Naomi Simulizi |+1 205 767 8163 |naomisimulizi@gmail.com Mapenzi & Pesa! - PART 2 - SEHEMU YA 42. - Naomi Simulizi

Mapenzi & Pesa! - PART 2 - SEHEMU YA 42.

Jelini akaishiwa nguvu baada ya kusikia ni Love. Ila akawa muungwana akijua hana chakubadili. Kwanza anataarifiwa. “Asante kwa taarifa. Na poleni sana. Mungu atasaidia atapona.” Colins akajua ameharibu. “Nimesikika kama nimetoa tu taarifa, si ndivyo?” Jelini akanyamaza. “Samahani Jelini.” “Huna haja yakuomba msamaha. Ni sawa tu.” “Lazima. Ila ujue natamani kama ningekuwa na wewe usiku huu. Ila...” Akakwama. “Mimi naelewa Colins. Familia kwanza.” Colins akazidi kuumia akiona Jelini ameona anatoa kipaumbele kwa Love akimuona yeye muhimu kuliko yeye. “Usiku mwema Colins. Tafadhali unijulishe hali ya mgonjwa. Wape na wazazi pole.” “Asante.” Jelini akakata simu na kumuacha Colins amekufa ganzi, akili imegoma kufikiria.

Jelini aliyepokea simu, si aliyemuaga. Alimpokea kwa furaha kubwa sana akisikika kufurahia kutoka kwao. Akajihisi ni kama amempiga kibao kingine cha usoni. Lakini hakuwa na jinsi.  Hali aliyokuwa nayo hapo, ilikuwa mbaya kuliko Love aliyelazwa hospitalini, amelala kwa madawa ya maumivu, hana habari.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Alibaki ameshikilia simu mpaka aliposhitushwa na honi, kuashiria wazazi wapo tayari anatakiwa atoke kwake. Aliingia kwenye gari, akakaa kiti cha nyuma, kimya kama aliyepigwa shoti ya umeme. Mwili umepoa, akili imegoma kufanya kazi. Yeye mwenyewe yupo kwenye mshituko, haamini kama hiyo safari ni ya kwenda kumuona Love na si Jelini.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Huku kwa Jelini yeye hata hakutoka tena chumbani. Alichokifanya ni kubadili nguo, na kuosha uso kutoa vipodozi. Akanywa dawa za usingizi kabisa ili kuepuka kufikiria, akapanda kitandani, kimya akisubiria usingizi.

Mama Jema akahisi ukimya. Ile hekaheka ya kujiandaa na shamrashamra ya safari imeisha! Akajua pengine alishaondoka. “Lakini hawezi kuondoka bila ya kuniaga!” Akaanza kuita kwa sauti ya chini kidogo kwani Jeremy alishakwenda kulala, kesho yake shule. Kimya. Kutoka kuangalia chumbani kwake, taa zimezimwa. Akaamua kwenda kuhakikisha, akakuta amelala. Hakuamini.

“Jelini!” “Dawa za usingizi zinaanza kunichukua mama. Lakini kesho usije niacha hapa ndani. Niamshe twende wote, nikaanze kazi.” “Sijaelewa! Kwani hamtoki tena?” “Kisicho riziki mama yangu, hakiliki! Mpenzi wa Colins amelazwa, ameanza kuugua leo gafla, akakimbizwa hospitalini, amekutwa apendex imepasuka, amefanyiwa upasuaji, ndio nafikiri habari alizokutana nazo aliporudi kwao. Ndio amekwenda kumuona.” Mama Jema akawa hajaelewa.

“Kwamba huyu Colins kumbe jaa yote ile humu ndani, anaye bado yule mwanamke wake!?” “Ya ulimwengu mengi mama yangu. Naona kweli nifuate ushauri wako. Nitulie, nishike moja la kazi, linaloeleweka. Nitayumba yumba nikipoteza muda, na umri nao unakwenda. Kesho tutoke wote.” “Sawa. Pole mama yangu. Pole sana. Mungu atakujalia na wewe.” “Nashukuru mama. Usiku mwema.” Mama Jema akatoka akiwa ameumia haswa. Akaumia zaidi ya Jelini mwenyewe ila hakuwa na jinsi.

Huko Hospitalini.

Walifika Colins akiwa ametulia haswa. Hakuzungumza neno hata moja. Mzee akaongoza njia kibabe, Colins akamsaidia mama yake kubeba vitu vya mgonjwa mpaka ndani. Wakawakuta familia ya Simba na Connie. Colins akasalimia akiweka vitu sehemu zake. Kisha akasogelea kitanda cha mgonjwa maana Love alikuwa macho tu. “Aisee pole sana.” “Asante, na nashukuru kuja kuniona.” “Unajisikiaje?” “Wamenipa madawa ya maumivu, sasahivi nipo sawa.” “Pole sana.” Alipomaliza tu hivyo, akatafuta kona yake, akaenda kukaa kimya.

Connie akamsogelea na kukaa pembeni yake kisha akamsukuma kidogo kwa bega. Colins akamwangalia. Akajua kaka yake hayupo sawa. “Nisindikize hapo nje.” Akamnong’oneza kaka yake ila wakasikiwa. Ile Colins amesimama tu, mzee Simba akaanza. “Nilikutafuta sana mida ya saa nane mchana wakati Love akitayarishwa kwenda kufanyiwa upasuaji, alitaka kuzungumza na wewe kabla hajaingizwa huko.” Colins akajua anaambiwa yeye. “Simu ilizima. Nilikuja kujua niliporudi nyumbani wakati nipo getini mlinzi akiniambia mama ananitafuta, ndipo nikajua sababu. Poleni sana.” “Tunashukuru Mungu asiee. Ilikuwa mbaya sana.” “Poleni. Naamini atapona tu.” Colins akaongeza akiwa amesimama kama watoke.

Ndipo mama Simba naye akaanza kueleza ukubwa wa kile kilichompata mwanae. Akaeleza kwa masikitiko na uchungu, lakini wote walimjua jinsi anavyopenda kukuza tatizo. Aliongea mpaka kina Connie wakarudi kukaa maana baba yao alikuwa akiwatizama, wakajua wanaambiwa watulie. Colins naye akatafuta sehemu ya kujiegemeza na kuendelea kusikiliza huku wote wakitoa pole za hapa na pale.

Love akamfanyia ishara amsogelee. Colins akataka kuinyamazia lakini kila mtu aliona. Akajisogeza tena mpaka pale kitandani. “Najua tumeumizana sana Colins. Lakini leo nilipokaribia kuonja mauti, ndio nikagundua uthamani wa kile mtu alicho nacho.” Love akaongea na sauti iliyosikika ya kigonjwa. “Tunakuwa tukihangaika kutafuta zaidi na zaid…” “Ukisema ‘tuna’ unakosea. Mimi sikuwahi kutafuta zaidi. Wakati wote nilikuhakikishia mimi nimetulia na wewe Love na ndivyo ilivyokuwa. Lakini hata hivyo, kwa kuwa hatari ya kifo imeisha, kuna uhakika wa kupona, nashauri tulia mpaka upone, kisha fikiria unachotaka kuzungumza na mimi. Kwa sababu hichi unachotaka kukianzisha hapa, tumekifanya kwa zaidi ya miaka tutakayoweza kumbuka. Kinachobadilika ni matukio tu, na mahali.”

“Najua nimekua mbinafsi nikijifikiria mimi peke yangu bila kuzingatia juhudi za wazazi wetu kwa kizazi chetu na mpaka kizazi kijacho ili juhudi zao zisipotee bure. Watoto wetu sisi ndio warithi jasho lao.” Hapo akapata mioyo ya wazazi wote. Wakiona anaongea cha maana. Colins alijua anafanya kusudi tu akitaka wote wawe upande wake wamuunge mkono.

“Nakiri nimekosa Colins. Maisha yamenipa nafasi ya pili ya kutengeneza. Si kwa ajili yetu tu, kwa ajili ya wazazi wetu, na kizazi kijacho. Mimi nipo tayari kubadilika kwa garama yeyote ile.” “Hapana Love. Tafadhali tulia. Kama unataka kuzungumzia haya, iwe wakati umepona kabisa, halafu ndipo tutapata muda wa kuwekana sawa, kwa mara ingine tena. Maana tushapita hapa mara nyingi sana. Na tunapoteza tu muda. Binafsi…” “Colins, nafikiri ushauri wako ni sahihi, msubiri mpaka apone.” Mama yake akamkatiza kwa haraka sana akimzuia asisema alichotaka kusema.

Naye Colins hakubisha. Akanyamaza na kujivuta tena pembeni. Pakazuka ukimya wa hali yake, Love akasikika akilia taratibu. Sasa ikaanza kazi ya kumbembeleza ili asitoneshe mshono. Wote hapo ndani wakawa wakimtuliza, Colins akisikiliza ila kuepusha shari, akapenyeza pole yake hapo katikati yakumbembeleza, ila akiwa amekaa mbali kabisa. Baada ya yote, akalala.

Walikuja kuondoka hapo karibia saa tano usiku. Connie yeye alirudi chuo, Colins na wazazi wakarudi nyumbani, njia nzima hakuna aliyemuongelesha mwenzie mpaka nyumbani. Wakamshusha Colins usawa wa nyumbani kwake, mama yake akashusha kioo. “Colins, kwenye saa 11:30 asubuhi supu itakuwa imeshakuwa tayari. Usichelewe.” “Kwamba unataka nipeleke hiyo supu hospitalini, tena?!” “Unamaanisha nini ukisema tena?” Mzee akauliza kwa ukali kidogo. “Kwamba hujui kama leo Love amelala hospitalini na si nyumbani?!” Mzee akauliza kwa mkwara. “Nitakuja kuichukua, bila ya kuchelewa.” Colins akajibu hivyo na kuondoka.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Alipoingia tu ndani akaangalia tena muda, ilishakuwa saa tano na nusu usiku. Akajaribu kumpigia Jelini, hakuwa hewani kabisa. Akajaribu kama mara tano kana kwamba hajaelewa, kisha akatuma ujumbe. ‘Nimejaribu kukupigia, sijakupata. Ndio tumetoka hospitalini sasahivi. Nilitaka kukusikia kabla sijalala.’ Akatuma huo ujumbe. Akaona kabisa haujasomwa kuashiria haujafika pia. Akajirudisha kitandani akiwaza chakufanya bila jibu.

Siku Inayofuata.

Aliamshwa na alam alfajiri na mapema, asijue kama alilala au alikuwa macho muda wote. Akaoga kwa haraka na kufuata hicho chakula chakupeleka hospitalini. Akakuta msichana wa kazi jikoni, akamwambia mama amemuachia maagizo apeleke hicho kikapu hospitalini, yeye amerudi kujiandaa. Colins akabeba kama kilivyo akatoka hapo mbio ili aende hospitalini, kisha amuwahi Jelini nyumbani kwao, maana mpaka hapo ujumbe ulionekana haujafika.

Kabla hajaambiwa anatakiwa kurudi hospitalini kupeleka chakula asubuhi hiyo, usiku wake akiwa hospitalini alipanga asubuhi na mapema aamkie kwa Jelini, akamkumbatie, mambo yakae sawa. Ikawa tofauti, ndio katumwa yeye hospitalini kupeleka hicho chakula. Akakanyaga mafuta, kwa mwendo kasi kama anayekimbizwa.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Huku kwa Jelini yeye usingizi ulimuishia mapema tu. Akaamka yeye wa kwanza hapo ndani na kuanza kuandaa kila kitu. Muda ulipofika akaenda kumuamsha mwanae, akamsaidia kujiandaa, mama yake akifanya mengine. Mtoto alipokuja tu kuchukuliwa na basi, na wao wakatoka hapo, Jelini asiamini na asubuhi hiyo Colins hajadamkia kwake. Akaumia wivu, ila akaona anyamaze tu.

“Leo nipitishe kote ambako unaenda kuzunguka.” “Utaweza Jelini mwanangu? Mimi nahangaika humo njiani, kwengine natembea mbali.” “Isiwe tu kuumwa kichwa. Vinginevyo, twende wote.” Siku ikaanza kwa mama na mwana. Jelini akili ameweka kazini.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Colins alitokea hospitalini moja kwa moja akili zikamuongoza kwa kina Jelini. Mpaka anamaliza kupambana na foleni, saa mbili na nusu ndio anafika nyumbani kwa kina Jelini. Mama Jema alishatoa notice kwa walinzi. Mwisho ulikuwa tarehe 31 ya mwezi wa 12. Akakuta geti limefungwa kabisa na kufuli la nje kuashiria hakuna mtu ndani. Akajua Jelini ameanza kazi. Ikaanza kazi ya kumpigia simu mpaka akachoka.

Akaamua kumpigia simu James. “Unafahamu sehemu zilipo biashara za mama mkwe wako?” James akafikiria kwa haraka na kushindwa kukumbuka. “Yule mama ana mambo mengi kila mahali. Sina uhakika…” “Huna uhakika au hujui?” James akajua si shwari. “Sijui. Na Jema angekuwepo ningekuulizia, ila asubuhi hii alisema ni vikao tupu. Kwema lakini?” “Namtafuta Jelini.” James akafikiria kwa haraka. Akajua maswali mengi yatamkera, akaona amuache tu. Colins akakata simu. Na kurudi kwake.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Kwenye mida ya saa nne akiwa kwake akicheza game kama kawaida yake akiwa na hasira, hawezi kufikiria, basi atavaa headphones zake kubwa na kuanza kucheza game mpaka utamsahau. Simu ikaita asisikie. Baada ya kama lisaa, anaangalia simu, akakutana hiyo missed call na ujumbe kutoka kwa Jelini. Nusura alie. ‘Colins, samahani kwa usumbufu. Ila nilipiga kuulizia tu hali ya mgonjwa. Poleni sana. Naamini Mungu atamsaidia, atapona. Nawatakia kila la kheri, mgonjwa ague pole.’ Alipompigia hakumpata tena. Colins akaona machozi yakimtoka. Hakutarajia. Akajifuta kwa haraka. Nakubaki akitizama ile simu asijue chakufanya.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Mchana mama Jema ndiye aliyerudi kumpokea mtoto, Jelini akabaki dukani mpaka wakafunga duka saa tatu usiku ndipo akarudi nyumbani. Anafika getini kwao baada ya kushushwa na pikipiki, akakutana na gari ya Colins kama na yeye ndio amefika hapo. Jelini akamsogelea. “Poleni sana Colins. Vipi hali yake?” “Sikupati kwa simu siku nzima, Jelini! Kuna nini!?” “Nilibadili mawazo ya kuiuza ile simu ili kupata pesa. Nimeona niongeze juhudi kwenye kazi kuliko kuanza kuuza vitu. Kwa hiyo sasahivi ndiyo ninayotumia.” “Kwamba umerudi kutumia namba yako ya zamani?” “Ndiyo.” Colins akaumia sana.

Akatulia kwa muda akimtizama. “Ningekukaribisha ndani, lakini najihisi kuchoka na kichwa kinaniuma sana. Nataka nikanywe dawa nilale moja kwa moja.” “Labda niulize ni kwa nini umerudisha namba ya zamani?” “Nimefuata ushauri wako Colins. Lazima kupambana na changamoto zangu, si kukimbia. Kubadili namba ni kumpa nguvu yeyote ninayebadili namba kwa ajili yake. Sina sababu ya kufanya hivyo. Nimeona niishi kwa kupokea ukweli. Ila hujaniambia hali ya Love. Anaendeleaje?” “Vizuri, kesho anatoka. Nashukuru.”

“Afadhali. Uwe na usiku mwema.” Jelini akataka kuondoka, amuache palepale nje ya geti. “Umenibadilikia Jelini!” “Unamaanisha nini?” Jelini akamuuliza tu vizuri. “Ila ujue sikukusudia kuvunja makubaliano yetu.” “Colins, tafadhali usijisikie vibaya. Mimi nimeelewa kabisa. Kuna uhalisia wa maisha, huwezi kupingana nao, hata iweje. Mimi na wewe sasahivi tunaishi kwenye uhalisia wa maisha. Tupende tusipende, ndio ipo hivyo. Na binafsi nimekataa kuendelea kujidanganya, maana nimeshajichelewesha vyakutosha. Sitafanya hivyo Colins, kwa sababu kwa mara ya kwanza kwenye maisha yangu, nimejua kwa hakika ni nini nataka. Na sitakata tamaa mpaka nikipate. Na nipo tayari kulipa garama yeyote ile.” Jelini akaendelea.

“Na niamini nikikwambia sijakukasirikia kabisa. Nina amani kabisa maana ninaujua msimamo wako unapoamua kufanya jambo lako. Usiku mwema Colins.” Jelini akaingia ndani na kumuacha Colins amesimama nje ya geti akitafakari maneno yake. Alijua sentensi ya mwisho si nzuri. Jelini amemfikishia ujumbe. Yeye ni king’ang’anizi kwenye mambo yake. Hakubali kushindwa mpaka apate anachotaka. Kutotokea jana yake na kwenda kumuona Love, ni chaguzi si kushindwa. Akahisi miguu kuishiwa nguvu, akatamani ajiegemeze pengine atatoka tena amkaribishe ndani lakini akasikia sauti ya geti kufungwa kwa ndani, ndio akajua anatakiwa kuondoka.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Haukuwa usiku mzuri kati ya hata mmoja wao. Colins alikuwa akifikiria nakushindwa kuhema. “Inamaana mawasiliano kati yake na yule mzee ndio yanarudi tena!” Akawaza Colins. Wivu ulimfanya ashindwe kulala. Na hakuwa amekula. Kwa Jelini yeye alimeza tena dawa ya usingizi, akaenda kulala.

Wakati Wote Maisha Hutoa Mbadala.

Ila Upi Ni Sahihi!

Akiwa amejilaza kitandani kwake Belinda akampigia. “Naomba uje hapa kwenye gari nisaidie kubeba vitu.” Vai akatoka akijua anapopenda kuegesha gari Felix. Na kweli akamkuta Felix, Belinda na kijana mwingine. Mtanashati tu. Akawasalimia wote maana walikuwa wametulia garini kana kwamba wote walikuwa wakimsubiria yeye, mida hiyo ya jioni. Giza lilishaanza kuingia.

“Kwema?” Akaanza Vai. “Bwana mtoto unawaka kama jua gizani! Kweli picha hazijaongopa! Naitwa Victor.” “Victor kwa haraka! Hata husubiri utambulisho!” “Kizuri chajiuza Belinda. Ukisubiri kuuzwa, utaoza.” Vai akacheka kidogo. “Basi naona utambulisho umekamilika. Victor ni rafiki yetu. Alikuwa kajifungia, naona amechoka ndio ametoka kuangaza macho.” Vai akawa kama hajaelewa.

“Naona na mwanzo si mbaya. Kuanza tu unakutana na neema kama hii! Mungu anipe nini mimi?” Victor akaendelea nakumfanya Belinda na Felix wacheke ila bado Vai akaachwa hajaelewa. Akaona ajiachie tu. Akamgeukia Belinda kama kujua amsaidie nini. Felix akafungua buti, Belinda na Vai wakaelekea huko nyuma ya gari. Kweli alikuwa na mizigo mingi, kuashiria ametoka kufanya manunuzi ya haja.

Akamsaidia kubeba baadhi. Akarudi kuaga. “Jioni njema jamani.” “Asante. Na wewe unakaribishwa kwa chakula cha usiku. Sio watu wengi. Ni kama hivi tulivyo hapa. Usitie shaka.” Vai akapatwa kigugumizi. “Ni chakula tu. Eti Vai?” Felix akadakia kuongeza ushawishi. “Au Vai wewe huli?” Victor akaongeza swali lakishawishi. Wakamchangia Alex na Victor kwa maneno ya ushawishi, mwishoe Vai akakubali.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Akiwa anavaa chumbani kwake, Belinda akamfuata. “Mbona kama umepania sana!?” Akawa kama anamsuta. Vai akaishiwa nguvu. “Mbona hii nguo ya kawaida sana tu! Hata wewe unaijua. Sasa nimepania nini hapa?” “Ujue si lazima kwenda!” Vai akashangaa. “Kwa nini tena?!” Belinda akababaika asitoe jibu la maana, Vai akimtizama. “Si wamesema ni chakula tu. Au? Maana wakati mnanialika pale mimi sijaagiza chakula cha usiku na njaa inaniuma, chakula alichonipa Bale mlikishambulia chote mkakimaliza. Sasa sema ueleweke. Hutaki niende au?” Akamuuliza. “Mimi sitaki uone kama unalazimishwa. Ila kama unataka kwenda, twende.” Kisha akatoka na kumuacha Vai haelewi. Maana hata uchangamfu wake na maneno mengi vilimuisha. Vai akampuuza akijua pengine anayake tu. Asijue kinachoendelea moyoni mwake.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Mida ya saa mbili na nusu Felix akawafuata akionekana amebadili kabisa na yupo tayari kwa mapumziko ya jioni. Vai naye akawa amependeza tu ila akashangaa kutomuona tena Victor. Akaondoka nao Belinda akiwa amekaa mbele na Felix yeye nyuma. Ndio ikawa kwa mara ya kwanza kupanda hilo gari la Felix. Ule ukimya ndani ya gari ukamtoa pale kimawazo, mawazo yakahamia kwa Bale. Njia nzima akawa akimuwaza yeye. Hamu naye ilishamuingia.

Wawili hao kutoka lilishakuwa jambo la kawaida. Kwenda kula mishikaki au chochote mtaani wakiwa wawili wakicheka na Bale akimsikiliza na kuonekana kumfurahia vilivyo. Akajisikia kunyongea akitamani kama Bale angekuwepo hapo. Kwa hakika huwa wanakuwa na wakati mzuri. Si kitajiri, bali utulivu na amani ya aina yake. Halafu ukweli Bale anamvuto wake. Vai akawa amepoa hapo garini, kimya hata asijue kinachoendelea kati ya wapenzi hao waliokuwa wamekaa viti vya mbele yake.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Kwa mara ya kwanza akajikuta anaingia kwenye hoteli ya kula kwa kisu na uma, yenye meza zilizotandikwa kwa vitambaa vya maana na vitambaa vya kujifutia midomo. Hakuna kunawishana mikono. Kila mtu kisu na uma. Hajawahi tumia. Akatulia kwanza. Wakati wanataka kuagiza vinywaji Victor akatokea akiwa amejiwakilisha haswa. Na amependeza.

Akakaa kwa kujiamini akiwa amevutia. Harufu safi kuashiria amejisafi na kujipuliza manukato ya kiume ikaenea hapo bila kukera. Akamsalimia Vai kwa kumpa mkono kwa heshima tu na upendo wa aina yake, ilimradi tu kumkarimu akimuita mgeni wake. “Umependeza sana Vai. Na hiyo rangi nyeusi imekufanya upendeze zaidi.” “Asante. Na wewe umependeza.” “Duuuh! Kama umenikubali, basi umeufanya usiku wangu uwe mzuri.” “Umevunja kabati nini?” Felix akamtania. “Nakwambia nilikuwa na kazi ya kubadili mpaka nikaona nitachelewa! Ila kumbe juhudi yangu imelipa. Vai amenikubali bwana!” Wakacheka Vai akimtizama na kucheka taratibu kama ambaye hajamuelewa bado huyo Victor.

Muhudumu alipotaka kuendelea kupokea oda, ikabidi watulie ili aweze kusikia. Vai akaagiza juisi. Belinda ambaye alikuwa kimya kwenye simu yake hata hakuwa akicheka wala kuchangia neno, akaanza kumbeza. “Kwa udogo gani na wewe kama si kujidai tu? Wote tutakunywa. Kwa nini na wewe usinywe, au kutaka kuonekana mtakatifu hapa mbele ya kina Victor?” Wote wakashangaa vile Belinda alivyozungumza kwa jazba.

 “Kutokunywa pombe si utakatifu. Ni maamuzi tu. Binafsi pombe zilinishinda uchungu ila si kwa utakatifu.” Vai akajibu kiuungwana tu bila jazba. “Kweli bia zina uchungu wake ambao wengine ndio starehe yao. Nakuagizia sweet wine. Utapenda. Ipo kama juisi tu. Ukishindwa acha sio lazima, nitakuagizia juisi utakayopenda.” Victor yeye akapoozesha ile hali ya ukali ya Belinda kwa tabasamu na sauti ya kubembeleza, muhudumu akiwasubiria. Akakubali, ndipo muhudumu akaondoka na kurudi na vinywaji vyote ikiwepo hiyo sweet red wine.

Alipoionja haikuwa mbaya. Akapenda. Chakula kikaletwa. Wakaendelea kula na kunywa akiagiziwa wine zaidi. Yenyewe ni tamu kama juisi tu. Akaendelea kunywa na maongezi ya hapa na pale mpaka mtu wa ndani akaanza kubadilika. Usingizi ukawa mzito ila furaha na uhuru wa namna yake ukaongezeka.  Mawazo yote yakapotea. Ujasiri wa kufanya chochote atakacho ukaongezeka.

Glasi za wine zikaongezeka mpaka akapoteza ufahamu wake. Felix na Belinda wao walikuwa wakinywa bia aina ya heineken. Wakaonekana wazoefu wa pombe. Waliendelea kunywa kwa kujinafasi, yeye akinywa wine kama juisi. Victor aliagiza glasi moja tu ya margarita. Ikaletwa kwenye glasi kama ya wine lakini na kijipande cha limao kilichoegeshwa kwenye glasi kwa umaridadi wake ikapendezesha glasi. Akawa akinywa kidogo kidogo tu kama ambaye hakutaka iishe. Baada ya muda, Vai hakujua tena lililoendelea kwa kulewa.

Siku Inayofuata.

Alikuja kuamka yupo kitandani. Hajui alipo, kichwa kizito. Kujipapasa akitaka kuvuta shuka sababu ya baridi, akajigundua yupo kama alivyozaliwa, shuka halivutiki. Kumbe amelilalia Victor aliyekuwa amelala pembeni yake. Vai alishituka nusura aruke kitandani. Victor na yeye alikuwa amelala mtupu, hata shuka hakuwa amejifunika, ila kulilalia.

Akakaa kwa haraka. Jinsi alivyoona chupi na sidiria yake pale sakafuni, akajua wazi kuna mchezo ulichezwa usiku huo. Hakuwa hata akimfahamu Victor, lakini wazi iliashiria walifanya mapenzi! “Mungu wangu mimi jamani!” Vai alilalamika kwa hofu. Akatoka kitandani na kuanza kuokota nguo zake kwa haraka, Victor akaamka.

“Vipi?” Akamuuliza. Vai akashituka, akamtizama na kujaribu kuficha matiti yake. Victor akacheka taratibu. “Hapa ni wapi?” “Tulichukua chumba hapahapa. Niliona si sawa kukurudisha chuoni usiku ukiwa na hali ile.” Vai akabaki akivuta kumbukumbu asikumbuke. Inamaana alilewa sana na hapo wapo upande wa kulala wageni, pale walipokuwa wakinywa usiku uliopita.

“Vai, kumbe ndio unafujo nzuri hivyo ukilewa!” Akamtoa mawazoni. Vai akamtizama asijue kama ndio anamsifia au kumkejeli! Akaona aendelea kuokota nguo zake atoke hapo.

“Kina Belinda nao kama walifikia muafaka wakulala hapa watakuwa na wao walichukua chumba hapahapa. Niliwaacha wakiwa wanashauriana kama usiku wa jana waumalizie wapi. Tuoge, nitampigia Felix nione kama wapo tayari kupata kifungua kinywa pamoja na sisi.” “Mimi nataka kurudi chuo.” “Mbona mbiombio kama umefukuzwa tena?!” Hakujibu, akakusanya vitu vyake na kuelekea upande lilipo bafu. Hata chumba chenyewe kiliashiria wamelala kwa wenye pesa. Bafu safu linanukia harufu nzuri. Akatafuta sehemu na kuweka vitu vyake.

Victor akaingia akiwa mtupu kama alivyozaliwa. Akajisaidia, Vai akiwa amevuta taulo amejifunika kama asimuone. Victor akacheka. “Vipi tena Vai?” “Mimi sijui kilichoendelea jana usiku mpaka kujikuta hapa.” “Kwamba hukumbuki kabisa?!” Jinsi alivyomuuliza, ikamfanya Vai asite kujibu.

“Usijali. Tulipata wakati mzuri. Na wewe uliongoza shoo nzima. Na mimi nikafurahia. Kwa kifupi, tulipata wakati mzuri wa pamoja. Tafadhali usijisikie vibaya. Oga, tupate kifungua kinywa kwanza, ndipo ukitaka nitakurudisha chuoni leo. Huna haja ya kukimbia. Hamna la ajabu lililotendeka, na mimi ni mstaarabu.” Kimya, akishindwa kujibu hata kumwangalia.

Akamfungulia maji yakuoga. “Yape muda kidogo ili yapate moto. Niliweka chumba baridi ya juu kidogo, kwa kuwa wote tulikuwa tukitokwa jasho jana usiku na hukutaka mapumziko mpaka ulipopotelea usingizini. Na mimi nikalala, nikasahau kupunguza a/c.” Anayaongea hayo na tabasamu kama jambo la kawaida asijue jinsi anavyomfedhehesha Vai. Akazidi kujisikia vibaya. Akayashika maji ya bafuni, Vai akimtizama.

“Naona moto wake mzuri. Ingia uoge.” Ikabidi tu Vai kutoa taulo na kuingia akimtizama. Kisha akarudi chumbani, baada ya muda akarudi. Vai akashitukia anaingia na yeye bafuni! Akajivuta mwisho kama kumpisha. “Naomba kukushukuru Vai. Baada ya kipindi kirefu cha upweke, jana nimepata wakati mzuri sana. Sijui wewe, binafsi nilihitaji.” Vai akamtizama hapo bafuni na kugeukia maji.

“Nimekuwa mpweke kwa muda mrefu. Nilihitaji usiku kama wa jana. Samahani kama hukumbuki, lakini nakuhakikishia na wewe ulikuwa kwenye furaha ya namna yake.” Swala la upweke Vai aligundua alikuwa akilirudiarudia na kumshangaza. Victor alionekana kijana wa kileo na mzuri tu. Anakuaje mpweke ndani ya jiji lililojaa wanawake wenye uchu!?

“Mimi sikufahamu Victor. Nisingelala na wewe bila ya kukufahamu! Pombe ndiyo ilinifanya nifanye mambo ya ajabu.” “Hapakuwa na la ajabu. Tafadhali usijilaumu. Na mimi si kwamba nililala na wewe tu. Nilishapata habari zako, ndio maana sikuona shida kuwa na wewe jana. Najua umetulia Vai. Hilo nilihakikishiwa. Na niliambiwa hata nikikuweka karibu, hutanisumbua. Ikaniingia akilini. Sasa usiku uliponitaka kimapenzi na hivyo ulivyo, na mimi nilikuwa tayari pombe kidogo imeshaingia kichwani, nikajitosa tu.” Vai akazidi kujisikia aibu, na kushindwa kumwangalia kabisa.

“Geuka nikupake sabuni mgongoni. Usikae nje ya maji muda mrefu utaingia baridi.” “Sikumbuki kabisa kukuomba mapenzi jana.” Vai akaongea kuonyesha wazi kuishiwa ujasiri. “Silazima ukumbuke na usijisikie vibaya. Na mimi nilipenda.” Akamsogeza kwenye shawa. Akamgeuza kama kuupata mgongo.

Akaanza kumpaka sabuni taratibu. “Vai wewe ni mzuri!” Hakujibu akabaki amesimama amempa mgongo, anaangalia ukuta akisikilizia mikono ya kiume mwilini mwake. Akaendelea kumpaka sabuni. Shingoni mpaka kiunoni. Akaanza kama kumchua mabega. “Naomba urelax tafadhali. Upo na tension! Misuli yote umekaza!” Akamwambia taratibu na busu la shingoni akiendelea kumchua mabegani akiteleza na sabuni. “Haupo hatarini.” Akaendelea kuzungumza naye kwa kumbembeleza akimchua mpaka akasikia kutulia.

Akahisi kabisa mashine yake amesimama nyuma yake. Ile mikono ikaendelea kutembea begani, mbele. Victor alikuwa mrefu. Haikuwa shida kufikia kifua cha Vai mbele. Taratibu mikono ikahamia kwenye matiti. Akajisikia raha, mikono yote akaweka ukutani kama anayeshikilia kuta zisianguke. Victor akapata uhuru wote kwenye ule mwili wake, maji yakiendelea kuleta joto kwenye chumba hicho cha baridi. Mabusu na kupapaswa kukaendelea.

Mkono mmoja kwenye matiti, mwingine ukampapasa kushuka chini. Mwishoe akamkumbatia kabisa, bado akiwa nyuma yake, mikono inatembea mbele. Raha aliyokuwa akijisikia Vai ambaye hajalala na mwanaume muda mrefu, hata usiku uliopita hakuwa akikumbuka, akaachanisha miguu. Ndipo Victor akapenyeza vidole katikati ya uke wake, kisha akaanza kumchua na vidole vya kiume taratibu ila kwa nguvu iliyomfanya Vai kuanza kunung’unika maana Victor alijua kutembeza hivyo vidole ipasavyo. Aliendelea hivyo kwa muda mpaka akawa hajiwezi tena kusimama.

Bila papara, akampenyezea kwa nyuma taratibu, Vai akawa akisikilizia mashine ikiingia bila pupa na kurudisha vidole mbele. Ukweli Victor alitulia kwenye penzi. Akawa akiingia na kutoka ila bado akimchezea. Aliweza kumfikia vizuri. Vidole vya kiume virefu na nguvu yake. Alimchezea Vai huku na yeye akigugumia raha, mpaka Vai akapiga bao kwa sauti akiwa ameinama kidogo ila amempa mgongo. Alipomaliza tu, akamkamata kiuno kwa mikono yote miwili. Alicheza na hicho kiuno, akipiga taratibu mpaka na yeye akamaliza.

Lakini hiyo toka yake yenyewe, Vai akashangaa. “Mbona kama alimaliza!” Akajiuliza akiwa bado ameshikiliwa kiuno, anatoka kama anayemalizia, kisha anarudi. Akafanya hivyo kwa muda, kisha akamuhisi amesimamisha kabisa. Akachomoa na kuanza kumsafisha Vai kwa nje. Alipotaka kujimalizia kujisafisha mwenyewe, akamuwahi. “Naomba hii iwe kazi yangu.” Akamnong’oneza masikioni, mkono kinenani. “Nimefundishwa kuosha chombo nilichotumia kulia.” Victor akaendelea taratibu. Sasa huo usafishaji wenyewe, mapigo ya Vai yakawa yameshabadilika tena. Usafishwaji wa aina yake, mashine anaisikia ipo kamili kwenye matako.

~~~~~~~~~~~~~~~~

Vai Mikononi Kwa Victor Anayeonekana Kumfahamu Vilivyo, Yeye Hamfahamu Ila Amemuachia Kila Mahali. Hajiwezi, Ila Amefanikiwa Kumfikisha Vilivyo. Anataka Tena Na Tena.

Nini Kitaendelea Kwenye 5 Star Hotel?  

Victor ni Nani?

Kipi Kinachomfanya Belinda Kubadilika?

Usipitwe.

CONVERSATION

0 Comments:

Post a Comment