Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com Nilipotea! – Sehemu ya 13. - Naomi Simulizi

Nilipotea! – Sehemu ya 13.

 

A

kaanza kupitia zile namba za simu  alizoiba kwenye simu ya Kinny wakiwa hotelini. Akachagua jina moja la meneja wa  bandari. Alishamuona akijibu tuhuma  za wizi unaoendelea huko kwenye  bandari ya Dar kwenye luninga. Jina  lake likavuma kwa kuwa yeye ndio  alikuwa kama mkanushaji mkuu wa tuhuma hizo. Alikuwa mstari wa  mbele kusafisha kwa kukanusha na  kutoa ushahidi. “Huyu huyu.” Tunda  akamchagua yeye.  Akakaa sawa nakuamua kumtumia  ujumbe. Samahani kwa ukimya. Nimekuwa  na mambo mengi. Lakini naahidi kukutafuta  week ijayo.’ Akamtumia huo ujumbe.  Alichojichanganya, ni pale alipopiga  kutaka kujua ni nani. Tunda akacheka  nafsini mwake wakati simu yake  ikiingia.

Alijulikana kama Tewele.  Tunda akatumia akili ya haraka.  “Samahani kipenzi. Nipo katikati ya jambo. Naweza kukupigia baadaye kidogo, Tere?” Tunda alipokea akionyesha na haraka  kwa Tere, na sauti nzuri sana. Nafikiri  umekosea namba. Mimi ni Mr. Tewele sio Tere. Oooh Nooo. Samahani kaka yangu.  Samahani sana. Nahisi kwa kuwa majina yenu yanafuatana kwenye orodha yangu ya  simu, nimeandika ujumbe nikiwa na haraka  huku nikijilaumu kwa kutomtafuta Tere  wakati anashida na mimi. Naomba nisamehe  kaka yangu. Samahani sana kwa usumbufu.” Tunda alijilalamisha kwa sauti ya deko  huku akimwita kaka, wakati ni baba  mtu mzima tu tena mkubwa hata kwa  umbile. 

Akamsikia akicheka taratibu. “Usijali.  Hamna usumbufu wowote ule. Nilitaka  kuhakikisha napata ujumbe wangu sio wa  mwingine ndio maana nikapiga kuhakikisha.” Samahani sana kaka yangu. Nafuta kabisa  namba yako. Sijui nan..”Akajidai amesita.  “Haitatokea tena.” “Kabla hujafuta namba  yangu, na kunitupilia mbali mapema, inabidi  uniambie wewe ni nani na imekuaje wewe una namba yangu, wakati mimi sina namba yako.” Na yeye aliongea kwa sauti iliyotulia na kama Tunda.   

“Ni kwambie ukweli? Ila sitakutajia aliyenipa  namba yako.” Mbona masharti tena? “Unataka kuambiwa ukweli au kudanganywa?” “Ukweli mzuri, japo wakati  mwingine unauma.” Tunda akacheka.  Basi kwa kuwa nipo kwenye kitu cha  muhimu, naomba nikupigie baadaye  tafadhali.” “Nasubiri. Tunda akacheka  kidogo. Mida gani mizuri? Tunda  akauliza taratibu. Kwanza nitajie jina  lako, ili nitunze namba yako kabisa. Nikiona  sipati hiyo sauti nzuri mpaka kesho, nipige  mwenyewe.” Tunda akacheka sana.  Nitapiga. Hata kama haitakuwa leo, lakini  nitapiga. Na nilikuwa na shida na wewe ndio  maana nikapewa hiyo namba, nikaambiwa  wewe, Tewele, ndio jibu la mambo yote.  Nikikupata wewe, shida yangu imeisha.” Tewele akacheka sana.

“Kweli tena.” Tunda akamuhakikishia. Sasa mbona  hujanitafuta, au nimeshapata msaidizi?“Mmmh! Kwa kiasi kikubwa ni kama  nimepata ufumbuzi. Nitakueleza zaidi  baadaye. Naomba nikuage kwa sasa, na  samahani sana.” Hamna shida. Nani tena? Tewele akitaka kumfahamu jina.  Irene.” “Asante Irene. Nimefurahi  kukufahamu. Naamini tutawasiliana. Asante.Tunda akashukuru na kukata  simu. “Yesss!”Akaruka pale kitandani  akishangilia kwa ushindi.   

Mbawala!

I

likuwa siku ya jumatano Tunda akakumbuka ahadi yake kwa Mbawala. Akaamua  kumtumia ujumbe.  “Huyu naye asitake kunizoea. Siku mbili kwani mimi  mkewe!” Akajiambia Tunda huku  akimwandikia huo ujumbe Mbawala. ‘Samahani. Naona ijumaa imeshindikana.  Nitakuona jumamosi.’ Hapo hapo  Mbawala akapiga. “Mpaka moyo  umepasuka!” Tunda akaanza kucheka.  Pole.” “Mbona napata siku moja tu? Lakini hutakaa ukaijutia. Nimeshindwa kubadilisha ile miahadi niliyokwambia. Na  nimuhimu sana. Ila nitahakikisha inafidia na  hiyo ijumaa.” Tunda akaongea kwa  kujiamini. Yesss!Mbawala akasikika  akishangilia. Tunda  akacheka. “Ninavyokusubiri kwa hamu, utafikiri nini  sijui! Tunda akacheka taratibu.  “Naamini tutapata wakati mzuri.” Asante Fina.” Mbawala akashukuru kwa  heshima zote, utafikiri amepewa  alumasi, kumbe ni kutembelewa na  Tunda!  

Tena mambo yenu naona kabla hata ya  ijumaa yatakuwa safi. Mwenzangu  ameafikiana kwa haraka sababu ya bei. Ukija  jumamosi, utakuta nimekuandalia kila kitu.  Nitakukabidhi ukija.” Hilo akalifurahia zaidi  Tunda. “Heshima   itaongezeka kwa mjinga yule. Akimaanisha Kinny ambaye  alishamchukia. Inamaana  yeye  ndio  atamkabidhi Kinny!  Na inamaana atalipwa  pesa yake bila shida! “Naua ndege  wawili kwa jiwe moja!”Akajiambia  Tunda.  Umeongeza umuhimu wa hiyo safari. Mbona unanivunja nguvu tena? Mbawala  akalalamika. Kwa nini tena?” Tunda  akauliza huku akicheka.

 Naona kama umenitoa uthamani.” Hata kidogo.  Tuombeane uzima, labda shukurani zangu utazielewa kwa vitendo.” “Ninavyozisubiria  kwa hamu! Tunda akacheka. Naomba  nikuage  Mbawala.  Tutawasiliana.” Naruhusiwa kupiga wakati mwingine? Hilo  ndilo alilojiambia hatakaa akafanya, kuanza tabia ya kupokea simu au kutumiana jumbe  za mapenzi na yeyote yule. Naomba  usijisikie vibaya. Nakuwa busy sana. Wakati  mwingine mpaka simu naona kero. Naomba  uniamini kuwa nitakuja siku ya jumamosi. Upo  kwenye ratiba yangu. Na huwa sio  mbambaishaji.” Nimekuelewa Fina. Basi  niruhusu nikate mimi tiketi na nitume pesa ya  taksii itakayokupeleka uwanja wa ndege. Ila  huku ujue mimi nitakuwa nikikusubiri  uwanja wa ndege.” Nakushukuru Mbawala.  Asante sana.Tunda akashukuru na  kukata simu bila yakuongea maneno mengi.

    Ukimsikia akizungumza kwenye simu,  unaweza kumdhania ni msomi wa hali  ya juu na yupo na majukumu mazito na  muhimu.  Kumbe  kama  hapo  alipokuwa akizungumza na Mbawala  na Tewele yupo kitandani kwake  ametulia wala hana pakwenda au  chakufanya. 

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Mpaka hapo akajiambia anao watu  watatu tayari wakumwingizia pesa kwa wakati huo.  Mambo safi. Akacheka. Akiwa kwenye ile hali ya furaha akaona simu yake imeingia ujumbe kuwa pesa imeingia. Akatazama ile pesa  akajipongeza. Mbawala ndiye aliyemtumia ile pesa. Hajakaa sawa akiwa anafurahia pesa, ujumbe mwingine ukaingia. Safari hii ulikuwa ukitoka kwa Kinny. Tunda  akafikiria. Hakutaka hata kuusoma. Akaamua kutoka hapo kitandani na kuelekea maliwatoni, kuoga, ili sasa atoke hapo ndani akatengenezwe tena huo mwili alioamua kuufanyia biashara.  

Mwili wa Tunda ulikuwa ukifanyiwa waxing mara kwa mara. Usingekuta  vinyweleo popote, au kipele hata  kimoja. Laini na nyororo wakati wote.  Akakusudia siku hiyo ya jumatano  mpaka alhamisi iwe ni mwili wake tu.  Utengenezwe. Waxing, sauna, masaji  na kubadili nywele na kucha.  Alitoka bafuni akakuta Kinny amepiga  simu na kutuma tena ujumbe. Baada ya  muda akaona anapiga tena simu.  Akajifikiria.  Apokee!?  “Huyu  mbambaishaji tu. Sina mpango naye  kwa sasa mpaka nikitoka Dodoma na  kazi yake. Anipe pesa yangu,  niachane  naye  kwa  amani.” Akakusudia kumpuuza. Akaweka simu  pembeni, na kuendelea kujitengeneza.  Akamkumbuka Tewele,  akaona amuweke kidogo. Amsubirishe, asije kumuona anajirahisisha. 

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Wakati anakaribia kutoka nyumbani  kwake ujumbe mwingine ukaingia  kwenye simu yake. Akautizama  akidhani ni Kinny, akakuta ni Tewele.  ‘Natoka kwa ajili ya chakula cha mchana.  Kama ungependa kuungana nami karibu.’ Akamwandikia jina la sehemu  atakayo kwenda kula. Tunda akasoma  nakubaki akifikiri chakujibu. ‘Naweza  kukupigia sasa hivi?’ Tewele akatuma ujumbe mwingine. Tunda akampigia  yeye.  “Umenisahau Irene!” Tunda akacheka.  Lakini ningekupigia.” “Unanafasi sasa hivi? Kwa muda mfupi. Lakini sehemu uliyonitajia  ni wazi sana na wewe mtu mkubwa sana.  Sitaki kuwa magazetini kesho. Tewele  akacheka sana huku akifurahia na yeye hilo  wazo la kutoonekana  naye  hadharani. Hata kwake itakuwa salama  japo alilisahau hilo kwa uchu.

“Basi  chagua ni wapi ungependa tukale. Ili  tufahamiane zaidi. Hiyo sauti imegoma kutoka kichwani kwangu. Nataka niiweke  kwenye sura sahihi.” Tunda akacheka  kidogo. Labda uchukue chakula, halafu  twende tukale sehemu. Mimi na wewe tu sio  hata na dereva wako. Hilo nalo Tewele  akalikubali bila shida.  Unataka kula nini?” “Mimi sio mchaguzi Tewele. Utakachokula ndio na mimi nitakula hichohicho. Ni  surprise.” Tewele akafurahia na hilo.  Sasa nitakukuta wapi nikishakuwa na hicho  chakula?” “Unafikiri itakuchukua muda gani kuwa na hicho chakula na kufika Mlimani  city?” “Nipe kama dakika 30 hivi. Nimtume  dereva akalete chakula chetu, halafu nikufuate  hapo Mlimani city.” Sawa, lakini naomba usiniweke tafadhali. Ufike baada ya dakika 30 kweli.” Tunda akasisitiza kama  asiyetaka kupotezewa muda.  Akamtia hofu Tewele, yakuonekana  hovyo kwa mara ya kwanza.

“Basi  sababu ya foleni ambazo hazitabiriki hapa  mjini, tufanye baada ya lisaa.” Sawa. Tunda akakata simu. Akacheka na  kurudi kukaa akisubiria muda.  Akaangalia saa yake, akajua ni saa  ngapi atoke hapo. Akakaa kwenye  kochi akisubiria muda.  Ni kweli Tunda hakuwa akipenda kelele. Hata luninga aliwasha kwa  sauti ya chini tu. Akakaa pale akiangalia luninga huku akimfikiria Tewele. Nini amfanyie ili  kumpagawisha  kiasi chakuingia  kwenye orodha ya watakao muweka  mjini! Alikaa pale mpaka muda wake  aliokusudia kutoka ulipofika. Akaita taksii. 

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

     Alipokuwa akiingia Mlimani City  akiwa ndani ya hiyo taksii akampigia  simu Tewele. Akamwambia alishafika, anamsubiria. Akamuelekeza aina ya  gari yake, na sehemu alipoegesha.  Tunda akamuaga. Akamlipa yule  dereva taksii, nakumwambia amshushe  mbali kidogo tu. Akatembea taratibu  mpaka dirishani kwake. Akagonga.  Tewele akabaki ameduaa. Tunda  akatabasamu na kuangalia muda.  “Naona nimefika kwa wakati.” Akaona amtoe kwenye ule mshangao.  Tewele akabonyeza sehemu ya  kufungua mlango. Ingia garini Irene. Ni kweli hujachelewa.Tunda  akaingia.  Na  hapo  alikuwa amependeza haswa.

“Mmmh!” Mbona  unaguna tena?Tunda akamuuliza  wakati anafunga mkanda. Heri  nilivyokuomba tuonane. Ningepitwa. Tunda akacheka. Pole na kazi. Akaanza Tunda taratibu na tabasamu  usoni. Asante. Na wewe pole na  majukumu.” Asante. Tewele  akabaki amekodoa macho. Tunda  akacheka.  Alikuwa amevaa kigauni tena. Chenye  mikono mifupi tu, mpaka kwenye  viwiko, ila safari hii kifupi zaidi.  Kimechanua kidogo. Rangi moja tu,  rangi ya bahari. Akavaa na kiatu cha  juu cha wazi. Rangi ya kama kile  kigauni. Yaani vilifanana. Cheni  yake vile vile mguuni. Ila alikuwa na  pochi nyeusi iliyoendana na mkanda  mwembamba mweusi kiunoni. Hereni  fupi na cheni yakawaida isiyo na kidani. 

“Kina nani hao wanaopata bahati ya miahadi na wewe mchana?” Tunda  akacheka kidogo. Kuna mtu nilikuwa  nakutana naye. Ni mambo ya kikazi,  nashukuru Mungu mambo yameenda  salama.  Njaa  inauma  Tewele.  Sijanywa chai, nimekuwa busy tokea  asubuhi!” “Nina chakula hapo  nyuma.” Naipata hiyo harufu nzuri. Tunda akasifia huku akigeuka nyuma.  Chagua sehemu unayotaka twende  tukale, na mimi nishibishe macho  yangu. Umependeza, huchoshi  kuangalia!Tunda akacheka. Asante  Tewele. Hata wewe upo vizuri. Ila  naomba nilegeze hiyo tai bwana.  Utafikiri upo na raisi!” Wewe ndio umenifanya nitoke hivi.” “Mimi  tena!? Tunda akauliza huku akicheka. 

“Ndiyo!  Hukutaka  nichelewe. Koti lenyewe nimevulia  kwenye gari kwa haraka. Hilo hapo nyuma.” Basi acha mimi nikutoe tai.Mbawala akacheka. Sawa. Akakubali.  Tunda alimsogelea mpaka karibu sana.  Una macho mazuri Irene!” “Macho  tu?Tunda akauliza huku akiisogelea  ile tai. Sauti nilishasifia. Au  umesahau?” Tunda akacheka bila  kujibu akiwa amemsogelea akijaribu  kulegeza tai. Akamfungua kifungo cha  kwanza kilichokuwa kimeshikilia hiyo  tai.  Akamtizama  machoni,  yakagongana. Akacheka na kulamba  midomo yake. Na cha pili?” Tunda  akamuuliza taratibu tu.  Hamna  shida.  Tewele  akakubali kwa haraka. 

Tunda  akakifungua, akaachanisha hilo shati kidogo tu, kwa kupitisha kidole kimoja  ndani  kama anayemtengeneza, kumbe nia ni  ilikuwa  kumsisimua tu. Akaona amevuta pumzi  kwa nguvu. Akajua amemgusa sawa.  Kisha akamkabidhi tai yake.  “Mmmmh!”Akavuta pumzi kwa  nguvu. Au niitundike tai hapo  nyuma?Tunda akauliza taratibu.  Hujaniambia wapi ungependa twende  tukale.” Nisawa tukaenda kuegesha  mitaa ya Osterbay kule baharini? Hakuna watu wengi, hasa mida hii na  siku kama ya leo ya kazi. Tutakula kwa  utulivu na wewe utakuwa salama bila  kashfa.Hilo akaliafiki na kutoa gari  hapo akiwa ametulia. Tunda naye  akatulia akiwa amekaa kiti cha  pembeni, kigauni nusu mapaja,  amekunja nne.  

Akamuona Tewele anatupia macho  mara kwa mara. Tunda akacheka.  “Huwa unaweza kuendesha na mkono  mmoja?” Tunda alishamuona anahali  mbaya. Hakutaka ajali nyingine.  “Kabisa. Kwa nini?” Nakuruhusu  unishike ili utulize akili barabarani. Tewele akababaika sana. Hapana. Nimetulia. Ila nilitaka kuhakikisha  umefunga mkanda vizuri.Tunda akamtizama kwa kumsuta, akacheka. “Samahani  bwana.  Naona  nimevutiwa. Sikutegemea kukutana  na..” Tunda akachukua mkono wake  mmoja taratibu, akauweka juu ya paja  lake. Hata hivyo suruali ilishakuwa imetuna tokea wanatoka Mlimani City.

Akaanza kumpapasa taratibu. Irene wewe ni mzuri. Laini!” Akasifia huku  akimshika na kumminya minya. Tunda akacheka na kunyamaza. “Ni hivyo upo na haraka. Tungeenda  kupumzika sehemu.” Leo ni siku ya  kazi Tewele. Tusichanganye mambo. Ni kweli.Akajirudi kwa haraka. Kwani weekend hii utakuwa na  majukumu yanayokufunga? Akamuuliza.  Nitakuwa safarini  kikazi. Nitarudi jumapili usiku. Ulitaka  nini?” “Tupane nafasi.” “Basi  nitafute week ijayo tupange vizuri.  Week hii ipo na mambo mengi kidogo.  Hata hivyo leo ni kwakuwa  nakuheshimu sana na nilikukosea  asubuhi. Nikalazimishia tuonane, ili  usije kuniona mimi muhuni tu. Lakini  nisingeweza kukuona week hii.” Hata  hivyo nimefurahi kukosea kwako. Wakacheka. Mkono pajani anashindwa  hata kusogeza.   

Tunda akahisi anatetemeka. Akaona  amtoe hofu arudi kwenye maswala ya  kawaida. Kila swali alilomuuliza,  alichukua muda  kujibu kama anayesikilizia  raha na hataki kusumbuliwa. Tunda akaona amuache andelee kufaidi hayo mapaja. Wakafika baharini akaegesha mbali  kabisa. Wakajikuta wao peke yao.  “Tuhamie kiti cha nyuma ili tule kwa  uhuru.” Tewele akakubali kwa haraka. Wakashuka na kuhamia kiti cha  nyuma. Huko ulipokaa mbali Irene.” Nilifikiri unataka kula kwanza? Naweza kula kwa mkono mmoja pia.Tunda akacheka.  Alimuona hata ongea yake imebadilika  yupo kama mjinga. Akamsogelea, akamfungua tu mkanda wa suruali.  Tewele akaanza kuhangaika pale  kitini.

Naomba utulie Tewele.” “Nakusaidia Irene.” Hapana. Tulia tu ufurahie msamaha wa usumbufu  niliokusababishia asubuhi.” “Sawa  mama.Tewele akaweka mikono  pembeni kumpisha. Kwa kuwa  alikuwa  tayari,  Tunda  hakumchelewesha. Hata dakika tano  hazikuisha, Tewele alishamaliza kila  kitu. Tunda akajivuta pembeni.  Akachukua chakula kwenye lunch  boksi moja, akaanza kula wakati  Tewele akijaribu kutulia pembeni. 

“Wewe ni mtaalamu Irene. Umewezaje ku..” Kula chakula, uwahi kazini.” “Nitakuona wapi tena?” “Nimekupa ruhusa yakunitafuta week ijayo. Umesahau?” “Umenichanganya mpaka nimesahau!Tunda akacheka  taratibu huku akila. Walikula hapo  kwenye gari mpaka wakamaliza. Kwa kuwa unaelekea posta, naomba lifti  mpaka karibu na ubalozi wa Ufaransa. Nakwenda Saluni.” Nitakusogeza na kulipia hizo garama za saluni.Tunda  akacheka na kushukuru. 

Mpaka anaachana na Tewele, akawa ametengeneza pesa kwa penzi la  harakaharaka tena garini tu. Na ahadi  yakutafutwa juma lijalo juu. Tunda akawa  anacheka yeye mwenyewe akiwa  anatembea taratibu kuvuka barabara  kuelekea sehemu ya Sauna na masaji.  Ilikuwa kesho yake ni kutengeneza nywele na  kucha. Anapumzika tayari kwa safari ya jumamosi, kwa Mbawala. Bila kutegemea, Tewele naye akawa ameingia kwenye hilo juma pia, ambapo alipanga awe naye juma lijalo. Akaongeza kipato cha juma hilo na uhakika wa kutengeneza zaidi juma lijalo watakapoonana tena.  Akacheka na kufurahia nafsini mwake.

 ~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Aliposhushwa tu, akangia sahemu  ambayo wanamfanyia masaji na kuna  sauna. Kinny akampigia tena. Kisha  akatuma  ujumbe.  ‘Huna  haja  yakuzungumza chochote Fina. Nisikilize tu, tafadhli.’ Tunda akasoma ule ujumbe. Akaamua  kujibu. ‘Nitakurafuta jumatatu inayokuja.’ Akamjibu tu hivyo. ‘Nashukuru Fina.  Nasubiria simu yako kwa hamu hiyo  jumatatu.’ Kinny akarudisha huo  ujumbe, lakini Tunda hakumjibu tena.  Angalau kukawa kimya. Akaendelea  na  maandalizi  ya  Dodoma.  Kutengeneza mwili. Na muonekano  wake. 

Ijumaa asubuhi Mbawala akatuma tena pesa bila ujumbe wala kupiga simu.  Tunda akajiuliza ndio anamkumbushia au!? “Mbona alishatuma pesa, au  kachanganyikiwa?” Tunda akajiuliza  ila akafurahia kile alichofanya, kutopiga au kutuma ujumbe. “Huyu anaakili na muelewa. Akiambiwa jambo anashika.” Hilo likamfurahisha Tunda. Nitatuma jumbe za mapenzi  kwa wangapi! Au nitapokea simu za  wangapi!  Ndio  mwanzo  wakufungulia mlango matatizo ya  ndoa za watu kama kwa baba Tom.  Sifanyi mchezo wa kitoto tena.” Tunda akajisemea akiwa anaangalia  pesa alizotumiwa na Mbawala. Hapo alishakata tiketi ya ndege iliyokuwa  ikiondoka kwenye viwanja vya  mwalimu Nyerere siku ya jumamosi,  asubuhi.  

Tunda & Mbawala Jr.

Jumamosi ikafika Tunda akiwa amejitayarisha vilivyo, ili kwenda  kukutana na Mbawala na kutumia hiyo siku ya jumamosi mpaka jumapili  pamoja. Aliondoka jijini Dar akiwa  amewahi tu uwanja wa ndege. Alikaa  kama lisaa ndipo ndege ilipoondoka.  Majira ya saa sita na nusu mchana,  Tunda alikuwa akitoka nje ya uwanja wa  ndege wa Dodoma akiwa na pochi  kubwa kidogo mkono wakulia na  ndogo mkono wa kushoto.  Alikuwa amevaa pensi ya kijani,  imefika katikati ya mapaja. Kiblauzi kilichombana juu kikawa kama  amekichomekea mbele. Kilikuwa na maua  machache yanayofanana na ile pensi.  Kilikuwa  kata  mikono.  Yaani hakina mikono kabisa. Ila kimezunguka maziwa tu. Rangi yake ya mwili nyeusi  ya mgongoni, laini na yakuwaka,  ilikuwa mpaka miguuni. Akavaa na  sendozi ndefu, akaweka ile ile cheni  yake nzito mguuni. Huo mguu mpaka  mapajani, kulikuwa kunawaka, kwa  kuangalia ni kama mtoto mchanga.  Kucha ndefu, zilizotengenezwa kwa  ustadi, zilikuwa na tips nyeupe. 

Mbawala naye akabaki ameduwaa. Tunda  akatabasamu  wakati  akimsogelea.  “Fina!” Habari  Mbawala!Tunda akasalimia akiwa  anaweka miwani yake ya jua kichwani,  kwenye nywele ndefu alizokuwa  ameshonea, za mawimbi madogo  madogo yakaanguka mpaka katikati ya  mgongo, ikafunika kidogo mabega  kwa pembeni. Akazirudisha zile nywele zote nyuma  na ile miwani  aliyoweka kichwani. Hereni kubwa za muundo wa alumasi, zikaonekana  masikioni na kuzidi kuvutia. 

“Oooh My!” Mbawala akajikuta  anaongea peke yake. Fina!” Akarudia tena. “Acha utundu bwana Mbawala.” “Nilitaka tukapitie sehemu  tule  kwanza, halafu..” Tunda akacheka. Twende. “Sidhani kama nitaweza kuendesha. Tunda akacheka sana. Twende mimi nikuendeshe. Halafu tuchukue chakula,  tukalie unapotaka wewe.” Chumbani  kwangu.  Hapana,  namaanisha  nyumbani kwangu.Tunda akacheka  na kutingisha kichwa. Acha  kuchanganyikiwa  bwana!  Twende. Tunda akatangulia,  Mbawala akamkimbilia na kumpokea  mikoba yote. “Unabeba mpaka pochi!  Ni nini lakini Mbawala!” Acha  nibebe mama. Angalau na mimi niguse chochote chako. Maana siku ile ulinipa busu la shavu, nikashindwa  hata kuosha uso.” Tunda alicheka  mpaka Akasimama. 

Unavyoonekana na haya maneno,  haviendani hata kidogo!” “Hali yangu  mbaya, kuliko haya maneno. Ni hivyo mimi mtoto wa kiume. Nimefundishwa  kujikaza.” “Na mama yako?” “Baba  huyo!Tunda akazidi kucheka huku  anatingisha kichwa.  Tunda ndiye aliyekuwa anaendesha.  Mbawala anamwangalia. Mapajani na  usoni. “Daah!” Ni nini?” “Hata nikisema hutanielewa mama. Acha tu  niumie ndani kwa ndani.” “Toa hayo macho huko ulipoyaweka, angalia barabarani ili tuweze kuzungumza.” Unafikiri sijajaribu!?Tunda akazidi  kucheka. Kila nikipeleka macho  mbele, shingo inavutwa. Niangalie hali yangu.”

Sasa mimi nina wazo. Ili  usiende kutia aibu huko mbele za watu, tuanzie kwako. Si ndiko ulikosema tunakwenda?” “Nakushukuru mama  yangu, kunizaa mtoto wa kiume mimi!Mbawala akaweka mikono  kichwani. Tunda alicheka mpaka  akaweka gari pembeni.  “Naomba twende Fina. Hali mbaya.  Naweza nikajiabisha hapa.” Ni nini  sasa?” “Nakwambia huwezi  kunielewa. Basi niruhusu hata kushika  tu. Ndio naona nitatulia mpaka  nyumbani. Sifiki mbali. Naweka tu  mkono hapo kwenye paja wakati  unaendesha.” Usinogewe  tu. Najua utanielewa mama.” “Hapana  Mbawala.  Mimi  sipakumbuki  nyumbani kwako. Lazima uniongoze  njia.” “Basi nitaweka nidhamu. Acha tu mkono utulie hapo kwenye paja, roho itulie.” Tunda akatingisha  kichwa, akawasha gari. 

Sasa si niweke?Akauliza tena  Mbawala. Tunda akamwangalia na  kurudisha macho barabarani, akatingisha  kichwa  kama  anayemsikitikia. Akaanza kukohoa kama  amepaliwa huku akikodolea macho hayo mapaja. “Mapaja yenyewe yanatia mpaka hofu  kushika! Unaangalia mikono nakujiuliza kama ni misafi au la!” “Acha fujo Mbawala.” “Sikutanii Fina. Masafiii, kwa macho tu  yanaonekana laini, halafu! Daah!  Acha tu nijikaze nishike.Akajifuta  mara kadhaa kwenye shati lake, kisha akaweka mkono kwenye paja la Tunda  taratibu na kwa tahadhari kubwa.  “Ooooh!” Tunda akamsikia  akigugumia. Akageuka kumwangalia, akamuona amefunga macho, mkono  pajani.

Taratibu akaanza kuminya kwa tahadhari kama anayeogopa.  Akaingia mpaka ndani ya geti la  Mbawala. Mlinzi akafungua baada  yakuona gari ya mwenye nyumba.  Tunda akapitisha gari mpaka pembeni  kabisa ya hiyo nyumba. Ukifikiri  Dodoma ni pakame, hutaamini ukifika  hapo kwa Mbawala. Kijani tupu. Na  nyumba yake ilikuwa na miti mifupi  mifupi iliyokatwa vizuri.  Tunda akasogeza gari mpaka kwenye  kona ya hiyo nyumba. Akamfanyia  kama alivyomfanyia Kinny. Palepale  ndani ya gari. Akalaza kiti chake baada  ya kujifungua yeye mkanda na  kumfungua na yeye, akaanza utundu  wake hapo hapo kwenye gari mpaka  akafanikiwa.

Tunda akajua amemaliza, ndio atatulia lakini wapi.  “Naomba tuingie ndani Fina. Siwezi  kutulia mpaka ni, ni..” Tunda  akacheka. Nahisi ni ile tamaa ya tokea  siku ya kwanza nimekuona. Hebu  niangalie. Bado kabisa. Nisaidie  mama, ndio tukale.” “Twende. Wakashuka kwa haraka Tunda akiwa  ameacha vitu vyake vyote ndani ya  gari.  Ile Mbawala amefungua mlango na  Tunda ameingia tu ndani, akamdaka.  Hapo hapo sebuleni wala hakufika  chumbani au kumvua nguo ya juu,  akamng’ang’ania kwa muda, kisha  akajitupa kwenye kochi. “Umeridhika  sasa?” Tunda akamuuliza taratibu.  Naona tu aibu. Lakini bado.  Ningepata..” Tunda akashangaa nguvu yakiume aliyonayo  Mbawala! Maana mchezo waliotoka kumaliza hapo haukua mdogo. Na bado alionekana kana kwamba ndio anaanza!

Alijua angechoka, lakini  akamtoa hapo na kumvutia chumbani.  Ilikuwa mara ya kwanza kwa Tunda  kukutana na mwanaume mwenye  stamina kwa kiasi hicho. Ni kama  alikuwa amepagawa. Alivyomshika na  jinsi alivyokuwa akifanya mitindo  yake tu, Tunda alihisi ameshikwa na  mwanaume kweli kweli. Wakati  wanahamia  chumbani,  alikuwa  ameshapata mabao mawili, lakini  alikuwa kama anaanza.  Walishindwa kutoka siku hiyo. Mpaka  anamwachia,  Tunda  mwenyewe  alikuwa hoi, akaishia kulala, hata  hamu ya chakula alikuwa hana.  Akajiambia amekutana na kiboko  yake. Alilala zaidi ya masaa manne  bila hata kujua alipo.

Akahisi mtu  anambusu kwenye kitomvu taratibu huku anachezea ile cheni yake kiunoni  kwa chini. Akafungua macho taratibu  na tabasamu. “Fina wewe ni mzuri  sana. Unavutia hata hapo kitandani!” Tunda akatoa kicheko cha usingizi.  Umenifurahisha,  mwepesi!” Na wewe upo na stamina. Unanguvu!Mbawala akacheka.  “Nilikuwa na hali mbaya. Ila sasa hivi angalau umenituliza akili. Nimeweza hata  kutoka na kwenda kununua chakula!Tunda akacheka huku akikaa.  Njaa imenikamata kweli!” Twende  tukale.Wakatoka hapo kitandani. Baada ya chakula, Mbawala ambaye hakuwa amepumzika kabisa, akataka  waanze tena. Tunda aliyekuwa angalau  amechukua mapumziko ya masaa  machache, akaendeleza kwa bidii zote  kutumika. Kuja kufika saa tano usiku,  ndio Mbawala akawa amefika mwisho. Hoi.

Baada ya muda mfupi tu, akaanza  kukoroma. Tunda akacheka.  Akavuta  simu  yake. Akakuta  imewekwa password ya finger print.  Akamtizama vile alivyolala kama mfu,  akamtingisha  kuhakikisha  kweli  amelala kabisa. Akajiridhisha kuwa  amelala kabisa. Akaanza kujaribu  kidole kimoja hadi kidole gumba cha mkono wa kulia ndicho kikaweza kufungu hiyo simu. Tunda alitamani kushangilia kwa sauti.  Ni Mbawala! Mtoto wa waziri wa  mambo ya nje. Na mfanyakazi wa ofisi  za Bunge, Dodoma. Tena yupo ngazi  ya juu! Mungu ampe nini Tunda!  Alichofanya, ni kucopy na kupaste  conctact list yoote ya Mbawala. 

“Hawezi akawa na mawasiliano ya watu wajinga wajinga.” Tunda akawaza  huku akiendelea kuiba namba za simu.  Kwanza alivyo jeuri na dharau  huyu, lazima kila mtu hapa, ananufaika naye. Tunda akaendelea  kuwaza huku akihamisha zile namba  huku akiomba Mungu, Mbawala asije  kuamka kabla hajamaliza. Alikutana  na majina ya mawaziri humo, wabunge, manaibu wao. Akawa  anacheka tu kama aliyekabidhiwa  ulimwengu mzima.  “Dad!” Tunda akatulia alipofika hapo  kwenye hiyo namba ya simu. Akabaki  ameduaa.

Akacheka baada ya wazo kupita na kulikubali. “Oooh my  Tunda! Nakula dad na mwana!” Akacheka huku akimtizama Mbawala  mdogo jinsi alivyolala pale. Lazima  nile pesa ya Mbawala mwenyewe pia.  Wasiniletee mchezo. Pesa yao haina  kazi hawa. Tunda akacheka peke yake. “Ngoja na yeye nikamuonje  kama ana nguvu kama za mwanae au  uzee tayari!”Akaanza kumfikiria baba  yake Mbawala. Akavuta taswira yake  akaanza kumfikiria. Nampataje? Ndio likawa swali kwa Tunda. Akaona  aendelee kuiba zile namba zote za  simu mpaka amalize, mengine  atakwenda kufikiria akiwa nyumbani  kwake. 

Mbawala alikuja kuamka asubuhi.  Tunda  alikuwa  amejilaza  akimwangalia. Akacheka. “Nakoroma  nini?”Akamuuliza Tunda. Kidogo  tu.Tunda akajibu huku akicheka.  Mbawala na yeye akacheka. “Daah!  Samahani. Nilicheza kwa puma jana,  nikalala hoi! Nisamehe  kama  nimekulaza macho.” Wala usijali. Nipo tu sawa.” “Acha basi kuniangalia hivyo Fina, unanifanya  nizidi kuona aibu.” Tunda akacheka  sana.

“Lakini kukoroma ni kitu cha kawaida  sana.Tunda akamfariji, lakini ni  kweli hakulala. Tunda hakuwa  akipenda kabisa mtu anayekoroma.  Kwanza hakuwa akiweza hata kupata usingizi. Akajifariji atalala akifika nyumbani  kwake. Akabaki pale akimtizama jinsi  anavyokoroma huku akihesabu dakika,  muda wake uuishe aondoke.  Walitumia hiyo siku hapo ndani,  mpaka mchana alipokuwa anarudi Dar.

“Naomba urudi Fina.” Tunda  akacheka. Naomba isiwe juma hili  linaloanza au lijalo. Nipo na mambo mengi sana. Ila kuanzia ile nyingine, naweza  hata kupata kijinafasi.” Mimi naweza  kuja Dar. Tukapata hata siku moja  kama hii. Au hata usiku mmoja tu. Lakini usiniweke nikisubiri kwa majuma matatu! Huko mbali Fina,  mama.” Tunda alijua ameshakolea.  Akamuweka mteja wa kwanza kwenye  orodha ya watakao muweka mjini.  Alishamkabidhi bahasha yake ya pesa  na yenye nyaraka za Kinny, akarudi jijini akiwa  amefunga juma vizuri na kipato cha kueleweka.

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Juma likaanza likiwa na ahadi ya kuingiziwa pesa na Kinny kwa kumfanikishia tenda na  Tewele aliyechanganywa na penzi la garini. Tewele na yeye alitaka kumuweka  karibu kama Mbawala. Ila Kinny hakutaka muendelezo naye kabisa. Alipanga amalizane naye kwa  kumpa ile bahasha aliyopewa na  Mbawala, waachane baada ya kumlipa  pesa yake, iwe basi. Kwa uchovu wa  kutolala usiku wa jumamosi kuamkia  jumapili huku Mbawala akiwa anampa  mchezo wa nguvu, Tunda alikuwa hoi.  Palipambazuka, akakaanga mayai  mawili na glasi ya maziwa. Akala  kisha akarudi kulala.  Alilala mpaka saa kumi jioni.

Ujumbe  kutoka kwa Kinny ukamtoa usingizini. Akachukia kutozima simu. Akasoma.  ‘Leo jumatatu Fina. Nakukumbushia tu.’ Akaka na kuangalia muda.  Akajibu. ‘Nitakupigia baada ya kama dakika 20 hivi kuanzia sasa. Nina majibu ya kazi  yako.’ Akajibu hivyo na kwenda kuoga.  Akatoka akiwa amechangamka.  Akakuta Kinny amerudisha ujumbe.  Alijua siku moja aliyokuwa naye pale  hotelini, amechanganyikiwa, anataka  tena. Lakini alishamkera Tunda.  Akaamua kumpigia. “Ulisoma  ujumbe wangu wa mwisho?” Tunda  akaanza kwa hilo swali. Fina! Tafadhali  nielewe. Nia yakukutafuta muda wote sio  kazi. Ni kuwekana sawa mimi na wewe. Natafuta amani.” “Amani mbona ipo! Usiwe  na wasiwasi. Mimi sina mambo ya ajabu. Namsoma mtu na kumuelewa kwa haraka sana. Kuanzia hapa  tutaendelea vizuri tu. Hapatakuwa na migongano tena.” Tunda akazidi  kumuumiza. Daah! Nahisi mimi utakuwa  umenisoma vibaya. Mimi sio mnyanyasaji. Tunda akanyamaza.

“Fina?”Hamna shida Kinny. Nimekamilisha  kazi yako. Naomba tukutane, nikukabidhi.” Unamaanisha ile kazi ya Dodoma!? Ndiyo. Kinny akawa kama hajaelewa.  Alitegemea kutafutwa yeye binafsi na  Mbawala. Unamaanisha ile tenda ya  bunge!?” “Labda tukionana, utaelewa zaidi. Nina nafasi jioni hii. Kati ya saa 11:30 mpaka 6:30.  Tunaweza kukutana pale pale Mlimani City.  Nitakuwa nikikusubiria ndani kwenye  mgahawa wa..” Tunda akamuelekeza,  wakaagana kuwa wakutane saa 6 kamili  jioni hiyo. Kinny alijua Tunda ameshamtoa  umaana. Hapakuwa na kicheko tena  wala kukutana usiku au kwenye gari  yake. Mazungumzo ni nje hadharani.  Hakuna faragha tena.   

 Kwa Kinny!

I

lipokaribia muda wa kukutana,  Tunda akaita Uber, mtu akaja  Ikumchukua  na  kumpeleka mapaka Mlimani City. Alikusudia kumuumiza Kinny. Alitaka humuonyesha hata  kama alimuona akiwa uchi, akapata  penzi, bado uthamani upo na atakosa  mengi. Safari hii alivaa gauni refu  mpaka chini. Lilikuwa kama la mpira  tu. Lilimshika kila mahali. Kola yake  ilikuwa imemwagika ikatengeneza duara kwa nyuma na  cheni ikapita kutoka bega moja  kwenda jingine kushikilia ile pindo ya  kola. Ilikuwa ya rangi ya kijani kibichi  ikachanganywa na pink. Alivaa hereni  bila cheni. Kiatu cha juu cha pink  kama moja ya duara lililopo pembeni  ya hips moja. Ile nywele ya mawimbi,    akaibana pembeni na kuacha chache  zimeanguka kwenye kipanda uso.

Ni  kweli Tunda alipendeza. Ungeweza  sema ni mwana mitindo wa Holywood.  Kwa kuwa alikuwa na vidole virefu,  alipanga pete mbili mbili kwenye  vidole viwili vya kila mkono. Na  kucha alizokuwa nazo, ungependa.  Alishika pochi nzuri inayoendana na  kiatu chake, akashika na file lililokuwa  na nyaraka za Kinny. Ungesema  msemaji wa ofisi ya raisi.  Alitembea taratibu bila haraka mpaka  kwenye ule mgahawa. Akamkuta  Kinny akimsubiria nje. Akabaki  ameduaa. “Habari yako Kinny?” Tunda akaanza kwa sauti tulivu.  Lakini yakikazi. Umependeza sana  Tunda.” “Asante. Tunaweza kuingia  ndani? Nataka kuagiza chakula. Njaa  inauma.” Bila  kusubiria  jibu, akatangulia ndani, Kinny akabaki  amekodolea mgongo. Kiuno, sehemu  ya juu ilipoachwa wazi na nywele  kuwekwa pembeni kama aliyekusudia  kuonyesha ule mgongo, chini ya hicho  kiuno jinsi kulivyobanwa vizuri na  umbile la chini lilivyopendeza kwenye  hilo gauni, Kinny akabaki ameduaa  pale mlangoni.

 Baada  yakukaa,  Kinny  naye  akamfuata. Muhudumu akaja, Tunda  akaagiza juisi ya embe na chakula.  Kinny akaomba na yeye juisi ya embe tu.  “Hili faili ni lako Kinny. Kila kitu  kimekamilika. Na zipo namba za simu  za msaidizi wa Mbawala. Amesema  kama utakuwa na swali lolote, umpigie  yeye huyo msaidizi wake ili kuwekana  sawa. Ila kila kitu kipo hapo. Nashauri  pata muda wa kupitia taratibu.” Kinny alibaki  amekodoa  macho.  Hakutegemea kusikia hivyo. Mbawala  anamtuma Fina/Tunda kwake? Tena  na kumuelekeza kwa msaidizi wake!  Kiroho kikamuuma kidogo Kinny.  “Wamekutana wapi mpaka kumpa  yote haya? Kwa nini asinitafute mimi  mwenyewe?” Kinny akawaza huku  akiumia.

Tunda akamsogezea tena karibu lile kabrasha.  Akashtuka kidogo. Daah! Siamini  bwana. Kama utani umekamilisha hii  dili!” “Hongera. Nimeipitia na mimi,  inaonekana ni kweli ni kazi kubwa umeipata. Mambo yako yatakuwa safi.” Akaongeza Tunda taratibu, asijue maumivu ya Kinny. Nilijua baada ya pale, angenitumia mimi mwenyewe au hata kunitumia haya yote kwenye  email yangu!Akajikuta anaropoka  kile kilichojaza moyo wake kwa  kulalamika. Tunda hakujibu kitu. Akanyamaza kimya. “Lakini hata hivi  ni sawa tu, nakushukuru sana.” Akajirudi kwa haraka. Juisi ikawa  imeletwa, Tunda akachukua yake na  kuanza  kuinywa  taratibu  tu.  Ungependa vile Tunda alivyoshika hiyo glasi na hivyo vidole.  Akamuona anavuta pumzi kwa nguvu,  akamwangalia.

“Na kuhusu sisi?” Tunda  akakunja  uso  taratibu. Namaanisha mahusiano yetu.  “Nafikiri nilikueleza tukiwa Dodoma, Kinny. Au unamaanisha nini? Lakini nimeomba msamaha Fina.” “Mbona nimekwambia hakuna neno  kabisa! Naomba uwe na amani Kinny.  Tushukuru Mungu kazi uliyoniamini  nayo nimeikamilisha. Furahia wewe na mkeo.Kinny akazidi kuishiwa  nguvu.

“Basi naomba nikurudishie ile pesa uliyonirudishia tulipokuwa hotelini  Dodoma.” Tunda akakunja uso. Kwa  nini!? Nahesabu  ni  kama  umeniziria.” “Hata kidogo. Basi labda  kukupa amani, hesabu hivi, mahusiano  yetu ni ya kikazi. Uliniazima nauli  kwenda Dodoma kufanya kazi.  Nilifanya kazi yangu, umeshanilipa  kwa mara ya kwanza, unanimalizia kwa kukubali kuwa garama za kazi  yote ilikuwa juu yangu isipokuwa  malazi ya siku moja. Wewe bosi wangu  au  kampuni  ya  Kinny  ndio  imegaramia. Basi. Rahisi kama hivyo.  Tunaachana kwa amani. Ukiwa na  kazi nyingine unayotaka nikufanyie,  nitafute. Rahisi hivyo na kuweka  tofauti zetu kando.” Sasa hizo tofauti  ndizo nataka tuzimalize.Kinny  akaendelea.

“Tafadhali nisamehe Fina. Umekuwa  mtu  mwema  sana  kwangu.  Umenifanyia jambo kubwa sana, ni  vile hufahamu tu. Hiyo tenda itabadili  maisha yangu na familia yangu. Kama  ulivyoona mwenyewe, inalipa pesa  nzuri tu. Nitapata nafasi ya kuwa na  watoto wangu hapa nchini. Yote ni  wewe  umesaidia.  Mbawala  alishanikatalia, akawa ananikwepa. Nisingependa unifanikishie hivi, halafu nikageuka kukuumiza. Yani unaleta  mafanikio kwa garama ya kuumia!  Hapana Fina. Naomba nisamehe.  Tafadhali. Ulinipa wakati mzuri sana ambao nilihitaji kwa muda mrefu.  Nilikufurahia na nimependa utulivu wako na natamani tuendelee kuwa pamoja.” Tunda akacheka kidogo na  kuinama kama anayefikiria.

“Naomba niwe mkweli kwako Kinny.” Karibu.Kinny akajiweka sawa.  “Wewe ni mume wa mtu na baba wa  watoto wawili. Hakuna namna  yakuweka tofauti zako na zangu sawa.  Hatuwezi kufikia sehemu tukawa ukurasa mmoja kwa kuwa wewe ni  mpitaji tu kwenye maisha yangu. Na  nasikitika kwenye huo upande mwingine ilitokea nikaumia. Nahisi sio  wewe uliyeniumiza moja kwa moja ila  umenikumbusha tu mambo ya nyuma.  Na kwa kuwa muungwana ili tuachane  salama, naweza kusema hukukusudia.  Nina vidonda vyangu ambavyo  havijapona, na wewe ukatokea  ukakanyaga  huko huko  vilipo,  umenitonesha.” Daah! Kinny  akasikika akisikitika.

“Kufupisha tu stori ndefu na tumalizane hapa ili kila mtu aendelee  na shuguli zake, naomba rejea  mazungumzo  yetu  au  kile  nilichokwambia Dodoma. Tubakie  kwenye maswala ya kikazi tu. Ukiona  ipo  kazi  unataka  nikufanyie,  tukafikiana bei.” Hapo Tunda  akacheka kidogo, kuweka msisitizo na kumkumbusha anamdai. Tafadhali usisite kunitafuta. Lakini si haya  mahusiano ya mapenzi ya wizi. Mkeo  anakuja, naamini utakuwa sawa tu.” Chakula kikaja, Tunda akainamia  sahani yake.  Kwa kumtizama tu, alikuwa ameumia  mpaka usoni. Ujanja wote ulimwisha  Kinny mtoto wa jiji. Kukataliwa  kubaya! Haswa na mrembo kama  Tunda ambaye alishamuonjesha penzi ambalo alitaka kuliendeleza kwa wizi. 

“Huyu ni Mbawala tu.” Kinny  aliwaza akiwa mbele ya Tunda  aliyekuwa anakula chakula kwa  madaha. Na watakuwa wamekwenda  kuonana tena Dodoma. Jamaa  amenipora  mwanamke  wangu.” Akachukia Kinny. Chakula cha hapa  ni kizuri sana! Umeshawahi kula hapa? Tunda akavunja ukimya. Mara moja  nafikiri. Wanampishi mzuri.Kinny  akajibu, Tunda akaendelea kula.  Vipande vidogo mdomoni, kutafuna  taratibu kama hataki.  Nimeumia sana Fina.” Tunda  akanyanyua uso kumtizama, hakujibu  kitu. Naomba leo nikulipe kwa hundi.  Sikuja na pesa yeyote, kwa kuwa  sikutegemea kama Mbawala atakutafuta wewe na mkamalizana  naye. Nilikuwa nikisubiria mawasiliano yake kwa barua pepe. Nilipanga kuwa nikishapokea ndipo  nikutafute, nikulipe.” Hamna neno. Akajibu hivyo tu, Tunda akarudi  kuinamia sahani yake. Alijua fika  Kinny ameumia kwa Mbawala kutomtafuta yeye na kumsukumia kwa  msaidizi wake. Ni kama amemdharau.  Tunda akaendelea kula. 

Kinny akatoa hundi. Akaandika kiasi cha pesa kwa malipo na kuweka  saini. Jina akaacha wazi, kitu  kilichomfurahisha Tunda. “Nashukuru  sana Fina. Naamini hiki kiasi ni  sawa.” Bila  kuangalia, Tunda akashukuru. Kinny akamtizama kwa  muda na kuondoka. Ndipo Tunda akavuta ile hundi, akasoma na  kucheka. “Bingooo!” Akajipongeza  moyoni akaendelea kula. Tunda  akajiangalia  vile  alivyopendeza,    amelala mchana! “Siwezi kurudi  nyumbani. Heri hata nikangalie  movie.” Akaendelea kula taratibu huku  akifikiria.

 Tewele!

A

lipokuwa akila simu kutoka kwa Tewele ikaingia. Tunda akacheka.  Upo?Tunda akaanza. Tokea uniache siku ile, nimekaa nakufikiria tu. Tunda  akacheka taratibu. “Unanifikiria kwa  mema au mabaya?” Natamani unishike tena Irene. Na hivi unatumia muda mfupi, nisaidie mama. Angalau unitulize. Sitakuweka sana. Mmmh! Tunda akajidai kufikiria.  Lakini alimpenda Tewele. Alikuwa  anatimiza haja zake haraka sana, sio  kama Mbawala.  “Tafadhali Irene. Angalau akili itulie.” Uko  wapi na ulitaka tukutane wapi?” “Popote  unapotaka wewe. Nitakulipia pesa ya usafiri.  "Basi tukutane pale pale kwa siku ile. Ila leo  ujiandae.”Akamsikia anacheka.

Nitakaa  na wewe mpaka uridhike.” “Asante mama. Basi utanikuta hapo. Si unasogea sasa hivi? Akauliza Tewele. Unajua mimi  sipendi kuwekwa. Kwa hiyo uniambie tunakutana baada ya muda gani?” Mimi ndio natoka hapa ofisini. “Basi na mimi natafuta usafiri,  nakuja. Lakini nafikiri ili wasijue  tunapokwenda, nichukue nje ya Kanisa la St.Peters. Nitamwambia anishushe pale. Wakakubaliana upande  atakaokuwepo. Wakaagana. Tunda  akafurahi kupendeza kwake sio bure. Akatoka hapo akiwa ameshiba, swafi, tayari kwa kazi.

Alipofika  pale  walipokubaliana,  akamkuta ameegesha gari anamsubiria.  Tunda akacheka. “Kiu gani hii!” Akajiuliza wakati anatembea taratibu  akimfuata. Akampigia simu. Toka sasa kwenye gari unipokee.” Tewele akacheka. Nia ili amuone jinsi alivyopendeza.  Akamuona kwa mbali anashuka.  Tunda akakata simu huku akimfuata.  Akamsogelea. Umependeza. Geuka. Akamtaka ageuke.  Mmmh! Akamsikia akiguna wakati anageuka  taratibu mbele yake. Tunda akacheka.  “Leo Irene nipe kila kitu, sio  nusunusu.” Ni wewe tu na muda  wako. Usiku huu wote nakupa wewe. Akastuka.  Sasa kama ni hivyo, kwa nini  tusitafute sehemu?” “Sawa.Tunda  akakubali bila kumzungusha.

“Basi tuongozane mpaka pale  Moroco. Mimi nitachukua taksii  mpaka  kwenye  hoteli.” Tunda  akamuelekeza sehemu ilipo hiyo hoteli  ambayo alijua ipo salama kwao, kisha  akaendelea. Nitachukua chumba,  halafu nitakwambia ni wapi nilipo, uje moja kwa moja, usipite mapokezi  ukaonekana  na  watu  wanaokufahamu.” Hapo utakuwa  umenisaidia mama.Wakaingia ndani  ya gari.

 ~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

     Wakati wanaingia tu, simu ya Tewele ikaita akapokea kwa haraka. Mihayo! Akaita Tewele. Ile kutaja tu lile jina,  moyo wa Tunda ulipasuka. Mihayo ni  jina linalo fanana kama jina la mume  wake shangazi yake. Aliyempiga kama  mwizi na kumpasua hovyo mwili wake  na kuvunja mifupa yake. Tunda  akabaki anatetemeka kwa hasira pale  kwenye kiti. Tewele akasikika  akiongea kwa heshima sana, akipokea  maagizo. Akakata.   

“Samahani bwana. Ilibidi tu kupokea.  Huyu ni Mkurugenzi wetu. Msumbufu  sana. Tunamwita mkoloni. Jeuri na  majivuno kweli. Anataka anachoengea  yeye ndio kiwe hivyo hivyo.  Hashauriki.” Pole. Anaitwa nani? Mihayo. Jamaa amesoma. Na..” Kadiri alivyokuwa akimuelezea,  Tunda akajua lazima ni yeye tu. Akili  ilishavurugika. Chuki ikaibuka kali  sana. Akakumbuka vile alivyomuharibu sura yake. Tewele aliendelea kuongea akimlalamikia kwa hili na lile, Tunda  kimya. 

Wakafanya kama walivyokubaliana.  Tunda akapata chumba kilichojificha,  ndipo akampigia simu Tewele afike  hapo. Alikuwa amemuacha kituo cha  Moroco. Baada ya muda akafika hapo.  Akaingia mpaka hapo chumbani.   

“Acha nitumie choo kwanza.” Huwezi kwenda na suruali bwana. Njoo nikuvue.Tewele akacheka huku  akimsogelea, asijue nia ya Tunda.  Aliona simu ipo mfuko wa nyuma wa  suruali yake. Akamtoa ile suruali na  chipu, kwa madaha yote huku  akimpapasa,  Tewele  akifurahia  kushikwa na binti huyo mdogo,  mrembo wa kuvutia.  “Uwahi  huko  chooni,  maana ushanichanganya!” Tewele akakimbilia  chooni huku anacheka. Bila kupoteza muda,  akaingia kwenye simu ya Teweele kwa  haraka sana. Moja kwa moja kwenye  namba ya mwisho iliyoingia. ‘Mihayo.’ Ilikuwa imeandikwa hivyo. Ewaah! Akafurahi kuipata ile namba kwa  haraka. Kwa kuokoa muda asije  akakamatwa, akajitumia ile namba kwa ujumbe, kwa kutumia simu ileile ya Tewele, kisha akafuta ule ujumbe aliojitumia namba. Ile anamaliza tu,  Tewele naye anatoka chooni. Tunda  akaruka  kwa  haraka  kama  anayekwenda kumuwahi kumpokea  kwa mahaba, kumbe ni mshtuko wa kukamatwa, na  simu akarusha  pembeni. Uzuri aliitupia palepale  kwenye kochi. Tewele hakuwa  ameelewa alijua mambo ya mahaba. 

Kwa kupaniki, Tunda alimfanyia  mengi ambayo hata hakukusudia.  Tewele alikuwa akigugumia na  kufurahia kila kitu.  Tunda alimzungusha hapo chumbani,  uzuri Tewele mwenyewe hakuwa  akiweza mengi. Mwili mkubwa, umri  ulishaenda, basi, hata kabla ya lisaa  kuisha akawa hoi. Amemaliza.  “Utaniua Irene.” Tunda akacheka.  “Tatizo ni lako. Mtamu, halafu  unanukia vizuri.” Pafyume ya paris  hiyo.” “Ukienda uniletee na mimi.” Au twende wote?Tunda akaa kwa  haraka.

Ufaransa?” “Sasa je! Fikiria  kupata usiku kama huu kwa uhuru.  Mbali  na  macho  ya  watu  wanaotuwinda! Tunakula vitu vyetu  kwa nafasi bila haraka, tena kwa kituo! Tunda akacheka, asiamini. “Wewe  andaa safari twende nikakubembeleze  huko.” Tewele akacheka.  Sio sasa siku ifike, unipe sababu? “Ni lini?” “Aaah! Tatizo ni Mihayo. Anabana kweli! Hali haikuwa hivi.  Sasa hivi anaogopa kutoa safari.  Anasema viongozi wote macho yapo  bandari. Basi hakuna safari. Ila ipo  moja hiyo, nafikiri ataiidhinisha tu.  Ngoja tuendelee kumlamba.” Tunda akazidi kumchukia mume wa shangazi  yake. 

Akafikiria kwa haraka. “Sasa na wewe  lazima ujue kula na vipofu.” Sio  yule.Akabisha Tewele. Hakuna mtu asiyenunulika. Kila mtu anao udhaifu  wake Tewele. Unatakiwa kuufahamu wake ndio uutumie.” “Mmmh! Akaguna kama anayemfikiria Mihayo.  Nakwambia ukweli.” “Sio yule  jamaa. Nakwambia ni mkoloni.” “Aliyekwambia wakoloni  hawanunuliki ni nani?” “Kwa njia  gani?Akauliza Tewele.  Kwanza lazima ujue ni nini  anapenda. Anakunywa wapi na rafiki  zake! Siku gani? Wewe unaweza kuingiaje kwenye kundi lao la  marafiki! Kisha na wewe unajiwekea  muda wa kwenda hapo kunywa na  unahakikisha wanakuona kama na wewe upo hapo kwenye maeneo yao.  Usijikaribishe kwenye meza yao kwa  haraka au pupa mpaka wao wenyewe wa kukaribishe, huku ukichunguza  aina  gani  ya  mazungumzo  wanazungumza. Kama ni michezo,  michezo gani! Mpira wa miguu, tenesi,  golf, ni nini! Wasomi na matajiri huwa  wanaunganishwa na vitu fulani ndio  maana  wanaweza  kuchukuliana.  Hawazungumzi kila kitu. Sasa kazi  yako kubwa ni kujua ni nini anapenda  na kinamfurahisha.” Tunda akaendelea.

Basi na wewe unapata nafasi ya kuwasoma taratibu. Jipitishe.  Hakikisha wanakutambua kuwa na wewe upo pale kwenye viwanja vya hadhi yao, wasalimie na kuwapa  ofa tu. Usikae. Kumuonyesha upo, na  mazingira anayofika yeye na wewe  upo. Na sio wakati wote unamlilia shida. Muonyeshe unao uwezo. Heshima unayompa kazini sio kwa  sababu ya dhiki, ni nidhamu ya kazi tu.  Watu kama hao wana kiburi.  Akishakuona hivyo na wala hukimbilii  kwenye meza yao kutaka kukaa nao  kama limbukeni, na upo sawa nao  kwenye maisha, taratibu utajikuta  unakaribishwa kwenye meza zao.” Tunda akaendelea. 

Na ukishakaribishwa mara moja  kwenye meza yao, sio sasa unazidisha  pombe na kuongea kila kitu au mambo  wanayopinga wao, au kumzungumzia  kiongozi fulani  ambaye wao hawampendi mpaka  uwakere! Hapana. Hapo tena ndio unakuwa  mstaarabu na kumuonyesha unafahamu mambo wanayoyapenda  kama wao.” Kama wanapenda kitu  ambacho mimi sina hata ufahamu nacho?” Tewele akauliza.  We Tewele!?Tunda akavuta shuka  akakaa huku amejifunika na mshangao  usoni. Karine hii unauliza unajuaje  mambo! Kila kitu kipo mtandaoni.  Ndio maana nilikwambia chunguza  wanachopenda. Ukishakijua na wewe  kifanyie kazi. Hakikisha kama ni  mchezo unajua wachezaji wa mpaka  wa kimataifa. Mjini hapa, unakula na  watu kwa akili. Na ninakuhakikishia  Tewele, ukiweza kuwepo kwenye meza  yao, ukaongea mambo ya maana. Sio  kujiliza shida. Ukafanikiwa kuongeza  uthamani wako nje ya mambo ya kazi,  tena kirafiki, hata ofisini atakuangalia  kwa jicho la karibu.” Tewele  akaonekana kufurahia hilo wazo, asijue Tunda anaongea kwa jinsi  anavyomfahamu huyo mjomba wake. 

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Alishaishi naye, anamjua yeye na  wanaomzunguka. Ile haiba yao ya  kiburi na dharau kwa wengine wanao  waona hawajafikia daraja lao.  Aliwaona wakiwa wanakuja nyumbani  kwake. Aina ya watu anaoweza  kuwakaribisha au hata kuzungumza  nao. Wote walikuwa wasomi sana.  Watu  wa  viwango  vya  juu.  Walioelimika na wenye nyadhifa za  juu. Tunda hakuwahi kuona mtu wa  hali ya kawaida, wala si chini, wa  kawaida tu, kufika pale kwa shangazi  yao. Kila aliyekaribishwa pale,  alikuwa na sifa fulani tena za juu. Na  ndivyo ilivyokuwa hata kwa binti zao.  Hawakuwa na marafiki wengi. Na  mara nyingi aliwasikia wakilalamikia  watu kuwa wanaongea vitu vya ajabu.  Mazungumzo ya kijinga.   

~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Ule ushauri ukamwingia Tewele, na  yeye akakaa “Hiyo akili.” Jua sasa  anapokunywa na wenzake.” “Tena nasikia wenzake watu wa totozi  kweli.” “Na yeye?” Tunda akauliza akitaka kujua ya sirini. “Yeye simba  mwenda pole. Nasikia yupo makini  sana. Alishakuwa na mahusiano na mfanyakazi mmoja hivi, pale pale  bandari. Walikuwa wasiri sana. Yaani  mtu wa karibu wa yule dada ndio  alikuja kutuambia, tena baadaye  baada ya yule dada kuacha kazi pale.  Lakini kwa kuwa watu wanamuogopa,  ikaishia chini chini. Hakuna aliyejua kilichoendelea baada ya yule dada kuondoka pale. Na aliondoka bila hata  kuaga au kusema ni kwa nini anaacha  kazi, wakati alikuwa msichana mdogo  tu, halafu mzuri kweli! Tukashangaa anawezaje kuacha kazi bandari!  Lakini hakuna aliyeuliza, sababu ya  hofu. Hata huyo dada aliyesema  alikujaga kukanusha. Nafikiri kwa  hofu pia. Lakini nasikia ni kweli.” Tunda akafurahi sana kupata hizo  habari. 

Si umeona? Hakuna asiye na  udhaifu?” “Kweli bwana.Akakubali  Tewele. Wapi anapokunywa na  wenzake?” “Nasikia Lidazi.” “Basi. Kumbe umeshajua. Na kinywaji gani anapendelea?” “Hapo ndio sijui. Yeye Tunda alijua. Lakini mwiko  kuropoka. Hilo sio tatizo. Jipitishe  pitishe. Jenga mahusiano ya zaidi. Na  weka deni ambalo hatasahau kulipa  fadhila. Au hata fanya nyama choma  na wewe Tewele!” Wapi sasa? Tewele akauliza. Si nyumbani kwako!  Tafuta tu weekend moja, mkaribishe yeye na mkewe na mtu mwingine  muhimu. Sio walevi unaojua sio  wastaarabu. Mkaribishe mapema  kama hata week mbili kabla ya siku  unayotaka wafike kwako. Mtajie mtu  mkubwa wa sehemu fulani ambaye  naye atakuwepo. Ataona umuhimu wa  kuja. Halafu kwa mwanzoni, muwe tu  wachache. Andaa mazingira mazuri na  ya heshima. Na yeye atapata deni la  kuja kukukaribisha siku moja. Na  kazini sio tena kila ukimuona au  ukiingia ofisini kwake unamkumbushia  safari za kikazi!” Tewele akacheka. 

Kweli tena. Jipitishe au hata  ukimkuta sehemu rusha tu neno. Mpe  matokeo ya mpira ya siku iliyopita.  Kama anapenda mpira lakini.” Tunda  alimjua mjomba wake mlevi wa mpira  wa mguu. Alijua anachomshauri. “Na hapo sasa sio tena na wewe uanze  kujisahau na kujigeuza kama ndio  wewe mtangazaji wa hiyo mechi wakati mpo kazini! Unaongea kuanzia kona walizopiga, makosa waliyofanya uwanjani, yooote wakati ni  muda wa kazi! Hapana bwana.” Tewele akacheka sana. 

Kidogo tu, unapita kama ndio  salamu. Acha kujitetemesha hovyo.  Ndio maana anakuweka kwenye kundi  la wajinga wajinga. Na taratibu.  Jiwekee kuwa ni malengo ya muda  mrefu. Sio kila kitu kwa mara moja.  Atakushtukia. Usipompata yeye kwa  haraka, basi rafiki zake.” Tewele  akafurahia  sana  hilo  wazo.  Akaonekana kuchangamka kweli  kweli. Tunda akawa anacheka.

Tewele aliondoka, akamuacha Tunda  hapo chumbani na pesa nzuri tu japo  sio nyingi sana. Lakini Tunda  akajiambia hata hivyo hakutumia  nguvu nyingi, inatosha. Aliwahi  kuondoka,  akasema  anawahi nyumbani.  Tunda akabaki akimfikiria mjomba  wake akiwa amejilaza palepale  chumbani. “Mihayo!” Akawaza.  Hakika atalipa. Nitamlipa kisasi,  yeye na familia yake watajuta. Tunda akaendelea kuwaza wakati  akiingalia ile namba yake ya simu.  Hakika na mkewe atajuta kila  unyama alionitendea. Nitahakikisha  na yeye anaumia.” Roho ya chuki  ikamwingia Tunda.   

Akakumbuka mahusiano ya wizi Tewele aliyoambiwa  alikuwa nayo huko kazini. “Kumbe na yeye  yumo!” Akacheka  vile  alivyo  nyumbani, akijionyesha baba mwenye  maadili, “kumbe hovyoo!” Tunda  akafyoza kabisa akiwa amemdharau kutoka moyoni na kudhamiria kuwalipa vibaya sana.

  ~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~~

Nini Tunda atafanya kwa familia ya Shangazi yake? Mikasa ipi inamsubiria mbeleni? Ameshapata namba ya waziri Mbawala mwenyewe. Je, atamtafuta baba mtu baada ya kula kichwa ya mtoto? Usikose muendelezo.

CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment