga.” Hapo hapo akakata na  kuzima simu yake. Akuitupa kwenye  kochi kwa hasira. Akaelekea chooni.

Ndio Tunda akaelewa sasa. “Labda  ndio maana baba yake alisema  hamna shida akionekana na mimi  hadharani na hana haraka yakurudi  nyumbani!” Tunda akawaza. Nashuguli yote ile, inawezekana alikuwa na ukame wa miaka! Akaendelea kuwaza. Akamuhurumia jinsi alivyomuacha na kumwambia hatamtafuta tena huku waziri akimwambia anatamani kuja  kumuona tena! “Atajiona ana mkosi  baba wa watu. Kila mwanamke anamkataa.” Tunda akawaza akiwa  peke yake pale chumbani, bado  Mbawala alikuwa amejifungia chooni.  Hakutaka hata kumfuata. Akaona  ajipumzishe. Walishazungushana hapo kwa muda mrefu bila kupumzika. Mbawala Junior akiendeleza rafu zake. 

“Alikuwa Afrika ya kusini, kidogo  tukapumua. Akatulia kwa siku mbili  tatu wala hakutafuta mtu. Amerudi na  kelele. Na T naye anamsikiliza kwa  kila jambo! Mimi ndio nakuwa mbaya  badala ya mkewe!” Akatoka Mbawala  akiwa  amekasirika  akiongea.  Umekula?Tunda akamuuliza kwa upole tu. Naona tuagize chakula tule.  Washanichanganya na kunikata stimu  yote!Akajitupa pale kitandani, Tunda  akapiga simu kuagiza chakula.  “Hayanihusu tena? Hata nikijua,  siwezi kusaidia. Huyu baba  anaonekana anatafuta mwanamke wa kudumu. Nikimtafuta tu, na hivi  alishaanza kunichunguza, atakuja  kufufua hata ambayo hayatamkiki.  Atanidharau na kunihukumu kwa atakayoyasikia.” Tunda akawaza na  kuamua kukaa nao mbali. 

Waziri  alikuwa  mtu  mzuri,  alimfurahia. Lakini katika maongezi na  mtoto wake huyo, alihisi ni kama  anazo mbio za kuja kugombea uraisi. Na hivi hana shida yakuonekana na  mimi hadharani, watu wataanza  kunichimbua. Watakuja kuanika  uozo wangu wote! Hapana. Sipo  tayari kuja kuzungumzia hadharani  maisha yangu ya nyuma.”Tunda  aliendelea kuwaza  alipokuwa na Mbawala Junior hapo  hotelini mpaka kesho yake muda wote wanaachana, Mbawala akimwambia  anakwenda nyumbani kwao kwenda kusikiliza matatizo ambayo hayajaisha na wanayazungumzia zaidi ya miaka  miwili.

Tunda  alichukua  pesa  zake,  akajiondokea hapo hotelini akiwa na  usingizi. Hakika Mbawala huyu  alikuwa mkoromaji sio kama baba  yake  aliyekuwa  analala  amemkumbatia. Tunda alikesha hapo. Na asubuhi hiyo pia, alimuaga kama  ndio wanakutana wakati wametoka  kulala kitanda kimoja!

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Tokea anatoka kwa Mbawala pale  hotelini alianza kupanga mipango ya  jinsi ya kumkabili mjomba wake,  Mihayo huko Bagamoyo. Nini afanye?  Ajifiche na kumfanyia ujanja au  ajitambulishe ili amkumbuke Tunda  aliyemtesa ndiye huyu wa sasa! Lakini  hakutaka Tewele hata ahisi kuwa  wanafahamiana. Atafanyaje? Ndicho  kilichokuwa kikimuumiza kichwa Tunda. Juu ya mapenzi kwa Tewele,  hilo hakulitilia shaka hata kidogo. Tewele mchokaji. Mara moja au mbili  kama akijitahidi sana. Tena hana  purukushani nyingi. Alimuona mwili  wake unamlemea. Hilo alilifurahia sana Tunda na kujiona anakula pesa kwa  urahisi. Tewele akamuona Tunda kinara,  sababu hakuwa akiweza shuguli  nyingi. Sehemu kubwa, Tunda alifanya  kazi yote yeye akiwa ametulia  akifurahia tu.  

Tunda alipiza kisasi chake kwa Ulaini,  Mambo yote yanajipanga huko  Bagamoyo

T

ewele alimpitia hapo Mlimani  city ikiwa mapema tu hiyo siku ya  alhamisi  kama  walivyokubaliana. “Ulivyopendeza!” Tewele akamsifia wakati anaingia  garini. Yote hii kwa ajili yako. Nakushukuru Irene. Najua tutapata  wakati mzuri. Na hivi tutalipwa,  naamini pesa ya safari hii haitakuwa  ndogo.” Hilo likamfurahisha Tunda.  Walipofika Bagamoyo kwenye hoteli  wanayofanyia huo mkutano na kulala,  ilibidi Tewele ashuke akachukue  chumba chake kama mfanyakazi wa  Bandari, ndipo ampigie simu Tunda  amfuate. Sio kuongoza.

Kama kawaida ya Tunda, akawa ametulia kimya pale  ndani ya gari.  Akiwa amekaa, akashangaa kumuona Mihayo anatoka ndani ya ile hoteli  akiwa kwenye simu. Ikasogea gari aina ya RAV 4 mpyaa, ikasimama karibu kabisa na  Mihayo. Ilikuwa gari nzuri sana ya  rangi ya damu ya mzee inayowaka  vizuri. Tunda akaendelea kuangalia.  Akamuona Mihayo, mjomba wake  akienda moja kwa moja mlango wa nyuma. Akapunga mkono huku  akicheka. Kwa haraka sana Tunda  akatoa simu yake nakuanza kuchukua  video. Akamuona mjomba wake  anafungua mlango na kuinama kwa  muda. Hakuwa akisikia chochote  sababu gari aliyokuwepo ilikuwa  imefungwa vioo mpaka juu, gari bado  imewashwa.  Mziki  ukiendelea  kutumbuiza taratibu. Tewele aliacha miziki yake ambayo kwanza hata  Tunda hakuwa akisikiliza. 

Akashuka dereva kwenye ile gari ya aina ya RAV 4, alikuwa mdada.  Alionekana sio mtu mzima, lakini anamwili mkubwa. Sio kama shangazi yake aliyekuwa mwembamba. Ila yeye  mrembo na ana rangi nyeupe.  Akamuona mjomba wake anamtoa  mtoto kwenye gari. “Haaaa!” Tunda  akahamaki nakuendelea kuchukua  video. Akazima redio na kushusha  kioo ili angalau aweze kupata maneno.  Alikuwa mtoto wa kiume. Mzuri sana. Umri kama miaka miwili hivi. Nywele  zilikatwa vizuri, na alikuwa nadhifu  sana. Mihayo alipomnyanyua juu huku  akimbusu, yeye akiwa amempa Tunda  mgongo lakini mtoto ni kama  wanatizamana na Tunda. “Haaaa!” Tunda akahamaki tena. Walifanana sana na mjomba wake, kama mapacha, kasoro  rangi yule mtoto alikuwa mweupe.

Tunda akaanza kupiga picha huku  akiwachukua video wote watatu.  Hakuwa mbali sana, lakini Mihayo na yule dada, walionekana kujali mambo  yao tu. Hawakuangalia kulia wala  kushoto ila wao. Akamuona mjomba  wake anambusu midomoni yule dada,  tena kwa hatua wala si haraka. Akiwa  amembeba mtoto, dada amesimama  pembeni yao akipokea busu.  Simu ya Tewele ikaingia. Akachukia  Tunda, lakini ikabidi apokee kwa  kuwa ilijaa kwenye kioo chote cha simu, hakuona tena kinachoendelea  kwa  familia  hiyo  aliyokuwa  akiichukua video.

“Nimekutumia ujumbe wa chumba nilichopo. Umepata?” Nakuja  sasa hivi. Tunda akajibu kwa kifupi tu,  na kukata simu. Akarudisha akili na macho kwa mjomba wake na nyumba  ndogo yake. Akamuona akiwa amebeba  mtoto na badhi ya mizigo yao,  wanazunguka nyuma ya ile hoteli  kama wasiotaka kupitia mbele njia ya  kawaida, yule dada akifuata nyuma na  baadhi ya  mizigo. Akachukia kuwachelewa kidogo akiwa  anazungumza na Tewele. Lakini  akawachukua tena video huku  akiwapiga picha wakati wanapotelea vyumbani.

Wazo likamjia kwa haraka. Akashuka ndani ya lile gari akawakimbilia kujua  wameelekea chumba  gani. “Nikikamwatwa  hapa!”  Tunda  akacheka. Alipokata tu kona ili kujua walipo, hakuwaona tena. “Aaaahhaaa!” Akasikitika na kurudi garini kuchukua vitu vyake asiamini  macho yake. Akajikuta akicheka peke yake. “Looooh!” Akaanza kuangalia  picha alizopata na ile video. “Sasa  hapa ni kuwinda mpaka nipate picha  zao kwa karibu. Wote watatu.  Washenzi wakubwa hawa.” Tunda  akaondoka na kuelekea chumbani kwa  Tewele.

Akamkuta akimsubiria kwa hamu lakini hakumwambia aliyokutana nayo.  Ngoja nikukaribishe Bagamoyo. Tunda akamwambia mara alipoingia. Tewele akacheka cheka akionyesha wasiwasi usoni. Tunda akamshtukia.  “Vipi, mama alikuaga nini?” Tunda  akamuuliza. Alimjua ufanyaji wake  mapenzi. Kidogo tu. Lakini si  unajua tena?” “Basi usiku zamu yangu. Hata sasa hivi tunaweza kujaribu. Lakini nilitaka kukwambia ukiona  jamaa anagoma, ujue sababu hiyo.  Alinibana, nikashindwa kumkwepa.” Wala usijali. Tunazo siku mbili, zetu peke yetu.” Tunda akamtuliza. Kidogo  akatoa ile soni. 

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Kesho yake wakati wamekwenda  kwenye mkutano, Tunda alimka na kuamua kutoka akatembee nje. Ilikuwa hoteli nzuri sana.Wao walikuwa  wakila ukumbini. Akamwambia Tunda yeye anaweza kula popote. Na kwa  kuwa kilikuwa kikao cha siku mbili,  alimuonyesha ratiba, walionekana kubanwa huko mkutanoni. Iliwalazimu kuwepo huko kuanzia asubuhi mpaka saa 10 jioni.  Tunda akajiambia ni wakati wakutalii.  Hakuwa amepata hata kifungua  kinywa. Akatoka taratibu mpaka  sehemu ya kulia chakula.

Akaagiza  juisi ya chungwa, mayai mawili na sausage.Wakati anasuburi, akamuona  yule dada na yule mtoto wanakuja pale. Akasikia akimwita kwa jina la Junior.  Ukweli alikuwa mtoto mzuri. Afya nzuri, nguo safi halafu nzuri. Wazi alionyesha ni  mtoto mwenye matunzo mazuri.  Walikuja wakitembea taratibu, akiwa  amemshika mtoto wake mkono,  akimuongelesha kitoto na kucheka.  Rangi ya yule dada ilikuwa kali. Na  ndiyo mtoto wake alirithi. Ila sura, ni  kweli alifanana na mjomba wake. 

Tunda akajidai anatuma ujumbe huku simu imesimama mbele yake kama  ameificha mtu wa nyuma asione, ikaiiegesha juu ya meza. Akaendelea  kuwachukua video huku akiwapiga na picha.  Ile wamemsogelea tu, Mihayo akawa  anaingia hapo kwa haraka. “Vipi,  mmepata?” Akamsikia mjomba wake akiuliza kwa kujali. Tunda akavuta nywele mbele  kama kujiziba. “Ndio tunafika. Si unajua tembea yenyewe? Kila  anachokutana nacho njiani anataka  aokote, ashike. Akiangalie ndio safari iendelee.” Akajibu  mama mtoto. Mihayo akacheka.  Akaina na kumnyanyua.

Mihayo mwenyewe alikuwa  msafi kama kawaida yake. Suti kali  iliyomkaa sawia mwilini. Tunda  hakupoteza muda. Akapata picha za  haraka haraka. Za wote watatu,  Mihayo na mtoto wake.  “Basi mimi narudi kwenye kikao.  Baadaye. Naamini utapata tu.  Zungumza nao. Hata kwa pesa wewe  nunua.” Mjomba wake akamwambia  yule mama mtoto na busu kubwa ambalo Tunda hakulikosa kwa video na picha. Asante.Mama mtoto  akashukuru. “Acha niwahi. Tupo katikati ya kikao.  Nitawaona baadaye kidogo. Nitumie  ujumbe ukikwama kwa chochote,  nitatoka kwa haraka.” Usiwe na  wasiwasi. Sisi tutakuwa sawa tu. Si  ndiyo Junior?Dada akamgeukia mtoto wake, akamchukua baada ya  kumpa busu huyo mwanae akiwa  mikononi mwa baba yake. Mtoto  akacheka wakati anakwenda kwa  mama yake. Mjomba naye akambusu  akiwa mikononi kwa mama yake. “Love youuuu!” Mihayo akamwambia mtoto huku akimbusu tena kama kumuaga. Mtoto akacheka na kujibu, Lovu dady.” “Haaaa!Tunda  akashangaa kwa wazi. Akajifunga  mdomo kwa haraka. Uzuri hakusikika.  Mihayo akaondoka kwa haraka.

Furaha aliyokuwa nayo Tunda, hakuna  jinsi angeeleza mtu akamuelewa. Hata  Tewele asingemlipa, angeondoka hapo  ameridhika kabisa. Mambo yalijipanga  vizuri. Akapata yote tena kirahisi sana. Alifika hapo Bagamoyo akiwa bado  hajui  kitu  chakufanya  pindi  atakapomkuta mjomba wake huko.  Lakini akawa kama aliyeagiza chakula,  akaletewa kikiwa kimepikwa vizuri  sana, tena kikapambwa kwa unadhifu, kisha akasogezewa mpaka mikononi mwake. Alijawa  furaha isiyoweza kutamkika. 

Akabaki sasa akiwatizama mama na  mtoto. Wakasogea mpaka kwa  muhudumu, akaomba chupa ya maji ya  moto. “Itakuwa kwa ajili ya mtoto wao.” Akajisemea Tunda huku  akiwatizama. Hakuacha kuwapiga  picha. Ukweli yule dada alikuwa  mnene. Alivaa nguo ya kuachia tu. Gauni jeupe tu kata mikono. Mwili ukaonekana mkubwa na akaonekana  ameridhika. Wakapewa walichoomba,  wakaondoka bila hata kumgeukia  Tunda.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Tewele alimshusha Tunda Mlimani City, akiwa ameshamlipa pesa nzuri tu.  Akashindwa kurudi nyumbani kwake.  “Mpaka kieleweke leo.” Akajisemea  Tunda wakati anafuata taksii yakumpeleka sehemu ya kusafishia picha iliyopo vichochoroni sio  mwangani kama hapo Mlimani city. Akamueleza dereva aina ya sehemu  anayotaka kwenda kusafisha hizo picha, dereva akamuelewa.  Na kweli akamfikisha sehemu  aliyoridhika. Kilikuwa kiji studio  kidogo tu. Akashuka Tunda baada ya kumlipa, akaingia ndani.

Alimkuta mtu  mmoja tu, ambaye alijitambulisha  kuwa ndio anafanya kazi hapo.  Akamuonyesha zile picha kwenye  simu yake, na kumuomba amtolee  nakala tatu tatu kila picha. Yule kijana  akafanya kwa haraka tu. Kwani mteja  alikuwa  Tunda  peke  yake.  Akahakikisha  amezifuta  kwenye  kompyuta yake. Akanunua bahasha  kubwa tatu. Ndipo akarudi nyumbani kwake sasa.  Alikuwa anacheka mfululizo kila  akizitizama zile picha. Akazigawa kwa mafungu matatu. Shangazi yake, Sera  mtoto mkubwa wa mjomba wake na Samatha kipenzi cha baba yao. 

Akazipanga zile picha vizuri kuanzia  vile yule mjomba wake anawapokea mpaka  pale sehemu ya kulia chakula. Akaanza kufikiria jinsi ya kutuma zile  video. Hakuwa na namba zao za simu.  Akawaza Tunda. “Hataa! Picha huwa  wanakanusha.  Wanasema  wamebambikiziwa vichwa. Video hawezi kupinga.” Akashindwa hata kukaa hapo. Akaita Uber ili imchukue kumrudisha  tena  kwa  yuleyule  kijana  aliyemsafishia zile picha. Alipapenda  pale, hapakuwa na watu wengi. Akajua  atakuwa salama. Umerudi tena  dada?” Yule kijana alimuwahi  alipomuona anafungua mlango.  Ndiyo. Ila safari hii ninashida ya tofauti.Akaanza Tunda.

Nina video ndefu tu. Nataka kumtumia mtu, lakini sio kwa simu. Nitamfikishiaje? Ushaiweka pamoja na umeridhika kuituma?” Tunda akafikiria.  Akakumbuka aliichukua kwa vipande. “Naweza kuiweka yote kwenye ile kompyuta ya mwisho kabisa. Nikakuonyesha  jinsi unavyoweza  kuiweka pamoja, kisha tukawatumia  kwa email.” Hapana. Nataka  kuwafikishia  mkononi.” Tunda  akamsahihisha.  Basi  tutaweka kwenye flash drive.Akamuonyesha aina ya hiyo flash drive maana alikuwa nazo akiziuza hapohapo, Tunda akaridhika. Hapo sawa.Tunda akakaa kwenye  kompyuta na kuanza kuandaa ile video huku akicheka. 

Mahaba ya Bagamoyo. Yakawa meneno ya ufunguzi wa hiyo video. “Mihayo na  familia yake ya pili.” Akaweka na tarehe.  “Hapa akiwa anapokea familia yake iliyompa  mtoto wa kiume wa pekee. Junior Mihayo.” Akaweka tena hayo maneno chini ya ile video. “Akimkaribisha mkewe kwa busu zito lililodumu kwa sekunde kadhaa, kama  mnavyoona hapo, na mtoto wake Junior.” Ikaendelea  kuonekana  Mihayo  akimbusu yule dada na Junior wakiwa tu ndio wamefika pale hotelini sehemu  ya kuegeshea magari. “Huyu ndiye Junior. Aliyejaliwa rangi ya  mama, sura ya dad.” Akaweka na hayo  maneno. “Huyu ndiye mwanamke aliyeweza  kuleta mrithi wa Mihayo hapa duniani.” Akaendelea kuongeza yale maneno  yakukera. “Mihayo Junior na mama yake.” Na hayo maneno pia akayaweka kwenye hiyo hiyo video akionekana yule mtoto na mama  yake tu.

 “Mihayo akiwa na familia yake. Yeye, mkewe na mtoto wao.” Akaweka hayo maneno  kwenye video aliyokuwa  amewachukua kwa karibu wakiwa  kule Bagamoyo sehemu ya  mgahawani. Akaongeza na baadhi ya picha zao wote watatu. Nyingine  akiwa Junior na baba yake, nyingine Junior peke yake ilimaradi tu kuwakera zaidi  maana ni kweli Junior alifanana na  baba  yake.  Huwezi  kukana.  Akaziweka picha nyingi za yule mtoto  akiwa amemvuta karibu na kuonekana  sawia, kisha mtoto na mjomba wake  kwa pamoja.  Tunda akacheka sana. “Duuuuh!” Akajikuta akihamaki kila akiangalia  zile picha alizoziongeza kwenye ile  video.

Akaona aongeze tena picha za wote watatu ili kuwakera zaidi. Kweli  watoto wanaunganisha sura za wazazi wao.” Akaongeza hayo maneno chini ya zile  picha alizokuwa ameongeza kwenye  hiyo video za wote watatu.  Basi zile picha akazipunguza mwendo  wakupita kwenye ile video. Zikawa  zinapita taratibuu. Ni kweli wawili hao  walifananishwa na huyo mtoto. Akacheka sana na kujisikia ameridhika moyoni.  Ilishakuwa usiku wa saa mbili wakati  Tunda amehitimisha kazi yake akiwa  ameridhika nayo. Ni kweli alitumia muda mrefu sana pale kwenye ile  studio, na yule kijana akimsaidia. 

“Sasa wakati Mzee anafaidi na familia ndogo Bagamoyo, acha  familia ya huku ya wajuaji, nao wafaidi pia. Wajue kinachoendelea  kwa dad mtukufu.” Tunda akajisemea na kufyoza.  Akatengenezewa na kuhifadhiwa hizo video kwenye flash tatu.  Akatumbukiza kwenye zile bahasha  tatu. Kisha akamtuma yule yule kijana  akamtafutie usafiri. Alirudi na  kumwambia amepata taksii, Tunda  akamlipa vizuri tu na pesa ya shukurani. Akatoka.

Akapanda tena taksii mpaka nyumbani shangazi wake, alipokuwa akiishi kwa mateso akinyanyaswa vibaya sana. Akajua kwa muda huo  wote watakuwepo kama bado wanaishi  nyumbani kwao. Akamwambia dereva,  akamkabidhi mlinzi, na amsisitizie  amkabidhi  kila  muhusika  bila  kuchanganya.  Na ahakikishe  anawakabidhi mkononi mwao. Kama  sio wote, basi mmoja wao awe  amepokea. Akamwambia na asubirie  jibu kama wamepokea. Dereva  akashuka  na  kufanya  kama  alivyoambiwa.  Baada ya muda akarudi yule dereva  ndani ya ile taksii aliyokuwa  amemuacha Tunda. “Mlinzi anasema  amemkabidhi mama.” Tunda akafurahi  sana. Tuondoke.” Tunda  akamuamuru yule dereva kwa furaha  zote. Akajua ujumbe umefika kwa muhusika mkuu.

Alimrudisha  Tunda  Mlimani City. Hakutaka dereva yuleyule aliyeletewa na kijana wa pale studio, ndio amfikishe nyumbani  kwake.  “Kuna mambo mengi siku hizi.  Wanaweza kufuatilia wakajua ni wapi nimetolea ile video. Wakambana yule kijana, kijana akamtafuta  mwenye taksii, wakaletwa kwangu.  Sitaki watu nyumbani kwangu.” Akajiambia Tunda wakati anashuka  hapo. Mpaka hapo bado hakuna  aliyejua ni wapi anaishi Tunda.  Hakuwahi hata kuropoka kwa yeyote,  hata usingizini. Hilo alilikusudia kuwa lake. Baada ya purukushani nyingi za  maisha, alijiambia angalau apate  pakujificha. Kuficha huzuni zake,  kupumzisha mwili na mawazo yake  bila mwingiliano wowote hata salamu  ya majirani. Alirudi kwake, akalala  kama mtoto mchanga kwa furaha zote na kusahau mkasa uliomuhuzunisha  wa waziri kwa muda.

 ~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Hiyo week hakutoka ndani kabisa.  Alikusudia kupumzisha huo mwili  baada yakutumiwa mfululizo, kwanza ni kama aliingiza kipato kikubwa sana. Akaona aupongeze mwili wake kwa kuupa mapumziko mazuri. Mwili huo  ulistahili mapumziko. Kwani alianza  nao waziri Mbawala. Alimtumia sana kwenye gari, wakaja kumalizia Sauzi.  Lakini yeye hakumlalamikia sana  sababu ya ustaarabu wake, japo  ilikuwa mfululizo, tena kwa juhudi  zote. Haya, akaja kwa mwanae waziri,  ambaye huyo ndio shuguli haswa.  “Junior!” Tunda akamuwaza. Masaa  machache na huyo kijana, lakini Tunda  alihesabu ni kama kuwapa wanaume  watatu kutumia mwili wake mfululizo.

Ni kweli alimtumia kwa pupa. Huyu  ni wakumtoa kwenye orodha kwa  haraka sana, pindi nitakapompata anayenihonga  vizuri.” Tunda  akafyoza kabisa kwa hasira. Haya,  akapumzika ndipo akaenda kwa  Tewele, Bagamoyo. Tewele haikuwa  shuguli nzito. Ni kama alipumzika  kidogo.“Ni Kweli nastahili mapumziko.Akajiambia Tunda.

Kupambana Kuishi Mjini.

Swali la wapi anampata muhongaji mzuri  likaanza  kuwa  ndilo  linalozunguka kichwani. Ni kweli  namba za simu za watu wa maana alikuwa nazo. Lakini akahofia  kuwatafuta,  historia  ya  waziri  Mbawala isije kujirudia. “Watataka  kuanza kuchimbua mambo mengii.” Akajiambia Tunda. Wasomi hao na  pesa zao. Nyadhifa wanazoshika ni za  juu, wanakuwa wanamaadui wengi. Akaendelea kufikiria Tunda.  Ikabidi kubadili utaratibu. Akaamua  kuanza kwa upya jinsi anavyosaka  wateja wake. Huku bado akiwa na yale  majina, lakini akaona awatafute kwa  njia nyingine itakayowafanya hata wao  waelewe ni biashara tu, sio kufuatana  nyuma kumtaka kumjua zaidi na  kuanza kusikiliza matatizo ya wake zao au familia zao. Ndio anafanyaje!?

Akazidi kuwaza Tunda.  Akaanza kutembelea hoteli na baa  kubwa kubwa tu ambazo alijua  atakutana na watu wa maana wenye  pesa isiyo na matumizi mengi. Basi,  ataingia hapo kwa heshima sio kama  changu. Kama msomi, dada mwenye  mipango na kujielewa.  Hakuwahi kujikosea hata mara moja.  Unadhifu wake vilevile na aliendana  na siku. Akienda ufukweni, utampenda  jinsi atakavyovaa na rangi yake ya  pekee aliyojaliwa na umbile lake,  huwezi kuacha kumtizama. Na  ukitupia jicho kwenye huo mwili  wake, hapo ndipo utakutana na mengi,  tena mazuri kwenye huo mwili wake.

Akihisi hajafanya vizuri anapokuwa  anaingia na kuvuta macho ya wengi,  basi atatulia kwenye meza na kuanza  kusoma mazingira  hapo. Akishakuchagua anaanza  kukupigia mahesabu. Hata kama mpo wawili. Tabia yake yakusoma  muonekano wa mtu ulikuwa pale pale.  “Kama anaweka saa ya ya bei ya chini kwenye mwili wake, hawezi kuhonga  pesa ya kuelewe kwa mwingine.” Alishajiambia Tunda.  Aliyejithamini ndiye aliyemfuata. Na  alijua ukifanikiwa kukuvuta kwenye  mwili wake. Ukamtazama tu, alijua ni  lazima atakuchomoa tu. Hata kama upo hapo na mwanamke mwingine.  Atakuchomoa katikati ya kundi na  kwenda kukuhudumia hata kwenye  gari au chooni. Hapo anakuonjesha. Lazima utakuja kumtafuta tu siku  nyingine tena sio nyingi. 

Akiona hujamuona na yeye anakutaka,  akiona unanyanyuka kwenda chooni,  na yeye anaweza kutoka mezani kwake  akijidai anakwenda kuzungumza na  simu mbali na pale. Lugha yake na  sauti yake, atakavyoanza kuondoka  pale akizungumza na ile simu, lazima  wa pembeni au aliowaacha nyuma,  mtamsindikiza kwa macho. Na hapo  ndipo wengine watashikwa na tamaa  baada yakumtizama sasa vizuri. Hana  kelele, taratibu lakini lazima uvutiwe kumtizama. Sasa yule aliyesimama na kumfuata, lazima atasababisha ajali hukohuko  kama sio nje ya choo cha kiume, basi  alikoelekea.

Na wakati wote kila anapofika popote,  ataagiza red wine. Basi watagongana  kwa nguvu, na atahakikisha ile wine  inaishia kwa yule mwanaume. Hapo  atashtuka mpaka utamuhurumia yeye. Atamuaga mtu aliyekuwa akijifanya  anazungumza naye kwenye simu.  Ataomba msamaha wa kukubembeleza  huku akifuta hiyo wine mwilini  akigusa sehemu utakazopenda asiache.  Ukimwangalia tu, kosa. Kama sio  mwanaume imara, lazima macho  yatakuvuta. Anaweza hata kuomba  shati lililoingia hiyo wine akafue  chooni. Hapo ujue basi tena.  Ameshakunasa.  Wale aliowaacha nyuma na wengine  watamuwinda  na  yeye.  Hapo  atakuchangamkia kwa mahesabu. Sio  papara. Kama asiyetaka, lakini atahakikisha  anakuweka  kwenye angaza zake, chini yake.

Kama  akishahudumia hapo hapo hotelini na hakupata aliyemwambia  anachukua chumba labda wamekuja na  wanawake zao, basi atakwambia uje umtafute wakati mwingine. Tena kwa  ujumbe sio kupiga simu hovyo ukamsumbua akiwa na wateja  wengine.  Akaondoa utaratibu wa kupigiana simu  kwa wateja zake wote. Hakutaka  kuzungumza na mtu kwenye simu. Na  alishawafikisha Mbawala Junior na Tewele sehemu ambayo wanahitaji  huduma yake kwa hali na mali. Akajua  hawawezi  kupotea  hata  akiwabadilishia utaratibu. Kwa hiyo  akaweka utaratibu huo mpya kwa  wateja zake wa zamani na hao wapya.  Marufuku kumpigia simu na ukianza jumbe  za  mapenzi,  anakukata mapemaa.

Sijui jumbe za uliamka  salama. Unaendeleaje? Uko wapi?  Hapana. Hakutaka mahusiano nje ya  kile mnachokifanya kwa wakati  aliokubali yeye.  Alishajiambia wote mnaiba, hakuna kudanganyana. Na wanaume hao  aliokuwa akiwahudumia, aliwadharau  sana. Hata waliotaka kuonyesha  mahusiano au kujidai wanataka  kumuoa ilikuwa kama kumchefua. “Ili  uniweke ndani ukaibe nje kama hivi?” Hilo ni swali alilokuwa akiwauliza bila  hata kukwepesha macho. Wewe furahia hapa, rudi kwa mkeo au  mwanamke wako. Tuachane kwa  amani. Usinidanganye. Mimi sio mtoto  mdogo.” Hapo Tunda ataongea kwa  ukali, bila kificho. Tena unaweza ukamkera zaidi akakuacha kabisa.  Chuki yake kwa wanaume ikaendelea. 

Ilianzishwa na baba Tom, wengine  wote aliona ni wale wale. Aliwatumia  kama chombo cha kujinufaisha nao.  Alimuona vile baba Tom akiiba. Sadiki. Akaja kukumbuka mjomba  wake jinsi anavyojidai kuwa mtu  mwadilifu nyumbani kwa shangazi  yake. Sheria kali kwa watoto zake na  mkewe. Makini kila anapokuwepo  nyumbani na kujiwekea mikakati  mikubwa kama mtu mwadilifu! Kumbe  mwizi ambaye amehamia hukohuko! Ameanzisha familia ya pili ndani ya  familia inayoonekana bora sana!  Akazidi kuchukia wanaume. Na  akikukamata, anaweza kukuchomoa  pesa yote ukarudi kwa mkeo huna hata  shilingi. Alikuwa akichukua pesa yao  bila  huruma. 

“Wanaume si wameubwa  mateso?  Basi  akahangaike kutafuta nyingine.” Hapo atawaza kimoyomoyo huku  akiingia kwenye wallet yake. Na  macho yake hayo na sauti, utatoa tu  zote.  Kama unataka huduma yake unatuma  ujumbe tu. Tena mapema. Sio  umshtukize. Umueleze muda utakao  mtaka awepo hapo, siku na mahali,  basi. Kama anakufuata mkoani, basi  ugaramie nauli yake. Tena kwa ndege.  Anakufuata, anakupa huduma ambayo  anajua, ukiwa na pesa inayoendana na  garama yake, lazima utamtafuta yeye, au hata utakopa tu, kumfanya akurudie.  Hakuna aliyeonja penzi la Tunda  akatosheka. Wazee hao wasomi wa  mjini na wafanyabiashara wakubwa  nchini, walikuwa kama watoto mbele ya  Tunda.

 Wengine  waliokuwa  wakisafiri mikoani kikazi, walimtaka  ende nao, au hata palepale mjini  wengine walidanganya kwa wake zao  wanasafiri kikazi kumbe wapo  wamejifungia na Tunda kwenye  nyumba za wageni.  Alikuwa yupo busy sana, kuanzia  jumatatu mpaka jumatatu. Wale wenye wake wanaojua kubana, walimtumia  Tunda kipindi cha muda wa  mapumziko wa chakula cha mchana  wakiwa maofisi. Kwa ujuzi wa Tunda,  hakuhitaji  muda  mrefu  sana  kumridhisha mteja wake mwenye  muda mfupi. Alijitahidi kwenda na  muda, kitu kilichowavutia wateja wake  wengi. Muda wa mchana, katikati ya  siku, jua likiwa linawaka nje, basi  ndani ya gari yako au kwenye nyumba  za kulala wageni. Hata kama una dakika 20 tu, Tunda alijua kuzitumia  vizuri. 

Basi wateja wake hao wa muda mfupi,  hawakuisha. Wakati mwingine endapo mmoja  akichukua chumba labda kwenye hoteli  nzuri. Akiondoka kuwahi kazini au  nyumbani ili asikamatwe na mkewe,  hapo anaweza kuingiza hata wanaume  wengine wawili au watatu wa haraka  haraka kwenye hicho hicho chumba.  Na sheria ni ukifika hapo hotelini,  usipite mapokezi. Moja kwa moja kuelekea kwenye chumba atakachokuelekeza  yupo yeye akikusubiri.  Hilo wakapenda wengi wenye wake  wa kali na wasiokuwa na muda mrefu  wa uwizi. Hatakutafuta baadae  kwamba ufumaniwe na jumbe za  mapenzi. Hataki kujua majina yako,  kwamba mtafutane nje ya kile   kinachowakutanisha pale na wala  hutajua jina lake la ukweli.

Basi ikawa  rahisi kwa wengi. Unapewa huduma  yako. Kama hukufumaniwa wakati wa tukio, basi ujue hutakamatwa kwa sababu ya Tunda. Kwanza yeye  mwenyewe alikuwa makini. Hakutaka kugonganisha wateja wake. Na wala usingekuta simu ya Tunda ina  kelele hata mara moja. Akiwa na  wewe, ujue ni wewe tu. Simu yake ipo  kwenye pochi. Na haina sauti. Kama  mteja akimtafuta, ni kwa ujumbe tu.  Kwa hiyo kama siku hiyo na muda huo  unaomuhitaji hatakuwa na mteja  mwingine, atajibu kwa kifupi tu “OK”.  Basi hapo utahitajika kutafuta mahali. 

Kwa wale wenye nyadhifa za juu,  aliwaelewa. Yeye ndiye aliyekuwa  akitafuta sehemu ambazo alijua hata  wahudumu hawatamuona. Atakwenda kuchukua  chumba  huo  muda  uliomwambia unayo nafasi, kisha  anakutumia ujumbe ni wapi umfuate.  Na hataki umcheleweshe. Umuweke  hapo masaa, uje umwambie kulikuwa  na foleni ndio maana umechelewa! Au  sijui mtoto wako anaumwa ukapitia  duka la madawa na habari ndefu za  kifamilia, hazimuhusu.  Na kama hana nafasi atakupa yeye  siku na muda atakaokuwa tayari. 

Lakini kabla hamjakutana lazima  umrushie pesa yake nusu na baada ya  kukuhudumia, ndipo unamalizana  naye. Hakuwa akipokea pesa taslimu,  kwa kuhofia kuporwa. Wateja wake  wote walimrushia kwa simu. Na  wakati wote hakukosa wateja sababu  ya ubunifu wake wa kuwanasa na  kitandani.

Na endapo yeye ndiye anayetafuta  sehemu ya kukutania, pia pesa  unamtumia kabla. Ili kama utachelewa  zaidi ya muda mliopanga, akiondoka  iwe juu yako. Na pesa ya usafiri wake  kumfikisha hapo pia unatuma kabla ya  kukutana. Na jinsi anavyoomba kwa  upole na unyenyekevu, usingejua kama  ni moja ya taratibu za muhimu sana  alizojiwekea. Kuwa lazima hayo  malipo uyatangulize. Atakuomba kwa  upendo na kukubembeleza. Na hata atakapoondoka endapo umechelewa hapo hoteli wala  hatagomba. Atakutumia ujumbe wa  kukuomba msamaha kuwa kwa kuwa  umechelewa, inabidi aondoke, anayo  miahadi mingine ya muhimu sana,  hawezi kuendelea kusubiri.   

Basi atakusihi wakati mwingine  utakapopata nafasi, umtafute. Huwezi  kumchukia. Hapo ujue amekwenda  kwa mteja mwingine. Ataondoka  kwako akiwa hajaingia hasara.

Garama  za chumba na usafiri wakumfikisha  hapo ni mteja amegaramia mwenyewe.  Na ukijibu kuonyesha ni makosa yako  mtapanga wakati mwingine, basi  anakuhakikishia hapo ameondoka, lakini si kweli kwamba ataachia kile chumba mteja alichogharamia, atakachofanya ni kutafuta mteja wake mwingine.  Watatumia chumba hichohicho, lakini  mteja huyu wa pili, atakilipia tena kana  kwamba hakijalipiwa.  Hapo Tunda anakuwa ameingiza pesa  zaidi. Inaweza kufanya hivyo kwa mteja wa pili  na watatu pia. Inategemea na aina ya  mteja. Wale ambao hawana shida  kulala nje na makwao, basi ndio ujue  mtalala naye hapo hapo kwenye chumba hicho kilicholipiwa na mteja  wa kwanza, na hataingiza mteja  mwingine.

Ila ukilala naye usiku  kucha, ujue pesa atakayokuchomoa  hapo, ni zaidi.  Akiona huo mwezi upo kimya.  Hajafikisha pesa aliyojipangia. Labda  anapata wateja wachache wa pesa  ndogo, anarudi kwenye orodha ya  majina ya watu aliyoiba kwa Mbawala  Junior au Tewele. Ataipitia majina yote. Yule aliyetaka kumtumia kama ni waziri au mtu mwenye nyadhifa ya  juu nchini au pesa nyingi kama  mfanyabiashara  ambae  hasubirii  mshahara, basi alihakikisha anajua  ratiba ya huyo mtu hata kwa  kukufuatilia kwenye vyombo vya  habari. Kisha anachunguza sehemu  zake anazopenda kwenda kwa starehe  au mapumziko.

 Hata kwa kuingia kwenye istagram zao na wake zao wale wanaopenda kutangaza matukio ya familia zao, twitter au  facebook. Alifungua huko akaunti sio  kwa ajili yake. Kwaajili yakufuatilia  watu. Ajue huyo anayemuinda alipo. Hata kama upo na  familia yako. Ilimradi ajue kwa wakati  huo uko wapi.  Akishajua huyo mtu anayemuwinda  yupo sehemu fulani, atakwenda akiwa  amependeza  sana  na  amevaa  kiheshima tu. Atapita mbele yake,  lakini atahakikisha anajua kama  amepita. Hata kwa kudondosha simu  itakayomfanya  ahamaki  kwa  kulalamika kwa sauti yake yakuvutia.  Akishamaliza kuiokota na pengine  kama huyo mtu ni muungwana,  atampa pole, pengine na kusaidia hata  kumuokotea. Basi, atakushukuru huku akikutizama na macho yake ya mtego.  Kisha atakwenda kukaa sehemu anayojua utamuona hata kwa mgongo  tu. 

Na kwa kuwa alikuwa na umbile  ambalo alijua akisimama lazima  mwanaume yeyote mwenye uchu  atamsindikiza japo kwa macho tu, basi  akishakaa na kuagiza kinywaji chake  kile kile red wine. Mtindo wake uleule, hataacha kwenda msalani au  kujidai anatoka nje kuongea na simu.  Asipofanikiwa kuona muhudumu  anamfuata kumwambia ametumwa  kutoka meza fulani kumuuliza anataka  nini, basi ujue huyo waziri au mtu,  atamwagiwa wine tu. Hawezi kuepuka  kuloweshwa na kinywaji hicho kama  usipomfuata mapema kwa hiari yake.  Au kama amekwenda kuwinda club,  basi atamkanyaga huyo mtu kwa nguvu mpaka aumie na yeye ndio  atampa pole na kubembeleza. Na hapo ujue hataishia kukubembeleza huo  mguu tu.

Na kama anayemtaka akijua ni baba  wa familia. Unapenda familia yake.  Zaidi watoto ndio wamejaa kwenye  akaunti zako za Facebook na Instagram, basi ataanza kufuatilia  sehemu unazopenda kwenda na hiyo  familia yako. Akijua labda umepeleka  familia yako sehemu fulani, basi  atakufuata hukohuko.  Hata kama ni kuogelea. Na yeye  atavaa nguo za heshima tu za  kuogelea.  Lakini  kwa  jinsi  alivyojaliwa, hawezi kuwepo kwenye  vazi la ufukweni, ukaacha kutizama  hizo sehemu zilizoachwa wazi. Hata  kama mke mtu ndio yupo ndani ya maji na hao watoto, basi atakuwa mwema  kwa mwanamke na wale watoto. Atatengeneza vimichezo ndani ya yale  maji akiogelea na hao watoto, mpaka  watoto wampende.  Wakishaanza tu anti, anti ndani ya yale  maji, basi ujue na baba mtu atavutiwa. 

Hapo ndipo atakufuatilia. Mke na  watoto ndani ya maji, yeye anaweza  hata kumfuata baba mtu hata chooni akiona ananyanyuka. Anatoka ndani ya  hayo maji taratibu na kuacha familia  yake ndani ya maji, anamfuata baba  mtu sasa. Huko ndipo atahamisha  mitego kwa huyo baba. Na kwa kuwa  ulishavutiwa naye tokea mwanzo, na  nguvu ya ushawishi aliyokuwa nayo,  kama hatakuhudumia hapohapo, basi  lazima mtawekeana miahadi ya  baadaye tu.  Na akishafanikiwa kulala na mkuu  mmoja, labla ni waziri au mbunge, au  tajiri  mkubwa  mwenye  pesa yakueleweka, basi anakuwa na uhakika  wakupata anayefuata mwenye pesa  kama huyo.

“Paka anatembea au  kuzungukwa na paka wa aina yake.” Alikuwa akijiambia Tunda. Kwa hiyo meza aliyokaa mwenye pesa mmoja  aliyekuwa akimfuatilia, alijua wenzake  pia watakuwa hivyo hivyo.  Akimpata mmoja wao, ujue atapata na  wengine tu. Kama hakufanikiwa kwa  kujipitisha wakamtongoza, basi ile tabia ya kuiba namba za simu kwa  mteja aliyempata, aliitumia kama  akiona sio hatari ataiba tu. Iwe wakati  huyo mteja akiwa bafuni akioga baada  ya shuguli nzito za Tunda hapo  kitandani, kabla Tunda mwenyewe  hajaingia kuoga naye, ndipo ataiba  hizo namba za simu za aliokuona nao  na anayemtaka yeye au kama ni mteja wa usiku kucha, atahakikisha yeye  halali mpaka amepitia simu ya huyu  mteja aliyelala naye hapo ili kupata namba za  marafiki zake. 

Utaratibu  wake ukawa  ni  uleule.  Akishazipata hizo namba kwa  kuzihamishia kwenye simu yake ambayo kwanza ilikuwa inajizima kila  baada ya sekunde 10  kama hajaishika,  na ilifunguka kwa kuingalia. Yaani  macho yake yeye Tunda ndiyo  yalifungua simu hiyo ya pesa nyingi  sana. Kwanza ukumbuke hakuwa  akiitoa hovyo. Ilikuwa ikikaa kwenye  pochi yake wakati wote. Kwa kuwa  hakutaka muingiliano anapokuwa  kwenye kazi moja, mteja wake  amuone yupo busy na simu. Labda  muwe sehemu ya hadharani yupo na  wale wateja wasiogopa kuiba naye.  Wakiwa wapo nje, hadharani, labda huyo mteja anakunywa, basi hapo  ndipo utamkuta ameinamia simu yake  anacheza games zake kwenye simu  yake, akiendelea kunywa maji yake  taratibu lakini kama yupo chumbani na  mteja, usingemkuta akichezea simu au  kushika simu yake hovyo akisoma  jumbe za wateja wengine.

Labda  kipindi hicho cha kuiba namba. Na  akishamaliza kujihamishia hizo namba  za simu, anairudisha simu yake  kwenye pochi yake, basi. Hutaikuta  simu yake imezagaa hovyo au hata  mezani.  Kipindi cha bunge, ndio kilikuwa  kipindi cha neema kwake. Alikiita  kipindi cha mavuno. Alikuwa na  viongozi wake ambao ni wateja wake  wa mara kwa mara. Kwa hiyo kipindi  hicho cha Bunge, anatafuta kwenda na mmoja wao huko Dodoma, na  kuwabadilisha huko atakavyo.

Yeye ndiye aliyewapanga kwa muda wake,  lakini usiku aliishia kulala na  aliyemwita au aliyempeleka pale jijini Dodoma.  Wakati  mwingine  aliweza  kuwatongoza wakiwa wamekaa meza  moja wakila na kunywa. Ikitokea  mteja mmoja amemwita kwenye baa,  wakaja rafiki zake kula na kunywa  nao.  Akishagundua udhaifu kwenye  maongezi na akajua ni mtoaji,  alihakikisha akiwa anaondoka na  aliyekuja naye, pia ataondoka na  namba ya simu ya atakayemchagua, au  atamuachia yeye namba akiwa na  uhakika wa kutafutwa siku inayofuata,  kwani alikuwa na uwezo wa  kumchomoa anayemtaka palepale mezani, wakatoka kwenda naye chooni  au kwenye gari.

Na dakika tano kwa  Tunda  zilikuwa  nyingi  sana,  kuwachanganya kwa ufupi, na lazima  watadai huduma ndefu siku nyingine.  Tunda hakujali ulipo, au hakuangalia  sura, au umbile wala umri wa  mwanaume anayetaka pesa yake. Kila  mazingira alipo alijua jinsi ya  kuyasoma na jinsi yakuyatumia vizuri  kutengeneza pesa. Kwake yeye  kwenye baa au kwenye mahoteli ni  sehemu ya kazi sio starehe.  Kwa hiyo kila alipokuwepo kwenye  maeneo hayo akili yake ilikuwa  ikifanya kazi kwa makini sana.  Akiangalia wateja wapya, jinsi ya  kumtoa kwenye meza yako hata kama  upo na mkeo au mwanamke mwingine,  na eneo gani atakalokuonjesha kwa muda mfupi ili kesho umtafute. 

Hakutaka kuwa rafiki na pombe  kabisa, ili asije kulala na mwanaume  yeyote bila akili yake kujua anachofanya.  Japokuwa hakuwa akinywa pombe kabisa, lakini hakuacha kuagiza red  wine kila sehemu aliyokwenda hasa akiwa anakwenda kuwinda, basi  atakuwa na maji pembeni ambayo  hayo aliyanywa. Tunda alikuwa  mnywaji mzuri wa maji.

Tabia yake ile yakutokulala na mwanaume yeyote bila kondum, hiyo hakuwahi kubadilika  hata kusahau. Hata uweje au unampa  kiasi gani cha pesa au mtakuwa naye  kwa muda gani, hatasahau kondom.  Madhara aliyoyapata kutoka kwa baba  wa kambo, kumpa mimba na kutolewa kikatili, kuvuja damu kwa wingi na maumivu makali aliyoyapitia baada yakutolewa ile mimba! Bado aliyakumbuka  kana  kwamba  yametokea siku iliyopita. Aliapa  kutothubutu kuingiza mtoto wa mtu  yeyote tumboni mwake kama bado  anao huo uwezo, maana kipindi  anaishi kwa shangazi yake, aliwasikia  shangazi yake na watoto wake,  wakimwambia mama yake alimtoa  kizazi kabisa.  Hakuwa ameelewa kwani bado  alikuwa akiendelea kupata siku zake  kama kawaida. Alinyamaza, asijue ni  jinsi gani mama yake au hao  wataalamu walikitoa hicho kizazi  chake.  Lakini  pia,  hakutaka  kukaribisha mtoto tumboni mwake  wala hakutaka gonjwa lolote mwilini  mwake.

“Malaya hawa, wala situmii  nguvu  nyingi  kuwatongoza! Wamejawa tamaa! Wanalala na wangapi? Watakuja kuniua bure.” Tunda akaendelea kuzingatia huo  mkakati.  Kuna  kipindi  Mbawala  Junior  aliponogewa akamuomba waache  kutumia Kondom, Tunda alimkatalia,  na  kuanza  kumkwepa  kwa  kumpunguzia  muda wakukutana.  Alijua atakuwa amechoshwa na  kondom, maana hata katikati ya tendo,  Tunda  alipokuwa  akimuona  anakwenda mwendo mkali na mrefu,  alikuwa akimbadilisha kondom, na  yeye kujipaka jeli ndipo wanaendelea.  Akajua ameanza kuchoshwa na huo  utaratibu na kuanza kumzoea. Akaanza  kumpunguzia kukutana na muda.  Wakati mwingine alimwambia yupo  Dodoma anaweza  kikazi,  basi  kumuona hata kwa lisaa. Basi hapo   

walitumia hilo lisaa, kisha Tunda  anaendelea na wengine. Akaacha  kumpa masaa  yakutumia mwili  wake. 

Hakuwa na rafiki wa kike hata mmoja,  hata hivyo hakuwa na muda na  marafiki. Muda ambao hakuwa na  wateja aliutumia yeye mwenyewe.  Kufanya manunuzi ya vitu vya  kumpendezesha, au kwenda saluni kutengenezwa kucha na nywele au  alitumia muda huo kupumzika kwa  kulala kabisa tayari kwa kazi nyingine. Na hakutaka mahusiano hata na watu  wanao muhudumia huko masaluni.  Akifika anakuwa kimya. Ukijitahidi ni  kutoa tabasamu. Hata umuulize jina  lake, atatoa tu tabasamu, kimya.  Atahudumiwa, na kulipa. Atashukuru  kwa heshima zote, na kutoa tip kitu walichopenda  wanaomuhudumia na kuondoka.  Na  Hatachangia wala kuzungumza na  simu pale saluni. Hakutaka kuacha stori  zake pale saluni kama alivyokuwa  akisikia za wengine. Mwishoe  wakamzoea! Hapana. Hayo ndiyo yakawa maisha ya Tunda kwa ufupi na urefu.

 

Mwanzo wa Gabriel.

Tunda  akiwa  amepumzika  kwenye hoteli moja mjini  Arusha wakati mteja wake  amemuaga anakwenda kuonana na mtu  mahali, aliamua kufungua tv. Alikutana na taarifa ya habari ambayo  ilionyesha kijana mmoja huko jijini  Dar, akitoa misaada kwa watu wenye  ulemavu wa ngozi. Mtangazaji alisema kiasi  cha  pesa  kijana  huyo  aliyejulikana kwa jina ya Gabriel,  alichotoa, ili kuwawezesha walemavu  hao kuwa na kitengo chao maalumu.  Zilikuwa pesa nyingi sana zilizomtoa  mate Tunda. “Huyu ndio mteja  ninayemtaka mimi. Akihonga mara  moja, hamtafutani tena mpaka baada  ya miezi. Na wewe unapumzika  kabisa.” Tunda aliwaza.

Aliendelea kusikiliza habari za Gabriel, akajua ofisi zake zilipo. “Najipa mapumziko ili kumsaka huyu  kaka mpaka nimpate.” Tunda  alijisemea.  Aliporudi mteja wake, alimwambia  amepata dharula Dar, lazima aondoke  na ndege ya kesho yake. “Mbona  hatujamalizana mimi na wewe?” Nitarudi baada ya siku tatu.Tunda  akamtuliza kwa maneno mazuri mpaka  akaridhika na kumruhusu lakini  akamuomba aondoke na ndege ya jioni  ili siku hiyo inayofuata wawe wote  hapo hotelini. Tunda akaona ni haki.  Akakubali. 

Aliondoka jijini Arusha siku inayofuata  akirudi jijini Dar, kumsaka Gabriel, kijana milionea, aliyemuona luningani.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Usikose mazito na ya kusisimua katika harakati za Tunda, na huyo milionea Gabriel anayemsaka na yeye anayo yake. Usipitwe na kukosa muendelezo. Tunda atapitishwa kwenye mengi mno japo anazo taratibu zake makini alizojiwekea mwenyewe. Ndege mjanja... 

CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment